Search This Blog

Tuesday, June 21, 2022

BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!

  

IMEANDIKWA NA IDDI MAKENGO

 

FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!


Kitu pekee kinachokuja kichwani kwangu nikisikia neno “Baba” ni sauti ya Mama yangu ikitokea chumbani kwake, nikiwa nimejifungia chumbani mimi na Dada (Alikua ni mfanyakazi wetu wa ndani). Mama alikua akipiga kelele kuomba msaada lakini hakuupata, kicheko cha Shangazi sebuleni kilinifanya kuogopa kutoka ndani. Wakati huo nilikua na miaka minne lakini hizo kelele mpaka leo haziwezi kutoka kichwani kwangu.


JOIN US ON TELEGRAM

Hakuna kitu kingine ninachokikumbuka kutoka kwa Baba yangu zaidi ya hicho, najaribu kukumbuka mambo mengine, lakini hakuna, hata sura yake naikumbukia kwenye picha lakini si nikiwa mdogo. Sina uhakika kama alikua ni Baba mzuri, pamoja na Shangazi yangu kujari bu kunionyesha picha za Baba yangu akiwa kanipakata anacheka, picha akiwa katutyoa out tunakula lakini sina kumbukumbu ya namna hiyo kabisa.


Kwangu nikisikia jina “Baba” najikuta nashtuka na kutamani kujifungia ndani, na ukubwa huu bado nina ndoto za mimi nikiwa nimejifungia chumbani mimi na Dada. Kitu kingine ambacho kuhusu utoto wangu ambacho mpaka leo hakijanitoka ni picha ya Mama akiwa mjamzito,  nakumbuka namna nilivyokua nashika tumbo lake, ananiambia ni mdogo wangu ataenda kumnunua hospitalini.


Lakini picha hiiyo haikai sana, inafutwa na picha ya Mama akitoka chumbani analia, damu zinamtoka sehmeu za siri huku Baba akimkimbiza kwa nyuma na kuendelea kimpiga, anadondoka chini na kutulia, halii tena na baada ya hapo kila nikimuuliza kuhusu tumbo lake na yeye kwenda kumnunua mdogo wangu anaishia tu kulia. Kwa wakati huo sikujua kuwa mdogo wangu alienda wapi, lakini baada ya kuwa mkubwa ndipo nilijua kuwa ile mimba ilitoka kutokana na kipigo cha Baba.


Baba yangu hakuchukua muda, alifariki kipindi hichohicho, nakumbuka tu watu walikua wengi nyumbani na Mama likua analia sana akimlilia Baba. Pale nyumbani tulikua tukiishi na Shangazi yangu, ambaye ni mdogo wake na Baba, yeye alikua ndiyo kila kitu kwa Baba, Baba yangu alikua ni mfanyakazi wa Shirika moja kubwa, alikua analipwa msahara mzuri, ana akipato kikubwa, akafungua Biashara nyingi ambazo alikua akisimamia Shangazi.


Mama hakuruhusiwa kutfanya chochote, kazi yake ilikua ni kukaa nyumbani na kila kitu alikua ni Baba na Shangazi tu. Baada ya Baba kufariki, nilishanga atu Mama hayupo, nakumbuka nilikua shuleni, miezi kama mitatu hivi baada ya Baba kufariki, narudi nyumbani nakuta hakuna mtu, hakuna Shangazi, hakuna Mama wala Dada. Nililazimika kukaa nnje mapaka usiku kama saa nne hivi. Shangazia likuja na kunikuta nimekaa pale nnje, basi alianza kwa kunifokea nafanya nini nnje wakati ule.


“Milango imefungwa, hakuna mtu ndani….” Nilimuambia kwa sauti ya shida, nilikua na njaa sana, nilikua nimechoka.


“Milango imefungwa, Mama yako yuko wapi?” Aliniuliza huku akinishika na kuninyanyua, hata kutembea ilikua ni shida kwani tangu nilipokunywa uji shuleni saa nne mpaka wakati huo saa nne usiku nilikua sijaingiza kitu kingine tumboni.


Alilazimika kunibeba mpaka ndani, akaanza kukagua chumba kimoja mpaka kingine kisha akarudi.


“Mama yako kaondoka, kachukua vitu vyake vyote, kakutelekeza, kakukimbia, atakua ameenda na mwanaume mwingine, mimi nilijua tu kuwa huyu Malaya ataondoka…” Aliongea maneno mengi sana akimshurumu Mama yangu, lakini mimi nilikua nimechoka, nina njaa na nilihitaji chakula.


“Shangazi nina njaa…” Nilimuambia, nilikua nimelala kwenye chakula, aliingia jikoni na kukuta hakuna kitu.


Aliingia kwenye friji na kutoa icecream kisha kunipa, kumbuka nilikua nanjaa sijala mchana kutwa ananipa ice cream. Nilifanya kosa ambalo mpaka leo nalijutia, nikidhani labda nipo na Mama yangu nadeka niliitupa ile icecream chini na kumuambia siiitaki.


“Mimi nina njaa nataka chakula!” Nilimuambia kwa hasira huku nikirudisha kichwa changu chini na kulala kwenye kochi. Lakini kichwa hakikufika, nakumbuka nilikua na nywele ndefu za kubana nyuma, Mama yangu alipenda sana kunisuka na kwakua nina nwele nzuri kama singasinga absi zinakua haraka.


Shangazi alinishika nywele na kuninyanyua mpaka juu, kisha akanishika shingo, akaniimanisha kichwa changu mpaka ilipokua ile Icecream, zilikua ni zile icecream za kwenye vikopo hivyo nilivyoirusha chini ilimwagika, alinisukumiza kichwa changu na kunilazimisha nilambe mpaka iishe.


”Utalamba mpaka iishe na hicho ndiyo kitakua chakula chako! Mshenzi mkubwa wewe unataka kuniharibia siku yangu, nimetoka huko nahangaika narudi nakuta Mama yako hayupo halafu leo unaniletea maujinga ujinga yako, mimi si Mama yako au Baba yako! Weewe ni yatima Baba yako amekufa na Mama yako amekufa hivyo nakusaidia, hutakiwi kudeka!”


Alitukana sana, akamtukana sana Mama yangu,a kamtukana na Baba yangu, ni kama alikua na hasira nao, alinisukumiza kichwa chini mpaka nikamaliza kuilamba ile icecream iliyokua imedondoka chini, kuna kidogo ilikua imebaki kwenye kikopo, akaniambia kuwa niilambe.


“Hicho ndiyo chakula chako mshenzi mkubwa wewe!” Aliniambia kisha akanivuta mpaka chumbani kwangu, akafunga mpango kwa nnje ksiha akaondoka zake. Nilikaa macho mpaka asubuhi, pamoja na njaa niliyokua nayo lakini kutokana na uoga sikua na nguvui hata ya kulala.


Usiku mzima nilikua nikiwaza niwapi Mama alikua ameenda na ni kwanini aliondoka na kuniacha mimi sikua nikijua chochjote kilichokua kinaendelea kwa wakati huo, nakumbuka baada ya kifo cha Baba kulikua na vikao vingi sana pale nyumbani, kila wakati baada ya kikao Mama alikua akiondoka analia lakini nilipokua nikimuuliza alikua ananiambia hakuna kitu hajisikii tu vizuri.


Babu alishafariki dunia siku nyingi, Bibi alikuepo na kuna wakati alitaka kunichukua lakini Mama alikataa na kuniambia kuwa atabaki na mimi. Kuna siku nakumbuka nilimsikia Mama akibishana na Shangazi.


“Sina shida na mali zenu lakini mwanangu nitaondoka naye!” mama alikua anamuambia Shangazi.


“Kama ulikuja na mtoto hapa ndiyo utamchukua, huyu mtoto ni wakwetu, ni damu ya Kaka yangu, siwezi kukuacha uondoke naye, au unataka Kaka yangu anilaani huko kaburini!?” Shangazi alimuambia, walibishana sana nusu kupigana, Mama alitaka kunipigania mimi, ili tu aondoke na mimi.


Lakini ghafla nashangaa kaondoka, asubuhi ananiaga vizuri naenda shuleni narudi hayupo. Kwanini aondoke na wakati kila sikua nananiambia kuwa ananipenda? Ni swali ambalo sikulipatia jibu. Niliwaza mpaka jua likatoka, ilikua imefika asubuhi, nilienda mlangoni kufungua lakini bado mlango ulikua umefungwa, nilikaa mpaka kwenye saa nne hivi ndipo mlango ukafunguliwa.


“Una njaa mwanangu, basi twende ukanywe chai!” Shanmgazi aliniambia, alikua kachangamka tofauti na jana yake. Nilitoka na kunywa chai ya maziwa na mikate. Nilikunywa kwa kasi sana, ingawa nilikua si mlaji mzuri lakini nilikua na njaa, yaani sijui hata hiyo nguvu ya kula ilitoka wpau ila nilikula kama mchwa nikamaliza ule mkate mdogo na bado nilikua na njaa, ni kama nilitamani kula tena sema nilimuogopa Shangazi.


“Mimi sio Mama yako, mimi nafanya kazi, Mama yako kaondoka na hatarudi tena, wewe mchukulie kama amekufa, usimtafute tena, kuanzia sasa mimi ndiyo nitakua Mama yako nitakua Baba yako. Kitu chochote utaniambia mimi, sitaki uongee na mtu yoyote, ukitoka shule ni kurudi nyumbani, utakua unakaa kule kwenye nyumba ndogo mpaka mimi narudi, sitaki utoke, sitaki uongee na mtu, kama nikisikia unaongea na mtu absi utamfuata Mama yako kaburini?”


Aliongea, aliniambia mambo mengi ya kunitisha lakini mimi nilishika kitu kimoja ambacho kilinichanganya “Utamfuata Mama yako Kaburini” iliniumiza kichwa sana kwani jana yake aliniambia kuwa Mama kaondoka na kuniacha na kamchukua na Dada ili sisi tubaki wawili. Leo ananiambia nitamfuata Mama yangu kaburini, inamaana Mama naye amekufa kama Baba? Nilijiuliza bila majibu, niliogopa kumuuliza lakini tangu siku hiyo kila wakati Shangazi akikasirika alikua ananiambia atanipiga mpaka nimfuiate Mama yangu Kaburini.


Baada ya kama siku mbili hivi Shangazi aliletamfanyakazi, huyu alikua ni kama mbaba hivi mtu mzima mzima, aliniambia kuwa huyo ndiyo atakua mfanyakazi akifanya kazi zote za ndani. Mimi sikua na chakufanya kwani bado nilikua mdogo an nilikua sielewi chochote kilichokua kinaendelea. Baba naliacha mauka mawili makubwa, nyumba niliyokua naifahamu ni hiyo tuliyokua tunaishi ila kuna wakati nilimsikiaMama akisema kuwa Baba ana nyumba nyingi lakini Shangazi aliishia kumtukana na kumuambia kuwa hawezi kuchukua hata moja.


Kutokana na Biashara zake Shangazi alikua anakua bize sana na mara nyingi kusafiri bila taarifa. Alikua akiniacha nyumbani na Martin (sio jina lake halisi). Kwa kazi Martina likua akifanya, usafi wa ndani, kupika, kupiga deki kila kitu alikua akifanya, alikua ananifulia mimi pamoja na shangazi. Wakati naishi na Mama alinifundisha kuoga mwenyewe hivyo nilikua naoga mwenyewe.


Lakini baada ya Anko Martin kuja nyumbani, wiki moja Shangazi alikua kasafiri hivyo tukawa tumebaki sisi wawili nyumbani, alianza kuniambia kuwa siogi vizuri hivyo aweaananiogesha. Mwanzo nilikataa, lakini baadaye alinaimbia kuwa Shangazi ndiyo kasema.


“Mimi kila siku nagombezwa kuwa wewe unakua mchafu, Shangazi yako anasema niwe nakuogesha, kama hutaki nimuambia, si unajua jinsi alivyomkali!” Alinitisha, ingawa hakua na muda sana pale nyumbani lakini alishaona tabia za Shangazi yangu.


Alikua ni mtu wa hasira, alipenda sana kunipiga na kunitukana, mara nyingi bila sbabau alikua ananipiga sana na kunitukana hukua kirudia kuwa atanuipiga mpaka nimfuate Mama yangu Kaburini.


“Au unataka kumfuata Mama yako kaburini?” Aliniuliza, basi mimi nilikataa kwenda kaburini na kumuambia niko ayari kuogeshwa, alianza kunoigesha taratibu. Lakini kila sikua kiwa ananiogesha, kila akifika sehemu zangu za siri basi anaanza kuingiza kidole kwa madai kuwa ananitoa uchafu.


“Huku kunakau na uchafu mwingi sana kunanuna sana!” Alikua akiniambia, basi mimi nilinyamaza, nilikua namuangalia jinsi anavyofanya, yeye alionekana kufurahia na alikua analegea kabisa, kwa wakati huo mimi sikujua kabisa sababu ya yeye kufanya hivyo na niliamini kuwa ni uchafu kweli.


Simulizi yetu ndiyo kwanza inaanza…. Je Fatma ni nani na kapitia mambo gani, hembu endelea kufuatilia leo ni kionjo tu.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA PILI


Martin hakuwahi kunigusa, kwa maana ya kufanya mapenzi na mimi, yeye alipenda tu kunishika na kunichezea, mwanzo niliona kama kero lakini baadaye nilizoea na kuona kama kawaida. Pia alikua akinisaidia sana kazi nilizokua nikipewa na Shangazi. Ingawa alikuepo na alikua na uwezo wa kufanya kila kitu lakini Shangazi hakutaka kabisa mimi kukaa na kupumzika, kama akiwepo nyumbani alikua akihakikisha nafanya kila kitu.


Shangazi alikua hajaolewa na alikua hana mtoto, kila siku alikua anachelewa kurudi nyumbani na akirudi hata kama nimelala ananiamsha, anavua nguo zake na kuniambia nimfulie. Yaani hata kama hana nguo chafu, atavua hata chupi na kunirudisha, hata kama ni saa anne usiku ataniambia nimfulie na hakutaka kabisa Martin kunisaidia, madai yake ni kuwa alikua ananifundisha kazi na kama nikisaidiwa basi sitajua.


