Search This Blog

Wednesday, June 22, 2022

BAKI NA NDOA YAKO MIMI NABAKI NA MAISHA YANGU

  


IMEANDIKWA NA IDDI MAKENGO



KWAHERI; BAKI NA NDOA YAKO MIMI NABAKI NA MAISHA YANGU---SEHEMU YA KWANZA

Mama alianza kupiga kelele kuwa tumbo linamuuma, alikua katika maumivu makali kiasi kwamba alishindwa hata kunyanyuka, alidondoka chini na kuanza kupiga kelele huku akijiviringisha viringisha chini akisema.

“Mpigie Baba simu! Mpigie Baba simu nakufaa! Nakufaaa! Nakukufaaa! Naku… nakuu… nakuu…” Aliongea mpaka sauti ya kukatika katika akawa kama amezimia, nilinyanyuka na kuanza kutafuta simu yangu ili kumpigia Baba. Lakini ilikua haina pesa hivyo nilijaribu kuchukua simu ya Mama lakini ilikua na Password hivyo nilishindwa kabisa kuifungua.

Kabla ya kuendelea bonyeza hapa kuingia kwenye Ukurasa wetu mpya @AziraniHow @aziranihow @aziranihow kuna mengi yanakuja huko.

Nilikua nimechanganyikiwa kwakweli kwani Mama alikua kalala chini, alikua kalala chali huku kashikilia tumbo, niliata wazo la kutoka kwenda kuita majirani kabla ya kutoka nnje nilimpiga jiocho Mama. Nilianza kuona vitu vyeusi vikitoka sehemu zake za siri, vilikua kama damu lakini nyeusi ambayo ilitoka kwa wingi. Mama alikua na ujauzito wa miezi tisa na wakati wowote alikua ni mtuwa kujifungua. Nililetwa pale ili kumhudumia na kuwa naye kwani Baba alikua ni mtu wa kusafirisafiri.

Mwanzo alitakiwa kwenda kijijini kujifungulia ukweni lakini kutokana na mimba yake kumsumbuasumbua basi waliamua abaki na Bibi kuja kumhudumia. Bibi alishakuja mjini wiki mbili kabla lakini mpaka wakati huo alikua kwa Shangazi mkubwa, kila alipokua akiambiwa aje alikua akipiga terehe, ingawa Baba ndiyo alimfuata kijijini kwaajili ya kumhudumia Mama lakini hakuja pale, alitaka kushukia kwa watoto wake wengine kabla ya kuja pale akidai muda wa kujifungua bado.

Nilipaniki zaidi baada ya kuona zile damu, nilitoka nnje kuwaita majirani lakini ile natoka tu nilikutana na Bibi. Sikua nikimfahamu kwa kumuona kwani tangu kufika pale alikua hajawahi kuja mjini lakini kwa kumuangalia namna alivyokua kafanana na watoto wake hasa Shangazi mkubwa ambaye ndiiyo alikua kwake na baadhi ya picha nilizokua nikiziona katika simu za Shangazi na Mama nilijua kuwa ni yeye. Nilimsalimia huku nikiwa nimepaniki, nilimshukuru kwakuja na kumuambia kilichotokea.

“Wewe umemfanya nini mwanangu, kama kuna kitu kibaya umekifanya basi jua kuwa wewe ndiy utalipa. Huyo mtoto kama akifa utamla nyama!” Bibi aliongea kwa hasira, ilikua ni mara yangu ya kwanza kumuona lakini nilimuogopa, nilijitetea kwa uoga kumuambia kuwa sijafanya kitu chochote lakini hakutaka kunisikiliza.
“Mshike huko!” Aliniambia huku akimpanua miguu, mwanzo nilidhani kuwa anataka kumshika Mama na kumnyanyua, lakini haikua hivyo, alikua akimpanua miguu, alimpanua na kumnyanyua juu gauni alilokua amevaa kisha akamvua nguo ya ndani.

Niliona aibu na kuangalia pembeni.
“Unaona aibu gani? Wewe si mwanamke kuna kitu gani kimya hukijui hapa!” Aliniambia hukua kiendelea kumvua nguo ya ndani, ilikua imeloa zile damu nyeusi.
“Kwani ndiyo Mama anataka kuzaa? Eti mtu akitaka kuzaa ndiyo inakua hivi?” nilimuuliza kwa uoga, hakunijibu, aliitoa ile nguo ya ndani ya Mama iliyokua imejaa damu, chakushangaza aliichukua na kuiweka katika mfuko mweusi wa plastiki, baada ya hapo alizoa baadhi yadamu kwa mikono yake na kuiweka katika mfuko uleule kisha vite akaweka katika pochi yake.

Nilishangaa lakini nilishindwa kuuliza.
“Kalete beseni la kukaushia maji, hivi una akili kweli wewe mtoto hujui hapa chini pamechafuka.” Aliniambia wka hasira, nilinyanyuka na kwenda kuleta beseni, harakaharaka alianza kudeki mule ndani kukausha zile damu, mimi niulishangaa kwani mwanzo nilijua labda Mama alikua anajifungua na ndiyo inavyokua lakini nilishangaa zaidi kwani badla aya kuhangaika kumsaidia kujifungua au hata kumpeleka hospitalini yeye alikua bize kupiga deki.

Nilitaka kuuliza lakini niliogopa, alikausha pale chini vizuri huku akimgeuzageuza Mama, alimvua nguo zote akaniambia nilete nguo nyingine akambadilisha, alimbalisha na kuwa viozuri kabisa, nikidhani labda ndiyo anataka kumpeleka hospitalini aliniambia nimsaidie kumpandisha Mama kwenye kochi.
“Hatumpeleki hospitalini?” Nilimuuliza, pamoja na uoga wote niliokua nao lakini nilijikaza na kuuliza.
“Hopspitali ya nini? Kwani umesikia kuwa anaumwa? Huyu mzima kabisa mimba ndiyo zinakua hivyo!”
“Lakini Bibi mbona alikua anatoa damu?” Niliuliza, sikuridhika na jibu lake.
“Una miaka mingapi?”
“16!”
“Ulishawahi kubeba mimba?”
“Hapana!”
“Ulishawahi kuzaa?”
“Hapana lakini….”
“Lakini nini? Mimi nimeshawaki kuzaa, hili tumbo limetoa watoto ha inane na maiti watatu, najua mimba zilivyo, huyu hana tatizo lolote, muache apumzike, kwanza toka nnje kafue hizo nguo, na usiongee chochote, ukinyanyua mdomo wako basi jua kuwa nitakukata ulimi!”

Bibi aliongea huku akininyanyua kwa kunifinya mabega, aliniamrisha kutoka nnje kwenda kufua nguo za Mama. Ingawa bdo nilikua na wasiwasi lakini sikua na namna, nilienda kufua huku nikiomba Mungu Mama apone kwani nilishaanza kumuogopa Bibi.
“Mbona umeniacha nimelala ndani wakati Mama kaja, kwanini hukunishtua?” Nilishtuliwa na sauti ya Mama, kama dakika kumi tu baada ya kutoka kufua Mama alizindika na kuja nnje, aliniona ndiyo nimemaliza kumwaga maji ya kwanza na kutoa damu zote nilikua naloweka nguo kwenye sabuni.

“Mama umepona? Unaendeleaje?” Nilimuuliza, lakini kabla hajajibu chochote Bibi alikuja, ni kama alikua hataki niongee kitu, alinikata jicho la onyo mwenyewe nikanywea.
“Ingia ndani mwanangu kwa hali yako hiyo hutakiwi kutembeatembea, mimi niko sawa, wifi yako atakuja na mizigo yangu jioni. Mjini rah asana, nimekaa kule nimejisahau kabisa kuwa nina mzazi….” Bibi alijiongelesha hukua kimshika Mama na kumuingiza ndani, hakutana niongee naye kabisa. Sikujua nini kilikua kinaendelea lakini nilihisi kuwa kuna kitu kibaya ambacho Bibi anataka kukifanya.

Pamoja na hisia zangu hizo lakini sikua na namna, nilibaki kimya tu kusubiria nini kitatokea. Jioni Baba alirejea na Mama ni kama alikua hakumbuki chochote, nakumbuka nikiwa nnje kama kawaida Mama alijitahidi kutoka kumpokea Baba, alimshika tumbo na kumuulizia mtoto anaendeleaje, alimuambia yuko vizuri, Baba aliinama kusikilizia mapigo ya moyo nya mtoto na kumtania kuwa kampiga teke. Mama alikua na furaha sana ni kama hakuna kitu kilichokua kimetokea mchana wake, Shangazi nao walikuja, wakasalimia kwa kuchangamka na kuleta nguo za Bibi.

Baada ya kama siku tatu hivi Mama alipata uchungu, walimpeleka hospitalini ambapo alikaa siku mbili akipigania kujifungua. Nilikua sielewi wala siambiwi chochote zaidi ya akina Shangazi na baba mdogo kuja kuchukua chakula, Bibi kutoka kwenda hospitali na kurudi nilikua najua kuwa Mama anaendelea vizuri. Jioni ya siku ya tatu niliambiwa kuwa Mama anarudi, sikuambiwa kitu kingine chochote zaidi ya kuwa anarudi. Nikitegemea kuwa kajifungua salama nilisubiri kuwa arudi na mtoto lakini waliingia ndani, Mama alikua analia muda wote, walimfanya kumbeba.

“Wifi ungekaa tu hospitalini….” Shangazi mdogo ambaye kipindi hicho alikua chuo aliongea.
“Kufanya nini? Kufanya nini? Wamemchukua mwanangu, wale watu ni washenzi, kule ndiyo wamaniulia mwanangu….” Alipiga kelele ambazo zilinishtua, sikuelewa nini kimetokea lakini nilihisi tu alijifungua mtoto akafa, sikuweza kuuliza. Babaa likua anatembea lakini kwa shida, Baba mdogo alimshikilia, alionekana kulia sana.
“Miaka kitatu mdogo wangu! miaka mitatu!” Alikua akiongea hukua kijifuta machozi.
“Jikaze sana Kaka, jikaze kwaajili ya shemeji, yote hiyo ni mipango ya Mungu.” Baba mdogo alimuambia, Waliingia ndani Baba akakaa sebuleni lakini Mama alielekea chumbani na kina Shangazi.

“Kajitingisha tena mshono unatoa damu, huna namba ya Daktari yoyote aje kumuangalia kwani hospitali kakataa katakata?” Shangazi mdogo Aziza (sio jina lake halisi) aliongea baada ya kutoka chumbani. Baba alichukua simu yake, akatafuta namba akaipiga kisha akampa Baba mdogo Karim (sio jina lake halisi) aongee naye. Aliongea na kumuomba kuja kumuona Mama, ni kama walikubaliana kwani kama nusu saa hivi rafiki yake na Baba ambaye nilikua nishamuona kabla alikuja na kumhudumia Mama. Alimpiga na sindano ya usingizi ilia pumzike kwani alikua kali asana na kachoka sana.

Baadaye ndipo nilikuja kujua kwamba kumbe Mama alijifungua lakini mtoto alifia tumbani, mbaya zaidi aloijifungua kwa oparesheni jana yake, hali yake ilikua mbaya lakini baada ya kunyanyuka na kuambiwa kuwa mtoto wake alikuia kafariki alikasirika, alianza kupiga kelele na kulazimisha kumtoa hospitalini hata kama alikua hajapona vizuri. Walimbembeleza sana lakini aligoma akiwalaumu manesi na madaktari kwa kumuulia mtoto wake. Nyumba ilikua na huzini, kila mtu alikua akisikitika kivyake.

Nilijikuta nalia bila kujijua, ingawa sikua na muda sana katika ile nyumba nilishatokea kumpenda Mama, alikua mkaribu, anajua kujali na alinipenda kama mwanae. Pia nilimuonea huruma kwani ndoa yake ilikua na miaka mitatu na katika kipindi hicho alikua hajawahi kupata ujauzito hivyo alikua na hamu sana na mtoto. Nikimuangalia Baba alivyokua anahangaika,a lishanunua na vinguo vya mtoto, alikua akimpenda mke wake akimdekeza na jina la mtoto tayari walishalipata, niliumia sana kwakweli.

Nilikua nishamaliza kufanya kazi zangu za ndani, mpaka chakula cha usiku nilishapika, kutokana na hali ya ukimya ya mule ndani niliboreka kwani hakuna mtu aliyekua anaongea na Mimi. Niliamua kutoka nnje, sijui ni kwasababu gani lakini nilitoka na kuanza kuzunguka nyuma ya nyumba. Nikiwa kule nnje nilisikia kama kuna kitu kinatembea, nilienda kuchungulia nikaona mtu kainama.
“Wewe ni nani?” Nililiuliza kwani nilidhani kuwa ni mwizi. Kila mtu alikua ndani na kigiza giza kilishaanza kuingia. Yule mtu alishtuka na kusimama, alikua ni mwanamke, mkono wa kulia alikua kashikilia Jembe na chini kulikua na Pochi ya kike, sikuiona vizuri kutokana na giza lakini nilidhani labda ni pochi amabyo alikua kaiiba.
“Mwiziii!” Nilijikuta naogia kelele lakini kabla sijaita mara ya pili nilisikia sauti ambayo niliitambua.
“Acha ujinga mimi Bibi yako…”

Aliongea kwa hasira, alinifuata na kunishika mdomo ili nisiendelee kuongea.
“Afadhali umekuja unisaidie kuchimba…” Aliongea, hakunipa muda wa kumuuliza maswali, kila nilipotaka kuuliza alikua mkali na kuniambia kuwa nifanye kila anachoniambia huku akisema nichimbe harakaharaka kwani watu wanaweza kuja. Nilijikuta nachukua jembe na kuchimba, alitaka shiomo refu kidogo.
“Chimba refu mbwa wasije kupitia…” Aliniambia, sikujua anamaanisha nini mpaka nilipomaliza, nilimuona anatoa ule mfukoa mbao ulikua na nguo ya ndani ya Mama ambayo ina damu na kuudumbukiza akaufukia.

NB; Kuna wanawake wengi ni Single Mother leo kwakua tu walipaniki sana walipobeba mimba. Pia kelele za ndugu namajirani ziliwachanganya sana.





Nlikua natetemeka kwa uoga kwani nilikua bado sijamzoea Bibi, katika kipindi kifupi ambacho nilimjua alifanya matukio amabyo yaliniogopesha. Baada ya kufukia alichukua ndoo ya maua na kuweka juu yake, kulirudi kama kawaida.
“Iwe siri yetu sawa Mama, ukiendelea na ujasiri huu basi utadumu hapa na nitakupenda, lakini ukilogwa ukaropoka basi hii nyumba ndiyo itakua nyumba yako ya mwisho kufanya kazi, hutatoka humu na kuliona jua tena.” Aliongea hukua kinifinya finya mashavu, mikono yake migumu iliniumiza lakini hakujali na mimi sikuweza kuongea kitu chochote.

Alirudi ndani na kukaa na wengine kana kwamba hakuna kitu kilikua kimetokea. Aliingia chumbani kumsalimia Mama, wakakaa huko na kuongea mimi nilirudi chumbani kwangu, baada ya chakula cha usiku niliingia kulala. Shangazi na Baba wadogo walilala pale hivyo nyumba ilikua imejaa, usiku kama saa tano hivi Bibi alikuja chumbani kwangu.
“Nitakua nalala huku, tangu Babu yako kufariki nakua mpweke sana, sjui kwanini, ila wewe ushakua shoga yangu, unaonekana una akili sana, kesho kuna sehemu nataka twende kuna kitu nataka kukuonyesha.”

Bibi aliongea huku akipanda kitandani, ingawa alikua na chumba chake lakini tangu siku ile alihamia chumbani kwangu akilazimishia tuwe marafiki. Usiku ule sikulala kabisa, kichwani kuna mambo yalikua hayaendi sawa, matukio ya Bibi yalinichanganya na nilikua naogopa sana. Nilikesha mpaka asubuhi, niliogopa hata kufunga macho, saa kumi na mbili kamili niliamka kwaajili ya kufanya shughuli za ndani, cha ajabu Bibi alikua taayari kashaamka.

“Mimi nishazoea kwangu, yaani siwezi kulala kabisa, kijijini tunaamka mapema kabisa.” Aliongea, mimi nilimsalimia, aliitikia na kila neno aliloongea aliniita shogaa…shogaa… aliongea kana kwamba ni mtu ambaye tunajuana sana. Kwenye saa moja za asubuhi hivi wengine nao waliamka. Baba alitoka nnje akimuita Bibi, ni kama kuna kitu alitaka kumuambia, nilimsalimia Baba akaniitikia vizuri, alionekana kunyong’onyea hakua na furaha kabisa na alivyokua akiitikia ni machozi yalikua yanamlenga lenga.

“Mke wako anaendeleaje? Kaamka kweli maana nilitaka kumuaga kwanza.” Bibi alimuambia, sikujua Bibi alikua anataka kwenda wapi lakini niliposikia neno ‘kuaga’ nilipata ka ahueni flani, nilijua lazima atakua anaondoka kwani hakuna mtu anayeaga na kuendelea kubaki apo. Nilinyamaza nikisikiliza nikitamani iwe Bibi kachoka kuishi mjini au kaona kabisa kuwa kazi iliyomleta imeshindikana labda kwakua hakuna mtoto wa kulea basi anaondoka.

“Kwani ni lazima uondoke leo?” Ndiyo mwanangu, naondoka lakini nitarudi, kuna mambo yangu sijaweka sawa ni lazima kuondoka.
“Ningekupeleka lakini si unajua Mke wangu bado hajatulia, siwezi kumuach…”
“Umpeleke nani? wewe mtoto mbona uantaka kuniletea balaa, mimi naweza kwenda mwenyewe, mke wako kalala kitandani na mshono wewe uondoke kiguu na Mama yako! Watu watanielewaje, si watajua hata mimi ndiyo mchawi wa ndoa yako, sijawa Mama mkwe wa namna hiyo, nenda kakaa na mke wako mimi nitaenda mwenyewe na nitarudi mwenyewe!” Bibi alimkatisha, alionyesha kabisa alikua anamanaisha.

“Basi nenda na Karim?” Baba alimuambia.
“Nimpeleke wapi? Hivi wanangu mbona mnaniona kama sina akili, nimekua nesi Muhimbili tangu hujazaliwa, nimesafiri kutoka Ifakara kwa treni ndiyo nishindwe kusafiri na basi, hembua cheni kuniona kama sina akili, nimezeeka mwili lakini sijazeeka akili!” Aliongea kwa hasira, mimi nilinyamaza tu, walionekana walishaongea na Baba alikua anajua safari ya Bibi.
“Nitaondoka na huyu shoga yangu hapa.” Aliongea hukua kinigeukia, mshituko niliopata baada ya kusikia hivyo kidogo nidondoke. Tulikua hatujaongea chochote na nilishindwa kukataa chochote.

Baba alionekana kukubaliana naye bila hata kuniuliza, aliingia ndani na hapo ndipo Bibi aliniambia kuwa nikajiandae asubuhi hiyo hiyo tunasafari ya kwenda Morogoro. Nilitaka kuuliza lakini Shangazi Mkubwa Mama Jamila (si jina lake halisi) na kuanza kuongea na Bibi kuhusu kuondoka.
“Unarudi kwanini sasa, Mimi naona Kaka amuache huyu mwanamke, hata zaa na akifa mali zote za Kaka anachukua yeye! Mama ukiondoka usirudi, kwanini huongei na Kaka, wewe anakusikiliza sisi wengine anatuona kama tuna chuki, huyu si mwanamke….”

“Ukomee hapohapo! Maneno gani hayo yakuongea mbele ya mtoto? Hivi una akili kweli, vitu vingine unakaa navyo, ushakua mkubwa mwanangu, umeshakua umeona ulimwengu ulivyo, ndiyo Kaka yako ana majonzi kafiwa na mwanae leo unaanza kuongea habari za kuachana, kila jambo lina wakati wake, mwanangu! Wewe jamila angekufa leo halafu Mama mkwe wakoa namuambia mumeo akuache ungejisikiaje. Mbona hutumii akili mwanangu, kwanini kumwaga mchele kwenye Kuku wengu!”

Bibi alifoka na Mama Jamila alibaki kimya, alipojaribu kujitetea Bibi alimkatiza na kumuambia kuwa anaondoka kwenda kuangalia nyumba yake na kuweka mambo sawa na baada ya hapo basi atakuja moja kwa moja kumhudumia Mama katika kipindi hiki kigumu. Aliniambia niingie ndani kujiandaa kwani tunaondoka asubuhi ileile, hakutaka maswali, niliingia ndani nikajiandaa na kweli siku ile tuliondoka, Karim alitusindikiza mpaka stendi,a litaka kutupeleka lakini Bibi alikataa katakata akimsisitiza akakae na Baba ili kumfariji katika kipindi hiki kigumu cha kupoteza mtoto wake.

****

Tulifika Ifakara usiku, kwakua tulishakula njiani ilikua ni kuoga na kulala ingawa kulikua na chakula kimeandaliwa na Mdada aliyekua kaachiwa nyumba na Bibi. Nilikua nimechoka sana, nilipanda kitandani na kulala kama maiti.
“Kuna vitu nataka nikufundishe…” Ilikua ni sauti ya Bibi akiniamsha.
“Umeshakua kama mjukuu wangu, kwani wewe umeshawhi kufanya mapenzi?” Nilishtuka kwani nilikua katikati ya usingizi, sikujua anauliza nini usiku ule.
“Hapana!” nilijibu kwa mkato huku nikifikichafikicha macho kwani mwanga wa taa ulikua ni mkali.
“Nimekukagua kweli hujawahi kufanya, nilitaka tu kuhakikisha. Wewe unafaa kabisa kuwa rafiki yangu.”

Aliniambia, nilishtuka kujiona kuwa nilikua uchi kitandani wakati nililala na nguo, sijui alinivua saa ngapi lakini katikati ya mapaja yangu kulikua na vitu vyeusi vyeusi. Usingizi ulikata ghalla, nilitaka kunyanyuka kwa hasira na uoga ili kukimbia, lakini ile nanyanyuka natembea hatua mbili nilikanyaga kitu cha kuteleza ambacho kilikua katikati ya njia ya kuendea mlangoni. Nilidondoka lakini sikuumia, nilinyanyuka tena huku nikiangalia ni kitu gani nilikua nimekikanyaga.

