Search This Blog

Tuesday, June 21, 2022

NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA

  

IMEANDIKWA NA IDDI MAKENGO

GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA—SEHEMU YA KWANZA


Wakati nakutana naye alikua katoka kuachana na mwanaume wake, alikua na ujauzito wa miezi miwili tu. Alinielezea matatizo yake na kweli niliamua kumchukua, tukawa tunaishi naye kama mke na mume. Nilimhudumia kwa kila kitu, akanitambulisha kwao, kwakua yule mwanaume alikua kamkataa na kumuambia atoe mimba yake basi nilimchukulia mwanae kama mwanangu.


JOIN US ON TELEGRAM

Baada ya kujifungua nilienda kwao kumtolea mahari, nikamtafutia mtaji kwa kukopa kazini na kumfungulia Duka zuri tu la vyombo vya nyumbani. Mwanzo mambo yalikua mazuri tu, lakini baadaye alibadilika, akawa hataki kusikia kuhusu kufunga ndoa na kila nikimuuliza mambo ya dukani akawa anakasirika tu.


Mwanzo nilikua namfuata dukani, tunafunga na kurudi wote, lakini akanipiga marufuku kufika dukani kwa madai kuwa namharibia kwa wateja wake, hali hiyo ilinikesa sana na kila nilipokua nikienda basi aliishia kunitukana, kunifanyia vituko na kuongea maneno mabaya mabaya.


Alikua ananinunia bila sababu huku akilalamika kuwa namdahlilisha kwakua tu naenda dukani kwake bila idhini yake, aliniambia namnyanyasa kwakua nimempa mtaji hivyo akasema kama siwezi kuacha kwenda dukani basi ni bora kuachana. Kwakua nilikua nampenda sikuona sababu ya kuachana naye. Niliacha kwenda dukani, pesa nikawa siioni, mwanzo tulikua tunakaa na kupanga vitu lakini akawa kila kitu anafanya mwenyewe.


Nyumbani mimi ndiyo nilikua nahudumia kila kitu, akawa hajali tena kuhusu familia, kumbuka ana mtoto ambaye nilimchukulia kama mtoto wetu lakini alikua hata kumnunulia nguo hawezi. Mimi nilichukua mkopo hivyo nikawa nakatwa mshaara kila mwezi na Biashara anasimamia yeye, malengo ilikua ni Biashara ikianza kutengeneza faida basi anisadie majukumu ya nyumbani lakini haikua hivyo.


Duka lilizidi kupanuka, nilikua naona kabisa anauza vitu, yaani naona kama linakua kubwa lakini nikimuuliza kuhusu pesa ananiambia kama vipi tuachane yeye kachoka kuulizwa ulizwa kama mtoto.


“Si ulinipa milioni kumi, basi mimi naweza kukurudishia pesa yako kila mtu ashike njia yake, siwezi kusimamiwa simamiwa kama mtoto!” Aliniambia huku akijifanya kukasirika. Hapo basi ananuna hata mwezi mzima huku akimpigia simu kila mtu kuwa ninamnyanyasa, namsumbua na nataka kumfukuza kwakua tu nilimfungulia duka.


Nilikua nakasirika sana lakini kwakua nilikua nampenda basi nilivumilia. Alikua haachi pesa ya chakula, wakati huo nilishachukua mikopo mpaka napata laki moja na nusu kwa mwezi kwani mahitaji ya nyumbani yalikua makubwa, haachi kitu lakini akirudi anatumia mpaka kugawa kwa marafiki zake na ndugu zake, nikiongea anakua mkali huku akilalamika kuwa siwapendi ndugu zake.


Kwa hela hiyo nililazimika kulipia kodi, kununua chakula, kumnunulia mtoto nguo na kumpa kila kitu lakini bado alikua hanithamini. Hata binti wa kazi aliyekua akikaa na mtoto wake nilikua namlipa mimi nikimuambia anasema yeye hana pesa. Nakumbuka kuna siku alinijibu kwa dharau mpaka nikatamani kumpiga, nilimuambia kuhusu mshara wa binti wa kazi akaniambia.


“Kama unafanya kazi huwezi kupata elfu hamsini ya kumlipa mfanyakazi si bora ubaki nyumbani mimi nitakulipa hiyo hela, Mwanaume unajiita mwanaume halafu unafanya kazi ambayo huwezi kupata elfu hamsini!” Nilikasirika sana bila kudhamiria nikajikuta namtandika makofi, hapo ndipo kila kitu kilibadilika, alienda Polisi na kunichukulia RB.


Nilikuja kukamatwa na nilikaa ndani siku tatu bila dhamana, nilipokuja kufuatilia nikuwa alikua akitembea na mkuu wa kituo, Asikari wa pale ndiyo waliniambia huku wakishangaa kuwa yule mwanamke ni mke wa mtu kwani mbali na kutembea na mkuu wa kituo lakini alikua na wanaume wengi tu anawahcnganya na wengi walikua ni maaskari.


Nilikaa Polisi mapaka Mama yake mzazi alipokuja kuniwekea dhamana, lakini niliporudi nyumbani nilikuta ameondoka na kumuacha mtoto kwa Mama yake huku yeye na hiyo ndiyo sababu Mama yake alikuja kuniwekea dhamana ili tu nityoke na kukaa na mtoto! Alienda kuishi na mwanaume mwingine ambaye alikua ni mume wa mtu. Kwakua mtoto wake alikua kanizoea sana na kila mtu akijua kuwa mimi ndiyo Baba yake nilienda kumchukua na maisha yaliendelea.


Hakukaa sana kwa huyo mwanaume, kama mwezi mmoja hivi alirudi, hakuniambia kama anarudi, hakuomba msamaha nilimkuta tu ndani, baada ya kama siku mbili hivi alianza kuumwa, aliumwa sana nilipompeleka hospitalini ndipo iligundulika kuwa ametoa mimba ambayo nilikua na uhakika kuwa si yangu kwani zaidi ya mwaka alikua hajaniruhusu kuugusa mwili wake.


Nilimhudumia mpaka alipopona, lakini hata hakujali kuniomba msamaha wala kuongea na mimi kwa upole, hapana, alikua na hasira zake, alikua akiongea kana kwamba mimi ndiyo nilimsababishia yeye kuwa vile. Kila siku alikua ni mtu wa kunilalamikia, akiongea na watu anaongea kana kwamba mimi namnyanyasa, nampiga, namtukana lakini tofauti na siku ile nilikua sijawahi kumpiga wala kumtukana pamoja na kunifanyia vituko vingi.


Pamoja na kwamba hakuomba msamaha lakini nilimsamehe, siku moja niliamua kumtoa out nikiamini kuwa labda kuna kitu nilikua nimemkosea ndiyo maana alikua akinifanyia vituko. Nakumbuka nilimpeleka kwenye Baa moja maarufu hivi, nilimuona kama mke wangu hivyo nilitaka kumtoa out nikidhani labda kwakua nimekua bize sana na kazi kuna mambo nakosea.


Mimi nakunywa pombe na mara moja moja nikiwa sijabanwa na majukumu. Tulifika na kukaa, niliagiza nilichokua nikiagiza lakini kama dakika 20 hivi niliona vinywaji vinaanza kumiminika kwenye meza yetu, nilishangaa nikamuuliza mhudumu ni nani kaagiza ndipo yeye alinijibu kwa hasira, yaani aliona kama vile ninamdhalilisha wka kuuliza vile.


“Kunywa unataka kujua ili iweje? Mtu mwenyewe pesa za mawazo kwani ukinunuliwa kuna shida gani?”


Nilijisikia vibaya nikawa sina amani, nikawa naangalia angalia kuona ni nani alikua anaagiza, niliona meza ya jamaa mmoja aliyekua anaagiza kwani nilipomgeukia ni kama alikua anaongea na mhudumu na alinichekea kinafiki kama vile ananiambia “Kuywa tu ushalipiwa huku!”


Mhudumu alipokuja tena kutuletea vinuywaji nilimuambia kuwa sitaki.


“Muambie tunashukuru lakini tuko sawa, mrudishie vinjwaji vyake!” Lakini cha ajabu mpenzi wangu alinyanyuka kwa hasira na kuondoka kwa madai kuwa namdhalilisha.


“Unanidhalilisha kwa wanaume zangu wamaana, yaani mijitu mingine haina hata shukurani! Ujinga mtupu!”


Baada ya kama dakika mbili hivi nami nilitoka, kufika nnje sikumkuta, nilijaribu kumpigia simu yake lakini ilikua haipokelewi na mwisho ikazimwa, sikua na namna zadi ya kurudi nyumbani kuona kama ameshafika lakini hakufika. Nikaanza kuhangaika kumtafuta kwa marafiki zake mpaka kumpigia Mama yake ila hakuna aliyemuona. Hakurudi mpaka asubuhi alipokuja na kuniambia kuwa anataka tuachane na kila mtu ashike hamsini zake.


Niliona kama utani ila siku ileile vitu vilikuja kuchukuliwa, akamchukua na mtoto na hapo ndipo nilimuona yule mwanaume wa jana yake aliyekua anatununulia vinywaji alikua alikuja kumchukua na gari. Nilikasirika na kuona kama nimedhalilishwa hivyo sikumuomba msamaha wala kutaka kuongea naye chochote. Aliondoka na mtoto wake, ingawa niliumia sana lakini sikua na namna.


Nilikaa kama wiki mbili hivi nikiamini kuwa atarudi lakini hakurudi, nilifika dukani na kukuta makufuli, kuulizia nikaambiwa kuwa alishachukua kila kitu na hawajui ameenda wapi. Nilienda mpaka nyumbani kwao kujaribu kuongea na Mama yake lakini safari hii ilionekana kama yupo pamoja na mwanae haktaka hata kuongea na mimi!


“Mama Amekasirika, umekuja umetolea Dada mahari lakini hutaki kumuoa, ameona ni bora achukue mahari nyingine.” Aliniambia mdogo wake, mpaka wakati huo nilikua sijajua nimekosea wapi wala nifanye nini, niliumia sana nilipogundua kuwa kuna mwanaume alikua akiishi naye, mbaya zaidi nikuwa, alikua kahamishia duka langu sehemu nyingine na huko ndipo alikua akiishi na huyo mwanaume.


Kilichoniuma zaidi ni mambo aliyokua kaongea kwa ndugu zake, aliwaambia kuwa mimi nilimnyima kufanya kazi, hata duka ambalo nilichukua mkopo kumfungulia alikua kajibana na huyo mwanaume ambaye alienda kuishi naye ndiyo alimuongezea mtaji. Aliwaambia kuwa simpendi mtoto wake, kuwa ile mara ya kwanza tuligombana nikampiga na alinipeleka Polisi kwakua nilimtishia kumuua. Aliwaambia kuwa suala la Ndoa ni kitu ambacho ananiambia kila siku lakini mimi sitaki, hivyo ameamua kuondoka kwani anaona akiishi na mimi basi nisipomuua yeye nitamuua mtoto wake.


Nilijaribu kumtafuta ili angalau aniambie nilikua nimemkosea nini lakini hakunipa jibu, aliniambia tu hanitaki nimuache na maisha yake. Kilikua ni kipindi kugumu sana kwangu, nilikua nampenda yule mwanamke, alikua ni kila kitu changu, kibaya zaidi ni kininyang’anya mtoto na nilipojaribu kumdai alitangaza kwa kila mtu kuwa yule hakua ni mtoto wangu mimi sina uwezo wa kumpa mimba mwanamke na ndiyo sbabau ya kuniacha.


Iliniuma sana kwani ilinidhalilisha sana, nikawa mtu wa kukaa ndani, nikawa mtu wa pombe yaani nakunywa pombe mpaka nasahau nyumbani ni wapi? Mwaka mzima nilikua nasumbuka kumuomba msamaha, nilikua nahangaika kila siku kwenda kwake, ananitukana yeye na mwanaume wake lakini sikujali, nilikua nampenda mpaka ndugu zangu waliingilia kati na kuja kunichukua baada ya kufukuzwa kazi kutokana na pombe na kutokwenda kazini.


Miaka minne niliyoishi naye nilikua sijawahi kumsaliti wala kumfanyia kitu chochote kibaya, nilimuona kama mke wangu ingawa suala la ndoa kila siku alikua akinipiga chenga. Hali yangu ilikua mbaya sana, nilikua sioni sababu ya kuishi hasa alivyotangaza kwa kila mtu kuwa yule mtoto alikua si mtoto wangu na mimi sina nguvu za kiume siwezi kumpa mwanamke ujauzito.


Ingawa nilimpenda sana mtoto wake lakini hata mimi nilikua na hamu sana ya kuwa na mtoto wangu, lakini katika miaka yote hiyo minne alikua hajawahi kubeba ujauzito wangu hivyo yale maneno yaliniumiza na kuna wakati nilijikuta naamini kuwa nina matatizo siwezi kumpa mwanamke ujauzito, ingawa sala la nguvu za kiume nilijua kabisa kuwa ni uongo ila ishu ya mtoto iliniumiza sana.


Nilikaa kwa ndugu zangu kama miezi sita, nikawa vizuri kabisa, kwa bahati nzuri nilipata kazi sehemu nyingine kwenye kampuni moja kubwa na cheo kikubwa kabisa. Maisha yaliendelea, ingawa ilikua ngumu kwangu lakibni nilimsahau kabisa Salma, sikua na mahusiano mengine kwani nilikua siamini tena wanawake.


Pale ofisini nilikua na Dada mmoja ambaye alikua ni rafiki yangu sana, hakua mpenzi wangu lakini tulikua na ukaribu sana na kwa kiasi kikubwa yeye ndiyo alinisaidia kumsahau Salma. Siku moja alikuja ofisini kwangu huku akicheka, hakuonekana kukasirika bali alionekana kama vile haamini.


“Kumbe umeoa ndugu yangu hutuambii?” Aliniuliza, huku akinikabidhi simu yake.


“Mke wako naye mtata, sasa ndiyo vitisho vyote hivyo vya nini?” Aliendelea kuongea, alikua anaongea kama utani, mimi nilishtuka kidogo kwani baada ya kuipokea ile simu moja kwa moja niliona namba ya X wangu, Salma (Sio jina lake halisi).


Ni namba ambayo ilikua haijawahi kutoka kichwani kwangu, nilikua naikumbuka na mara nyingi sana nilikua nikishika simu yangu, naiangalia nasubiria labda atapiga au kutuma meseji ila hakufanya hivyo.


“Achana na mume wangu, humjui nitakufanya kitu kibaya. Kila mwanaume unamchekea tu, unajionana hilo tako lako unafikiri unamtisha nani, Nimeshakuambia George ni wakwangu hawezi kuwa na mwanamke mwingine zaidi yangu!”


GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA~~~SEHEMU YA PILI


Kitu kilipiga “Paaap!” Kwenye moyo wangu nilikua na hasira kidogo lakini kuna namna falani ni kama nilikua najisikia raha tena sana. Muda mrefu ulikua umepita bila kuwasilianan na Salma, nilkikua nishaanza kumsahau ingawa mara moja moja nilikua nikimkumbuka huku nikiwaza “Hivi kwanini aliniacha?”


“Kumbe bado ananipenda, yaani mpaka kuchunguza kuwa nina mwanamke mwingine itakua ananifuatilia na amenikumbuka, aisee! Nataka anayeye aumie kama nilivyoumia mimi!” Niliwaza huku nikitabasamu. Jackline (Sio jina lake halisi) aliniangalia kwa mshangao kidogho kwani sisi hatukua wapenzi na hakuna hata simu moja nilishawahi kumuambia kuhusu mimi kuwa wkenye mahusiano.


Mara nyingi kila alipokua akiniuliza kuhusu mahusiano nilikua nabadilisha mada na kujifanya kama sijamsikia vizuri.


“Ni nani huyo ambaye anataka kuniua kwaajili yako? G, nawewe una siri, yaani unataka kuniambia nina wifi yangu huko lakini simjui? Nitambulishe bwana, mimi sitaki mambo ya kuja kupigwa huko mtaani kwasababu yako…” aliongea kwa utani, nilimuambia hakuna kitu ni mtu tu nilikua naye lakini si ishu siriasi.


“Sikujua hata ananipenda kiasi hiki mpaka kufikia kukufuatilia, usijali nitaongea naye na nitemuelezea kuhusu wewe, sitaki aje kukusumbua.” Nilimuambia kwa mkato, hata alipotaka kumjua huyo mwanamke sikua na chakumuambia, kusema ukweli nilimtamani kujisifia mbele yake, kumuambia kuwa ni mwanamke wengi, niko naye na tunampenda, ana wivu sana lakini bado nilikua sijawa na uhakika ni kwanini Salma aliamua kumtafuta rafiki yangu na kumpa vitisho kana kwamba ni mwanamke wangu.


Nilijiaminisha kuwa nishaachana naye na sina mpango naye kabisa, lakini katika kipindi chote cha mahusiano hakuna siku niliyojisikia vuzuri na kijisikia kama mwanaume zaidi ya siku ile.  Ilikua ni mara yangu ya kwanza kugombaniwa na mwanamke, aisee nilisikia raha. Mara nyingi wakati mimi nasumbuliwa, namfumania mwanamke wangu na kunifanyia vituko vingi nilikua nikisikia rafiki zangu wakiwaongelea wanawake zao


Namna walivyokua wakibadilisha wanawake, kufumaniwa na wao kuombwa msamaha ilikua inaniumiza sana kiasi kwamba nilikua sijioni kama mwanaume.


