Search This Blog

Tuesday, June 21, 2022

NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU

  

IMEANDIKWA NA IDDI MAKENGO

IMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA KWANZA.


“Kwahiyo ndiyo unanirudia saa nne? Unajiona mw3anaume sana na hao rafiki zako ambao kila siku wanakudanganya? Wenzako hawajaoa lakini kila siku ni kuhangaika nao, unazunguka nao kama vile hujaoa, saa nne mimi nikufungulie mpango?” Nilimuambia mume wangu kwa hasira, kusema kweli mume wangu hakua ni mtu wa kuchelewa sana kurudi nyumbani lakini karibuni kama wiki moja hivi alibadilika.


JOIN US ON TELEGRAM

“Naomba uniache, nimechoka sana, nilishakuambia kwanini nachelewa lakini hunielewi, mimi si mtoto mdogo wa kugombezwa kila siku, nimechoka kupiga kelele!” Mume wangu aliongea kwa ustaarabu, alinipita na kuingia chumbani, moja kwa moja alijilaza bila kula wala kuingia bafuni kuoga. Nilimfuata na kuanza kumnusa kuona kama alikua kaoga huko na kujipaka mafuta mengine lakini sikusikia chochote.


Pamoja na kutokusikia kitu lakini bado sikuamini, niliwaza alikua wapi? kama ni kazi mbona hana ubize huo, ananirudia saa ne halafu hataki kula ikimaanisha kuwa ameshibana kuoga haogi ikimaanisha kuwa ameoga huko alipokua. Niliongea sana lakini mume wangu hakunyanyuka wala kunyanyua mdomo kunijibu, kwangu ilikua ni dharau kubwa, nilikasirika na kwenda kulala chumba cha watoto ambao wlaikua shule bweni.


Asubuhi kama kawaida niliwahi kuamka, sikumuandalia mume wangu kitu chochote, nilijiandaa ili kwenda kazini, nilipomaliza nilitoka kukaa kwenye gari kumsubiri anipelkekazini kwanza, mume wangu alijiandaa na alitoka, alinisalimialakini sikumuitikia, nilikua nimenuna, naye hakusema chochote, aliingia kwenye gari akaendesha mpaka kunishusha kazini kwangu. Aliniaga lakini sikujibu, aliondoka mpaka kazini kwake.


Mchana mzima nilikua na kisirani, nilikua nimekasirika nikiamini kuwa mume wangu ananidharau na mabadiliko yale ni ya mwanamke mwingine. Nilimsimulia shoga yangu ambaye alizidi kunichanganya.


“Hata mume wangu alianza hivyo hivyo, hawa mbwa hawana shukurani, wanaanza kuchepewa kurudi baada ya muda unasikia mtu ana mwanamke mwingine, kaaza sijui nini, si unakumbuka mume wangu, mwanzo alianza kusema kuwa ana kazi nyingi, anachelewa kurudi, nashtuka anasafiri kikazi mara ana mtoto, hapana, kuwa makini, chunguza, usiruhusu akukalie kichwani!”


Rafiki yangu aliongea kwa hasira sana, aliumizwa sana na kitendo cha mume wake kuzaa nnje ya ndoa wakati alikua anampenda na alikua ni kama anamhudumia kwa kila kitu kwani mume wake tofauti na wangu si mtu wa kuhusumia familia.


“Sasa nifanyeje?” nilimuuliza.


“Kuwa mkali, wanaume ukiwachekea tu wanakufanya mjinga, kuwa mkali, usimchekee chekee, akichelewa kurudi gombana una kazi yako asikufanye mjinga, mimi nilishakosea kwa yule mbwa, nilimdekeza sana!”


Tuliongea mengi na shiga yangu, hata kazi hazikuenda, lakini kwenye saa sita na nusu hivi mume wangu alinipigia simu, nilitaka nisipokee lakini niliona ngoja nimsikiliza.


“Aiseee! Hatuwezi kuishi hivi, tuna watoto, nashindwa kufanya kazi kwa mambo ya kijinga, aisee tunatakiwa kuongea, kama hauko bize nakupitia tukele chakula cha mchana.” Mume wangu aliniambia kwa sauti ya kistaarabu, kwa namna alivyokua anaongea alikua anatia huruma, alionekana kama anataka kulia kabisa.


“Mimi nina kazi nyingi, nitafute jioni, kama utawahi kurudi basi tutaongea.”Nilimjibu wka mkatao kisha nikaakata simu, alijaribu kupiga tena lakini sikupokea, sikua na kitu cha kumjibu kwa wakati huo, nilishaanza kummiss na kumunea huruma, nilijua kama nitaongea naye basi nitamsamehe kitu ambacho sikua tayari kukifanya. Baada ya kukata simu nilimfuata shoga yangu, nikamuambia mume wangu kanipigia simu anataka kunitoa lunch ili tukaongee.


“Huyo ni Malaya kabisa, yaani najua tabia zao, wakishakosea ndiyo wanajifanya vizawadi na kuomba misamaha!” Alinaimbia kwa hasira, alinisihi sana kukataa na kuniambia kuwa kama nikikubali kizawadi cha kijinga kama chakula basi ndiyo utakua mwanzo wa ndoa ya mateso.


“Wanajua akili zetu, wanatuona sisi wajinga, mtu anakurudia saa nne halafu anaenda kukununulia chips kuku anataka usahau? Ujinga mtupu, nakuambia akija hata nnje usitoke, muambie una kazi!”


Aliniambia, nilimkubalia nakurudi ofisini kwangu, ni kweli nilikua sijawahi kumfumania mume wangu, yeye ni mkimya na mara nyingi ni wale watu hata kama ni wewe umekosea basi watajishusha ili tu kuwe na amani.


“Ananichukulia mjinga huyu, nimesema kuwa kama anataka tuongee basi akubali kuwa anachepuka na ana mwanamke mwingine!” Niliongea peke yangu, wakati huo huo meseji ya mume wangu iliingia.


“Jiandae nipo njiani, hatuwezi kuishi hivi.” Niliisoma na kusonya, kisha nikamjibu.


“Nina kikao.” Nilijibu na baada ya hapo nilizima simu, sikutaka anitafute tena kwani ninavyomjua mume wangu nikiongea kidogo angenishawishi na ningemsamehe.


Baada ya kama dakika kumi hivi mume wangu alikua ofisini kwangu, alisimama nnje ya ofisi na kuniomba nitoke. Nilitoka kwa kuchungulia nikamuambia kuwa nipo bize siwezi kwenda popote. Alisoge mlangoni huku akitaka kuingia ofisini kwangui, lakini sikumruhusu, nilikua kama namsukumiza kwa nnje.


“Acha kuwapa watu faida, nisikilize kwanza.” Aliniambia kistaarabu kama anaomba kuingia.


“Niondokee! Si uende kwa hao Malaya wako ukawanunulie chakula kama una pesa zinakuwasha!” Nilimjibu kwa hasira, kusema kweli sikupanga kufanya hivyo lakini kwa namna alivyokua anasisitiza kutaka kuingia ofisini kwangu niliona kama vile analazimishia, hasira zilinipaanda na bila kujijua nilijikuta nakasirika na kumsukuma mume wangu.


Mume wangu alishtuka kuona kuwa nilikua nimekasirika kiasi kile alitaka kuondoka lakini alishindwa, alipiga hatua kama mbi.i hivi kisha akageuka.


“Ni hili hili la mimi kuchelewa kurudi nyumbani au kuna jambo jingine mke wangu?” Aliniuliza lakini sikumjibu, nilifunga mlango na kuingia zangu ndani.


Nilirudi kwenye kitu na kukaa, nilianza kulia, “Nimefanya nini?” niliwaza baad aya kukaa na kutulia, ofisi yangu ipo ghorofani hivyo unaona kila kitu kinachoendelea chini. Nilisogea mpaka dirishani nikamuangalia mume wangu jinsi alivyokua anaondoka kwa unyonge mpaka nilimuonea huruma. Alitembea taratibu mpaka kwneye gari yake, alifungua mlango na kuingia, hakuondoka, alikaa kwenye gari kwa zaidi ya nusu saa bila kuondoka.


Nilijisikia vibaya na kutaka kutoka kumfuata, lakini malngoni nilikutana na shoga yangu.


“Yule mshenzi nimesikia kaja hapa, lakini umefanya vizuri ulivyomfukuza, sasa hivi atashika adabu, hawezi kukusumbua tena, unafikir wanaume ni watu, sasa sababu ya kuja mpaka ofisini ninini kama si kutaka tu kujishaua watuwamuone anajali.” Aliongea maneno mengi kiasi kwamba nilijikuta naacha kwenda, niliona ni sawa nilivyofanya, nilirudi na kukaa kwneye kiti huku nikichungulia getini, niliona gari ya mume wangu ikitoka hapo ndipo nilijua kuwa kaondoka.


***


Jioni mume wangu aliwahi kurudi, hakuchelewa kama jana yake, saa mbili tu alikua nyumbani. Alinisalimia vizuri na mimi nilimuitikia, kwahi kwake kurudi niliona kabisa kuwa kweli kajifunza, ingaw abado nilikua na wasiwasi kuwa ana mwanamke mwingine lakini sikutaka kuingiza kisirani. Aliingia ndani na kukaa, baad aya kuoga alinifuata sebuleni, tayari nilishaanda achakula cha usiku, wakati tunakula alianza kukumbushia mambo yaliyopita.


“Hivi mke wangu kuna nini? Naona kama umebadilika sana, unakua mtu wa hasira, si mtu wa kunisikiliza, hembu niambie kuna nini?” Aliniuliza kwa ustaarabu lakini ni kama aliamshha mashetani yangu.


“Mimi si wa hivyo, mimi si mjinga kama hao wanawake wengine, yaani makosa ufanye wewe halafu ujaribu kunigeuzia kibao. Nani anarudi usiku! Nani ambaye hajibu sms! Nani ambaye kila ukimpigia simu anajifanya kuwa yuko bize na kazi, yaani kila kitu ni wewe unafanya lakini sas ahivi unataka kunilaumu, kwa taarifa yako mbinu zako zote nazijua, wewe ni Malaya lakini unataka kunigeuzia kibao ili mimi ndiyo nionekane kama nina kisirani, hapana!”


Nilimuambia, nilitukana sana lakini mume wangu hakujibu chochote, kitendo cha mume wangu kukaa kimya kiliniumiza sana, nilijua kuwa ni dharau, nilianza kulalamika kuwa ana dharau, anafanya makosa kisha ananigeuzia kibao na kujifanya mwema. Alinisihi sana nitulie lakini niliishia kumtukana, nilivyoona hajibu kitu nilichukua sahani ya chakula na kumrushia, nilitaka kumpiga kichwani ila kwa bahati aliikwepa, nilimfuata na kuanza kumpiga mangumi huku nikimtukana lakini hakujibu zaidi ya kunishika kwa nguvu ili nisimguse.


Nilijitoa mikononi mwake na kuondoka moja kwa moja mpaka chumba cha watoto, asubuhi niliwahi kuamka sikumsalimia wala sikumsubiri. Nilienda kazini ambapo sikukaa sana, sikuongea kitu chochote kwa mtu, nilikaa kidogo nikashindwa kufanya kazi, nilitoka mpaka kwa Mama, nilimuambia kila kitu kuwa Mume wangu kabadilika, amekua mtu wa kurudi usiku na nikimuuliza ananuna, hanisemeshi, niliongea mambo mengi sana nikamuambia kuwa nahitaji kupumzika kubaki nyumbani lakini Mama alinigomea.


Alikataa hata kuita wazee aliniambia kuwa hayo ni mambo madogo niende ni kamalizane na mume wangu niache kufaidisha ulimwengu. Hata Baba hakumuambia alisema ni mambo ya kitoto, nilimuambia hata ampigie simu mume wanyu na kumanya lakinia likataa. Kwa kumsikiliza niliona kama Mama yupo upende wa mume wangu, nilikasirika zazidi kwani yeye ndiyo nilimuona kama mkombozi wangu. Sikua na namna nilirudi nyumbani kwa kununa hivyo hivyo, sikuomba msamaha wala mume wangu hakunisemesha, yalienda hivyo hivyo kimya kimya mpaka yakaisha.


Maisha yaliendelea lakini sikumuamini tena mume wangu, nilianza kumfualtilia, kila siku niishika simu yake na kuangalia wanawake ambao anachata nao, mara ntyingi nilikua nikichukua namba za wanawake katika simu yake na kuwatukana sana kuwaambia waachane na mume wangu. Hali hiyo ilimkera mume wangu, akawa anakasirika na mwisho aliweka simu yape password kitu ambacho kilinikasirisha zaidi, nilaimini kuwa ni kweli anachepuka ndiyo maana anaficha hataki nione kilichomo ndani.


Ndoa yetu ilianza kuwa ya migogoro, kila siku kelele, mume wangu alizidisha kuchelewa, akisingizia kazi lakini mimi niliamini kuwa ana mwanamke mwingine. Siku moja kulikua na sherehe kazini kwao, aliniambia wiki moja kabla, nilikataa kwenda lakini nilipoongea na shoga yangu aliniambia niende ili kama anachepuka basi michepuko yake ambayo labda aliidanganya kuwa hajaoa au tumeachana basi inione tukiwa na furaha.


Siku ya tukio wakati ashamaliza kujiandaa basi nilimuambia mimi naenda, alishangaa lakini alilazimika kunisubiri kwani kwa makusudi kabisa ili kumchelewesha na kumuudhi nilijiandaa taratibu. Sherehe ilikua inaanza saa mbili usiku lakini sisi tulifika saa nne. Watu walishajaa na hakukua na siri za kukaa pamoja, mume wangu alinitafutia mimi sehemu nzuri ya kukaa kisha yeye akaenda kukaa nyuma kabisa kwani shugui ilikua inaendelea hivyo asingeweza kunyanyua watu.


Mimi nilikaa mbele hivyo sikuweza kumuona mume wangu vizuri, yeye alikaa kwenye kiti tu hakukaa kwenye meza, pamoja na kuwa alikua na cheo kikubwa lakini mume wangu si mtu wa kujikweza hivyop aliniacha mimi nikae kwenye siti yake na hata mtu alipojitolea kumpisha aligoma kwani aliyateka kunyanyuka naye alikua na mke wake. Sherehe iliendelea nikiwa sina raha kabisa, nilikua nina wasiwasi nikitamani kuwa karibu na mume wangu ili watu wasiniibie, wka sababu hiyo nilijikuta nanyanyuka mara kwa mara kutoka kana naenda kujisaidia kumbe nilikua namchungulia mume wangu kwani sehemu aliyokua amekaa ilikua karibu na choo.


Nilitoka zaidi ya mara tatu, ya nne nikiwa narudi nilimuona dada mmoja, alikua kakaa jirani na mume wangu, walikua wameinamiana na mume wangu alikua akimuonyesha kitu kwenye simu yake. Mara zote wakati napita yule dada hakua pale, siti aliyokua kakalia ilikaliwa na Kaka mwingine, inamaana alikua katoka alipokua kumfuata mume wangu. Nilijikuta napandwa na hasira niliwafuata na kumnyanyua mume wangu.


Yule dada alinyanyua uso kuniangalia, nilimuona na kumkumbuka, miezi kama miwili nyuma siku ya kuzaliwa kwa mume wangu alipost picha ya mume wangu na kumtakia heri mume wangu, nilikasirikaga na kumuuliza mume wangu lakini aliniambia kuwa ni rafiki tu. Nilipomuona nilijikuat anapandwa na hasira, nilimshika mume wangu na kumnyanyua, bila kujali nilikua wpai nilianza kumuambia tuondoke, mume wangu alijua nishakasirika hivyo alinyanyuka harakaharaka ili kuondoa aibu.


Alinishika mkono na kuniambia tutoke nnje, lakini kabla hatujaondoka yule dada aliyekua amekaa alianza kucheka kwa dharau, nilijisikia vibaya, nilipepesa macho pembeni, kwenye meza ya jirani kulikua na chupa ya bia. Niliichukua na kumrudhia yule dada, aliiona na kuikwepa ikaenda kumpiga mgongoni mhudumu ambay ealikua anapita. Nilianza kutukana bila kujali tulikua wapi, mume wangu alinishika kwa nguvu na kunitoa nnje ili kuepuka aibu, mimi niliendelea kutukana mpaka aliponiingiza kwneye gari.


Hakufanya chochote aliendesha mpaka nyumbani, njia nzima nilikua nikimtukana na kumuambia kuwa tukifika nyumbani nataka talaka yangu kwani simtaki.


“yaqani unanipeleka kwenye shrehe yenu ili wkenda kunionyesha Malaya wenu, hapana, nimesema kuwa sitaki! Nataka talaka yangu!” Nilipiga kelele lakini mume wangu hakujibu neno hata moja, alikua kakasirika sana, alielekeza akili yake kwenye kuendesha gari tu. Tulifika nyumbani ndiyo akaanza kuongea akilalamika kuwa nilikua nimemuaibisha sana.


Ni kama aliamsha mashe4ani yangu, nilimtukana sana huku nikimpiga mangumi kila sehemu, alinishika lakini nilijipigiza na kujirusharusha sana. Mume wangu kuona vile alitoka nnje ili kuondoka, lakini sikutaka kumpa nafasi, nilimfauta huko huko, aliingia kwenye gari na kuiwasha, lakini kabla ya kuondoka nilifungua mlango wa abiria, mume wangua llishaondoa gari kwani geti lilikua bado halijafungwa wakati tunaingia ananiingiza ndani aliliacha wazi.


Sijui kama aakuniona au ilikuaje lakini nilishikilia mlango, nikawa kama nabembea, wakati anarudisha gari nyuma nikawa kama naburuzwa, nilianza kupiga kelee nikusema anataka kuniua. Mume wangu alishtuka, alisimamisha gari hataka na kunifuata.


“Kwanini unafanya upumbavu, unafanya utoto sana najaribu kukukwepa lakini naona kuna kitu unakitaka!” Aliniambia ka hasira huku akinishika kama vile ananikaba. Na mimi nilimshika na kuanza kumpiga kwa hasira.


“Kama ni mwanaume kweli basi nipige, si unajifanya kidume, nipige kama hujaoze jela na ndoa ndiyo naondoka.” Nilimuambia huku nikimsukuma sukuma.


“Nipig—“ niliendelea kuongea lakini mume wangu ahsira zilimzidi, nilinyamaziswha na kofi, kabla sijakaa vizuri nilishikwa na kurushwa juju kama takataka, ile nafika chini mume wangu alinikanyanga kwa mguu wa kulia, alianza kunipiga pale chini kwa hasira, alikua anatukana, anaongea maneno mengi, alinipiga sana bila huruma, alikua anapigakelele akiniambia kuwa amechoka na ataniua ili nayeye ajiue.


Alinipiga sana mpaka nikawa siwezi hata kunyanyuka, aliingia kwenye gari na kuniacha pale chini nikigalagala, alirudisha gari nyuma vibaya kiasi kwamba badala ya kutoka nalo getini basi alirudisha nyuma akagonga ukuta, nilikua nimelala chini, nina fahamu zangu sijiwezi lakini namuona namna anavyohangaika, anaenda mbele anarudi anagomba anageuza anagonga alifanya hivyo mpakaakafanikiwa kutoka, mimi mwili ulikua unauma, damu zinanitoka puani na mdomoni, mwisho nilishindwa hata kuhema nikapoteza fahamu.


SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA PILI.


Sikujua kilichoendelea mpaka baada ya masaa mawili hivi, binti wa kazai alisikia tulivyokua tunagombana na mume wangu, lakini pia kelele zangu na jinsi mume wangu alivyokua anagongesha gari ziliwaamsha majirani ambao walikuja na kunichukua, walinipeleka hospitalini ambapo nilitakiwa PF#, waliennda kuchukua na nilitibiwa.


Sikuwa nimeumia sana zaidi ya kuvimba mwili mzima lakini sikuvunjika sehemu na kichwani nilikua sawa, lakini nilikua kwenye maumivu makali huku nikilia kila wakati kwa uchungu wa maumivu na uchungu wa mume wangu kunipiga. Ilikua ndiyo mara yangu ya kwanza mume wangu kunipiga, nilijisikia vibaya nikiamini kuwa alikua kanipiga kwababu ya mwanamke mwingine.


Kwa upande wa mume wangu baada tu ya kunipiga na kugonga gonga ukuta alihisi kama vile ameniua, hakwenda mbali, alienda mpoja kwa moja mpaka polisi na kuwaambia kuwa anahisi kuwa kamuua mke wake. Alikamatwa na kuwekwa ndani mpaka siku iliyofuata ndipo yey e alipewa taarifa kuwa nipo salama lakini alikua na kesi ya kunipiga kwani niliumia na tayari nilishakua na RB yake.


Aliandikisha maelezo ambapo alikiri kunipiga, hakukataa kitu chochote, mimi kesho yake nilitoka hospitalini, lakini sikurudi nyumbani, w3akati nipo hospitalini shoga yangu alikuja, tulionge mambo mengi na kubwa kabisa ni kuhusiana na mchepuko wa mume wangu.


“Mumo wako namjua, hajawahi kukupiga hata siku moja, lakini leo umegombana namwanamke wake basi anakupiga mpaka unalazwa, nina uhakika kuwa huyo mwanamke anatembea naye na kinachomuuma ni kuwa umemdhalilisha mbele za watu na mchepuko wake.” Aliniambia.


Ni kweli mume wangu alikua hajawahi kunipiga na alionekana kuumizwa sana na mimi kumdhalilisha.


“Mbona siku zote tunagombana, hata kunitumana mume wangu hajawahi kunitukana!”Nilimuambia.


“Aisee usirudi mpakaachane na huyo mwanamke, wanaume nawajua akishaanza kukupiga hivi basi jua kuwa ndiyo kila siku hali itakua hivyo hivyo!” Aliniambia, nilimuelewa kweli kuwa mume wangu ana mwanamke mwingine nd ndiyo sbabau ya kunipiga, iliniuma sana kuona kuwa mume wangu ananipiga kwasababu ya mchepuko.


Ndugu zangu walikua wananipigia simu kujua hali yangu, asubuhi Mama alikuja kuniona, wakati anakuja ndiyo nilikua naruhusiwa kutoka hospitalini. Aliniambia niongozane naye mpaka nyumbani lakini niligoma, nilimuambia naenda kukaa kwanza kwa rafiki yangu kabla ya kurudi kwa mume wangfu, kwanza Mama yangu alishangaa lakini pili aligoma kabisa kwa kuniambia kuwa natakaiwa kurudi kwa mume wangu.


“Mama unaona alivyompiga, hivi una uchungu kweli na mwanao, yaani mwanaume anampiga hivi haafu unatakaa rudi?” Shoga yangu alimuambia Mama, ingawa Mama alimuambia asiingilie chochote lakini hata mimi nilikua na hasira, nilitaka kupumzika na sikutaka kurudi nyumbani, Mama alinisihi sana, aliniambia hata kama kwelis itaki kurudi kwa mume wangu basi nirudi nyumbani, nilikataa kwa madai kuwa nyumbani kwetu ni mbali sana na kazini hivyo nataka kwenda kutuliza kichwa kwa shoga yangu.


Mama aliondoka kurudi nyumbani huku mimi nikiondoka na kwenda kwa shoga yangu, mume wake alikataa kunipokea lakini shoga yangu alikua hamsikilizi, ndoa yao ni kama ilishakufa kwani kila siku walikua wanagombana, mwanamke ndiyo alikua anahudumia kila kitu hivyo mwanaume hakua na kauli, ingawa alikua na kazi lakini shemeji yangu hakua mwanaume wa kujali familia kabisa.


Nilikaa pale kwa iki mbili huku nikienda kazini palepale, wakati huo mume wangu alikua ameshat0ka kwa dhamana, kesi bado ilikua haijapalekwa mahakamani, pamoja na mume wangu kukiri na kuwa tayari kwa lolote hata kama ni kufunguwa lakini polisi walishauri ishu yetu kwenda kwenye dawati la jinsia ili tuongee kwani mume wangu angeweza kufungwa. Mimi niligoma kabisa, nilitaka mume wangu kufungwa ili kufundishwa adabu, bado nilikua na hasira kutokana na yeye kunipiga kwasababu ya mwanamke mwingine.


Ingawa watu wengi walinisihi kusamehe wakiniambia kama akifungwa atapoteza kazi lakini sikukubali, nilikua nimedhamiria kumfunga na katika kipindi chote hicho pamoja na kuniomba msamaha sana lakini niligoma hata kuongea naye. siku moja nakumbuka ilikua ni jumapili usiku.  Mama alikuja kwa rafiki yangu nilipokua nikiishi, alikua kaongozana na Kaka yangu, alitaka kuongea na mimi lakini niligoma.


Ndugu zangu wote walishageuka na kuwa upande wa mume wangu hivyo nilikua nimekasirika sana.


“Najua hutaki kuongea lakini nitaongea mimi. Mimi ni Mama yako na nikuambie tu kuwa umeniaibisha sana, namfahamu mume wako na nakufahamu wewe. Sitaki kujua kilichotokea, sitaki kuamini kuwa yule mwanaume alipkupiga bila sababu, lakini kwakua yeye hasemi anaomba msamaha basi nitaongea mimi….”


Mpaka wakati huo mume wangu alikua hajamuambia ndugu yangu yoyote kuwa nilikua nimemuaibisha kazini kwake, alikua anaomba tu msamaha na kusema yeye ndiyo mwenye makosa kwa kunipiga.


“Kesho mume wako anatakiwa kupelekwa mahakamani, anaweza kufungwa na kupoteza kila kitu, utaenda kule na kufuta hiyop kesi, mtaongea na kesho utarudi kwa mume wako. Hii ni mara yangu ya mwisho kuongea na wewe, kama hutafanya hivyo basi jua kuwa mimi si Mama yako, narudia mimi si Mama yako, sitaki kukuoana nikiwa hao na nikifa basi hata kunizika usije….”


Mama alishindwa kuongea, alianza kulia kama mtoto, nilijisikia vibaya kwani alionekana kuumia sana, alinyanyuka na kumuambia Kaka yangu ampeleke nyumbani. Nilitamani kunyanyuka kumfuata lakini nilisita, maneno yake yaliniingia sana kichwani kwangu. Sikuweza kulala siku ile na kweli kesho yake nilienda Polisi, niliongea na mume wangu na kuamua kumsamehe. Tulirudi nyumbani pamoja, mume wangu hakua na hasira kabisa,a liniomba msamaha huku akisisitiza kujutia kwa kitendo chake.


“Sijui ni nini kilitokea mke wangu, ningeweza kukuua siku ile, nilishaapa katika maisha yangu siwezi kumgusa mwanamke, naomba unisamehe, sijui wanangu wakijua kuwa nimempiga Mama yao watajisikiaje…” Mume wangu aliniambia, alikua akiomba msamaha njia nzima, nilimuambia nimemsamehe lakini nataka akiri kuwa amechepuka na huyo mwanamke na ndiyo sababu ya kunipiga.


“Hapo nitakua nimekudanganya mke wangu, yule binti hata mazoe anaye sina, yule ni kama mdogo wangu, mimi ni bosi wake na kama unavyojua pale ofisini kila mtu ananipenda…” Aliniambia, sikutaka kumsikiliza kuhusu hilo, nilishaamini kuwa anachepuka ilikua ngumu sana kwangu kuamini vingine. Pamoja na kumbana sana lakini mume wangu aligoma kabisa kukubali kuwa anachepuka.


****


Maisha yaliendelea, pamoja na kumsamehe mume wangu lakini bado nilikuana hasira, kitendo cha yeye kukataa kukubali kuwa anatembea na yule binti na ndiyo sbabau ya kunipiga kiliniuma sana, kilininyima amani na mtu pekee ambaye angeweza kunipa faraja alikua ni shoga yangu.


“Unafikiri wanaume wanakubali, hata umkute anafanya mapenzi hatakubali, huyo ni Malaya, na kwakua kila mtu anamuona mpole basi wewe ndiyo unaonekana kama una makosa kila wakati.” Aliniambia, kweli kila mtu aliniona kama mimi ndiyo nina makosa.


Ingawa mume wangu hakua na kinyongo an alitaka amani lakini ndugu wengine hasa ndugu zangu waliniona tofauti, waliniona kama mimi ndiyo nina makosa, waliniona mshenzi sanma. Hali hiyo iliniuma sana nilijikuta ni mtu mwenye mawazo na muda mwingi niliutumia kwa rafiki yangu. lakini mume wangu alizidisha upole, alikua kama vile ananiogopa, alikua haniulizi chochote, hata nikikosea mimi basi alikua yeye ndiyo wakwanza kuniomba msamaha ili kuleta amani.


Hapo awali nilikua sinyi pombe, nilikua naichukia lakini baaada ya muda mwingi kuwa na shoga yangu kupenda kutoka kwenye sehemu za burudani nilijikuta naanza kunywa pombe. Mume wangu alikua anakunywa lakini akaacha, nilipoanza kunywa alijua, aliongea na mimi sana na kunisihi lakini sikumsikiliza, nilimuambia kuwa ni maisha yangu.


“Wewe ndiyo umenifanya kunyw apombe, nakunywa ili kuondoa mawazo…” nilimuambia, aliishia kuniomba msamaha kwani hakutaka nizungumzie tena suala la yeye kunipiga.


Masra nyingi nilikua nakunywa mchana siku za weekend kwani shoga yangu alikua haruhusiwi kurudi nyumbani zaidi ya saa kumi na mbili jioni, ingawa mume wake alikua ni mlevi na mtu wa wanawake lakini alikua anambana sana, alikua anampiga sana hivyo alikua akimsikiliza, kwakua sikua na uzoefu nilipenda kampani yake hivyo nilikua nakunywa mchana tu. Katika pitapita zangu kwnyepombe nilijikuta naanzisha mahusiano na Kaka mmoja ambaye alikua ni mume wa mtu.


Yalianza kama utani, huyo Kaka alikua kama rafiki nikimuelezea namna ambavyo mume wangu alinipiga na yeye kama shoga yangu aliniambia kuwa nilipigwa kwakua mume wangu ni Malaya.


“Mwanaume hawezi kukupiga hivyo kwa sababu nyingine. Mimi ni mwanaume najua, mume wako ni Malaya lakini ni wale wanaume amabo hawapendi kuonekana kama Malaya, mbele za watu wanapenda kuonekana kama malaika hivyo ulivyomdhalilisha mbele ya wafanyakazi wenzake aliumia kwani sasa wameijua vizuri tabia yake.” Aliniambia.


Tofauti na mume wangu huyu Kaka alikua ni mchangamfu sana, mtu wa kuongea, kutaniana na kikubwa zaidia likua anajua mapenzi, si ktandani, hapana, kitandani mume wangu alikua ni fundi anamzidi sana lakinia likua anajua kujali. Ni aina ya wanaume ambao anaweza klukushika mbele za wtau, akakukumbatia na hata kukunyonya mate mbele za watu bila aibu. Nilikua napenda jinsi ambayo anakushika, anakua huru nawe, mnataniana na ni mtu ambaye anatuma meseji mpaka unachanganyikiwa.


Unaweza upo kazini akakutumia mseji, unafanya nini ukimjibu akakuambia hembu funga mpango wa ofisi, nenda vua nguo ya ndani ipige picha unitumia nina kazi nayo. Yaani namna anavyochat mwenyewe unachanganyikiwa, unaweza kuwa wkenye kikao ukajikuta unajiloanisha kwa meseji zake. Ni mtu wa kukumbuka vitu yaani sio siku yako ya kuzaliwa au kitu ambahco ulimuambia utakifanya, anaweza kukutumia meseji usiku kukukumbusha asubuhi usije kusahau kufanya kitu flani ambacho mliongea jana yake.


Kwakifupi alikua ni mtu tofauti kabisa na mume wangi, alikua kachangamka. Nilianza mahusiano naye taratibu na kwa muda nilijihisi mtu tofauti kabisa, nilianza kumpenda na nilianzaa dharau kwa mume wangu.  Mwanzo mume wangu hakushtuka, alihisi bado nina hasira za kunipiga, lakini nilijikuta nashindwa kumficha, katika nfsi yangu kuna kitu kiliniambia kuwa muonyeshe kuwa wewe ni nani! Muonyeshe kwua unaweza kuwa na furaha bila yeye.


Nilitamani kumuambia mume wangu kuwa nachepuka, nilitamani kumtukana kabisa na kumuacha, raha nilizokua nikizipata zilinichanganya na kuanza mumuona mume wangu kama takataka.


“hivi ikitokea kama mume wangu akinifuania utafanyaje?” Nilimuuliza mchepuko wangu, tulikua kwenye gari yangu narudi nyumbani, yeye ndiyo alikua akiniendesha na  nilipenda sana, alipunguza mwendo, akasogeza gari pembeni, aliwahsa taa za hatari kisha akanigeukia, alinikutambatia, huku mikono yake ikinitomasa kiunoni kushuka chini alipeleka ulimi wake wkenye masikio yangu, alianza kuninyonya masikio, nilichanganyikiwa kwekeli.


“Akikuacha asubuhi jioni nakuoa….” Aliniambia k3wa saui ya mahaba, kusema kweli nilikua katika wakati mgumu, nilishindwa hata kupumua, nilimuacha auchezee mwili wangu anavyotaka, nilikua ho kabisa.


“Naaa…naaa.. naaa mke wako?” Nilijikaza kumuuliza.


“Kwani yey hafai kuacha, nakupenda wewe, nimemuoa mke wangu kwakua nilikua sijakutana na wewe, wewe ni mwanamke mwenye akili, mtamu na kila kitu amabcho mwanaume anataak, mke wangu naweza kumaucha hata sasa hivi, sio kama nampenda, nipo naye kwakua tu sikuwahi kukutana na mwanamke kama wewe huko nyuma na sasa hivi wewe ni mke wa mtu, ukiachwa hata kesho yeye anabadilika kutoka kuwa mke na kuwa mke wa zamani…”


Nilijihisi kuchanganyikiwa kwakweli, nilitamani siku ileile kwenda nyumbani na kumuambia mume wangu kuwa simtaki nataka talaka, alinichezea chezea kiasi kwamba nililana palepale, alitaka kunirudisha nyumbani lakini niligoma.


“Nipeleke gest, leo siwezi kulala na mume wangu, nataka tukalale mpaka ausubuhi, sitaki, kama mume wangu ananiacha aniahe lakini nataka kulala na wewe.” Nilimuambia, tangu kuanza mahusiano na huyo Kaka karibu miezi mitano tulikua hatujawahi kulala pamoja mpaka ausbuhi.


Mara nyingi tulikua tunafanya mapenzi mchana, na kikubwa kilichokua kikituzuia ilikua ni ndoa zetu hasa mimi. Nilikua naogopa sana kulala nnje kwani bado nilikua nampenda mume wangu na sikutaka kumuacha. Mwanzo nilikua nachepuka kwakua nilikua nina mawazo ya mume wangu kuwa na mwanamke mwingine, sikuchukulia sitiasi lakini siku ile nilikua siriasi, nilikua nipo tayari kumuacha mume wangu kwaajili ya yule Kaka.


Baada ya kumuambia kuwa nipo tayari kwenda kulala naye alisita kidogo, alirudi kwenye usukani na kuniambia kuwa ni kitu ambcho hakiwezekanai.


“Kwanini? Unamuogipa mke wako?” Nilimuuliza, alionekana kama ni mtu mwenye mawazo kidogo.


“Hapana, shida si mke wangu, tatizo ni kwako, wewe ni mke wa mtu na mume wako akijua itakua shida. Mimi sina shida, mke wangu hana shida, mimi ni mwanaume bwana…” Aliniambia.


“Nishakuambia mimi mume wangu niachei mimi, nitapambana naye, labda kama wewe hutaki, ladba kama unamuogopa mke wako?”


“Hapana, mimi ni mwanaume siwezi kuogopa mwanamke, kama unaona kuwa haina shida kwa ndoa yako basi tende.”


Aliniambia, niliona kabisa hana raha  ni kama alikua anaogopa, nilihisi anamuogopa mume wangu nikamuambia kuwa asiwe na wasiwasi kwani mimi sijali kabisa kuhusiana na mume wangu, ahtaa kinaicha sijali. Alinikubalia, tuliondoka mpaka kwenye hoteli moja kubwa, alichukua chumba na tukaingia ndani. Tuliagiza vinywaji, na kuanza kunywa, tulikunywa sana mpaka wkenye saa nne hivi, mimi nilianza kulewa, simu yangu ilianza kuita na alikua ni mume wangu.


Sikutaka kupokea lakini aliendelea kupiga simu, niliikata na kumtumia mseji.


“Nitalala kwa rafiki yangu, bado nina hasira na wewe!” nilituma meseji kisha nikachukua simu yangu, nilimpigia shoga yangu na kumuambia kama mume wangu akimpigia simu na kumuuliza chochote basi amuambie nimelala kwake ninalia na nina hasira hivyo sitaki kusumbuliwa. Baada ya hapo nilizima simu, tuliendelea kunywa lakini muda kidogo simu ya yule Kaka iliita, alionekana kuipaniki, akasimama na kutoka nnje kwani tulikua chumbani.


Alikaa huko kwa kama dakika tano hivi kisha akarudi, aliporudi alinivamia kitandani na kuniambia kuwa anataka tufanye mapenzi, mimi niliona muda bdao, tulikua bado tunakunywa hata kula hatujala na tulikua tuna usiku mzima wa kufanya mapenzi. Nilimuambia kuwa siko tayari tusubiri lakini alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa, alinishika kwa nguvu nguvu akanipandisha kitandani, alianza kunivua nguo na bila kufanya mapenzi vizuri aliniparamia kamavile ananibaka.


Hakuchukua muda alifanya kama dakika tano hivi kisha akaniambia kuwa tulale yeye hawezi kufanya tena. Mimi nilishangaa kwani sikufurahia chochote, tofauti na siku nyingine ingawa ni mtu wa dakika tano lakini huniandaa vizuri mpaka nafurhia tendo la ndoa.


“Mke wangu kapiga simu, natakaiwa kurudi nyumbani, kuna mtu atakua kaniona, sijui ni nani, lakini mke wangu kapaniki, mimi naondoka, nataka kuondoka, sitaki….”