Chini kulikua na mfuko mkubwa wa Rambo ambao ulionekana kuwa na kitu ndani yake.
“Unakimbia nini? Kaa ujifunze, huna pakwenda mjukuu wangu, wewe ndiyo nataaka unisaidie mambo yangu sas aunakimbia tena?” aliongea huku akinyanyuka, alinishika na kunikalisha kitandani, aliuchukua ule mfuko, alikaa nao kitandani akaufungua huku akiwa ameupakatia kwenye mapaja yake. Ile kufungua tu harufu kama ya nyama iliyooza ilianza kusikika. Nilikohoa kupiga chafya huku nikiziba oua kwani harufu ilikua kali.

“Tumemchelewesha sana, alitakiwa kufanyiwa kazi siku ileile!” Bibi aliongea huku akitoa kitoto kichanga, kilikua cheusi, kimevimba kinatoa harufu.
“Hii ni maiti ya mtoto wa …” Niliuliza lakini alinikatisha.
“Ndiyo, nimeichukua kuja kuizika, au unafikiri tungeacha mtoto wetu azikwe na watu wengine. Hembu acha kunicheleweshja, nenda jikoni kaniletee kisu.” Bibi aliongea huku akinisukuma kunyanyuka, alikua haionekani kuwa na wasiwasi kabisa, nilinyanyuka huku nikitetemeka kwa uoga, bila kujijua nikiwa sijui hata jikoni ni wapi nilitembea na kutafuta niakkutana na kisu kikubwa nikamletea.

Alikichukua na kuniambia nikae pemebni yake, kwa uoga nilishindwa kukaa nikabaki nimesimama tu. Hakutaka kupotreza muda, alichukua kile kisu na kuanza kuichoma choma ile maiti ya mtoto huku akiongea maneno ambayo hata sikuyaelewa. Ilikua ni mara yangu ya kwanza kuona maiti katika maisha yangu, lakini katika ule umri wa miaka 16 nilikua nikijua kuwa mtu akifa dau inaganda, lakini pale niliona tofauti, ni kama yule mtoto bado alikua hai.

Ile kuchoma kisu kimoja tu damu ilianza kutoka, ilikua inaruka kama mtu akuchome kisu ukiwa hai, Bibi alikichoma kile ichanga visu zaidi ya hamsini, yaani ni kama alikua anatoboatoboa, kitanda na yeye mwenyewe, pale chini na kila sehemu kulijaa damu lakini hakuajli.
“Hii damu yote imetoka wapi? Mbona bado katoto haka!” niliwaza lakini nilishindwa kumuuliza kwani nilisimama kwa uoga na tayari nilishajikojolea, aliniangalia bila kusema chochote, baada ya kumaliza kukichoma kile kichanga vizu alikirudisha kwenye mfuko.

Alinyanyuka na kuondoka, aliniacha pale nikiwa nimesimama, mpaka anarudi na kuanza kudeki ndani nilikua nimesimama, aliondoa kila kitu, akafanya usafi kisha akaniambia tutoke nikamsaidie kufua usiku uleule, nilifanya hivyo. Cha aajabu yule dada ambaye tulimkuta kule hakuamka na wala hakusikia chochote wakati tunafanya mambo yote yale. Baada ya kumaliza kufua alinifuata chumbani na kuanza kunielezea nini kilikua kimetokea, aliniuliza kama nin asawali lolote lakini nilimjibu hapana, kwa namna nilivyokua naogopa nilishindwa hata kuuliza ingawa nilikua na maswali mengi.

“Najua unaniogopa na kuniona kama mnyama, lakini si hivyo mimi ni mwanamke na ni Mama. Siku ukiwa Mama utakuja kunielewa ila kwa sasa sitaki unenielewe, nataka tu unisaidie ili kupambana na hii hali.” Aliongea, mimi nilimuitikia tu sawa kwa kutingisha kichwa, sikutaka maneno mengi, kichwani niliwaza kuwa siwezi kuishi katika ile nyumba, nikirudi tu Dar nachukua vilivyo vyangu naondoka hata bila kuaga, kwana nilikua na nauli yangu kwanini kuhangaika. Lakini ni kama alikua anasoma mawazo yangu kitu ambacho kiliniogopesha zaidi.

“Najua unawaza kuondoka lakini huna haja ya kufanya hivyo, mambo yote haya ninayoyafanya nakua namsaidia Mama yako, yeye ana matatizo, miaka mitatu katika ndoa bila mtoto na sasa mtoto kafia tumboni ilibidi sadaka itolewe la sivyo asingezaa tena.” Aliendelea kuongea, alikua akiongea kana kwamba alikua akifanya matambiko kumsaidia Mama lakini mimi niliona kabisa kuwa anamloga, mambo aliyokua anayafanya na namna alivyokua anafanya ilikua ni kama matambiko au mauza uza mengine ya ajabu.

Nililazimika kumsikiliza na kukubaliana naye kwa kila kitu, tulikaa Ifakara kwa siku moja, siku iliyofuata Bibi alisema kuwa hawezi kusafiri, Karibu alitaka kuja kumchukua lakini Mama Jamila alilazimishia na kuja na gari ya Baba kumchukua, yeye alikua hana gari lakini mara nyingi alikua akitumia gari ya Baba kwani Baba yeye alikua anatumia Gari ya Mama. Tangu kuambiwa kupumzika kutokana na ujauzito alikua haruhusiwi kuendesha gari wala kufanya chochote.
“Unajua Kaka anateseka sana!” Shangazi aliongea, tulikua njiani tunarejea mjini.

“Kwanini? Amekuambia kwamba anateseka? Anaumwa au nini?” Bibi alimuuliza, alioneysha ukali kana kwamba kuna kitu alikua anataka kuzuia shanagzi asikiongee.
“Hapana lakini mimi namjua mdogo wangu, ni mkimya si mtu wa kuongea, yule mwanamke atakua anamsumbua sana, yaani nimeona siku mbili hizi mtu hataki kula anawaza mtoto, kidonda hakitaki kupona kinataka kuoza lakini hajali yeye ni kulia tu, anamuumiza Kaka hata kwenda kazini hawezi. Yule mwanamke anatakiwa kuachwa kudekezwa la sivyo atamuua Kaka. Yaani mimi hata sijui kwanini yuko naye?”

Alilalamika, bibi alimuangalia kwa hasira ksiaha kamuuliza.
“Ulishawahi kupoteza mtoto wewe?”
“Hapana…”
“Sasa unaongea upuuzi gani, kwanini usinyamaze, kama hujui uchungu wakupoteza mtoto basi huwezi kumpangia mtu namna ya kuomboleza.” Aliongea na shangazi alinyamaza.
“Samahani Mama Sikumaanisha hivyo.” Shangazi aliongea baada ya Bibi kukaa kimya kwa muda huku machozi yakimlenga lenga.
“Mama usilie, sijazungumzia kumpoteza mtoto, nilikua natania tu.” Aliongea, Shangazi alionyesha kunywea na kumuonea huruma Bibi, alibadilisha mada lakini Bibi hakukubali.

“Unabeba mimba miezi tisa mtoto anafia tumboni, hivi unafikiru uzazi ni kitu kidogo, nilipoteza Kaka zako watatu kabla ya wewe kuzaliwa tena wote walikua washatimiza muda wa kuzaliwa ahlafu wewe unakuja na ujinga ujinga wako hapa? Mwenzako kajifungua kwa kisu halafu anaangalia kovu tu na hakuna mtoto hivi unafikiria kweli atakua na amani, unataka ale ili nini? Muache mtoto wa watu na kama unaona anakukera hujaitwa, rudi kwa mume wako kakae na familia yako uone kama atakuja kukukerea huko!”

Shangazi hakuongea tena mpaka tunafika Dar, njia nzima ilikua kimya, alitufikisha nyumbani na kutuacha hapo. Alipofika alipokelewa vizuri na Baba, aliniita chumbani na kuniambia kuwa nisiongee chochote kwani watu wakijua nitaharibu kila kitu. Shangazi naye alituacha na kuondoka zake, hakuja pale mpaka baada ya siku tatu. Alikua kachangamka na walikua wakiongea vizuri na Bibi kana kwamba hakunakitu kimetokea, mpaka wakati huo mimi nilikua siwaelewi.

Baba alijisikia vizuri na kuendelea na kazi, lakini hali ya Mama ilizidi kuwa mbaya, alirudishwa hospitalini lakini mshono ulikua haukauki, ulikua umeoza na unatoa wadudu.
“Si ushavunja ungo wewe?” Siku moja Bibi aliniuliza, zilikua zimepita wiki mbili, Mama alirudishwa nyumbani akawa anauguziwa hapo na kidonda kiligoma kabisa kupona.
“Ndiyo.” Nilijibu kwa uoga, sikujua sababu lakini niliogopa kumdanganya kwani nilihisi kama Bibi anajua kila kitu.
“Unaingia lini katika siku zako?” Aliniuliza, nilitafakari kidogo na kuwaza nikamuambia wiki inayofuata. Aliniambia sawa na kunyamaza hakulizungumzia hilo tena.

Siklu iliyofuata nilishangaa Shangazi ananiletea Pedi za kuvaa, mara zote Mama ndiyo alikua akininunulia, yeye ndiyo alinifundisha usafi, namna ya kuzivaa na kujisafisha kwani nilivunjia ungo kwake na nilikua sijui chochote.
“Shika Mama yako anaumwa, tumia hizi ndiyo nzuri kwa mwanamke, si unajua namna ya kujisafisha au huyu mwanamke hajakufundisha?” Aliniuliza kwa dharau, ni kama alikua ananikejeli flani, nilimuambia najua na jnilifundishwa vizuri.
“Basi ukianza kuona dalili unaingia huko vaa usije kututia aibu hapa.’ Aliniambia, nilimyuitikia kumkubalia bila kusema chochote.

Hatukuliongelea hilo swala mpaka siku nilipoingia kwenye siku zangu, kwa kawaida mimi nikiingia kwenye siku zangu tumbo linaniuma sana, Bibi aliniuliza niakamuambia nipo kwenye siku zangu. Alikua kama kafurahi flani, cha ajabu alikua akinifuatilia sana, nilipotoa Pedi ya kwanza alilichukua, nilishangaa anapeleka wapi, lakini aliniambioa nisijali kuna kitu anataka kufanya. Aliniuliza tena lile swali ambalo aliniuliza kipindi kile nikiwa kijijini kama nilishawahi kufanya mapenzi nikamuambia hapana, alifurahi.

Alichukua Pedi, akatafuta bakuli, bila kinyaa bila kuhisi chochote aliishika na kukamualia damu zote katika bakuli. Kweli niliogopa na sikujua ni nini kilikua kinaendelea, alifanya hivyo tena nilipobadilisha yapili na yatatu. Nilishindwa kumuuliza kwani niliogopa sana, nilihisi yeye na Shangazi kuna kitu wanataka kunifanyia lakini kila wakati alikua akinitoa wasiwasi kuwa nisiogope hainihusu mimi. Asubuhi aliingia jikonio na kuandaa uji, cha ajabu hakutumia maji ya kawaida, alichukua maji ayaliyochanganyika na damu za heshi yangu ndiyo akatumia kupika uji.

Alifanya mambo yote hayo mimi nikimuangalia, nilishindwa kuvumilia na kuamua kumuuliza.
“Unafikiri Mama yako ataponaje, kile kidonda kinatakiwa kukauka, anatakiwa kunywa huu uji.” Aliongea kwa kujiamini, alikua hajali na kwake kilikua kama kitu cha kawaida.
“Bibi hapana! Huo ni uchafu, siwezi kukubali Mama nywe uchafu wangu! Niliongea huku nikijaribu kujizuia kutapika.” Aliniangalia na kucheka hukua kiniambia.
“Kua uyaone mjukuu wangu…”




“Unataka Mama apone au afe?” Bibi aliniuliza, nilimuangalia kwa uoga lakini hakujali, alianza kunielezea naman aile ilikua ni dawa nzuri amabayo ingemsaidia Mama kupona, pamoja na maelezo mengi lakini sikumualewa. Niliona kama uchafu na nilikua na wasiwasi kuwa labda ni mambo ya kishirikina na hivyo vitu vinaweza kuniumiza na mimi.
“Baba anajua?” Nilimuuliza kwani kama ni dawa inamaana hata Baba alitakiwa kujua kwani aliniambia kuwa Mama hatakiwi kujua anakunywa dawa gani kwani itamuathiri.

“Unavuka mipaka sasa, naona nimekudekeza sana, wewe ni mfanyakazi hapa, kazi yako ni kutumwa tu, huwezi kuniuliza ujinga ujinga wako! Chukua huu uji mplekee Mama yako, hawezi kujua kama umechanganywa na nini kama wewe hutamuambia. Ingawa uji ulikua na wekundu wekundu lakini kwakua ulikua ni uji wa ulezi basi Mama hakuweza kujua kuna nini, Bibi alinilazimishia kumpelekea na kuhakikisha kuwa anakunywa wote. Huku nikitetemeka niliompelekea Mama, nikakaa pembeni yake mpaka akamaliza kunywa.

“Unaona sasa, kumbe una akili, sasa ndiyo tutakua marafiki, chukua hii…” Aliongea huku akinipa noti mbili za Shilingi elfu kumikumu. Nilizipokea kwa shongo upande, aliendelea kufanya hivyo kwa siku tatu mpaka nilipomaliza siku zangu. Chakushangaza nikuwa baada tu ya kumaliza siku zangu Mama kidonda kilifunga, kilikauka kabisa na kupona, kila mtu alishangaa kwani kabla kilikua kama kimeoza siku tatu nyuma.

“Unaona, nilikuambia kuwa unamsaidia Mama yako wewe ukaniona kama ni mchawi, sasa hivi anarudia katika hali ya kawaida, anaweza kurudi kazini na anaweza kubeba mimba nyingine.” Bibi aliongea kuna wakati nilitaka kumuamini, nilihisi kama kweli alikua akimsaidia Mama kwani alirudi katika hali yake ya kawaida, hakua akilalamika maumivu tena na baada ya kama wiki moja Bibi aliondoka na kurudi kijijini kwake. Nilifurahia kwani nilishamuogopa na nilijua kuwa maisha yatakua kama kawaida.

“Kaka huyo mwanamke hazai!” Mama Jamila aliongea, ulikua ni usiku na Mama alikua amesafiri, alienda kijijini kwao kwakua kulikua na msiba.
“Unamaanisha nini? Mke wangu hana matatizo, juzi ndiyo katika kujifungua tu!” Baba aliongea kwa hasira, ilikua ni siku ya pili mfululizi Shangazi anaongelea lile swala, ni kama alikua anataka Baba kuchepuka na kumuacha Mama.
“Unafikiri hata kama kizazi anacho, hivi kubeba mimba ni lini tena? Hivi unajua mtu aliyefanyiwa upasuaji anatakiwa kukaa angalau miaka mitatu kabla ya kubeba mimba, hivi wewe uvumilie miaka mitatu mingine bila mtoto?

Shangazi aliuliza, Baba alimkatisha tena, alikasirika na kuongea maneno ya kumuambia asifuatilie maisha yake lakini wapi. Shangazi alimgombeza Baba, aliongea kwa hasira na kumuambia kuwa hawamtaki Mama na kama yeye anamng’ang;ania basi akipata matatizo asiwafuate. Baba aliksirika, aliondoka na kuingia chumbani akimuacha Shangazi peke yake sebuleni. Baada ya kuondoka Shangazi naye akuondoka kwani aliona kama kaachwa mwenyewe, lakini wakati anaondoka alikua akijiapiza kuwa ni lazima Mama ataondoka.

Ilikua imepita miezi mitatu tu tangu Mama kujifungua na kupoteza mtoto wake, kwa namna Shangazi alivyokua akilikomalia lile swala nilimuonea Mama huruma. Usiku ule Baba alipigiwa simu, Mama alidondoka huko kwao na kupelekwa hospitalini ambapo aligundulika kuwa ni mjamzito. Babaa lifurahia lile swala la Shangazi kupata mimba, nilimsikia wakati anaongea na simu namna alivyokua anataka kujua kuwa nini kimetokea, kujua hali ya Mama na namna alivyokua akiwaambia atulie ataenda kumchukua yeye mwenyewe kwani anahofia akipanda basi mimba inaweza kutoka.

Alimpigia simu Mama yake, lakini ghafla baada ya kuongea na Bibi nilimuona Baba kanywea, ule uchangamfu, ile amshaamsha aliyokua nayo ilipotea kabisa, sikuelewa sababu lakini nilihisi kuwa labda kuna kitu Bibi kamuambia. Asubuhi Baba aliondoka kumfuata Mama na alirudi naye jioni, wakati anarudi nilishangaa wameongozana na Bibi, kumbuka Mama alienda kwenye msiba chalinze na Bibi alikua Morogoro hivyo Bibi alipanda gari ili kuja kumuona Mama ghafala, si safari aliyokua ameipanga.

Bibi alionekana kuwa na mawazo mengi, alikua haongei lakini nilimuona kabisa kuwa ana kitu, usiku kama kawaida yake alilala chumbani kwangu, ingawa kulikua na vyumba vingi lakinia liniita shogaa.
“Nimekuja kumuuguza mwanangu, sasa hivi nataak mjukuu, nitaitunza hii mimba mpaka aajifungue, sitaki wafanye makosa kama kipindi kile!” Aliniambai, sikumuuliza chochote lakini alinielezea mwenyewe, ni kama alikua na kitu rohoni kimemkaba lakini anashindwa kuongea, ingawa sikutaka kujua sana lakini nilijikuta namuuliza.
“Makosa gani?’ Niliuliza, ulikua usiku, kila mtu kalala kageukia upande wake.

“Unataka kujua mjukuu wangu?” Aliniuliza, baada ya lile swali sikuona kama nataka kujua. Nilinyamaza kimya lakini aliendelea kunielezea kuwa vyakula alivyokua anakula Mama kipindi ni mjamzito havikuandaliwa vizuri na hivyo ndiyo vilimuua mtoto. Aliniambia, nilikua na maswali mengi lakini niliamua kunyamaza, sikutaka kubishana naye kwani nilijua kabisa siwezi kuapta jibu la maana, nilijifanya kuchoka na kulala, sikutaka mazoea sana na Bibi ingawa yeye alitaka kuniambia kila kitu.

****

“Kwanini umetangaza kuhusu mimba yangu, mimi ndiyo nimejua, nimekuambia tu ushampigia simu kila mtu kuwa nina mimba, mimba hata mwezi haina lakini ushaanza kutangaza!” Mama aliongea, nilikua jikoni nimekaa napika, Bibi na ndugu wengine walikua sebuleni, Ilikua ni siku ya pili tangu kurudi lakini ndugu zake wote walikuja pale na kuanza kumopa Mama hongera kitu ambacho kilimuuma kwani hakutaka kumuambia mtu.
“Kwahiyo unaona shida mimi kuwaambia ndugu zangu? Nimetangaza wapi mimi? Hiyo mimba si niyakwangu au una mwanaume mwingine?”

Baba aliuliza kwa hasira, alionekana kuchukizwa na maswali ya Mama na kwa ilivyoonekana ni kama walishagomabana sana huko nyuma.
“Hapana ni yako lakini mimi mwenyewe nimeenda kupimwa hata Mama yangu sijamuambia, sijamuambia mtu majibu yangu kwakua ni mapema sana, yaani juzi tu nakuambia nakuta Mama yako kashakuja kabisa kunihudumia, leo nashangaa ndugu zako wote hawa hapa wanakuja kunipa hongera, mimba yenyewe hata mwezi haina, si kunitafutia mabalaa hapa!”

“Mabalaa, kwahiyo unaona ndugu zangu ni wachawi, unaona ndugu zangu wachawi? Nakuuliza si ujibu wewe mwanamke?” Baba alikasirika, aliongea huku akimkwida Mama shingo kutaka kumpiga, hakumpiga lakini kwa namna alivyokua kakasirika hata mimi nilishangaa kwani tangu kuingia katika ile nyumba nilikua sijamuona katika hali ile tena. Baba alitoka pale kwa hasira na kunioacha nikiendelea na mambo yangu, baada ya Baba kutoka ndipo Mama aliniona, alikua hajui kama niko jikoni, hakunisemesha chochote aliondoka zake.

Nilitoka sebuleni kuwaangalia wageni niliona wote wamatoka nnje, ni kama walikua wamesikia jinsi Baba livyokua akibishana na Mama. Walitoka kwa kununa na kuseama kama anawaita wachawi basi wanaondoka na kumuachia nyumba yao. Bibi alikua akiongea huku akilia kabisa, nilishindwa kuwaelewa kwani Mama hakusema kitu hicho ni Baba alisema na hakumuelewa vizuri.
“Muombe Mama yangu msamaha umemtukana sana!” Baba alimuambia Mama, walikua sebuleni alimshika kumtoa nnje ili kuwaomba ndugui zake msamaha.

Mama alijaribu kujitetea lakini Baba hakumuelewa, alimuambia kuwa hawezi kugombana na ndugu zake kwajili yake. Ili kuepusha shari Mama alitoka nnje na kwenda kuomba msamaha, walimsamehe kishingo upande, Bibi alirudi ndani lakini kina Shangazi waliondoka hata bila kula pamoja na kwamba nilishawaandalia chakula na haikua kawaida yao. Maisha yaliendelea, lakini hali ya Mama iliendele akubadilika, alikua akikonda tu siku hadi siku, mwanzo nilidhani ni mawazo tu ya kawaida lakini alianza kuishiwa na damu.

Alikua akiishiwa na damu, anadondoka anaenda kulazwa mpaka hospitalini anaongezewa lakini baada ya wiki tena anadondoka anaishiwa damu kabisa. Mmmbo yaliyokua yanaendelea hospitalini nilikua siyajui lakini siku moja walirudi wakiwa hawaeleweki. Baba alikua kakasirika akimnunia Mama kwa kutoa mimba yake, Bibi alikua akimbembeleza na kumuambia amsikilize mkewe kwani hivyo vitu vinatokea. Kwa maelezo yao ni kwamba mama alipopimwa baada ya miezi nne alikutwa hana ujauzito, hakuumwa tumbo wala nini kusema kuwa labda mimba ilitoka bali alipimwa wakati wiki moja kabla alivyodondoka alikua na mimba..

Baba alikua kakasirika sana, alikua kakasirika kwani alionyesha kuwa na hamu sana na mtoto hivyo alihisi labda Mama alikua hataki ndiyo maana akaitoa. Waligombana sana lakini Bibi alikua akimkingia kifua Mama akimuambia labda vipimo vilidanganya hakua na mimba. Baba hakukubali kabisa aliingia chumbani akimuacha Mama sebuleni akiwa analiakama mtoto, hata yeye alikua haelewi nini kilikua kimetokea. Mawazo yangu yote mimi yalikua kwa Bibi, nilihisi kama kafanya kitu kibaya.