“Atakua bado ananipenda na hata afanye nini siwezi kurudiana naye, nilikua tayari kubadilisha mpaka dini kwa ajili yake akaniacha tena kwa kunidhalilisha halafu leo ananifuatilia, hapana, akinitafuta na kuniambia kuwa anataka turudiane basi namtukanawee kisha namuambia kuwa sikutaki nina mtu wangu! Tena huyuhuyu Jack ndiyo atanisaidia, aisee, lazima ajue kuwa na mimi ni mwanaume aliniona wanini, basi mimi naanza kumuona wa kazi gani!”


Nilijiambia mwenyewe huku bado nikitabasamu, Jack alikua akiniangalia nikiwaza mwenyewe, aliniangalia nayeye akacheka.


“Unajua wewe ni mwehu, yaani mwenzako natishwa ila wewe unacheka!” Aliniambia kwa utani huku akinipiga kakofi kauso kama kakimapenzi hivi.


“Hahahahaha…. Hapana bwana, sijacheka, nimeshangaa tu mambo yenu wanawake, mnakuaga na wivu mwingine wa ajabu… hata hakuna kitu, nitaongea naye, mtu mwenyewe si kama niko naye siriasi kihivyo lakini anapanini kuniona niko na wewe!”


Niliongea huku nimkimshika na kumkumbatia Jack kwa nyuma, yaye alikua ni mfupi kwangu hivyo nilimshika kwa nyuma nikamkumbatia kama nainama huko makalio yake  makubwa yakihangaika na mwili wangu, alikua ni mzuri, kila siku nilimuona kama ni mzuri lakini hakuna hata siku moja nilishawahi kumtamani. Mara zote nikiwa naye hata akikaa vibaya nilikua nikimuona kama mwanaume mwenzangu, hata kusisimkwa nilikua sisisimkwi.


Lakini siku hiyo ni kama nilikua nimerudishiwa uanaume wangu. Nikiwa nimemshika nilijikuta nasisimkwa mpaka uume wangu kusimama, aliusikia na makusudi alijitingisha tingisha kama vile anajiondoa mikononi mwangu lakini sikumpa hiyo nafasi.


“Unataka kufanya nini wewe?”  Aliuliza kwa hasira kidogo kwani ni kama nilizidisha kumshika kwa nguvu hivyo akashtuka labda ninataka kumfanyia kitu kibaya.


Hapo ndipo na mimi nilishtuka na kujua kuwa nishaharibu


“Hakuna kitu bwana, nimekushika tu nikajikuta imekua hivyo.” Nilimuambia huku nikijitoa kwake kwa aibu.


“Mimi sitaki mambo yako, yaani ndiyo tumetoka kuongea kuhusu mwanamke wako halafu unanishika, hivi wanaume mkoje, kwahiyo sikuzote huniambii chochote leo najua una mwanamke ndiyo unajifanya kama unanipenda?”


Aliniuliza, nilikua sijamuambia kama nampenda lakini yeye ni kama alishajiongeze, hali hiyo ilinifanya kujisikia vizuri zaidi, kawivu alikokua ananionyesha na hasa namna alivyokua ananiongeolea kana kwamba mimi ni malaya ilinifanya kuzidi kuchanganyikiwa zaidi. nilihisi kama na mimi nagombaniwa na wanawake wawili.


“Kwahiyo uansemaje? Umekasirika?” Bila kujijua nilijikuta nimejibu kwa sauri ya juu iliyokua imejaa kadharau flani. Ni kama vile alikua ni mpenzi wangu amenifumania amekasirika.


Aliniangalia kwa hasira na kunisukuma pembeni.


“Wanaume wote kumbe Mbwa tu, hata wewe nilijua mstaarabu kumbe walewale!” Aliongea kwa hasira na kutoka zake nnje, sikumfauata wala kujaribu kumuuliza kitu chochote. Kwangu kugombaniwa na wanawake wawili ilikua ni hatua kubwa sana, nilijihisi furahaa nikawa sasa nasubiria simu ya Salma, nilijua kuwa lazima kuna kitu ambacho si sawa huko kwake ndiyo maana kaamua kumtafuta Jack akiamini kuwa ni mepnezi wangu. Niliamini kuwa labda ananipenda na atakuja kunitafuta tu, sikutaka kumtafuta nilitaka yeye ndiyo aanze kunitafuta.


*****


Furaha yangu haikudumu kwa muda mrefu, nikiwa naamini kabisa kuwa Salma ananifuatilia ndiyo maana amemtafuta Jack, nikiwa naamini kuwa labda atarudi kwangu atannitafuta yeye mwenyewe wiki ilipita bila kiusikia simu yake. Ni kitu ambcho nilikua ninakingojea kama mfanyakazi anavyosubiria msharaa mwisho wa mwezi, kila dakika kuangalia kwenye simu yake kama meseji ya muamala imeingia.


Sikutaka kuanza kumpigia ingawa namba yake nilikua nayo kichwani, nilitaka anitafute yeye ili nimjibu vibaya na kumuambia kuwa sitakia anisumbue mimi nina mtu wangu nampenda sana. Kichwani nilikua nikiamini kuwa huko aliko mambo si sawa, wiki nzima nilikua nikiiangalia simu kila dakika, wiki nzima nilikau situlii, sina amani lakini huwezi amini hakunitafuta. Raha yote niliyokua nayo iliyeyuka, kila kitu kilibadilika, nikajikuta nakua na hasira basi mimi ndiyo nikaanza kumfuatilia.


Nilifuatilia nikaja kujua kuwa alikua bado alikua akiishi na yule mwanaume wake,  Biashara ilishakua kubwa na huyo mwanaume ndiyoa likua akiisimamia, niliuliza kuwa mbali na huyo mwanaume aliyekua naye alikua na mwanaume mwingine ambaye kipindi hicho alikua ni mbunge tena maarufu sana, ni mara kibao alikua akienda Dodoma na huyo mwanaume, mbali na huyo alikua na wanaume wengine wawwili, mmoja alikua ni Dereva Bajaji na  mwingine alikua ni mume wa rafiki yake.


Nikisema rafiki yake namaanisha ni rafiki yake damudamu, yaani walee wapika na pakua. Rafiki yake ambaye hata kipindi ananiacha nilijaribu kumtafuta ili kujua shida ni nini kaanz akunitukana namna nilivyokua nikimnyanyasa rafiki yake na kuniambia nimuache na maisha yake. Alikua akitembea na mume wake tena mara nyingi akisafiri anaenda kulala mpaka kwa huyo rafiki yake.


“Sasa kama ana wanaume wote hawa kwanini anahangaika na mimi? Anashida gani huyu mshenzi?” Nilijiulzia lakini sikupata majibu.  Baada ya kuona  kuwa hanitafuti na hahangaiki na mimi basi niliamua kumuonyesha kwua na mimi nilikua na furaha, sina mpango na yeye na mimi nina maisha yangu.


Tangu kutokea kwa lile tukio nilikua bado sijaongea na Jack, tulikua tunakutana ofisini lakini nikimsalimia alikua anajifanya kutokusikia na kama tunakua mbele za watu basia taitiokia kidogo tui kwa shingo upanda. Baada ya kuona kwua kule mambo hayendi vizuri niliamua kumtafuta, nikaomba kuongea naye, ni kama naye alikua anasubiri nimtafute, ni kama alinimisi kwania linipa nafasi ya kuongea naye.


Nilimuomba msamaha na kuamua kumuambia kuhusu mahusiano yetu ya nyuma. Sikumuambia kama niliachwa na mwanamke akanidhalilisha, hapana, nilimuambiambia kuwa nilikua naishi na huyo wmanamke, namlelea mtoto wake lakini nilikuja kuachana naye kwasababu ya dini.


“Wakati nakutana naye alikua na ujauzito wa mwanaume mwingine, mimi nilimsaidia kama rafiki kwakua tangu mwanzo nilijua kuwa yeye ni muislamu na mimi nilishaapa kuwa siwezi kuoa muisalamu.lakini kwa jinsi tulivyokua karibu bila kujijua tukaingia kwenye mahusiano, ile kujakuja kwangu tukazama, aliniambia kuwa atakubadili kubadilisha dini na kwelia likua tayari kwa hilo.


Lakini yalipokuja masuala ya nyumbani, kwao waligoma kabisa asibadilishe dini, kuona hivyo namimi nikaona hakuna namna kwani mbali ya kwamba mimi mwenyewe sikua tayari kuao muislamu lakini nyumbani nako waligoma. Hapo nikampa mtaji na kumuambia tuachane, naona bado hajanisaidau kwani ni karibu miaka miwili sasa ila bado ananisumbua. Siko kwenye mahusiano nayeye na niko karibu nawewe kwakua unanivuria ila sikutaka kukurupuka nilitaka tujuaje vizuri kwanza.”


Nilimuambia, ulikua ni uongo lakinia mbao uliendana kidogo na ukweli, nilijua kama ningemdanganya sana ipo sikua ngegundua kuwa nilishawahi kuishi na mwanamke na ingekua shida. Alinisikia na kunielewa ila bado alikua na hasira, nilimuombakumtoa out siku hiyo ili tukaongee vizuri na kweli alikubali.


Kusema kweli sikua na mpango kabisa wa kutoka naye lakini nilishachunguza ratiba ya Salma, sehemua bazo anapenda kwenda hivyo nilitaka kutoka naye nikiamini kuwa hata kama asipo9niona yeye, watu hao hao aliowatumia mpaka kujua kuwa nipo na Jack, akapata wivu angewatumia kuchunguz anajujua kuwa siku ile nilitoka naye. Nilitaka sana ajue kuwa nina maisha yangu na sihangaiki tena nayeye. Ukweli nikuwa nilikua naumia na nilitaka kwenda kila sehemu ambayo niliambiwa kuwa huwa anaendaga.


Nilihangaika sana kutoka na Jack karibu kila siku lakini hakuna hata siku moja ambayo nilikutana na Salama, hali hiyo ilizidi kiniumiza. Ni kama alikua na maisha yake mengine na hana shida na mimi. “Lakini kwanini alimtafuta, kwanini anakumbushia maumivu?” Nilijiuliza bila majibu. Baada ya kuona hanitafuti na wala sikutani naye niliamua kuanzisha mahusiano rasmi na Jack, tulishakua marafiki kwa muda mrefu na niliona kumbe nayeye alikua akinipenda, nilianzisha mahusiano rasmi huku nikilazimishia kuwa nataka kuzaa naye.


Sijui kanini lakini bado maneno ya kuwa siwezi kumpa mwanamke ujauzito yaliniingia kichwani nilitaka kuwa na mtoto ili kuuonyesha ulimwengu mzima kuwa mimi ni kidume. Jack alikua akinijua, nilikua rafiki yake na alikua anapenda kuwa na mimi, nilipomuambia suala la mtoto aliniambia hawezi kubeba mimba yangu mpaka nijitambulishe kwao.


“Hakuna shida, kama ni kukuchunguza nilishakuchunguza sana hivyo naamini wewe ndiyo utakua mke wangu. Nilienda kujitambulisha kwao mimi kama mimi huku tukipanga namna ambavyo nitatuma watu. Nilikua na wasiwasi sana nikamuambia kuwa nahitaji mtoto kwanza kabla ya chochote, hata yeye ni kitu alichokua akikitaka sana. Alibeba ujauzito wangu, kusema kweli sikuamini kwani kila siku nilishajua kuwa sina uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito laklini tulipojaribu siku moja tu mimba ailiingia.


Alipima kwanza kwa kipimo cha haraka kisha kwenda hospitalini kabisa, baada tu ya kuhakikisha kweli ana mimba nilijikuta naanza kutangaza. Mara napost picha Mama kijacho, mara nampenda na kila kitu nikitaka ulimwengu kuona kuwa nimeweza kumpam mwanamke ujauzito.


“Hongwara naona unaenda kuwa Baba….” Siku moja usiku wa manane simu yangu iliita, ilikua ni namba mpya lakini nilipopokea sauti ilikua ni ya Salma. Ni simu ambayonilikua naisubiria kwa muda mrefu, karibu ya kila kitu nilichokua nikikifanya nilifanya kwaajili yake, nilitaka kumuonyesha kuwa mimi ni kidume!


“Nashukuru, mambo ya kawaida sana hatyyo….” Nilimuambia kwa kujishaua nikiona kama namuumiza.


“Huyo mwanamke naye ana moyo, ndiyo kaamua kukuzalia… Hahahahahaha hahhahahahah…” aliniambia kwa dharaau, nilijua kaumia hivyo na mimi nikataka kumchoma.


“Wewe si ulishindwa ukaanza kunitangaza kuwa siwezi kuzalisha mwanam ke, sasa ndiyo hivyo…”


“Ningetaka kuzaa na wewe ningezaa, hivi unajua ni mimba zako ngapi nilizitoa? Asikutaka kuharibu maisha yangu kwa kuwa na mwanaume kama wewe! Huyo dada naye atakua fala tu!” Alijibu kwa hasira na kukata simu, ingawa niliumia kuwa alikua anatoa mimba zangu lakini sikujali sana, nilimpotezea kama siku mbili hivi bila kumtafuta huku nikiendelea kupost picha zangu nikiwa na Jack.


Siku ya nne hivi jioni Salma alinipigia simu, aliniambia kuwa anataka kuonana na mimi hivyo anaomba kuja kwangu. Nilimkatalia sana na kumuambia kuwasimhitaji lakinia likazania, nikiwa sina hili wala lile huyu hapa mlangoni, alianza kugonga kwa fujo huku akilazimishia kuingia, ili kukwepa kudhalilika nilimfungulia mlango.


“Unafikiri unaweza kuniacha kirahisi namna hiyo, yaani hivi hivi tu uende kuwa na mwanamke mwingine, hapana!” Aliongea huikua kilia, nilihisi kama ni machozi ya uongo lakini yalikua ni ya kweli.


“Huwezi kuoa mwanamke mwingine, mimi bado nakupenda, nilifanya makosa kuachana na wewe, yaani bora kufa kuliko kukuona ukiwa na mwanamke mwingine!” Alizidi kuongea, nilimshika na kutaka kumtoa nnje lakini hakuataka kabisa, sijui alikua na nini ila ni kama mimi ndiyo nilikua nimemkosea.


“Wewe si una mwanaume wako, si unaishi na mwanaume, si unatembea na mbunge, si uinatembe na flani na flani….” Alishtuka kidogo kuona kuwa najua mambo yake lakini hakujali sana, aliniambia kuwa bado ananipenda na hawezi kuniacha.


“Najua nilikukosea ila unatakiwa kunisamehe, sina furaha kabisa, sidhani kama naweza kupata mwanaume kama wewwe, najua hata wewe unanipenda, nataka unipe muda niachane na kila mtu nije tuishi wote, nahitaji kufanya mapenzi na wewe, nipo kwenye siku zangi za hatari na nitabeba mimba yako!”


Aliongea mambo mengi kwa wakati mmoja, mimi kwangu ilikua ni sherehe, kilikua ni kisasi ambacho nilikisubiri kwa muda mrefu sana, sikua na mpango naye kabisa nilifurahi kuwa kumbe bado ananipenda.


Namuacha kila mtu nataka uwe mume wangu, nipo tayari kubadilisha dini kwaajili yako mwanangu anakupenda sana mpaka leo anakuulizia!” Aliniambia lakini sikua tayari kuendelea naye, nilimuambia simtaki, nikamshika na kutaka kumtoa nnje kwa nguvu.


Alinisihi sana lakini niligoma, nilimuambia nina mtu wangu, nishajitambulisha kwao hivyo siwezi kumsaliti kwaajili yake yeye aendelee na maisha yake tu.


“Basia cha nichukue Pochi yangu, huna haja ya kunitoa kihivyo ngoja nitoke mwenyewe….” Aliniambia, nilimuachaia akahcukua Pochi yake, alitembea mpaka mlangoni ile kufika tu nilishangaa kafungua Pochi, akatoa kisu kikubwa na kuitupa Pochi pembeni.


“Kama hutaki kuwa na mimi ni bora kufa, nife mnimi au ufe wewe ila sitaki kuachana na wewe. Huwezi kuniacha nakupenda sana….” Alichukua kilam kisi na kutishia kujuia.


“Siwezi kuishi bila wewe na ukiniacha najiua. Nikiwa sina hili wala lile alinyanyua kile kisu kweli na kujichoma tumboni, Damu zilianza kumwagika kimasiharaa masihara niliona kama anakufa mbele yangu.


GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA~~~SEHEMU YA TATU


Nilimkimbilia na kumshika, alikua kajichoma kisu kweli, ingawa hakikuingia sana lakini damu zilikua zinamtoka. Kisu alishakiachia kilikua chini!


“Nataka kufa, huwezi kuwa na mwanamke mwingine, mimi ndiyo wmanamke wako, mwnamke wa maisha yako, kwanini uniache?” Aliongea huku akipiga kelele za maumivu. Nilimnyanyua na kumuingiza kwenye gari nikampeleka hospitalini, halikua jereha kubwa sana alishonwa na kuruhusiwa. Nilitaka kumpeleka kwake lakini aligoma.