Mimi sikua na namna zaidi ya kufanya hizo kazi, hali hiyo ilinifanya kuwa nachoka sana na darasani kial siku ni mtu wa kulala.  Alikua akiitwa shuleni kuhusu mimi, lakini akifika kule, kama akielezewa kuwa mimi nalala darasani basi aliishia kunuipiga hivyo nikiwa darasani nilikua najitahisi sana nisilale ingawa ilikua ni ngumu. Shangazi hakua ameolewa, na mpaka wakati huo nakumbuka nipo darasa la tatu nilikua sijawahi kumuona na mwanaume kabisa.


Nyumbani kwao Baba walizaliwa wawili tu wa tumbo moja, Babu alikua na mwanamke mwingine na alimuacha Bibi kwenda kwa huyo mwanamke, Bibi yeye alikua akiishi kijijini, aligoma kabisa kuja mjini kwakua tu Babu alikua hataki yeye aje mjini. Ingawa ni kama walikua wameachana lakini alikua hawezi kuondoka bila ruhusa ya mume wake. Kwa maana hiyo mali zote za Baba alikua kabaki nazo Shangazi ambaye alijifanya kunilea wakati alikua ananinyanyasa sana.


Nikiwa darasa la tatu Shangazi alienda shuleni kwetu kuniombea uhamisho, aliwaambia kuwa ananihamishia shule nyingine, lakini tuliporudi nyumbani aliniambia kuwa, hakuna sababu ya mimi kusoma wakati nitaishia kuolewa na kuwa Mama wa nyumbani. Wakati huo nilikua na miaka nane tu,  aliniambia nitakua na kaa nyumbani na kufanya kazi zote . martin bado alikua akiishi pale, lakini  tofauti na zamani ambapo alikua akilala katika chumba chake alihamia katika chumba cha Shangazi, walikua wapenzi na mara nyingi alikua akienda naye dukani hivyo mimi kubaki mwenyewe kufanya kazi za ndani.


Siku moja Shangazi alitoka na Martin,  ilikua ni lazima mimi kuwasubiri mpaka kurudi kwani nilikua sijui kupika, nilishafanya usafi wote ndani na kila kitu kilikua sawa. Waliondoka asubuhi na kuniacha ndani na mkate tu, mpaka usiku saa nane hivi bado walikua hawajarudi, nilikua na njaa sana na  nilikua nasinzia, kwakua nilishaona mara nyingi Martin akipika na niliamini kuwa ninaweza kupika niliamua kujipikia mwenyewe.


Ndani kulikua na maziwa ya mtindi hivyo nilitaka kupika ugali wa maziwa, kulikua na samaki na nyama pia lakini mimi nilikua siruhusiwi kula samaki na nyama,  hivyo vilikua ni vyakula vya Shangazi na Martin. Niliwasha jiko la umeme , nikaweka maji na kuyachemsha ili kupika ugali. Maji yalichemka lakini shida ikaja kwneye kusonga ugali, haikua rahisi kama nilivyodhani, kwanza mimi nilikua mfupi hivyo nilikua sifikii sufuria vizuri, nilichukua kiti na kukipanda juu ili kuweza kufikia jiko ambalo lilikua  refu.


Lakini ugali haukusongeka, niliishia kumwaga maji juu ya jiko,  na kuchafua jiko nzima. Kwa bahati nzuri sikupiga shoti nyumba, nilipoona maji yamenishinda na kumwagika nilizima harakaharaka jiko. Lakini wakati nasafisha jiko ili Shangazi akija asinione shanagzi ndiyo ulikua muda wake wa kuingia, alinikuta jikoni nasafisha jiko na pambeni kuna sufuria, aliniangalia tu lakini hakusema kitu.


Kusema kweli niliogopa, kwa Shangazi kuniona nimemwaga vitu na bila kusema chochote iliniumiza zaidi kuliko kunipiga, aliingia chumbani kwake. Martin alinifuata na kuniuliza nini kilikua kimetokea, nilikua natetemeka kwa uoga.


“Usijali, leo yuko kwenye Moodi nzuri, hawezi kukupiga.” Aliniambia huku akinisaidia kusafisha pale, kama dakika mbili hivi Shangazi alirudi, alishavua nguo alizokua amevaa, kumuona tu nilishtuka nikijua sasa ni kiama, niliamini kuwa amekuja kunipiga.


Lakini haikua hivyo, alikua tofauti kiasi kwamba hata Martin alishangaa.


“Vipi mbona hivyo, unafanya nini jikoni usiku huu?” Martin alimuuliza kana kwamba anamshika, alihisi anataka kunipiga kwani alikua anapekuapekua, akagusa karai ambalo lilikua na vyombo akawa anatoa mwiko.


“Ni bahati mbaya, muache usimpige usiku huu….” Martin alimuambia huku akitaka kumshika, lakini Shangazi alionekana kushangaa.


“Wewe vipi, hivi unafikiri ninaweza kumpiga mwanangu kwa kitu cha kijinga namna hii, mtoto alitaka kupika ugali, moja kwa moja ni kuwa ana njaa, sasa kwanini nisimpikie, au unafikiri mtoto kama huyu anaweza kupika mwenyewe?” Alimuuliza huku akichukua sufuria.


“Hapana, lakini tangu lini wewe ukapika, kama vipi acha nimsongee mimi huo ugali?” Martina limuambia akitaka kumnyang’anya mwiko.


“Wewe vipi, Mseng* nini? Yaani kulala na mimi kunakufanya uwe na kiburi, unataka kunipanda kichwani, hembo ondoka hapa mpuuzi mkubwa wewe, acha nimpikie mwanangu!” Aliongea kwa hasira hukua kimsukuma, Martin ni kama alikua kamwagiwa maji ya baridi, baada ya kuambiwa vile aliondoka taratibu bila kusema chochote.


“Mwanangu si una njaa, ngoja nikupikie ugali, au una chakula gani?” Shangazi aliniuliza huku akiwa kaniinamia, aliuliza kwa upendo lakini sikuuamini upendo wake.


Mikononi alikua kashikilia sufuria mkono mmoja na mwingine kashika mwiki,  kwa namna alivyokua amenisimamia nilikua nimewekwa katikati, yaani akili yangu iligoma kuamini kuwa napikiwa, nilihisi kuna wakati atanipiga kichwani na vile vitu hivyo nilisimama kwa kujihami.


“Huohuo ugali Anti.” Nilimiambia.


“Basi nenda kapumzike chumbani kwako mimi nakuja kukuamsha baada ya kumaliza kupika.” Niliondoka kama kipanga, sikuamini kuwa kaniacha, nilienda na kupanda kitandani, sikulala, pamoja na njaa yangu lakini akili yangu haikua kwenye tumbo, ilikua kwa Shangazi nikiwaza hivi huyu kweli ni wa kuniacha hivi hivi!


Lakini sikua na jibu, nililazimika kusubiri, kutokana na uchovu, kuchoka na mawazo nilijikuta napitiwa na usingizi kidogo. Yaani zilikua kama dakika tano lakini nililala kama mtu aliyelala wiki nzima, nilikua nimechoka sana kwani mchana kutwa nilikua na kufanya kazi ya usafi wa nyumba nzima. Basi ile tu nimelala nilisikia mlango unafunguliwa, nilitaka kuamka lakini kuna kitu kiliniambia, subiri, lala lala, niliendelea kufunga macho, lakini kuna kitu kingine kiliniambia ampa ni Shangazi.


Taa ilikua imezimwa kwani shanagzi alishakata umeme chumbani kwangu, mwanzo nilikua naogopa kulala na giza Baada ya Dada kuondoka hivyo alikata umeme akiniambia kuwa nammalizia umeme nitamfilisi hivyo nilikua nikilala giza siku zote.


“Uko wapi?” Nilisikia sauri ya Shangazi ikiuliza, nilinyanyuka harakaharaka na kumuambia sehemu nilipo.


“Npo huku Shangazi, sijalala, nipo macho, sijalala….” Nilianza kujitetea hata kabla hajaniuliza kwanini nilikua nimelala wakatiti hakuniruhusu, nilijua lazima atauliza, lakini kabla sijapata majibu ya nilichokiongea, nilisikia tu “Pwaaaa!”.


“Mbwa wewe! Si ulitaka kuniunguzia nyumba? Sasa ngoja nikuonjeshe joto ya jiwe!” Maji ya moto yalinimwagikia tumboni na kushuka mpaka miguuni, yalikua ya moto sana, nilipiga kelele sana huku nikikimbiakimbia chumbani, najigongagonga kila sehemu nikiomba msaada lakini Shangazi alishatoka. Alitoka hukua kitukana, wakati nilipapasapapasa mpaka nikafanikiwa kuuona mlango, nilitoka mpaka sebuleni ambapo kulikua na mwanga, nilikua na maumivu makali sana.


Nilikua nimeungua sana sehemu ya tumbo mpaka kifuani, na miguuni, nguo nilizokua nimevaa zilifanya maji kubaki zaidi tumboni na kuzidi kuniunguza. Maumivu yalikua makali, nilipiga kelele sana lakini hakukua na mtu wa kunisaidia, si Shangazi wala Martin, Shangazi aliingia zake chumbani, nilijikuta napoteza fahamu, mpaka asubuhi nilipomka nilikua nipo uchi chumbani. Tumbo lote lilikua limeungua, Shangazi alichemsha maji ya moto na kunimwagia wakati yakiwa yanachemka.


Martin alikua pembeni yangu, alikua akshikilia kopo la asali akinikadna vidonda vyangu.


“Shangazi yako katoka, kasema nikuache hivi hivi lakini naona utakufa, unatakiwa kupakwa asali….” Aliongea hukua kilia, tumbo lote lilikua limeungua na ngozi kutoka kabisa, mapaja nayo yaliungua lakini miguu haikuwa imetoka ngozi ingawa uilikua inauma sana. Nilikua katika maumivu makali sana,.


“Naomba unipeleke hospitali, nitakufa?” Bilijikuta namaumbia, aliniangalia kwa huruma na kutingisha kichwa kukataa.


“Shangazi yako akijua atakuua, hapana, baki hapa, hivi ni vidonda tu baada ya muda vitapona1” Martin hakunipeleka hospiyalini na Shangazi aliporudi alimsema sana akimtukana kwanini kinisaidia.


“Atakufa huyu, hivi unajau ameungua sana!” Martin alimuamibia, mimi nilikua chumbani nimelala siwezi hata kunyanyuka na wao walikua humo humo chumbani.


“Kwani akifa kuna shida gani, tena ndiyo niapata uhuru wa kufurahia mali zangu. Hivi unajua Kaka yangu aliacha mali kiasi gani? Unajua kuwa hizo mali zina majina ya nani? Ni huyu huyu mbwa, alikua anampenda huyu mbwa mpaka basi. Nina hasira naye sana, hivi unajua Kaka alikua ananidanganya kuwa vitu anaandika majina yangu, namuamini, najua ni ndugu yangu ila mwisho nakuja kukuta kamuandika huyu mbwa.


Siwezi kuuza kitu chochote mpaka huyu mbwa afe, yaani, nakuambia kama akifa sawa tu, anishi amisha ya shida kwa ajili yake! Bora afe awafuate wazazi wake!” Aliongwa kwa hasira mimi nikiwa pembeni yake, hapo ndipo nilijua hasira za Shangazi zilikua zinasababishwa na nini?


“Kwani Mama yake naye amekufa?” Martin alimuuliza, yeye alikua ni mgeni pale na hakua akimfahamu Mama yangu, mara nyingi nilikua namuambia kuwa nitaondoka kumfuata Mama yangu hivyo alikua akijua kuwa naongea hivyo kwakua Mama yangu bado yupo hai.


“Unauliza ili nini? Unataka kujua ili? Nimemuambia kuwa nakuacha hapa kwakua unanitom** vizuri lakini zaidi ya hapo ningekua nishakumalizia mbali, unajifanya kumpenda huyu mtoto kwani ni damu yako! Mimi ni damu yangu lakini simtaki, nataka afe nizike, hivi unajaua kuwa Baba yake aliacha wosia, yaani mimi nisimamie mali zake mpaka huyu awe mkubwa au akifa ndiyo mimi nichukue. Hivi unafikiri jkwa umri huu mpaka anakufa mimi si nitakua nishaoza kaburini!”


Martin hakuongea kitu, Shangazi alikuja kitandani, akachukua asali niliyokua napakwa na kuondoka nayo.


“Nisikie tena unajileta chumbani kwa huyu mtu, utamuacha afie hapa tutazika, kwani yeye ndiyo wa kwanza, nina mambo mengi yananisumbua, kama ukiendelea kuniletea ujinga wako na wewe nitakuondoa ukaendeele kukata majani huko!” Alimuambia martina mbaye aliondoka, sikuwahi kumuona tena Shangazi katika chumba changu wala martin hakuja kunipa dawa ya aina yoyote ile.


Nilikua kwenye maumivu makali, kikubwa alichokua akikifanya Martin nikuniletea chakula anakiacha mlangoni anaondoka. Nilikaa siku tatu tu vidonda vikaanza kuoza, vinatoa usaha kabisa, maumvu yalikua makali kiasi kwamba kuna wakati naweza kupoteza fahamu hata kwa masaa kumi bila kujijua. Sikupewa dawa yoyote ile na Shangazi hakuja kuniangalia.


Hali ilikua mbaya, siku moja nikiwa nimelala niko mkama nimepoteza fahamu, niliona sura kama ya Baba inanijia, niliikumbuka kwa namna alivyokua anampiga Mama, Baba alikua kama kakaa mbele yangu ananiangalia huku akilia, alikua analia sana, si kwa sauti ila machozi yalikua yanamtiririka mpaka basi. Alionekana kama anataka kuongea kitu lakini hawezi, alikua kama anataka kusimama lakini hawezi, ila kitu cha ajbu nikuwa, namna ambavyo Baba alikua anataka kusimama ndiyo jinsi ambavyo mimi nilikua napata nguvu.


Sikumuona kama anataka kunisaidia bali kama anataka kunipiga, kama nilivyosema huko nyuma, sura pekee na wakati pekee ambapo namkumbuka Baba yangu ni wakati ambao alikua anampiga Mama yangu, hivyo jinsi alivyuokua anataka kunyanyuka kunifuata mimi niliona kama vile anataka kunifuata ili kunipiga. Nilipata nguvu na kunyanyuka, sikusikia maumivu yoyote kwa wakati huo kwani nilikua bado nimelala, ilikua ni kama ndotyo flani ila nilijihisi kabisa na nyanyuka.