“Kesho nataka kuondoka…” Usiku Bibi aliniambia, nilijua kashamaliza kasi yake.
“Sawa…” Nilimjibu kwa kifupi huku nikijifanya kulala.
“Hutaki hata kujua kwanini naondoka?” Aliniuliza.
“Si Mama hana mimba tena, nilijua umekuja kumhudumia na sasa hivi hana mimba ndiyo maana unaondoka.” Nilimjibu kwa kifupi kusema kweli nilishahidi amemfanyia Mama mambo mabaya hivyo sikutaka kujua, niliona kama nikijua nitazidi kuumia na nitakua sehemu ya ushenzi wake, nilizuga kuelewa.

“Tumefanya kazi nzuri sana, tunatakiwa kujipongeza, unataka zawadi gani nitamuambia shangazi yako akupe.”
“Tumefanya?” nilimuuliza baada ya kuona anatumia neno ‘tume’ wakati mimi sikufanya chochote.
“Ndiyo wewe ndiyo mshirika wangu humu ndani, tunamlinda Baba yako, unafikiri bila wewe mimi ningeweza? Hapana…” Aliongea, kusema kweli nilitaka kujua kuwa ni kitu gani nilikua nimefanya lakini niliogopa kuuliza. Cha ajabu nikuwa Bibi alitaka kuniambia hivyo hivyo, alianza kuelezea ushenzi aliokua ameufanya, yeye aliona kawaida akidhani labda anamsaidia Mama na Baba.

“Huyo mwanamke hawezi kuzaa sasa hivi, nilikuja kumpikia ili kuipoteza mimba, tatizo mwanangu si muelewa nikimuambia wasubiri, hajatoa mimba imepotea asubiri kwanza kuzaa.” Bado nilibaki kimya, niliwaza hivi ni kwanini Bibi ananiambia mambo yake lakini sikupata jibu, nilifumba macho kulazimisha kulala huku nikishukuru Mungu kuwa Bibi anaondoka. Asubuhi kweli aliondoka na Baba mdogo Karomu ambaye alimpeleka, lakini baada ya Bibi kuondoka nyumba haikua na amani, Baba alikua ni mtu wa hasira tu kila mara akimshutumu Mama kuwa ametoa mimba yake.

Migogoro kati ya Mama na Baba ilimfanya Baba kuwa karibu zaidi na ndugu zake hasa Mama Jamila, pamoja na kuwa alikua na ndoa yake, familia yake na maisha yake lakini muda mwingi aliutumia pale nyumbani, yeye alikua ndiyo kama Mama mwenye nyumba akiamua kitu kinakua. Mama jamila alikua na visa, vimaneno maneno vya kejeli na mara kwa mara alikua ni mtu wa kumtukana Mama waziwazi na Baba naye hakuongea kitu akiambiwa alikua mkali na kumuambia kuwa anawachukia ndugu zake.

Siku moja Shangazi alikuja nyumbani, nakumbuka ilikua ni jioni na tulishapika hivyo tulikua tumekaa sebulani tunaangalia TV mimi na Mama, alikuja bila kusalimia alikaa. Aliagiza kuletewa maji ya kunywa, nilinyanyuka kwenda na kumletea lakini nilipompa tu aliipiga glasi chini.
“Hivi mimi ndiyo wakuletewa maji na mfanyakazi wa ndani? Wewe kazi yako ni nini? Kuzaa huzaio kazi ni kutoa tu mimba za Kaka yangu halafu hata maji huwezi kuniletea!” Alijifanya kuongea kwa hasira, Mama hakumjibu, alinyanyuka na kwenda kumletea maji.

Aliyachukua na kunywa lakini alipomaliza tu alianza kupiga kelele kuwa tumbo linamuuma, kuna kitu kinamkata tumboni, alipiga kelele sana mpakatukahisi kwelia anaumwa. Tulilazimika kumpeleka hospitalini huku akilalamika kuwa kuna kitu amelishwa kwani alihisi kama kanyweshwa sumu. Alikua anajirusha rusha kwenye gari hukua kimlaumu Mama kuwa anataka kumuua, alikua akilalamika sana mpaka tunafika hospitalini alikua kachoka anaongea kwa sauti ya chini chini akiuambia kila mtu kuwa kalishwa sumu.




Hakuonekana kama ana kitu pamoja na vipimo mbalimbali, aliambiwa haumwi chochote lakini yeye bado aliendelea kusisitiza kuwa Mama kamlisha sumu. Aliruhusiwa kuondoka, badala ya kurudi kwake alirudi nyumbani na Mama. Baba aliporudi alimkuta kitandani na kuanza kulalamika kuwa Mama kamlisha sumu. Babaa liongea sana kumshutumu Mama, alimtukana sana lakini Mama alibaki kimya, hakumjibu chochote zaidi ya kujitetea kuwa yeye hajafanya chochote.

Maisha yaliendelea lakini kila siku ilikua ni maneno maneno tu, Baba alikua mtu wa kumtukana Mama na kumfanyia madharau mengi, mimi nilishangaa ni kwanini Mama alikua akivumilia wakati alikua na kazi yake nzuri tu. Shangazi Mama Jamila ndiyo alikua kama Mama wa ile nyumba, ingawa alikua hakai pale lakini kila siku alipiga simu kutaka kujua nini kinaendelea. Bibi naye alikua ananipigia simu kuniulizia hali ikoje na kwakua nilikua nikimuogopa basi nililazimika kumuambia.

Kuna wakati nilitamani kuondoka kwani nyumba haikua na amani lakini nilishindwa kwani Bibi alikataa na kwakua alikua akinilipa pesa nyingine tofauti na mshahara basi nilibaki.
“Ataondoka tu humu ndani nakuambia!” Shangazi aliongea, nakumbuka ilikua ni usiku, Shangazi siku hiyo alikuja nyumbani, Mama alikua katoka na Baba, walienda kwenye sherehe ya kazini kwa kina Mama, Shangazi alipokuja na kuwakosa aliniuliza nikamuambia,a likasirika sana kwanini walitoka pamoja, alionekana kuumia sana.
“Huyu mwanamke hampendi Kaka yangu, ni pesa zake, hivi unafikiri mdogo wangu akifa hapa hizi mali si atachukua yeye!”

Aluiongea kwa hasira.
“Inamaana kila siku wanatoka opamoja?” Aliniuliza.
“Hapana, inatokea mara moja moja.” Nilimjibu kwa mkato, ingawa walikua wakitoka mara kwa mara, wakati mwingine hata wakigombana kwenye kutoka wanapatana lakini sikutaka kumuambia, niliupna wivu wake kama wa mke mwenza hivyo sikutaka kuharibu siku yangu.
“Najua unanificha, hivi unajua kuwa ukiwa karibu na mimi utafaidi sana, hivi wanakulipa Shilingi ngapi?” Aliniuliza, nilitafakari kidogo nikaona pesa hizi mbele yangu.
“Elfu hamsini…” Nilimjibu.
“Unaona pesa gani hiyo wanakupa, mali zaote hizi anakupa hiyo pesa, mimi nishakuambia kuwa huyu mwanamke ni shetrani, Kaka yangu anatakiwa kuoa mwanamke mwingine, tena mwenye akilia mabye atakupenda na wewe, huyu hana kitu!” Aliongea, mimi nilinyamaza tu, kusema kweli nilishaichoka ile familia lakini kuna kitu kama kilikua kinaniambia kuwa baki uone mwisho wake.
“Mimi nitakua nakupa laki moja keshi, mara mbili ya hizo pesa wanazokupa, ninachotaka ni wewe kunisikiliza mimi na kunifanyia kazi zangu!” Aliniambia, sikua na namna zaidi ya kukubali kwa kichwa.

“Kwani ni lazima kufanya chochote?” Niliwaza “Pesa nachukua lakini sifanyi chochote anachoniambia.” Shangazi aliongea maneno mengi, ilikua ni usiku na mimi nilikua nishachoka, nilitaka kwenda kulala kwani baba waliondoka na funguo za Geti hivyo nisingekua na sababu ya kuwafungulia, lakini Shangazi alikua pale na alikua akijiongelesha ongelesha hivyo nililazimika kukaa sebuleni kumsikiliza. Kuna muda nilipitiwa na usingizi, nilishtuka baada ya kusikia mtu anafunga mlango, nikijua labda ni akina Baba nilimuona Shangazi akitoka chumbani kwa Baba.

Nilishtuka, mlango ulikua kweli haujafungwa lakini nilijua kuwa Baba hapendi mtu kuingia chumbani kwake na kama angejua ingekua kazi.
“Mimi naondoka, kama nilivyokuambia nitakua nakulipa mimi, ila sitaki uongee chochote, leo nimemkosa mdogo wangu, akija sitaki hata umuambie kuwa nilikua hapa.” Aliongea huu akitaka kutoka, lakini kabla ya kiufanya hivyo huko nnje mlango ulisikika ukifunguliwa. Shangazi alisikia, alipaniki sana alianza kuzunguka zunguka kutaka kujificha, mara aingie kwenye mapazia, mara ajifiche pembeni ya masofa na vituko kibao.

“Kaka hatakiwi kuniona kabla ya kuingia chumbani, anatakiwa kuniona akitoka…” Aliongea, mimi sikujua sababu zake na wala sikujali. Baba walikua wanakaribia kuingia kwani niliwasikia kabisa wakifiia mlango, Shangazi alikimbilia jikoni na kujibanza huko. Baba waliingia na Mama wakiwa na furaha zao, walikua wakiongea mambo yaliyotokea kwenye sherehe, walikua kawaida sana. Walishangaa kuniona pale wakati waliniambia wameondoka na funguo ili wasinisumbue, nilitaka kuwaambia kuwa Shangazi alikuja lakini niliogopa kwani alsihasama kuwa hataki watu wajue kama alikuja.

Baba aliingia chumbani na kuniacha mimi na Mama sebuleni, Mama alikua amesimama mimi nimekaa kwenye kochi, alikua akinisisitiza kuwa nikalale.
“Mshenzi mkubwa wewe! Utakua na wanaume zako unanoichora kunichekea chekea na masharehe, kuna yule mlinzi ulikua unaongea naye nini?” Ghafla Baba alitoka chumbani, alikua kavaa Bukta tu, ilikua ni mara yangu ya kwanza kumuona vile. Alikua kakasirika sana, kanuna kavimba, alikua akitukana matusi ya nguoni ambayo hayaandikiki.

Mama alimsihi anyamaze kwania najidhalilisha lakini ni kama alipalia mkaa, Baba alizidi kuongea, alimfuata na kumshika, hapo ndipo niliona kuwa kumbe Baba alikua kashikilia Panga mkononi. Sijui alilitoa wapi lakinia likua kashikilai Panga, aliniambia niondoke kwani anataka kufanya kitu kibaya na hataki niwe shahidi. Kwa uoga nilikimbilia chumbani, huku nyuma nilisikia Mama akipiga kelele za kuomba msaada, alikua akipigwa na mabapa ya mapanga, alipigwa sana kwa zaidi ya nusu saa hivi, baada ya hapo kila kitu kilikua kimya.

Niliogopa hata kutoka chumbani kuangalia, nilikaa macho mpaka asubuhi, sikusikia chochote. Asubihi nilitoka nnje nikiamini kuwa Mama atakua ashakufa, lakini haikua hivyo, nilimkuta Baba kakaa sebuleni, panga lipo pembeni kamshikilia Mama amemlaza kwenye mapaja yake.
“Mama yao hataki kuamka, sijui nini kimempata, tumekorofishana nimempiga kidogo yeye kazimia.” Aliniambia, nilikua natetemeka nilishindwa hata kumjibu kuwa yeye ndiyo kampiga. Nilitembea harakaharaka kuelekea jikoni, sikumkuta Shangazi, sijui alitoka saa ngapi lakini hakua ndani.

Nnje geti lilikua limerudishiwa tu hapo ndipo nilijua kuwa Shangazi alikua katoka. Nilirudi sebileni na kukuta Mama alishaamka, Baba alikua akimuomba msamaha na kulia kama mtoto, Mama alikua kama kachanganyikiwa flani alikua bado haelewi nini kilikua kimetokea. Baba alimsaidia kunyanyuka, hapo ndipo niliona uso wa Mama ukiwa umevimba, nguo zimemchanika na alikua kavimbavimba sehemu mablimbali za mwili wake. Baba alimsaidia kuingia ndani kwakumbembeleza huku akiomba msamaha.

Kwa kipigo alichokipata nilijua kabisa kuwa lazima Mama ataondoka. Baada ya kuingia ndani Baba alitoka na kuniambia kuwa Mama kalala asisumbuliwe na mtu yeyote kwani hajisikii vizuri, nilimuitikia, aliondoka na kwenda kazini bila wasiwasi wowote, ni kama hakukua na kitu chochote kilichotokea. Nilimgongea Mama aliniambia hawezi kutoka, hakutoka mpaka usiku wake. Shangazi alinipigia akiniuliza Kama Mama hajaondoka bado, nilimuambia hapana.

“Lakini waligombana?” Aliniuliza, nilimuambia ukweli kuwa Baba alimpiga Mama mpaka kuzimia, alishangilia na kuniambia.
“Ataondoka tu, anafikiri hapo ni kwake, kama asipoondoka mzima basia taondoka maiti.” Nilijifanya nina kazi ya kufanya na kukata simu, usiku Mama aliptoka, bado alikua na maumvimbeuvimbe, nilitamani kuongea naye lakini nilishindwa, nilikua namuonea huruma sana. Siku hiyo Bbaa alichelewa kurudi, kwenye saa nne hivi tulikua tunaangalia tamthilia, nilisikia honi. Mama alikua hajisikii vizuri, aliniambia nikamfungulie Baba mlango kwani kutokana na kipigo yeye hata kusimama ilikua ni shida.

“Mama yako yuko wapi?” Baba aliniuliza nilipofungua geti, alishusha kioo cha gari, hakuendesha gari alikua akiniangalia tu.
“Yupo ndnai hajiskiii vizuri.”
“Funga geti muambie aje kufungua mlango.” Baba aliongea kwa hasira, sikutaka kubishana naye, nilifunga geti kama nilivyoagizwa na kwenda kumuambia Mama. Kwa shida hivyo hivyo alienda kufungua.
“Nakufaaaaa!” Nilisikia kelele kutoka nnje. Nilichungulia harakaharaka dirishani na kuona Gari ya Baba ikiserereka mpaka karibia na kugonga ukuta wa nyumba.

“Mungu wangu! Baba anataka kumuua Mama!” Nilijikuta napiga kelel. Baba hakusubiri Mama afungue geti, alipomuona tu pale getini, alikanyama mafuta kwa kasi, ni kama alikua anataka kumgonga lakini Mam alimona nahisi alijrusha pembeni kwani gari ilipita na yey nilimuona kalala pembeni. Lakini Baba haukoma, baada yakuona kama hajampata alianza kurudisha gari nyuma ili kumgonga. Mama sijui alipata wapi ujasiri, alinyanyuka na kukimbia nnje huku akipiga kelele.

Kilikua ni kitendo cha sekunde kadadhaa, Baba baada ya kuona kuwa Mama katoka kukimbilia nnje, alirudisha gari nyuma na kugeuza akaondoka. Kutokana na kelele za Mama watru walikuja, si wengi sana lakini walikuja pale nyumbani kuulizia nini kilikua kimetokea. Lakini walichelewa kwani Baba alikua kashaondoka, walikaa kaa pale na kumshauri Mama kwenda Polisi au kuondoka, Mama aligoma kabisa kwenda Polisi ndipo walimshauri kuondoka kwani kama Baba kamshindwa kumgonga basi anaweza kumuua.

Mama alikua akitoa sbabau sababu ili tu asiondoke, lakini mjumbe wa nyumba kumi aligoma kabis akumsikiliza. Alimuambia hata kama hawezi kuondona usiku ule basi aende kulala kwake na asubuhi ndiyo wayaongee hayo mambo. Mama alikubali kwa shingo upande na kuondoka kwenda kwa mjumbe. Niliogopa kubaki pale nyumbani peke yangu, nilikua nahofia kuwa labda Baba akitoka huko anaweza kuja na kunifanyia kitu kibaya.

Tulifunga nyumba na kundoka, lakini wakati naondoka Shangazi alinipigia simu, aliniuliza ni kitu gani kimetokea? Kwa namna alivyokua anaongea ni kama alikua anategemea kuna kitu kibaya kitamtokea.
“Kwahiyo hajafa?” Aliniuliza.
“Hapana, hata hajaumia, Baba kaondoka na hatujui kaenda wapi.”
“Afadhali, akifa Kaka watamfunga!” Aliongea, lakini cha ajabu alinisihi nirudi nyumbani, nilimuambia mimi naogopa lakinia linisisistizia kuwa sina kitu cha kuogopa kwani baba hawezi kunifanya chochote mimi nirudi.

“Wewe si mgomvi wake, rudi usiache nyumba peke yake! Huyo Malaya ndiyo atakoma, safari hii nina uhakika ataondoka!” Aliongea kwa hasira, mimi kazi yangu ilikua ni kusikiliza tu na kukubaliana na kila kitu anachoongea, sikua na jambo jingine lakumuambia. Pamoja na kunisihi sana kubaki lakini nilikua naogopa, sikutaka kubaki hivyo nilienda kulekule na Mama. Asubuhi simu yangu amabyo ni kama ya nyumbani iliita, niliondoka nayo mimi kwani ndiyo mara kwa mara naituia. Alikua niBaba ambaye aliniuliza kama Mama anaendeleaje?

Nilimuambia kila kitu, ghafla nilisikia Baba akilia, alikua analia huku akionekana kalewa sana. Alikua akiniambia kuwa hajui kilichotokea na hajui ni kwanini alikua anataka kumuua mke wake, mimi nilinyamaza kwani sikua na kitu cha kumjibu. Aliongea sana akiwa kama ananiomba msamaha mimi, hakumuongelea Mama bali alikua akiniambia kuwa anajutia na yeye si mnyama hivyo nisindoke na kumuacha peke yake, alikua analia sana akinibembeleza mimi.

“Nikupe uongee na Mama?” ilibidi kumuuliza baada ya kuona ananiomba mimi msamaha zaidi wakati mtua liyemkosea alikua ni Mama. Baada ya kukata simu tu Bibi naye alipiga, alikua kapaniki akiulizia ni kitu gani kilikua kimetokea, nilimuelezea kila kitu tangu jana yake, Bibi hakuamini lakini nilimuambia ni kweli. Aliniahidi kuja kusuluhisha kila kitu siku hiyo hiyo hukua kinisisitiza nifanye juu chii Mama asiende Polisi wala kuongea na ndugu yake kumuambia mambo yaliyotokea.

Nilimkubalia lakini sikuona kama ni sawa, baada tu ya kukata simu nilimfuata Mama na kumuambia ni kwanini asimpigie simu Kaka yake. Mama alikua na ndugu wengi lakini kuna Kaka yake ambaye walikua Mapacha niliona kama anampenda sana na siku zote alikua upande wake. Nilihisi Mama kafanyiwa mambo ya kishirikina ndiyo maana hawezi kuondoka kwa Baba, nilijua anahitaji msaada wa nnje ili kuondoka pale. Nilipomtajia tu jina la Kaka yake alikasirika sana nsna kunaimbia kuwa sitakiwi kuingilia mambo ya ndoa yake kwani hayanihusu.

Mama alikua mkali kabisa, hataki kuongea na mimi, lakini niliona kama natakiwa kufanya kitu kwani wakati namuambia alitoka na kurudi nyumbani. Alikataa kabisa kusikiliza watu waliokua wanamuambia aondoke, yaani baada ya mimi kuongea na Bibi niliona Mama kama kawehuka hataki kusikia chochote zaidi ya kurudi kwa mume wake. Tulirudi ndani, wakati anapigwa Mama hakutoka na simu yake, zote mbili zilikua sebuleni, niliingia na kuziona, niliona simu dnogo na kupata wazo la kuchukua namba za pacha wake.

Nilitaka kumuambia kinachotokea nimuambie aje amchukua ndugu yake kwani wanamloga. Nilichukua simu yake na kwakua sikua na vocha niliitumia simu hiyo hiyo kumpigia, Mama alikua chumbani na mimi nilitoka nnje. Kwa bahati nzuri alipokea na nilianza kumuelezea, lakini kabla sijamaliza nilisikia kofi la sikioni, simu ikawa kama imeunganishwa na sikio, nilijikuta napata kizunguzungu.
“Unatembea na mume wangu, kwanini nunakazania sana mimi kuachika? Nimekuona upo katibu sanana na wifi yangu wewe ndiyo umeandaliwa uje kumzalia!”



“Hapana Mama watakuja kukuua!” Nilimuambia kwa hasira, simu ilishadondoka chini, aliiokota na kuanza kuongea na Kaka yake.
“Huyu mtoto ni mnafiki, anashirikiana na wifi yangu kutaka kuniondoa humu ndani, ni katoto kadogo lakini kana mdomo kama nini? Kanataka kuninyang’anya mume wangu!” Mama alillamika sana kwenyesimu, nilimuangalia na kusema kuwa hazikua akili zake.
“Hivi haoni anavyonyanyasika?” Nilijiuliza. “Najutaaa kuingilia mambo ya watu!” waliongea sana na Kaka yake amabeye alionyesha kumuelewa, baada ya kumaliza kuongea naye alinipa simu na kulazimisha niombe msmaaha kwa kudanganya.

Nikikumbuka kila kibao alichoonipiga nilinyanyuka na kuomba msamaha.
“NIkusikie tena ukiongea, utaondoka hapa na kama nikisikia umemuambia mume wangu au wakwe zangu kuwa umetangaza matatizo yangu ya ndoa kwa watu nitakuua. Hii ni ndoa yangu, kama ni kuvumilia navumilia mimi, najua mume wangu anakosea lakini kutangaza matatizo si suluhu. Mume wangu ananikasirikia na kunipiga kwakua sina mtoto siku nikipata mtoto atanipenda na hatanipiga tena.” Aliniambia kwa sauti ya ukali, nilitingisha kichwa kumkubalia na kumuonyesha kwamba nimeelewa.

“Njoo hapa mdogo wangu.” Aliniambia huku akitembea na kukaa kwenye benchi la kupumzikia pale nnje, alinishika na kunikalisha pembeni yake, aliniangalia usoni alipokua amenipiga kofi, akaanza kunifuta isha kuanza kunibembeleza.
“Samahani kwa kukupiga, ni hasira tu, najua ulifanya hivyo kwakua unanipenda lakini mwanangu ndoa ngumu, hujui tu, mume wangu naye anateseka, anataka mtoto, ukikua utajua, mwanamke sio ukipigwa tu kidogo unaondoka, kama kila mwanamke angekua anaondoka basi kusingekua na ndoa duniani.