“Nataka kwenda kwako, siwezi kuishi bila wewe….” Aliniambia, sikua na namna kwa wakati ule nilijua kuwa kama nikimuacha peke yake anaweza kujiua kitu ambacho sikua tayari kukiona kikitokea. Nilimchukua mpaka nyumbani kwangu, kwakua ilikua ni usiku nilijua kwua Jack hawezi kuja kwangu bila taarifa hivyo nilikua sina wasiwasi kabisa. Nilitaka kumlaza sebuleni lakini aligoma huku akining’ang’ania kuwa ananitaka hawezi kulala mbali na mimi.


Kusema kweli nilikua nimekasirika lakini sijui ni nini ila kuna kakitu katika mwili wangu ni kama kalikua kanafurahia mambo aliyokua akinifanyia nilimpeleka mpaka kitandani ambapo alivua nguo zote nakulala. Nilimuangalia kwa tamaaa ila kila dakika nilikua nikikemea ili nisimguse.


Nilitoka kwenda kulala sebuleni, hakuniita wala kuniambia chochote, nilikaa kule kwa kama dakika kumi hivi nikasema hapana, ngoja nirudi chumbani kwangy. Kichwani nilikua namchukia lakini moyo ulikua hautaki kabisa.


“Aliniacha kwa dharau sana ngoja nikamuonyeshe, nilipe kisasai, natembea naye halafu kesho namuacha!” 


Nilimuambia huku nikielekea mlangoni, taa ilikua imewashwa, nilishika kitasa ili kufungua mlango lakini kabla ya kuufungua nilisikia mtu anaongea, mwanzo nilidhani kama ananiita anaongea na mimi labda kuna kitu anakihitaji lakini haikua hivyo, Salma alikua anaongea kwenye simu na mtu mwingine kabisa.


“Baby, nimekuambia nimepata ajali lakini husikii, angalia, gari haijaumia sana lakini nitahitaji pesa kidogo….’ Alikua akiongea kwa sauti ya mahaba huku akikugumia kwa maumivu. Nilifungua mlango kwa hasira, ile kuingia nilimuona akiongea Video call, alikua uchi wa mnyama huku kashikilia simu yake mkononi akimuonyesha huyo aliyekua anaongea naye maungo yake.


Nilipoingia aliniona, lakini hakushtuka kuniona, aligeuzia simu pembeni ili nisionekane kisha akaweka kidole chake mdomoni kama kwa ishara kuwa ninyamaze. Nilihisi kama kitu kiziro kimenippiga, yaani anaongea na mwanaume mwingione tena akiwa nyumbani kwangu, video call hgalafu anakuja na kuniambia kuwa ananipenda anataka kufa kwaajili yangu?


Aisee nilishindwa kuvumilai, nilikimbia hakarakaharaka na kumfuata kitandani, nilimvamia kama nataka kumpiga.


“Baby, Dada anaingia, nakata dada anaingia!” aliongea harahaharaka huki akukata simu. Baada tu ya kukata bila kujali mshono alinyanyuka na kunisukuma pembani.


|Unanionea wivu wa nini? Wewe sibado una mwamke wako umeschaachana naye? Umeachana naye? Nakuuliza umeachana naye?? Aliongea kwa hasira na kunigeuzia kibao kuwa sikua na haki yoyote ya kumkasirikia yeye kuongea na mwanaume mwingine kama bado nina mwanamke wangu.


“Mimi nakupenda, kama bado unanipenda na unataka kuwa na mimi naimbie, nitaachana na wanaume wote nilio nao kwaajili yako!” Aliongea kwa hasira huku akilia, kwa namna alivyokua anaongea ni kama alikua ananuilaumu mimi.


“Wewe ndiyo umeniharibia maisha yangu, umenifanya nimekua malaya, umenifanya nimekua mtu wa kutangatanga, nakupenda tangu zamani lakini hata hunijali.” Aliniambia nilishangaa alikua anamaanisha nini kusema nimekua sijali wakati tangu zamani mimi nilikua nampenda na nilikua tayari kwa chochote.


“Una akili kweli wewe mwanamke, wewe si ndiyo uliniacha na kwena kuishi na mwanaume mwingine!” nilimuuliza.


|hiyo ndiyo shdia yako George,m kimi sikua na mpango wa kukuacha, hnilichepuka kwakua nilikua naona kama hunijali, hunifuatilii, hunionei wivu, yaani unanipa kila kitu lakini hata siku moja hujawahi kukagua simu yangu, hivi wewe ni wmanaume wa namna gani? Mimi ni mwanamke, nahitaji kupendwa, nahitaji kufuatilia, nahangaika mwanangu anateseka na wanaume kila siku!


Hivi unadhani mimi napenda? Niliondoka na kukuacha lakini ulinitafuta, ulikuja kwetu hata kulia? Kwanini hata hukujidai kuwa unataaka kujiua? Hukua tayari kufa kwaajili yangu, ningejueaje unanipenda kama unachonipa ni machakula tu!” Aliongea kwa hasira huku akilia, sijui ni upendo au ni ujinga lakini kwa nusu saa nzima aliyokua akiongea kila kitu kilibadilika, alikua akinilalamikia mimi na mimi nilijiona kama vile ndiyo nimekosea.


“Kwahioyo bado unanipenda?” Niliuliza swali ambali liliibua mengine.


“Hilo ni swali kweli? Hivi wewe ndiyo wakinuiuliza kama nakupenda au la? Yaani nimefanya kila kitu kwaajiliyako, nimejaribu hata kufa kwaajili yako lakini bado unaona kama vile sikupendi?” alizidi kulia mpaka nikaanza tena kazi ya kumbembleza, nilianza kujisikia vibaya na kuhisi kuwa labda alikua ananipenda siku nyingi lakini mimi ndiyo nilikau sijui sijamuonyesha upendo.”


Tulikumbatiana na kulala mpaka subuhi, hatukufanya kitu chochote lakini usiku mzima nilikua na mawazo, kichwa kilikua kinachanganya mbaya sana, nilikua sina uhakika kama ananipenda au ananidanganya. Nilikua nawaza huko nyuma kutaka kujua ni wapi nilikosea, kuna vitu vingine alikuaakivilalamikia labda kuwa mimi simfuatilii, sishiki simu yake na vingine vya namna hiyo vilikua vyakwel, niliwaza mpaka kuanza kuamini kuwa mimi ndiyo nilikua tatizo.


*****


Asubuhi nilikua nawaza sana kama Salma atakubali kuondoka au ndiyo atasababisha vurugu. Nilikua namujua na siku hiyo nilipanga kukutaana na Jack, niliamka nikiwa na wasiwasi sana kwani sikutaka Jack jue kitu chochote, bado nilikua sijafanya maamuzi kuwa nimchukue nani, lakini kuamka yhali ilikua toafuati kabisa, salma alikua kashajiandaa anataka kuondoka, alionekana kama ana haraka sana.


Ingawa nilitaka aondoke harakaharaka lakini baada ya kumuona kama anataka kuondoka nilijisikia bibaya, nilihisi labda hanihitaji tena au anaenda kuonana na mwanaume mwingine.


“Una nini, mbona unataka kuondoka, umekuja kwangu jana unajifanya kunitaka sana lakini sas ahivi unaondoka?” Nilimuuliza huku niki8simama mlangoni nikiwa kama namzuia flani.


“Baaba sikiliza, nina maisha yangu, acha kuniletea drama, nimelala kwako jana hujanigusa halafu unataka nibaki ausbuihi ili nifanye nini?” Aliongea kwa dhara, akanisukuma pembeni na kutoka zake.


“Usije kunitafuta, nitakutafuta mimi nikiwa na shida nawewe!” aliongea huku akiondoka, hakutaka hata nimsindikize aliondoka na kuniacha nimeduwaa.


Nilijisikia vibaya lakini sikua na namna, sikua vizuri kabisa, nilikua na hasira na sikutaka kuonanana na mtu yoyote. Nilichukua simu yangu na kumpigia Jack.


“Usdije nyumbani, nina safari…” nilimuambia kwa mkato lakini hakutaka kusikia.


“Una nini mbona hukuniambia mapema?” aliniuliza kistaarabu sana, kwa namna nilivyokua naongea alishrtukia kitu, alitaka kujua sababu za mimi kuahirisha, aliniuliza kama niko sawa au naume, alikua anauliza kwa upendo sana kama mwanamek anayemjali mume wake lakini bila sababu nilijikuta namkasirikia.


“Unataka kunipanda kichwani? Hiovi una akili kweli wewe? Mbona kama hukusoma, yaani nakuambia kitu unahnibishia, unaniona mimi nani! Uhuniheshimu wewe, au kuja kwenu ndiyo imekua shida, hicho kimimba ndiyo kinakupa kiburi, sijakuoa bado ushaanza kunipangi amaisha nikikuoa itakuaje….”


Niliongea maneno mengi ya kashfa ambayo hayakua na msingi, kila nilivyokua nikizidi kuongea ndivyo alikua anzidi kuniombgha msmaaha na kwangu hasira ndiyo zilikua zinazidi kuongezeka, nilikua nakasirika sana, nilijikuta namtukana sana na kumkatia simu bila sababu. Alinitumia meseji nyingi kuulizia shida nini huku akiniomba msamaha, alipioga lakini sikupokea, mwisho niliona kero nikamblock kabisa.


Nilikua kama mtu aliyechanganyikiwa, mchana nilijaribu kumtafuta Salma lakini hakupokea simku yangu. Nilipiga simu sana lakini hakupokea, kichwa kilikua hakifanyi kazi nikiwaza kama ananipenda kwanini hataki kupokea hata simu zangu. Wakati huohuo Jack naye alikua akinitafuta lakini hata nilikua sijali, jioni Jack alikuja wkangu, nilikua tu nyumbani nimejikalia sina hili wala lile.


“Una matatizo gani, upo sawa kweli?” Aliniuliza baada ya kuingia ndani, sikutaka hata aingie ndani lakini kwa namna alivyokuja nilijisikia vibaya, alikuja kistaarabu kama vile4 hakuna kitu kilichoitokea, kama vile sikumtukana kiasi kwamba nikajikuta naywea mweneywe.


“Hauko sawa,una umwa au una matatikzo gani?” Aliniuliza hukua kinisogelea kama Mama anayetaka kubembeleza mtoto ili amuembie ana shida gani.


“Sina matatizo sitaki tu kuongea kwani ulikua na shida gani, si nimekublock wewe?” Nilimuuliza kwa hasira huku nikinyanyuka, nilitaka kumkwepa lakini yeye hakujali, alikua mkimya, katulia yaani kama mtu aliyeenda hospitalini kumsalimia mgonjw awa kichaa ambaye analeta fujo.


“Naomba uondoke, mimi sitaki kuongea na wewe, naomba uondoke!” Nilimuambia huku nikimnyanyua na kutaka kumuondoa pale, lakini yeye hakujali, alitaka kukaa na kujua tatizo ni nini?


“Umenituakana kwasababu ya huyu?” Aliniambia huku akinionyesha picha kwenye simu yake, zilikua ni picha za Salama akiwa uchi kitandani.


“Umezipata wapi? Nakuuliza umezipata wapi kwanini unafuatilia maisha yangu?” Nilimuuliza kwa hasira huku nikimshika kutaka kumnyang’anya simu. Hata hakupanikii, alinipa simu ili niangalie.


“Najua jana alikua hapa kwani alinitumia hizi picha nyie mkiwa chumbani na video mkiombana misamaha, najua kila kitu lakini bado sijakasirika, nakuuliza wewe huyu ndiyo mwanamke anayekufanya kunitelekeza mimi?”


Kusema kweli sikua na majibu, zilikua ni picha za kudhalilisha, Salma akiwa kitandani kwangu.


“Angalia vizuri hizo picha maana naona kama unataka kiufuta kwa hasira, huyo mshenzi wako alikua ananitumia picha ili kuniumiza roho lakini angalaia lichofanyam, kanitumia na mafaili mengine ambayo hayanihusu. Huyu si ulisema ni mpenzi wako, mbona sasa anatembea na rafiki yako mpaka wanapiga mapicha ya kijinga!”


Aliniambia hukua kiichukua ile simu na kunionyesha picha nyingine. Niliziangalia nilihisi kuchanganyikiwa, katika kumtumia picha Jack salama alijichanganya, alimtumia pamoja na picha nyingine za wanaume wawili, mmoja alikua ni rafiki yangu mkubwa mtu ambaye alikua akinisaidia katika mambo mengi na mwingine ambaye Jack hakumjua alikua nis hemeji yangu. Ndiyo Salma alikua akitembea na mume wa Dada yangu mkubwa tumbo moja na walipuga picha.


Nilijikuta nakaa chini nguvu zimeniishia, nilishindwa niongee nini, mwili ulikua unatetemeaka kama vile nimemwagiwa maji ya barafu. Kila kitu kilikua ni kama kiini macho, nilikua najua kuwa Salama ni malaya na pengine labda hawezi kubadilika ndivyoa  livyo lakini sikudhani kama anweza kutembea na watu wangu wakaribu namna ile. Watu waliokua karibu yangu kipindi nimechanganyikiwa.


Nikiwa chizi nilikua nakaa kwa Dada yangu, mume wake ananihudumia kama mdogo wake, ananipa ushauri, rafiki yangu huyo ndiyoa likua mtu wangu wa karibu, mtu ambaye nampigai simu na kumuambia matatizo yangu, kumuambia maumivu yangu, yaani nilishindwa kujua nifanye nini.


“Unajua ni kwanini sijakasirika kihivyo? Jack aliniuliza, nilimuangalia bila kummaliza, sikumjibu chiochote lakini aliendelea.


“Wewe ni kama mtumwa kwa yule mwanamke, umemuacha akakukalia kichwani, najua hujatemeba naye kwania livyokua mshenzi angenitumia video mkiwa kitandani, huyo mwanamke ni shetani, nilifuatilia mambo aliyokufanyia nimejua ukweli wote na nataka kukusaidia….” Aliniambia, lakini kabla hata hajamaliz akuongea mlango ulifunguliwa.


Tulikua tumekaa sebuleni tukiangalianaa, Salma aliingia ni kama alikua anamfuatilia Jack na alijua kuwa atakua pale. Bila kuongea chochote alimvamia na kumpiga teke la tumboni.


“Unajifanya kuingilia ndoa za wtau basi nitakuonyesha malaya mkubwa wewe! Jack alikua hajajiandaa, kila kitu kilikua ni ghafla, aliviringika pembenai na Salma akamfuata hukohuko hukua kimpiga tumboni.


Nilijua anachotaka, alitaka kumpiga tumboni kwakua alikua anajua ni mjamzito labda ili mimba itoke. Nikasema hapana, hawezi kuniulia mktoto wangu, nilimshika na kumnyanyaua, Jack naye alisimama, wakataka kuanza kupigana lakini niliwaamua hivyo wakatengana. Salama alikua na hasira kana kwamba yeye ndiyo kaibiwa mume huku Jack akiwa katulia tu.


“Sitaki kumuona huyu Malaya nyumbani kwako, nataka aondoke, ni uamuzi wako, ni mimi au yeye?” Salama aliniambia kwa kiburi, nilinyamaza bila kumjibu, alipoona kuwa sisemi chochote alinifuata na kunikumbatia kwa nguvu.


“Nakupenda lakini siwezi kuchanganywa na huyu masikini mba mchafu, kama huwezi kumuacha basi mimi nakuacha!” aliniambia huku akiniacha na kutaka kutokan nnje.


“Nikitoka humu ndani jua kuwa sitarudi tena, nakuambia siraudi n ahata kwenye mazishi yangu sitaki uje…” aliniambia hukua kifungua mlango kutaka kutoka. Lakini sijui ni kitu gani kilinishika nikajikuta namuita.


“Subiri kwanza Salma, subiri usiondoke kwanza…” nilimuambia huku nikimkimbilia, yeye alikua kama hataki akafunga mlango kwa nguvu lakini abdo nilimfuata, jack alikua kabaki ameduwaa anaangalia tu hajui chakufanya.


Mambo ndiyo kwanza yanaanza, unadhani George anataka kumuambia nini? Je, atamrudia au itakuaje? Vipi Jack, vipi na mtoto?” Nisikuchoshe.


GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA~~~SEHEMU YA NNE


Kusema kweli nilikua bado nampenda lakini kuna kitu kilinimbia, “Acha kua fala huyo mwanamke hawezi kuwa wako, huu ndiyo wakati wako wa kulipa kisasi.”


Salma aligeuka kama hataki vile, kwa akili yake alidhani kuwa naenda kumuomba msamaha lakini haikua hivyo. Nilikua sihitaji kabisa kumuomba msamaha, nilishaamua kuwa na furaha yangu na niliamini Jack ndiyo mwanamke sahihi wa kunipa furaha.


“Umesema unaondoka hutarudi tena, una uhakika?” Nilimuuliza huku nikimshika bega.


“Ndiyo, sikutaki, umenitesa sana, huwezi kupata mwanamke mvumilivu kama mimi nakuambia, tutaona, utakuja kunitafuta!” Aliniambia hukua kiutoa mkono wangu begani kwake, alijua nishaingia laini sina cha kufanya juu yake.


“Hahhahahahah! Hhahahahahah!” Nilicheka kwa dharau,  “Sitapata mwanamke kama wewe? Hivi unafikiri kuna mwanaume mwenye akili timamu atamuomba Mungu kuwa na mwanamke kama wewe? Nakuambia hivi sikutaki, sikutaki, sikutaki! Yaani sio tu hata ukifa nisije kwenye mazishi yako! Nakuambia hivii, hata ukifa nikisikia taarifa yako kwenye Radio naivunja na hiyo Radio mbwa wewe! Ondoka mshenzi mkubwa wewe, umeona nina amani ndiyo unajifanya kujirudi nenda kaendelee kufanya umalaya wako huko! Kama nikijuia huna haja ya kujichoma kisu, niambie nitakugonga na Gari mimi mwenyewe ukafilie mbali!” Nilimuambia huku nikimtukana, nilimtukana sana tena mambo ya kuhdalilisha mpaka Jack akaingilia kati.