Nilinyanyuka na kuchukua kitambaa, nikaanza kufuta vidonda vyangu, yaani ilikua nakwangua wadudu pamoja na uozouozo, nilikwangu bila kuhisi chochote, baada ya hapo nilichukua kitambaa na kujifunga mimi mwenyewe tumboni ambapo ndipo kulikua kumeharibika sana, hizi sehemu nyingine nilizisafisha tu. Baada ya kumaliza kila kitu ndipo nilizinduka usingizini, maumivu niliyoyapata hapo yalikua ni mara mbili ya yale ya kwanza ambayo niliyapata kipindi namwagiwa maji.


Nilikua kwenye ndoto lakini nilikua nimejisafisha kidonda changu na kujifunga kitambaa, nguvu ziliiniishia tena na kupoteza fahamu. Kuamka bado nilikua na maumivu lakini tangu siku ile nilishangaa vidonda vyangu vinakauka na ndani ya wiki mbili vilipona kabisa. Nilitoka nnje na Shangazi alishangaa kuniona, hakuniambia chochote, hakukua na pole wala nini lakini tangu siku hiyo akili zangu zilianza kufanya kazi kikubwa, nilijua kuwa natakiwa kuondoka pale kwani lengo la Shangazi yangu ni kuniua.


Unadhani Fatma ataondoka, na je kama ni kuondoka ataondokaje basi nisikuchoshe tukutane sehemu ya tatu.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE! — SEHEMU YA TATU!


Nilipona kabisa na maisha yakaendelea, mwili ulikua na makovu lakini niliamini yataisha, kilichokua kinanisumbua ni Shangazi. Pamoja na kumfanyia kila kitu lakini hakuniacha na amanui, kila siku alikua ananikumbusha kuwa sitakuja kuolewa kwakua nina makovu mwili mzima.  Kwa wakati huo nilikua sijui ndoa ni nini lakini kwa namna alivyokua anaongea nilikua naumia sana. Kila siku nilikua mtu wa kulia na hali hiyo ilinifanya njichukie sana.


“Utaishi peke yako kama mchawi, hakuna mwanaume atakuja kukupenda wewe mbwa!” Alinitukana, wakati huo yeye alikua na miaka kama 30 hivi na alikua bado hajaolewa. Mwanaume pekee niliyekua nikimuona naye ni Martin ingawa alikua hakubali kama ni mwanaume wake, hasa mbele za marafiki zake lakini alikua anampenda sana na kumuonea wivu hata akiongea na mimi. Alikua akikasirika na kunitukana sana matusi amabyo sikuyaelewa.


Nilikua sina amani kabisa lakini sikua na namna, niliendelea kuteseka kwa Shangazi mpaka nilipofikisha miaka 12.  Wakati huo Shangazi alikua ahsamfukuza Martin, sijui waligombana nini lakini alimuondoa nyumbani hivyo kazi za nyumbani zote nilikua nafanya mimi. Nilishakomaa kiakili nakwakua nilikua na umbo kubwa niliweza kuzimudu kazi zote, sikua na namna, ilikua ni lazima kufanya, shnagazi hakuniruhusu kutoka, hakuruhusu kuopngea na mtu, hakuruhusu chochote kile.


Nakumbuka kipindi hicho Bibi yangu alifariki dunia, nialienda na kuniacha nyumbani, hakuruhusu niende popote. Nilishayazoea yale maisha, alikua hataki nionekane na watu, hata akija na rafiki zake nilikua nafungiwa chumbani. Lakini siku moja mchana alikuja na rafiki yake, haikua kawaida yake kurudi mchana hasa siku za kazi, hivyo nilipomuona tu nilikimbilia chumbani kwani nilijua kuwa atakasirika nikionekana pale. Alikuja na kufungua mlango mwenyewe, akaingia na rafiki yake.


Nikiwa chumbani nilishangaa Shangazi anakuja, moja kwa  moja nilianza kutetemeka kwani nilijua kabisa kuwa anakiuja kunipiga. Lakini tofauti na siku nyingine alikuja na kukaa pembeni yangu, alinishika mabenani na kuniambia.


“Usiogope, mbona unaniogopa, unajua mimi ni Shangazi yako, mimi ni damu yako, unaona Baba yako amekufa hivyo mimi ndiyo nimepewa jukumu la kukulea.  Mama yako ameshakukimbia, hakutaki tena….” Aliongea kuhusu Mama yangu kidogo nichanganyikiwa, nilimkumbuka sana, hakuna hata siku moja ambayo nilikua simuwazi Mama.


Sauti yake akiniambia kuwa hawezi kuniacha iligoma kabisa kutoka kichwani kwangu.


“Shangazi wkani Mama hajafa?” Nilijikuta namuuliza, aliniangalia kwa ukali kidogo nilihisi napigwa hivyo nikaanza kuomba msamaha, lakini haikua hivyo.


“Sikupigi, tuache kumzungumzia huyo mtu kabisa, ndiyo Mama ako huko alipo amekufa, msahau, wewe ni yatima na mimi ndiyo nitakulea.  Nimekuja kukuambia kitu kizuri, huyo dada unayemuona hapo ni rafiki yangu, anataka kukupa kazi hivyo anataka uende kuishi kwake.” Aliniambia, kwanza nilikua sijamuona vizuri huyo dada mwenyewe, nilimuona tu wakatio wanaingia tena kwakuchungulia kidogo tu kwani nilipoona wapo wawili kwenye gari nilikimbia kama sina akili zote.


“Wewe hujasoma, huna akili hivyo hutakuja kupata kazi ya maana, halafu wewe ni mbaya angalia ulivyoungua, hata kuolewa hutaolewa, hivyo nenda kafanye kazi kwa huyo dada, ni rafiki yangu, fanya kila kitu anachokuambia, umesikia, ukifanya vizuri ukirudi nitakutafutia kazi nyingine!” Aliniambia, halikua ni ombi, kila wakati alikua akiongea na mimi anahakikisha kuwa najisikia vibaya kwa kuniambia kuwa mimi ni mbaya na sitakaa kuolewa . Alifanikiwa kwa hilo kwani kuna wakati nilikua najichukia mpaka natamani kufa kabisa.


Aliongea kana kwamba ananiomba lakini nilijua kuwa ile ilikua ni lazima,. Nilitingisha kichwa kukubali kisha akaniambia nitoke nnje kumsalimia mgeni. Nilitoka na kumkuta huyo rafiki yake, amabye abada ya kuniona tu alinyoosha mikono akaipanua ili kunikumbatia. Nilibaki nimeganda kwani kwa wakati huop nilikua sijui kile ni nini? Ingawa Mama yangua likua akinikumbatia kwa upendo lakini nilishayazoea mateso kiasi kwamba mtu akinyanyua mikono kwangu ni kama anataka kunipiga.


“Nenda kamkumbatie Mama yako, huyo ndiyo Mama yako mpya, mimi nishamaliza kukulea, ni tabia gani unaonyesha?”  Shangazi alijongelesha hukua kichekacheka, sikua na namna nilimfuata na kumkumbatia,  alikua ananukia vizuri sana, nilijikuta nakaa kifuani kwake kwa muda mpaka pale aliponiondoa.


“Shoga huyu ataweza kweli?” Yule Dada,   “Mama Sam” alimuuliza Shangazi yangu.


“Ataweza sana tu, mbona kazi zote humu dnani anafanya yeye mwenyewe, ataweza….” Shangazi ambaye muda wote huo alikua bado kasimama aliongea huku akikaa.


“Hapana, sizungumzii kufanya kazi, nazungumzia mambo mengine, huyu mbona mdogo sana?” Alimuuliza kwa wasiwasi,  lakini Shangazi hakuonekana kujali.


Aliniangalia kisha akaniita kwa macho, ndiyo Shangazi yangu alikua na jicho lake flani hivi ambalo akikuangalia nalo unaenda tu bila kujijua. Nilimsogelea kwa uoga, bado nilikua nahihisi kama nimefanya kitu kibaya, nilienda kwa kutetemeaka.


“Wewe na wewe, mbona kama unaniogopa, unataka mpaka watu waseme nakunyanyasa?” Aliniuliza, kusema hivy o nilijua chakufanya, nilitakiwa kucheka hata kama sina furaha. Aliona kama nachelewa kumfikia hivyo alinivuta upande wake, nilikua nimevaa kagauni kabovukabovu akakachana kwa juu.


“Unaona , huyu umri mdogo ila matiti yashakua makubwa, hembu angalia, unafikiri yanarefishwa na nini, kashaanza umalaya muda mrefu tu nakaangalia, nakuambia kanaweza!” Alimuambia shoga yake huku akinishika kifuani, ni kweli niliwahi kupevuka na matiti yangu yalishaanza kuwa makubwa ingawa si sana, aliyashika kwa kuyavutavuta huku akinigeuza kwa nyuma.


“Unaona na huku nyma, angalia kalivyojazia, nakuambia kazi kataweza. Fatma mwanangu, Mama yako anasema hutaweza kazi ni kweli?” 


“Nitaweza! Nitaweza! Nitaweza….” Ingawa nilikua sijui kama ni kazi  ani lakini nilijibu kwa haraka, swali  lake lilikua halihitaji maelezo yoyote, Shangazi akisema kitu ni wewe kukubaliana tu na mawazo yake.


“Huna haja ya kutafuta mtu mwingine shoga yangu, haya mambo ni nyeti, ukitafuta mtu mwingine yakivuja utajuta kuzaliwa! Ila huyu mimi na mmudu, hakuna mtu wa kukugeuka, nakuambia mpango utakamilika, wanaume hawa ni wajinga tu nakuambia!” Alimuambia, Mama Sam aliitikia kukubali ingawa alionekana kuwa na wasiwadi.


“Mimi namuona mtoto, huyu si umri wa Sam wangu?” Alimuuliza.


“Wwasiwasi wako tu, huyu mtu mzima, Sam wako mtoto, hal;afu shogaa watoto wakiume  wanachelewa kukua, huyu kashakua Mama, mchukue ataweza kazi. Fatma Mama, nenda kafanye kazi, atakulipa vizuri, atakua anakupa pesa!”  Aliniambia, mimi niliitikia tu kukubali. Sikua najua chochote lakini sikua na namna zaidi ya kukubali.


*****


Ingawa nilikua najua anaitwa Mama Sam lakini sikuwahi kumuona huyo Sam wala mtoto mwingine mpaka naondoka katika ile nyumba. Nilijua nimepelekwa kwaajili ya kufanya kazi za ndani, ni kweli nilienda kufanya kazi za ndani, lakini hakukua na mtoto mdogo wala nini. Ilikua ni nyumba kubwa na ya Kifahari, Baba Sam alikua ni Mwanajeshi wa cheo kikubwa tu na alikua na Biashara zake nyingi, mara nyingi alikua bize na kazi na ni mara moja moja alikua nyumbani.


Kwangu alikua ni mtu wa kujali, baba amabye sikuwahi kuwa naye, aliponiona tu kwa mara ya kwanza aligombana na mke wake.


“Hivi una akili mkweli, huyu si mtoto anatakiwa kuwepo shule, unamleta kufanya kazi gani humu ndani ambayo wewe huwezi kuifanya, kazi ni kujikalia tu halafu unaleta mtoto kufanya kazi.” Niliwasikia wanagombana huko chumbani, waligombana sana na kutukanana, mwisho nilimuona yule Baba akitoka chumbani kwake na kwenda kulala chumba kingine.


Ilikua ni hivyo kila siku akiwpo ingawa hakua akikaa pale nyumbani muda mwingi. Kuhusu Mama Sam yeye alikua na visirani vyake tu, hakua na mkono wa kupiga kama Shangazi lakini anapokua kakasirika alikua akitukana kila mtu kuanzia mume wake pamoja na kijana mwingine mlinzi wa mule ndani. Lakinia kiwa yuko sawa alikua ni mtu wa kujali, kunionyesha upendo, alikua ananinunulia vizawadi, ananitopa out yaani anakua Mama kabisa, nilikua nafurahia na kujiona kama niko peponi.


Siku moja nilitoka naye, akiwa kwenye gari simu yake iliita, aliikata, lakini baadaye ikaita tena, akakata, ila ikaita mara  ya  tatu ndipo akapokea.


“Nimekuambia nitafanya, leo usiku nitafanya, mume wangu alisafiri sasa unategemea nini? Mimi ningefanyaje bila yeye kuwepo!” Alilalamika, walibishana sana na upande wa pili, hasira zilimpenda, akili zikamchanganya nusu agongea lakini tulifika salama.  Mara nyingi akiwa na hasira namna ile anakua mkali, akishamaliza kuongea na simu anakua na kisirani hivyo simuongeleshi, lakini siku ile ilikua tofauti alizidi kunichangamkia na kila dakika alikua ananiuliza kama niko sawa.


“Unapenda maisha tunayoishi?”  Aliniuliza, alinipeleka sehemu ina michezo ya watoto, mimi kwangu sikuifurahia kwani nilikua sijaizoea na sijioni mtoto tena. Kutokana na nilivyolelewa na Shangazi yangu nilijua moja kwa moja kuwa hilo halikua swali bali maelekezo, nilipaswa kukubaliana naye kuwa nafurahia aina ya maisha tunayoishi.


“Basi kuna kitu nataka unifanyie tukifika nyumbani, si utaweza?” Aliniuliza, bila kujiuliza kama ni kitu gani nilikubali, nilijua ni rafiki yake na shangazi hivyo kama nikikataa basi ni kipigo, ingawa alikua hajawahi kunipiga lakini nilijua anaweza kumuambia Shangazi amabye angeweza kuniua.


Tuliendelea kula Icecream na michezo mingine ya watoto, yeye alidhani nafurahia kumbe wapi, lakini sikua na namna zaidi ya kuilazimisha furaha. Tulirudi nyumbani jioni, siku hiyo tulimkuta Baba, hakuepo kama siku tatu nyuma. Walisalimiana kwa chukichuki flani, nilijua wamegombana, basi mimi niliingia ndani na kuanza kufanya kazi za ndani, Mama alikuja akapika na kuandaa chakula. Kwenye kula kila mtu alikua kivyake, Baba alikua akijaribu kunichekesha lakini nilona kabisa kuwa hawakosawa.