Wanaume ndyo walivyo, wakati mwingine wanakua na hasira na wakati mwingine wanakua na upendo. Mimi naamini Baba yako ananipenda lakini ni hasira tu za kukosa mtoto, akipata mtoto nina uhakika hata nipiga tena. Natakiwa kuvumilia kwani akiniacha siwezi kupata mwanaume mwingine wakunivumilia. Umenielewa mdogo wangu?” Aliniuliza.
“Nimekuelewa dada…” Nilijibu kwa mkato, ingawa sikua nimeelewa lakini sikua na namna, aliongea kwa upole sana mpaka machozi yakaanza kumtoka, alikua anaumia, nilisahau hata maumivu yangu ya kofi na kuanza kumuonea huruma.

“Usije ukamuambia mtu mdogo wangu. Mama amepiga simu anakuja, Mama mkwe wangu ananipenda sana, amejua nimepigwa amekuja, usiwe unatangaza matatizo yangu, usiwe unaongea, akija wewe muambie tu ulikosea lakini hakuna kitu kibaya kimetokea.” Alinibembeleza, niliitikia kwa kichwa huku nikijuta kunyanyua mdomo wangu, nilikua namchukia sana Bibi na nilijua kabisa kuja yake haikua ya usalama, nilija lazima kuna kitu anakuja kufanya ambacho kingemdhuru Mama, lakini sikua na namna, ilikua ni lazima kukubabaliana na kila kitu ninachoambiwa kwani mimi pale nilikua ni mfanyakazi tu.

Sijui waliongea nini lakini Bibi alikuja, safari hii hakunishirikisha kwa chochote, hata haulala chumbani kwangu, alimchukua Baba na Mama na kwenda nao kwa Shangazi Mama Jamila. Walirudi usiku sana na kesho yake bibi aliondoka, hatukuongea chochote. Mama alionekana kuwa na furaha sana na Baba alionekana kuchangamka kama zamani, kisrani kiliondoka kwa muda, siku moja Baba aliwahi kurudi nyumbani, Mama alichelewa kidogo na kumkuta Baba kashafika, alikuja na kumsalimia lakini Baba hakuitika, alikua kanuna mpaka basi.

“Kuna nini? Mbona Baba yako kanuna hivyo?” Mama aliniuliza, alinifuata jikoni baada ya kuweka vitu vyake ndani. Mimi sikua na jibu sikua najua sababu ya Baba kukasirika.
“Nataka uache kazi, Biashara zangu zinakwama sana.” Baba hakusubiria hata chakula kije sebuleni, alimfuata Mama jikoni wakati tunapika chakula cha jioni.
“Niache kazi, kivipi wakati nina habari nzuri, Bosi wangu anahama, nikikomaa naweza kupandishwa cheo.” Mama aliongea lakini Baba alishaondoka, alikua kashafikia maamuzi yake na hakuonekana kuyumba.

Mama alimfuata nyuma na kumuelezea akimuomba abaki kazini lakini Baba hakuongea sana.
“Nimeshakuambia, nataka mtu wa kusimamia Biashara zangu, mama kaniambia nikuweke wewe. sasa ni maamuzi yako, uchague kati ya ndoa au kazi.” Baba alimaliza na kutoka kabisa ndani, usiku ule hakurudi nyumbani, nilijua kwakua Mama alikesha na mimi, alikua akinielezea mambo mengi kuhusu kazi, alikua akilalamika, alikua akipiga simu za Baba hazipatikani, Mama laichanganyikiwa, mpaka asubuhi wote hatukuweza kulala.

Wakati wote alikua akijaribu kunishawishi mimi ili nimuambie kuwa ni sawa kwake kuacha kazi, mimi sikuona kama ni sawa, niliona kama ni unyanyasaji tu. Baba alikua na Biashara na zilikua zinaendavizuri kweli lakini sikuona sababu ya Mama kuacha kazi. Siku ile ilikua siku ya kazi lakini Mama hakuenda kazini, nilimsahuri kwakua anapatana na Bibi basi ampigie simu na kumuambia aongee na Baba. Alimpigia lakini Bibi alikua na jibu moja tu.
“Msikiliza mume wako, acha kazi kwani unakosa nini mpaka kujihangaisha na vikazi?” Mama alibaki kimya, hakua na jibu zaidi ya kuaga na kukata simu.

Siku ile Baba hakurudi na kesho yake hakurudi pia. Kesho yake Mama alienda kazini kwake, akaandika barua ya kuacha kazi masaa 24, akarudi nyumbani, ni kama Baba alikua na mtu anamfuatilia Mama kwani baada ya kusikia kuwa ameacha kazi alirudi nyumbani. Alionekana kuwa na furaha sana, alimuambia Mama kuwa hawezi kumnyanyasa, alimuambia kwa anataka kumfungulia bishara na ni kama alishajiandaa kwani alimuonyesha Document Biashara zaote za Baba alishazibadilisha majina na kuweka majina ya Mama.

Mama alishangaa kwani si kitu alichokua amekitegemea, alijua kuwa akiambiwa kuacha kazi basi ndyo anakua Mama wa nyumbani lakini Baba hakutaka hivyo, alitaka Mama afanye Biashara na kila bishara isimamiwe na Mama. Niliiona furaha ya Mama kwani ingawa nilikua sijui kitu chochote kuhusiana na hivyo vitu lakini aliniletea, alinionyesha mamikataba, akanionyesha jinsi Biashara zilivyozake, alinielezea mambo mengi ambayo hata sikuyelewa, alifurahia sana kuacha kazi na kukabidhiwa Biashara za Baba.

Wasiwasi wangu mimi ilikua ni kwa Bibi, sikujua kama atakubaliana na Baba kumuandika Mama majina yake yote katika bishara zake. Kwa nilivyokua nikifahamu nikuwa Baba alikua hawezi kufanya kitu bila idhini ya Bibi, ni kama bado alikua mtoto mchanga ambaye anasubiria kuambiwa fanya kitu flani acha kitu flani. Kwa namna alivbyokua akizilinda mali za Baba nilijua kabisa hatakubali na kitazuka kizungumkuti. Lakini jambo la kushangaza nikuwa baada tu ya kuambiwa vile Bibi alipiga simu na kuanza kumpongeza Mama na kumuambia ashikilie kwani mali zile ni zake, hapo ndipo nilipata wasiwasi kidogo, kuna kitu kilikua hakiko sawa kabisa.

***

Mvua kubwa ilikua inanyesha, mama alichelewa kutoka dukani, Baba alishafika nyumbani na aliponiuliza kama Mama kafika nilimuambia hapana. Nilishangaa kwa swali lile kwani mara zote Baba humchukua Mama asubuhi, wakati anaenda kazini basi humuacha Mama dukani na akitoka humpitia, nilishangaa ni kwanini siku ile alikua hajampitia na alikua akiniuliza mimi.
“Mbona sijamuona dukani, au kuna sehemu kakuambia kuwa atapitia, maana na simu yake haipatikani?” Aliniuliza kwa wasiwasi.
“Hapana, hakuniambia kitu, mimi niliongea naye tu jioni akaniambia nipike chakula basi hajaniambia kitu kingine.”

Nilijibu kwa wasiwasi, nilimuona Baba akibadilika taratibu, hasira zilikua zinampanda lakini zilichanganyika na uoga. Tangu Bibi kuja na kwenda kuongea na Baba kule kwa Shangazi kila kitu kilikua kimebadilika, shangazi alikoma kabisa kukanyaga pale nyumbani. Ndugu wengine wa Baba nao walionekana kukerwa na kitendo cha Bbaa kumpa usimamizi wa mali zake Mama, walikasirika zaidi pale ambapo kila kitu aliandika jina la Mama, mara nyingi walikua wakiongea kwbamba atashindwa, wakisema Mama kamloga Kaka yao na maneno mengine kibao.

Lakini Baba hakujali na cha ajabu Bibi alikua upande wake na alionyesha kumpenda sana Mama. Ingawa wengine walizungumzia kuhusu mtoto lakini Bibi alisema ni mipango ya Mungu na kuwaambia kuwa hata yeye alipitia mateso ya mimba kutoka mpaka kufikia kuwazaa wao. Walinyamaza kwakua walikuwa wakimugopa na kumheshimu Bibi lakini kiukweli ile hali iliwekera na kwa namna flani walimtenga Bba. Biashara zake zilizidi kuchanua, akanunua magari, malori na kila kitu alindika jina la Mama hivyo walilazimuika kuja kujipendekeza kila walipokua na shida.

“Kaenda wapi huyu?” Baba aliuliza huku akichukua simu yake na ku[iga tena namba ya Mama, lakini ilikua haipatikani, alizunguka zunguka ndani ksha aakatoka ma mwamvuli, aliingia kwenye gari na kuzunguma mpaka saa nane usiku alirudi akiwa kachoka, Mama alikua haonekani, alishawapigia simu ndugu zake kuwaulizia, alipigia rafiki zake, alirudi na kuniuliza kama sijui kweli lakini sikua na jibu kabisa. Kwa hasira aliingia ndani kulala, aliniaga kuwa analala lakini haikuchukua hata dakika kumi, kuna watu walikuja na kugonga mlango.

Baba alitoka na kuongea nao, mimi sikusikia chochote lakini walikua wakimtajataja Mama, nilihisi kuna kitu lakini sikuweza kuuliza. Baba alitoka nao bila kujali mvua alitoka mpaka huko alikokua na baada ya kama nusu saa hivi alirudi na Mama. Sijui kilichokua kimetokea lakini alikua peke yaka, hakua na wale watu tena, Mama alikua kaloana, mwili umemjaa matope, alikua kama hajitambui.
“Nilikua nimevaa chupi lakini sasa hivi hakuna kitu.” Mama alikua anaongea, hakuongea maneno mengine zaidi ya hayo, alikua kama mwenda wazimu flani.

“Nyamaza bwana, kikubwa mzima, chupi kitu gani, unajidhalilsha tu!” Baba alimfokea, lakini Mama ni kama alikua hamsikii, aliendelea kusema maneno yale.
“Mpeleke bafuni kamsafishe…” Baba aliniambia, kwanza nilishtuka kuambiwa vile, kama Baba asingekuepo basi ningefanya hivyo bila shida lakini alikuepo na yule alikua ni mke wake.
“Lakini Baba….” Nilitaka kubisha kidogo, ila alinikata jicho mpaka nikakubali, Mama alikua kama zuzu, nilimpeleka bafuni, nimakvua nguo na kumkalihsa, lakini haikua nguo ya ndani tu, niliona Mama alikua kachanjwa kwenye mapaja, alikua kapigwa chale na zilikua zimepakwa dawa nyeusi. Pamoja na Mama kuola mvua nguo kujaa maji lakini mapaja yake yalikua makavu sana. Nilitaka kumuambia Baba lakini niliona aibu, nilinyamaza kimya na kumuogesha Mama kama mtoto.

“Wameondoka?” Mama aliniuliza, alionekana kama ana wasiwasi, kana kwamba kuna watu alikua akiwahofia.
“Akina nani?” Nilimuuliza.
“Wanataka kuniua, wameondoka na chupi yangu, naitaka chupi yangu, wanataka kuniua!” Mama aliendelea kuongea, nilimuuliza maswali mengi kumdodosa kama atasema ni akina nani hao lakini hakusema. Aliendelea kuuliza kitu kilekile, nilimsafisha na kumaliza, nilienda kuomgongea Baba chumbani kwake, nikamuomba nguo akanipa, nikampa Mama akazivaa mwenyewe, alivaa nguo zote na kumalizia na nguo ya ndani.

“Unafanya nini hapa? Huoni hapa ni chooni nahitaji privacy?” Aliniuliza kwa hasira, baada tu ya kuvaa chupi Mama alikua kama amepata akili zake, alinishangaa kwa kuwa pale chooni.
“Leo mvua ilikua kali, nilitoka na mwamvuli lakini huwezi amini kuwa nimeloana, yaani hata haujasaidia kitu chochote, Baba yako yuko wapi?” Nilimuambia yuko ndani kisha nikatoka, nilikutana na Baba sebuleni, aliniuliza kama anaendeleaje nikamuambia hali yake si nzuri naona kama hajielewi.
“Kwanini tusimpeleke hospitali?” Nilimuuliza Baba.
“Hospitali ya nini wakati mtu ni mzima, alidondoka tu wakati anatoka gizani akaangukia kichwa lakini yuko sawa, wasamaria wema walimsaidia.”

Baba alimaliza kuongea, wakati huo Mama naye alikua anatoka, walisalimiana kama vile hakuna kilichotokea. Baba alizuga kama vile alikua hajui.
“Umakuja saa ngapi?” Baba alimuuliza, nilimkata jicho Baba na kushangaa unafiki wake lakini hata hakujali. Waliongea ongea na Mama pale kisha Mama akarudi chumbani kupumzika, hakula chochote, ulikua ni usiku wa manene nilipanda kitandani na kulala lakini usingizi haukuja, nilikua naogopa na niliwaza kuondoka, mambo yaliyokua yanatokea katika ile nyumba yalikua ni ya ajabu ajabu sana. Nilipanga kuondoka kwani nilijua kuwa ipo siku hayo mambo yatanitokea na mimi, ile familia nilikua siielewi.

Lakini asubuhi nilikua kama napitiwa na kausingizi kidogo, mpaka saa mbili nilikua bado sijaamka, niliamshwa na kelele kuoka chumbani kwa Mama.
“Nini kimeoza humu ndani? Nini kimeoza humu ndani wwe mtoto?” Mama aliga kelele hukua kiniita, nilitoka mpaka sebuleni lakini sikufika mbali, kulikua na gharufu kali sana. Ilikua ni harufu ya kitu kilichooza, Mama aliongea hukua kitoka chumbani kwake. Ile kumuona tu nilishtuka, mama alikua kavaa nguo fupi ya kulalia kama kigauni hivi ambacho kiliacha sehemu kubwa ya mwili wake nnje.

Mapaja yalikua wazi na alikua akittembea kama anachechemea hivi, alikua kaipanua miguu anatembea kama anavuruta kitu.
“Hicho ni nini Mama?” Nilimuuliza huku nikimsogelea bila kujali ile harufu. Mama alishtuka na kuangalia chini, kama umewahi kuona mtu kajifungua au mnyama halafu konde la uzazi bado halijatoka na mtoto yuko chini ndiyo ilikua kwa Mama, sikujua ni lini alikua na ujauzito lakini Mama alikua kajifungua, katoto ambako kalikua kadogo keusi kama mkaa kalikua kanaburuzika chini na Mama alikua hajui, nilipomshitua ndiyo alishangaa kuona vile.



Mama alidondoka chini na kupoteza fahamu, mule ndani nilikua peke yangu, sikujua hata itu cha kufanya. Nilichukua simu yangu kumtafuta Baba lakini alikua hapatikani, nilitoka nnje kukimbia nakuita majirani, alikuja Mama mmoja ambaye alikua nyumba ya jirani, alikua ni mtu mzima hivi, sikua nikimfahamu, alikua ni mpita njia, nilimuambia kuwa Mama kajifungua na kadondoka chini kapoteza fahamu. Pamoja na uzee wake lakini baada ya kusikia hivyo alikimbia mpaka ndani, alimkuta Mama kalala chini.

Aliangalia mapigo ya moyo ya Mama,a kakaangalia katoto, hakakua katoto, kalikua kanaumbo la mtu lakini kalikua bado hakajakua.
“Huyu Mama ni wakuwahishwa hospitali, atakufa, nenda nnje kaite watu, atakufa humu ndani.” Aliniambia, nilitoka na kuita watu, kurudi yule mama alishamsafisha Mama na kumsiriri. Walimchukua na kumpeleka hospitali, huko walimhudumia na Mama alipata fahamu, mimi nilikua sijui chochote kuhusu mimba hivyo watu walivyokua wakiniuliza niliishia kubaki tu kimya.

Bado niliendelea kumpigia Baba simu lakini sikumpata, nilipata wazo la kujaribu mtu mwingine, nilimpigia Bibi ambaye alipokea, nilipomuambia tu alionekana kupaniki, hakua akijua kuwa Mama ni mjamzito, nilipomuambia kuwa mimba imetoka kitu cha kwanza aliachokiulizia ni katoto kako wapi! Nilimuambia kuwa mimi sijui, labda wamekachukua, alipaniki akiniambia nizunguke hospitali nzima kuulizia kuwa kako wapi.
“Nataka ukachukue!” Aliongea kwa kuchanganyikiwa.
“Ndiyo nataka ukachukue!” Alirudia tena, mimi nilimjibu sawa ingawa sikujua ni kwa namna gani ningeweza kukachukua.

Nilikata simu lakini sikuzunguka, baadaye Baba alinitafuta, aliniuliza tulipo akaja, hata yeye alikua hajui kama Mama ni mjamzito, alikasirika sana, naye kama Bibi alitaka kujua mwanae yuko wapi. Kwakua yeye alikua mtu mzima alionyeshwa na sikujua tena ni kitu gani kiliendelea kwani mpaka Mama anarudi nyumbani hakakuletwa nyumbani na wala sikuulizia. Aliporudi nyumbani ulizuka ugomvi mwingine, Baba alikua kakasirika kwanini hakumuambia kuwa ana mimba. Nikweli mama alineneapa sana lakini nilishindwa kuelewa ni kwanini Baba hakujua wakati walikua wakilala naye kitanda kimoja.

“Nilikua sitaki matangazo, huwezi kunyamaza, kila kitu ukisikia unaongea, kipindi kile nilikuambia kuwa nina mimba ukatangaza kwa kila mtu, niliona nizae kwanza ndiyo niongee.” Mama alimjibu, alionekana kuchoka na hakujali chochote, kwa namna alivyokua anaongea, namna alivyokuaa naonekana kukata tamaa Baba alinyamaza kimya. Hakumuongelesha na wala Bibi hakuja tena pale. Maisha yaliendelea, Mama alipata mimba nyingine tatu na zote zilitoka, moja ilitoka ikiwa na miezi nane, nyingine mbili watoto walifariki wakati anajifungua tena kwa oparesheni.

Kilichokua kinashangaza nikuwa, kalba ya kufanyiwa oparesheni mtoto alikua anacheza tumboni lakini wakifungua tumbo wakitoa mtoto ni maiti. Kwa upande wa Biashara zilikua zinaenda vizuri sana, Mama ndiyo aliendelea kusimamia ingawa matumizi ya pesa yalibaki kwa Baba. Mama alikua anasimamia biashar zote za Baba ila, kila akikusanya pesa nachukua Baba na ndiyo huamua zitumikeje, Mama hakua na uhuru wa kufanya chochote, maamuzi mengi ya mule ndani yalikua yakifanywa na Babu tena kupitia Bibi.

Suala la mtoto lilionekana kumuumiza Mama zaidi, kila siku alikua ni mtu wa kulia, alikua ni mtu wa maombi ingwa Baba alikua hapendi. Siku moja nakumbuka ilikua siku ya jimapili, Mama alikua kalala ndani, mmoja wa mshono wake ulikua umefumuka na ulikua unauma sana, Mama alikua na mishono minne ambayo alipasuliwa wakati wa kujifungua kwa watoto wote ambao walifariki. Pamoja na kuambiwa aache kuzaa kwa muda lakini alikataa, alikua anataka mtoto na hakujali kuhusu afya yake.

Mshono ulikua unatoa usaha, na tumbo lilikua inapanuka tu. Mwanzo hakuna aliyejua kilichokua kinaendelea, lakini jinsi hali ilivyokua inazizi kuwa mbaya Mama aliamua kuongea. Alimuambia Baba kuwa ana mimba ya miezi minne, kumbuka hapo alikua hata hajamaliza mwaka tangu kumpoteza mtoto wa nne ambaye naye alijifungua kwa oparesheni na alishakaa na mimba kwa miezi tisa mpaka siku ya mwisho mtoto akiwa hai. Baba alipaniki, alimlaumu kwa kubeba mimba, Mama alikua katika maumivu makali sana.

Pamoja na kuwa kwenye maumivu makali lakini Baba alijifanya kukasirika.
“Wewe si hutaki kuniambia mambo yako, si unaniona mimi mchawi sasa nakuacha hapa! Utakufa mwenyewe mshenzi mkubwa!” Baba aliongea na kutoka nnje kwa hasira. Mama alikua anazidi kupiga kelele akiomba msaada, nilimfuata na kumbembeleza lakini alikua katika maumivu, aliniomba nikaite watu ili wampeleke hospitali. Nilitoka harakaharaka kwenda nnje, lakini sikufika mbali, Baba alikua kasimama mbele yangu anaongea na simu kama analia.

“Mimi nilikua sijui Mama, siku hizi haniambii mambo yake!” Baba aliongea, nilijua kabisa anaongea na Bibi.
“Hapana sitaki mtoto, mimi nafanya tu, huyu mwanamke ananitegeshea mimba, mimi huwa sijui, mbona mimba nyingine mimi huwa nakuambiaga, kwanini nikufiche, sitaki mtoto.” Baba aliongea, walionekana kubishana sana na Bibi, ni kama Bibi alikua akimshutumu kuwa anataka mtoto hivyo kaamua kumdanganya kuwa hakujua kuwa Mama ana mimba. Nilisimama na kushindwa kutoka kwani sikutaka Baba kujua kuwa nimesikia mambo yao.

Nikijua kama ataendelea kutembea mbele labda atoke nnje kabisa ili nipate nafasi ya kuita watu Baba alisimama. Kabla sijafanya chochote ilisikika sauti kubwa kutoka ndani.
“Nisaidieni nakufaaa!” ilikua ni sauti kubwa sana ambayo ilitoka ndani, ni Mama alikua akipiga kelele. Nilimuona Baba akigeuza, alinipita kama vile hanioni na kuingia ndani.
“Anaweza kumfanyia kitu kibaya huyu!” Niliwaza, nilishaanza kumuogopa Baba kwani wakati mwanzo nilikua nikihisi labda Baba hajui mambo Bibi anayofanya zamu hii niliona hapana, anajua ndiyo maana alikua anaongea naye vile.

“Anaweza kumuua!” Niliwaza na kukimbilia kwenda ndani, tulifika wote pamoja, tulimkuta Mama shatembea mpaka sebuleni, alikua kashikilia kisu mkononi nguvu zimamuishia. Tumboni alionekana anatoa damu.
“Mungu wangu!” Nilipiga kelele baada ya kumuona Mama katika hali ile, huwezi amini Mama alikua kachukua kisu na alikua akijipasua tumbo kutaka kumtoa mtoto. Baba alimnyanyua lakini alikua kachoka sana, alikua kalegea hivyo kuwa mzito. Aliniambia nimsaidie kumnyanyua, nilimshika na tukamnyanyua kumpeleka kwenye gari.