Aliongea kwa hasira, alikua kapaniki sana, mimi nilikua namshangaakwani kwa namna alivyokua anaongea ni kama alikua anamuogopa mke wake. Wakati anaongea simu yake iliita tena, ilikua ni namba ya mke wake, kwani alimsave My wife, kwa hasira niliichukua ile simu na kuipoke.


“Halooo!” Niliongea, lakini kabla ya kuongea kitu alininyan’ganya simu.


“Wewe si unasema unataka kumuacha mke wako!?” Niliropoka, alinitukia na kuanza kunipiga, alinippiga huku akinitukana, nilipiga kelele, alinipiga sana, akinilaumu kwa kumharibia ndoa yake, nilipiga kelele mpaka watu wakaja, w3aligonga mpango na kunikuta nikiwa uchi wa mnyama kwani wakati tunagombana ndiyo tulikua tumetoka kufanya mapenzi.


Watu wa vyumba vya jirani walitokja kwani nilipiga kelele nyingi, karibu wote walikua wanaume kasoro dada mmoja ambaye kwa wakati huo sikumtambua, aliingia harakaharaka na kuchukua shuka, mimi bado nilikua nimeshikwa na bumbuwazai sijitambui, hata kujisitiri nilishindwa. Alichukua shuka na kunifunika, wakati ananifunika ndiyo mimi nilimtambua na yeye alinitambua.


“Wifi unafanya nini hapa na huyu ni nani?” Aliniuliza, kumuangalia alikua ni mdogo wake na mume wangu. Yeye alikua ameolewa na walikua wakiishi arusha. Kunyanyua macho nilimuona mume wake kasimama, alikua ni mmoja wa wale wanaume walikuja kuamua baada ya kusikia keleel, alikua amemshikilia yule Kaka aliyekua ananipiga. Mwili wote ulikufa ganzi, nilishindwa kunyanyua mdomo kujibu nilibaki natetemeka tu kama mtu aliyemwagiwa maji ya barafu.


SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA TATU.


“Naomba mniachie, nataka kurudi nyumbani kwa mke wangu, huyu malaya anataka kuniharibia ndoa yangu!” yuile kijana aliongea kwa hasira, bado watu walikua wamemshikilia, alifanya vurugu mpaka wakamuachia, aliondoka na kuniacha pale ndani.


“Ondokeni sasa si yameshaisha mnashangaa nini?” Wifi yangu aliwaambia baadhi ya wahudumu na watu ambao walikua pale.


“Halafu mbona mnaaibisha, kwanini mnapiga picha, mnajua hili ni kosa la jina!” Wifi yangu aliongea, kulikua na dada mmoja kashikilia simu ananipiga picha, wifi alimfuata na kumkunyja, alichukua simu yake na kumuamrisha afute picha zote, alifuta lakini bado wifi hakuridhika.


“Mlinzi chukua hii simu, hakikisha kuwa kafuta mpaka kwenye Google Drive, mpaka nihakikishe mimi ndiyo atyaichukua his imu, kama ukimpa basi jua kuwa kesho nipo mahakamani hii hoteli yenu mtaeleza kwanini mnaruhusu watu kupiga picha wageni.” Wifi yangu aliongea kwa hasira, alimnyang’anya yule dada simu, mume wake alichukua simu za watu wengine pale na kumpa mlinzi, alimuambia ni lazima wao kuridhika, kwanamna walivyokua wanaongea mpaka mlinzi aliogopa, alizichukua simu zote na kwenda nazo kuzikagua.


Wifi alimuambia mume wake kwenda naye ili kuhakikisha kuwa kila kitu kimefutwa. Baada ya watu wote kuondoka alichukua nguo zangu na kunipa nivae, nilikua bado naona aibu na sikujua kuwa ni kwanini alikua kaamua kunisitiri.


“Kwanini unafanya hivyo wakati nimemsaliti kaka yako?” nilijikuta namuuliza. Wakati ananipa nguo aliona kuwa kwenye shuka kuna shahawa za yule mwanaume, alijua kuwa nimefanya mapenzi hivyo aliniambia nikaoge, nikiwa bafuni niliwaza sana sikupata majibu, nilipotoka nilimkuta kakaa ananisubiri. Nilishindwa kuvumilia ndiyo nikaamua kumuuliza.


“Ndoa sina mambo mengi ndugu yangu, lakini kwa yote yale wewe ni wifi yangu, mke wa Kaka yangu, lakini kikubwa wewe ni Mama, una wanangu, hivi unafikiri hao mbwa wakiamua kukudhalilisha  siku mtoto wakoa anona picha zako za uchi kwenye mitandao atakua sawa?” Aliniuliza, nilijikuta natokwa na machozi, ni kitu ambacho hata mimi sikukifikiria lakini wifi yangu alikua kafikiria, alionyesha kujali kuliko mimi.


“Nisamehe wifi, mimi na Kaka yako sasa hivi hatuko vizuri ndiyo maana nika….”


“Mama kila mtu ana dhambi zake, sina haja ya kukusamehe, sijakuoa mimi, aliyekuoa ndiyo wmenye kazi ya kukuchunga, kama kakushindwa muachane wenyewe kwa sababu zenu amabzo hazinihusu, sikuepo wakati mnatongozana na wala sitaki kuwa sababu ya nyinyi kuachana. Una sababu zako za kumsaliti Kaka yangu na hasininusu. Ninachotaka mimi sasa hivi ni wewe kutoka hapa salama, hujakutana na mimi, hujakutana na mume wangu na wala sitarudia hiki kitu, hii ni ndoa yenu sio yangu!”


Aliongea kwa uchungu lakini kwa kumaanisha, tulikaa pale hcumbani kwa lisaa lizima, baada ya hapo mume wake alirudi, alituambia kuwa kila kitu kiopo salama hivyo tuanaweza kuondopka.


“Nataka tutoke wote, usione aibu na wala usiangalie mtu, tutaongozana.” Aliniambia, nilitoka naye mpaka kwenye gari yangu, nikaingia akaniuliza kama nitaweza kuendesha mwenyewe mpaka nyumbani niakamuambia ndiyo, lakini ukweli nikuwa sikua sa3wa, nilikua natetemeka sana, alichukua simu na kumpigia mume wake ilia toke. Alitoka akaingia kwenye gari langu akaendesha mpaka nyumbani kwangu, mume wake alikua anatufuata nyuma na gari yao.


Tulipokaribia nyumbani alishuka na kuniambia hapa unaweza kuendelea, nenda utajua mwenyewe cha kumuambia mume wako l;akini mimi na mume wangu hatujawahi kukutana. Alishuka na kuniacha, waliondoka na mume wake, niliendesha gari mpaka nyumbani, nilsihindwa kuingia getini, nikawa nimesimama tu kwa nnje gari ipo silent, nilikaa kwenye usukani kama lisaa lizima huku nalia sijui niingie ndani au nifanye nini?


Wakati nikiwa pale kumbe mume wangua liniona, alisikia mngurumo wa gari, alitoka na kuniangalia, alinikuta nimeegemea usukani nalia.


“Unanini mbona uko hivyo?” Mume wangu aliniuliza. Sikua na jibu, nilimuambia tu niko sawa, alitaka kuniingiza ndani lakini niligoma, niliendelea kulia tu, mume wangu alikua anani8angalia kwa huruma, mara akaanza kuomba msamaha akidhani kuwa bado nilikua nimekasirika kwasababu ya yeye kunipiga kipindi kile, niliboreka na msamaha wake nikaamua kuingia ndani bila kusema chochote.


Sikula wala kufanya kitu, moja kwa moja nilielekea chumbani na kulala asubuhi baado nilikua na mawazo, sikua nikimuwaza mume wangu bali yule Kaka. Kwa kipindi chote cha mahusiano yetu nijua kuwa ananipenda, nilijua kuwa yupo tayari kumuacha mke wake kwaajili yangu, lakini usiku ule wakati mimi nikiweka rehani ndoa yangu yeye alikua anambembeleza mke wake, alikua hataki hata mke wake kujua kuwa yuko na mimi.


Kitendo hicho kiliniuma sana, ilikua nis iku ya kazi lakini nilishindwa hata kwenda kasini. Mume wangu aliniacha na huzuni na kumuambia kuwa siko sawa siwezi kwenda kazini. Nilipiga simu kazini na kuwaambia kuwa naumwa, lakini ilipofika saa nne nilishindwa kuvumilia, niliingia kwenye gari na kwenda kazini. Nilikua na mawazo sana hivyo nilitaka mtu wa kuongea naye kwani nilijihisi kama kuchanganyikiwa.


Nilimfuata shoga yangu na kumuambia kila kitu kilichotokea, nilimuambia jinsi nilivoumizwa.


“Unafikiri kwelia ananipenda,a naweza kumuacha mke wake?” Nilimuuliza, abdo nilikua nampenda yule kijana, sijui ni nini kilikua kinaniumiza zaidi yeye kunipiga au kile kitendo cha yeye kukasirika baada ya mimi kuongea na mke wake. Mpaka wakati huo alikua hajanitafuta na mimi nilikua sijamtafuta nikimtegea yeye ndiyo aanze kunitafuta, nilikua kwenye maumivu makali sana.


“Wewe nawe, unataka amuache mke wake ili nini? Wanaume kama wale ni wakupoozea, sasa unataka kuolewa wakati una ndoa?” rafiki yangu aliongea kwa hasira, alinichamba sana kwanini nilikua nataka kumuacha mume wangu kwasababu ya mchepuko, safari hii hakua upande wangu kabisa. Alinishauri mambo mengi lakini sikutaka kumsikiliza, niliona kama nayeye ananichanganya tu, nilimuaga na kurudi nyumbani, njia nzima nilikua na mawazo, niliendesha gari mara mbili nikitaka kwenda kwa yule Kaka lakini nilisita, alikua hajawahi kunilepeka kwake lakini nilishachunguza na kupajua, hata mke wake nilikua namjua.


Baada ya kuzunguka sana mjini nililamua kurudi nyumbani kwangu. Nilimkuta mume wangu asharudi na alikua ameniandalia chakula cha mchana, mume wangu anajua sana kupika, pamoja na ubize wake lakini mara nyingi nikiwa nina mawazo alikua ananipikia chakula kizuri, huwa napenda ndizi hivyo anazimenya mwenyewe na anazipika.


“Nimekupikia ndizi, nilijua utakua nyumbani, nahisi utakua sawa.” Aliniambia, niliziangalia zile ndizi na kuona kama kinyesi tu, nilikua na mawazo yangu niliona kama vile nayeye ananichanganya tu.


“Siaki kual mimi siko sawa, nimeshiba!” Nilimuambia kwa hasira na kuingia zangu chumbani, uzalendo ulinishinda, nilichukau simu yangu na kuanza kumpigia yule kijana, nilipiga zaiodi ya mara tano lakini hakupokea, baada ya kuona kimya nilazna kutuma meseji, nilituma meseji nyingi sana za lawama huku nikimuuliza kama badoa ananipenda, kwanini aliniacha na mambo kama hayo, niiuliza mambo mengi lakinihaikujibiwa hata meseji mopja.


Baada ya kuonakuwa hapokei simu zangu niliamua kuchukua simu ya mume wangu, nilimpigia kwa namba ya mume wangua ambayo hakua nayo, simu iliita mara moja akapokea.


“Halooo! Halooo! Halooo! Halooo!”  Aliongea, nilisikia sauri yake nikaw akama nimechanganyikiwa, sikusema kitu chochote nilitaka tu kuendelea kumsikiliza.


“Wewe nani mbona huongei? Haloo! Halooo!…” Aliendelea kuongea, alipoona sioongei chochote alkata simu, akanitumia meseji kwenye simu yangu.


“Wewe Malaya syuitaki uendelea kunitafuta kama huna cha kufanya kaaa na huyo bwege wako hata mtengeneze watoto msinisumbue mbwa mkubwa wewe!”


Nilijikuta naanza kulia, mume wangu alikua sebuleni anaangalia mpira, nilimrudishia simu yake na kurudi cnumbani, alikua hana chakufanya kwani hata mpira wenyewe aliokua akiangalia ulikua ni marudio, alikua na mawazo sana,a liponiona nalia alikuja chumbani, hakunisemesha chochote alikaa pembeni yangu na kuniuliza.


“Hivi mke wangu unafikiri kuna wakati tunaweza kurudi kama nyuma, unaweza kuja kunisamehe kweli?” Aliniuliza. Mimi nilibaki kimya nalia tu.


“Najua nilikosea kukupiga, zilikua ni hasira ila tuna watoto, nikuambie tu kuwa sijawahi kuchepuka, lakini kama unaona kukiri kwangu kutakupa amani basi niliwahi kuwa na mahusiano na yule dada na naomba unisamehe kwa hilo.” Sijui nilipata wapi nguvu lakini baada ya kusikia kukiri kwake nilinyanyuka kitandani, ni kama alikua kanipa kiotu cha ukweli cha kukasirikia. Katika kipindi chote nilikua namkasirikia mume wangu wka dhaana kuwa anchepuka lakini sasa hivi alikuakakubali mwenyewe kuwa kachepuka hivyo nilikua nasababu ya ukweli ya kumkasirikia.


“Nilijua tu kuwa upo na yule mwanamke, ndiyo maana hunipendi, hujawahio kunipiga hata siku moja wala kunitukana lakini nilipomgusa Malaya wako ukanipiga!” nilikasirika sana, nikamtukana mpamka basi, nilimuambia kuwa simtaki ni bure tutengene, kwakua kila mtu alikua ananiona kama mimi ndiyo mwenye matatizo, nilchjukua simu na kumpigia Mama yangu, yeye ndiyo alikua mtu wa kwanza kunishutumu na kuniambia kuwa namsingizia mume wangu.


Nilimpigia simu na kumuambia kuwa mume wangu kakubali kuwa alichepuka an ananiomba msamaha, Mama yangu alinisikiliza na kunaimbia maneno ambayo yalizidi kunipa hasira.


“Wewe ni mpumbavu, unavunja ndoa yako kwa mikono yako, acha huo ujinga mwanangu….” Nilimkatia simu sikutaka aharibu furaha yangu. Nilianza kupigia ndugu wengine, nikapigia simu mpaka wakwe zangu na kila mtu kumuambia kuwa mume wangu anachepuka na amekiri. Wakati wote huo mume wangu alikua mkimya, kanyamaza ananiangalia ninachofanya.


“Kama hicho ndiyi kitakupa furaha unisamehe basi muambie kila mtu ila nataka kurudisha mke wangu wa zamani, nimechoka kuishi haya maisha ya kununiana kila siku.” Mume wangu aliniambia, nilikasirika kwani alionekana kama vile anakubali uongo wakati mimi nilishajiaminisha kuwa mume wangu ni msheni anachepuka. Nilinyanyuka harakaharaka kitandani na kuanza kukusnaya nguo zangu, nilimuambia kuwa siwezi kukaa naye nyumba moja kwani kanisaliti hivyo ninachotaka ni talaka yangu.


Sikweli kama nilikua nataka talaka lakini nilitaka aache kuongea ili nifurahie angalau kaushindi kidogo, nilitaka kuwa naye. alinisihi sana nisiondoke kwabni nilikua sijafanya kosa lolote.


“Kama ni kuondoka nitaondoka mimi, keshokutwa watoto wanarudi kutoka shuleni, ni bora kukuta Baba hayupo kuliko Mama, kama huwezi kuishi na mimi, kama unahiraji muda wa kufikiria basi mimi nitaondoka, nitaaga kuwa nimesafiri kikazi ili watoto wasiju tuna matatizo.” Aliniambia kwa upole lakini nilijikuta nazidi kukasirika.


“Inamaana unataka kuonekana malaika, mimi nikikosea unataka kila mtu ajue, lakini wewe mwema umekosea hutaki watoto wajue. Tunawafundisha nini watoto kama hatutawaambia ukweli, ni lazima wajue ukweli kuwa Baba yao ni Malaya na wajue kuwa kuvurugika kwa  familia hii ni makosa yako si yangu!” Nilimuambia, niliongea sana mpaka mume wangu akaanza kupatwa na hasira.


“Ngoja nikuache maana naona kama hatutaelewana.” Aliniambia, hasira zilimpanda hivyo hakutaka kukaa karibu na mimi, aliondoka na kuniacha chumbani nikiwa namuwaza mchepuko wangu.


****


Wiki moja ilipita bila yule Kaka kunitafuta, nilishamtumia meseji nyingi lakini hakujibu hata moja. Kila siku nilikua nikienda baa nikimuambia mume wangu kuwa nataka kupunguza mawazo lakini haikua kweli, lengo langu kubwa lilikua ni kukutana na yule kaka. Nilihangaika kwa kumuulizia lakini hakuna mtu hata mmoja ambaye aliniambia ukweli, roho iliniuma sana, nilijisikia sana vibaya kwani aliniacha kama takataka.


Sikumoja nakumbuka ilikua kwenye saa mbili usiku, mume wangu alinipigia simu lakini sikupokea, nilishakua mlevi kila siku nakunywa najifanya nina mawazo ya kusalitiwa. Nikiwa pale yule Kaka alikuja, tofauti na nilivyidhani kuwa atanikasirikia alikuja na kunisalimia, alionekana kuchangamka, nilitamani kumpotezea ili angalau anibembeleze lakini nilishindwa, nilikua nampenda sana hivyo nilijikuta namuitikia vizuri tu.


“Unajua wewe huna akili…” alianza kuongea kwa dhauaru ile ya kweli kweli, pamoja na mwanga hafifu wa taa lakini niliona macho yake yalivyokua yakiniangalia kwa kinyaa. Nilijitahidi kubnyamaza, sikutaka kumjibu nilikaa kimya.


“Nikwavile tu nakupenda lakini tofauto na hapo ningekuachilia mbali.” Aliniambia, nilinyamaza kimya, nilitamani kumrukia na kumukumbatia baada ya kuniambia kuwa ananipenda lakini nilijizuia, nilitaka amalize kuongea, sikutaka kuonyesha pupa.


“Wewe nimekuambia kuwa nataka kumuacha mke wangu taratibu, sasa hivi umefanya ujinga mpaka kajua kuwa ninachepuka. Amejua kuwa nataka kumuacha amekasirika, umenifanya hata nikutukane ili tu aamini kuwa sikupendi lakini kakasirika na sasa naataka tuachane kabla mipango yetu haijakaa sawa.” Aliniambia, nilishtuka kidogo, alianza kunielezea kuwa ananipenda lakini siku ile alikasirika kwakua mimi niliongea na mke wake kabla mambo yake hayajaw asawa.


Aliniambia kuwa jkuna mali nyingi sana ambazo alichuma kwa majina ya mke wake kwakua alikua anampenda, aliniambia kuwa alitaka nimpe muda ilia badilishe majina, baad aya mimi kupokea simu yake na kutuma mesji basi mke wake alishtuka na sasa hivi amekua mkali, ameficha nyaraka zote na hajui kama atafanya nini.


“Kwahiyo ulikua unanitukana ili kumridhisha mke wako?” Nilimuuliza, aliniangalia kwa tabasamu, alichukua mikono yake na kuipitisha kifuani kwangu, alianza kunitomasama matiti huku akichezea chuchu zangu kama vile anachambua maharage, nilisikia raha ya ajabu, hakuona aibu na mimi nilishindwa kujizuia.