Baada ya chakula Baba aliinngia chumbani kulala. Mama alinifuata na kaunza kunipa maelekezo.


“Leo sitaki ulale kwenye chumba chako, nataka ulale chumba hiki, usifunge mlango wewe ingia na lala. Kitu chochote kikitokea basi piga kelele, hii nyumba ina mashetani hivyo piga  kelele sana!” Aliniambia, sikujua anataka kufanya nini lakini niliingia katika kile chumba nilichoelekezwa, kilikua ni chumba cha wageni ambacho mara zote   wakigombana na Baba basi hukimbilia kule.


Niliingia kulala lakini sikupata usingizi, nilikua naogopa kuhusu vitu vibaya mpaka sababu  ya yeye kuniambia nipige keleel. Sikulala mpaka usiku wa  manane, nilishangaa mlango  unafunguliwa, mtu alitaka kuwasha ta a lakini ilikua haitaki kuwaka. Nilibaki natetemeka, nusu kujikojolea, nilitamani kupiga kelele lakini niliogopa sana, mara nikashangaa kitu kizito kinanidondokea mwilini!


“Mamaamamaam!!” Nilijikuta napiga kelele, alikua ni Baba kwani baada ya mimi kupiga kelele alinyanyuka na yeye kuanza kupiga kelel e si za uoga bali za kuuliza wewe ni nani? Nilijikuta nazidi kupiga kelele kama nilivyoelekezwa, kufumba na kufumbua Mama Sam huyu hapa na yeye akaanza kupiga kelele.


“Anabaka mtoto! Anabaka mtoto! Anabaka mtoto!” Aliendelea kupiga kelele, mume  wake alishatoka chumbani, yeye aliingia na kunishika, akanichania nguo nilizokua nimevaa kisha akanitoa nnje,  aliniambia niendelee kupiga kelele huku nayeye akipiga kelele kuwa mume wake alikua anataka kunibaka!


Unadhani ni nini kinaendelea? Kwanini Mama Sam anataka mume wake kuonekana kama anataka kumbaka Fatma? Je nini kitatokea kwa Fatma, usikos Sehemu ya Nne.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE— SEHEMU YA NNE


Baba Sam alipoona vile alishtukia mchezo, harakaharaka alikimbilia mpaka mlangoni. Akafunga mpango ili mke wake asitoke nnje, lakini bado mke wake alikua akipiga kelele kuashiria kuwa ninabakwa. Mimi niliacha kupiga kelele nikanyamaza kimya, wakati tunabaki tunashangaa kuna watu waligonga mlango, ilikua ni usiku na kwa zile kelele haikua rahisi kwa majirani kusikia kwani Baba Sam alikimbilia kufungua mpango na nyumba ilikua kubwa sana.


“Huu ndiyo mpango wako, kunijazia watu kweli?” Alimuuliza mke wake ambaye bado alijifanya kupiga kelele.


“Mpangp gani? Mpango gani? Nakuuliza mpango gani, mwanaume mshenzi kabisa wewe, yaani unataka kumbaka mtoto wa watu halafu unajifanya mpango!” Mama alijifanya kulalamika huku akijiliza uongo, alikuja na kunikumbatia kama vile ananipa pole.


“Amekufanya nini? Amekuumiza, na tunaenda polisi, amekuingilia kinyume na maumbile?” Alinuliiza huku aknivua chupi na kuniangalia sehemu za nyuma. Mimi nilikua sawa, sikua nikijua kitu kilichokua kinaendelea.


“Hapana Mama Baba hajanuguza popote mimi nimepiga tu kelele kama ulivyoniambia….” Nilijikuta naongea ukweli, kwa wakati huo sikuona kama nakosea, Mama alinitandika kofi na kunisukumiza chini, kidogo ni dondoke lakini Baba aliruka na kunikamata.


“Hivi wewe mwanamke una akili kweli, yaani kisa unataka kuniacha ndiyo unamuingiza na huyu mtotyo, unataka unisingizie na kosa la kubaka! Humfikirii huyu mtoto, kama ni talaka tu si useme!? Baba alimuuliza kwa hasira, bado watu waliendelea kugonga, wakati Baba kanishikilia Mama alikimbia na kufungua mlango, vijana kama saba hivi amabo walishika fimbo na wengina marungu waliingia.


“Pigeni kelele mume wangu anambaka binti yangu, ni mtoto wa rafiki yangu alikuja kunisalimia.”  Mama aliwaambia, wale vijana ambao wote walikua ni mabaunsa waliingia na kumfuata Baba, walishapanga kumpiga, Mama alitoka nnje na kuanza kupiga kelele kama anaomba msaada kwa majirani.


Walitaka kumvamia Baba pale chini alipokua kanishikilia, lakini sijui alirukia wapi na kuwakwepa. Aliingia chumbani na kukaa kama dakika moja hivi, kisha akatoka.


“Nawewe ulikua kwenye huu mpango, naona kaficha na Bastola yangu?” mimi hata nilikua sijui chochote, wale vijana walimfuata tena, walikua wanamzuia wakitaka kumbananisha kwenye kona. Sijui nini kilitokea lakini aliwakwepa, alikimbia mpaka mlangoni, lakini badala ya kutoka nnje aliufunga mlango kisha akawageukia wale vijana ambao bado walikua wamesimama wanamuangalia wanataka kumpiga.


“Hamtatoka humu ndani, kutoka kwenu ni labda mimi niwe maiti au nyie mtoke mkiwa maiti.” Aliongea, huku akicheka, wale vijana nao walicheka na kuonyesha dharau flani.


“Mwanangu, ingia ndani, hiki ninachotaka kukifanya hutakiwi kukiona, ingia ndani jifungie, wewe bdao mtoto hutakiwi kuona ninachoenda kukifanya.” Aliniamrisha, niliingia chumbani kwa uoga na kujifungia, kuingia tu nilianza kusikia kelele, sikujua kilichokua kikiendelea ila dakika kama tano hivi. Nilisikia watu wengi wakiongea kwa nnje, Baba alikua kama anawaelekeza.


“Nyie mmeitwa kuwa ninabaka binti mdogo, hembu waulizeni hawa watu kuwa kwangu wamekuja kufanya nini, si wenyeji wa mtaa huuu ndiyo niseme kuwa wamasikia kelel wakaingia, nyumba ilikua na geti tena kubwa tu, waulizeni walikuja kufanya nini?” Nilimsikia Baba akiongea kwa hasira, watu mmoja wa wale vijana aliwaambia kuwa yeye alikuja pale kwakua aliambiwa kuna kazi ya kumiga Baba, wasimuue lakini wampige ili kuonekana kama ni wananchi wamempiga baada ya kusikia kelele kuwa anataka kumbaka mtoto.


Alielezea kuwa walikua wamelipwa hivyo walikua hawajui sababu ni nini? Baba aliniita kutyoka ndani, kulikua na watu wengi ingawa si sana, wale vinana walikua wamelala chini hoi na Baba alikua vizuri tu.


“Naomba mumuulize huyu binti kama nimemgusa au nimemfanya chochote.” Baba aliwaambia wale watu, waliniuliza na mimi bila hiyana nilisema ukweli kuwa Baba hajawahi kunigusa na Mama aliniambia nilale kile chumba ila kitu kikiniusa usiku nipige kelele.


“Mmesikia, sijamgusa huyu binti, basi ondokeni maana mengine hayawahusu, kuhusu mke wangu niachieni nitamalizana naye mwenyewe.”


“Hapana, lakini mimi mwenyekiti wa mtaa, hili ni suala la kisheria, lazima twende polisi, hawa vijana wamekuja kwenye mtaa wangu…” Baba mmoja alijaribu kumuelezea lakini Baba alimkatisha.


“Hapana, huna haja ya kuhanagika mzee wangu, nishapiga simu vijana wangu wanakuja, hawa vijana nina uhakika wakitoka huko hawatakuja kumdhuru tena mtu mwingine. Watakua raia wema sana, kuhusu mke wangu huyu na mmudu, ni mke wangu na hakuhusu.” Baba aliongea kwa ukali kidogo hukua kiwalazimisha watu kutoka, walitoka akafunga mlango tukabaki kule ndani mimi Mama na wale vijana saba.


Hakuongea kitu, alikaa akma anasubiri kitu, Mama alikua akitetemeka kwa uoga, wale vijana walikua hoi chini. Baada ya kama nusu saa hivi mlango uligongwa, Baba alienda kuufungua, waliingia vina watatu ambao walikua wamevaa sare a jeshi.


“Vijana wangu, hawa watu watawapa lifti kuwarudisha makwenu.” Aliwaambia wale vijana saba ambao baada ya kuona tu wale wanajeshi walichanganyikiwa na kuanza kuomba msamaha huku wakipiga magoti.


“Hakuna shida, nishawasamehe ila sasa hivi ni usiku na nyie mmechoka sana, hivyo ondokeni na hawa vijana wataawapa lift, wapelekeni nyumbani hawa vijana wangu hawana shida.”


Aliwaambia lakini hawakumuamini, waliendelea kumuomba msamaha ila yeye alisisitiza kuwa waondoke. Waligomagoma lakini wale wanajeshi waliwashika kwa nguvu na kuwatoa nnje. Baba alifunga mlango, akaingia chumbani kwake kulala bila kumsemesha Mama kitu chochote. Mimi na Mama tulibaki sebuleni, Mama alikua akiniangalia kwa hasira lakini hakufanya kitu chochote, alikua kama kachanganyikiwa, usiku ule alizunguka nyumba nzima, alikua aingia chumba hiki anatoka,a nataka kuingia chumbani kwake alipokua Baba lakini anashindwa, yaani alikau kama chizi. Mpaka kunakucha alikua hajafanya chochote.


Asubihi kabisa Baba alitoka kuwa anaenda kazini, kwa kawaida akiwa anaenda kazini huwa havai nguo za kijeshi, tangu mimi kuingia hapo nilikua sijamuona kavaa hizo nguo, mara nyingi alikua anavaa zake kawaida basi. Ila siku hiyo asubuhi alivaa nguo zake za jeshi na kutoka. Bado wote tulikua sebuleni, mimi siajalala kwakua Mama alikau hajalala.


“Unafahamu kwenu?” Alikuja na kuniinamia, nilimuangalia huku nikitetemeka, niliogopa sana, alinitoa hofu.


“Huna kosa lolote, huna haja ya kuogopa, kama unafahamu kwenu niambie nikupeleke, hatuhitaji tena mfanyakazi….” Sikua na kitu cha kumjibu nilikua namuangalia Mama. Nilikua natetemeka, Mama naye alikua anatetemeka, alimsogelea mume wake na kumpigia magoti kuomba msamaha.


“Najua ulichikua unataka ni mali, najua kila kitu, si ni mali ili uje kuishi na mwanaume wako?” Alimuuliza, Mama alijifanya kukataa. Unapojaribu kufanya unyama hakikisha unakua mnyama, nahisi uliniona kama mume ila hukujua kuwa mimi ni nani? Hivi unadhani kwakua unanitukanatukana nakuangalia mimi ni mjinga kiasi hicho, nimekuvumilia kwa muda mrefu lakini sasa hivi imefika mwisho, si ni mali ulikua unazitaka, basi jua kuwa naondoka, jinsi unavyoniona hivi ndiyo naondoka, nakuachia kila kitu, sichukui kitu chochote, hii nyumba uliyokua unaitaka nakuachia ili uje uishi na huyo mwanaume wako.


Mchana watamleta mwanaume wako, nikuambie tu hawajamgusa popote na wala hawajamfanyia kitu chochote kibaya, wle vijana waliongea kila kitu hivyo huna hata haja ya kujitetea, naondoka sitarudi tena humu ndani tutakutana tu mahakamani kwenye talaka. Sitashirikisha mtu yoyote na sitaki msamaha wako, huwezi kuwa mke wangu tena, naomba uelewe kuwa bado nakupenda lakini siwezi kukuamini tena hivyo siwezi kuishi nawewe tena.” Baba aliongea na kuondoka zake alimuacha Mama akiwa analia huku akiomba msamaha lakini hakusikilizwa.


Mchana kwenye saa sita hivi bado nilikua nipo pale, mlanmgo uligongwa, mama alifungua kwa uoga, aliingia Kaka mmoja ambaye walionekana kujuana, nyuma yake kulikua na wanajeshi wawili.


“Mama tumemleta huyu hapa, Baba katuambia kuwa aje na vitu vyake viko nnje.” Waliongea, kabla hata Mama hajajibu kitu chochote vijana wengine ambao pia walikua wamevalia nguo za kijeshi walikuja na kuanza kuingiza mabegi, kitanda na sofa moja ndani. Yule kijana alikua amesimama anatetemeka, alionekana mzima hakuonekana kuumia popote. Waliingiza vitu ndani wakavipeleka chumba ambacho kilikua tupu kisha wakatoka na kumuaga Mama, walimuacha yule kijana pale.


“Kwanini hukuniambia kuwa mume wako ni mwanajeshi tena ni mtu mkubwa?” Yule kijana alimuuliza Mama alionekana kuchoka sana kwani hata ongea yake ilikua ni ya mtu aliyechoka.


“Ingesaidia nini? Ningekuambia kuwa ni mwanajeshi ungekubali kutembea na mimi?” Mama alimuuliza kwa hasira.


“Sikutaki, sitaki kuendelea na wewe, usinijue, narudia usinijue, sitaki chochote na wewe, naondoka usinitafute naenda kuanza maisha yangu upya!” Yule Kaka aliongea kwa hasira, aliondoka kwa kukimbia, hakuchukua kitu chake chochote, aliondoka na kuniacha mimi na Mama pale.


“Unaangalia nini? Hembu kusanya vitu vyako nikupeleke kwa Shangazi yako mshenzi mkubwa wewe….” Alinitukana sana, nilikusnaya vitu vyangu, nikatoka, nilimkuta naye ana begi, sikumuuliza chochote nilitoka mpaka kwenye gari. Akafunga milango tukaenda m[paka dukani kwa Shangazi ambaye alikuja kwenye ngari, alimuelezea kila kitu kilichotokea, Shangazi naye aliogopa.