“Hataki kutoka, mtoto hataki kutoka…” Mama aliongea kwa suti ya chini wakati tunambeba. Tulimuingiza kwenye gari na Baba akaanza kuendesha kuelekea hospitali, mimi nilikua nimemshikilia mama, nilikua nimechukua khanga na kuibania tumboni kwake, nimemshikilia kwa nguvu kwani alikua anajirusharuha akilalamika kuwa anataka kumtoa mototo. Hospitalini walimpokea na kumpatia huduma ya kwanza. Aligundulika kuwa ana ujauzito wa miezi minne na kwa mara nyingine Baba alikua hajui.

Baada ya kupatiwa huduma ya kwanza Baba alikaa vizuri. Wakati wote huo nilikua na simu ya Mama niliichukua wakati namsaidia, wakati anahudumiwa simu yake iliita. Alikua ni Pacha wake na Mama, mimi nilipokea na kumuambia kuhusu Mama.
“Hivi huyu ana matatizo gani? Kwanini anang’ang’ania sana hiyo ndoa, kama imeshindikana si aondoke!” Alifoka na kukata simu, kama nusu saa hivi alikuja na mke wake, Baba alishangaa kumuona pale, mara nyingi walikua wakificha magonjwa ya Mama, hata Mama mwenyewe alikua akificha na ndugu zake walikua wanakuja kugundua baadaye ashatoka na hospitalini.

Walisalimiana kinafiki kwani kila mtu alikua akimchukia mwenzake, Pacha wa Mama aliingia ndani kumuangalia Mama mimi nikabaki nnje na mke wake ambaye alijaribu kunidodosa mambo mengi ila sikusema chochote. Sikutaka kuingilia ndoa yao, Pacha wa Mama alikaa kwa muda wa kama nusu saa akaondoka, nahisi ni kama walikorofishana na Mama huko ndani kwani alitoka kwa hasira, hata mke wake alipotaka kwenda kumuona Mama alimkatalia na kumuambia waache watajuana wenyewe mimi nimechoka na huyu mtu.

Waliondoka na kutuacha pale, mama alikaa hospitalini kwa wiki mbili, walisema anahitaji uangaliazi maalum kwani mimba yake inaathri mshono amabo ulikua haujapona vizuri. Siku anapata nafuu nakutoka hospitalini tulishangaa tunamkuta Bibi nyumbani, alikua hajasema kuwa anakuja lakini baada ya kumuona Mama alimuambia kuwa atoe ile mimba, Mama alikataa, waligombana sana Bibi akijifanya kuwa anajali afya yake lakini mama alikataa na kusema atazaa hata kama nikufa afe lakini atazaa.

Baba bila hata ya kuuliza sababu alikaa upande wa Bibi na kumshinikiza atoe ila mimba, kilikua kimbembe, waligombana na kugombana lakini mama alikataa, alimuamba baba kama anamuacha amuache lakini hawezi kutoa ile mimba. Kwa hasira Baba aliondoka na Bibi, hawakurudi usiku wote huo.
“Najua nitakufa, hii ndiyo mimba yangu ya mwisho, nisipopfanikiwa kupata mtoto sitabeba tena mimba, nafunga na kizazi, kama nikufa nikimzaa nife tu. Mama aliniambia, alionekana kukata tamaa ya maisha lakini hakuonekana kukata tamaa ya ile mimba.

“Wifi mna nini na Mama?” Aziza alimuuliza Mama. Tangu Mama kukabidhiwa Biashara za Baba karibu kila ndugu wa Baba alikua kama mamtenga, hata Aziza aambaye mwanzo walikua marafiki alimchukia, nilishangaa siku ile kuja pale tena usiku. Mama kama kawaida yake hakua na kinyongo alimsikiliza.
“Kwanini mimi sina tatizo naye, nikwakua wanataka tu nitoe hii mimba ila siwezi.” Mama aliongea.
“Siongei kuhusu hii mimba, kuna mambo yanatokea, unajua kuna meseji nimeziona kwenye simu ya Mama nikashangaa, sijui kuna tatizo gani kati yenu, naomba tu uziangalie.” Aliongea huku akitoa simu yake, alionyesha picha za mesejia lizokua kapiga katika simu ya Mama, ni meseji ambazo Mama alikua akimtumia Baba.

“Nimehangaika sana lakini huyu mtoto atapona, wewe ndiyo umekosea, hii mimba haitoki kabisa, na huyo mwanamke akizaa utakwisha.”
“Lakini mama muda wwa mimba zake kutoka Bado, si kama zile nyngine, huyu mtoto hatazaliwa.” Baba alimjibu kwa meseji.
“Hapana, hunielewei, nakuambia kuwa nimehangaika kila nikiangalia inaonekana kama huyu mwanamke atazaa safari hii, nakuambia tu kuwa haisha hatoki hospitali, mpe hata dawa na hata kama ni sumu ya kuua mtoto mpe lakini akizaa tumekwisha, ni mimi na wewe hatakiwi kuzaa.” Meseji ilisomeka.
“Sawa Mama nitajitahidi lakini hata kulala halali sijui nitafanya nini?” Baba alimjibu.

Mbali na hizi meseji Aziza alimuonyesha na picha nyingine, zilikua ni picha za Baba na mwanamke mwingine, walikua katika nyumba kubwa tu, Baba kabeba mtoto mdogo na kulikua na kitoto kingine cha kiume kimesimama pembeni yake. Alionyesha picha nyingi nyingi ambazo zilimuonyesha Baba ni kama ana familia nyingine, mwanamke mwingine na watoto na alikua akifurahia maisha.
“Wewe umezitoa wapi hizi?” Mama alimuuliza, alikua kapaniki, naona kakasirika.
“Kwenye simu ya Mama, nimeziona jana, mimi mwenyewe sikuamini lakini kuna maneno walikua wakiongea Mama na Kaka, nahisi Mama yangu ni mchawi!”

Aziza aliongea huku machozi yakimtoka, wakati huo Aziza ndiyo alikua kaolewa na ndoa yake ilikua ina mwaka mmoja, naye alikua badi hajapata mtoto.
“Kwanini unsasema hivyo, yaani kwasababu ya hizi picha tu?” Mama alimuuliza, ni kama alikua hamuamini.
“Hapana wifi, kuna vitu vingi, siwezi kukuambia yote lakini sina aimani na Mama yangu, kuna watu tangu zamani walikua wanasema hivyo lakini sikuwaamini kwakua ni Mama yangu. lakini jana Mama baada ya kuondoka huku kwako kaka alimleta kwangu, kama unavyojua kuwa Mama hapatani na Mama Jamila na yote ni sababu yako, alikua akimuambia kuwa anamloga Kaka ili akuache na kwakua mali zote zina majina yako.

Lakini mimi siamini kama mali zina majina yako, naona kama wewe ni chambo tu, Baba anaonekana anatumia nyota yako na wewe kuzaa ni tatizo. Kuna maneno Mama alikua ananiambia jana nilishtuka ndiyo nikaamua kushika simu yake. Mama yangu nahisi mchawi na wewe ndiyo unatumika.”
“Mimi sikuamini, wewe utakua umetumwa, kwanini useme Mama yako ni mchawi, kwani Kaka yako kuwa na mtoto nnje ya ndoa ni shida, mbona wanaume wengi wanakua nao, najua hamnipendi lakini siwezi kuachana na mume wangu kwaajili yenu, kweni wewe una mtoto.”
“Hapana wifi lakini…”

“Lakini nini? Au na wewe Mama yako kakuloga?” Mama hakuonekana kuamini kua kalogwa, alikua na kama hasira flani hivi.
“Mimi naona uondoke, najua mnachokitaka wewe na ndugu zako lakini hamtakipata, mume wangu hawezi kuniloga na hii mimba anataka nitoe kwakua ananipenda anaogopa nitakufa kwasababu ya mishono, asingekua hanipendi angeniacha nife, tena na hii mimba nitatoa basi ili kumridhisha!” Mama aliongea kwa hasira.



“Wewe hujaona kitu kibaya chochote hapa?” Aziza aliniuliza. Mama alikataa katakata kumuamini, aliona kama vile anataka kumharibia ndoa yake, kila wakati alikua akimtetea Baba kuwa hawezi kumfanyia mambo yaliokua yakisemwa.
“Hapana, sijaona!” Nilikua najua kila kitu, nilitaka kumuambia lakini nilishikwa na uoga.
“Ngoja tutaona, hawawezi kumuua huyu mtoto tena, ni Mama yangu lakini kwa alichonifanyia siwezi kumsamehe na Kaka kashakua zezeta hachomoi kwa Mama!” Aliongea kwa hasira, alirudi chumbani kwa Mama na kujaribu kuongea naye lakini hakumsikiliza, alimfukuza na kumuambia akahangaike na ndoa yake.

“Nitarudi, ila mdogo wangu naomba, kama kuna kitu chochote kitatokea naomba uniambia, wewe ni mwanamke, hujaolewa bado ila ukiolewa utajua thamani ya ndoa, bosi wako anateseka lakini hajijui bado najua yote hayo ni Mama, alishajaribu kwangu akashindwa.” Aliongea taratibu lakini kwa uchungu sana, alinipa laki moja na nusu na kuniambia kuwa ni ya vocha.
“Najua watarudi, kuna vitu wameenda kuvifanya ila havitafanikiwa, kama wanajiona wao ni wajanja basi mimi ni mjanja zaidi!” shangazi alikua akilengwa lengwa na machozi, nilimuonea huruma kwani ilionekana dhahiri kuwa kuna kitu kibaya ambacho Mama yake kamfanyia, na kwa nilivyokuwa namfahamu Bibi nilijua ni kitu kikubwa.

“Kwani kuna nini, mbona unahuzuni hivyo?” Nilimuuliza, lakini hakuonekana kuwa tayari kuniambia, aliondoka na kuniambia kuwa nimuangalie Mama kwani nikizubaa huyo mtoto hawezi kumzaa.
“Kwanini usiongee na Kaka, yake, Mama anamsikiliza sana, anaweza kukubali kuondoka.” Nilimuambia.
“Nimeshajaribu, unafikiri mpaka kuja hapa sijajaribu, nimehangaika kila kitu lakini naye anasema ashamchoka atajua mwenyewe. Wewe ndiyo wakusaidia, kama kweli unampenda basi hakikisha kuwa unamlinda, mimi nitahangaika kivyangu lakini na wewe hangaika.” Aliniambia nakuondoka, aliondoka kama mtu mwenye haraka kama kuna kitu alikua anakiwahi.

Baba alirudi peke yake usiku, alikua kakasirika, hakurudi na Bibi, aliingia ndani bila kusalimia mtu. Aliingia chumbani, sijui kwanini lakini nilijihisi kama natakiwa kwenda kuchungulia na kuona jkinachoendelea. Nilisikia Mama akimsalimia lakini hakuitikia.
“Mdogo wako alikuja hapa, kuna maneno kaongea mimi sijayapenda, hivi lakini kwanini familia yako inanifanyia chokochoko namna hii, kama mnaugomvi wenu si mmalize wenyewe kwanini kuniingiza mimi.” Mama aliongea, Baba hakujibu chichote, mimi bado nilikua mlangoni nasikiliza.

“Anasema Mama yako ni mchawi eti ndiyo hataki tupate watoto na kanionyesha na picha kabisa kuwa wewe una watoto wengine huko….” Mama aliendelea kuongea, lakini hata hakumalizia.
“Mshenzi wewe, kwanini unamuita Mama yangu mchawi…” Alimgeuzia kibao, Mama alijaribu kujitetea lakini Baba alimrukia, nilisikia tu mangumi, Mama Kipiga kelele, huku Baba naye akimtukana.
“Na nakuambia sitaki mtoto na wewe mshenzi kabisa, kama Mama yangu mchawi basi na mimi mchawi, kwanini uzae na wachawi, kwanini usikae tu, unakosa nini hapa mpaka unataka kuzaa, nishakuambia huwezi kuzaa, tangu upate hii mimba mambo yangu yamesimama, biahsra zangu zimesimama kabisa, hii lazima utoe! Sisi si wachawi kwanini uzae na wachawi!”

Baba alimpiga sana, Mama alikua akilalamika usinipige tumboni utaniulia mwanangu, utaniulia mwanangu lakini Baba ni kama alikua anataka kumtoa mimba kwa kipigo kwani alikua anapiga hukohuko, nilishindwa kuvumilia, nilitaka kuingia lakini mlango ulifungwa kwa ndani. Nilipata wazo la kumpigia shangazi Aziza, nilipompigia tu aliniambia kuwa nikate simu nitoke nnje niite majirani yeye anakuja n a Polisi. Nilitoka na kuita watu, walikuja na kuvinja mlango kwani Baba hakufungua pamoja na kusikia wakigonga, aliendelea kumpiga Mama, watu walipofungua walimkamata Baba wakamfunga Kamba.

Alikua kama mtu aliyechjanganyikiwa, Mama alikua kapigwa sana, mishono imepasuka na madamu yametapakaa.
“Mke wangu anataka kuniua! Mke wangu anataka kuniua! Mke wangu anataka kuniua!” Baba alipiga kelele, kwa kumuangalia Mama nilijua kuwa asingepona, alikua kaumia sana, alikua bado anapumua lakini alikua kaharibika, alikua kama mtu aliyemwagiwa damu, hatamaniki kavimba kila sehemu. Watu walitaka kumpiga Baba lakini Polisi walifika na kumuokoa, Shangazi Aziza ndiyo aliwapigia na kuja kumchukua, walimchukua Mama na kumpeleka hospitalini, shangazi yeye alikuja baadaye, aliongozana na Mama mpaka hospitalini mimi nilibaki tu ndani na wasiwasi wangu.

Hakuna mtu aliyeniambia kitu chochote mpaka asubuhi yake, Baba alirudi nyumbani baada ya kulala mahabusu kwa siku moja. Nilishangaa lakini sikusema chochote. Kwa kumuangalia tu nilikua naogopa, kwa kawaida mambo kama hayo yakitokea Bibi alikua ananipigia simu, lakini siku ila hakunipigia mpaka asubuhi kwahiyo sikua najua chochote na sikua najua ni kwa namna gani Baba alitoka. Aliingia ndani na kubadilisha ngu alitoka kama vile hakuna kitu kimetokea, bado roho ilikua juu sielewei elewi nini kimetokea. Baada ya hapo aliondoka huku akiniaga kuwa anaenda hospitalini kumuangalia Mama.

Niliogopa kwa kweli, nikidhani labda Bibi kajua kuwa mimi ndiyo nilipeleka umbea kwa Aziza na kumuambia kuwa Baba anampiga Mama niliona siwezi kuendelea kuishi tena katika ile nyumba kwani hata mimi wanaweza kuniua. Nilichukua simu yangu nakumpigia Aziza, nikamuambia kuwa Baba katoka, haya yeye alishangaa lakini mwisho alisema.
“Pesa imeongea, hii nchi hii unaweza ukaua na usisemeshwe chochote! Ndiyo maana wanawake wngi hawapendi kwenda Polisi kwani hata hawasaidii chochote!” Nilimuuliza kuhusu hali ya Mama akaniambia kuwa anaendelea vizuri, alipoteza damu nyingi sana lakini Mungu ni mkubwa na mtoto atazaliwa.

“Muache aje hospitalini, atapambana na mimi, huyu mtoto atazaliwa, nife mimi au afe Mama lakini tutapambana, atazaliwa na kama ni hizo mali zitaisha washenzi wakubwa hawa!” Aliniuliza kama Bibi ashanipigia simu nikakuambia hapana, aliniambia niwe makini kwani si mtu mzuri. Nilimuambia kuwa nataka kuondoka akaniambia hapana, nisiondoke mpaka Mama atoke hospitalini kwani anataka kujua mipango yao yote.
“Lakini wanaweza kunidhuru?”
“Hapana, mama yangu ni shetani lakini hawezi kukugusa, wewe si ndiyo ulitoa damu ya hedhi mkamlisha wifi yangu, hawezi kukugusa na wewe hutaondoka. Anajua kitakachomtokea kama akikuguza.”

Nilishtuka kidogo nidondoke, nilikua nimesimama nikakaa chini, kile kitu nilikua sijamuambia mtu yeyote, nilishangaa alijulia wapi, simu kiodgo idondoke.
“Najua kila kitu mdogo wangu, hata wewe si akili zako, nikikuambia kuw ahuyu mtoto atazaliwa basi naamaanisha, labda nife mimi lakini huyu mtoto atazaliwa.” Nilinyamaza na kuitikia kila kitu alichoniambia, nilikua naogopa sana, nilianza kumuogoppa Aziza kuliko hata nilivyokua namuogopa Mama, sikujua ni namna gani alijua kitu ambacho nilikifanya na Mama yake zaidi ya miaka mitano nyuma, nilikua sijamuambia mtu yeyote na nilijua Bibi hawezi kusema.

Baa tu ya Aziza kukata simu Bibia linipigia simu, aliniuliza kilichotokea, ilionekana kuwa hata yeye alikua hajui kitu.
“Ni shangazi gani huyo amabye anasema mimi ni mchawi?” Aliniuliza, mimi nilikaa kimya.
“Najua ni Mama jamila, yeye ndiyo ana mambo ya kishiurikina, hivi unajua kuwa anahangaika sana ili mdogo wake kumuacha mke wake lakini kashindwa. mimi si mchawi lakini nalinda ndoa ya mwanangu!” Bibi alanza kubwabwaja, alianza kuropoka mambo ambayo mengi nilikua siyajui, akiamini kuwa Mama jamila ndiyo anamuita mchawi aliniambia kila kitu.

Kumbe kipindi kile ambacho mimba ya Mama ilitoka na Baba akaanza kumchukia Mama, Mama Jamila alienda kwa mganga akidhani kuwa Mama kamloga Baba, alikua anataka waachane na alipokuja aliwawekea dawa chumbani ili tu waachane. Wao walijua kuwa Mama ni mchawi na kamteka ndugu yao ndiyo maana hataki kumuacha, waliona kuwa hana mtoto naye lakini mali zote kamuandika yeye, waligombana sana na Mama yao kuhusu hiyo ishu.
“Mjukuu wangu najua kakujaza maneno, mimi na wewe tumefanya mengi lakini si kwaajili ya kuloga bali kulinda hiyo ndoa. Mali zote unazoona hapo zinatokana na Mama yako, yeye ndiyo mwenye nyota, akimuacha anafilisika. Mwanangu anaweza kuzaa na mwanamke yeyote yule lakini si mke wake wa ndoa, akitaka kuwa na mali lazima wasizae.”

Bibi alinambia, aliniambia mambo mengi ambayo yaliniogopesha, mwisho alimalizia.
“Nimekuambia kila kitu kwakua sitaki uondoke, wewe ndiyo unajua siri znagu hivyo hapo ni kwako, hutaondoka kamwe, utabaki hapo hapo, najua huyo Mama Jamila kakuambia mambo mengi mabaya lakini hajui chochote, hajui ni kwa namna gani Kaka yao kajitolea kwaajili yao. Maisha mazuri yote wanayoishi nikwakua Kaka yao kajitolea. Mimi mwenyewe niliteseka sana katika ndoa yangu mpaka kupata mtoto, nilitoa sadaka nyingi sana lakini unaona sasa hivi niko wapi naishi vizuri na wote walionicheka ndiyo wanakuja kwangu kuomba misaada!”

Bibi alingea kana kwamba kitu alichokua ananiambia kilikua ni kitu kizuri sana, niliogopa sana, nilikua natetemeka nilishindwa hata chakumjibu. Familia nzima ilikua haieleweki, Aziza alikua anaongea kama anajua kila kitu yaani kama na yeye ni Mganga, Mama Jamila naye kumbe alikua akihangika kuloga ili kuvuruga ndoa ya Kaka yake huku Mama yao akiwa ndiyo mchawi hasa na alionekana kama hajali kabisa. Ingawa nilikua naogopa lakini sikutaka tena kuendelea kukaa kwenye ile nyumba, wote niliwaona wachawi na nilihisi ipo siku yatakuja kunikuta.

Pesa zangu za mshaahara alikua akiniwekea Mama, lakini kwakua nilikua na vipesa vingi nakusanya sikuzihitaji, niliona uhai wangu ni bora zaidi, sikutaka kumuambia mtu kuwa naondoka, nilijua kuwa kama wakifahamu naondoka watanizuia, kwanza nilikua naogopa sana, hata wakati nakusanya nguo zangu na kuzipaka kwenye mabegi nilikua naogopa nahisi labda wana ngu flani zakujua niko wapi. Nilimpigia simu rafiki yangu na kumuambia nimefukuzwa kazi hivyo nataka kwenda kwake kulala siku moja kabla ya kurudi kwetu, sikutaka kuendelea tena kulala katika ile nyumba niliona maruweruwe.

“Umefumaniwa na bosi nini? Sema Bosi wako handsome, hata mimi ningelala naye?” Alinitania.
“Nitakuambia nikija huko. Mimi siwezi kutembea na Bosi wangu…” Nilimjibu nakukata simu, lakini ile nageuka tu Baba alikua kasimama pembeni yangu. Nilishangaa ni kwanini aliingia chumbani kwangu, kwa zaidi ya miaka sita ambayo nilikua nimekaa kwenye ile nyumba Baba alikua hajawahi kuingia chumbani kwangu.
“Kwanini huwezi kulala na mimi? Mimi nina kasoro gani?” Aliniuliza, alionekana kuwa na mawazo sana yaliyochanganyika na hasira.

“Hakuna sio wewe…” Nilijiteteea.
“Sio mimi, ina maana una Bosi mwingine?”
“Hapana, Baba, sina ila….”
“Ila nini, kwanini hunipendi? Unaona kama wewe ni mzuri sana, akwakua nakuheshimu ndiyo maana unaona kuwa mimi siwezi kitu….” Aliongea maneno mengi ambayo yalikua hayaeleweki, ghafla alibadilika na kuacha kunizungumzia mimi akawa analalamika kuhusu Mama, anasema kuwa hajui alipo, kaenda hospitalini hajui, aliniuliza nikamuambia kuwa sijui.

“Sasa mbona unapaki mabegi? Ndiyo wamekuambia kuwa uendea kufanya kazi huko au unaenda wapi?” Aliniuliza, nilikua sina jibu la kumpa, hasira zilimpanda zaidi akalalamika kuwa mimi napanga na dada zake kuvunja ndoa yake. Nilimuambia kuwa mimi sijui chochote akawa anasema kuwa kwanini sasa nataka kuondoka naenda wapi jioni ile na mabegi. Nilishindwa kumjibu, nikiwa sina hili na lile, baba alinivamia na kunikumbatia, alikua ananuka sana pombe, nilitaka kumsukuma lakini alinizidi nguvu, hakunipiga, alinidondosha chini na kunibana kwa nguvu huku akinivua nguo na yeye kuvua nguo zake, wakati anafanya hivyo mimi nikimsukuma yeye bado alikua akimtaja mke wake akisema ndugu zake wanataka kumuua.