“Muache aondoke, si sawa unavyofanya, huyu ni mwanamke mwenzangu siwezi kuvumilia nikiona unamdhalilisha namna hiyo!” Jack aliniambia huku akimshika na kumtoa nnje. Salma alikua haamini, alijitahidi kuongea kama vile ananisuta na kuonyesha kuwa hajali chochote lakini uzalendo ulimshinda, mwisho aliishia kulia na kuondoka akiwa kanywea kama kamwagiwa maji ya baridi vile!


“Ungeniacha ningempiga, yule mwanamke hana akili kabisa, kanitesa sana sasa hivi anajifanya yeye ndiyo mnyonge, yaani anataka kunifanya mimi nijisikie vibaya! Nakupenda sana na wewe ni mwanamke wa ndoto zangu, hata siku moja siwezi kumkumbuka yule shetani, nataka nikuoe hata kesho!” Nilimuambia Jack ambaye alionekana kama vile hajafurahia, nilimuambia kuwa nataka kumuoa lakini niliona kama akili yake haiku pale.


“Una nini na wewe mbona kama na wewe unataka kuniletea kisirani chako?” Nilimuuliza kwa hasira, aliniangalia chini juu bila kunimaliza kisha akaenda kukaa bila kuongea kitu chochote.


“Unamaana gani? Mbona nakuongelesha lakini hunijibu?” Nilimuuliza huku nikimfuata, nilishaanza kuwa mshari kidogo hivyo alilazimika kunijibu.


“Sikuelewi, yaani umekua na hasira mpaka nashindwa kuelewa kama wewe ni George ninayekufahamu au ni mwingine, umeona jinsi ulivyokua unamtukana X wako, ni kama bado unampenda yaani unaonekana kama bado una hasira naye!”


“Hivi una akili kweli wewe au kichwa chako kimejaa Makamasi? Mimi ndiyo mtu wa kumpenda yule Mbwa, si umeona jinsi nilivyomtukana, yaani unataka kuniletea kisirani? Hivi wanawake huwa mnatakaga nini nyie Mbuzi!” Nilijikuta naongea kwa hsaira, niliopna kama naye ananichanganya alinyanyuka kutoka alipokua amekaa na kutoka nnje, sikumfuata mpaka alipoondoka kabisa ndipo nilianza kumpigia simu kutaka kujua ni kwanini kaondoka.


“Inamaana hujui ulichokifanya?” Hakupokea simku zangu lakini alinitumia meseji, sikuijibu lakini siku hiyo nzima nilikua nikiwaza ni wapi nilikua nimekosea sikuona kosa langu. Kwangu mimi niliona kama nilikua sawa kumchagua yeye, sikuona shida kwakua nilimtukana mwanamke mwingine nilidhani kuwa naye atafurahia lakini haikua hivyo.


Nilikaa kimya kwa siku tatu bila kumtafuta Jack nayeye hakunitafuta, nilikua na mawazo sana hivyo nilimtafuta mimi kazini na kweli alinisikiliza na kukubali kuongea. Aliniambia kuwa  siku ile alikasirika kwani ni kama nilionekana kumpenda sana Salma, kwa namna nilivyokua namtukana ni kama nilikua  naumia na nilimtumia yeye kama kumpa wivu na si kuwa nampenda.


Niligundua kosa langu nikaomba msamaha na kweli alikubali. Mahusiano yalianze tena upya lakini sasa hivi yalikua ya kasi sana, nilikua natumia muda mwingi sana kwake na mwanzo tulikua na amani ila nilishangaa kila mara tunaanza kugombana gombana bila sababu za msingi. Pamoja na kwamba nilikua nimeshaachana na Salma lakini bado nilikua naumia kuwa hajaumia vyakutosha. Nilitaka aone kuwa maisha yangu yameendelea mbele na simhitaji tena.


Tangu siku ile tulipogombana hakuwahi kunitafuta wala kuonyesha dalili kuwa ananihitaji. Nilifungua akaunti feki kwenye mitandao kumuangalia kuona kama ana maisha ya aina gani na hapo ndipo nilizidi kuchanganyikiwa. Alikua na furaha, anapost Biashara zake mtoto wake na nilichanganyikiwa zaidi siku alipo post kuwa ni mjamzito na kumshukuru Mungu. Ingawa hata mimi nilikua nikitegemea mtoto lakini niliumia kwanini nayeye anategemea mtoto?


Ni kama nilitamani asiwe na furaha tena, hali hiyo ilinifanya kuwa na wivu hivyo na mimi nikaanza kumpost Jack na mimba yake. Nilimlazimisha kupiga picha, tukaenda mpaka studio napiga picha napost kwa caption za kuonyesha kuwa tunafuraha lakini sikua na furaha.


“Anapost picha kuwa ana mimba kwakua anajua tunaenda kupata mtoto, mimi hata simuamini kama ana mimba….” Siku moja uzalendo ulinishinda, nilikua kitandani nafanya mapenzi na Jack lakini akili yangu yote ilikua kwenye picha ambayo aliipost Salma mchana wake.


Hakikua hata picha mbaya tuseme labda ni ya uchi hapa,alipost picha akiwa kashikwa tumbo na huyo mwanaume wake.


“Sema kuna wanaume wajinga, yaani anamdanganya kuwa ana mimba kumbe hana, na hata kama basi ana mimba sidhani kama ile mimba ni yake, hivi unajua kuwa anatembea na Mbunge….” Nilizidi kuongea, ni kama nilikua najiongelesha mwenyewe kwani Jack alinisukuma pembeni na kugeuka upende mwingine.


Niliongea mwenyewe kwa zaidi ya nusu saa ndipo nilishtuka kuwa nilikua nafanya mapenzi na mpenzi wangu. Alikua kajilaza kitandani kachukua mto kajifunika kichwani kama kuziba masikio ili asisikie nilichokua nikikiongea. Nilijua nimefamnya kosa hivyo nilianza kumshika tena kutaka tuendelee kufanya mapenzi.


“Sitaki bwana niache, sina hamu tena ya kufanya mapenzi na wewe usiniguse….” Aliniambia kwa hasira, hakulalamika sana, hata mimi sikua na mood ya kuendelea kufanya mapenzi hivyo nilimuacha tukalala mpaka asubuhi.


****


“Leo ni maajabu unanipeleka kininiki daa Mungu mkubwa!”  Ujauzito wa Jack ulishafikisha miezi sita lakini katika kipindi chote hicho alikua akiniomba nisindikize kiliniki nilikaataa. Lakini siku hiyo mimi ndiyo nilimuambia kuwa nataka kumpeleka kiliniki, alishangaa lakini alijiandaa harakaharakakwa furaha.


“Afadhali maana wale Manesi ukienda mwenyewe wanaona kama umezaa na mizimu, hata ukiwahi utakaa kwenye foleni mpaka waliokuja na wuame zao wahudumiwe, utaona leo dakika kumi tu tusharudi.”


Aliniambia lakini mimi hata sikumsikiliza, nilikua na yangu kichwani, alishaangaa nilipompeleka kwenye Hospitali ambayo hakuizoea.


“Hapa ni wapi? Hivi unajua kuwa mimi sijagi kiliniki ya huku?” Aliniuliza baada ya kuona nimempeleka kwenye Hospitali tofauti kabisa.


“Kwani Hospitali si zilezile, utaanza kiliniki hapa kama unataka niwe nakuleta, najuana na hawa madaktari hivyo watakuhamishia huku.” Nilimuambia kwa ukali, niliona kama nataka kuleta ubishiubishi wake. Wakati tukiwa tumesimama hata kuingia hataki akiwa hajui kwanini nilimpeleka pale mara Salama aliingia, alikua na Mwanaume wake hapo ndipo Jack alijua ni kwanini nilikua nimempeleka Pale.


Bila kuongea chochote aliondoka mpaka kwanye gari, funguo nilikua nazo mimi hivyo alisimama kwa nnje. Mimi hata sikumjali, sikujali kama kakasirika wala nini, nilitaka tu Salma kupita mbele yangu ili nione kama atanisalimia au la.


“Mambo vipi?” Salma alinisalimia kwa Bashasha baada tu ya kunifikia.


“Poa habari… naona umekuja kiliniki kumbe nawewe unakuja hapa nimemleta mke wangu yule pale kaenda kusimama pale kwani hijisikii vizuri?” Nilimuuliza kwa dharau flani, huku nikijielezea mambo ambayo nilikua hata sijaulizwa, yeye hakuonekana kujali, alionekana kama yuko sawa hivyo nilizidi kukasirika na kutaka kumharibia.


“Haka kakijana ni kanani?” Niliuliza kwa dharau kabla ya kunijibu nilijifanya kujiongeza na kuzidi kuonyesha dharau.


“Ndio Bodaboda wako au maana na hali yako hiyo hutakiwi kutumia Bodaboda?” Niliuliza kwa dharau pamoja na kuliona gari lake pale. Nilikua namfahamu yule kijana kuwa ni mpenzi wake hivyo nilitaka tu kumkera.


“Huyu ni Baba wa mtoto wangu mume wangu mtarajiwa….” Alitulia kidogo huku akiniangalia kwa tabasamu kisha akamgeukia mwanaume wake.


“Baby huyu ndiyo yule Kaka nilikua nakuambia, mke wake yule pale kasimama kwenye gari….”


Aliongea kistaarabu bila kusema alichokua anamuambia kijana wake lakini nilishangaa yule kija akinipa mkono kutaka kunisalimia kiheshima. Nilikua sina namna nikaitikia tukapeana mikono kwa aibu niliondoka mpaka kwenye gari nikafungua mlango, Jack alikua bado kazubaazubaa amesimama anawaangalia, nilikua na hasira hivyo sikua na muda wa kumsubiri. Niliwasha gari kwa hasira, nikashusha kioo kisha nikaanza kumfokea.


“Unaondoka au unabaki hapa utembee?” Nilimuuliza kwa hasira, alishika mlango kuufungua nikaona kama ananichelewesha, niliachia mafuta gari ikaenda mbele kidogo.


“Harakaharaka bwana unanichelewesha wewe vipi?” Nilizidi kuongea kwa hasira, kwa namna nilivyokua nataka kuondoka kila mtu pale alishangaa kwani nilikua ni mshari shari sana. Aliingia kwenya gari harakaharaka ila hata kabla hajafunga mlango vizuri nilishaondoka kidogo adondoke na sikujali.


“Una nini mbona hivyo? Inamaana ulinielta huku ili kuja kuonana na mwanamke wako….” alianza kulalamika, mimi akili zangu zilikua kwingine kabisa, sikujali hata kama yupo mule ndani, niliendesha gari harakaharaka mpaka nyumbani, njia nzima alikua akiniongelesha kwa hasira bila mimi kujibu. Nilihisi kama anataka kunipanda kichwani, nilisikia kama ananitukana. Niliingiza gari mpaka ndani kisha nikashuka, kabla ya yeye kushuka nilienda mpaka kwenye mlango wake na kuufungua.


“Shuka! Shuka nimekuambia shuka!” nilimuambia kwa hasira, yeye bado alikua anashangaa shangaa.


“Unanilazimisha nini? Niache nitashuka mwenyewe au hata kwenye gari hutaki….”  Sikumpa hata nafasi amalizie kuongea, nilizishika nywele zake ambazo alikua kasuka rasta nikamvuta na kamrusha nnje ambapo alidondoka chini. Akiwa bado anakijizoazoa nilimshika mkono wake wa kulia na kuanza kumvuta kumuingiza ndani?


“Unataka kunipanda kichwani eee? Mimi ni mwanaume lakini naona unataka kunipanda kichwani, sasana ngoja nikufundishe heshima mshenzi wewe! Nilimuambia huku nikizidi kumvuta ndani kwa mkono mmoja, alikua akipiga kelele za maumivu huku akidai kuwa namvunja mkono wake lakini sikujali. Nilikua na hasira sana nilimvuta mpaka ndani kisha nikaingia chumbani, nilichukua pasi ambayo ilikua kwenye meza ya chumbani na kutoka nayo.


Niliishika ile pasi nikawa natumia ule waya wake kumchapia, nilimchapa sana lakini nilihisi kama vile hasikii. Niliacha kutumia mkanda wapasi nikaichukua ile pasi na kuanza kumpiga nayo kama vile mtu anaponda kitu na nyundo, nilimtwanga sana huku nikimtukana kuwa ni malaya na kumuambia hata huyo mtoto sidhani kama ni wangu.


Sijui kwanini lakini kila nilivyokua nazidi kupiga ndiyo nilikua nikisisikia raha na wakati nampiga matukio yote ambayo Salama alikua akinifanyia yalikua kichwani. Nilikua najua kabisa niliyekua nikimpiga ni Jack lakini kichwani alikua  Kajaa salama, hata nilipokua nikitukana nilikua nikikumbushia  matendo ya salma na si Jack.


Nilimpiga sana, pasi, mateke na ngumi huku nikimtukana, mwanzo alikua akipiga kelele tena sana lakini baada ya muda alitumlia kabisa, alikua haongei kitu chochote. Nilicheki mapigo yake ya moyo nakuona kama moyo umesimama. Hapo ndipo nilikua kama nimeshtuka nikajua kuwa nimeua, yaani akili zangu ndiyo zilirudi.


“Nimeua, nimeua!” Nilijikuta napiga kelele kama chizi. Wakati nikiwaza kuwa nifanye nini kwani nilishaiona jela hii hapa nilipata wazo la kumfungia chumbani. Nilimvuta mpaka chumbani kisha nikafunga mlango nikatoka. Nilitoka mpaka kwenye gari nikasema hapana, kule ataonekana na kama akikutwa humu ndani kwangu basi nitakamatwa mimi kwani hata hospitalini kuna watu waliniona.


Akili iliniambia rudi mfiche mpaka jioni ukamtupe kwani hapo chumbani si salama. Nilirudi chumbani nikamchukua mpaka choo cha ndani kulekule chumbani nikaenda nikamfungia ndani kisha nikafunga milango yote na kuondoka. Nilirudi kazini kwakua ilikua ni siku ya kazi, huko nilijifanya kama vile hakuna kitu kilichotokea.


Ili nisionekane kama mimi ndiyo nimemuua kule kazini nilianza kuuliza kila mtu kuwa amemuona Jack? Wakati natoka nyumbani nilichukua simu yake na kuizima, hivyo kila mtu akipiga alikua anaambiwa kuwa simu zake hazipatikani.


“Nilimpeleka kiliniki akaniambia nimuache nyumbani kwake atakuja kazini ila mpaka sasa hivi sijamuona na simu zake hazipatikani?” Niliomngea huku nikijifanya kuwa nina mawazo sana, sikuishia kuuliza tu watu wa kazini, hata nyumbani kwao niliwapigia kuwaulizia lengo kuonekana hata mimi nilikua simuoni.


Tayari nilishajua amekufa hivyo nilijipanga kwenda kumtupa mtaroni karibu kwake, nimwagie pombe ili kuonekana alikua kalewa na labda kupigwa na wahuni, sikutaka kuishia jela. Kusema kweli nilikua sijui kwanini nilimpiga kwani katika maisha nyangu nilikua sijawahi kumpiga mwanamke lakini kila nilipokua nampiga, kila nikinyanyua mkono nilikua nikijisikia raha nikiona kama vile uanaume wangu umerudi.


Baada ya kumpiga na kumuumiza, nikajua kuwa nimeua ndipo akili yangu ilirudi na kujiona kuwa nimefanya makosa makubwa. Jioni sikurudi moja kwa moja nyumbani, sikutaka kukaa na maiti ndani kwa muda mrefu hivyo nilikaa mpaka kwenye saa tano usiku hukubado nikipigia simu ndugu zake kumuulizia hapo na waliponiambia kuwa hawajui ndipo niliamua kwenda nyumbani ili kuchukua maiti ya Jack na kwenda kuitupa kweye mtaro karibu na kwake.


GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA—SEHEMU YA TANO


(ILIPOISHIA SEHEMU YA NNE; Salma anarudi kwa George baada ya kusikia ana mwanamke mwingine, wanagombana mpaka anataka kujiua lakini anapona. Jack anakuja wanagombana na George anamfukuza Salma,  ila anakua na hasira ambazo anazihamishia kwa Jack, anampiga na kumfungia ndani, akijua kuwa ameshamuua basi anarudi ili kwenda kumtupa. ENDELEA….)


Nilifika nyumbani nikiamini kuwa Jack atakua ameshafariki dunia, nilijua nishaua hivyo natakiwa kutafuta sehemu ya kumtupa. Nilifungua milango taratibu mpaka chooni, bado alikua amelala chini palepale nilipokua nimemuacha. Niliiinama harakaharaka ili kumbeba, wakati nahangaika naye nilisikia sutiti yake.


“Usinipige tena, utamuua mtoto wako George….” Ilikua ni sauti ambayo ilinishtua kwani nilijua kuwa nimeshika maiti. Lakini haikua hivyo, Jack alikua mzima kabisa ingawa alikua kachoka sana nilishangaa alikua na nguvu kidogo.