“Kwahiyo unarudi kwako?” Alimuuliza.


“Hapana, yule mwanaume simuamini, nahisi anaweza kuniua, simuamini kabisa nataka nikae kwako kwa muda nikijipanga….”


“Ukae kwa nani? Hivi una akili kweli, huyo mwanaume unataka ajue kuwa mimi nahusika kwa upuuzi wako, Mama una kwenu nenda!” Shangazi alimkatisha, hakutaka kabisa kujihusisha na Mama Sam.


“Lakini wewe ndiyo ulinishauri kuwa kama nikimsingizia kesi ya kubaka basia naweza kufungwa na mimi kubaki na kila kitu. Mimi bado nampenda mume wangu, wewe ndiyo ulisababisha mpaka mimi niakchepuka, mume wangua likua ananiopa kila kitu….”


“Mama una akili zako, wewe ndiyo ulikua unalalamika kuwa mumeo mnakaa miezi sita bila kugusana, sasa ulitaka mimi nifanye nini? Una akili zako na maisha yako, nimekuambia kuwa siwezi kuishi na wewe, hivi unafikiri mume wako akijua kuwa mimi nahusika na ujinga wako atanielewaje? Mume wako ananiamini sana, alikua ni rafiki wa marehemu Kaka yangu, aisee hapana, siwezi kukubali huu ujinga, hapana aisee!”


Waligombana sana lakini mwisho Shangazi alinishusha kwenye gari na tukaondoka. Yule dada alibaki kwneye gari kama nusu saa hivi, baadaye alishuka huku akilia lakini Shangazi alipoona kuwa anamfuatafuata basi aliingia kwenye gari na kuondoka, hata mimi aliniacha pale dukani. Mama Sam kuona vile aliondoka zake, jioni Shangazi alikuja nakunichukua mpaka nyumbani. Hakuniuliza chochote, alikua tu kakasirika na mimi sikuongea kitu kwani nilihofia kupigwa.


****


Baada ya lile tukio Shangazi alikua kama amebadilika flani, aliku anaongea na mimi vizuri na hakua akinipiga tena, sikujua sababu ya mabadiliko yake lakini alionekana kama ni mtu mwenye furaha. Lakini bado alikua hataki nionane na rafiki zake au wageni waliokua wakija pale nyumbani. Tulikua tukiishi wawili tu hivyo kazi zote za ndani nilikua nikifanya mimi, alikua akiingiza wanaume usiku, akiwa namwanaume basi mimi nilikua nabaki chumbani na asubuhi nilikua siruhusiwi kutoka mpaka yeye kujakuniamsha ndiyo nitoke. Mchana kama alikua anashinda na mwanaume bai mimi nilitakiwa kukaa ndani bila kutoka na chakula alikua akiniletea, ila hata kama nikisikia njaa nayeye hajapika basi nililazimika kuvumilia.


Lakini siku moja tu Shangazi aliniambia nikusanye vitu vyangu, aliniambia nimepata kazi hivyo anataka niondoke kufanya. Wakati huo nilikua na maika 15 na Shangazi alikua akiishi na mwanaume ambaye ni mtu mzima lakini alikua hafanyi kazi yoyote. Basi niliondoka akanipeleka kwa Kaka mmoja, haikua nyumbani bali ilikua k3wenye gari, alinipandisha kwenye gari na huyo Kaka na kuniambia kuwa naenda kufanya kazi za ndani.


Sikua na chakuongea, lakini safari haikua fupi kabisa, ilikua ni safari ya suiku mbili kwani tulichelewa sana kuondoka Dar hivyo tulilala njiani ambapo huyo Kaka alinipangishia chumba changu. Baadaye ndipo niligundua kuwa tumekuja Mwanza, huyo kakaa linipeleka nyumbani kwake, nikaanza kufanya kazi hapo. Alikua akiishi na familia yake, mwanzo mambo yalikua mazuri sana, mke wake alinipenda na kunichukulia kama mtoto wake, huyo Kaka naye alikua ni mstaarabu, hakunigusa wala kuongea na mimi vibaya.


Kazi za mule ndani hazikua nyingi sana, huyo dada alikua ni mjamzito, hakukua na mtoto hivyo sikua na kazi nyingi sana. Lakini siku moja nikiwa nimelala chumbani, dada alikuja na kugonga mpango wangu. Alikua na mimba kubwa, yule Kaka alikua kasafiri.


“Nimeogopa kulala mwenyewe hivyo nataka tulale wote….” Alianza kujiongelesha, mimi sikujali, niliona ni mwanamke mwenzangu na kwakua alikua ananionyesha upendo basi nilikubali.


Lakini nilishangaa anavua nguo, sikumuangalia, alivua nguo na kupanda kitandani, kishaa kanifuata na kujifunika blancketi nililokua nimejifunika.


“Mbona unalala na nguo?” Aliniuliza baada ya mwili wake kugusana na mwili wangu.


“Nimezoea hivyo, siwezi kulala uchi….” Nilimuambia, aliniambia kuwa yeye hawezi kulala na mtu ambaye amevaa nguo hivyo nivue nguo ilniambia kama ananiamrisha, kwa uoga nikiwa sina hili wala lile nilivua nguo. Basi alifurahi na kuanza kunikuimbatia, mwanzo niliona kawaida, lakini nilishangaa anaanza kunishikashika kwenye kifua ananichezea, nilishtuka na kumuondoa.


“Unajisikiaje? Hupendi?” Aliniuliza, kwa uoga nilinyamaza, nilishazoea ukiulizwa kitu na mkubwa kama hupendi unanyamaza au unafanya kama anavyotaka. Alihisi sijisikii vizuri, akanyanyuka na kuwasha taa kisha akakaa kitandani, tumbo lake kubwa ujauzito wa kama miezi sita hivi ananiangalia,a likua uchi wa mnyama, mimi nilijaribu kujifunika na Blanketi lakini hakutaka, alinitunua.


“Una mwili mzuri sana, sijawahi kuona mwanamke mzuri kama wewe, nimevumilia sana lakini nimeshindwa, nakupenda sana, una mwili mzuri, alianza kuongea.” Nilsihajua mambo ya mapenzi na nilijua kuwa watu wanaotakiwa kupendana ni mwanaume na mwanamke, nilishangaa ni kwa namna gani mwanamke anakuja na kunipenda.


“Kila nikikuona nachanganyikiwa, leo nimeshindwa, mume wangu hayupo, nyumba katuachia sisi wenyewe. Njoo, hembu nishike matiti, shika vizuri….” Aliniambia huku akinifundisha naman ya kumshika. Nilimshika nikiona kama labda namkandakanda lakini nilishangaa anapiga keleel, anmaniambia shika zaidi, anaonyesha anapoata raha. Mimi sikua na sikia chochote, niliona kama kushika tu mwili wangu, nilikua namshangaa namna alivyokua anapiga kelele, ghafla alinifuata na kunikuambatia akaanza kunilambalamba mwili mzima, alinambia nifanye hivyo lakini nilishindwa, bila kujijua nilijikuta nakasirika.


Tulikua tumekaa kitandani, nilijisogeza pembeni ili kumkwepa, lakini alinisogelea huku akinibembeleza.


“Usiniache njiani, niasidie njoo usiniache njiani….” Aliniambia huku bado akinisogelea, nililazimika kurudi nyuma nakujibanza ukutani, nilisimama kutaka kuruka lakini naye alisimama, akaja tena kama anataka kunikumbatia, bila kudhamiria nilijikuta napandwa na hasira, nilimsukuma, kwakua alikau kasimama juu kiotanda alipepesuka kidogo, akashindwa kujibalansi akadondoka chini Puu!


“Nakufaaa!” Nilisikia akipiha kelele kwa sauti moja, sikumsikia tena likua amedondoka kichwa kimegonga kwenye stuli ya kioo ambayo ilikua pale chumbani. Damu zilianza kumtoka kichwani kwenye utosi, nilijikuta nimeganda pale tu kitandani sijui nifanye nini. Alikua hajitingishi na hata nilipojaribu kumuita akubaki kimya, nilikaa kama dakika tano hivi ndiyo nikazinduka kutoka kwenye bumbuwazi, nikamfuta kujaribu kumnyanyua lakini alikua hanyanyuki.


Safari ya Fatma nnje ya Shangazi yake ndiyo kwanza inaanza, ana miaka 15 na ameondoka wkao, unajua nini kitatokea? Bai usikose, itaendelea.


ITAENDELEA…


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE! —SEHEMU YA TANO


Nilimuona katulia, nilijua sijafanya kitu chochote, kwakua sikuweza kumnyanyua basi nilitoka nnje kutafuta majirani. Ilikua ni usiku lakini sikuogopa, niliwagongea majirani wawili na kuwaambia Mama kadondoka na Baba hayupo, basi walikuja na kumsitiri kisha kuangalia kama alikua amekufa au la. Bahati nzuri alikua badoa napumua, walimchukua na kumpeleka hospitalini, akiwa njiani alizinduka na kuwabia kuwa hajaumia sana lakini bado walilazimishia na kumpeleka hospitalini.


Kichwani alikua kapasuka, akashonwa nyuzi sita, walimuangalia mtoto alikua vizuri tumboni, akaambiwa kuwa hakua na shida ila walitaka kumuangalia kwa usiku ule ili kuone kama hali itabadilika. Basi mimi nilikua naye na ndiyo nilibaki naye mpaka asubuhi kwani hata kurudi nyumbani peke yangu nilioghopa. Asubuhi aliruhusiwa na kurudi nyumbani.


“Unajua kidogo uniue? Nikimuambia mume wangu kuwa ulitaka kuniua mimi na mtoto atakachokufanyia hata mimi sijui?” Aliniambia, ilikua ni mchana, baada ya Baba kuambiwa kuwa Mama kadondoka alirudi siku hiyo hiyo. Alikua anampenda sana, alikua Dar lakini alipanda ndege ya mchana an jioni alikua Mwanza. Wakati huo mimi nilikua jikoni napika, Baba alikua chumbani kapumzika na Mama alinifuata jikoni.


“Nisamehe Mama, mimi sikupanga kukuumiza…” Nilianza kuomba msamaha huku nikipiga magoti.


“Nikusamehe na wewe utanifanyia nini?” Aliniuliza, sikua na jibu, sikua na kitu cha kumpa na kwa wkaati huo kwakweli nilikua sielewi kabisa ni kitu gani anataka.


“Nitakupa mshaara wangu wote wa mwezi huu?” Nilimuambia kuhu nikitetemeka, kwanza alicheka kwa dharau, kisha kanishika mikono na kuninyanyua, alisimama mbele yangu na kupitisha mikono yake kwenye matoto yangu, alianza kuyabonyeza huku akinisifia.


“Unanipa mshara wako, mshaara wenyewe tunaokupa ni elfu kumi kwa mwezi, nyingine zote anachukua Shangazi yako unataka kunpa elfu kumi mimi?” Aliniuliza huku akiendelea kunitomasatomasa matiti yangu. yeye alikua akifanya hivyo anafunga macho kwa raha lakini mimi akili yangu haikua pale kabisa. Kwa wakati huo nilikua sijui hata anafanya nini, sikua nikijua mambo ya kusagana au mapenzi ya jinsia moja, ila yeye alionekana kufurahi.


Niliwaza nakuona kweli kuwa msahara wangu si kitu, mshaara wangu kwa mwezi amabo niliambiw akuwa nitalipwa ilikua ni elfu hamsini, kwa wakti huo ilikua ni nyingi sana kwa mtu kama mimi ambaye nilikua sijawahi kushika hata shilingi elfu mbili ya kwangu. Lakini kitu cha ajabu ni kuwa, shanagzi yangu pamoja na kuwa na pesa nyingi, kuchukua pesa nyingi za Baba na kumiliki mali zote hakutaka niwa na pesa.


Alikubaliana kuwa, shilingi elifu arubaini atakua anatumiwa yeye kwa madao kuwa ananiwekea na mimi za kwangu zitakua ni elfu kumi.tena zenyewe aliwaambia kuwa wasinipe mpaka niwe na shida sana, waniweekee kwani hakutaka kabisa mimi kuwa na pesa.


“Kama unataka nisiongee inabidi ufanye kila kitu ninachotaka mimi!” Aliniambia huku akinyanyua gauni lake alilokua amevaa, ndani hakua amevaa kitu.


“Mbona nafanya kila kitu Mamas, mbona kazi zote nafanya!” Nilimuambia.


“Hapana Baaby, si kazi, hizo hata mimi nafanaya, mimi nataka tufanye mengine, nataka uwe mpenzi wangu, kuna mambo mengi nitakufundisha sitaki umuambie mume wangu, sitaki umuambie mtu yoyote. Hata Shangazi yako sitaki umuambie, ukimuambia mimi nitasema kuwa ulitaka kuniua, nitakupeleka polisi utafungwa. Lakini kabla ya kufungwa naamini kuwa mume wangua naweza kuwa ameshakuua, aisee mume wangu ni mkali sana!” aliniambia, mimi niliabki tu na shangaa, nilikua sijui mambo ya kuwa mpenzi, nilitamani kucheka kwani nilimuona kama kachanganyikiwa.


“Mimi ni mwanamke, sasa nitakuaje mpenzi wako, mimi najua mwanaume na mwanamke ndiyo wanakua wapenzi?” Nilimuuliza, lakini hakujibu kwa mdomo, alijibu kwa matendo, alinyanyua gauni lake mpaka juu, akaniambia niiname na kuanza kumnyonya sheemu zake za siri.


“Hapana, hata kama nio kufa nife!” Niliwaza wakati anajaribu kunisukumizia nilikua nahisi kinyaa, alipoona nasitasita aliniambia nimfuate chumbani kwangu. Tuliiingia ambapo aliniambia mimi nicvue nguo ili anifundishe namna ya kufanya, basi nilivua nikiwa sijui anataka kufanya nini, ile kuvua tu aliniparamia,a kanilaa kitandani kisha yeye ndiyo akaanza kuchezea sehemu zangu za siri.