“Sasa mbona umefanya mapenzi na mimi?” Nilimuuliza Baba baada ya kumaliza, pamoja na kwamba alinilazimishia lakini nilifurahi, haikua mara yangu ya kwanza kufanya mapenzi, wakati huo nakumbuka nilikua na miaka kama 22 hivi na Baba alikua ni mwanaume wangu wa tatu.
“Kwani hupendi? Hujafurahia?” Aliniuliza kimtego.
“Mimi sijapenda, wewe si umenilazimishia…” Nilimuambia kwa aibu, bado nilikua uchi, nilikua sijavaa nguo, alikua akianiangalia, kichwani kuna kama kitu kilikua kinaniambia mume huyu hapa, Sabra, umasikini wako wote unaishia hapa leo.

“Mbona kama umependa?” Aliogea huku akiisogeza mikono yake kushika kifuani kwangu,alinikamata kwenye chichu na kuanza kunitekenya, nilipata msisimko wa ajabu na kujikuta napiga kelel.
“Lakini baba wewe una mke wako, upo na Mama na unampenda sana….” Nilipiga kelele huku niiuachia mwili wangu na kumuacha afanya enachotaka, Baba ni kama alijua kuwa nataka, alikua akinipasha moto kasha ananiachia, yaani ananipa raha huku ananiacha, alinitesa sana.

“Huy mke wangu mchawi sana, simtaki tena, najua mambo amabyo wananifanyia. Anashirikiana na Mama jamila kutaka kuniua, wanataka mali zangu lakini hawatazipata, mimi nimetoka mbali, wamanisingizia mambo mengi mimi na Mama yangu…” Aliongea, waati mkono wake mmoja ukiwa kifuani mwingine ulishuka chini na kuanza kunitekenya. Pamoja na kwamba nilishawahi kufanya mapenzi lakini nilikua nikifanya na watoto, sikupata raha kama zile. Wakati anakuja mara ya kwanza a likua akijilazimishia kwangu, alikua hajaniandaa, nilimuona kama Baba anayetaka kunibaka, lakini sasa kil kitu kilibadilika.

Nilimuona kama mwanaume ambaye anataka kunishughulikia, kwa namna alivyokua akinishika basi mwili mzima ulilegea.
“Unanipenda kweli?” Nilijikuta na muuliza. Aliniangalia na kutabasamu, kasha akanivamia na kunidondosha kitandani.
“Kwanini unauliza hivyo, kwani nilishawahi kukufanyia kitu chochote kibaya?” Alikua akiniongeleshea sikkioni kwangu, sauti ilipenya huku akiwa kama anang’atang’ata sikio langu.
“Hapana, lakini unampenda sana Mama, mimi naogopa, akija akijua kama nimetembea na wewe ataniua.”
“Akija wapi, si amsema anazaa, mimi sitaki mtoto, kama anazaa mimi hawezi kurudi kwangu. Yule mwanamke hanipendi, hivi unafikiri kama angekua ananipenda angeniepeleka Polisi kweli?”

Aliongea kwa hasira kidogo, nilijua kabisa kaumizwa na kitendo cha Polisi, nilinyamaza kwani nilijua kuwa Mama siye alishitaki na mimi ndiyo nilimpigia shangazi Aziza na kumuambia kasha akaenda Polisi. Ili kumaliza ile mada, sikutaka anidodose tena, nilimvutia kwnagu tukaendelea kufanya mapenzi, sasa nilifurahia zaidi kwani nilijiandaa kumpokea. Baada ya kumaliza alitoka bila kuongea chochote, hakuniamba nibaki au niondoke, nilibaki nikiangalia mabegi yangu nikijiuliza kama niondoke aau la? Akili ilikua haifanyi kazi vizuri, mara simu ya yule rafiki yangu ambaye nilikua naenda kwake iliita.

Alikua ananiulizia kama naenda au la? Umbea ulikua umenibana nilishindwa kuvumilia na kumuambia kilichotokea.
“Lakini wewe si umeniambia kuwa ni wachawi?” Aliniuliza, ni kama alinizindua usingizini.
“Hapana, sidhani kama Baba ni mchawi, Mama yake najua lakini huyu Baba ni mstaarabu sana, hata kama anafanya nadhani ni kwakulazimishwa!” NIlijikuta naongea kwa suti ya juu kidopgo, yaani kwa raha zote nilizokua nimepata mtu anataka kuniaharibia.
“Kua makini, kwahiyo huji tena?” Aliniuliza.
“Niko makini, nitakuja lakini ngoja niangalie kwenza, anaweza kunipa pesa nyingi, mtu ahsanitumia, akinipa pesa nyingi naondoka kuanza maisha yangu.

Siwezi kukubali kubaki hapa kwani sitaki kupitia mateso aliyopitia yule Mama. Hapana, lakini ngoja nibakimbaki siku mbili kuangalia kama atanipa pes aya kueleweka. Hii familia inasambaratika, Mama akirudi kutoka hospitalini mimi naondoka.” Nilimuambia, kichwani nilikua namaanisha kuwa naondoka kweli, hali ya mule ndani ilikua si ya mchezo, nilishajua tabia zao zote hivyo sikutaka kubaki kuteseka. Nilikua nimechoka sana, sikua nimepika lakini nilirudi kitandani na kulala fofofo.

Nilikuja kushtuka usiku, Baba ndiyo aliniamsha, alikuja chumbani kwangu na kunikuta nimelala kama nilivyozaliwa. Alinifunika na kuwasha taa kisha akaniamsha.
“Uwe unajifaunika ukialala…” Aliniambia, nilishtuka kwa aibu, namna alivyiniambia na alivyokua akiniangalia ni kama alikua hanitaki, si kama alivyoua ananiangalia mwanzo.
“Wamekuambia kitu gani? Ni nani alileta umbea hapa nyumbani?” Aliniuliza baad aya kuamka, nilijifunga funga shuka ili kujistiri, hakua akiniangalia tena kama mwanzoni, alianza kuniangalia kama mtoto wake na si kama mpenzi wake.

“Mimi sijui kwani mimi nimesema nini?” Sikuelewa alikua anataka kujibiwa nini.
“Nani alimuambia Mama yako kuhusu mambo ya mimi kuwa na familia nyingine. Mama Jamila nimeenda kuongea naye anaonekana hata hajui chochote, kuna mtu kaleta umbea, ni yeye ananidanganya au kuna mtu mwingine.”
“Shangazi Azizaa alikuja, yeye ndiyo alimuambia Mama kila kitu, Mama Jamila hajaja hapa muda mrefu. Anasema mama anamloga na wewe unajua, eti ni kwasababu ya mali…” Nilijikuta namuambia kila kitu, ni kama nilikua namchongea ili ajue mabaya yao, kwa namna nilivyokua naongea ni kama alikua anasingiziwa na mimi nilikua nikimkumbusha wabaya wake.

“Wewe unaamini nini? Unaniona mimi mchawi?” Aliniuliza, nilijikuta natetemeka tetemeka mdomo sijui hata chakumjibu.
“Unaamini mimi naweza kumloga mke wangu kwaajili ya mali, hivi ukiona ninavyohjangaika kutafuta dawa. Mama yangu amekua akihangaika usiku na mchana, kila mtu kijijini anamuita mchawi kwaajili yangu. Wangejua namna ambavyo Mama yangu alihangaika ili nipate mtoto na mke wangu wasingesema chochote, mama kateseka sana lakini naona kila mtu kamgeuka. Kijijini kote wanmuita mchawi kwa kuhangaika kwa waganga kila siku, mimi mwenyewe kuna kipindi nilidhani Mama yangu ananiloga, lakini nilivyojua ukweli nilinyamaza.

Mke wangu kalogwa, hawezi kupata mtoto mpaka baadhi ya mambo yafanyike, nilikua namuambia atoe hii mimba kwakua si mimba wkeli. Hivi ni mimba gani mtu anakaa mpaka anafikia kujifungua lakini mimi mume wake sijui, kweli. Mimba zote za mke wangu ni mimba za nguvu za giza, mke wangu ana majini ndiyo maana hawezi kuzaa kwani hakuna binadamu amabye anaweza kuzaa jinni. Mama anahangaika kila siku ili kubadilisha hiyo hali lakini si ndugu wala mke wangu anayekubali, ile mimba inatakiwa kutoka la sivyo mke wangu atakufa, sitaki kumuona mke wangu akifa.”

Baba alionge huku akilia kama mtoto, alionyesha kuwa na uchungu sana, kwa namna alivyokua anaongea nilijikuta hata namuamini, nilijikuta namuonea hutuma na kuamini kuwa labda mambo yote aliyokua akiyafanya Bibi nikwakua alikua anampenda Mama.
“Sabra…” Aliniita, lakini sasa kwa sauti ya mahaba.
“Mimi siwezi kukudanganya, nina watoto watatu, sina shida ya mtoto bali najua mke wangu anaahitaji mtoto kwa hali na mali, ndiyo maana nahangaika. Hivi unaona mali zote nimemuandika yeye, unafikiri kwanini?” Aliniuliza, nilitinisha kichwa kuashiria kuwa nilikua sijui sababu ya yeye ufanya hivyo.

“Ndugu zangu wanampiga vitra ten asana, najua nikifa hama kila kitu wanamnyang’anya, sitaki ateseke kisa hatuna mtoto. Unamuona Karim, si kaoa, unaona siku hizi haongei na mimi unajua kwanini?” Aliniuliza.
“Hapana, sijui…”
“Basi nitakuambia, wewe ushakua kama familia, alikuja na kuniambia kuwa nimuache mke wangu. Alikua ananiambia mambo mengi kuwa mke wangu anahamishia mali zangu kwa ndugu zake, alinionyesha vitu vingi sana. Lakini siku mbili baaddaye nikakuta meseji anamtongoza mke wangu, anamuambia mke wangu kuwa hawezi kuwa na mtoto na mimi kwakua mimi mbegu zangu hazina nguvu ndiyo maana wtoto wanafia tumboni.

Alikua akimuambia kuwa kama anataka mtoto basi azae naye kisa yeye ana mtoto. Wote hawajui kama nina watoto wengine, nina familia, Mama yangu pekee ndiyo anajua. Mama jamila ndiyo usiseme, naamini uchawi wake ulishauona, kipindi kile akanifanya mpaka nampiga mke wangu. Asingekua Mama ningekua jela leo, lengo lake lilikua mimi kumpiga na kumuua Mke wangu ili nifungwe kwakua sina watoto basi mali ziwe zao. Aziza pekee ndiyo nilikua namuona wamaaana lakini naona naye kaingia huo mkumbo mpaka anamuita Mama yangu mchawi.” Aliniambia, Baba alikua anaongea kwa uchungu mpaka nilimuonea huruma, alikua akiongea huku akilia kama mtoto.

Sijui kwanini lakini nilijikuta namuamini na kumuonea ruhuma, lakini mwisho aliniudhi kwani aliniambia kuwa atapambana kuhakikisha kuwa anamrudisha mke wake. Hapo ndipo alinikera, sijui kwanini lakini nilijikuta napandwa na hasira na kutamani hata kuamuambia amuache lakini niliona niaharibu.
“Usijali Baba mimi nitakua hapa kukusaidia na sitamuambia mtu yeyote kuhusu mahusiano yetu…” Nilimbembeleza huku nikimsogelea, lakini kitu cha ajabu nikuwa hakutaka nimguse.
“Mahusiano gani? Mimi nina mahusiano na wewe! Hembu ondoka na ukome kabisa, wewe ni mtoto mdogo sana mimi kuwa na mahusiano nawe. Mimi ni mtu mzima na akili zangu, hivi unafikiri watu wakijua natembea na House Girl italeta picha gani.

Nafasi yako hapa ni Dada wa kazi tu hakuna kitu kingine, naomba uniheshimua na sitaki unyanyue mdomontena kuongea mambo ya mapenzi. Nimetembea na wewe mara moja tu kwakua nilikua na mawazo, haitajirudia tena na kamwe usijekuhisi hata kama naupenda!|” liongea kwa hasira, alinyanyuka na kutoka chumbani kwangu. Nilimuangalia kwa uchungu wakati anatoak, hasira zilinipanda, kwa namana livyokua ananiambia matatizo yake nilihisi ananiona kama binadamu mwenzake kumbe alikua akiniona kama dada wa kazi tu.

Nikikumbuka mamboa ambyo alinifanyia cmhaan wake nilipatwa na hasira zaidi. Nilikaa chumbani nikilia huku nikijilaza, sikutaka na wala sikupata hata tone la usingizi mpaka asubuhi. Sikumuona Baba kwa siku mbili zote nilibaki na maumivu yangu. Hakuna mtu ambaye alinipigia simu, ni kama walikua wamenisahau na mimi sikutaka kuwapigia, hata Bibi shoga yangu naye hakunipigia, nilikua naogopa lakini sikuondoka. Baba alishatembea na mimi na nilianza kujihisi kama vile ananipenda.

Jioni ya siku ya pili Shangazi Aziza alinipigia simu, aliniambia kuwa Mama anaerudi nyumbani, amegoma kabisa kuchana na Baba hivyo anatakiwa kumlinda. Nilijifanya kama vile nataka kuondoka kwani naogopa hali ya mule ndani lakini alinisihi kuvumilia kwani kama nikiondoka wanaweza kumfanyia Mama vitu vibaya.
“Huyo mtoto anatakiwa kuzaliwa, kwa hali na mali anatakiwa kuzaliwa. Kuna nguvu kubwa za giza zinamzunguka na Mama yangu ndiyo chanzo, najua wifi hawezi kuelewa lakini mimi najua kwani na mimi nimehangaika, hata mimi natafuta mtoto na kila ninapoenda naambiwa Mama yangu ndityo katrufunga.”

Aliniambia, nilitaka kujua zaidi lakini alikataa kuniambia kila kitu.
“Kwsasa jua tu kuwa nakuhitaji ten asana. Mama yangu anakuamini sana, ushenzi wote mlioufanmya pamoja naujua hivyo wewe hawezi kukudhuru, hawezi kukugusa kabisa kwani anajua akikugusa nayeye anaondoka.” Alinaimbia, maneno yake yalinitisha kwani ni kama alikua ananiona na mimi ni mchawi, sikumuelewa kabisa alikua anamaanisha nini, nilimbembeleza aniambie lakini hakutaka.
“Nitakupa laki tatu kwa mwezi kwa kukaa hapo na kuhakikisha huyo mtoto anazaliwa.” Aliniambia, sikutaka kufikiria mara mbili, mimi mwenyewe nilikua sitaki kuondoka nilishaanza kumpenda Baba na nilitaka kubaki kwaajili ya kulinda penzi lake.

Baada ya kumkubalia alikua na amani akakata simu, sekunde chache tu baada ya Aziza kukata simu Bibi naye alinipigia simu.
“Nimesikia mambo yaliyotokea, ningekua nimekuja lakini afya yangu si njema, nataka uwe jicho langu hapo.” Aliniambia, nilimuambia kuwa nishachoka kwani naona mauza uza tu, nataka kuondoka huku njikidanganya kuwa namuogopa Aziza anaweza kunifanyia kitu kibaya.
“Hawezi, wewe ni kama mwanangu, nakulinda, najua kuwa wana mauchwai yao lakini hawataweza. Mimi nakuambia kuwa baki kwaajili ya Mama yako, wanataka kumuua na hiyo mimba si mimba, huo ni upepo tu ambao wewe ukiondoka basi atakufa.

Hakuna mtu mwingine ambaye namuamini zaidi yako, wewe ndiyo mtu8 pekee ambaye unaweza kunisaidia, nitakupa mshahara hata mara kumi lakini baki hapo, Mama yako anakuamini sana hivyo baki.”
“Lakini namuogopa sana Baba, siku hizi amekua na hasira sana, anaweza kunifanyia mambo mabaya…” Nilijilalamisha.
“Huna kitu cha kuogopa mwanangu, Baba yako nammudu mimi, nitamuambia akuongezee mshahara na hatakufanya chochote. Wanamfanyia madawa ndiyo maana anakua na hasira sana lakini yeye ni mtu mwema.” Aliniambia, nilikubali huku nikijua nia yake ni mimi kuhakikisha kuwa mimba ya Mama inatoka.




Kila mtu alikua akiniambia lakwake na kila mmoja alikua na nia yake, wakati Bibi alitaka mtoto asizaliwa Shangazi Aziza alitaka mtoto azaliwe. Mimi nilikua nampenda baba, ingawa nilijua fika kuwa kama akizaa na Mama dawa za Bibi zitaisha nguvu na wanaweza waachane lakini kweli sikutaka kabisa azae, nilimuonea wivu na kila siku nilijisemea kuwa kama ni mtoto basi mimi nitakua wakwanza kumpa Baba mtoto. Nilifahamu fika ana watoto wengine lakini kwakua walikua hawajulikani sikuwaona kama watoto.

Nilikubaliana na wote lakini nia yangu ilikua kuhakikisha kuwa mimba ya Mama inatoka na namteka Baba mpapa anamuacha Mama.
“Nitakua Dada wa kazi mpaka lini?” Nilijiuliza, baada ya Baba kufanya mapenzi na mimi nilihiusi alikua ananipenda kwa muda mrefu lakini tatizo alikua ni Mama.
“Huyu Mbwa ndio anazuia riziki yangu, Baba akikosa mwaname atakuja kwangu tu.” Nilijisemea huku nikiapa kuwa nafanya juu chini kuhakikisha Mama anaondoka mule ndani. Niliamua kujifanya mjinga kwa muda ili tu kumuondoa pale.

Ingawa Baba alimkataza lakini Shangazi alikua anakuja mara kwa mara pale nyumbani, alikua anakuja kumuona Mama, nilijifanya kumfurahia lakinia kiondoka nilimgeuka, nilijua nia yake kuwa anataka mtoto kuzaliwa, mimi sikutaka kabisa mtoto azaliwa, lakini pamoja na kutokutaka sikua na ujasiri wa kumuua. Kwangu hiyo ilikua ni dhambi kubwa sana.
“Kuna hizi dawa nataka uwe unamchanganya Mama yako kwenye chakula, mimi nikimpa hatachukua.” Shangazi aliniambia, nilizipokea kishingo upande.
“Ni dawa za nini?” Nilimuuliza.
“Za mtoto, wewe mpe tu, hakikisha unamuwekea kila siku.” Alijibu kwa kifupi lakini hakutoa maelezo yoyote.

Nilizipokea kishongo upande lakini sikumpa Mama. “Mimi siamini mambo ya kishirikina.” Nilisema, lakini Baba naye kila wiki alikua akienda kwa Bibi, alikua anakuja na dawa zake naye pia alikua akinipa nimuwekee Mama kwenye chakula. Nazo nilizipokea, nikijua nia yake niliamua kujitoa kwa wote. “Sitaki kuingilia kazi ya Mungu.” Nilijiambia, niliamua kuacha kumpa Mama dawa ya aina yotyote, wakati kila mmoja akidhani natoa dawa niliamua kumuachia Mungu kila kitu, sikutaka Mama azae lakini pia sikutaka damu ya mtu mikononi mwanagu.

Mpaka miezi tisa inafika Bibi alijua kuwa Mama anakunywa dawa, tofauti na kipindi kingine amabpo ikikaribia Mam kujifungua huja dar kipindi hiki hakuja. Mwanzo sikujua kwanini lakini ukweli nikuwa Bibi alikua anaumwa sana. Nakumbuka siku moja usiku alinipigia simu. Mama alikua hospitalini ameenda kujifungua. Baba ndiyo alimpeleka mimi nilibaki nyumbani.
“Hukumpa zile dawa….” Aliniambia baada tu ya kusalimiana. Nilibisha na kumuambia kuwa nimempa kama alivyoniagiza.
“Kama umempa mbona mimi siponi?” Aliniuliza, kwanza ilikua ni mara yangu ya kwanza kusikia kama Bibi anaumwa.

“He! Bibi unaumwa, mbona mimi sijasikia.” Alitulia kidogo kama mtua nayewaza kitu, alikua anapumua kwa nguvu kama mtu aliyekua akikimbizwa.
“Umeniua…umeniua…mtoto atazaliwa, mtotoa mezaliwa…nimekwisha….” Aliongea na simu ilikata, sikumsikia tena Bibi akiongea, nilikata simu na kupiga tena lakini haikupokelewa, nilipiga sana iliita bila kupokelewa. Nilipatwa na wasiwasi na kuamua kumpigia simu Baba ili kumuambia.
“Mama yako kajifungua mtoto wakiume…” Baba aliongea na kukata simu, hakutaka hata nimuambie sababu ya mimi kupiga simu.

Kabla hata sijafanya chochote simu yangu iliita, alikua ni Shangazi ambaye alikua na furaha sana, sijui ni nani almimuambia lakini aali ilinishukuru na kuniambia nina zawadi yangu Mama kajifungua. Tena alikua kajifungua kwa jia ya kawaida kabisa na hakupatabtatizo lolote. Rohoni nilifurahi kwakua nilikua nikimuonea huruma Mama lakini kuna kitu kilinipa hasira kwani niliamini kuwa baada ya Mama kupata mtoto basi ndiyo itakua mwisho wangu pale ndani.

“Siwezi kukaa kumlea mtoto wa mwanamke mwenzangu!” Nilijiongelesha kwa hasira, suiku ule sikupata usingizi kabisa, kila nikijaribu kulala nilikua nikikumbuka siku ambayo Baba alinishika na kufanya mapenzi na mimi.
“Kwanini hakurudia? Mimi nina kasoro gani? Hivi kwanini hata haniangalii kama mpenzi wake?” Nilijiuliza hata sikupata majibu, mpaka asubuhi hata sikukumbuka kama Bibi alidondoka au alifanya nini huko aliko. Asubuhi ilichelewa sana kufika lakini ilifika, nilifanya shughuli zangu kama kawaida lakni kivivu vivu.

Kwenye saa nne hivi Baba lirudi, nilimuuliza kuhusu Mama aliniambia anaendelea vizuri na kashatoka hospitalini.”MBona sasa hauko naye?” Nilimuuliza.
“Maswali gani hayo yakuniuliza, wewe ni kama nani?” Alijibu kwa hasira mpaka niliogopa, nilitaka kujua kilicoendelea lakini niliogopa kuuliza tena.
“Hata kama na wewe unataka kuondoka basi ondoka, naweza kuishi mwenyewe, naweza kuishi pekle yangu! Kwanza nina familia yangu, ondokeni wote, mimi si ni mchawi, ondokeni.” Alijiongelea mwenyewe kwa hasira, niliogopa kumjibu na kubaki kimya.