“Upo hai! Upo hai mke wangu! Upo hai mke wangu nisamehe!” Nilianza kupiga kelele huku nikimnyanyua harakaharaka, sijui nilipata wapi nguvu lakini nilimbeba kama karatasi mpaka kitandani. Hapo nilimkalisha lakini alishindwa kukaa, alilala kitandani huku akijitahidi kuongea kunisisitiza kuwa nisimpige tena kwaajili ya mtoto.


“Usijali, siwezi kukupiga, nakuahidi kabisa kwua siwezi kukupiga, kaa utulie. Nakupenda sana mke wangu, nakupenda siwezi kukupiga tena, niamini alikua ni shetani!”


Nilimuambia huku nikimchunguza mwili wake ambao ulikua umevimba sana, alikua kaumia karibu kila sehemu yaani alikua hatazamiki. Kwa kumuangalia niliona kama ni mtu mpya kwangu, ilikua kama nimemuokota akiwa vile akiwa kapigwa na mtu mwingine.


“Hivi mtu atafanyaje unyama wa namna hii? Huyu sio mimi atakua ni shetani tu, sio mimi!”


Kwa akili yangu na namna alivyokua ameumia ilikua ngumu kwangu kukubali kuwa mimi ndiyo nilikua niemfanya vile.


“Nisameha mke wangu, nisame sana, yaani sijui ni kitu gani kimeniingia akilini kwangu lakini nisamehe….” Niliomba msamaha sana lakini yeye ni kama hakunisikia.


“Mwanangu hachezi kabisa, kaacha kupigapiga, sijui kuna nini George, nipeleke hospitalini, najihisi siko sawa, sioni kama mwanangu yuko sawa….” Alizidi kuniambia, niliona ni sawa, nilimsaidia kunyanyuka, nilitaka abaidlishe nguo lakini alikataa, bado alikua ana nguvunguvu ingawa nilimuacha muda mrefu nikiwa nimemfungia ndani bila chakula wala nini?


“Upate chakula kwanza, usiende hivi Hospitalini…” nilimuambia lakini bado alikataa.


“Nimeshakula, mimi niko sawa kabisa, sitaki chochote, nilikua nakunywa maji ya chooni na niemshiba ninachotaka sasa hivi ni kujua hali ya mwanangu tumboni. Nataka sana mtoto na najua unamtaka sana, kama sitakua imara huyu mtoto atafia tumboni.” Kusema kweli alikua anajikaza, kwa namna alivyokua kavimba, mwili mzima umevimbia damu hata mimi kumshika ilikua shida, kila nikimgusa niliona kama namuumiza lakini yeye wala hakujali. Alikua akimuwazia mtoto wetu tu.


Nilimbeba mpaka kwenye gari ili kumpeleka hospitalini, hapo akili yangu ilikua haiwzi kitu zaidi ya mtoto, kama vile si mimi niliyempiga nilihisi kama kafanyiwa unyama flani hivi na mtu mwingine. Lakini nikiwa njiani nakaribia kufika Hospitalini akili ilianza kuzinduka na kufanya kazi vizuri.


“Watauliza kafanya nini? Kwa hali yake hii ni lazima watataka PF3. Nilijikuta nasita.


“Hivi hatanitaja kweli kuwa mimi ndiyo nimefnanyia hivi?” Niliwaza huku nikipunguza mwendo mpaka nikasimama.


“Vipi mbona umesimama?” Aliniuliza, nilizima gari na kumgeukia.


“Tunaenda kusema nini tukifika huko?” Nilimuuliza swali ambalo nadhani hakulitarajia.


“Kusema nini hukusu nini?” Aliniuliza, nilijaribu kumuelewesha kuwa kwa hali yake aliyokua naye hospitalini wasingekubali kumtibu mpaka wapiti Polisi.


“Mimi sipo tayari kufungwa, na kama umeshanisamehe sioni kama kuna haja ya kushirikisha Polisi….” Nilimuambia kwa sauti ya ukali kidogo.


“Hata mimi sitaki mambo ya Polisi, nitawaambia kuwa nimeondoka kwenye ngazi…” Aliniambia, nilikaa na kufikiria kwa muda nikasema hapana, huu ni ujinga, hakuna mtu anayedondoka kwenye ngazi akang’oka nywele, huyu lazima atanifunga!” Niliwaza huku nikifungua mlango wa gari na kutoka, nilirudi mpaka siti ya nyuma alipokua amelala. Nikafungua mlango kisha nikamuamuru atoke nnje. Mwanzo alikataa lakini nilipomtishia alitoka.


Nilirudi upande wa dereva nikazima taa za gari, nikamshika mkono na kumsogeza pembezoni kabisa mwa Barabara ambapo kulikua na mtaro mkubwa bila kuwaza mara mbili nilimsukumia huko.


“Watu watakuokota na kujua umepigwa kwakua ulikua umelewa.” Nilimuambia akiwa kule chini ambapo alianza kupiga kelele.


Nilikumbuka chupa za pombe ambazo nilikua nazo kwenye gari, nilizichukua ili nikitupa maiti yake nimmwagie mwili mzima ili ionekane kama vile alikua kalewa wahuni wakamvamia. Nilizichukua na kuzifungua kisha nikaanza kumwagia akiwa pale chini, moja niliivunja kisha nikaondoka eneo lile.


“Piga kelele watu watakuja kukuokota….” Nilimuambia wakati nawasha gari na kuondoka kwa kasi. Ile sehemu ilikua haijajificha sana na kwa usiku ule nilijua lazima kuna watu watapita hivyo kama akipiga kelele basi itakua rahisi kupata msaada. Sikutaka hata kusubiri, niliondoka moja kwa moja mpaka nyumbani, niliingia chumbani na kupanga vitu vizuri, nikaingia bafuni na kufuta damu zilizokua zimegandiana sakafuni kisha nikapanda kitandani kusubiria simu kuwa mke wangu kaokotwa.


Nilijua ni lazima atanitaja lakini kwa hali ilivyokua na namna nilivyokua mstaraabu, mtu wa Kanisani, kila mtu ananipenda nilijua moja kwa moja kuwa hata akisema ni mimi nimempiga hakuna mtu wa kumuamini. Nilisubiri simu mpaka asubuhi lakini sikusikia simu ya yeye kupatinaka, zaidi simu nilizokua napigiwa zilikua ni ndugu zake nao wakiulizia yuko wapi, hali hiyo ilizidi kunichanganya zaidi kwani nilihisi labda atakua kaumia sana au nilivyomsukuma alijigonga sehemu na kufia hapohapo.


Mpaka subuhi bado nilikua macho, sikupata hata lepe la usingizi. Asubuhi nilipigiwa simu na Mama yake, nilijua labda naye ananiulizia lakini hapana, alikua Hospitalini aliniambia kuwa mke wangu ameokotwa mtaroni.


“Najua unaenda kazini Baba lakini nimeamua kukuambia ili usipate wasiwasi, hali yake ni mbaya lakini Mungu atasaidia.” Mama yake aliniambia huku akilia.


“Mama mbona unalia, ni kitu gani kimempata mke wangu, naimbie….” Nilimuuliza nikionyesha kama nimepaniki, Mama mkweli alijaribu kunisihi nisipaniki na kuniambia kuwa yuko salama lakini name sikutaka kukubali.


“Mama mbona unaongea kama unalia?” Nilimuuliza. “Niambie mke wangu ni mzima?”


Nilimuuliza, alisisitiza kuwa ni mzima lakini nilipomuulizia kuhusu ujauzito nikamuulizia kuhusu mtoto wangu hapo alikaa kimya.


“Mama kuna nini? Ni kitu gani kimempata mwanangu?” Niliuliza kwa masikitiko, kusema kweli pamoja na unyama nilikua nimemfanyia lakini bado nilikua naumia, nilijua kuwa matendo yangu inawezekana yakaharibu maisha yangu yote nilikua na hamu sana na mtoto na sikujua ni kwanini nilimpiga mke wangu.


“Mwanangu, kila kitu kiko sawa wewe nenda tu kazini, nenda tu Baba hata ukija hapa hakuna kitu unaweza ku….” Mama mkwe alijaribu kuongea lakini alishindwa, alianza kulia hivyo nikaanza kazi ya kumbembeleza.


Nilimuomba anielekeze hospitali aliyokuepo lakini aligoma akiniambia hataki niende.


“Naona aibu mimi mwanangu, naona aibu sana, naona aibu….” Aliongea, alijikaza sana kutokulia lakini alishindwa alianza tena kulia. Hapo ndipo nilimlazimisha sana mpaka akakubali kuniambia alipokua. Nilikua napajua na hakukua mbali sana na kwangu, sehemu niyomuacha nilijua lazima watakao muokota watampeleka pale.


Niliwasha gari na kwenda kumuona Mama mkwe, alikua kakaa nnje kwenye chumba cha upasuaji.


“Kuna nini Mama?” Nilimuuliza, alianza kulia huku akiniomba msamaha, aliniomba sana msamaha huku akimlaumu binti yake.


“Mwanangu, kumbe wakati tunangaika na kumtafuta yeye anafanya starehe zake, yaani hajionei hata huruma. Karudia tabia zake za chuo amerudi tena kunywa pombe. Amepona lakini kaniulia mjukuu wangu. Mwanangu mwanao hayupo tena, mwanangu kamuua mwanao, nisamehe mimi kwakua ndiyo nilishindwa kumlea vizuri, nisamehe Mama!”


Mama alikua anaongea kama charahani huku akilia. Niliona kabisa kuwa msala aumemgeukia Jack. Mama yake alianza kufunguka tabia zake kipindi akiwa chuo, hata hazikua tabia mbaya sana ni mambo ambayo hata mimi niliyafanya lakini kwakua Mama yake alikua ni mtu wa dini walikua wanagombana sana.


Kwanza ilikua ni kuhusu kuvaa kwake na pili alikua anakunywa pombe kitu ambacho Mama yake alikua hapendi kabisa. Ingwa niliumia sana kumpoteza mwanangu lakini angalau nilipata ka ahueni kidogo kuwa msala hauwezi kunigeukia.


“Nisamehe mimi mwanangu, yaani sijui hata hii aibu naipeleka wapi? Baba zake nitawaambia nini, alishaniabisha kubeba mimba sasa hivi tena wakijua kuwa imetoka tena amepigwa na wahuni huko aklifanya umalaya na kunywa mipombe yake si nitaaibika mimi?


Kanisani mimi ni kiongozi, nawasema mabinti wa watu lakini wakwangu ndiyo hivi, kaniaibisha sijui nitafanya nini jamani….” Mama aliongea kwa uchungu sana, alikua anaumia kiasi kwamba nilijikuta na mimi machozi yananitoka.


“Pole kijana wangu, hivi kwanini wanawake tunakua hivi, mtu unapata kijana mzuri kama huyu lakini bado hatulii, ana kazi nzuri lakini hatulii, sijui nina laana gani mimi jamani, daaa!”


Aliendelea kulalamika, alikua anaongea kwa uchungu yeye ndiyo mtu wa kwanza kupigiwa na alikua hajamuambia mtu mwingine yoyote, alikua anaona aibu hata kuwaambia Kaka zake na Jack, alikua anaona kama kadhalilishwa yeye.


“Mama huyu ni mke wangu, nilikuja kwako kujitambulisha kwa heshima baada ya yeye kubeba ujauzito wangu, nilimuambia kuwa nitamuoa na kweli nitamuoa. Akitoka hapa nataka aje kwangu, nitamuuguza mimi mwenyewe kama mke wangu na sitamuambia mtu yoyote. Huyu ni mke wangu, kazi ya mume ni kumfichia mke wake aibu zake kwani ni aibu zangu mimi nitamhudumia mimi mwenyewe na kama mtu akiuliza basi alipata ajali ndiyo akawa hivyo. Mama mimi ndiyo nilimpa huu ujauzito na kukuaibisha sitakubali uaibike tena Mama.”


Nilimuambia Mama mkwe, nilijua kabisa kuwa, kama nikiziteka akili za Mama mkwe basi hakuna kitu ambacho angesema na kuaminika. Kwa namana Mama yake alivyokua anaongea nilijua kabisa kuwa hajamuambia kitu chochote. Nilijifanya mwema sana mpaka Mama mkwe alishangaa. Lengo langu halikua kumuoa bali nilijua kama nikimuacha akahudumiwa na ndugu zake basi ni rahisi yeye kuongea ukweli na kuniharibia sifa yangu.


****


Alikaa hospitalini kwa wiki mbili, alifanyiwa upasuaji mara mbili ndani ya hizo wiki mbili kwani kuna matatizo yalitokea wakati akifanyiwaupasuaji wa kwanza ambao ulikua ni mdogo tu ila huu wapili ulilazimika kufanyika mkubwa. Kilikua ni kipindi kigumu sana kwangu kwani nilikua sijielewei, nilikua na mawazo sana kila nikimuangalia hali yake nikiona kuwa mimi ndiyo nilikua nimemfanyia vile haikuingia akilini kabisa.


Hakua amemuambia mtuyeyote  kitu chochote kilichokua kimetokea, nadhani alikatishwa tamaa na maneno ya Mama yake ambayo alimuambia baada tu ya kupata nafuu.


“Umenivua nguo mwanangu, najuta hata wewe kuwa mtoto wangu, kwa ulivyonidhalilisha natamani hata hao uliokua unakunywa nao wangekuua kabisa nikazika.”


Wakati Mama yake anamuambia hivyo nilikua nipo hapo, nilimuona kanyong’onyea akashindwa hata kuongea. Hali yake haikua mbaya sana lakini baada ya Mama yake kumuombea kifo niliona kama moyo wake umepooza. Alibadilika, akabaki kimya, ni kama alikua kafungwa mdomo. Wakati wa kutoka hospitalini alitaka kwenda kwa kaka yake, wifi yake alikuja na kutaka kumchukua ili akamhudumie lakini Mama yake alikataa.


“Unataka akakuvunjie na ndoa yako? Huyu ana mwanaume wake, muache akaishi maisha yake!” Mama yake alimuambia, alikua na hasira iliyojaa chuki. Nilimuelewa kwani alikua akiamini kuwa binti yake alikua katoroka usiku kwenda kunywa pombe na huko akavamiwa na wanaume wakampiga mpaka mimba kutoka, alimuona mwanae kama mnyama na hakumpa muda wa kuongea. Ingawa kesi ilishafika Polisi kwani waliomuokota waliripoti lakini aligoma kuongea kitu chochote, aliwaambia alikua hakumbuki kitu.


Naamini baadaya kumsikia Mama yake akiongea vile alimuacha aamini alivyokua anaamini. Nilijifanya msamaria mwema nikamchukua na kuanza kuishi naye, hakusema kitu chochote, ingawa kila dakika nilikua namuomba msamaha lakini hakujibu kitu. Alikua ni mtu wa kulala tu, haongei na hafanyi chochote, kwa kumuangalia ni kama alikua kashakua taahira flani, sijui ni mawazo au mshituko lakini alikua anaboa na kutia hasira kuishi naye.


“Utakaa hivi mpaka lini, umeshapona unatakiwa kurudi kazini!” Nilimuambia, mwezi mmoja baada ya lile tukio alikua hajaongea kitu chochote. Ingawa nilishajitutumua na kumuambia kila mtu kuwa ninamuoa lakini niliogopa kwani alikua haongei kitu, haonyeshi hasira wala kuniambia kitu chochote. Alishapona lakini alikua hataki kurudi kazini, walishamuita zaidi ya mara tatu lakini aligoma.


“Siwezi kuishi na wewe hivi, kama huwezi kubadilika basi ondoka kwangu!” Nilimuambia kama kumtishia, lakini siku hiyo natoka kazini nilikuta kachukua kila kitu chake na kuondoka. Kesho yake nafika kazini naambiwa kaandika barua ya kuacha kazi.


“Nimempa likizo, naona hayuko sawa ila ongea naye, hii ofisi si yangu hivyo siwezi kumbeba muda mrefu!” Afisa utumishi aliniambia, nilijisikia vibaya kwani moja kwa moja niliona kama mimi ndiyo nimeyaharibu maisha yake.


Akili zilisharudi hivyo niliamua kwenda kuomba msamaha tena.


“Ndio kosa gani hili ambalo halisameheki tena?” Nilijiuliza bila majibu, nakumbuka ilikua ni usiku, niliamua kwenda kwake, nilijua bado alikua hajahama na kweli nilimkuta. Alinikaribisha vizuri tofauti na mwanzo, alionekana kuchangamka flani hivi, nilifika pale na kuanza kuongea.


Nilimpa risala ndefu nikijaribu kumuambia kuwa hana haja ya kukasirika vile na kuacha kazi, mimi niko tayari kumuoa.


“Shukuru Mungu uko salama, najua umempoteza mtoto wako kwa makosa yangu lakini niamini nikimuambia nimejifunza na nimeamua kubadilika. Kama ni ishu ya mtoto tutapata mwingine tena sasa hivi tukiwa ndani ya ndoa.” Nilimuambia lakini ndiyo kama nilikua nimeupalia mkaa, alianza kulia kama mtoto hivyo nikapata kazi ya kuanza kumbembeleza tena.


“Wewe utaoata mwingine lakini mmimi siwezi kuapta mtoto mwingine tena.” Aliniambia hukua kiendelea kulia.