Mwanzo niliona kawaida tu, sikusikia kitu chochote lakini kadri alivyokua akiendelea nilianza kupata msisimko wa ajabu, nilisikai raha mpaka nikawa napiga kele. Kuona vile alisiisha, akaniambia nsiipige kelele sana kwani mume wake yupo chumbani. Aliniambia name nimfanyie kama alivyokua ananifanyia lakini nilishindwa, niliogopa kama atakasirika lakini hakukasirika, alinikalisha kitandani na kuanza kunielezea kuwa  ni kawaida.


“Hii ni mara yako ya kwanza, utaona kama ni uchafu lakini jua kuwa utapenda huko mebleni na hutaacha. Kwani una miaka mingapi?” Aliniyuliza, mikono yake ilikua kiunoni kwangua kinishiakshika.


“Nina miaka 15.” Nilimuambia.


“Basi ni kama mimi, mimi nilianza na maiak 14 nikiwa sekondari, kuna dada alinifundisha na mpaka leo napenda, si kitu kibaya, ila unahitaji mtu mwenye akili kufanya naye, utajua tu kila kitu. Nimeolewa lakini mume wangu simfurahii, wewe unaonekana kama una akili, kwanza umzuri, unajielewa, unanisikiliza.


Kuna mwenzako nilijaribu kufanya naye basi kutwa nzima akawa analia,  ikajua kuwa mume wangu atajua nikamfukuza, nikaleta mwingine lakini alikua ni cmhafu, absi nikamfumkuza, mume wangu analalamika kuwa nina mdomo sikai na wafanyakazi lakini ukweli nikuwa ananiletea wafanyakazi wabovu. Angalia ulivyomzuri, hembua ngalia.” Aliongea hukua kinishikashika, nilijisikai vizuri alliponisifia kuwa mimi ni mzuri kwani tangu nakua shangazai alikau ananiambia kuwa mimi ni mbaya siwezi kupata mwanaume wakunioa.


“Hilo kovu ulifanya nini?” Ainiuliza, nilijisikia viabya kidogo nisimjibu, Kovu halikua kubwa sana lakini ndiyo ulikua ulemavu wangu, kila siku Shangazi alikua akinikumbusha kua siwezi kupata mwanaume wakunioa kwakua tu nina kovu, ananiambia nimbaya, nilishangaa nayueye kaliona.


“Inamaana mimi ni mbaya, hunipendi kwakua nina kovu, mbona ulikua unasema mimi ni mzuri?” Nilijikuta nauliza kwa hasira mpaka yeye mwenyewe akashtuka, alijua nimejisikia vibaya, alitabasmau na kuniambia.


“Nimuliza kutaka tu kujua, tena nalipenda.” Palepale aliiga magoti mbele yangu na mimba yake akaanza kupitisha ulimi wake kwenye kovu langu. Nilipata raha ya ajabu na kuanza kupoga kelele tena. Aliniacha na kuniambia itabidi aniletee TV chumbani kwangtu kwani napiga kelele sana ili wakati tunafanyamapenzi basi tuiwashe. Sikuelewa alipokua anaseama kufanya mapenzi lakini nilifurahi kuwa ananipenda na kafurahia kovu langu, kusema ukweli kwa namna flani nilijisikia vizuiri na kutamani aendelee kunishika.


***


Mpaka anajifungua mimi na Mama hatukuahcana, ulikua ndiyo mchezo wetu wa kila siku. Baba akisfiri basi tunajimwaga mpaka chumbani kwake, akiwapo anakuja chumbani kwangu na kulala asubuhi anarudi kwa mume wake bila kugundulika.


“Nataka kujua, hivi nikiondoka kuna mtu anakuja hapa, maana Mama yako simuelewielewi?” Nakumbuka siku moja Baba aliniuliza, ilikua ni kama wiki moja hivi kabla ya Mama kujifungua. Walipanga mama kwenda kujifungulia kijijini lakini Daktari alisema kutokana na hali yake kutokua nzuri basi asisafiri.


Kwa maana hiyo alibaki na kujifungulia Dar, baba alikua ni mkimya, lakini baada ya kuanza mapenzi na mimi Mama alibadilika sana, alikua mkali kwa Baba, kila sikua alikua akitafuta sababuu ya kugombana naye ili kutoroka na kuja chumbani kwangu kufanya mapenzi. Kwangu mimi alikua mzuri, alikua ananijali, alinibadilishia mavazi, akawa ananivalisha nguo za kijanja, suruali na vimini, aliniambia kuwa anapenda hivyo.


Mimi pia nilifurahi, maisha yalikua mazuri na sikuishi kwa mateso tena.


“Mimi sijui, hakuna mtu….” Nilijibu kwa uogauoga kwani nilihisi labda Baba amegundua kuwa ninatembea na mke wake. Baba aliniangalia kwa wasiwasi, ni kama alihisi kuna kitu.


“Kuna kitu, mbona huniambii, kuna mtu yuko naye, wewe si ni shoga yake, niambie?” Aliniuliza tena lakini nilimuambia mimi sijui kitu. Aliondoka na hakuniuliza tena mpaka siku Mama alijifungua. Alijifungua kwa oparesheni hivyo alibaki hospitalini kwa muda. Pale nyumbani alikuja mdogo wake na Mama, kwaajili ya kumhudumia, lakini pia alikuepo na Bibi, kwa maana ya Mama yake na Mama ambaye alikuja kumhudumia.


Wakiwa wameenda hospitalini kumuona Mama nilibaki mwenyewe nyumbani, nikijua Baba yuko kazini nilivaa khanga moja tu na kuanza kufanya usafi wa ndani. Sikujua kama alikau chumbani na kwasababu Mama alitegemewa kutoka hospitalini siku ile basi Bibi aliniambia nihakikishe nafanya usafi chumbani kwa Mama. Niliingia na kuanza kufanya usafi bafuni, sikujua kuwa wakati napita Baba alikua amelala na hakunisemesha.


Niliingia bafuni, nikafanya usafi, wakati natoka ili kuendelea na usafi wa chumbani nilimuona Baba amesimama pembeni yangu kavaa nguo ya ndani tu. Kuniona alijifanya kushtuka na kuniuliza nilikua nafanya nini chumbani kwake.


“Mimi nilikua nafanaya usafi, samahani sikujua kama uko ndani.” Nilianza kumuomba msamaha huku nikifunga macho nikismuone, nilikua naona aibu kwa naman alivyokua amevaa.


“Unaenda wapi?” Aliniuliza kwa ukali kidogo, nilimuambia kuwa nilikua natoka kwenda kufanay usafi sebuleni ili kumpisha chumbani lakinia linikatalia.


“Hembu kaa hapa, nataka uniambie kwanini mke wangu amebadilika, tangu wew ekuja hapa mke wangu ahtaki hata kufanya mapenzi na mimi, anasingizia mimba lakini namjua yule mwanamkea napenda ngono sana na kila sikua alikua analalamika kuwa simridhishi, ila umekuja tu ghafla halalamiki, nataka kujua, kuna mwanaume gani anakuja humu ndani? Au anatoka mimi nikitoka?” aliniuliza kwa ukali, nilibaki kimya nikitongisha tu kichwa kumuambia kuwa mimi nilikua sijui kitu chochote.


“Unaona, hembu niangalie, miezi minne sasa simjui mwanamke!” Alilalamika, sikua na chakumjibu, nilinyanyuka ili kuondoka lakini alinishika, akanivuta nikamkalia, uume wake ulikua ushasisimka, sikusikai chochote, alinikumbatia na kuniuliza.


“Ulishawahi kufanya mapenzi?” Alininong’oneza kwenye sikio huku akinitomasatomasa, kunishikashika sehemu mbalimbali nilijikuta nachanganyikiwa. Hakusema kitu tena, aliingia vizole vyake sahemu zangu za siri na kuanza kunichezea.


“Umeshakau mkubwa, itabidi uwe mke wangu, yeye si anajifanya kuwa hataki kunipa, basi nakuambia utafurahi ukiwa na mimi, utapaat chochote kile unachotaka.”


Aliniambia, mwanzo nilikua kama nataka, lakini alipotaka kunifua nguo ya ndani nilikua kama mtu aliyeshtuka, picha ya Mama ilikuja kichwani kwangu na moja kwa moja nilijihisi kama namsaliti.


“Hapana, mimi siwezi kufanya hivi Baba, siwezi kumsaliti Mama, nampenda sana Mama na yeye ananipenda!” Nilijikuta anropoka, ingawa yeye alidhani kuwa nampenda Mama kama Mama kwakua ananijali na kunionyesha upendo lakini ukweli nikuwa nilikua nampenda Mama kama mpenzi wangu.


Kitendo cha Baba kutaka kufanya mapenzi na mimi kilinikasirisha, nilijikuta namsukuma na kutaka kuondoka. Lakini hakunipa nafsi, alishasisimkwa hivyo alinishika na kunivyia upande wake, kisha akanilazimisha klufanya mapenzi. Ilikua ndiyo mara yangu ya kwanza kufanya mapenzi na mwanaume, hakuniandaa, alikua analazimisha hivyo nilijisikia vibaya sana, niliumia sana nikawa napiga kelele lakini hakujali.


Baada ya kumaliza aliniambia nitoke chumbani kwake na kama nikithuburu kumaumbia mtu yoyote basi ataniua. Nilitoka huku nikilia, sehemu za siri zimechubuka na zinatoa damu kidogo, niliingia chumbani kwangu na kujisafisha kisha nikarudi kufanya kazi zangu za ndani. Mama aliporudi alinichangamkia kwa furaha lakini sikua na furaha kabisa, nilikua kwenye maumivu makali kiasi kwamba kila mtua linishangaa.


Waliniuliza nini tatizo lakini sikua na jibu, nilibaki kimya na kuwaambia kuwa nilikua sijisikii vizuri. Baba yeye hata hakujali, alichangamka na mkewe na kuonyesha mapenzi yote. Siku mbili baadaye Baba alinifuata tena, alikuaja chumbani kwangu na kutaka kufanya mapenzi na mimi, Bibi alikua jikoni anapika na shemeji yake alikua na Mama chumbani, lakini hakujali, aliingia chumbani akafunga mplango akavua nguo na kunilazimisha kufanya mapenzi.


Alikua analalamika kuwa mke wake ametoka kujifungua hivyo nitakua nikifanya naye mapenzi mpaka awe sawa. Nilikua naumia sana kwani sikua nampenda, hali hiyo ilinifanya kumchukia yeye pamoja na kuchukia wanaume, nilijikuta naapa kuwa katika maisha yangu sitakuja kufanya tena mapenzi na wanaume kwani sikufurahia tendo la ndoa kwa miezi mitatu ambayo Baba alikua ananibaka, nilikua na hamu sana na Mama nilikua nasubiria ili Bibi na mdogo wake waondoke sisi tuendelee kufanya mambo yetu.


Siku moja tulikua sebuleniu tunaangalia TV, mimi nilikua nimembeba mtoto, Mama alikua kakaa pembeni yangu, mara nyingi alipenda san kukaa pembeni yangu, alikua anafurahia zaidi kuwa na mimi kuliko hata kuwa na Baba. Baba ndiyo alikua katoka kazini amekuja na kukaa hata chumbani alikua bado hajaingia.


“Mama Kelvin una mpango gani na mfanyakazi, maana mdogo wakoa naondoka kesho na mimi naondoka wiki ijayo ila nakuona kimya una mpango gani namtu wa kukusaidia?” Bibi alimuuliza Mama, alijifungua mtoto wa kiume hivyo tulianza kumuita Mama kelvin.


“Mfanyakazi wa nini tena Mama, si huyu Fatma yupo, anafanya kazi zote, sina shida ya wafanyakazi wawili.” Mama alimjibu kwa mshangao hukua kiniangalia kwa tabasmau, mimi nilishtuka kwani nilihisi labda walishakaa na kuopanga kunifukuza wakidhani siwezi kukaa na moto.


“Huyu anatosha Mama hakuna haja ya kumbadilisha.” Baba naye alidakia.


“Kazi anafanya sawa, lakinia kijifungua unafikiri itakuaje, au uanwez akuhudumioa wazazi wawili?” Bibi aliuliza.


“Akijifungua? Kwani ana mimba?” Mamaa lijibu kwa mshtuko.


“Hana mimba, mbona unamzushia, akijifungua kivipi?” Baba naye aihamaki. Bibi alicheka na kuwaambia.


“Mbona mnakua kama watoto, huyu binti ni mjamzito, mimba mbona inaonekana kabisa au mlifikiri mnamlisha vizuri ndiyo maana kanenepa!” Mama kusikia hivyo alinigeukia kwa hasira na kunitandika kofi zito.


“Wewe mshenzi umenisaliti! Hiyo mimba ni ya nani mbwa mkubwa wewe?”


Ftma anabeba ujauzito, je ataendelea kubaki katika ile nyumba, vipi Mama Kelvin akijua kuwa mimba ni ya mume wake atafanya nini? Endelea kufuatilia ukurasa wangu huu.


ITAENDELEA…..


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE! —SEHEMU YA SITA


Baba alishtuka na kunyanyuka kutaka kuondoka, lakini Bibi alimuambia kuwa akae ili waliongelee hilo swala.


“Mimi siwezi kukaa, naona kila kitu kinataka kunigeuka, mambo ya kusalitiana yanatoka wapi? kama kabeba mimba aondoke!” Baba aliongea kwa hasira, wakati Mama analalamika kuwa nimemsaliti Baba alidhani kuwa labda Mama kagundu kuwa nimetembea naye, lakini ukweli nikuwa Mama aliona kuwa nimemsaliti kwakua nilikua natembea naye.


“Nataka kujua Baba wa mtoto, nataka kujua ni kwanini unahangaika na wanaume, unakosa nini kwangu, nimekukosea nini? Mama alilalamika, kwa kumsikiliza Mama ni kama aliku akachanganyikiwa.


Ingawa wengine hawakumuelewa ila mimi nilimuelewa, aliniangalia kwa hasira sana lakini mimi sikujali, nilikua nishachoka na maisha ya mule ndani. Nilikua nampenda Mama na nilifurahia namna nilivyokua nikiishi naye, lakini ile kubakwa kila siku na Baba iliniumiza sana.


“Kama mnanifukuza nifukuzeni, mimi nimechoka, sijui kama nina mimba na wala sijui kama ni ya nani!” Nilijikuta naongea, kusema kweli kwa wakati huo nilikua sijui hata ninaenda wapi lakini nilikua na hasira na Baba pia nilikua na maumivu ya kumsaliti Mama, nilijisikia vibaya sana, Mama alianza kulia kama mtoto.