“Unataka kuondoka? Unataka kuondoka? Sema kama unataka kuondoka nikufukuze?|” Baba aliuliza hukua kinifuata, alikua kama vile anataka kunipiga, alinishika shingoni kama ananikaba, alinibana mpak nikakosa pumzi.
“Hapa…ana …hapaaa…na mimi sitaki kuondoka, mimi sitaki kuondoka…nakupenda sitaki kuondoka…” Niliropoka kwa shida.
“Unanipenda? Unanipenda? Nyie si ndiyo mnakaa na kuniita mchawi, nyie si ndiyo mnaniona mchawi, wewe si nilikupa dawa umpe Mama yako ulimpa kweli? Sasa mbona kazaa, unafikiri mimi nitaishije, maliz angfu zitapotea zote, utaendelea bado kunipend au utapenda tu pesa zangu?”

Aliniuliza kwa hasira, kwa namna alivyonikaba niliishiwa pumzi, nilishindwa kuongea naye hakujali. Aliendelea kunikaba, niklkidhani kuwa labda anataka kuniua kwani pumzi zilishasisha kabs aalishusha mkono wake mpaka chini ya kiuno na kuanza kunichezea sehemu zangu za siri, mkono wa juu alilegeza, nikapata pumzi kidogo, shingo ilikua na maumivu makali lakini yalichanganyika na raha za kushikwa. Baba alinishika na kunivutia ndani tukaanza kufanya mapenzi. Tulisahau kila kitu hata sikuuliza ni kitu gani kilikua kimetokea.

***

Baada tu ya Mama kujifungua ni kama alizunduka, nasikia waligombana na Baba hosptalini, akimuita mchawi, ni kama aliona kila kitu akili yake ilirudi, alitukana sana na palepale kwa hasira Babaa limuandikia talaka tatu wakaachana wakiwa hospitalini. Wakati Baba anarudi walishaachana na Mama alichukuliw ana dnugu zake na kwenda kuishi na pacha wake. Nilipopata hizo habari nilifurahi, lakini furaha haikudumu sana kwani Bibi aliua anumwa sana na wiki moja baadaye tulienda kumzika.

Ndugu wote walikutana kule lakini kwa namna walivyokua wakiangaliana ni kama waliua maadui. Baada ya mazishi mimi na Baba tulirudi mjini. Nikiamini kuwa labda ni nafasi yangu mimi kuchukuliwa na Baba na kuanza kuishi naye kama mke na mume, Baba alienda na kuchukua familia yake, alimchukua mwanamke wake mwingine ambaye kumbe tayari walishafunga ndoa na kuanza kuishi naye, kila mtu alishangaa kumbe ana watoto lakini alikua akiwaficha.

Kwa upande wa Mama baada ya kupewa talaka hakuchukua chochote, mali zote zilikua kwa majina yake lakini alimkabidhi Baba akimuambia hataki vitu vilivyopatikana kwa njia haramu. Niliumia sana kuona kuwa Baba alikua amechukua mwanamke mwingine na sio mimi.
“Nafasi yangu hapa ni nini?” NIlimuuliza Baba, ilikua ni usiku wa manane, Baba alitoka chumbani kwake na kuja chumbani kwangu, alimuacha Mama Mpya na kuja kufanya mapenzi na mimi.
“Nafasi kivipi, kwani kuna nini?”
“Si hivi, kila siku unakuja chumbani kwangu kw akuvizia, una mke wako lakini hufanyi naye mapenzi unakuja kwangu, mimi ni kama nani kwako?”

Niliuuliza kwa hasira, alibaki aanawaza nikajua anatafuta uongo wa kuniambia.
“Hata mimio nina hisia, nakupenda nataka kujua nafasi yangu kwako?” Nilimuuliza.
“Wewe ni mpenzi wangu, nakupenda na itaendelea kuwa hivyo.” Alijibu, nilijua ananidanganya kwani alikua akinificha, hakutaka kuwa karibu na mimi, nyakati za mchana nilikua ni dada wa kazi ila usiku nilikua ndiyo mpenzi wake.
“Sasa kwanini unanificha, kwanini hutaki kunionyesha kwa mke wakeo, mimi nataka ndoa wote sisi ni waislamu tunaweza kuoana.” Nilimuambia, kama kawaida yake aliniambia nimpe mdua atafakari lakini hakufanya chochoite.

Hali ile ilinitia hasira, Mama ampya alikua na kisirani, kwanza alikua hanitaki kwakua niliwahi kufanya kazi na Mke wa kwanza wa Baba alijua bado tunawasiliana naye, alitaka nondoke lakini Baba alimgomea mimi kuondoka. Tulikua tunagombana sana mpaka kufikia kutukanana lakini alipotaka kunifukuza Baba alinikingia kifua.
“Umenikuta hapa na utaniacha, kama ni kuzaa hata mimi kizazi ninacho ila sijaamua tu.” Sikumoja nilimuambia kwa hasiira, aliniangalia kwa hasira kisha akacheka.
“Mdogo wangu si kila mwenye kizazi anazaa, uzae kwa ki[pi, hiyo mimba labda unywee kwenye uji, mume wangu anajielewa hawezi kuzaa na kinyongorokota kama wewe mpmbavu mkubwa, hata kukutamani hakutamani!”

“Hanitamani? Una uhakka na hilo?” Nilimuuliza kwa hasira, niliona ananipanda kichwani hivyo nilitaka kumkomesha na kumuonyesha kuwa na mimi ni mwanamke na mume wake ananiona na kunitamani kama mwanamke.
“Nina uhakika ten asana! Hawezi hata kukutamani!”
“Hivi usiku unalalaje wewe mbwa? Huoni kama wewe ni mke wa mchana mimi ni wa usiku, tangu uje hapa mwanaume hataki kukugusa kila sikua analalamika kuwa unanuka unafikiri analala wapi?” Nilimuuliza kwa dharau, nilimuona kabisa anaywea, alinyamaza kimya hakuongea chochote. Nilitoka na kumuacha ndani, usiku kama kawaida Baba alikuja chumbani kwangu, lakini kabla hatujfanya chochote mlango uligongwa.

Alikua ni Mama, alikua akipiga kelele kuwa Baba afungue mlango. Baba kwa hasira alifungua mlango na kumuuliza anataka nini? Akitegemea kwamba labda mimi ndiyo nitapigwa na kufukuzwa niliona Baba akimtandika makofi na kumuambia kuwa asimfuatilie fuatilia. Alilia sana na kutrishia kuondoka, Baba aliingia chumbani na kuchukua noti kadahaa na kumpa.
“kama unataka kuondoka basi nauli hii hapa!” Alimuambia, kusema kweli hata mimi nilishangaa, sikujua kama Baba ananipenda kiasi hichon, niliona kama miujiza. Dada wa watui alinyamaza kimya na kurudi chumbani kwake, kwa bahati nzuri watoto walikua shule, wote walikua wakisoma bweni hivyo hawakusikia chochote,.

Asubuhi ya siku iliyokua inafuata nilitoka kama bosi, Mama aliniangalia wakati natoka namuangalia kama takataka, alitabasamu na kuniambia.
“Kama unadhani nitaondoka basi unajidanganya, hii ndoa sikuipata hivi hivi, niliihangaikia sasa kama unadhani nitaondoka kijinga kijinga basi nenda kajipange. Nilimtoa mke mkubwa na sasa ni zamu yako!” Alinitishia.
“Huna lolote, mimi anafahamu kila kitu na sababu ya Mama kuachika naijua, kawatishie hao hao wajinga wenzako!” Nilimuambia.
“Wajingaeee, sasa tuone kama hutavaa pedi mwaka mzima tuone akija huko chumbani kwako mtafanya naye mapenzi kwa namna gani?” Aliniambia, nilijua ni vitisho vyake nilimtukana na kurudi zangu ndani.

Lakin haikuchukua muda, tumbo lilianza kuuma ten asana, likikua linakata sana, sikujua sababu lakini nilijikuta naloana, ilikua ni damu ha heshi, nilishangaa kwani ndiyo kwanza nilikua nina siku tano tangu kumaliza siku zangu. Nilipaniki kidogo, lakini kabla sijafanya chochote mlango wa chumbani kwangu ulifungulia.
“Wewe bado ni mtoto mdogo, najua umedanganywa ukaambiwa kuna ndoa, ondoka acha kushindana na watu ambao huwawezi. Hii familia huiwezi mdogo wangu, mimi naijua vizuri, usidhani hawa watoto nimewapata kwa kwenda msikitini, ondoka sina tatizo na wewe!” Mama aliniambia na kutoka akiniacha nimeduwaaa



Mwnzo nilikua kiburi, nilikua sitaki kuondoka kabisa katika ile nyumba, nilijisafisha vizuri na Baba alikua upande wangu, alipoona natoa harufu sehemu za siri aliniletea dawa moja ya kupaka, nilipaka na baada ya siku mbili harufu ilikata.

“Huyu Binti niliachiwa na Mama yangu, hawezi kuondoka, kama unataka ondoka wewe lakini huyu ni mfanyakazi niliachiwa na Mama yangu, ataendelea kubaki hapa!” Baba alimuambia, sasa alikua hachepuki kwa kificho tena, alikua anakuja chumbani kwangu hata mchana tena mbele ya Mama, ni kama alikua anafanya hivyo ili kumuuliza mke wake.

Nilijisikia raha sana kuona Baba ananipenda kuliko Mama, nilijiona kuwa mimi nina umuhimu zaidi, nilianza dharau na Baba alianza kunipeleka dukani. Wakati huo Biashara zilikua haziendi vizuri, tangu Mama kuondoka Baba Biashara zilikua zishaanza kuyumba, mauzo yalikua hayapo na Baba alianza kuuza vitu vingi vingi.

“Wewe una kismet kaa hapa dukani…” Aliniambia.
“Unaona jinsi ninavyokupenda, niekutoa kufanya kazi za ndani nimekuleta hapa, hili duka ni kama lako wewe kaa hapa uza na ukitaka chochote nunua, asikusemeshe mtu.” Aliniambia, nilijisikia vizuri, ingawa duka halikua kubwa sana kama kipindi Mama yupo lakini kwangu lilikua kubwa, nilikua nashika pesa nyingi sana ambazo katika maisha yangu nilikua sijawahi kuzishika.

Baba aliniweka karibu sana, mke wake alikua hamruhusu kabisa kufika dukani, kila kitu alifanya na mimi na alipolalamika ilikua ni vipigo.
“Hivi kwanini wanawake wengine hamjiongezi? Hivi kuzaa na mwanaume ndiyo unahangaika hivi? Mwnaume hakutaki lakini una mng’ang’ania mpaka basi?” Nilijiongelesha siku moja, nakumbuka ilikua siku ya jumapili, wote tulikua nyumbani, Baba alikuja kutoka kwenye mizunguko yake, ilikua ni mchana kabisa, alinichukua sebuleni na kwenda na mimi chumbani, wakati Mama akiwa sebuleni Baba alifanya mapenzi na mimi.

Siku hiyo ilikua tofauti kidogo kwani alikua kama ananilazimishia, alikua kama mtu mwenye haraka kwani baada ya kumaliza hakuruhusu hata niguse, hakuongea na mtu mwingine yeyote, hakuongea chochote aliva nguo zake na kuondoka. Nilipotoka chumbani Mama ambaye mara nyingi akiniona na Baba alikua anakasirika basi siku hiyo alikua anacheka, nilikasirika ndipo nikaamua kumchana.

“Wewe unafikiri unapendwa, hivi una akili gani wewe? Kutoka kijijini ndiyo kunakufanya mshamba namna hiyo? Yaani kabisa unakaa unadhani kuwa huyo mwanaume anakupenda? Hahahah! Ahahhaha!” Aliniuliza huku akicheka kwa dharau. Nilimuangalia kwa dharau na kuingia zangu ndani.

Nilikaa ndani kama nusu saa hivi, lakini kuna kama kitu kilikua hakija kaa sawa. Nilijihisi moyo mzito, kama unauma unaenda mbio. Nilishindwa kukaa ndani nikatoka mpaka sebuleni, Mama alikua sebuleni anaangalia TV.
“Vipi bado hujapigiwa simu?” Aliniuliza.

“Atanipigia tu, mimi ananipenda na taarifa yako nikitaka kuolewa naolewa hata kesho sembuse simu!” NIlimjibu kwa dharau, lakini nilikua naongea kwa shida, nilijiona kama nakosa pumzi nikakaa.

“Tulia binti, nimekuambia kuwa hii nyumba huiwezo, huiwezi kabisa, mimi mpaka kuingia hapa nimepitia mengi na siwezi kuondoka, kama mwenzako aliyekua analindwa na mizimu aliondoka sembuse wewe ambaye ni mweupe kabisa umetoka kijijini huna mbele wala nyuma?”

Nilitamani kumjibu lakini sikuweza, kabla sijaongea chochote simu yangu iliitya, niliichukua lakini nilikua mzito sana kupokea. Alianza kunisisitiza nipokee kwani ni simu kutoka kwetu, nilishangaa alijuaje kwani sikumuonyesha na ilikua ni namba na haikua na jina tu.

“Unashangaa nini? Mimi mwenyewe nimezika ndugu zangu sana mpaka kuja kuzalishwa, au unafikiri watu tumekuja kirahisi rahisi tu hapoa? Nimemzika Mama yangu mzazi nije kuondoka bila kitu, pokea simu Mama!”

Aliongea kwa dharau, ingawa sikumuelewa lakini niliogopa, nilihisi kuna kitu kibaya. Nilipokea simu na kukuta alikua ni Baba yangu mdogo, nilimsalimia ndipo akaniuliza kama Bosi wangu yupo.

“Baba anataka uniambie kweli, kuna nini? Mbona unaniulizia mambo ya Bosi wangu!? Nilianza kupiga kelele, alinisihi nimpe simu mtu mwingine, kabla hatujaelewana mama alichukua simu, aliiweka sikioni na kuseama.
“Tunajua kila kitu wewe sema ni nani kafa? Ni Mama yake au baba yake, wewe sema?” Aliuliza kwa hasira, alikaa kimya kama dakika mbili hivi kisha akakata simu na kuiweka chini.

“Nini? Nani? Baba anasemaje?” Nilimuuliza kwa uoga, aliniangalia tena kwa dharau kisha akasema.
“Washamuua mdogo wako, wewe kaa utulie ndani, yeye ataenda kuzika na wewe utabaki hapa unalinda mali zake! Mkijua kutumia basi mjue na kuzitafuta!”

Aliongea kama vile kilikua ni kitu cha kawaida, nilikua na wadogo zangu watatu, wawili wakike na mmoja pacha wangu Dotto ambaye nilikua namsomesha chuo. Baada ya mimi kushindwa kuendelea na masomo na kuanza kazi za ndani niliona ili kuikomboa familia yetu ni lazima yeye asome, kwanza alikua na akili, alikua mtu wa kufaulu kila siku, pili alikua ndiyo mkubwa wakiume, mimi nina dada zangu wengine ambao nao hawakusoma wameoelwa tu hivyo nilijua kuwa Sudi (si jina lake halisi) akisoma ndiyo atakuja kuiokoa familia.

Nilimuuliza alikua anamaanisha nini ndipo akaniambia kuwa Pacha wangu kafariki dunia, alidondoka ghafla asubuhi akiwa chuoni na kupelekwa hospitalini ambapo alifia huko. Nilidondoka na kuzimia, nlikuja kuzindiuka baadaye nikajikuta nipo kitandani. Baba alikuepo na aliniambia kuwa nipumzike nisiende kumzika ndugu yangu. Sijui kwanini lakini nilijikuta nacheka, nilimuangalia na kumuona kama mtu aliyechanganyikiwa, alianza kuniambia kuwa hali yangu ni mbaya, siwezi kwenda na kuongea maneno mengine mengi lakini sikumuelewa.

Nilipobisha sana alijifanya kukasirika na kuanza kunipiga akiniambia siwezi kuondoka.
“Wewe huoni kama Biashara zangu zinakufa! Nimekuambia kuwa baki humu, hutaondoka na kama ukiondoka huwezi kurudi tena humu ndani!” Aliongea huku akitoka na kufunga mlango kwa nnje. Hakurudi mpaka usiku, yeye alikua ashajiandaa anataka kwenda kwenye msiba wa ndugu yangu huku mimi akiniacha nyumbani. Sikua na namna nikubali kishongo upande. Aliondoka na kuniacha na mke wake, amabye alikua kama anachekelea.

“Huo ndiyo mwanzo tu, atawamaliza ndugu zako wote na hutapata chochote.” Aliniambia.
“Najua ni wivu unataka tu kubaki kwenye hii ndoa, mwanaume hakupendi.” Nilimuambia kwa hasira, ingawa niliona kama ni ukweli lakini sikutaka kukubali mbele yake.
“Mimi alianza kumua Mama yangu, akamuua na mdogo wangu ndipo nikazaa naye.” Aliniambia.
“Sasa kwanini huondoki kama unajua kuwa huyu ni mchawi?”
“Nilichelewa, nimejua tayari ashanizalisha na ndugu zangu ashawamaliza, lakini sasa hivi hawezi kunifanya chochote, kinachoniweka hapa nikuhakikisha kuwa nachukua kila senti yake na kumuacha, sipo hapa kwaajili ya mapenzi, hana mapenzi huyu mtu. Mwanaume ambaye alikua anaua watoto wake kwaajili ya mali unafikiri anaweza kupenda mtu.

Wewe unafikiri ni kwanini yule mwanamke hakuondoka na chochote, kwakua anajua kua hakuna mali ya halali hapa. Haendi kwenu kwenye msiba bali anaenda kuondoka na nguo ya marehemu. Nilijua kuwa mume wangu ni mchawi baada ya kuona nguo za ndani za marehemu Mama yangu na mdogo wangu chumbani kwake. Nilipomuuliza alionakana kama amechanganyikiwa, hapo ndipo alinioa, tena ni juzi tu baada ya mke wake kumuacha na Mama yake kufariki ndiyo nimekuja kugunuda ushenzi wake. Mimi hanigusu tena nishajidhatiti!”

Aliniambia, niliogopa kidogo lakini niliona kama ni stori flani, niliona kama vile ananitania aua annitisha ili niondoke na kumuacha mwanaume ambaye ananipenda.

“Wewe ulijuaje kuwa ni nguo za ndugu zako kama zingekua za wengine.” Kila nguo ilikua na jina, tarehe ya kifo na sbaabu za kifo, vilikua vimebandikwa vinaonekana. Niliogopa kidogo lakini sikumuonyesha.

“Kama huamini akirudi kagua bei lake, usipoona nguo yoyote ya ndugu yako basi mimi naondoka hapa.” Aliniambia, sikutaka kubishana naye kwani nilikua katika machungu makubwa, nilikua naumia kuhusiana na kifo cha mdogo wangu.

Niliamua tu kukaa kimya, ndugu zangu walinipigia simu kunipa pole kwani Baba aliwaambia kuwa baada ya kupata taarifa za msiba nilidondoka, nimezimia na hali yangu ni mbaya hospitalini. Nilishangaa kwani pamoja na kuzimia lakini hali yangu ilikua nzuri, nilipokea pole na kusubiria arudi. Haukaa sana msibani, alirudi kesho yake, sikumuuliza chochote, aliingia chumbani kwake, akabadilisha nguo nakutoka. Alipotoka nilinyata na kuingia chumbani kwake kukagua, chumba alichokua akilala yeye kilikua cha peke yake.

Pamoja na kuoa lakini walikua hawalali kitanda kimoja na Mama, alkua anajitenga na muda mwingi usikua likua chumbani kwangu. Alikua kafunga chumba chake na ufunguo, lakini nilikumbuka sehemu ambayo wanaweka ufunguo wa ziada kipindi Mama yule mwingine yupo, nilienda kuchukua na kufungua. Nilikagua kwenye begi lake, nilikuta nguo mbili za ndani, moja ilikua ya kike na nyingine ya kiume. Yakiume iliandikwa jina la Pacha wangu, sababu za kifo na tarehe ya kifo. Ile ya pili ilikua na jina la Mdogo wangu mwingine.

Hiyo ilikua na kikaratasi ambacho kiliandikwa jina lake, tarahe ya kuzaliwa na wakaandika tarehe ya kufariki wakaweka deshi deshi. Mwanzo nilihisi kama utani, nilihisi labda huyu Mama ndiyo kaandika, lakini wakati naakagua nilipitiwa Baba akaja na kunikuta, alipaniki kuniona pale, alikasirika na kuanza kunipiga akiniambia kwanini nakagua vitu vyake. Mimi niliishia tu kumshutumu kuwa ameniulia ndugu zangu, alinipiga sana na kunifungia ndani, alinifungia usiku mzima mpaka asubuhi ndiyo alikuja na kuniomba msamaha.

Kwa namna alivyokua anaongea ni kama kulikua hakuna kitu kikubwa kilichokua kimetokea. Aliombe msamaha wakunipiga lakini si wa kumuua mdogo wangu. Aliomba sana na kuniambia anataka kunioa, anataka kufunga ndoa na mimi, alibembeleza akinishawishi kuwa nikikubali kuolewa basi nitapata kila kitu chake, mali zote zitakua katika majina yangu, aliongea maneno mengi, alilia kama mtoto, huku akisisitizia kuwa hakupanga kunipiga bali ni shetani tu alimsukuma kufanya hivyo ila bado ananipenda.



Mwnzo nilikua kiburi, nilikua sitaki kuondoka kabisa katika ile nyumba, nilijisafisha vizuri na Baba alikua upande wangu, alipoona natoa harufu sehemu za siri aliniletea dawa moja ya kupaka, nilipaka na baada ya siku mbili harufu ilikata.

“Huyu Binti niliachiwa na Mama yangu, hawezi kuondoka, kama unataka ondoka wewe lakini huyu ni mfanyakazi niliachiwa na Mama yangu, ataendelea kubaki hapa!” Baba alimuambia, sasa alikua hachepuki kwa kificho tena, alikua anakuja chumbani kwangu hata mchana tena mbele ya Mama, ni kama alikua anafanya hivyo ili kumuuliza mke wake.

Nilijisikia raha sana kuona Baba ananipenda kuliko Mama, nilijiona kuwa mimi nina umuhimu zaidi, nilianza dharau na Baba alianza kunipeleka dukani. Wakati huo Biashara zilikua haziendi vizuri, tangu Mama kuondoka Baba Biashara zilikua zishaanza kuyumba, mauzo yalikua hayapo na Baba alianza kuuza vitu vingi vingi.