“Hivi kweli naweza kutukana mtoto mzuri kama wewe, nilitaka mke wangu ajisikie vizuri, ajue kuwa sikutaki lakini ukweli nikuwa yule mwba namuacha, umeniharibia lakini nifanye nini, bado nakupenda. Nimejaribu sana kukusahau, nilitaka kukununia, kukaambali na wewe lakini nimeshindwa. Mke wangu aliniambia kuwa hataki niwasiliane na wewe, hataki nitoke nyumbani lakini mimi ni mwanaume, siwezi kuishi bila hii kitu yako, sijui hata umeweka nini?” Alinaimbia, shid ahaikua maneno yake bali namna alivyokua anayatamka, kwa mwanamke yoyote angeweza kuchanganyikiwa kabisa.


“Jinsi ninavyokupenda nimeamua kumuacha mke wangu na kila kitu, yaani sitaki tena kuhangaika na mali, namuachia kila kitu nataka kuanza kuishi na wewe.” Aliniambia, kwanza nilishtuka kuona kuwa anaacha kila kitu, aliniambia ana nyumba mbili, magari manne na biashara, sasa anaacha vyote kwaajili yangu, nilishtuka lakini nilijisikia vizuri, nilijiona kama malikia ambaye napendwa mwanaume anakua tayari kuacha kila kitu kw3aajili yangu.


Tuliongea mengi sana, nilimuambia kuhusu mume wangu, nikamuambia kuwa tumegombana hivyo nataka kuachana naye, nataka talaka. Hapo alishtuka kidogo, niliona kama vile hataki nidai talaka kwa mume wangu.


“Mbona kama umeshtuka, inamaana hutaki niachane na mume wangu, hutaki nije kuoana na wewe tuwe pamoja?” Nilimuuliza, akabadilika kidogo, akatabasmu kisha akaniambia.


“Tatizo lako unakurupuka, unataka kumuacha mume wako kama mimi nilivyomuacha mke wangu, wewe ndiyo umesababisha mpaka mimi kaucha kila kitu, lakini mume wako bado hajajua kuwa unachepuka, unatakiwa kuchukua kila kiti kabla ya kumuacha, usiwe na pupa, maana mimi nimeacha kila kitu, sasa unafikiri kama na wewe ukiacha kila kitu tutaishije?”


Nilimuona kama yuko sawa, alinishauri mambomengi, aliniambia nijifanye mjinga, nimsamehe mume wangu, niwe karaibu naye na nimvumilie lakini wakati huo ananiomba msamaha nijipange kuchukua mali zangu.


“Ukitaka talaka utachelewa, hizi ndoa zetu zinachelewesha sana, mpaka mnamalizana mambo ya talaka ni miaka miwili mpaka mitatu, mpaka inafika hatua mnagawana mali miaka mitano, ni ngumu sana, unachotakiw akufanya ni kumfilisi mume wako, kuchukua mali zote mpaka anashtuka unamuacha hata pes aya kuhonga mahakamani hana, talaka unafanya miezi mitatu tu tunaishi pamoja wakati huo na mimi nishamuacha mke wangu.”


Alinishauri mambo mengi na yote niliyaona ya maana, aliniambia niache pombe na nibadilike sana ili mume wangu kuniamini, niahe kabisa mambo ya kuachana na mume wangu mpaka nitakapoochukua kila kitu. Niliondoka na kurudi nyumbani nikiwa na furaha, kitu cha kwanza kufanya ni kupiga magoti, nilimuomba msmaaha mume wangu kwa kuwa na hasira na kumshutumu vitu vibaya, nilimuambia kuwa hata kama kweli kafanya au hajafanya mimi sijalil yeye ni Baba wa watoto wangu hivyo nimemsamahe.


Mume wangu alishtuka kidogo lakini alifurahi, tuliongea mambo mengi usiku ule mpaka asubuhi. Mchana nikiwa kazini yule Kaka linipigia simu, aliniambia anataka kuonana na mimi mchana ule, nilienda kuonana naye, akaniambia kuwa anataka tufungue Biashara hivyo kitu cha kwanza cha kufanya ni mimi kuchukua hati ya nyumba ambay0 ina jina langu na kuchukua mkopo benki, bila kumuambia mume wangu na nilishachukua basi tufungue Biashara yetu pamoja mimi nayeye.


SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA NNE!


Mambo yalienda harakaharaka, yule kaka alikua na mipango mingi sana, alinipeleka sehemua mambapo alikua na rafiki yake, huyo rafiki yake alikua anauza Pikipiki kutoka china, aliniunganisha na kuniambia kuwa kama yukipata kama milioni mia mbili hivi basi itakua rahisi kuanza biahsara kubwa./


“Kizuri nikuwa utafanya kila kitu bado ukiwa kwenye ndoa na ni ngumu mume wako kujua kuwa nyumba umechukulia mkopo kwani tutakua tukirejesha kila mwezi.” Aliniambia, alikua na mawazo mazuri lakini nilikua siwaamini wanaume.


Nilishasikia wanawake wengi wakitapeliwa hivyo sikutaka kuwa mmoja wao.


“Lakini kila kitu kinakua kwenye jina langu maana pesa yote natoa mimi?” Nilimuuliza ili kumpima kama ananipenda au la, nilijua kwua kama anataka kunidanganya ili anitapeli basia tataka tuandike majina yake. Tulikua tumesimama kwenye duka la huyo Kaka, lilikua kubwa zuri linavutia, alikua akinielezea kuhusiana na hiyo biahsara. Yule kaak alinivuta upande wake,a kaniweka kifuani kwake nikawa namuangalia kwa juu, alizungusha mkono wake wakulia kwa nyuma, akaingiza kwenye suruali yangu na kuanza kunichezea makalio.


Aliniinamia shingoni, huku akiongea kwa sauti yake nzuto akinilambalamba shingo aliniambia.


“Mimi nakuamini, nakupenda, kila kitu kinakua kwa jina lako, sikukupendea mali nakupenda wewe, kama ni pesa mbona mimi ninazo, ninachotaka ni wewe uondoke katika dnoa yako ukiwa na kitu, nawajau wanaume, najua anaweza kukutapeli kila kitu.” Aliniambia, kusema kweli nilichanganyikiwa, nilihisi kamakuna minyoo inacheza kwenye tumbo langu, aliedneela kunichezea mbele ya rafiki yake, rafiki yake kuona vile alitoka, alipotoka tu aliniambia.


|Au tufanyie hapahapa, nina hamu sana na wewe, tangu uwe karibu na mume wako mpaka napata wivu….” Aliinamisha kichwa chake mpaka kifuani kwangu, ulimi wake ulianza kuchezea matoto yangu, nilitamani kumrukia palepale lakini niliona aibu.


Tuliachiana baad aya wateja kuingia. Ingawa kuchukua mkpo mkubwa kama ule inachukua muda mrefu lakini sijui alifanya nini, kila kitu kilikamilika ndani ya mwezi mmoja na kwakutuumia nyumba yangu ambayo tulijenga na mume wangu tulipata mkopo wa milioni 195. Zilikua ni pesa nyingi sana kwa watu wanaoanza Biashara lakini rafiki yake huyo ambaye ndiyo alinipeleka kwake alikua na Biashara kubwa zya zaidi ya milioni mia tano, benki walikua wanamjua.


Kweli Biashara ilifunguliwa na kila kitu kilikua na jina langu, yaani ni kila kitu, aliniaacha nisimamie mimi na hakua akichukau hata shilingi. Biashara ilienda vizuri, akwa anaenda mpaka China na huyo rafiki yake kuchukua mzigo huku mimi nikisimamia kila kitu huku Tanzania. Nilitamani sana kuchana na mume wangu lakini kilichokua kinanizuia ni yule Kaka. Kila sikua likua anataka kusogeza mbele suala la mimi kauchana na mume wangu, aliniambia kuwa kaachana na mke wake na kweli muda mwingi mchana alikua anatumai na mimi lakini usiku nililazimika kurudi mapema kwa mume wangu kwani alinisisitiza nisimuudhi mume wangu.


Nilishamuambia kuhusu kuachana lakini nilichoka, nilikua na kila kitu, Biashara ilikua inaenda vizuri sikuona sababu ya kuendelea kuhangaika na mume wangu. Kusema kweli nilishachoka kuigiza, kuishi na mwanaume ambaye naona kabisa simpendi, nalazimika kufanya naye mapenzi kila siku kweli nilikuanaona kabisa ni kama ananibaka hivyo nilitaka kuondoka na kuanza maisha yangu mapya ambayo hayamhusu yeye.


Siku moja mimi na mume wangu tulienda arusha, ilikua ni katika msiba, wifi yangu yule ambaye alinifumania na kunisitiiri alikua kafiwa na mtoto wake mdogo wa mwezi mmoja, alikua ndiyo katoka, yeye kaolewa huko hivyo mazishi yalifanyika huko huko, mimi na mume wangu tulienda kwani tuko vizuri tu. Lakini kufika kule, kumuona wifi yangu na kumuona mume wake nilijisikia vibaya, kuna kitu kama kisirani tu kiliiniingia, sijui kilitoka wapi lakini nilijihisi vibaya.


“Hivi kweli ilikua bahati mbaya au hawa washenzi walikua ananifuatilia?” Nilijiuliza wakati nasalimiana na wifi yangu, ndiyo tulikua tumeingia kwakua alikua ni mtoto na sisi tulichelewa basi alishazikwa, sisi tulifika jioni. Nilimsalimia wifi yangu ambaye aliniitikia vizuri, tu, alikua analia amelala kwa hali aliyokua nayo hakuweza hata kumzika mtoto wake, alikua kajifungua kwa oparesheni lakini mbaya zaidi alikua na presha ya kuanda na kila mara alikua ni mtu wa kuzimia kitu ambacho kilikua ni kibaya zaidi.


Baada ya kusalimiana naye mimi na mume wangu tulitoka, mume wake alikua hayupo hivyo wakati tunatoka sebuleni tunaenda jikoni kusalimia watu wengine tulikutana na mume wake. Alisalimiana na mume wangu ile kizungu, kukumbatiana na aliponisalimia mimi alitaka kufanya hivyo lakini niligoma, nilimpa mkono tena kwa haisra, ilikua ni jioni jioni hivyo watu wengi hawkauona kwani kigiza kilishaanza kuingia, lakini mume wangua liona, na kuuchuna.


Tuliachana naye tukaenda kusalimiana na ndugu wengine, mimi nilirudi ndani lakini wakati nikwia ndni mchepuko wangu ulipiga simu, nilityoka kidogo kwenda kuongea anye, niliongea kama dakika kumi hivi baada ya hapo nilirudi ndania lipokua wifi yangu. nilihisi kaama ananiangalia vibaya, nilijisikia vibaya, nikaachana naye nikawa nachat kwenye simu na Baby wangu.


“Wifi unaendeleaje na Kaka yangu, wazima huko?” Alijitahidi kuongea, kusema kweli nilihisi kama ananichokonoa, sikutaka kuongea naye nilitingisha kichwa kuonyesha kuwa tuko sawa kisha nikainamia simu yangu na kuendelea na mambo yangu.


Aliendelea kuniongelesha kitu ambacho kiliniumiza zaidi, nilinyanyuka na kutoka nnje, wakati natoka sasa nikakuta mume wangu amekaa na shemeji yake wapo wawili tu wanaongea. Kuna kitu kama kilinikaba kooni, nilihisi kama kuna kitu anamuambia, nilimfuata mume wangu, nikamshika mkono nakumuambia kuwa tutoke mimi siwezi kulala pale. Mume wangu alsihangaa, ili kuepusha shari alinifuatampaka kwenye gari yetu.


“Unajua kwanini sijamsalimia vizuri shemeji yako?” Nilimuuliza, mume wangu alibakia nanishangaa tu, alinitolea macho kana kwamba ananiambia sema.


“Ananitaka, yaani amekua akinitongoza mud amrefu, ananiabia mamboa ya dada yako mpaka naonaaibu.” Nilianza kumuelezea mume wangu, kusema kweli nilihisi labda shemeji yake anataka kumuambia kuhusu mimi na kumfumania. Niliamua kumuwahi ili kama ataongea basi aonekane muongo.


“Ananitongoza na kibaya zaidi anamsema vibaya wifi yangu, yaani anaongea maneno mengi hata kipindi wifi kajifuingua si alikuja Dar, basia linifuata mpaka kazini na kuniambia kuwa kaamua kukaa mbali na mke wake kwani anahofia kama akikaa karibu naye anaweza kumuua kwani anahisi kwua huyo mtoto si wake.” Nilimuambia mume wangu maneno mengi yauongo lakini hakuonekana kabisa kunisikia, alionekana kutokuniamini, nilitamania niamini san alakini hakuonekana kuniamini.


“Tuko kwenye msiba, tumalize msiba kwanza.” Mume wangu aliniambia nakuondoka kurudi ndani, mimi ndiyo nilikua na funguo za gari, hata mizigo yetu tulikua bado hatujashusha, kwa haisra niliingia kwenye gari, nikawasha na kwenda kutafuta chumba. Nilijua kuwa mume wangu atanifuata lakini hakunifuata, hakutuma meseji wala kupiga simu mpaka asubuhi, yaani nilikaisrika, asubuhi nilimtumia meseji na kumuambia kuwa simtaki nataka talaka yangu. Alionekana kuisoma ile meseji lakini hakujibu meseji na wala hakunipigia simu.


Mimi si mzoefu sana Barabarani lakini kwa hasira nilijaza gari mafuta nikazima simu zangu, nikaendesha gari kutoka arusha mpaka Dar, nilikua na hasira, sikusimama njiani, nilichoka sana niliondoka Arusha saa mbili asubuhi na kufika Dar saa sita usiku, nilichoka sana. Nililala mpaka asubuhi na mume wangu hakunitafuta kabisa, hali hiyo iliniumiza sana kwani alionekana kama vile kachoka, niliwaza mambo mengi nikihi labda wifi yangu kamuambia kila kitu ndiyo maana kakasirika.


Haikua kawaida ya mume wangu kuniona nimekasirika na kunyamaza tu, nilihisi kuna kitu, asubuhi kwakua nilikua na ruhusa ya wiku tano kazini sikua na pakwenda. Siku ilikua ndefu sana kwani nikimpigia kijana wangu alikua hapatikani, simu ilionekana kuzimwa. Nilivumilia nikashindwa, nikampigia simu mume wangu nakumuambia kuwa jana yake nilikasirika nikaendesha gari mpaka dar mimi mwenyewe, niliongea maneno mengi lakini alinipa jibu moja tu.


“Hongera umekua dereva mzuri.” Aliongea kisha akakata simu, nilijikuta napaniki, nachanganyikiwa, niliona kabisa kuwa mume wangu huyu ananiacha, nilijisikia vibaya sana kuona kuwa mume wangu ananidharau kiasi kile.


Akili yangu iliwaza tu kwa wifi yangu na mume wake, nilishindwa kujizuia, nilichukua simu yangu na kuanza kumtumia wifi yangu meseji. Kwanza nilianza kumshutumu kwa kunitangaza kuwa mimi ni maloaya, niliandika mambo mengi sana lakini mwisho nilimuandikia.


“Ukinitangaza kuwa mimi ni Malaya usisahau na kumtangaza na mume wako au hujui kuwa alishanitongoza na alikua ananitaka.” Nilimtumia ile meseji, dakika mbili tu alinipigia simu na kuniuliza nilikua namaanisha nini?


“Sasa hivi ndiyo unajifanya kuwa unaona meseji zangu, baada ya kumtaja mume wako ndiyo unashituka, ulikua unaona ndoa yako ina amani sana lakini nikuambie tu kuwa huna tofauti na mimi, mume wako ni Malaya na alishanitongoza mara kibao, ningetaka kumchukua ningemchukua, hata nikimtaka leo namchukua, na kwa taarifa yako huyo mtoto alishamkataa, si wake hivyo usione anakuchekea ukadhani anakufurahia, mume wako ni Malaya na kama mshanitangaza kuwa ni Malaya basi jua kuwa hata wewe unaishi na Malaya.” Nilimuambia maneno mengi sana, alinisikiliza kisha akaniambia.


“Mimi na mume wangu hatuingilii ndoa za watu, naomba usimuingize mwanangu kwenye mambo yako, malizana na mume wako.” Alikata simu na nilipomiga tena haikua ikipatikana, nilikasirika sana nilimpigia tena simu mume wangu lakini hakupokea, nilianza kumtumia meseji nyingi za kumtishia kumuacha lakini hakuijbu hata moja. Niliumia sana, nilitoka ndani nakuazna kuzunguka na gari, bila kujijua nilijikuta nimefika nyumbani kwa mchepuko wangu. Sikui nilienda kufanya nini lakini nilishuka kwenye gari, nikagonga mpango na kufunguliwa, nilimuulizia Mama lakini niliambiwa kasafiri, Baba nikaambiwa ndiyo katoka. Basi niliaga nakuondoka huku nikiwa na mawazo mengi.


“Kama kaachana na mke wake kwanini bado anaishi hapa, vipi kule alikosema kaenda kupanga, atakua anaishi kule kwelia u ni nini?” nilijiuliza maswali mengi bil majibu, nilizunguka sana mwisho nikaamua kurudi nyumbani kwangu. Jioni kwenye saa kumi na mbili hivi simu yangu iliita,  alikua ni yule Kaka mchepuko wangu, nilipokea kwa furaha kutaka kumuambia kuwa nimemkiss lakini hakunipa nafasi.


“Siku nyingine ukifanya ujinga wa kuja nyumbani kwangu nitakukeketa kwa meno!” Aliniambia, nilijifanya kukasirika kumuuliza kuhusiana na mke wake na kwanini alinidnaganya kwua kashaachana na mke wake kumbe bado.


“Nadhani hujanisikia, naona unataka kunipanda kichwani kama unavyompanda huyo mume wako, sikiliza wewe Malaya na usikilize vizuri. Siku ukithubutu kukanyaga nyumbani kwangu basi jua kuwa nitakukeketa kwa meno, ndoa yangu iko vizuri, nimejaribu kuisuluhisha baada ya upumbavu wako lakini etu inakuja kwangu kuniulizia? Hivi una akili kweli, nimekuambia kuwa usikanyage kwangu na sitaki kukuona kabisa mbwa kabisa wewe!” Aliniambia kisha akakata simu, nilitamani kukasirika lakini nilikumbuka kuwa alishanitukana mwanzo inawezekana yupo na mke wake ndiyo maana ananitukana.


Ingawa nilikua na wasiwasi lakini nilijipa moyo kuwa hawezi kuniacha kwani ananipenda niyo maana tumefungua Biashara pamoja. Niliondoka na kwenda ukani, niliangalia kila kitu nikakuta kiko sawa, nilimuulizia kama yeye kafika pale dukani lakini nikaambiwa hapana, basi nilirudi nyumbani ambapo nilikua nimechoka, nilipanda kitandai huku nikiangalia simu yangu kuona kama atapiga simu lakini hakupiga tena, mume wangu naye hakunipigia.