“Kuna haja gani ya kuendelea kuishi kama siwezi kwua Mama tena, sina haja ya kufanya kazi, ni bora kufa. Kila mtu ananiona malaya, Mama yangu hanitaki anatamani ningekufa siku ile sasa kwanini nihangaike tena… hapana.” Aliongea kwa uchungu, sikumuelewa kabisa kwanini alikua anasema hivyo.


Kwanini umekata tamaa, kama ni mtoto tutahangaika na tutapata mwingine.” Nilimuambia, alinyanyuka kwa hasira na kubadilika ghafla, mwili wake ulikua mwekundu mpaka nikahisi anaweza kunidhuru, alikua kavimba.


“Tutapataje mwingine wakati walinitoa kizazi?” Aliniambia, nilikua sijui hilo hivyo nilibaki nauliza uliza.


“Unamaanisha nini kusema hivyo?” Nilimuuliza.


“Namaanisha umeharibu maisha yangu, kwenye oparesheni ya pili walinitoa na kizazi hivyo siwezi kuzaa tena na sitamani kuishi tena, sina sababu hata ya kufanya kazi.”


GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA—SEHEMU YA SITA


Nilimsikiliza Jack na kujikuta naanza kulia kama mtoto, nilihisi mamumivu makubwa. Katika maisha yangu yote nilikua siajwahi kumpiga mwanamke, nilikua na sababu nyingi sana za kumpiga mwanamke lakini sikuwahi kufanya hivyo. Nilijua kabisa kuwa ni kitu kibaya kumpiga mwanamke, lakini siku moja tu niliamua kumpiga mwanamke ambaya hakuwahi kunifanyia kitu kibaya chochote kile.


Nilimuomba sana msamaha lakini haikusaidia kabisa, aliniangalia tu bila kusema kitu chochote, kwa masaa mawili nilikua nikilia huku nikimuomba msamaha.


“Niko tayari kukuoa, nipo tayari kuishi na wewe, nipo tayari kwa chochote kile, sitaki tena mtoto, tutaadopt mtoto, tutafanya chochote lakini usiache kazi kwani nakupenda sana na maisha yangu bila wewe sioni kama ni maisha.”


Niliongea kwa uchungu sana, yeye hakuongea kitu chochote, hakulia wala kufanya kitu chochote alikua akiniangalia tu mwisho aliniambia.


“Sihitaji kuonewa huruma, kama ni kulia nilishalia sana lakini sihitaji kuolewa kwa kuonewa huruma! Hata kama nisingetolewa kizazi lakini sihitaji mwanaume kama wewe. Nimechoka na haya maisha, sihitaji kufanya kazi, sihitaji kitu chochote, ondoka na ukawe na maisha mema.” Aliniambia, niliona kama vile ananiaga, nilihisi kama vile kuna kitu kibaya ambacho anataka kujifanyia, nilimuomba sana asije kujidhuru lakini alionekana yuko sawa kabisa.


“Hahahahahah! Hapana, siwezi kufa kwaajili yako, nataka nikuone ukiteseka, nataka nikuone ukirudia kua chizi, hicho ndiyo kisasi changu, nataka nione maisha yako yakiangamia na nakuahidi yataangamia, siwezi kufa na kukuacha ukiishi kwa amani. Ondoka nyumbani kwangu kabla sijakufanyia kitu kibaya, nilikuacha unipige kama mjinga lakini sitarudia tena hilo kosa, sina kitu cha kupoteza hivyo ondoka kwangu!”


Mwanzo aliongea kama utani, niliona kama vile hawezi kufanya kitu chochote, ila ghafla alinyanyuka kwa hasira, aliingia chumbani kwake na kutoka na Panga, nilinyanyuka harakaharaka huku nikumsihi asijekufanya kitu kibaya. Lakini kabla ya kuongea alirusha lile panga, nilinyanyua mkono kulikwepa alinikata mkono na damu zilianza kutoka.


“Kaa mbali na maisha yangu mshenzi mkubwa wewe! Yaani umenipiga kama mbwa halafu unakuja kuniomba msamaha, utarudisha kizazi changu wewe shetani? Umemgeuza Mama yangu mpaka akaniona kama nina laana, yaani umefanya mpaka naonekana mshenzi naiaibisha familia yangu halafu unakuja hapa unajifanya kujali? Hunijui wewe mbwa ondoka, sina cha kupoeza mbwa kabisa, nisikuone kabisa katika maisha yangu!”


Aliongea kwa hasira sana hukua kinifuata, nilijua kuwa alikua hatanii na alikua hana chakupoteza, alikua kama chizi hivyo nilitoka mbio na kuingia kwenye gari kisha nikaondoka. Damu nyingi zilikua zikivuja kwani alinikata pakubwa, nilivua shati na kufunga mkono lakini damu zilizidi kunitoka, sikua na namna zaidi ya kwenda hospitalini.


“Vibaka, walikua wanataka kuninyang’anya gari lakini nimefanikiwa kuwadhibiti.” Niliwaambia, nilipatiwa huduma ya kwanza, kwakua walikua wakinijua kulikua hakuna haja ya kwenda Polisi.


*****


Siku tatu sikwenda kazini, nilikua naumwa na bado kichwa changu kilikua hakijakaa sawa, nilikua na mawazo sana kuhusu Jack nikiamini kuwa kachanganyikiwa na anaweza kuharibu maisha yake kwaajili yangu. Kichwa kilikua kinauma, nilikua na mwazo sana nikiwaza kumtafuta mtu wake wa karibu ili kumuambia kuhusu Jack, hali yake iliniumiza sana kwani ni mtu ambaye hakua mbaya kwangu, lakini kila nikiwaza kuongea na ndugu zake nilikua naogopa, alishaniambia nikae mbali na familia yake hahitaji msaada wangu kabisa. Roho ilikua inaniuma lakini nilikua sina namna ya kuweza kumsaidia kabisa.


Nilienda kazini nikijua kuwa ashaacha kazi, ile nafika tu nilikutana na Afisa Utumishi ambaye aliniita pembeni.


“Sijui ni kitu gani umekifanya lakini umensaidia sana, yaani amerudi kazini na jana kapata barua ya kupandishwa cheo, amekua Mkuu wa Idara, yaani kuumwa kwake imekua kama baraka kwake.” Afisa utumishi aliniambia huku akitabasamu. Ingawa nilikua najua kabisa alikua akimzungumzia nani lakini nilikua kama nimeshikwa na bumbuwazi, nilibaki kimya nikishangaa.


Nani huyo kapandishwa cheo? Nilimuuliza kwa mshangao kama vile sijui chochote.


“Jack, ndiyo Bosi wetu sasa hivi, anaandika barua ya kuacha kazi hukua anapandishwa cheo….” Aliendelea kuongea lakini sikumsikia, ni kama alikua anaongea na mtu mwingine kabisa. Nilijisikia vibaya, nilijisikia kuchanganyikiwa yaani kila kitu kilikua tofauti kabisa, nilimuacha Afisa Utumishi kasimama, nikaingia ndani kama chizi, kila aliyeniona alijua sipo sawa.


“Unaitwa kule ndani….” Ukiingia ofisini kwetu kitu cha kwanza unakutana na sehemu ya kusaini kwa kutumia vidole, pembeni yake kuna dada wa mapokezi ambaye kazi yake ni kuwaelekeza wageni, kupokea simu zote za ofisi na kuziunganisha na wahusika na kuulizia kama mtu flani yuko tayari kuonana na mtu flani. Basi nilipoingia tu ni kama alikua ananisubitia, aliniambia niingie katika ukumbi mdogo, niliingia huku bado nikitetemeka.


Huko nilikuta wafanyakazi wenzangu wa ngazi za chini wamekaa wanasubiria. Niliingia na kukaa, kama dakika tano hivi Jack alingia akiwa kaongozana na Mkurugenzi Mkuu pamoja na wakuu wenzake wa idara, wote tulisimama kwa heshima mpaka walipokaa. Kusema kweli sikusikia kitu chochote mpaka wanatoka, tulikaa kwa zaidi ya nusu saa ila sikusikia kitu, akili yangu ilikua ikiwaza maisha yangu ya pale, ningeishije na Jack kama Bosi? Kwa cheo chake kipya hakuna kazi ningeweza kuifanya bila kuruhusiwa nayeye, hakuna pesa ningeweza kuingiza bila kupata kibali chake, nilimuangalia nakuona maisha yangu yameisha.


Walitoka na kuondoka wakati natoka tena dada yuleyule aliniambia naitwa, alinielekeza ofisi ya Jack. Niliingia na kuona amekaa ananisubiria, tofauti na nilivyodhani kuwa atakua na hasira, ataniangalia kwa dharau au kitu kingine chochote kile lakini alinikaribisha vizuri, akaniambia anaamini tutafanya kazi vizuri kwakua sasa sisi si wapenzi hivyo akanisihi kuwa mimi nayeye ni kama hatujawahi kujuana hivyo nimeheshimu kama Basi wake.


“Kama hutaweza kufanya kazi na mimi niambie, uandike barua ya kuacha kazi kwakua hakuna namna nyingine zaidi ya hiyo!” Aliniambia kwa ukali kidogo, ni kitu ambacho nilikitamani lakini sikua na namna, nilishapitia maisha ya kutokua na kazi, kuhudumiwa na ndugu, nilikua naishi kwa shemeji yangu, yaani nilikua kama mtu aliyechanganyikiwa hivyo sikua tayari kabisa kwa hilo.


“Hakuna shida, mimi niko sawa nitafanya kazi nawewe vizuri na naamini kuwa hakutakua na shida. Yaliyotokea ni makosa yang…” Nilimuambia lakini hakua tayari kusikiliza alinikatisha.


“Nyamaza, hakuna kilichotokea, ulikua ni mpenzi wangu tumeachana mengine hayakuhusu, fanya kazi kama huwezi andika barua ondoka!” Aliniambia kwa hasira kidogo, nilibaki kimya bila kuongea chochote kwani nilijua sasa hivi ni Bosi wangu na kwa nafasi yake alikua na uwezo wa kunifukuza kazi wakati wowote, nilimsikiliza alivyokua anataka mwisho akaniambia nitoke kwani ana kazi nyingi za kufanya hukua kinisisitiza kuwa mimi nayeye hatujawahi kuwa wapenzi.


“Mambo ya afya yangu hayakuhusu kabisa, nikisikia nitasahau kama nilishawahi kukupenda, naamini unakumbuka kichaa changu? Hii kazi ndiyo kila kitu changu ukijaribu kuiharibu sitadili na wewe, safari hii panga litaanzia kwa Mama yako na kumalizikia kwa familia yako nzima, si unajua sina cha kupoteza!” Aliniambia huku akicheka lakini alikua akimaanisha.


****


Maisha ya pale kazini yalikua tofauti na nilivyodhani, Jack alikua Bosi wangu kweli, hakunibagua wala kunifanyia toafauti na wengine, alikua akinifanyia sawa, anaongea na mimi vizuri na safari za kikazi alikua akinipa sawa na wengine. Alikua ni Bosi mzuri na kila mtu alimpenda, kwanza aliwapa uhuru walipo chini yake wa kutimiza majukumu yao, alikua akielekeza zaidi ya kugombeza na kubwa zaidi alikua akitoa safari za kikazi kwa mzunguko.


Unapokua kazini kitu kikubwa kinachoingiza pesa zaidi ya mshaara ni safari za kikazi. Ofisi yetu ilikua na safari nyingi sana za kikazi lakini huko nyuma bosi ndiyo alikua akienda na watu wake wachache. Baada ya kuingia Jack aliweka utaratibu wa Mzunguko, aliitisha kikao na kutuambia kuwa safari zote ambazo hazimhitaji Bosi mwenyewe au mtu flani mahususi zitakua ni safari za kugawana, kutakua na zamu ya kila mmoja wetu. Kila mmoja zamu yake ikifika hata kama ni nnje ya nchini basi ni bahati yake hivyo ataenda na hataingilia.


Mwanzo hatukuamini ila baadaye ilikua ni kawaida na kila mtu alimpenda na kazi zilienda vizuri. Alikua na furaha na kulikua na tetesi kuwa yuko kwenye mahusaino na Mzungu mmoja ambaye ni rafiki yake anakuja kuja pale ofisini. Hali hiyo ilinitesa sana kwani alikua na furaha bila mimi, ingawa hakua akionyesha mahusiano yake wasiwasi lakini nilimfuatilia na kugundua kuwa ni kweli alikua kwenye mahusiano.


Nilihisi kuchanganyikiwa kwani mimi mwaka ulikua umepita bila kuingia kwenye mahusiano na mwanamke yoyote. Huku nyuma nilisikia Salma naye kaolewa, yaani nilichanganyikiwa zaidi kwani yeye alikua ni mtu wa kujionyesha, mara nyingi anapost picha kwenye mitandao namna alivyokua na furaha. Baada ya kuona hivyo nami niliamua kuingia kwenye mahusiano, niliingia kwenye mahusiano na dada mmoja ambaye alikua ni mtoto wa field ambaye alikuja pale ofisini.


Nilimuambia kuwa sijwahia kuwa kwenye mahusiano an nilimuonyesha upendo wa hali ya juu, nilimleta mpaka kwangu na akawa kama mke wangu. Lakini siku ya kwanza nataka kufanya naye mapenzi nilikua sina hisia kabisa, haikua kawaida yangu, nilimgusa kila sehemu lakini uume wangu haukuweza kusimama.


“Una shida gani Kaka mbona hivi?” Aliniulizia huku akinichezeachezea kuona kama nitashtuka lakini wapi! Akili yangu ilikua mbali sana, nilijisikia vibaya, niliona aibu na kila alivyokua anazidi kunishika ili kunishawishi nilijikuta nazidi kupandwa na hasira.


“Unanishikia nini mchawi mkubwa wewe!” Nilimuambia huku nikimsukuma, nilikua nimelala kitandani yeye akiwa juu yangu, nilimsukuma akadondoka chini. Alipiga kelele za maumivu lakini sikujali, nilinyanyuka na kuvaa nguo huko yeye akiwa bado pale chini.


“Kwani nimefanya nini mpaka unanifanyia hivi?” Aliniuliza, hapo ni kama aliupalia moto, nilimfuata na kuanza kumpiga mateke, bila kujali kama ni usiku au nini nilimpa nguo zake, nikamsukuma na kumtoa nikamfungia nnje.


Aliomba msamaha lakini sikutaka kumsikia, baada ya kuona kuwa sijali aliondoka zake. Nilijisikia vibaya sana huku nikiona kama maisha yangu yameisha, kwangu kile kitendo kilikua ni mara ya kwanza kunitokea hivyo nilihisi nina matatizo. Nilichukua simu yangu, nikaingia kwenye mitandao ya ngono, nikaanza kuangalia video za ngono ili kuona kama tatizo ni nini?


Wakati naangalia nilishangaa nasisimkwa, nilijisikia vizuri mpaka kufika kileleni. Niliona kama sina shida nikaamini kuwa yule binti ndiyo mwenye matatizo. Keshi yake nilikutana naye kazini, nikamfuata na kumuomba smamaha ana kuomba turudiane, kweli alikuja kwangu na siku hiyo nilifanikiwa kufanya naye mapenzi vizuri kabisa kwani nilikua najiamini. Lakini pamoja na kuweza kufanya naye tendo la ndoa nilijikuta nina hasira, niliona kama naye ni mwanamke hivyo si mtu mwema kwangu.


Bila yeye kunifanyia kitu chochote nilijikuta nankasirikia na kutamani kumfanyia kitu kibaya. Wakati tuko kitanda nafanya naye mapenzi, nilijifanya kukosea njia, nikafanya naye kinyume na maumbile, mwanzo alikataa lakini nilimbania chini na kumlazimishia, alipomaliza nilimpiga sana.


“Wewe si malaya tu, una tahamani gani? Umekuja kufanya field lakini unajirahisisha kiasi hicho, wewe ni malaya na hakuna kitu utanifanya?” Nilimtukana sana huku nikimpiga, kile kitendo kilinifanya kujisikia raha, nilijisikia kama mwanaume flani, yaani nilitamani niendelee kumfanyia mapenzi namna ile lakini nguvu nilikua sina hivyo niliishia kumtumkana nak umpiga. Baada ya kumaliza nilimfukuza na kumtoa nnje, nikamuambia kuwa simhitaji tena na asinitafute tena.


Aliopndoka huku akilia akiniuliza kama alikua kanikosea nini lakini mimi hata sikujali. Baada ya yeye kuondoka mimi nilitoka kwenda club, hayakua mambo yangu, tangu kupata matatizo nilishaacha pombe lakini siku hiyo nilikunywa tena sana na nilijisikia vizuri. Kesho yake niliamka vizuri na kwenda kazini, nikiamini yule binti hatanisemesha nililpofika kazini tu ni kama alikua ananisubiria.


“Kaka naomba tuongee, naomba sana unisikilize kama kuna kitu nimekukosea naomba sana.” Aliniambia huku akitaka hata kulia, kusema kweli sikutegemea hilo,. Wakati ananiomba msamaha akili yangu ilikua kwa Salma, nilikumbuka namna ambavyo alikua ananifanyia vituko lakini mimi ndiyo naishia kumuomba msamaha, nilikumbuka namna ambavyo nilimfumania na mwanaume mwingine, akaniambia hanitaki mimi ndiyo nikapiga magoti.


“Kumbe ni raha namna hii….” Nilijikuta najisema bila kujali kama binti wa watu kasikia au la. Nilimuita mpaka ofisini kwangu na kumuambia akae.