“Wewe una kismet kaa hapa dukani…” Aliniambia.
“Unaona jinsi ninavyokupenda, niekutoa kufanya kazi za ndani nimekuleta hapa, hili duka ni kama lako wewe kaa hapa uza na ukitaka chochote nunua, asikusemeshe mtu.” Aliniambia, nilijisikia vizuri, ingawa duka halikua kubwa sana kama kipindi Mama yupo lakini kwangu lilikua kubwa, nilikua nashika pesa nyingi sana ambazo katika maisha yangu nilikua sijawahi kuzishika.

Baba aliniweka karibu sana, mke wake alikua hamruhusu kabisa kufika dukani, kila kitu alifanya na mimi na alipolalamika ilikua ni vipigo.
“Hivi kwanini wanawake wengine hamjiongezi? Hivi kuzaa na mwanaume ndiyo unahangaika hivi? Mwnaume hakutaki lakini una mng’ang’ania mpaka basi?” Nilijiongelesha siku moja, nakumbuka ilikua siku ya jumapili, wote tulikua nyumbani, Baba alikuja kutoka kwenye mizunguko yake, ilikua ni mchana kabisa, alinichukua sebuleni na kwenda na mimi chumbani, wakati Mama akiwa sebuleni Baba alifanya mapenzi na mimi.

Siku hiyo ilikua tofauti kidogo kwani alikua kama ananilazimishia, alikua kama mtu mwenye haraka kwani baada ya kumaliza hakuruhusu hata niguse, hakuongea na mtu mwingine yeyote, hakuongea chochote aliva nguo zake na kuondoka. Nilipotoka chumbani Mama ambaye mara nyingi akiniona na Baba alikua anakasirika basi siku hiyo alikua anacheka, nilikasirika ndipo nikaamua kumchana.

“Wewe unafikiri unapendwa, hivi una akili gani wewe? Kutoka kijijini ndiyo kunakufanya mshamba namna hiyo? Yaani kabisa unakaa unadhani kuwa huyo mwanaume anakupenda? Hahahah! Ahahhaha!” Aliniuliza huku akicheka kwa dharau. Nilimuangalia kwa dharau na kuingia zangu ndani.

Nilikaa ndani kama nusu saa hivi, lakini kuna kama kitu kilikua hakija kaa sawa. Nilijihisi moyo mzito, kama unauma unaenda mbio. Nilishindwa kukaa ndani nikatoka mpaka sebuleni, Mama alikua sebuleni anaangalia TV.
“Vipi bado hujapigiwa simu?” Aliniuliza.

“Atanipigia tu, mimi ananipenda na taarifa yako nikitaka kuolewa naolewa hata kesho sembuse simu!” NIlimjibu kwa dharau, lakini nilikua naongea kwa shida, nilijiona kama nakosa pumzi nikakaa.

“Tulia binti, nimekuambia kuwa hii nyumba huiwezo, huiwezi kabisa, mimi mpaka kuingia hapa nimepitia mengi na siwezi kuondoka, kama mwenzako aliyekua analindwa na mizimu aliondoka sembuse wewe ambaye ni mweupe kabisa umetoka kijijini huna mbele wala nyuma?”

Nilitamani kumjibu lakini sikuweza, kabla sijaongea chochote simu yangu iliitya, niliichukua lakini nilikua mzito sana kupokea. Alianza kunisisitiza nipokee kwani ni simu kutoka kwetu, nilishangaa alijuaje kwani sikumuonyesha na ilikua ni namba na haikua na jina tu.

“Unashangaa nini? Mimi mwenyewe nimezika ndugu zangu sana mpaka kuja kuzalishwa, au unafikiri watu tumekuja kirahisi rahisi tu hapoa? Nimemzika Mama yangu mzazi nije kuondoka bila kitu, pokea simu Mama!”

Aliongea kwa dharau, ingawa sikumuelewa lakini niliogopa, nilihisi kuna kitu kibaya. Nilipokea simu na kukuta alikua ni Baba yangu mdogo, nilimsalimia ndipo akaniuliza kama Bosi wangu yupo.

“Baba anataka uniambie kweli, kuna nini? Mbona unaniulizia mambo ya Bosi wangu!? Nilianza kupiga kelele, alinisihi nimpe simu mtu mwingine, kabla hatujaelewana mama alichukua simu, aliiweka sikioni na kuseama.
“Tunajua kila kitu wewe sema ni nani kafa? Ni Mama yake au baba yake, wewe sema?” Aliuliza kwa hasira, alikaa kimya kama dakika mbili hivi kisha akakata simu na kuiweka chini.

“Nini? Nani? Baba anasemaje?” Nilimuuliza kwa uoga, aliniangalia tena kwa dharau kisha akasema.
“Washamuua mdogo wako, wewe kaa utulie ndani, yeye ataenda kuzika na wewe utabaki hapa unalinda mali zake! Mkijua kutumia basi mjue na kuzitafuta!”

Aliongea kama vile kilikua ni kitu cha kawaida, nilikua na wadogo zangu watatu, wawili wakike na mmoja pacha wangu Dotto ambaye nilikua namsomesha chuo. Baada ya mimi kushindwa kuendelea na masomo na kuanza kazi za ndani niliona ili kuikomboa familia yetu ni lazima yeye asome, kwanza alikua na akili, alikua mtu wa kufaulu kila siku, pili alikua ndiyo mkubwa wakiume, mimi nina dada zangu wengine ambao nao hawakusoma wameoelwa tu hivyo nilijua kuwa Sudi (si jina lake halisi) akisoma ndiyo atakuja kuiokoa familia.

Nilimuuliza alikua anamaanisha nini ndipo akaniambia kuwa Pacha wangu kafariki dunia, alidondoka ghafla asubuhi akiwa chuoni na kupelekwa hospitalini ambapo alifia huko. Nilidondoka na kuzimia, nlikuja kuzindiuka baadaye nikajikuta nipo kitandani. Baba alikuepo na aliniambia kuwa nipumzike nisiende kumzika ndugu yangu. Sijui kwanini lakini nilijikuta nacheka, nilimuangalia na kumuona kama mtu aliyechanganyikiwa, alianza kuniambia kuwa hali yangu ni mbaya, siwezi kwenda na kuongea maneno mengine mengi lakini sikumuelewa.

Nilipobisha sana alijifanya kukasirika na kuanza kunipiga akiniambia siwezi kuondoka.
“Wewe huoni kama Biashara zangu zinakufa! Nimekuambia kuwa baki humu, hutaondoka na kama ukiondoka huwezi kurudi tena humu ndani!” Aliongea huku akitoka na kufunga mlango kwa nnje. Hakurudi mpaka usiku, yeye alikua ashajiandaa anataka kwenda kwenye msiba wa ndugu yangu huku mimi akiniacha nyumbani. Sikua na namna nikubali kishongo upande. Aliondoka na kuniacha na mke wake, amabye alikua kama anachekelea.

“Huo ndiyo mwanzo tu, atawamaliza ndugu zako wote na hutapata chochote.” Aliniambia.
“Najua ni wivu unataka tu kubaki kwenye hii ndoa, mwanaume hakupendi.” Nilimuambia kwa hasira, ingawa niliona kama ni ukweli lakini sikutaka kukubali mbele yake.
“Mimi alianza kumua Mama yangu, akamuua na mdogo wangu ndipo nikazaa naye.” Aliniambia.
“Sasa kwanini huondoki kama unajua kuwa huyu ni mchawi?”
“Nilichelewa, nimejua tayari ashanizalisha na ndugu zangu ashawamaliza, lakini sasa hivi hawezi kunifanya chochote, kinachoniweka hapa nikuhakikisha kuwa nachukua kila senti yake na kumuacha, sipo hapa kwaajili ya mapenzi, hana mapenzi huyu mtu. Mwanaume ambaye alikua anaua watoto wake kwaajili ya mali unafikiri anaweza kupenda mtu.

Wewe unafikiri ni kwanini yule mwanamke hakuondoka na chochote, kwakua anajua kua hakuna mali ya halali hapa. Haendi kwenu kwenye msiba bali anaenda kuondoka na nguo ya marehemu. Nilijua kuwa mume wangu ni mchawi baada ya kuona nguo za ndani za marehemu Mama yangu na mdogo wangu chumbani kwake. Nilipomuuliza alionakana kama amechanganyikiwa, hapo ndipo alinioa, tena ni juzi tu baada ya mke wake kumuacha na Mama yake kufariki ndiyo nimekuja kugunuda ushenzi wake. Mimi hanigusu tena nishajidhatiti!”

Aliniambia, niliogopa kidogo lakini niliona kama ni stori flani, niliona kama vile ananitania aua annitisha ili niondoke na kumuacha mwanaume ambaye ananipenda.

“Wewe ulijuaje kuwa ni nguo za ndugu zako kama zingekua za wengine.” Kila nguo ilikua na jina, tarehe ya kifo na sbaabu za kifo, vilikua vimebandikwa vinaonekana. Niliogopa kidogo lakini sikumuonyesha.

“Kama huamini akirudi kagua bei lake, usipoona nguo yoyote ya ndugu yako basi mimi naondoka hapa.” Aliniambia, sikutaka kubishana naye kwani nilikua katika machungu makubwa, nilikua naumia kuhusiana na kifo cha mdogo wangu.

Niliamua tu kukaa kimya, ndugu zangu walinipigia simu kunipa pole kwani Baba aliwaambia kuwa baada ya kupata taarifa za msiba nilidondoka, nimezimia na hali yangu ni mbaya hospitalini. Nilishangaa kwani pamoja na kuzimia lakini hali yangu ilikua nzuri, nilipokea pole na kusubiria arudi. Haukaa sana msibani, alirudi kesho yake, sikumuuliza chochote, aliingia chumbani kwake, akabadilisha nguo nakutoka. Alipotoka nilinyata na kuingia chumbani kwake kukagua, chumba alichokua akilala yeye kilikua cha peke yake.

Pamoja na kuoa lakini walikua hawalali kitanda kimoja na Mama, alkua anajitenga na muda mwingi usikua likua chumbani kwangu. Alikua kafunga chumba chake na ufunguo, lakini nilikumbuka sehemu ambayo wanaweka ufunguo wa ziada kipindi Mama yule mwingine yupo, nilienda kuchukua na kufungua. Nilikagua kwenye begi lake, nilikuta nguo mbili za ndani, moja ilikua ya kike na nyingine ya kiume. Yakiume iliandikwa jina la Pacha wangu, sababu za kifo na tarehe ya kifo. Ile ya pili ilikua na jina la Mdogo wangu mwingine.

Hiyo ilikua na kikaratasi ambacho kiliandikwa jina lake, tarahe ya kuzaliwa na wakaandika tarehe ya kufariki wakaweka deshi deshi. Mwanzo nilihisi kama utani, nilihisi labda huyu Mama ndiyo kaandika, lakini wakati naakagua nilipitiwa Baba akaja na kunikuta, alipaniki kuniona pale, alikasirika na kuanza kunipiga akiniambia kwanini nakagua vitu vyake. Mimi niliishia tu kumshutumu kuwa ameniulia ndugu zangu, alinipiga sana na kunifungia ndani, alinifungia usiku mzima mpaka asubuhi ndiyo alikuja na kuniomba msamaha.

Kwa namna alivyokua anaongea ni kama kulikua hakuna kitu kikubwa kilichokua kimetokea. Aliombe msamaha wakunipiga lakini si wa kumuua mdogo wangu. Aliomba sana na kuniambia anataka kunioa, anataka kufunga ndoa na mimi, alibembeleza akinishawishi kuwa nikikubali kuolewa basi nitapata kila kitu chake, mali zote zitakua katika majina yangu, aliongea maneno mengi, alilia kama mtoto, huku akisisitizia kuwa hakupanga kunipiga bali ni shetani tu alimsukuma kufanya hivyo ila bado ananipenda.

NB: Kwa ushauri kuhusu Biashara hakikisha unanunua Kitabu cha Biashara 50.

Bei ya kitabu changu cha “Biashara 50” ni shilingi elfu 9,999/-, na unalipia kwa M-Pesa No. 0742-381-155 au Tigo Pesa No. 0657-552-222 Jina “Iddi Makengo” na Kitabu unatukiwa kwa Whatsapp/Email/Facebook, hakuna cha karatasi.

ITAENDELEA…

KWAHERI; BAKI NA NDOA YAKO MIMI NABAKI NA MAISHA YANGU---SEHEMU YA KUMI NA MOJA

“Acha kuamini mambo ya Kishirikina, hivi ni vikaratasi tu!” Baba alichukua vile vikaratasi na kuvichana. Aliniongelesha sana kuniomba msamaha kwa kipigo mpaka nilianza kumuamini. Niliamua kubaki wkwa sahariti kuwa anioe na amuache yule mwanamke mwingine.
“Mimi sitaki kuwa na mke mwenza, kama ni mimi iwe mimi tu, nataka tuanze wote maisha.” Nilimuambia, akili yangu ilikua inawaza mali, ingawa nilijua kuwa ni wa shirikina lakini nilijisemea kama kashamuua mdogo wangu ni lazima na mimi nilipe kisasi.
“Hakuna shida, huyo nitamucha, lakini sasa hivi watoto wapo shule, kama nikimuondoa haraka nitawaathiri masomo yao, ninachoomba unipe muda nimuache taratibu ndipo tuoane.”

Aliniambia, nilimkubalia kishingo upande, kusema kweli bado nilikua naogopa, na lengo langu kubwa lilikua kumrudubini nikishachuma mali za kutosha basi niondoke.
“Sawa ila nataka ukakae dukani…” Aliniambia, kusema kweli nilishangaa, hata siku mbili zilikua hazijapita tangu kufariki kwa mdogo wangu, tena pacha wangu, mtu ambaye nilikua nampenda kuliko hata Mama yangu.
“Una akili kweli, hata attu ya mdogo wangu bado unasema nikakae dukani, mimi ninachotaka ni kuondoka kwenda kumalizia msiba wa mdogo wangu.”

Nilimuambia, hapo ndipo kama nilimtibua, alikataa katakata na kuniambia kuwa ni baki nyumbani. Aliniambia kama sitaki kwenda dukani basi nibaki nyumbani lakini hawezi kuniruhusu kwenda kwenye mazishi. Hakuniambia sababu zaidi ya kusema kuwa kama nikiondoka basi ndiyo mwisho, nisirudi tena nyumbani kwake. Niliasirika na kumuambia kuwa kama ni hivyo basi aniache niondoke kwani sitaki tena kuendelea kuishi katika nyumba kama ile. Nilikazania kuwa nitaondoka na kama hataki basi lakini siwezi kuacha msiba wa mdogo wangu kupita bila mimi kwenda.

Baada ya kubishana sana alikubali, lakini aliniambia kuwa atanipeleka yeye kwa gari yake kwani kwa hali yangu siwezi kwenda mwenyewe. Hapo nilikubali akaniambia kuwa nijiandae kesho yake tutaenda. Baba aliondoka na kuniacha nyumbani, baada ya kuondoka tu Mama alikuja na kuanza kuniongelesha maneno maneno yake, mimi nilimuona kama mtu mwenye wivu tu.
“Hawezi kukuruhusu uende kuzika ndugu zako, nina uhakika ukienda basi jua kuwa kila kitu kitakua kimeisha, hata kua na haja na wewe tena, baada ya siku saba ndiyo atakuruhusu, nakumbia kama unajipenda basi ondoka, huyo si mwanaume atakumalizia familia.” Aliniambia.

“Mbona yakwako hajaimaliza?” Nilimuuliza, aliniakasirisha na kuna wakati niliona kama ananiambia niondoke si kwakunitakia meka basi ni kwasababu ya wivu. Alikua amekuja chumbani kwangu, nilipomuambia vile alienda na kufunga mlango, mimi nilihisi ananipiga lakini nilishangaa anaanza kuvua nguo. Alivua nguo zote na kubaki kama alivyopzaliwa. Alinifuata na kukaa pembeni yaangu. Kisha alichukua mikoni yake na kuanza kujibinya kwenye mapaja. Alikua akijibinya kama vile mtu anakamua jipu, alijibinya kwa nguvu mpaka ngozi ya paja ikaanza kupasuka.

Nilishangaa, alionekana kama anaumia lakini aliendelea kujibinya mpaka mpasua ukawa mkubwa.
“Kuna watu wanameza hirizi lakini mimi nimeshonewa.” Aliniambia hukua kiingiza mkono kwenyeile sehemu ya paja iliyopasuka na kutoa hirizi kubwa nyeusi. Nilishangaa kwani pamoja na hiyo sehemu kupasuka lakini hakutokwa na damu kabisa.
“Umefanya nini? Mbona hakuna damu?” halafu si hakukua na kidonda?” Nilimuuliza kwa mshangao.
“Hiki ndiyo kitu kinanisaidia mimi, hawawezi kunifanya chochote lakini wewe na familia yako ni weupe kabisa, atawamaliza wote sababu ya mali na kama unahisi kuwa utakua na amani basi sahau.”

Aliniamba, baada ya kunionyesha hizizi yake aliirudisha kwenye paja lake, kwa kuangalia kilikua kama kimfuko cha ndani kwa ndani, yaani kama ngozi yake ilichanwa na kutengenezewa kamfuko. Alipoirudisha alitoka huku kashikilia paja lake, alikua kama anakimba hakukumbuka hata kuvaa nguo. Kitendo kile kiliniogopesha na kufikiria mara mbili kama kweli nahitaji kuendelea kuishi pale. Niliwaza sana lakini kabla ya kufanya chochote simu yangu iliita. Alikua ni Mama yangu mdogo, alikua akiniuliza kama nitaenda lini. Nilimuambia kesho yake naenda, aliniambia nifanye haraka.

Kwa namna alivyokua anaongea nilihisi kuwa kuna kitu, haikua msiba tu, nilimuuliza lakini hakuniambia. Nilibaki na wasiwasi mpaka jioni Baba aliporudi, nilimkumbushia kuhusu safari akaniambia hapana, hatuwezi kwenda tusubiri mpaka wiki inayofauata.
“Mdogo wako anaumwa, anahitaji kuletwa hospitali huku?” Aliniambia, nilishangaa kwani sikujua anamaanisha nini.
“Mdogo wangu? Mdogo wangu gani huyo tena?” Nilimuuliza huku nikiwa nimepaniki. Alitaja jina la mdogo wangu yuleyule ambaye alimuandoka kwenye kile kikaratasi.

“Ukimuua huyu na mimi nakuua, siwezi kukubali umuue mdogo wangu!” Nilipiga kelele huku nikimvamia kumpiga.
“Nani amuue, mdogo wako presha imepanda kadondoka, anaweza kupooza mimi ndiyo namsaidia, jaa hapa akipona ndiyo utaondoka, nimewaambia wamleta kumuuguzia hapa.” Aliongea, hakutoa maelezo mengi jinsi alivyojua kuwa mdogo wangu anaumwa. Aliondoka na kuniambia safari hamna.
“Huyo hatakufa, atakuja hapa na utateseka naye mpaka kuzeeka.” Mama aliniambia, nilimuangalia kwa hasira na kunyamaza.
“Ushawaona wale watu wana pesa nyingi lakini wana mtoto zezeta, basi wewe unaenda kuolewa na mdogo wako ndiyo atakua zezeta.”

Aliendelea kuongea maneno ambayo yalizidi kunikasirhsa. Aliniambia kuwa mimi ndiyo kila kitu kwa Baba, hana msaada mwingine, anaweza kufanya chochote kwaajili ya mali hivyo kama nikiondoka mimi hatakua na mtu mwingine wa karibu wa kumtoa sadaka kwakua yeye wanae hawezi kuwagusa, ndugu zake walishamtenga mimi pekee ndiyo kama ndugu yake hivyo kama nikunioa atanioa lakini sitafaidi ndoa kwnai nitaishia kulea mdogo wangu na mtoto sitazaa.

“Kwahiyo nifanye nini?” Nilimuuliza.
“Ondoka kabla ya ndugu yako kuja hapa, nenda kaguse tu mchanga wa kaburi la ndugu yako, ukiugusa tu siku ndani ya siku saba hawezi kukufanya kitu chochote tena.” Aliniambia nakuondoka zake, ulikua ni usiku lakini sikua tayari kuona tena ndugu yangu mwingine akifariki dunia sababu ya mali. Nilishahoka yale maisha, niliamua kuondoka na sikutaka kubeba chcochote. Kwakua nisingeweza kuondoka usiku ule na sikutaka Baba ajue kama natoroka, nilimuambia kuwa nitabaki lakini mdogo wangu wasimlete mpaka hizo siku saba ziishe na mimi kwenda mwenyewe kumchukua kwani nitaeleweka vibaya.

Baba alikubali, asibuhi aliniambia niende dukani, nlikubali na kwenda kufungua duka, alinipeleka mpaka dukani nikafungua duka, lakini alipoondoka kwenda kazini, nilimuaga kijana wa kazi na kumuambia natoka huku nikimuambia asije kumuambia Baba kuwa nimeondoka. Nilienda stend na kupanda mabasi, nilifika nyumbani usiku. Kila mtu alinishangaa kwani nilikua sijamuambia mtu yeyote kuwa naenda. Nilipofika kitu cha kwanza nilitaka kuonyeshwa kaburi la mdogo wangu, waliniambia kuwa mdogo wangu mwingine kalazwa hospitali lakini sikujali.

Nilienda mpaka kwenye kaburi la mdogo wangu, nilishika mchanga wa kauri lake. Sikusikia chochote, nilirudi nyumbani lakini baada ya kama masaa mawili hivi nilishanga awatu wanakuja, mdogo wangu aliyekua hospitalini alikua kapona mzima anakuja ananikimbilia ananiita dada. Nilimkumbatia huku nikitokwa na machozi.
“Umeamua kuniua?” Ilikua ni meseji kutoka kwa Baba. Sikuijibu, nilizima simu kabisa na kutoa laini, sikutaka kusikia chochote kuhusu ile familia. Niliamua kuendelea na maisha yangu na kusema kama ni ndoa basi bora kufa msela.

Baba naye hakunitafuta tena, nilikua na kiasi changu kikubwa tu cha pesa ambazo nilikua nachjo benki, baada ya kutulia niliamua kufungua Biashara. Miaka kama miwili baadaye ndipo nilikutana na yule Mama mpya, aliniambia kuwa aliachana na Baba kwani bada ya mimi kuondoka mtoto wake mkubwa alianza kuugua. Aliondoka na sasa hivi Baba kabaki na kazi yake, hana Biashara yoyote anaishi maisha tu yakawaida na hajawahi kuoa tena. Mama (Yule wa kwanza) yeye aliolewa na ana mtoto mwingine mmoja ana maisha yake mazuri.

***MWISHO

0 comments:

Post a Comment

BLOG