Ingawa nilikua na ruhusa kazini lakini nilishabpreka kukaa nyumbani, nilitondoka kwenda kasini, ile nafika tu yule Kaka alinipigia simu, alitaka tuonane, alikua anaongea kwa ustaarabu kabisa, nilimsikiliza nikijua kuwa ataomba msamaha kwasababu ya kunitukana lakini hakufanya hivyo, tuliongea mambo mengi ila mwisho akaja kuniambia kuwa hataki tena kuendelea na mimi kwani anaona kuwa namtia mikosi tu hakuna raha yoyote naayopata.


“Rudi kwa mume wako na mimi nirudi kwa mke wangu.” Aliniambia, nililia sana kumuomba msamaha lakini hakukubali, aliniambia kuwa ananiachia kila kitu na hachukui hata shilingi kumi.


“Nitalipaje deni la benki? Nitaendeshaje Biashara, mimi sijui chochote, naomba unisaidie, naomba….” Nilimbembeleza sana mpaka akakubali kunisaidia kuhusu biahsara mpaka nitakapomaliza deni benki, aliniaga na kuondoka. Kusema kwlei niliumia sana lakini nililazimika kuendelea kuwa naye kwani kuna mzigo kama wa milioni 120 ambao tulikua tumeagiza china nayeye ndiyoa likua anajuana na muagizaji hivyo sikutaka kumuudhi, ingawa niliumia lakini nilijua kuwa kama nisipokua makini nitapoteza kila kitu.


Nilirudi nyumbani nikiwa kama nimechanganyikiwa, sikua sawa kabisa, nikikumbuka mamboa mmbayo nimeyafanya msibani nilijua kuwa itakua ngumu sana kwa mume wangu kunsamehe. Mume wangu alirudi siku hiyo hiyo kwenye saa nne usiku ndiyo alifika nyumbani, nilimsalimia vizuri nikijua labda ana hasira ila aliniitikia vizuri. Aliingia akaoga lakini nilipomtengea chakula mezani hakutaka kula, aliniambia kashiba hivyo hawezi kula.


Lakini aliniita chumbani alikua na mazungumzo. Kwa namana livyokua anaongea nilijihisi kuna kitu kikubwa kaambiwa.


“Nakupenda sana lakini naona kuna wakati mwingine mapenzi hayatoshi. Juzi uliondoka, sikukufuata kwakua nilishachoka, dada yangu kafiwa na mtoto wake halafu unataka tuhangaike na mambo ya kijinga…” alianza kuongea, nilitaka kumkatisha lakini alinizuia.


“Kila siku unataka kuongea wewe lakini leo naomba nionge, usinikatishe kwani hii ndiyo mara yangu ya mwisho kuongea na wewe. Kuna mambo mengi sana unafanya, najua lakini kama mwanaume ambaye napenda familia isimame basi navumilia nakua mjinga.


Tangu kukuoa sijawhai kukusaliti, mimi najua, wewe unajua na Mungu anajua,   hata wewe siwezi kusema kama umenisaliti kwakua sijawahi kukufumania, najua umuaminifu na unanipenda lakini kuna wakati mapenzi tu hayatoshi, naona kama vile nitachanganyikiwa na nitafanya maamuzi mabaya. Nilitaka kuishi pamoja kwaajili ya watoto lakini naona kuwa haifai, nikiwa kwenye gari nimesoma meseji zako zote ila kusema kweli naona nikupenafasi, nahisi umenichoka sana.”


Mume wangu alikua anaonghea huku analia, nilishangaa kwani kwa maneno yake ilionekana kabisa kuwa wifi yangu alikua hajamuambia kitu chopchote. Aliongea mambo mengi lakini alisisitiza kuwa hajwahi kunisaliti na anashukuru Mungu na mimi nimuaminifu.


“Nimekuvumilia mambo mengi kwakua pamoja na kuwa una changamoto zako lakini umuaminifu kwnagu.  Pamoja na yote hayo lakini siajwahi kusikia kuwa una mwanaume mwingine au unanisaliti, hilo kwangu nikubwa, ndiyo maana nilikua nakuelewa unapokasirika na kuwa na wivu kwani najua ni mapenzi.


Lakini kama umeona kuwa huwezi kuwa na mimi naona kabisa ni suala la kuahcana, inabidi tutengane kidogo kweli sitaki kukupa talaka ila sidhani kama naweza kuendelea kuishi na wewe waktai najua kuwa hunitaki….” Nilishindwa kuvumilia, nilimfuta mume wangu nakumpigia magoti, nililia sana na kuomba msamaha, nilimuambia kuwa nimejutia anipa nafasi nyingine lakini aligoma, aliniambia mimi ndiyo natakiwa kukaa pale kwenye nyumba nayeye ataondoka. Kuna nyumba nyingine ambayo alikua anajenga, ilikua bado haijakamilika vizuri lakinia lihamia hivyo hivyo.


***


Mume wangu aligoma kabisa kunisamehe, alikua si kwamba alikua haniamini labda nina wanaume wengine hapana, hilo hakuonekana kuwa na hsaka nalo, mpaka nilishangaa kuwa pamoja na yote lakini dada yake hakumuambia ukweli, kuna wakati nilidhani hata labda ananizuga anajua ukweli lakini haikua hivyo. Alikaa peke yake kwa mwezi mmoja, wakati wote huo mimi nilikua namuomba msamaha. Alinaiambia kuwa hayuukovizuri kurudi kwani anaona kuwa ana hasira sana.


Wakati wote huo biahsara ilikua inaenda vizuri, bado nilikua nasubiria mzigo kutoka china, waliniambia kuw3a ndiyo uko majini na picha nilitumiwa. Yule Kaka alikata mawasiliano kabisa na mimi, hakua akipokea zimu zangu na aliniblock kabisa, mara moja moja akitaka kuongea kuhusu Biashara alikua akinipigia kwa namba ngeni ambayo baada ya muda alikua hapatikani. Nilishamuomba msamaha mpaka nikachoka ikafikia wakati nikaamua kubaki tu na mume wangu.


Watoto walifunga shule, aliporudi nyumbani kitu cha kwanza ilikua ni kumuulizia Baba yao, niliwaambia kasafiri, jioni yake nililazimika kumtafuta mume wangu na kumuomba kurudi nyumbani katika kipindi cha likizo ili angalau watoto wamuone. Kwakua alikua anawapenda sana watoto wake na hakutaka kuwaumiza alirudi, maisha yaliendelea, tulikua tunalala chumba kimoja lakini mume wangu alikua akilala chini.


Mume wangu ananipenda hivyo nilijjua kuwa kwa kurudi hawezi kuvumilia, nilimfantyyia vituiko, nikabadilika na kujidekeza mpaka tukarudiana, hata watoto walipomaliza likizo hakurudi tena kule alipokua akiishi tulirudiana na maisha yaliendelea. Nilikua na amani na nilaimua kabisa kuwa natulia na ndoa yangu, lakini shiod ailikua kwenye hatai ya nyumba na Biashara. Yule Kaka kila mara alikua anakuja dukani kuchukua pes, alikua ananiambia anaagiza mzigo mwingine, kumbuka hapo mzigo wa kwanza naambiwa upo kwenye maji.


Alichukua mpaka nikaona kama duka linakua jeupe, nilimuuliza na kuamua kuwa mkali, ndipo aliniambia kuwa. Kule China kuna mtu wanamtumia, katika kutoa mzigo iligundulika kuwa huyo mtu anajihusiha na dawa za kulevia na alikamatwa karibu miezi miwili nyuma hivyo pesa alizokua anachukua kila mara kuniambia kuwa analipia mzigo mwingine ilikua ni kwaajili ya kuhonga lakini anasema kuwa imeshindikana hivyo kila kitu kimetaifishwa.


“Hakuna namna hapa, yaani mtu ukienda kufuatilia utaonekana kama wewe ndiyo umemtuma.” Alikua anaongea kana kwamba ni kitu kirahsi, ukipiga mahesabu ya pesa za mwanzo na alizokua anachukua mara moja moja basi unakuta zishafika zaidi ya milioni 180. Yeye alikua anaongea kama vile hakuna kitu, nililia, nikakasirika, nikatamani kwend apolisi lakini hakuna hata sehemu moja ambayo tuliandikishaiana, pesa zote nilimpa kama mpenzi na hakuna hata sehemua mabayo tulisainishana.


“Ngoja nikuache utulie kwanza, anjua uliweka nyumba yako rehani, ngoja niongee an washikaji tuone namna ya kukusaidia.” Aliniambia nakuondoka,a liniacha nikiwa nimechanganyikiwa, nilirudi nyumbani kama chizi, sioni njia, wakati huo mimi na mume wangu tulishaanza kuwa vizuri, nilitamani kumuambia kuwa nilichukua mkopo na kufungua duka lakini ningeanzia wapi, nyumba ile ilikua ndiyo nyumba yetui ya kwanza.


Kwanz akiwanja kilikua sehemu nzuri sana, mume wangu alikinunua na kuandika jina langu kwakua wakati ananunua tulikua naviwanja viwili, yeye akalipia kimoja akaandika jina lake na mimi nikalipia kile nikaandika jina langu. Wakati wa kujenga tuliamua kujenga kile kwianja kwakua kuwanj ahcake kilikua sehemu mbaya ila pia kilikua na mgogoro, tulikua tunapoendana sana kiasi kwamba mume wangu hakujali chochote.


Ilikua ni nyumba kubwa, imejengwa wkenye kiwanja kikubwa na ina kama ka ghorofa flani, nilijihisi kuchanganyikiwa, nilimuambia mume wangu naumwa na tumbo hivyo siwezi hata kuongea, kwakua tulikua vizuri aliniamini. Duka lilishakufa kulikua hakuna kitu, nilichanganyikiwa kabisa nikawa mtu wa mawazo sijui hata nifanye nin? Siku moja nipo nyumbani sina hili wala lile simu ya mume wangu iliitaalikua anaongea na mtu mara nikasikia.


“Mkopo gani huo, mbona mimi sikuelewi, mimi sina duka wala sina cha mkopo.!” Alikata simu kwa hasira kisha kunigeukia kwa wasiwasi.


SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA TANO!


“Nilipojua kuwa unachepuka nilipaniki sana, kwa kifupi nilichanganyikiwa, niliangalia wanawake wengine namana wanavyoachwa nikaona kuwa namimi ipo siku utaniacha. Nikiangalia wanangu namna walivyozoea maisha mazuri nikasema hapana, lazima nifanye kitu, niliamua kufungua Biashara kimya kimya bila kukuambia. Kuna rafiki yangu mmoja alinipa dili la Pikipiki, kutoka china, akanipa mchongo nikaona kuwa ni kitu ambacho natakiwa kufanya.”


“Rafiki yako au Bwana wako?” Mume wangu aliniuliza, alikua kakasirika sana, nilijau kuwa atanipiga na kuniua lakini hakufanya hivyo.


“Hapana, si wmanaume wangu, mume wangu wewe unanijua, nina kisirani na wakati mwingine nafanya mambo ya kijinga ila tangu zamani nakupenda wewe, ninachanganyikiwa sana inapokuja kuhusu wewe, unakumbuka zamani kipindi hatujaoana, nilikua nagombana na wanawake wengi kwa kuongea na wewe, nakupedna sijawahi kukusaliti na siwezi kukusaliti.”


Nilimuambia mume wangu, nilikua nalia sana, nilidanganya lakini sikua na namna. Baada ya mume wangu kupokea simu na kuambiwa kuhusu mkop alinigeukia na kuniuliza. Mume wangua likua kapigiwa simu na rafiki yake mmoja, yeye ni dalali wa kampuni moja ambayo inauzaga nyumba zilizochukuliwa mkipo na benki. Nyumba yetu watu walishaanza kuipigia mahesabu, baada ya kushindwa kupeleka marejesho mawili walishaanza kuitafutia wateja.


Alipoambiw akutafuta watu wa kimya kimya kabla ya kupigw amnada ndiyo alishangaa na kuamua kumuambia mume wangu. Mume wangu alionekana kukataa kuwa hakuna mkopo, alikataa hata mimi alikua aniuliza kama kiutani utani lakini hakutilia maanani. Nakumbuka ilipita siku mbili bila mume wangu kulikumbushia hilo swala, usiku mmoja ndiyo niliamua kumuambia ukweli, nilijua kabia kuwa nyumba itauzawa kwanis ikua na hata shilingi mia, pesa kwa wakati huo tulikua tunadaiwa kama milioni mia hamsini hivi, silikua ni pesa nyingi sana kwangu na hata kwa mume wangu.


Niliamua kumuambia mume wangu ukweli kuwa nilichukua mkopo kwaajii ya kufanya Biashara kwakua nilijua kuwa ataniacha na kwend akusihi na mwanamke mwingine hivyo nilitaka kujipanga na si kumdhulumu. Kwakua nilijua kuwa akichunguz aatagundua mtu niliyekua nikifanya naye kazi nilijifanya kuwa ule mchepuko wangu ni rafiki yangu na aliamua kunitapeli yeye na rafikii yake. Nilisema kila kitu isopokuwa kua na mahusiano na yule Kaka.


Mume wangu alinisikiliza kwa makini, niliona kabisa kakasirika lakini kama kawaid ayake ni mtu wa kutulia, anazizuia hasira zake sana.


“Unajua umenikwaza sana?” Aliniuliza, nilimuangalia usoni, tulikua tumekaa kitandani nilishuka chini na kupiga magoti kutaka kumuomba msamaha, alinishika na kuninyanyua.


“Acha kukufuru mume wangu, goti halipigwi kwangu.” Alinikalisha kitandani na kuniangalia usoni kwa kama nusu saa hivi bila kuongea kitu chochote. Baada ya hapo alinyanyuka na kutoka, hakurudi tena mpaka asubuhi na mimi sikulala mpaka asubuhi, alirudi akiwa amechangamka sana, nilijua atanifanyia kitu kibaya lakini haikua hivyo.


“Kwanini unanitesa hivyo lakini? Hivi unafikiri kuna kitu kinaweza kunifanya mimi kukuacha na kutelekeza watoto wangu?” Aliniulzia, nilijikuta nabaki tu kimya, sikua na jibu.


“Kwanini unajitesa hivyo unajua una wivu sana, yaani naona kama huna maisha, unaishi kwa kuteseka kuwaza kuwa nitakuacha, kwanini nikuache, ni mambo mangapi navumilia. Umejaribu kunitenganisha na familia yangu, umejaribu kunigombanisha na kila mtu, umenidhalilisha mara kibao nakuvumilia, lakini bado huniamini, hivi kweli nifanye nini wewe mwanamke ili ujuwa kuwa nakupenda na siwezi kukuacha?”


Aliniuliza, kusema kweli sikua na jibu, mume wangu nilishamfanyia vituko vingi, mara kibao nilishataka kuondoka na kumuacha kwa makosa kidogo tu, nilikua na kelele nyingi kiasi kwamba nyumba haina amanai, ilifikia kipindi mume wangu alikua anataoka kazini badlaa ya kuingia ndania naaka kwenye gari hata masaa manne ili tu akiingia nimechoka nimelala.


“Hata sijui, nimekufanyia mengi mume wangu lakini sijui hata ni kwanini bado unanipenda?” Nilikua sina jibu, kusema kweli nilsihakata tamaa, nilijua kwua mume wangu hawezi kunisamehe nishajiandaa kwa chochote.


“Umesema kuwa wamekutapeli? Una uhakika?” Alibadilisha mada, alikua tofauti kabisa, alichangamka kidogo, nilitaka kumuomba tena msamaha lakini alinikataza.


“Ndiyo mume wangu, ni watu ambao niliwaamini lakini wamechukua kila kitu.” Nilijitetea, mume wangu aliniangalia kwa uchungu, niliona hasira zake ni kama zinataka kupanda, nilimsogelea na kutaka kupiga magoti tena kumuomba msamaha lakini alinishika na kuninyanyua.


“Sitaki msamaha wako, sijui kwanini sikuamini lakini sitaki tena msamaha wako, sijui ulipozipeleka hiso pes alakini nazitaka, utalipa hilo dani la watu na nyumba itarudi.” Alininyanyua kwa hasira na kunisukumiza pembeni, alianza kutafuta aliingia kabatini na kuchukua nguo zangu, alizikusanya na kunipa.


“Kila iku nakudekeza, ukinikosea wewe naomba msamaha mimi, naondoka mimi lakini sasa hivi nimechoka, naona umeamua kunifanya ndondocha, sitaki tena upuuzi wako. Ninachotaka ni pesa zangu, ulipe hilo deni na hata ya nyumba niione hapa.” Alinitupia nguo zangu, niliomba msamaha sana lakini mume wangu hata hakunisikiliza. Nililia na kuigalagala chini ila hata hakujali, alinichukua na kunitoa nnje, akanitupia nguo zangu na kuniambia niondoke kwani hataki tena kuniona.


Nikiwa pale nnj endiyo nilijua kuwa mume wangu alikua yupo siriasi, ainmifungia na kurudi ndani. Kwa aibu nilichukuanvitu vyangu, nikachukua Bajaji mpaka kwa rafiki yangu. Nilimuambia kila kitu kuhusiana na mkopo na namna ambayo mume wangu alikua kanifukuza. Alinisikiliza sana kisha akaniambia.


“Huwezi kulala kwangu, ninachoweza mimi nikukupa pesa ukatafute sehemu ya kulala au urudi kwenu. Mume wangu amebadiolika sas ahivi anajali na kaniambia kuwa wewe ndiyi unaniharibu, tena ndiyo uondoke kabla ya kuniharibia ndoa yangu, ushavunja yako sitaki uvunje na yangu.”


Mwanzo nilijua kama ni utani, lakini shoga yangu alinifukuza kwake, kusema kweli shida yangu kwa wakati huo haikua pesa bali mtu wa kunifariji na kuongea naye. bado nilikua na pesa kidogo, niliend kupangisha chumba gest nikisubiri mume wangu kunipigia simu kutaka kurudiana na mimi, kwa nilivyokua namjua mume wangu nilijua kabisa hawezi kuishi bila mimi, nilijua kuwa hawezi kuniacha, ingawa nilikua na huzuni lakini nilijua ni jambo la muda tu atarudi.


Ulikua ni usku mrefu sana kwangu lakini ilikua ni lazima kulala, kesho yake ilikua ni siku ya kazi, ingawa usingizi ulikua ni wa shida lakini ilikua ni lazima niende kazini kwani kulikua na ukaguzi. Nilienda huku nikijifanya kuwa akuna kitu kilichotokea, nilisalimiana na kila mtu vizuri na wote ilikua kawaida kwani ni rafiki yangu mmoja tu ambaye alikua anajua kuhusu maisha yangu. Mambo yalikua mazuri mpaka ilipofika saa nne, nakumbuka nilikua nakunywa chai kantini, nilishangaa kila mtu ananifuata na kunipa pole.


“Pole ya nini?” niliuliza, walianza kunaimbia kuwa wanaume si watu wa kuamini, mara hivi, mara vile, yaani watu walikua wanaongea ongea mpaka nikaanza kuona aibu.


Niolimfuata rafiki yangu na kumuuliza kama amemuambia mtu kuhusu ishu yangu, mwanzo alikataa, baadaye akanimbia kuwa kuna mtu mmoja tu alimuambia, nilimlaumu sana kwa kuniaibisha na kunitangzaa.