“Huyu mtoto si wangu, mimi siajwahi kabisa kutembea na huyu binti!” Baba alianza kulalamika akijiteteea.


“Waambie ukweli? Sema ukweli Baba wa huyu mtoto ni nani? Cha kunivurugia ndao yangu, kama umetumwa sema lakini sitaki kuvurugiwa ndoa na kesho unaondoka!” Nilikua sijasema chochote lakini Baba alipaniki sana, alikua anaongea peke yake.


“Wewe nani kakuambia mimba ni yako?” Bibi alimuuliza kwani naye alichanganyikiwa.


“Siunaona mke wangu analia na kusema kasalitiwa, haya ndiyo mambo ambayo mimi siyataki, ndiyo maana nilikua sitaki binti wa kazi, huyu kesho anaondoka na mimba yake, akazalie huko!”


“Naondoka kweli, sitaki kuendelea kubakwa kila siku!” Baba aliongea maneno mengi, alikua akinitishia na kujitetea wakati nilikua sijaongea kitu chochote. Hasira zilinipanda na kujikuta naropoka.


“Kubwakwa?” Bibi aliuliza.


“Ndiyo, tangu Mama ajifungue kila siku Baba anakuja chumbani kwangu na kunilzaimisha kufanya naye mapenzi, ananibaka kwani mimi sitaki, sitaki kumsaliti Mama, Mama mimi nakupenda lakini Baba alikua ananibaka na kunitishia kuwa kama nikiongea basi ataniua, mimi sijali kuhusu kufa, nimechoka na haya maisah!”


Kila mtu alibaki kimya, nilitamani waniulize kilcihotokea na namna alivyokua ananifanya lakini hawakuuliza, walioneana aibu flani, hata Baba alishindwa cha kuongea. Nilijikuta mimi mwenyewe naelezea kila kitu, nawaambia namna alivyokua ananifanya, nikaelezea na maumbile yake na namna nilivyokua naumia. Bibi kuona mambo yanakua moto aliniambia ninyamaze, akamchukua mtoto wake wakatoka naye nnje usiku ule sisi tukabaki ndani tumeangaliana.


“Nenda ukalale tutayaongea kesho!” Bibi aliniambia, nilinyanyuka mpaka chumbani kwangu, huko nilianza kukusanya vitu vyangu kwani nilijua kuwa baada ya lile tukio basi kesho yake nitafukuzwa. Lakini subuhi Mama alikuja na kutaka kuongea na mimi, nilimuomba msamaha kwa kumsaliti na kumuambia kuwa haikua dhamira yangu kwani Baba alinilzaimisha.


“Usijali, wewe ni mtooto mdogo, najua alikulazimisha.” Aliniambia kwa upole, nilimuambia kuhusu kuondoka akaniambai kuwa siwezi kuondoka kwa hali yangu, alinisihi ni baki kwani bado ananipenda na kuhusu mtoto ni damu yao watalea.


“Sasa Baba atasemaje?” Nilimuuliza kwa wasiwasi.


“Nimeshaongea naye, yuko sawa, kaniomba msamaha na ameniahidi kuwa hatakugusa tena.” Aliniambia kwa upole mpaka nilijisikia vibaya kumsaliti, niliona upendo wake, ingawa sikufanya makusudi nililazimishwa lakini bado nilijisikia vibaya. Aliniambia nijiandae kwa chai kisha baadaye atanipeleka hospitalini ili kujua kama nina ujauzito kweli na ni wa muda gani. Nilifurahi kwa namna alivyokua anajali kama vile ni mtoto wake.


Kweli baadaye nilepelekwa hospitalini na kugundulika kuwa nina ujauzito wa miezi mitatu, kwakua nilikua sijawahi kutembea na mwanaume mwingine moja kwa moja nilijua kuwa ujauzito ni wa Baba. Tulitoka pale mpaka kwenye duka la dawa, Mama linipa dawa flani na kuniambia kuwa zitanisaidia kwaajili ya mtoto. Nilichukua na tulivyorudio nyumbani aliniambi nizinwe mchana na usiku wakati nalala. Mchana nilikunywa na nilikua vizuri tu, lakini usiku hali yangu ilianza kuwa mbaya, tumbo lilikua linaniuma sana, lilikua linakata kama mtu ana msumeno tumboni.


Nilianza kupiga kelele Mama alikua ndiyo mtu wa kwanza kuja, alinifuata kitandani na kunibamiza kwa nguvu. Alinishika mdomo akiniambia ninyamaze.


“Utanyamaza kimya mpaka hiyo mimba itoke, ulivyo mjinga ukadhani kuwa utazaa na mume wangu, kwa taarifa yako mimi ndiyo mwanamke pekee wa kuzaa naye msheni mkubwa wewe!” Alinishikilia chini huku kaniziba mdomo na pua, nilijitahidi kujiondoa lakini alinizidi nguvu, nilijirusharusha lakini hakujali, aliendelea kunibana.


“Siraki kusikia kelele na kwa taraifa yako sitaki uongee na mtu, unasema mume wangu kakubaka? Kwa sura gani uliyonayo mshenzi mkubwa wewe, yaani ulivyo ana kaili mbovu umeona umsingize mume wangu!” Alinibana sana mpaka nikaishia wanguvu, ndipoa liniachia, nilikua napumua kwa shida, akaniambia kuwa kama nikipiga kelele tena ataniua kwa mikono yake.


“Utaendelea kubaki hapa mpaka nihakikishe hiyo mimba imetoka, sitaki uondoke na kitu tumboni halafu baadaye uje kudai matunzo ya mtoto.” Aliniambia, alitoka na kufunga mpango kwa nnje. Hapo ndipo nilisikia akiongea na Bibi huko nnje lakinia limrudisha.


“Nimemuona, alikua anaota muache apumzike.” Alimuambia, nilibaki usiku mzima na maumivu makali, tumbo liikua linauma sana, nilitamani kupiga kelele lakinmi nilikua naogopa.


Namna Mama alivyokua kanibadilikia nilimuona kama niko na Shangazi yangu, alibadilika kutoka mwanamke mzuri ambaye ananijali na kunihudumia kila kitu na kuwa mnyama. Sikutaka kugombana naye, nilivumilia mpaka asubuhi. Wakati naingia chooni kujisaidia nilishangaa naanza kutokwa damu, kama mabonge mabonge, nilikua katika choo cha nnje, niliotamani kutoka lakini nilishindwa, nguvu ziliniishia nikapoteza fahamu palepale chooni.


Kwenye mchana hivi ndipo Bibi alikuja na kuniona, fahamu zilishanirudia lakini nilikua nimechoka sana.


“Kwanini umefanya hivi mjukuu wangu, hukua na sababu ya kuitoa hii mimba, hiki ni kiumbe cha Mungu, alikua ni mjukuu wangu….” Aliniambia mambo mengi lakini hata sikumjibu, sikua na nguvu kabsia ya kuongea. Nilibaki kimya ambapo alimuita mdogo wake Mama, wakaninyanyua na kunitoa chooni, waliniambia wananipeleka hospitalini lakini niliakataa ila Bibi alinilazimishia, nikapelekwa na kusafishwa vizuri.


“Sitaki aingie kwenye nyumba yangu, kama mnataka mtamtafutia sehemu nyingine lakini hawezi kutembea na mume wangu halafu nikamuacha hivi hivi?” Mama aliongea wakati sisi tunarudi. Alionyesha kuwa na hasira sana, hakumkasirikia Baba ambaye alinibaka bali alinikasirikia mimi.


“Unaaka aende wapi, huyu bado binti mzogo?” Bibi alimuuliza.


“Sijui lakini sikumzaa mimi, arudi kwa Shangazi yake, mimi simtaki, simtaki kabisa, nasema simtaki!” Aliongea, Bibi alijaribu kumsihi ili anisamehe lakinia ligoma.


Mwisho walikubaliana kuwa nibaki kwa siku hiyo kisha wanirudishe kwa shangazi yangu. kusikia neno shanagzi nilijihisi kuchanganyikiwa, nikiwaza mateso niliyokua nikipata kwake sikua tayari kurudi.


“Nimeshakua mkubwa, naweza kujitegemea, sitaki kuishi kwa mtu tena!” niliwaza wakati nikiwa chumbani, Baba aliporudi walimuambia.


“Nimeshaongea naye, anasema hamtaki lakini nimemchukulia kwake kesho nitamrudisha.” Baba aliongea kuhusu kunirudisha lakini Mama alikataa.


“Umarudishe ili mkapeane mimba tena, hapana huyu ni mtu mzima, anajua kwao ataenda mwenyewe!”


Walibishana sana kuhusu kunipeleka, Mama alionyesha kuwa na wivu ndiipo Bibi alishauri tuongozane na mdogo wake ili kama ni kuchepuka tusichepuke. Walikubaliana siku inayofuata nirudishwe Dar. Usiku sikulala kabisa, nilihisi kuchanganyikiwa, sikua tayari kurudi kwa Shangazi yangu, usiku ule wakati wakiwa wamelala nilichukua begi langu na akiba yangu kutoka pes alaizokaua ananipa Mama na Baba kwasababua ya kufanya nao mapenzi kisha nikatoka na kuondoka, nilitoka nnje na kuchukua bodaboda.


“Unaenda wapo?” Kaka wa bodaboda aliniuliza, nilikua katika mawazo sana, nilijua aondoka lakini sikujua kama naenda wapi, nilichotaka mimi kwa siku ile nikuondoka pale nyumbani basi iliu nisipelekwe kwa Shangazi yangu.


“Popote hata kwako unaweza kunipeleka…” Nilimuambia kwa utani kwani nilikau nimevurugwa, ila nikiwa sina hili wala lile alinipeleka mpaka kwake.


“Hapa ndipo ninapoishi, karibu ulele, si umesema kuwa huna sehemu ya kulala?” Aliniambia hukua kinisaidia Begi mpaka ndani, sijui kwanini ial sikujiuliza mara mbili, niliingia mpaka ndani.


Alikua anaishi kwenye chumba kimoja, kilikau kizuri tu ila sikujali, nilikau nimechoka na nilihitaji kulala. Akiwa hana hili wala lile nilifika na kukaa kitandani.


“Nimechoka mimi nataka kulala.” Nilimuambia, bado alikua ananishangaa, ilipoona kaduwaa hajibu nilivua nguo na kubaki na ngu ya ndani tu kisha nikapanda kitandani kulala. Nilimuona anavua nguo harakaharaka na kubaki kama alivyozaliwa, alipanda kitandani na kunivamia kama anataka kufanya mapenzi na mimi.


“Unataka nini?” Nilimuuliza.


“Inamaana hujui, acha kujifanya mtoto, mimi ni mwanaume, unafikiri umekuja kwangu nitakuacha hivi hivi?” Aliniuliza, nilinyanyuka na kukaa kitandani.


“Kaka, umenileta kwako kulala, sikuja kufanya mapenzi, kama unadhani hicho ndiyo kimenileta kwako basi sahau, sitafanya mpenzi na wewe na tambua kuwa huwezi kuniazimisha.” Niniliambia kwa utulivu huku nikirudi kulala, lakini hakuonekana kuridhika. Aliendelea kunishika, niliona kama ananikera hivyo nilinyanyuka tena.


“Kaka kama huwezi kulala na mwanamke bila kufanya mpenzi hembu fanya hivi, chukua shuka lala chini?” Nilimuambia, lakini hakunisikia, alianza kunifokea na kunioambia kama sitaki kufanya mapenzi nayeye basi niondoke nyumbani kwake.


“Huna akili kweli, kama ni kuondoka utaondoka wewe, mimi siondoki na kunigusa hunigusi, nina usingizi na nimechoka sana, sitaki shobo kabisa!” nilimjibu na kujifunika tena. Alibaki kakaa kwa muda ksiaha akanifuata kwa nyuma, alinishikashika, nilimuacha anishike, nilisubiti mpaka pale kasisikwa kisha nikanyanyuka.


“Si unataka kufanya mapenzi, haya mimi hapa, nifanye unachotaka ukimaliza utaniambia.” Nilinyayuka na kumalizia kuvua nguo ya ndani, yule Kaka alishagaa kwani hakuamini kama ninaweza kufanya vile.


“Unashanaga nini? Fanya kama wewe ni mwanaume kweli, unajidai kunishikashika, nifanyie unachotaka maliza niendelee kulala zangu nimechoka!” Alibaki ananiangalia tu, hata uume wake ulishindwa kusimama. Nilimuangalia kwa hasira na kulala nikiwa uchi vilevile, alipanda kitandani kulala lakini hakunigusa.


Asubuhi niliwahi kuamka na kutaka kuondoka zangu, sikujua naenda wapi lakini nilitaka kuondoka Mwanza kutafuta maisha sehemu nyingine, nilimuomba anipeleke stend, ilikua ni suabuhi sana, alinipeleka nilifika bila sababu nilipanda magari ya kwenda Dodoma. Nilifika Dodoma jioni, sikua na ndugu wala sehemu ya kulala, nilimtafuta Bodboda anielekeze sehemu ya kulala, anipeleke nyumba ya wageni ambayo ni ya Bei rahisi kwani sikua na pesa kabisa.


Nilishapanga kujitegemea, sikua tayari kurudi tena kwa Shangazi. Alinipeleka katika gest moja ambayo chumba ilikua ni elfu kumi, kwangu ilikua kubwa sana lakini sikua na namna, ilikua ni lazima kulipia huku nikijipanga na maisha ya baadaye. Niliinmgia ndani na kuoga, choo kilikua cha nnje, nilioga ila wakati natoka bafuni nilikutana na Kaka mmoja, alionekana kama kalewa hivi.


“Wewe ni mgeni hapa?” Aliniuliza.


“Ndiyo.” Nilimjibu huku nikitembea zangu kurudi chumbani, alinifuata nyuma.


“Nina elfu ishirini nakutaka.” Aliniambia, nilimuangalia kwa dharau na kumsukuma, niliingia ndani, nikavaa na kuwa sawa, usiku nilitoka wkaajili ya chakula. Katika ile Gest kuna na baa kwa nnje, hivyo kutoka nilikutana na wadada wengi wamevaa hovyohovyo, kwa wakati huo sikujua sababu ya wao kuvaa hivyo. Niliagiza chakula nikala nikamaliza, wakati nataka kulipa kuna Kaka mwingine alikuja na kuniambia kuwa anataka kunilipia, sikuona shida nilikubali.