“Una shida gani? Unataka nini?” Nilimuuliza lakini alibaki kaduwaa.


“Ondoka kama huna chakuongea, nina kazi nyingi sana, nilimuambia huku nikimnyanyuakua kutaka kumtoa kwa nguvu. Sikutaka kuendelea kuongea lakini wakati nimemshika namtoa mara mlango ulifunguliwa, nikiwa bado nashangaa Jack akaingia na kunikuta nimemshika yule binti namvuta kwa nguvu.”


“Kuna nini hapa? Binti anakusumbua? Vipi anataka kukufanyia kitu kibaya?” Jack aliuliza kwa hasira kama vile anataka kunipiga.


“Unataka kumbaka binti wa watu, wewe mshenzi nini?” Aliendelea kuongea kwa hasira.


“Niache!  Niache! Niahe! Niache! Utaniua niache!” Yule binti naye alipiga kelele kuona kama nilikua nikimlazimishia kitu. Nilimuachia huku nikitetemeka kwani nilikau kama nimefumaniwa vile.


GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA—SEHEMU YA SABA


“Mmenipangia, hii ilikua ni mipango yenu kabisa ili kuja kunidhalilisha! Yaani umekaa na kimwanamke chako huko unakuja hapa kusema nimebaka!” Nilijikuta naanza kupiga kelele, kwa akili yangu niliamini kabisa kuwa Jack alikua amepanga na yule binti. Tofauti na nilivyodhani labda Jack atanigeuzia kibao haikua hivyo, alimshika yule binti mkono na kutoka naye nnje, sijui waliongea nini lakini mimi hakuniongelesha kitu chochote, ni kama alinidharau.


Nilitoka ofisini kwa aibu na kwenda nyumbani, nilikua na hasira sana na hasira zangu zote zilikua ni kwa wanawake, siku hisikulala kabisa hata kesho yake si kwenda kazini nahata sikujali chochote. Kesho yake mchana wakati naangalia kwenye mitandao ya kijamii nikaona tangazo la Massage (kukandwa), sijui kwanini lakini niliamua kwenda.


Ilikua ni mara yangu ya kwanza kufanyiwa hivyo na niliamini kuwa kama nikifanya hivyo basi nitakua vizuri. Kweli yule dada alinifanyia vizuri baada ya kumaliza aliniuliza.


“Utaweza kujisugua mwenyewe au nikusaidie….” Nilikua naenda kuoga na wakati huo nilikua nimefunga kitaulo tu kiunoni, nilishangaa kwanini ananiuliza hivyo.


“Inamaana unataka kuniogesha?” Nilimuuliza.


“Ndiyo, hakuna shida au unaona aibu?” Nilibaki kimya bila kuongea kitu chochote, nilimuangalia kwa matamanio nikavua kile kitaulo na kumuacha aniongeshe.


“Kuna huduma nyingine unataka?” Aliniulzia,


nilikua simuelewi lakini namna alivyokua anaongea ananishikashika niligundua anataka nini.


“Kama ipo sawa bei gani?” Nilimuuluiza.


“Una elfu hamisini?”


“Ndiyo, lakini sitaki kufanya hapa, sitajisikia vizuri kama upo tayari nikitoka hapa tukutane sehemu.” Nilimuambia, hata hakubisha, hata hakujali kama yuko kazini, nilitoka pale tukaondoka naye, nikamchukua mpaka nyumbani kwangu, mwanzo alisita lakini nilimbembeleza mpaka akingia.


Tukaingia kwenye kufanya mapenzi nilijikuta tu napata hasira, baada ya kumaliza nikaanza kumuingilia kinyume na maumbile, mimi nilidhani kama namkomoa lakini yeye alikua kazoea na aliona sawa.


“Utaongeza pesa!” Aliniambia, nilijikuta nashangaa, ingawa nilikua na pesa ya kumpa lakini nilikataa, aligoma kufanya mapenzi kinyume na maumbile bila mimi kumuongezea pesa, palepale nilimvamia na kuanza kumpiga, nilimpiga sana mpaka kuvuja damu kisha nikamuingilia kinyume na maumbile na kumfukuza kwangu.


Alipoondoka nilijisikia raha sana.


“Hii ndiyo dawa ya hawa Malaya, hakuna wa kunisumbua tena, yaani akileta ujinga ni kupiga wanawake wote ni washenzi!” Nilijiongelesha wakati anaondoka, ingawa kuna kitu kilinifanya kujisikia vibaya lakini kuna namna nilifurahia kitu nilichokifanya, kuna namna nilikua najisikia vizuri na kuona kuwa yalikua ni makosa ya wanawake na sio mimi.


Baada ya hapo hiyo ndiyo ilikua kazi yangu, kununua wanawake nawalazimisha kufanya mapenzi kinyume na maumbile wakiakataa nawapiga. Wakati mwingine hata mwanamke akikubali nilikua nampiga, kwangu ilikua ni kama kufanya mapenzi mwenyewe, kumnyanyasa mwanamke na kumdhalilisha ilinipa raha ya ajabu kuliko tendo la ndoa lenyewe. Nilibadilisha wanawake kama nguo na hata siku moja sikujali hisia zao. Kwangu mimi niliona kama ni kitu cha kawaida. Baada ya kuona kuwa mtaani najulikana na karibu kila mwanamke nilihamia Facebook.


Huko ndipo ilikua ni rahisi kwangu kupata wanawake, nilikua naingia naangalia mdada mzuri kisha namtongoza, akiniomba pesa namtumia na kujifanya kama nimetoka kuumizwa na sasa hivi nataka mwanamke wa kuoa. Ilikua ni njia nzuri sana kwangu kwani muda wote nilikua online, wakiniomba pesa nawatumia ili tu waniamini na wao nawaomba picha za uchi wananitumia.


Baada ya hapo tunapanga kuonana na nikikutana nao nakua nataka kufanya nao mapenzi kinyume na maumbile. Kwakua wapo kwangu wanakua hawana namna, nilikua nadili sana na wanafunzi wa chuo ambao ndiyo hupenda kuomba pesa na kuamini kirahisi. Hiyo tabia iliendelea ikawa ndiyo maisha yangu, nikawa mtu wa kutuma nauli, pesa zangu zote ziliishia kwenye wanawake wa mitandaoni, nilikua nakaa mpaka saa nane usiku nachart na wanawake zaidi ya mia mbili kwenye simu kila mmoja akiamini kuwa nampenda na nitamuoa.


Nilizoea hiyo hali kiasi kwamba hata mahusiano ya kawaida kwangu ilikua ngumu, nilikua sina mwanamke zaidi ya wanawake wa kwenye mitandao na kila wiki nilikua nakutana na wanawake wawili wapya, nikishatembea naye nilikua sirudii kabisa, nikikutana naye kimwili nahakikisha namfanyia kitu cha ajabu ili asirudi kwangu tena. Walikua hawawezi hata kunishitaki kwani wengi wao wanakua washanitumia mapicha ya uchi hivyo nawaambia kabisa kama ukimuambia mtu yeyote basi nitazivujisha.


Nilibadilika sana, nikawa ni mtu wa kukaa nyumbani, sina mahusiano yoyote, ndugu zangu wakiniuliza kuhusu kuoa naishia kuwapiga kalenda, walinisumbua sana huku dada zangu wakinitafutia wanawake lakini nawakataa. Nakumbuka kuna wakati Dada yangu aliniunganisha kwa mtoto wa rafiki yake, alikua ni mzuri sana binti wa miaka 23 ndiyo kamaliza chuo, nilikua simtaki kwani nilikua sina haja naye lakini Dada alinisisitiza sana hata kuonana naye.


“Muone tu kwanza utaamua mwenyewe!” Aliniambia, kwakua ni mtu nilikua namheshimu nikawa sina namna, nilikubali kukutana na yule binti kuongea. Siku ya kwanza kumuona tu nilihisi kuchanganyikiwa, yule mtoto alikua ni mzuri, alikua kaumbika na alikua na nidhamu sana.


“Huyu nitamuoa, najua nikimuoa huyu wale Malaya wote walionipotezea muda watakuja kwangu kunipigia magoti!” Alinivutia sana lakini huwezi amini kila nikimuangalia nilikua nawaza kulipa kisasi, nilikua naamini kama ulimwengu mzima ulikua umenikosea hivyo natakiwa kuwalipia kisasi na nilijua kama nikimuoa huyo binti basi wote wataumia.


Siku hiyo nilikua tofauti kabisa niliongea na huyuo binti mambo mengi, nilimuambia kuhusu mimi kuwa nilishaingia kwenye mahusiano yakaniumiza hivyo nilikua nataka mtu siriasi na si mtu wa kunichezea, aliniambia kuwa yeye hajawahi kuingia kwenye mahusiano kwani katoka kwenye familia ya kilokole hivyo amejitunza kwaajili ya mume wake, aliniambia kabisa kuwa hawezi kukutana na mimi kimwili mpaka pale ambapo tutaingia kwenye ndoa.


Nilimuambia sawa hata mimi nataka hivyo basi tuliongea mengi na huo ndiyo ukawa mwanzo wa mahusiano yetu. Wazazi wake walikua wananijua lakini baada ya kama miezi miwili hivi ya kujuana ndipo alinitambulisha kwao rasmi kama Mchumba wake. Nilifurahi sana kutambulishwa, nilijisikia kama mtu na kweli yule binti alinifanya nijihisi nina furaha. Alikua anakuja kwangu, anakua huru kunipikia na mambo mengine kasoro kufanya tendo la ndoa tu.


Pamoja na kuwa naye lakini sikuweza kuacha mambo yangu, bado nilikua nabadilisha wanawake kama nguo na nilikua bize kwenye mitandao. Simu yangu ilikua na Password kama mia hivi kwani sikutaka ajue chochote kuhusu mimi. Siku moja akiwa kwangu sijui kilitokea nini wakati nachart nikawake simu chini nikatoka kidogo, kurudi namkuta kashikilia simu yangu anaangalia meseji zangu, huwa sifuti kitu chochote hivyo aliona kila kitu.


Nilimuangalia alivyobadilika, alikua mwekundu machozi yanamtoka kama maji, nilipiga magoti kumbembeleza sana nikamuambia sio kama hao wanawake naonana nao lakini ni kwakua tu nilishazoe kipindi siko naye, nilimuomba msamaha na kumuambia kuwa nitaacha lakini hakua tayari kunisikiliza, aliondoka bila kuaga na kuniacha nikiwa sina chakufanya.


Baada ya kuondoka nilimuomba sana msamaha, wiki mbili nilikua namuomba msamaha, naomba hata turidiane naye lakini hakua tayari, kama unavyojua wanawake baada ya kuona nazidisha kuomba msamaha alilainika na kunisamehe. Nilitaka kuharakisha mambo ya ndoa lakini yeye hakutaka, aliniambia anataka kunichunguza kwanza kama nimebadilika au la, kauli hiuyo iliniumiza na kuona kama anataka kuniacha kwani huko mwanzo yeye ndiyo alikua analazimishia sana mambo ya ndoa.


Siku moja alikuja kwangu kunisalimia, alitaka kushika simu yangu lakini nilimkatalia. Alikasirika na kuanza kunitukana huku akitaka kuondoka. Nilimshika na kumvuta kitandani huku nikimpiga makofi.


“Hivi unajiona nani wewe mbwa? Unajiona nani nakuambia? Nakuuliza unajiona nani? Kwanza mtu mwenyewe sikukutongoza ni Mama yako tu amekuuza kwangu halafu unajifanya mjanja! Niliongea huku nikimshika na kumvua nguo kutaka kufanya naye mapenzi, nilimuambia hata akipiga kelele kila mtu anajua ni mpenzi wangu na haitasaidia. Nilimbania chini huku nikijaribu kufanya naye mapenzi lakini huwezi amini nilishindwa kufanya naye mapenzi kabisa.


Uume wangu ulikua hausimami kabisa, ni binti mzuri lakini nilijaribu kufanya nikashindwa. Tulisumbuana sana lakini kwa aibu ya kuona kuwa nimeshindwa kufanya mapenzi nilimuacha akaondoka zake lakini sikua na amani kabisa. Nilitafuta mwanamke mwingine siku hiyohiyo nikajaribu kufanya nikafanikiwa, lakini katika kufanya mapenzi niligundua kitu kimoja, nilikua siwezi kufanya mapenzi kwa njia ya kawaida.


Kila nikifanya mapenzi njia ya kwaida uume wangu ulikua unalala, msisimko kulikua hakuna kabisa lakini kama nikimshika mwanamke makalio tu basi najisikia vizuri na kila kitu kinarudi kama kawaida. Mwanzo niliona kama kawaida kwakua kila mwanamke niliyekutana naye alikua ni wale wa kununua ambao walikua tayari kufanya chochote. Lakini nilipojaribu kuingia kwenye mahusiano na kutaka kufanya mpenzi kwa njia ya kwaida nilishindwa kabisa.


“Una matatizo gani?” Dada mmoja aliniuliza, alikua ni mfanyakazi Katika Benki moja hivi ambaye tulikua kwenye mahusiano kwa miezi kama mitatu hivi bila kukutana kimwili. Hata sijui, sijui leo ikoje….” Nilimuambia huku nikijaribu kumshika makalio ambapo ile kupitisha mkono wangu tu nilihisi kusisimkwa.


“Paaaaa!” Nilishangaa kaninasa kofi la usoni, kabla sijakaa sawa alinisukuma pembeni kwanguvu sana nikadondokea chini.


“Unataka kufanya nini, ndiyo nini kunishika hivyo makalio yangu!” Yule dada aliongea kwa hasira huku akinyanyuka.


Alikua kama kanitibua, nilihisi kama kanidhalilisha hivyo nilinyanyuka na kutaka kumfuata kumpiga, nilimmrukia pale kitandani huku nikimtukana.


“Malaya mkubwa wewe yaani unanisikuma mimi hivi unanijua!” Nilimuambia, lakini ni kama aliniona, alinikwepa sijui hata alinikwepaje, alisogea pembeni na kunyanyuka, mimi nilikua nimedondokea kitandani, hakunipa hata muda wa kunyanyuka, nikiwa pale chini alichukua kistuli kidogo cha kukalia na kunitwanga nacho mgongoni. Alinipiga kwa nguvu kiasi kwamba nilishindwa kunyanyuka.


“Mshenzi mkubwa wewe, yaani uhanithi wako ushindwe mwenyewe kufanya mapenzi halafu unataka kunipiga, hunijui wewe, sijwahi kupigwa na mwanaume yoyote na hakuna Mbwa hata mmoja atawahi nigusa!” Aliniambia huku akichukua nguo zake na kuanza kuvaa, wakati nikiwa bado naugulia maumivu nilianza kumtukana kuwa ni mbaya, malaya hana akili ndiyo maana nimeshindwa kufanya naye.


“Mbona nikiwa na wanawake wengine naweza, wewe unanuka huna akili ndiyo maana!” Nilimuambia, hata hakujali, aliendelea kuvaa zake taratibu huku akinigeuzia jicho kuniangalia namna nilivyokua naugulia mgongo. Nilijitahidi kidogo kujinyanyua ili kiumfuata, sikutaka kukubali kushindwa, nilitaka kumlipizia kisasi kwa kunipiga lakini niafadhali ningeacha.


Wakati nanyanyuka alikua ananiona, ile namsogelea ili kumvamia aliniwahi na teke kali katikati ya miguu. Aisee, hakuna maumivu ambayo nilishawahi kuyapata katika maisha yangu kama hayo, yaani nilihisi kama najifungua maana nilipiga kelele nikainama chini. Alivaa taratibu na kuondoka bila mimi kujua. Nilikaa pale chini bila kunyanyuka kwa masaa mawili mgongo unauma na hapa katikati kwenye zana zangu napo kunawaka moto.


Yalikua ni maumivu makali ambayo yalinifanya nisitamani kuonana na yule mwanmamke tena. Siku hiyo sikutoka kabisa, hata kula sikula mpaka asubuhi, yeye ndiyo alikua wakwanza kuniamsha, alinipigia simu kuniulizie naendeleaje.


“Wewe ni mshenzi nisikukamate!” Nilimuambia baada ya kupokea simu yake. Nilimtukana sana lakini yeye muda wote alikua amekaa kimya, mwisho aliniambia maneno ambayo yalinichoma kuliko hata maumivu ya lile teke.


“Utafikiri mwanaume anaongea, vitisho vyote hivi lakini nikivua chu*** unanywea!” Alikata simu na sikumtafuta tena, nilimblock na hata nikikuata naye njiani nilikua naona aibu, nilikua sitaki kuongea naye.


Maisha yaliendelea, tabia yangu ya umalaya sikuiacha kwani ilikua rahisi sana kwangu kupata wanawake katimka mitandao. Kwa muda sasa nilikua siwezi kutongoza kawaida, nikawa ni mtu wa mitandao masaa 24, niliacha kununua malaya na muda mwingi nikawa nautumia kwenye ngono ya mitandao. Kwakua mara kwa mara nikikutana na mwanamke nikijaribu kufanya naye mapenzi kawaida nashindwa hivyo wengine kuishia kugombana kwani hawataki kufanya mapenzi kinyume na maumbile niliacha kabisa kukutana na mwanamke.