“Mama, usinileteee, jilaumu kwa ujinga wako, nyie ndiyo washenzi mnachukua waume za watu, mnawachukulia mikopo! Mume wangu naye kuna mwba kwama wewe alifanya hivyo hivyo! Acha kuniletea umalaya wako hapa na kuniona sinich kwa kukutangaza wewe ni shetani tena unikome, sitaki hata unisogelee!


Usivyo na aibu unakuja kwangu kutaka eti nikupokee, unataka umchukua na mume wangu mbwa wewe, tena unikome sitaki na mazoea, kwa taarifa yako ukinitibua naenda kumwagia mume wako kila kitu ulichofanya na huyo Malaya wako, niondokee mshenzi mkubwa mbwa kabisa wewe! Nimeteseka sana kwenye ndoa yangu kwasababu ya washenzi akam wewe mnaojiona kuwa mnajua kila kitu!”


Alinitukana kwa sauti mpaka nikaishiwa posi, ni kama alikua na mambo yake moyoni alikua anashidnwa kuniambia. Niliumia sana kwani yeye ndiyo alikua ni rafiki yangu mkubwa, ndiyo mtu alikua akinishauri na mimi kumuambia kila kitu. Kinyonge kabisa nilirudi ofisini kwangu, kuna kazi nilikua na malizia kabla ya kuonana na wakaguzi, nisingeweza kuondoka na wala nisingeweza kufanya chochote, nilikaa mpaka jioni mume wangu hakunipigia simu wala kutuma meseji.


Nilirudi hotelini ambapo nilikaa kwa wiki nzima bila mume wangu kunitafuta, hata ndugu zangu alikua hajawaambia chochote kwani walikua wakinipigia simu tunaongea kawaida. Nilikua kwenye mawazo makubwa sana, nilikodnaa ndani ya wiki moja na kuwa kama mgonjwa wa muda mrefu. Kazini sikua na rafiki tena, kila mtu alinikimbia, hakuna mtu aliyeniamini, Benki napo walikua wakipiga simu mara kw amara wakitaka pesa.


Baada ya kama wiki moja hivi mume wangu alinipigia simu, aliniambia kuwa anataka kuonana na mimi, nilishukuru Mungu nikajua kuwa kashidnwa kuishi bila mimi hivyo anataka turudiane. Lakini nilikata tamaa tulipoonana mabapo alikua ananiulizia kuwa nimefikia wapi kuhusiana na kulipa deni. Sikua na jibu kwani sikua na kitu chochote, aliniambia nimpeleke wkenye duka ambalo nilifungua, nilimpeleka na kulikua hakuna kitu, pikipiki zilikua zimebaki kama 12 ambazo zilikua na thamani kama ya milioni 20 na kitu.


Aliangalia kwa masikitiko sana, niliumia kumuona katika hali ile.


“Nataka kuonana na hao jamaa, nataka kuonana na hao watu waliokutapeli.” Aliniambia, nilimuambia kuwa hawapokei simu zangu na wamenitishia kuwa hawawezi kunipa.


“Si unajua nyumbani kwao, au ulimpa mtu pes ayote hiyo hata hujui kwake?” Aliniuliza, sikua na jibu, nilibaki kimya, alinisisitiza kuwa anataka kuonana nao na kusisitiza zaidi kuwa anataka kwend anyumbani kwao. Kusema kweli nilitamani kumpeleka mume wangu lakini nilihofia, kwanza mke wa yule Kaka alikua akinifahamu, nahisi alishaona picha zangu ingawa nilikua sijawahi kuonana naye moja kwa moja.


Pili nilihofia kuwa labda wanaweza kupandishiana na mume wangu akasema kuwa nimewahi kutembea naye. Mume wangu alikua akiniamini sana kuhusiana na ishu ya mapenzi, alijua kuwa nampenda na mambo yote niliyokua nayafanya ilikua ni ujinga wa wivu, kwa namna alivyokua ananiamini alijua kuwa siwezi kumsaliti. Nilijua kuwa anaweza kunisamehe kitu kingine chochite kile lakini si usaliti. Lakini sikua na namna, ilikua ni lazima kumpeleka mume wangu kwa huyo Kaka.


Nilimkubalia, nikachukua simu yangu harahaharaka na kumtumia yule Kaka, nikamuambia kuwa mume wangu anakuja kwake, ameshajua kila kitu hivyo asijekusema kuwa alishawahi kutembea na mimi. Hakujibu meseji ingawa niliona kuwa imefika, tuliongozana na mume wangu mpaka kwa yule Kaka, kwa bahati nzuri mke wake alikua hayupo, alikua kasafiri kikazi. Mume wangu kwa kawaida ni mstaarabu, aliingia kistaarabu na yule Kaka alinisalimia kama ananijua.


Mume wangu alijitambulisha na kumuambia sababu ya sisi kwenda pale. Alipoambiwa alinmiruka kabisa, alisema ni kweli ananifahamu, ni kweli tulishawahi kuongea naye kuhusu kufanya biahsara lakini baada ya kluona Biashara yenyewe ni kubwa basi aliamua kuacha, hajawahi kuchukua pesa zangu wala kitu chochote kutoka kwangu.


“Mimi nimeoa Broo, nina maisha yangu, ni kweli mke wako namjua, tulikutana Baa, na aliniambia kuhusu Biashara, lakini mimi sikua na mtaji, mimi ni mtoto wa mjini tu, sina kazi ya maana.


Niipoteza kazi miaka mitano nyuma na tangu hapo nasimamia Biashara ndogo ndogo tu za mke wangu, mke wangu yeye anafanya kazi, anaanigiza mzigo china, mimi kwakua sina kazi naenda huko nachukua mzigo na kila kitu ni cha mke wangu. Sijawahi kufanya Biashara na mke wako kabisa, ningeanzia wapi, halafu hizo pesa unazotaja ni nyingi sana, hivi kwa maisha ninayoishi nipate milioni mia tu si ningekua mbali, wewe mwenyewe unaona, sasa hivi nipo nyumbani mke kasafiri sasa kweli niwe na milioni 100 nibaki hivi hivi.


Alichofanya mke wako ni hivi, mimi alinifuata na kutaka kufanya naye Biashara, alinaimbia kuna mchongo kapata china na kwakua mimi naenda huko bvasi nimpeleke na tufanye Biashara. Kuna watu ambao wanafanya biashara huko, akanitajia nikamuambia kabisa kuwa hiyo ni pesa nyingi kuwa makini na hao watu, usiwe unatoa toa pesa hivyo. Basi nikmsahauri kuhsu china lakini niliamua kukata mawasiliano na mke wako kwakua baada ya kuanza tu kuongea haya mambo basi mke wangu alihisi kuwa labda nachepuka.


Mkeo alikua anapiga simu mara kwa mara tena usiku, anatuma mseji, yalikua ni ammbo ya Biashara lakini kamka unavyojua ndoa zetu, mke wangu alikasirika sana mpaka ikafikia hatua nikakatisha mawasiliano na mke wako. Kama huamini basi angalia simu yangu, hizi meseji angalia nilimtumia lini, angalia nilivyokua namuambia.” Huyu Kaka alikua kajipanga, alikua anaongea kistaarabu,a likua anaongea kama malaika, alionyesha kana kwamba mimi ndiyo nilikua namsumbua.


Kama mnakumbuka kipindi kile baad aya kufumaniwa alitinumia meseji nyingi kunitukana, lakini mimi nilikua namtumia meseji nyingi kutaka kuoanna naye, kumuomba msamaha na mambo kama hayo. Nhuyu Kaka alikua ni tapeli kwania lifuta meseji zote zkuonyesha kuwa tulikua wapenzi, akabakiza meseji za mimi kuomba msamaha, mimi kutaka kuonana naye na kuacha meseji zake akinitukana na kuniambia kuwa nimuache kwani nitamharibia ndoa yake.


“Sijawahi kuwa na mahusiano na mke wako, lakini kuna vitu vilinichanganya kwani wakati anataka kuchukua mkopo aliniambia kuwa hajwahi kuolewa, aliniambia kuwa alikua anaishi na mwanaume wakaachana ndio maana hata nikakubali kuwa mdhamini wake, lakini si hivyo tu, alinionyesha hati ya nyumba ambayo ina majina yake, mimi nilichofanya ni kusaidini na kumsiadia kumuunganisha na watu wa Benki ili kuupata mkopo wake kwa urahisi. Lakini baadaye nilikuja kujua kuwa ameolewa, na kibaya ziadi akawa ananitumia msejei usiku na kunipgia simu.


Wewe upo kwenye ndoa, naamini mtu akimpigia simu mke wako usiku utajisikia vibaya na kudhani kuwa unasalitiwa, basi ndiyo kilitokea kwa mke wangu, baada tu ya kuona ananisumbua nikajua kuwa atanivunjia ndoa yangu nikampiga marufuku kabisa, sikutaka tena mawasiliano naye. Nahisi alitafuta watu wake wengine ambao walimsanganya ila mimi nilimuelewesha kila kitu kuhusu china na jinsi Biasharainavyokua na kumuambia awe makini.”


Aliongea hukua kimuonyesha mume wangu baadhi ya mesji ambazo alikua ananitumia kunielezea kuhusu Biashara ya Pikipiki huo china. Mimi sikua na chakuonyesha, nilikumbuka kuwa mara nyingi alikua ni mtu wa kuniambia nifute meseji zangu ili mume wangu aisje kuziona.


“Samahani kwa kukusumbua, nashukuru nimekuelewa, nilikua nimewaza kufanya mengine ila sasa hivi nimeshajua shetani ni nani?” Mume wangu alimuambia yule Kaka, alinyanyuka kwa hasira, bila hata kuniambia tunyanyuke wote aliondoka mpaka kwenye gari, nilimfuata na kutaka kupanda kwenye gari pamoja naye lakini alinikataza.


“Ukiingiza kichwa chako humu naenda kukugongesha kwenye nguzo kama ni kufa tufe wote!”  Mume wangu aliniambia ksiha akaingia kwenye gari na kuondoka.


SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA SITA


Mume wangu aliondoka, hakunitafuta tena na wala hakupokea simu zangu kabisa, kibaya zaidi hakumuambia mtu yoyote, kila kitu alifanya kimya kimya, nilaimua kutafuta chumba kwaajili ya kukaa kwa muda kwani gharama za hoteli zikukua kubwa. Baada ya kama wiki tatu hivi mume wangua linitafuta, alishaanza kulipa ule mkopo, kuna kiwanja kingine ambacho alikua ancho alikua ndiyo kaanza ujenzi, alikiuza na kupatakama milioni 22, alilipa yote, lakini mambo bado hayakua sawa, alinitafuta ili nimfungulie duka.


Kuna pesa nyingine ambayo aliipata kama milioni 12, sijui alikopa wapi lakini kuna rafiki yake alimsharu kuwa afungue duka langu, aanze kuuza vitu asimamie awe analipa mkopo kidogo kidogo. Kwelia lifanya hivyo, alifuingua na kila kitu tukabadilisha majina yakawa yake, akawa analisimamia yeye na kulipa mkopo yeye. Nilimuomba msamaha lakini hakutaka kusikia chochote, aliniambia nimuache kwani kichwa chake hakijatulia.


Mume wangu alipambana,m ndani ya miezi nene alifanikiwa kulipa ule mkopo, alimaliza deni, alirudishiwa hati yake, aliniita na kuniambia kuwa ile hati nibadilishe majina na niandike majina ya watoto wetu, sikua na namna nilibadilisha, lakini bado hakutaka kurudiana na mimi. Kwa mara ya kwanza nilienda kanisani, tuliitwa ili kusuluhishwa, mume wangu aliongea yake na mimi kuongea yake, wasiwasi wake ni kuwa nilikua nimemsaliti hivyo hawezi kukaa na mwanamke mzinifu,.


Niliapoa na kuapa kuwa sijawahi kumsaliti lakini hakunisikiliza, kanisani mambo yalishindikana, ikafikia hatua kuwa kila akiitwa anagoma kwenda. Katika kipindi nilipokua mbali na mume wangu dniyo niligundua kuwa nampenda sana mume wangu, niligundua kuwa siwezi kuishi vila yeye, maisha yalikua ni ya shida sana, sio kama sikua na pesa, hapana, nilikua napenda na nilikua na kila kitu lakini sikua na mapenzi, kila siku nilikua ni mtu wa mawazo, kulia na kusononeka.


Nilitamani sana kuwa karibu na mume wangu lakini ilishindikana, afya yangu ilizizi kuwa mbaya, nikawa ni mtu wa mawazo, kazini siendii tena bila taarifa, nilijikuta nakua mpeke wkani hata ndugu walikua kama wamenitanga hasa baadaya kusikia mambo niliyokua nimeyafanya. Mwaka mmoja baadaye mwanangu mdogo alianza kuumwa, ilitokea hgafla tu alikutwa na uvimbe shingoni na baada ya kwenda kupimwa aligundulika kuwa ana Kansa.


Kwasabbau ya mtoto nmume wangu aliniambia nirudi nyumbani, nilirudi nyumbani tukaanza kuhangaika katika kumtibu mtoto. Ile hali ilitududsiha karibu, nilijua kabisa mume wangu atakaua amenisamehe, maisha yaliendelea na yalikua mazuri, nilijikuta naanza kuwa na furaha tena, nilijikuta naona kama nimepata nafasi nyingine. Ingawa mume wangu hakuwahi kuniambia kuwa amenisamehe au kutaka kulala na mimi lakini nili0na kabisa kuwa upendo wake umerudi, niliona kuwa bado ananipenda na hasa namnaalivyokua ananisaidia kulea watoto wetu.


Kwa bahai mbaya baada ya miezi nane mtoto wetu alifariki dunia, ilikua ni huzuni kubwa sana kwangu, nilikua kama mtu aliyechanganyikiwa kwani alikua ni mtoto wangu pekee wa kiume, niliumia sana kila siku nikawa ni mtu wa kulialial mume wangu alikua karibu sana na mimi, alikua ananijali lakini hakuwahi hata siku moja kuongelea suala la mapenzi, kila wakati nilipotaka kugusia hayo mambo au kuonyesha dalili kuwa ninataka tukutane kimwili alinikwepa, mwanzo ilikua ni sababu ya mtoto anaumwa lakini baadaye alinikwepa tu na kunuiiambia kuwa hayuko sawa.


Nilikua naumia sana kwnai nilikua nampenda na kila siku nilikua naishi naye, kilichokua kinaniumiza zaidi nikuwa baada ya mazishi ya mtoto kumaliza 40 na kila kitu basi mume wangu alibadilika, hakua akininyanyasa lakini alihama chumba, alianza kubwa bize na kazi zake na mambo aliyokua anayafanya ni kama alitaka niondoke ila anaogopa kuniambia. Kwakua sikua na kazi yoyote nilikua mtu wa kukaa nyumbani, kila siku nina mawazo, nlikua mtu wa kujifungia ndani nalia mpaka basi.


Siku moja mume wangu alichelewa kurudi nyumbani, mpaka saa tano usiku napiga simu haipokelewi. Nilihangaika ktuma meseji lakini hazijibiwi, nilijikuta nahangika chumbani, kuna kitu kikaniambia nikague vitu vyake, sijui nilikua natafuta nini lakini mara nilijikuta kwenye mabegi yake na vitu vyake vya kazini. Wakati naangalia nilikutana na Document flani, mume wangu alionekana kukutana na mwanasheria kutaka talaka.


Kuna makaratasi niliyaona ya mwanasheria kuhusu mambo ya talaka lakini niliona kwenye diary yake kuwa tangu mtoto anaanza kuumwa alishapanga kunaicha lakinia lisitisha baada ya mtoto kuumwa, ila baada ya mtoto kufariki basi alitaka kuendelea na mchakato wa talaka. Niliumia sana, nilijihisi kuchanganyikiwa, baada ya kuona vile mume wangu kaandika wkenye diary yake kuwa hawezi kuendelea kuishi na mimi, hahisi kama ananipenda tena nilijua kuwa kila kitu kimeisha.


Nilijikuta naingia kabatini, kuna dawa za marehemu mwanangu alikua akizitumia kwaajili yya kumpunguzia maumivu kwani wakati wa mwisho wmisho alikua katika maumivu makali sana, analia mpaka wakati mwingine tunalazimika kumchoma sindano za usingizi kwani hali ilikua mbaya. Nilichukua kila dawa niliyokutana nayo hapo nabugia na maji. Haikuchukua muda nilidonoka na kupoteza fahamu.


****


Baada ya mtoto wangu mdogo kufariki tuliona kuwa haitakua busra kumuach adada yake bweni, alikua bado mdogoi na alikua akisoma na Kaka yake, walizoeana, kwanza tulimhamisha shule kwakua kule alikua na marafiki wengi ambao wangeweza kumuulizia kuhusu Kaka yake, lakini pili alikau akikaa kutwa. Nadhani pia hicho ndiyo kitu kilichokua kinamzuia mume wangu kuchelewa kuniacha, mara nyingi mume wangu alikua akiwahi kurudi kwaajili ya mtoto na ingawa alikua anajua kuwa mimi na Baba yeke tumetengana lakini hatukutaka kumchanganya.


Hata mume wangu aliponihama chumba hakufanya waziwazi, bado mtoto alijua kuwa tuko pamoja, nilijitahidi sana kuficha huzuni yangu kwani kila akiniona nipo kimya alikaua nadhani kuwa naumia kwasababu ya mdogo wake.


“Mama kwani mimi sitoshi au kwakua mimi ni mtoto wakike ndiyo maana huna furaha na mimi?” Nakumuka siku moja aliniuliza, nilikua nimekaa seuleni naangalia TV nakumbuka ilikua ni usiku, alinaimbia nimsaidie kufanya homework na nilimuambia nitaenda kumsaiodia, lakini kutokana na mawazo nilijikuta nasahau, wakati huo mume wangu alikua bado hjajarudi na akili yangu ilikua inawaza kuwa yupo na mwanamke mwingine anachepuka.


Wakati nimekaa nilijikuta nawaza mpaka machozi yanatoka mwenyewe, sikujua kama mwanangu alikua pembeni akiniangalia, kwa zaidi ya nusu saa alikua ananiangalia na yeye akaanza kulia ndiyo nilishatuka.


“K3wanini unasema hivyo mwanangu?” Niimuuliza huku nikimuita, alikuja nikaw anampakata.


“Kwasababu tangu Kaka afariki basi naona hakuna anayejali, wewe kila siku unalia na Baba kila siku anachelewa, mimi naona ni bora niende shule tu maana huku kama hamnitaki?” Manani yake yaliniumiza sana kwani yalionekana kuwa na ukweli, tangu mwanangu mdogo kufariki mapenzi ndnai ya nyumba yalipungua.


Mume wangu alikua bize na mambo ayake, kila wakati ni yeye na kazi bila kukumbuka kuwa ana mtoto mwingine huku mimi nikiwa mtu wakulia tu na huzuni kila saa.


“Hapana usiseme hivyo mwanangu, mimi na Baba yako tunakupenda tena sana, ni maisha tu ya kazi, tunakupenda.” Nilimuambia, alikubali lakini kishingo upande. Nakumbuka siku ambayo nagundua kuwa Baba yeke anataka kuniacha nilikua nahuzuni sana, alinifuata kutaka kuongea na mimi lakini nilimuambia kuwa ninaumwa hivyo asinisumbue, ndiyo niliingia chumbani na kuanza kupekua vitu na kujua kuwa mume wangu ana mwanamke mwingine.