Kila nikichart na mwanamke kwenye mitendao nataka tufanye phone sex, hiyo nilikua nafanya vizuri najichu ampaka nafika kileleni,. Niliizoe hiyo hali mpaka kila mwanamke nikipanga naye kukutana nilikua natafuta sababu. Walikua wananiamini kwasababu, kwanza nilikua nahonga sana, yaani mwanamke akiniomba pesa namtumia ili tu awe huru kunitumia picha zake za uchi. Pili nilikua naongea nao mpaka usiku, yaani hata video call ya saa nane usiku mimi nafanya hivyo mwanamke nikimuambia kuwa nampenda yeye tu na sina mtu mwingine sijaoa ananiamini hapohapo.


Kelele za kuoa zilizidi lakini hata sikujali, akili yangu ilikua ni kwa wanawake wa mitandao. Niliona kama ndiyo maisha yangu nilikaa kama mwaka hivi bila kukutana na mwanamke wa kawaida na niliona sawa. Nilikua najichua sana yaani nikiamka ausbuhi, nikiwa kazini mchana naweza kuingia chooni na simu yangu nikaanza kujichua na nikitoka kazini usiku nabadilisha tu wanawake wa kuwapigia simu kwwenye whatsapp wananiyonyesha maungo yao mimi najiridhisha.


Kila mwanamke niliyekua nikichart naye ilikua ni lazima kumuomnba picha za uchi, simu yangu ilikua imejaa mapicha ya wanawake zaidi ya mia tano ambao hata siwafahamu. Kuchart kwenye mitandao ilikua kama ndiyo kazi yangu, sikutamani hata wanawake wa kununua. Siku moja nikiwa kazini alikuja mwanamke mmoja, Salome (sio jina lake halisi) sikua nikimkumbuka, alinifuatilia mpaka kuja ofisini kwangu, mwanzo nilijua kama ni mteja lakini haikua hivyo.


Alikua ni mmmoja wa wanawkae niliokua nachart nao kwenye mitandao na mara nyingi alikua anaomba kuonana na mimi huku namzungusha. Kumbe alifuatilia mpaka kunipata, kusema kweli nilikua hata simkumbuki, nilikua na wanawake wengi na mara nyingi nawajibu kile wanachotaka kusikia na si kuwaangalia usoni.


“Imanaaana umenisahau wakati nishakutambulisha mpaka nyumbani kwetu, yaani mpaka Mama yangu anakujua, nilishakupa simu uongee na Mama yangu kweli hunikumbuki?”


Aliongea hukua kianza kulia, nikajua huu ushakua msala kwani suala la kutambulishwa kwa wanawake, kuongea na Mama wakwe ni wengi nilishaongea nao, wanawake wengi ukishatuma pesa mara mbili basi wanaona kama unawapenda, kwakua nachart nao mpaka usiku basi wanaona kama nawapenda hivyo suala la kuongea na ndugu ambao hata siwajui lilikua la kawaida sana kwangu.


Ili kuepusha kelele nilijifanya kama nimemkumbuka na kujifanya kama nilikosea.


“Aisee unaonekana mzuri sana uso kwa uso kuliko kwenye picha, yaani nahisi hata marafiki zako washawahi kukuambia, sikujua kama ni wewe….” Nililazimika kuzuga, wakati akiwa bado analia nilimfuata na kumkumbatia, nilianza kumsifia namna alivyokua ananukia, na kumuambia nashukuru kanitafuta na mambo kibao mpaka akasahau kama nilikua simkumbuki.


“Nimekuja kukaa kwako kama ulivyoniahidi…” Aliniambia.


“Ahadi gani tena jamani?” Niliwaza nikiwa sikumbuki kitu chochote.


“Nyumbani wanataka niolewe na mwanaume ambaye simpendi, nimewaambia kuhusu wewe hawataki wanasema ni kwanini huji, aisee nakupenda Sana G, nimekuja moja kwa moja maana nikikaa nyumbani ndoto zetu hazitatimia. Nimekuja si uliniambia niache kazi, niliongea na Afisa Utumishi akakubali waniandikie kama nimepunguzwa kazi ili niweze kupata NSSF yangu.”


Hapo ndipo nilichoka kabisa, akili ilikua haisomi, kusema kweli nilikua sijui kama nilishamuahidi hivyo, nachart na watu wengi na ni mara nyingi sana najibu meseji za wanawake bila kuzisoma vizuri lakini nyingi zilikua ni za mapenzi kama umekula, nimekumiss na si mambo ya kaucha kazi, kusema kweli nilichanganyikiwa kwani hata mwanamke mwenyewe nilikua simjui lakini alikua kaacha kazi kwenye kampuni moja kubwa sana kwajaili ya kunifuata mimi mume wake, mtu ambaye hata nilikua sijawahi kumuona, nilichoka kabisa.


GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA—SEHEMU YA NANE


(ILIPOISHIA SEHEMU YA SABA; Baadaya kuachana na Jack George anaachana kabisa na wanawake, anakua ni mtu wa mitandao kuanngalia picha za uchi na kudanganya wanawake kwenye mitandao kuwa atawao. Ghfla anashangaa Binti anakuja ofisini kwake, alimuahidi kumuoa na kaacha kazi kwajaili yake, unafikiri nini kitatokea? ENDELEA…)


Salome alikua kama mtu aliyechanganyikiwa, aliniambia hahitaji kitu chochote kile katika maisha yake zaidi ya kuwa na mimi. Dakika mbili tu alianza kunionyesha meseji nilizokua nikichart naye, kweli niliziona na ni mimi nilikua nikimjibu mambo ambayo hata sikuyajua. Ni kweli nilimuambia nitamuoa, nilimuambia aache kazi kuja kuishi na mimi na nilimuambia mambo mengi sana lakini sikumaanisha.


Nia yangu ilikua ni yeye kuendelea kunitumia picha za uchi na sikua hata na mpango wa kuja kuonana naye achilia mbali kumuoa na kuishi naye kama mke wangu.


“Dada yako ndiyo kanielekeza kwako, nilimtafuta akaniambia kuwa unafanya kazi hapa naweza kuja….” Aliniambia, ni kama alizidi kunichanganya kwani kumtaja Dada yangu ilimaanisha kuna mambo mengi ambayo walishaongea kuhusu mimi. Dada yangu alikua anataka mimi kuoa na nina ihakika angefanya kitu chochote kile ili mimi kuwa na mwamnamke.


Nilitaka kuongea naye na kumkataa palepale ofisini lakini nilijua isingesaidia, kwa hali yake angeleata vurugu na tusingeelewana kabisa. Nilirudi naye nyumbani kishingo upaende, sikua na mwanamke nyumbani hivyo sikua na kitu cha kuhofia, nilijua tu baada ya muda ataondoka mwenywe lakini haikua hivyo, siku ya kwanza, siku ya pili wiki mwezi na mwaka uliisha huku bado nikiishi na Salome.


Mwanzo niliona shida lakini baaadaye nilizoea, alikua ni mtu mzuri, binti mwenye akili ya maisha lakini alionekana kutendwa sana kwenye mahusiano, aliumizwa sana kiasi kwamba kuna wakati alikua anaweza kukaa analia mwenyewe hukua kitetemeka kama vile kamwagiwa maji ya baridi.


“Wanaume, wanaume si watu wazuri, niambie G wangu kuwa hutaniacha, niambie kuwa hutaniacha.” Aliniambia mara kwa mara na mimi nilimuambia kuwa siwezi kumuacha kwani nampenda sana.


Nadhani hali yake ilinikumbusha hali yangu, mimi pia nilikua nimeumizwa, maumivu ambayo yalinifanya kuchukia wanawake, yalinifanya kuwa na hasira na kufanya mambo yana kishenzi.


“Inamaana hutaki kufanya mapenzi na mimio au mimi ni mbaya namna hiyo?” Siku hiyo Salome aliniuliza, ulikua umepita mwaka mzima bila kukutana kimwili, tulikua tunaishi pamoja kama mke na mume lakini nilikua sijawahi kumgusa. Si kama nilikua sitaki bali nilikua siwezi, mwanzo nilikua nikimdanganya kuwa nasubiri tuzoeane, nikamuambia kuwa ninaumwa lakini siku hiyo aliingia bafuni na kunikuta nikijichua.


Alilia sana na kudhani kuwa namdharau, namuona kama si mwanamke ndiyo maana naishi naye kama dada yangu huku nikijichua. Ni hali ambayo hata mimi iliniumiza sana, baada ya kuonana na Salome niliamua kubadilika,. Nilipunguza kutumia muda mwingi kwenye mitandao na kuwa nayeye. Ingawa sikuacha kabisa lakini nilipunguza sana kwani nilikua na hamu sana ya kutengeneza familia lakini ni kitu ambacho hakikuwezekana.


Nilikua nikitamani kufanya naye mapenzi lakini kila nikimgusa hisia zilikua mbali, nilishindwa kabisa. Kuna wakati nikimuangalia makalio yake nilikua nikisisimkwa lakini nilikua namheshimu sana, nilikua sitaki kumuingiza katika hiyo dhambi pia hata mimi nilitaka kuacha. Nilijua kama nisipoacha nikianza kufanya naye basi utakua ni mchezo wangu wa kila siku. Siku hiyo alilia sana ndipo nikaamua kujikaza ili nifanye naye mapenzi.


Kusema kweli nilishindwa, nilijaribu kila kitu hata kumshika makalio lakini bado nilishindwa. Akili yangu ilishahamia kwenye kujichua na uume ulikua umelegea tu. Huwezi amini hata kwenye kujichua nako ilikua ngumu, yaani kuna wakati nilikua nikijichua lakini nuume hausimami au sifiki mwisho.


Niliona kama maisha yangu yameisha, nilijiona kama nimekufa, kila kitu kilisimama kwangu. Kushindwa kabisa kufanya tendo la ndoa kulinipa hasira nyingi sana kulinipa mawazo, kila nikirudi nyumbani nilikua mtu wa kutukana, mtu wa kumdhalilisha sana yule binti.


“Huna akili wewe, ulikuja na kunikuta na maisha yangu, nina furaha umekuja kuniloga. Wewe ni mbaya, sura mbaya kwanza unanuka ndiyo maana siwezi kufanya mapenzi na wewe, mbona nikiwa na wanawake wengine naweza kufanya vizuri, kwanini kwako nisindwe!”


Nilimtukana, yalikua ni maneno yangu ya kila siku kwa Salome, yeye alikua akiishia kuomba msamaha lakini hakuondoka. Kichwani nilijua kabisa hajanikosea kitu chochote, lakini niliamini kua, kama nikimuacha akahisi kuwa tatizo ni langu basi ataondoka na kunitangaza huko mitaani kitu ambacho sikua tayari kukiona.


“Nitakakuja kwenu, nataka kuja kukuoa, unajua kuna kitu nimekaa nikafikiri, naamini hii hali imekuja kwakua sisi si wana ndoa,. Hatujahalalisha mahusiano yetu. Najikuta nakua na wasiwasi kufanya mapenzi na mwanamke ambaye si mke wangu, naomba tuingie kwenye ndoa labda kila kitu kitabadilika.” Nilimuambia siku moja, nilifikiria sana na kuona kama nitaaibika, nilishajau hakuna uwezekano wa kupona kwani nilishaanza kutumia dawa za nguvu za kiume nyingi tu lakini sikuona mabadiliko yoyote.


“Siwezi kufa kwa aibu, hapana, mimi ni mwanaume lazima niwe na mke, kwa umri wangu ni bora kua na mke kuliko kuaibika kuwa sina nguvu za kiume!” niliwaza, lakini Salome niliona kama kabadilika, mwanzo wakati anakuja kwangu alikua kama chizi, nilikua namfanyia mambo mengi mabaya lakini alikua anavumilia na kila siku alikua ni mtu wa kuniambia kuwa anataka ndoa na mimi, alitaka niongee na ndugu zake na alitaka niende kwao kujitambuilisha.


Wakati huo nilikua naringa ila siku nilipomuambia kuwa nataka kumua aliisita kidogo.


“Mbona haraka hivyo?” Aliniuliza, lilikua ni swali la kawaida ambalo mara nyingi mimi ndiyo nilikua nikimuuliza alipokua ananiambia kuhusu ndoa lakini aliponiuliza nilihisi kama kasema hapana, hanitaki mimi si mwanaume, nilijikuta napaniki na kuona kama ananiacha, sijui ni kitu gani kilitokea lakini nilinyanyuka harakaharaka nikachukua simu yake nikamuambia aifungue password lakini aligoma, hapo ndipo alizidi kunichemsha kwani nilihisi kabisa anachepuka na ana mwanaume mwingine.


Huko mwanzo hakua msiri kihivyo na sikua nikimfuatilia kwani niliona kama hana pakwenda, mwanamke mwenyewe amejileta kwangu ni kwanini nihangaike naye. Aligoma kufungua simu nikaanza kumpiga, nilimpiga sana lakini aligoma, kila nilivyokua nikimpiga na kumtukana ndivyo ambavyo nilijisikia vizuri, nilijisikia mwanaume na nilitamani kuendelea kumpiga.


Yeye aliishia kuomba msamaha, lakini katika kupigana alinisukuma kidogo nikadondoka hapo ndipo alipata upenyo na kutoroka, alikimbia, alirudi na Polisi na kuchukua vitu vyake, wakati anaondoka aliniambia kua hawezi kua na mimi kwani ana mimba ya mtu mwingine na mimi si mwanaume.


“Tafuta msaada…” aliniambia, nilijisikia vibaya, ingawa hakuongea kwa nguvu watu wakasiikia lakini namna alivyoniacha ni kama alikua ananionea huruma, ni kama alikua ashanichoka muda mrefu naye alikua akitafuta sababu ya kuniacha.


“Kama huyu naye akniacha mimi nitakua mgeni wa nani?” Niliwaza wakati anaondoka si kama nilimpenda Salome lakini nilimuona naye kama mtu aliyechanganyikiwa, mtu mwenye hamu sana ya mwanaume hivyo nilimini kuwa atanivumilia pamoja na matatizo yangu. Aliniacha nikiwa na huzuni sana, nilishindwa hata kuenda kazini, nilijisikia vibaya.


“Mbona nilikua kijana mzuri, nilikua na nguvu zangu za kiume nyingi tu, nilikua napendwea na wanawake, nilikua na maisha yangu nini kimebadilika?” Niliwaza sana bila kupata majibu, nilianza kujichukia, nilianza kuyachukua maisha na kutaka kufa kabisa. Nilishatumia dawa nyingi za kuongeza nguvu za kiume bila mafanikio, nilishafanya kila kitu bila mafanikio, sikuweza hata kujichua, hata uume ulikua kama haushtuki tena.


“Nini hiki, inamaana ndiyo maisha yangu yamekua hivi? Inamaana siwezi kupata mtoto tena?” Niliwaza bila majibu, nilikua naumia sana nikiona rafiki zangu wakiwa na watoto, swali la unaona lini lilikua likiniumiza sana. Ndugu waliongea wakachoka lakini sikuwa na uwezo wa kufanya mapenzi na mwanamke na hali hiyo ilinifanya kuogopa sana kuwasogelea wanawake nikiamini kuwa watanitangaza.


Nimekua mtu wa hasira, nimekua mtu wa kudhalilisha wanawake kwenye mitandao na mabaa medi, nawalipa ili kuwashikashika na kuwahdalilisha najikuta nawapiga bila sababu. Nimerudi kwenye kunywa pombe na kuchart na wanawake, wakinitumia picha za uchi basi nafurahi jinsi wanavyodhalilika. Wake za marafiki zangu ambao wananiona kama kijana mzuri, wanajilengesha natumia pesa naishia kuwapiga picha za uchi na kutuma kwenye magroup ya Telegram.


Mwanzo nilikua napata raha nikiona wanadhalilika, nikiona rafiki yangu kaona picha za uchi ambazo mke wake kanitumia kwenye mitandao basi najisiki raha sana, ile hali ya wao kukosa amani nahisi wanakua kama mimi lakini sasa hivi sina raha tena. Nimechoka na haya maisha, natamani kufa, sitamani kuishi tena, natamani nisiwepo, natamani kufa lakini bado sijaitwa Baba sijui nifanye nini kwani sioni tena sababu ya kuishi.


Natamani uandike kisa changu kwani mara nyingi unaandika kuhusu wanawake, wapo wanaume ambao tumeumizwa, wapo ambao bado tunabeba maumivu ya zamani, wapo ambao maumivu yameafanya kuwa wanyama kama mimi. Nimefanya mambo mengi mabaya na yote ni kutokana na hasira za X wangu, nilimpenda lakini hakuonyesha kunijali na kila nilivyozidi kumpenda ndivyo aliziodisha maumivu.


Mpaka sasa hajaondoka kichwani kwangu, nikiongea na mwanamke namuona yeye, nikimuona namna alivyo na furaha kwneye mitandao ya kijamii natamani kumfuta kumpiga lakini nilishajaribu nikishamuona nakua kama mtoto mchanga, nakua sina nguvu tena ya kufanya chochote.


Nachukua mwanamke mwingine ambaye hata siwezi mfanya chochote namlewesha na kuishia kumpiga, kweli nimechoka natamani sana kufa lakini sina mtoto, sijui hata nifanye nini, niemchoka hii hali ya kudhalilisha wanawake? Nafanya kazi nzuri lakini maisha yangu hayana thamani tena kwani nyumbani siheshimiki, kazini nadharaulika, wananiona mlevi wananiona kama nimechanganyikiwa na kwakua tu sijaitwa Baba na siwezi kuoa.


MWISHO

0 comments:

Post a Comment

BLOG