Kumbe mwanangu naye hakulala, baada ya kumuambia kuwa asinisumbue alikaa sebuleni kuangalia TV, alikaa mpaka kwenye sa anane hivi za usiku, usingizi ulimpitia hivyo wakati Baba yake anarudi anagonga alishtuka, Binti wa kazi ndiyo alienda kumfungulia Baba yake mlango, alipofika sebuleni alimkuta ndiyo anaamka. Baba yake alishangaa kumuona palemkwani haikua kawaida yake, ilikua ni siku ya shule lakini alikua bado hajalala. Baba yake alimuambia kuwa aende akalale lakini kabla ya kwenda alimuambia.


“Baba mimi nataka mnirudishe bweni sitaki tena kuendelea kukaa hapa.” Alimuambia Baba yake, Baba yake alishangaa, alirudi na kukaa huku akimuuliza kuwa kwanini alikua hataki kukaa pale nyumbani.


“Nyie hamnipendi, mlishaachana na sisi tulikua tumekubali, hata Dan (sio jina  lake halisi) alishakubali kuwa mmeachana lakini baada ya dn kuanza kuumwa nyie mlirudiana kwaajili yake, nikajua mmerudiana tukawa na furaha lakini sasa hivi dan kafa hamtaki tena kuonge. Nyie hamtutaki ndiyo maana tangu zamani mnatupeleka bweni tu bila kutuuliza kama tunapenda au la, mnakaa wenyewe, sasa hivi wewe ni kukaa tu huko kazini na Mama kila siku ni mtu wa kulia tu anamlilia Dani ambaye amekufa wakati mimi nipo.


Mimi hapa kila siku nakua kama niko mwenyewe, sina familia, familia yangu alikua ni Kaka yangu Dan, amekufa namimi nikikaa hapa nitakufa, nirudishe shule yangu ya zamani nikakae bweni kwani kule nina marafikia mbao wananipenda kweli.” Aliongea huku akilia, maneno yake yalimchoma sana mume wangu, ni kama alizinduka nakujua kuwa alikua anaishi maisha yake mpaka kusahau kuwa alikua na watoto.


Mume wangu alimbembeleza mtoto na kumuahidi kubadilika, lakini Rahel (sio jina lake kamili) hakumsikiliza, alimuambia kwua yeye ameshakua mkubwa na anajua kuwa hataiwi hivyo hataki kuishi pale hyumbani. Mume wangu alimuambia akalale na atabadilika,a likuja chumbani ili kuongea na mimi lakini dniyo alinikuta nimelala nimepoteza fahamu. Aliangalia kitandani na kuona diary yake pamoja na vidonge, alitoka na kuita watu, walininyanyua na kunipeleka hospitalinia mbapo nililazwa na kuja kuzinduka asubuhi yake.


Pembeni yangu kulikua na askari kwani nilitaka kujiua. Baada ya kuzinduka mume wangu alikuja, hakuongea chochote lakini alionekna kukasirika ingawa alikua analazimika kucheka, nilikaa hospitalini kwa siku tatu, hali yangu ilikua nzuri na niliruhusiwa, mume wangu alishafanya michakato na kumaliza ishu ya Polisi hivyo nilirudi nyumbani. Niliporudi ndiyo alinielezea maongezi yake na Rachel na kuniambia kuwa hataki tena mambo ya talaka, hataki tena mambo ya kdanganyana na kjama nipo tayari basi turudiane na kama inawezekana basi tutafute mtoto mwingine.


Kwangu ilikua ni kama sherehe, sikutaka hata kuwaza mara mbili kuhusiana na hicho kitu, nilitaka kumuomba msamaha lakini alikataa na kuniambia ni wakati sasa tusamehe na kuachana na hayo mambo, aliniambia kuwa tutengeneze familia isiyo na visasi kwani mambo tunayoyafanya yanaweza kumathiri hata na mtoto. Nilikubaliana naye na kweli niliamua kubadiika na kusahau kila kitu kwani kwangu ilikua ni kama kupewa nafasi ya kuzaliwa upya sikutaka kuharibu tena, niliapa kubadilika na kuacha kumchunga mume wangu pamoja na kuendelea kumfanyia vituko.


***


 Maisha yalibadilika, kila kitu kilikua sawa, ile Biashara mume wangu alikua ahaisimamia mpaka ikawa kubwa, kwakua sikua na kazi ni Mama wa nyumbani na suala la ajira lilikua ngumu mume wangu aliniambia niende dukani niwe nasimamia. Nilienda kweli na kila kitu kilikua sawa, mume wangu aliniacha dukani lakini alikua haniamini tena, alikua ni mtu wa wasiwasi na kila wakati alikua anakuja kunikagua, kwakifupi nilikua ni kama mfanyakazi.


Ingawa alikua ananihudumia kwa kila kitu lakini kila pesa iliyokua inaingia ilikua jinagawanya mara tatu, kuna ambayo ilibaki dukani kuendeleza duka, nyingine aliweka kwenye akaunti ya mtoto na nyingine alibaki nayo yeye, mimi alikua akinipa kila kitu ila hakuniruhusu nisimamie pesa. Nilikubalianan na hiyo hali kwani nilijua kuwa itakua ngumu kwake kuniamini tena, niliendelea kujishusha ingawa hakuwahi kunizungumzia kuhusu mambo yaliyopita, mume wangu ni ile aina ya wanaume ambao akikusamehe anasahau.


Mungu alijaalia nilipata ujauzito, hapo mapenzi yaliongezeka, mipango ilikua nikajifungulie nyumbani kwetu lakini wakati nakaribia kujifungua dada yangu alipata ajli hivyo nilikosa mtu wa kunihudumia, nakwakua hjali yangu ilikua ni mbaya kwani mimba zangu zinasumbuasumbua ilimlazimu mume wangu kumuita Dada yake kuja kunihudumia, si yule ambaye alinifumania, hapana mwingine ambaye alikua si daa wa tumbo moja bali ni mtoto wa Mama yake mdogo.


Yeye alikua amemaliza chuo ila alikua hana kazi, mwanzo mambo yalikua mazuri, alikua ananihudumia vizuri, alinikanda na kujitahidi kuhakikisha kuwa niko sawa. Lakini mambo yalibadilika baada ya kama miezi miwili, nimeshamaliza uzani, nilianza kuona anakua karibu sana na  mume wangu, kwakua alikua hana kazi basi aliendelea kubaki pale wakati mume wangu akimtafutia kazi.


Nilianza kupata wasiwasi kwani muda mwingi walikua wanatumia pamoja, mume wangu al8impenda sana kwani alikua na akili na mara nyingi alikua anampa mawazo makubwa makubwa, kuna ushauri alimpa mume wangu wa kufungua kampuni ya kutoa mizigo bandarini, wazo lilikuja kuwa mume wangu anafanya Biashara, anatumia makampuni mengine kutoa mizigo kwanini asifungue kampuni yake na kuanza kufanya kazi hivyo kuchukua tenda hata za rafiki zake.


Mume wangu alikubali lile wazo, lakini shida ilikua kwenye kuandika wakurugenzi, mimi aliniweka akanipa hasilimia 20, yeye 20, watoto watu wawili akawapa kumi kumi na yule dada yake akampa asilimia 40. Niliumia sana kwani niliona kama kampa kiasi kikubwa wakati haajchangia chochote, mume wangu aliniambia kuwa yule ni mdogo wake na alichompa ni kiudogo kwani sisi kama familia tumechukua asilimia 60.


Pamoja na kuambiwa lakini nilikasirika, nilijihisi kama nimesalitiwa, mume wangu alimnunulia gari nayeye anidyo akaw amkurugenzi wa kampuni kwani mimi nilibaki dukani na mume wangu alikua na kazi yake. Alihama pale nyumbani baad aya kuona kuwa tunagombana lakini muda mwingi alikua anakuja na wanatumia muda mwingi kwenye ofisi ndogo ya mume wangu, nilijiona kama vile wananizunguka, kuna wivu niliupata mpaka kuna wakati nilihisi kuwa anatembea na mume wangu.


Nilianza kumfuatilai mume wanngu, kila sikua kairudi kazini nashiak simu yake, nikiona meseji albda wanachat hata kama ni kusalimiana basi naanza kukasirika, namuuliza kwanini mdua wmingi anachat na dada yake wakati mimi hachat na mimi. Ukiangalai chart zao hazikua za mapenzi lakini kulikua na utani mwingi, walikua kama marafiki wanaambiana vitu, hata vitu vikitopkea kwenye mitandao wifi yangu anamtumia mume wangu na mume wangu naye anamtumia.


Nilikua naumia sana tunagombana na mume wangu, ilifikia hatua akawa nafutya kila kitu, hapo pia tukawa tunagombana, nilihisi kuwa lazima kuna kitu ndiyo maana anfuta ili kuficha, mume wangua lipoona imekua shida basi alibadilsiha password kwenye simuyake, hapo ndiyo nilijikuta nakosa amani kabisa, niliamini kuwa lazima wanachepuka, nilainza kufuatilia kila mahali lakini sikuona chochote. Kutokana na kule kusumbuana wifi yangu alianza kundiaharau, mwanzo alikua ni mtu wa kunsalimia, ananipigai simu tunaongea lakini baadaye aliacha na hata kuja nyumbani ikawa mara moja moja.


Uvumilivu ulinishinda, niliamua kumfuata ofisini kwake na kumuambia kuwa natakaa aachane na mume wangu kwani ndoa yetu haina amanmi. Kwanza alinishangaa, lakini aliniambia maneno ambayo yalinichoma na kuniaminisha kuwa anatembea na mume wako.


“Yule ni Kaka yangu nmheshimu hivyo huo ujinga wako sitaki kuusikia, lakini hata kama ningekua natembea naye inakuhusu nini? Pambana na hali yako usiniletee shombo lako hapa, nimekuvumilia muda mrefu lakini naona unadhani mimi ni kama hao, kwakua Broo umempanda kichwani unafikiri kila mtu utamfanay hivyo hivyo, mambo yako kila mtu anajua hivyo acha kujifanya malaika. Kaka anakuheshimu lakini badala ya kukaautulie na ndoa yako basi kila siku ni kuhangaika kukizungusha! Tuliza makalio chini!”


Nilijisikia vibaya sana kutukanwa na yule binti kwangu alikua ni kama mtoto mdopgo, nilirudi nyumbani na kumuambia mume wangu, cha ajabu badala ya kuwa upande wangu basi alinigeukia.


“Nataka unisikilize wewe mwanamke, ulishanidhalilisha mara moja, ulishataka kuvunja ndoa ya dada yangu na kuharibu mahusiano ya familia yangu, ulisema shemeji yangu kakutongoza wakati hakuna kitu sasa hivi unasema kuwa natembea na mdogo wangu, acha kunidhalilisha, narudia acha kunidhalilisha, sijui una nini kila tukiwa na amani unataka tu kuharibu, chunga, sitaki kukuacha lakini kamwe sitaruhusu uharibu familia yangu!” Aliniambia.


Aliongea sana lakini sikumsikiliza, jinsi alivyokua anazidi kuongea niliona kama anamtetea ndugu yake, ndiyo alizidi kuniaminisha kuwa kweli anachepuka na mdogo wake. Nilijikuta sina amani nakua na kisiraniambacho siwezi kujizuia, kibaya zaidi nikuwa yule binti alianza tabia ya kumpost Kaka yake, kila wakitoka labda kwa chakula basi alikua akipost na kuweka caption kuonyesha kuwa alikua anampenda Kaka yake na kumshukuru, hali hiyo iliniumiza sana, nilimuambia mume wangu lakini hakujali, aliniambia niache kufuatilia mambo ya kijinga.


Hali ile ilinipa upweke, kila siku nilikua nagombana na mume wangu, akawa ni mtu wa kuchelewa kurudi nyumbani, akawa anakua bize sana na simu. Baada ya kuona vile niliona kama vile naachwa, ilikua nidfanye kitu, nilianza kumfuatilia yule Binti na kugundua kuwa alikua na mwanaume mwingine ambaye ni mpenzi wake wa muda mrefu tangu akiwa chuo, nilimtafuta yule Kaka na kumuambia kila kitu, nilimuambia kuwa mpenzi wake anatembea na mume wangu ambaye ni Kaka yake.


Nilimuonyesha baadhi ya meseji ambazo wifi yangua linijibu akinitukana kila nilipokua namshutumu kuwa anatembea na Kaka yake, katika meseji hakukataa zaidi alikua ananijibu ongea na mume wako acha kunisumbua mimi. Yule Kaka alionekana kuumia sana, aliniambia kuwa wapo kwenye mahusiano kwa zaidi ya miaka 6 na walikua na mipango mengi, ikiwa ni pamoja nakwenda kujitambulisha lakinihaoni kama anaweza kumuoa.


“Hapana, usimuache, nianchotaka ni wewe kuhakikisha kuwa unamshawishi ili aachane na mume wangu, yule ni Kaka yake na sitaki avunje ndoa yangu.” Nilimsihi sana yule kijana kuongea na mpenzi wake, alionekana kunielewa tukaagana. Jioni nilikua na amani kidogo, mume wangu alichelewa kidogo, aliporudi nilianza kwa kumuuliza kama alikua kwa w3ifi yangu, aliniangalia kwa hasira bila kunijibu, aliingia chumbani na mimi kimfuata.


Ila nakaribia tu kuingia mlangoni, mume wangu aliushikilia mlango, akaufunga kwa nguvu ukanipiga kichwani, nilidondoka mpaka chini, hakuishia hapo, alinifuiata na kuanza kunipiga, alinipiga sana huku akinitukana.


“Wewe mwanamke ni mshenzi sana, yaani umeniharibia maisha yangu, nimeishi wka madani, naishi kwa shida kwasbabau yako na sas ahivi unaharibu maisha ya ndugu zangu! Nitakuua hapa ili uniondokee kwani naona kama unataka kuniua kwa presha.” Aliongea huku akiwa kanishikilia chini ananikaba.


SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA   SABA!


Mume wangu alinipiga sana kisha akaondoka, hakurudi tena nyumbani kwa siku mbili, alirudi akiwa yuko kawaida kabisa, hakuonekana kukasirika, ilikua kama hakuna kitu kilichotokea, mimi niliumia niliona kama kaniddharau, nilimuambia kuwa nimechoka nataka kuondoka kurudi kwetu. Aliniangalia kwa dharau na kuniambia.


“Unataka nikupe talaka moja kwa moja au unaharaka talaka itakufuata kwenu?” Nilimuangalia mume wangu bila kummaliza, sikutegemea anaweza kuniambia hivyo.


Sikua na namna zaidi ya kunyamaza, mume wangu tangu hapo alibadilika sana, alikua ni mtu wa kuchelewa kurudi nyumbani, nikiongea kidogo basi atanipiga, wakati huo nilikua na mtoto mdogo lakini alikua hajali kabis. Mara nyingi akirudi nyumbani anacheza na mtoto wake kwani mtoto mkubwa alikua shuleni, alikua anafanya mambo yake kimya kimya hanishirikishi, pale dukani duka ambalo alinikabidhi mimi alileta kijana,  ingawa mimi nilikua kama bosi lakini yule kijana alikua akifanya karibu kila kitu na mimi kuwa kama mtazamaji.


Maisha yaliendelea hivyo hivyo, kila siku tunagombana na nikiongea sana nakua naishia kupigwa,  ilifikia hatua ikawa kama ni jambo la kawaida kwa mimi kupigwa, nikilalamika sana ananiambia kuwa kama nimechoka basi nimuache niondoke kwni nitakua nimempunguzia matatizo. Hali iliendelea hivyo mimi nikivumilia, kila siku nilikua nikiamini kuwa hizo ni hasira na ipo siku mume wangu atabadilika, atanipenda kama mwanzo.


Siku moja nilikua dukani, kuna dada mmoja alikuja na gari, hakushuka lakinia liposimama tu mfanyakazi wangu wa dukani alimfuata, yule dada alifungua kioo cha gari na mfanyakazi wangu alimpa pesa kisha akaondoka. Baada ya kuondoka nilimbana mfanyakazi kuniambia yule ni nani na ni kwanini alimpa pesa, mwanzo alikataa lakini baadaye aliniambia kuwa ni Mama mdogho.


“Mama mdogo, kipipi? Ni ndugu yako?” Nilimuuiliza, alitabasamu na kisha kuongea kwa dharau.


“Ni Mama mdogo mke wa Baba, inamaana hujui wakati ameshampeleka mpaka kwao na  wazazi wake wanataka amuoe yeye.” Alianza kuniambia, kusema kweli nilishangaa lakini yule kijana aliniambia tena kama ananikooa kwakua alikua ananichukia sana, mume wangu alikua na mwanamke mwingine, amempa moja ya nyumba yetu, ameshampeleka kwao na amemtambulisha huyo dada ana mimba yake anataka kumuoa.


Nilishangaa kwani tulikua na ndoa ya kanisani na mume wangu inakuaje anapeleka mwanamke mwingine nyumbani kwao. Nilipaniki, nilitaka kuongea na mume wangu lakini asingenisikiliza, nilimpigia simu Mama yake na kumuambia kila kitu huku nikimuuliza ni kwanini anataka kuoa mwanamke mwingine wakati mimi bado nina ndoa naye tena ya kanisani.


“Inamaana bado hajakuacha, wewe utakua umemloga mwanangu, haiwezekani kila siku tunamuambia aachane na wewe lakini hataki, kweli hawezi kuoa wanawake wawili hivyo ni lazima akuache, asije kutuaibisha.”


Mama mkwe wangu aliniambia, kwa muda mrefu nikigombana na mume wangu mimi ndiyo nilikua mtu wa kusema, ktu kidogo tu nilikua nampigia Mama yake na ndugu zake kuwaambia, ingawa walikua hawaniamini lakini anagalau walikua wananisikiliza na hata kumuita mume wangu kuongea naye, Mama yake ni mtu wa dini na hana majibu ya namna hiyo.


Nilijikuta nakata simu bila kuongea kitu kingine, niliona aibu na kujua kuwa kumbe kila mtu ameshanichoka. Mume wangu aliporudi aliongea kama kawaida, nilitaka kumuuliza lakini nilihofia sana, nilijua kuwa anaweza kuishia kunipiga na kama Mama yake anamuambia aniache basi nikipiga kelele anaweza kuniacha mazima.


“Tatizo ni yule mwanamke, nilazima nifanye kitu?” Niliwaza, hasira zilinipanda nikijua kuwa kumbe kuna mwanamke mwingine ananiharibia ndoa yangu, sikuona tena makosayangu nilijua kabisa kuwa huyo mwanamke ndiyo ambaye anataka kuniharibia ndoa yangu lakini mume wangua takua ananipenda.


Kesho yake kama kawaida nilienda dukani, niliamua kuwa karibu na yule kijana kwani alionekana anajua kila kitu na mume wangu alikua anamuamini. Nlichukua laki tano katika droo na kumpa.


“Ni zanin?” Aliniulzia kwa mshangao kwani haikua kawaida yangu kumpa hata shilingi kumi.


“Si nakupa, kwani kuna ubaya gani au hutaki pesa, kama hutaki nipe pesa zangu.” Nilimuambia nikitaka kumnyang’anya lakini alizing’ang’ania, akazichukua na kubaki nazo.


“Nataka uniambie kila kitu kuhusu huyo Malaya, najua mume wangu anaamini sana na anakupa wewe pesa hivyo ninachotaka namimi nakua nakupa na nataka kujua kila kitu.” Kwanza lisia kidogo, lakini aliniangalia na kuniuliza.


“Kweli unataka kujua?”


“Ndiyo nataka kuijua, huyo mwanamke anakaribia kunivunjia ndoa yangu unafikiri nitamuacha.”  Nilimuambia huku nikionyesha macho ya msisitizo, aliniangalia kwa huruma kama vile anataka kuniambia kitu lakini anasita, nilimsihi aniambie ndipo aliniambia mambo ambayo yalizidi kuniumiza.


Yule mwanamke alikua na ujauzito wa mume wangu, mume wangu alikua anatumia muda mwingi kule na kuna mara nyingi tu mume wangu humchukua mtoto wetu na kwenda kule, lakini pia wanaenda shulke kumtembelea mtoto na hata mtoto wangu mdogo alishampeleka. Kusemakweli nilikasirika sana kuona kuwa mumewangu pamoja na kunisaliti lakini anatumia wanangu kuniumiza, nilijua ana hasira na mimi lakini kwanini awapeleke wanangu kwa huyo Malaya wake, kweli niliumia sana.


Lakini pia nyumba aliyokua anaishi yule dada ambayo nilijenga na mume wangu na kiwanja tulinunua wote alishabadilisha jina na kumpa yule dada, hapo nilikasirika zaidi, nilijua kabisa kuwa mume wangu anakaribia kuniacha na kama asiponiacha basi atachukua kila kitu. Baada ya kujua nilikaa kimya kwa wiki mbili, siku nyingine yule dada alikuja dukanai kabisa, alishuka kwenye gari na kuja dukani, alikuja kama vile anaingia duka la jirani lakini nadhani alikua kuniangalia.


Kweli kwa kumuangalia alikua ni mjamzito na mimba ilikua ni kubwa, nilimuangalia na kupata hasira, nilitamani kumvamia na kumpiga lakini niliona kuwa nitaharibu, mume wangu alikua kuwa nimefanya vurugu basi ingekua shida.  Bnilinyamza lakini nikipanga cha kufanya, nilishapata hasira, moto umeniwaka na nilishaamua kuwa hakuna namna ambavyo nitaruhusu huyo mwanamke kuniharibia ndoa yangu.


“Mume wangu ananipenda, yuko na huyu malaya kwakua anajua tu sijabadilika, akijua nimebadilika basi atanirudia.” Nilijiambia, wakati nawaza yule dada alikuja dukani kwangu, akasimama mbele yangu, hakua akinunua kitu alikuaakiangalia, kwa kumuangalia tu nilijua kuwa kaja kunichora, mimi nilimcgangamkia na kujifanya sijui chochote, alijiongeelsha sana alipoona simsemeshi basi aliondoka, hakurudi kwenye gari balia lizunguka mpaka kwenye duka la jirani.


Baada ya kama dakika kumi hivi alirudi na kumuulizia mume wangu, nilimjibu kistaarabu na kumuambia kuwa siku za kazi mume wangu haji pale labda amtafute wkenye namba yake.


“Kama huna namba yake nikupa umpigie?” Nilimuuliza kimitego, kusema kweli nilikua na hasira lakini nilijikaza, sikutaka kuonekana mkosaji, sikutaka kuharibu mambo nilikua sijajua kuwa nitafanya nini lakini kila nikimuangalia yule dada nilikua najiambia kuwa lazima nitafanya kitu kibaya, hawezi kuniharibia ndoa yake.


“Ninayo sema nilitaka kuona tu duka letu.” Aliniambia, nilimsikia alichokisema, nilijua kasema makusudi uka letu ili kuniumiza kichwa lakini niliamua kuwa mpole, sikutaka kuharibu mambo mapema.


Nilinyamaza kimya, sikusema chochote, niliacha mpaka akaondoka, mfanyakazi wangu wkaati wote huo alikua anatetemeka, alijua mambo yataharibika lakini wapi.


“Nilijua mtapigana?” Aliniuliza baada ya yule dada kuondoka.


“Mimi? Nipigane kwaajili ya kile kinyago? Hapana, sijafikia hatua hiyo, watu wa namna hii unawaacha tu wajiaminishe kuwa wataolewa. Amekuja amekuta mali kajua zimepatikanaje, labda kama mimi siajzaliwa, labda kama mimi sikuzichuma hizi mali, ndiyoa taolewa, ataishia kuandikwa tu majina lakini hatachukua chochote!”


Nilifoka kwa hasira, nilikua nimekasirika kiasi kwamba nilikua nang’aya meno kwa hasira.


“Utafanya nini?” Aliniuliza, nilimuangalia nikacheka kisha nikamuambia.


“Nitafanya nini nini? Mimi siwezi kufanya kitu, hiyo ni kazi ya Mungu kudili na mashetani, mimi kazi yangu ni kupiga goti tu lakini najua Mungu hataruhusu mtoto wa zinaa kuzaliwa. Kusema kweli mpaka wakati huo sikua najua kitu chochote, nilikua na hasira tu ila nilijua kuwa siwezi kuruhusu yule mwanamke kuzaa.


****


Pamoja na kwamba sikufanya chochote lakini mume wangu alirudi nyumbani akiwa na hasira sana, alilalamika kuwa nimemfanyia mke wake vurugu, yaani alimuita mke, alinipiga sana na kuniambia kama naona kuwa ni shida yeye kuoa mwanamke mwingine basi nimuache niondoke zangu. Kusema kweli sikua tayari kwa hilo, nilichofanya ni kuomba msamaha ingawa sikujua kosa langu, hapo ndipo nilifungulia malngo wa maateso.


Mume wangu alikua analala nnje na kamaa kirudi nyumbani ni kwaajili ya kubadilisha nguo na kuondoka, anaacha nguo chafu mimi nakua napata kazi ya kufua tu. Lakini hata pale anapokua nyumbani basi ni mtu wa hasira, kuongea tu na huyo mwanamke na nikiongea kidogo ananitukana, alibadilika sana kiasi kwmaba kuna wakati nilitamani kuondoka ila sikulifruhusu hilo, nilishachuma vitu vingi na mume wangu sikua tayari kuondoka.


Niliwaza nini cha kufanya nikakosa jibu, kuna siku nilikua tu dukani, nilikua peke yangu kijana aliondoka kwani mume wangu alimpigia simu, hakuniambia alikokua anaenda lakini nilijua kwa huyo mwanamke. Nilikua na mawazo sana juu ya nini cha kufanya, wazo lilinijia kuwa kama yule dada asipozaa basi mume wangu anaweza kumuacha, niliwaza kuwa mume wangu labda alichepuka bahati mbaya kwani ananipenda lakini alipopata mimba basi ndiyo mapenzi yakakolewa.


Niliwaza kuhusu kutoa ile mimba lakini sikua najua ni namna gani ninaweza kufanya hivyo. Wakati nikiwa nimekaa apapita dada mmoja, alikua amevaa nguo za nesi, hapohapo wazo lilinijia kuwa kama nikitaka kumtoa mimba basi nimtumie nesi, sehemua mabayo anaenda kiliniki ili ampe dawa za kuhariobu mimba na mimba itoke. Niliwaza ni namna gani nitatekeleza wazo langu lakini ilikua ngumu sana, kwana ilikua ngumu kwa mimi kumpata huyo nesi lakini pili ilikua ngumu kwa huyo nesi kukubali kwani ni kama angepoteza kazi yake.


Lakini nililipenda wazo langu kwani mimi nsiingehusika kwa chochote, nilianza kufuatilia sehemu ambayo anaenda kiliniki, kwa bahati nzuti ilikua ni ahanati tu ya kawaida si hospitali kubwa kama nilivyodhani, nilifuatilia mpaka nikajua nesi anayemhusumia, nikajua familia yake na nikajua mpaka anaposali. Nilianza kua rafiki naye, nikimlaalamikia kuhusu ndoa yangu na kumuomba ushauri, tuliongea mambo mengi, mpaka tukashibana ndani ya wiki mbili tu.


Sikutaka kupoteza muda nilimuambia nia yangu kuwa huyo mwanamke anataka kuniharibia ndoa yangu hivyo nataka amtoe mimba. Tofauti na nilivyodhani kuwa labda atakataa na kutaka hata kunishtaki aliniambia kama ni kuharibu mimba yake basi nimpe milioni 5. Kwangu hazikua pesa nyingi ila tulipunguziana mpaka milioni 3, aliniambia anataka keshi na hataki mambo ya kutumiana.


Nilikubali na kumpa pesa yake, aliniambia atampa vidonge lakini mimi sikuaka kujua, nilichotaka ni kuhakikisha mimba inaharibika bila kumdhuru huyo dada wala yeye kuonekana kuwa kahusika kwani mambo yakiharibika basi nitakamatwa mimi. Kweli tilikubaliana nikampa pesa yake akaondoka, sikutaka mawasiliano naye tena, akanmiambia kuwa mambo yakikamilika atanijulisha kanisani lakini hataki mambo ya simu.


Kweli haikupita siku mbili, nakumbuka ulikua ni usiku wa manane, mimi nimelala na mume wangu, simu ya mume wangu iliita, wakati huo huyo mwanamke alikua na ujauzito wa miezi saba, mume wangu alipigiwa simu na kunyanyuka harakaharaka. Alionekana kupaniki, niliamka na kumuuliza ni nini kimetokea.


“Mke wangu kalazwa hospitalini, mimba imetoka nayeye yupo mahututi!” Aliniambia, nilijaribu kumododosa lakini alikasirka na kunisukuma akaondoka.


Nilipaniki kwani sikujua kilichokua kinaendelea, ni kweli nilisikia mimba imetoka lakini sikutaka kumuua yule dada.


“Nimemaliza, umesikia mimba imetoka, nipo hospitalini hata yeye hali ni mbaya anaweza kufa wakati wowote.”  Mesji iliingia kwenza niliogopa kujibu, namba nilikua naijua ni ya yule dada, ingawa nilishaifuta lakini nilishika namba ya mwisho, niliamua kumpigia akapokea lakinia alikua anaongea kwa sauti ya chini.


“Tuma meseji, nipo na watu ila kazi yako imeshaisha.” Aliniambia.


Niliana kutuma mesjei nyingi kumuuliza hali ya mgonjwa, nikimuambia kuwa mimi nimemuambia amtoe mimba si kumuua, alikua anajijibu kuwa imekua bahati mbaya dozi aliyompa ilikua kubwa na mambo mengine mengine. Tulichat sana baada ya muda aliacha kujibu meseji zangu na nilipompigia simu alikua hapatikani. Nilikua kwneye wakati mgumu sana nikitamani hata kwenda hospitalini kujua, mume wangu alikua hapokei simu zangu.


Nilimpigia kijana wadukani aliniambia kuwa hajui chochote, naye alijaribu kumpigia mume wangu lakini alikua hapokei. Kusema kwli nilishindwa kulala, nilijisikia vibaya na kuanza kuwaza nimefanya nini, nilijuta kwanini nsingemuacha azae. Asubuhi mume wangua likuja, alikua kaongozana na Dada yake, aliingia ndani, alionekana kuchoka sana, alikaa kwenye kochi na kuanza kulia, alilia sana, nilihisi kuna kitu kibaya, nilitamani kumfuata kumuuliza lakini miguu haikutembea, nilijihisi vibaya kwani mume wangu alionekana kuumia sana.


FebS7tr4mfuataray o1s, g202r10d  · 


SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU— SEHEMU YA NANE!


Mume wangu hakuongea chochote, alikaa pale sebuleni na dada yake huku akilia kisha akaingia chumbani. Aliniambia kuwa kachoka sana anataka kulala.


“Kuna nini mbona uko hivyo, unarudi unalia namna hiyo?” Nilimuuliza kwani nilikua nimechanganyikiwa kwa uoga.


“Hakuna kitu mke wangu, ila jua tu kuwa nilikupenda sana, nilikupenda mpaka nikapitiliza lakinmi umeharibu maisha yangu.” Aliniambia kisha akapanda kitandani, hakuongeza neno jingine, hata nilipomsemesha tena hakuongea./


Nilirudi sebuleni ambapo nilimkuta dada yake kakaa, alionekana kuwa na mawazo mengi sana, nililazimika kumuuliza kuna tatizo gani kwani namuona Kaka hayuko sawa.


“Unajua kuna wanawake wana bahari sana, hivi kwanini na mimi nsiingepata mume kama Kaka yangu?” Alianza kuongea, nilibaki na mshangao kwani sikujua anaongelea nini, nilitamani kumuuliza ni kwanini anasema hivyo lakini kuna kitu kama kiliniambia, acha, acha usuulize, lakini aliendelea.


“Unajua pamoja na yote uliyomfanyia lakini bado hataki kukaucha, badoa nakupenda, yaani sijui umemloga au ni nini?” Wifi yangu aliongea, nilimuuliza ni kitu gani lakini aligoma kuongea, aliniambia kuwa kama ni kuniambia ataniambia mume wangu.


“Akuambie mwenyewe, mimi nimekuaj naye hapa kuhakikisha kuwa hafanyi kitu kibaya, lakini wewe mwanamke ni shetani, sijui ni namna gani mtu anaweza kulala kitanda kimoja na wewe na bado akapata usingizi!” Aliongea kwa hasira, mimi sikumuelewa lakinia ligoma kuongea nini kilikua kimetokea.


Bvado nilikua na wasiwasi, sijui nini kimetokea, sijui kama yule mwanamke amekufa au la? Nesi alikua hapatrikani hivyo ilikua ngumu kwangu kujua chochote. Nilika sebuleni kama sakika kumi hivi, mume wangu alitoka, alionekana kama mtua liyekua anatafuta usingizi na kuukosa, alikuja na kukaa karibu yangu. alikua kashikilia simu tatu mkononi, mbili zilikua zake nazifahamu na moja ilikua mpya siiijui, ilionekana  kama ya kike kutokana nakava lake. Alinipa ile simu mpya na kuniambia niiangalie.


***


Mume wangu alikua na hela, angeweza kuupeleka mchepuko wake katika hospitali yoyote ile, lakini mwanamke alikataa, si kwakau alikua anapenda huduma za pale hapana ni kwakua, dada yake, mtoto wa Mama yake mdogo ambaye pia alikua ni shoga yake alikua akifanya kazi pale. Wakati anaanzisha mahusiano na mume wangu baadhi ya ndugu zake walijua,w alianza kumshauri kuachana na mume wa mtu lakini kama unavyojua wanawake wakishapenda basi huchanganyikiwa.


Kwa maana hiyo baada ya kupata ujauzito yule dada alitaka iwe siri, alienda kupimwa na ndugu yake, akapata majibu palepale na alikua anaenda kiliniki kimya kimya mpaka mimba ilivyokua kubwa ndiyo wakawa wanafanya waziwadi, hata mume wangu alikua anaongozana naye na hata kumsubiri, hwakufanya siri tena. Nesi ambaye nilimtafuta kwajaili ya kumtoa mimba mchepuko wa mume wangu alikua ndiyo huyo huyo dada yake.


Kwa maana hiyo nilichezewa, baada ya kujua huyo mwanamke ahakumuambia mume wangu mpaka siku ile usiku, alimpigia simu na kujifanya kuwa mimba imetoka, ndiyo maana alliongea na mimi kidogo na kuanza kutuma meseji ili kutengeneza ushahidi. Mume wangu alipofika aliambiwa, usiku wakati anaenda hospitalini akijua kuwa mwanamke wake mimba imetoka alimpigia simu dada yake ambaye waliongozana wakijua wamepoteza mtoto kumbe ulikua mchezo.


Mume wangu baada ya kuambiwa na kuona uthibitishoa likasirika sana ndiyo maana aliongozana na dada yake kuja kuniona. Alinipa ile simu ambayo ilikua ni ya nesi, tayari alishafungua meseji zanguambazo nilikua nimemtumia, nilishindwa hata kuzisoma, nilijua kuwa nishaharibu, ingawa nilijua kuwa ndoa imesiha lakini angalau nilijisikia vizuri kuona kuwa sijaua mtu, nilipomuona mume wangu anakuja analia nilijua moja kwa moja kuwa jela inanisubiri.


Kama kawaida yake mume wangu hakuongea sana, aliniambia tu kuwa imefika mwisho hivyo anaondoka. Mwanzo nilijau ni utani, lakini baadaye kama mchana hivi lilikuja gari, alichukua kila kilichochake na kuondoka. Nilijaribu kuomba msamaha lakini aliniambia kuwa imetosha, anahitaji kuwa na furaha. Mume wangu alihamia kwa yule mwanamke, baada ya kama wiki mbili hivi alianzisha mchakato wa talaka ambapo mimi niligoma kuachana naye.


Tulienda kanisani kusuluhishwa lakini mume wangua likataa katakata, hata hakuongea maneno mengi alisema tu kuwa hataki kuendelea kuishi na mimi, lakini bado hatukupewa barua ili mume wangu kwenda mahakamani. Tuliruidi nyumbani na siku iliyofuata mume wangu alienda ustawi wa jamii, sijui alifanya nini lakini alipata barua ya kwenda mahakamani na mchakato wa talaka ulianza.


Ingawa vitu vingi vilikua na majina yake lakini katika kuachana mume wangu aligawana na mimi kila kitu nusu kwa nusu na vitu vingine akaandika majina ya watoto. Mpaka napewa talaka sikuamini kama mume wangu ameniacha, nilikuja kuamini baada ya kufunga ndoa ya serikali miezi miwili tu baada ya kunipa talaka. hapo ndipo nilijua kuwa ndoa yangu imeisha na sina mume tena.


Nilibaki na watoto lakini nilikuja kunyang’anywa kwakua nilianza kunywa pombe, nilikunywa pombe kutokana na mawazo ya kumpoteza mume, upwek wa kutendwa na ugumu wa maisha. Haikuishia hapo, nilijikuta naingia kwenye dawa za kulevia, aada ya kuona hivyo mume wangua liingilia kati, alinipeleka Sober house ambapo nimefanikiwa kutoka nina mwaka sasa naishi kwa uangalizi wa mume wangu na ndugu zangu.


Watotyo wangu wanakuja kuniona mara moja kwa wiki, sina tena maisha na kila nikikumbuka namna nilivyochezea nafasi nazidi kujichukia. Nimeamua kuandika kisa changu ili angalau na wengine wajifunze, kama mtu ukipendwa basi chukulia upendo kama heshima na sikuona kuwa yule anayekupenda ni zuzu na hawezi kukuacha. Hakuna mtu ambaye hawezi kukaucha, jifunze kuacha baadhi ya mambo yapite, natamani kipindi changu kungekua na Kaka Iddi kwani sidhani kama ningefanya ujinga huu wa kuamsha shetani wa mume wangu ambaye alikua amekufa kabisa.


MWISHO.

0 comments:

Post a Comment

BLOG