Baada ya kulipa nilitaka kuondoka lakini aliniambia nipate kinywaji, niliagiza soda ila aliniambia nijaribu bia, nilikua sijawahi kunywa katika maisha yangu na wala nilikua sujui Bia ni nini, nilikua sijui kama inalewesha au la. Basi nilikunywa ilikua chungu ila alinisisitiza niendelee kunywa ni kawaidal nilikunywa sana mpaka nikazima.


Sikujua nimeondoka pale saa ngapi lakini nilikuja kushtuka asubuhi, nilikua sehemu tofauti kabisa na ile ambayo nilipangisha, nilikua nyumbani kwa yule Kaka, nilinyanyuka na kukuta mbegu za kiume sehemu zangu za siri na yule Kaka alikua lalala kazima kabisa. Nilishtuka na kuanza kutafuta nguo zangu, lakini kabla sijazipata nilisikia kama malngo unafunguliwa.


Nikiwa sina hili wala lile aliingia mwanamke Mama mtu mzima hivi, kwangu alikua ni mtu mzima lakini kwa kumuangalia yule mwanaume niliyekua nimelala naye walikua wamelingana.


“Wewe mshenzi nitakuua, yaani unaniletea mwanamke mwingine ndani mimi nimelala chumbani najua mume hajarudi kumbe umeleta malaya wako mpaka ndani!” Yule Mama alipiga kelele baada ya kuniona uchi nyumbani kwake, mume wake naye alikua kalala uchi kitandani jajitambui.


“Nakuua mshezi mkubwa wewe!” Aliongea yule Mama, mwili wake ulikua mkubwa kuliko mimi, nilijaribu kumponyoka lakini ilishindikana, alinisukuma mpa kitandani, nikadondoka chali nilijitahidi kujiondoa lakini nilishindwa. Nikiwa pale chini nilishangaa yule Mamasijuia litoa wapi kisu lakini alikichomoa na kunirushia akitaka kunichoma, lakini kwa bahati nilimkwepa ma kile kisu kikamchoma mume wake tumboni damu zikaanza kumwagika kama maji. Lakini yule Mama hakujali, alikichomoa na kunigeukia mimi tena akakirusha tena kile kisu kutaka kunichoma usoni.


Unadhani Fatma atachomoka salama, vipi nini kitaendelea katika maisha yake. Usikose.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE—SABA


Wakati yule Mama anataka kunichoma na kisu usoni mume wake alinyanyuka, alikua anavuja damu lakini hakuonekana kama alikua anasikia maumivu. Alimshika mke wake kama kumzuia lakini nguvu zilimuishia, akadondoa chini puu. Hapo ndipo mke wake alikua kama kashtuka flani na kujua kuwa kamuumiza mume wake. Aliniacha mimi na kumuinamia mume wake ambaye alikua haongei.


Hapo na mimi nilipata upenyo, nilivaa nguo zangu hakaharaka na kutoka nikikimbia. Nilihisi yule Mama kamuua mume wake na sikutaka kuwa shahyidi, nilitoka na kupanda Bodaboda nikiwa sina hata shuilingi kumi, sikutaka kurudi kwenye gest niliyokua nimeshukia kwani kwanza nilikua siikumbuki vizuri lakini kwa lile tukio moja kwa mmoja nilihisi kuwa yule Mama kamuua mume wake hivyo sikutaka kuwa shahidi.


Nilimuambia anipeleke stend ya mabasi ya mkoani, nilitaka tu kuondoka Dodoma na kwenda sehemu yoyote ile, sikua na pesa, sikua na kazi, sikua na chochote, pesa yote niliyotoka nayo mwanza, nguo na kila kitu nilikua nimeacha gest.


“Kaka naomba unisaidie mdogo wako?” Nilimuambia yuile kaka wakati nipo kwenye pikipiki.


“Nikusaidie nini? Sitaki mambo yako kabisa, kama huna pesa ushuke, siaki kabisa!” Alianza kuongea huku akipunguza mwendo, nilimsihi na kumuambia kuwa nitamlipa lakini aligoma.


“Tena nakurudisha huko ulikotoka sijui umefanya zali gani? Unataka kunipa msala wa polisi, kwanini unataka kuondoka Dom wakati huna pesa?” Aliniuliza, baada ya kusimamisha pikipiki, nilijaribu kujitetea na kudanganya lakini hakuniamini.


“Niambie uwkeli nikusamehe, nakupeleka stend na sisemi chochote?” Aliniuliza, kwa namna alivyokua anasisitiza kuwa anataka kujua na anataka kunisaidia nilijikuta namuamini na kumuambia uweli.


Nilimuambia kila kitu kilichotokea na kumuambia nahisi kuwa yule Mama kamuua mume wake.


“Kumbe ni kahaba, absi nipe mzigo nikusamehe nauli!” Aliniambia kwa dharau, kusema kweli nilijisikia vibaya ila sikua na namna zaidi ya kunyamaza kwani nilikua nahitaji msaada wake.


“Dada unanichelewesha, sema nikugongee wapi?” Aliniuliza, nilimuangalia kwa hasira na kutamani hata kumng’ata lakini mwisho niligundua kuwa kwa wakati huo hasira zisingenisaidia chochote. Nilizidi kumbembeleza alkini aligoma, alishaamini kuwa mimi ni Malaya hivyo hakuna namna angeniacha.


“Yaani unit*** kwa buku, hapana, kama unanitaka nipe na nauli nitafanya kama unavyotaka!” Nilijikuta nakubali kwani baada ya kumuambia ukweli alinitishia kuwa atanipeleka hospitalini.


“Nauli ya wapi?” Aliniuliza.


“Popote ni muhimu tu niondoke hapa Dodoma, sitaki kukaa tena hapa.” Nilimaumbia, alifikiria kidogo na kuniambia sawa, atanipa nauli ya kwenda popote, aliniambia nipande kwenye pikipiki yake, basi nilipanda akanipeleka sehemu ambao ni kama gereji hivia mabyo ilikua imetelekezwa, aliniambia nishuke.


“Siwezi kukuamini kukupeleka kwangu, tunamalizana hapahapa!” Aliniambia huku akinyoosha mkono kuonyesha kuwa alikua anatakanilalae chini nifanye mapenzi. Nilisita lakini alinilazimishia, palepale kwenye kachomba flani hivi, juu ya tairi alinilazimisha kufanya mapenzi. Sikufurahia kitu chochote kwani nilikua na hasira na wanaume na nilishazoea kufanya mapenzi na wanawake na kufurahia.


Alifanya mambo yake na kutaka kuondoka, lakini niliishika pikipiki yake. Sijui nilipata wapi ujasiri lakini nilimuambia.


“Unanipeleka stend na unanipa nauli, usichokijua nikuwa huko nilikokuambia kuwa nimefumaniwa mimi ndiyo nimechoma mtu kisu, nina kesi moja ya mauaji, kama sitatoka Dodoma leo basi haina shida kama nitakua na pesi ya pili ya mauaji na naamini utakua ni wewe mtu wa pili. Hunijui kaka ushanitumia nipe changu.”


Nilimuambia kwa hasira lakinia litaka kuleta ubabe, sijui nilipata wapi nguvu lakini wakati anaiwasha ile pikipiki ili kuondoka na kuniacha nilimsukuma pikipiki ikandodoka, nilimfuata palepale chini na kumkanyaga sehemu zake za siri, alianza kupiga kelele za maumivu, bila kumchelewesha niliinama na kuanza kupapasa mifokoni kwake, hakua na pesa zaidi ya elfu tano, niliichukua na kumuambia ainuke ili anipeleke stend.


Kilikua ni kitendo cha harakaharaka, hata yeye hakuamini kama ninaweza kufanya vile, alizimama na kupanda kenye pikipiki, huku akitetemeka alinipakia mpaka stend. Kufika aliniacha akaondoka, sikuwa najua kitu chochote, sikua najua nipande gari gani, lakini mbele yangu kulikua na Coster imesimama, walikua wanatangaza kuwa wanaenda Morogoro, kulikua na kijana anakatisha tiketi.


Kwa wakati huo hata sikua najua kama kuna mambo ya tiketi, sikua najua kama uatakiwa kulipia kabla ya kuingia. Basi mimi niliingia tu nikakaa kwenye siti, watu waliendelea kuingia mpaka gari ikajaa, nilikaa bila hata kulipia. Gari iliondoka, njiani kondakta Alianza kudai tiketi, kwa bahati nzuri aliponifikia aliniambia nisimame. Kwanza nilijua kama ananishusha lakini kumbe alidhani kama mimi niko na mtu mzima hivyo nisimame nipishe mtu.


Sijui ni kwanini lakini yule konda hakunidai nauli, nilisimama mpaka Morogoro, nilikua nimechoka lakini kwakua kulikua na watu wengine waliokua wamesimama sikuona shida. Nilifika Morogoro jioni kabisa, giza lilikua lishaanza kuingia na nilikua na elfu tano tu. Nilikua na njaa sana, nilimtafuta boaboda na kumuuliza ni sehemu ani ambayo naweza kupata chumba cha elfu mbili.


Kwanza alicheka lakini baadaye alihisi najiuza namtaka.


“Nina elfu kumi, nahitaji chapchap?” Aliniambia, nilikua simuelewi ndipo aliniambia kuwa anataka kufanya mapenzi na mimi ili anipe alfu kumi. Niliwaza mara mbili nikaona si sishu sana, nishafanya na wangapi? Basi nilikubaliana naye, alinichukua mpaka sehemu moja inaitwa Kahumba, huko niliona kuna wadada wengi wanajiuza, walikua wamevaa nusu uchi.


Alilipia chumba tukaingia tukafanya yetu, akanipa hela yangu na kuondoka zake. Nilitoka nnje na kukaa sehemu ya chips, niliagiza na kuanza kula. lakini wakati nakula kuna Kaka mwingine alikuja na kuniuliza Bi gani, nilihisi nichips nikamuelekeza kwa muuzaji.


“Nataka kulala na wewe mpaka subuhi?” Aliniambia, nilimuambia kuwa mimi sijuizi lakini aliendelea kung’ang’ania kuwa ananitaka. Niligoma kabisa nikamuambia kuwa sijuizi ila alinitajia kuwa ana shilingi elfu hamsini.


Hapo nilijikuta nalainika.


“Kwani nini, nimesjafanya mapenzi na wanaume wangapi leo? Hakuna jipya, nilimuambia anipe hiyo pesa, akanipa na kweli nikaenda naye mpaka hotali aliyokua amelala, asubuhi alikua anasafari zake na mimi nilibaki nikiwa na hela yangu yote, elfu sitini na tano. Mchana nilizunguka kutafuta sehemu ya kukaaa, chumba cha kupangisha lakini nilikosa, jioni niliudi tena Kahumba.


Nilishangaa wanaume wananifuata na kutaka kufanya mapenzi na mimi. Kwa wakati huo ilikua ni kama kitu kigeni lakini baada ya siku mbili nikazoea, nilipata rafiki pale amabye alikua akiishi geto na wadada wengine lakini alikua analalamika kuwa wanamuibia sana hivyo anataka kuhama ila anahitaji mtu wa kuhama naye.


“Sitaki kuishi sehemu ya kipuuzi, ukikaa kijinga jinga utakua unapata mabwana masikini. Mimi sitaki kuwa malaya maisha yangu yote, natamani siku moja na mimi kuwa na kazi yangu ya maana. Najikita kwenye waume za watu, nataka nichukue nyumba ya laki mbili lakini sina uwezo, kama vipi tuchange lakilaki….” Aliniambia, kwa wakati huo nilikua na pesa kwani nilikua napata wateja wengi wananipa pesa na sikua na mahesabu yoyote.


Nilimsikiliza nikampa laki tatyu nayeye akatoa laki tatu basi ndiyo ikawa tumehamia nyumba kubwa nzuri, ilikua ni nyumba ina vyumba viwili na sebule, kimoja kilikua Master na kingine cha kawaida, pia ilikua na jiko. Tulianza kuishi pale ndipo niligundua kuwa yeye alikua kamaliza chuo lakini hakua na kazi, alikua anajiuza lakini si kama wengine.


Mara nyingi yeye alikua anatemba na wababa watu wazima anasafiri nao lakini kama dili hama basi ndiyo anaenda Kahumba kujiuza kama watu wengine. Kila akitoka alikua ananichukua, namsindikiza, anapata wanaume nalipa vizuri, alinishauri mpaka kufungua akaunt Benki na mambo yalikua mazuri, kila siku nilikua nalala na wanaume wawili au watatu kama nikifanyia nyumbani kwa maana kuna wa mchana na usiku.


Lakini kama Biashara ya waume za watu wale wanaojiheshimu hakuna basi nilikua naenda hakumba ambapo huko nilikua nalala na wanaume mpaka 7 kutegemeana na siku, shida yao nikuwa walikua hawalipi vizuri hivyo unaishia kuchoka tu. Maisha yaliendelea, nilikua naweka akiba lakini haikukaa, matumizi nayo yalikua makubwa, nilishazoea anasa hivyo kama nikikosa mwanaume najikuta natumia akiba yangu yote inaisha narudi tenm kudanga.


Salma (sio jina lake halisi) naye alikua anaamini kuwa ipo sikua taiacha ile kazi, lakini ilikua ngumu kwani aina ya maisha tuliyokua tukiishi yalikua ni ya gharama sana. Kama hakuna wanaume unakuta tunatumia pesa yote mwisho wa siku tunaishia kujiwekea maloengo mapya kuwa mambo tunajikusnaya ili kuacha kazi lakini hakukua na kuacha kazi wala nini?’


Siku moja nilikutana na Kaka mmoja, nakumbuka kuna club moja kubwa ilikua imefunguliwa, Salma aliniambia kuwa kama nikitaka kupata wanaume wa maana kwanza nisivae uchi sana, nivae kama mtu wa heshima ambaye ameenda kula maisha, lakini pili nikiulizwa nafanya kazi gani basi niseme mimi ni mwanafunzi.


Aliniambia kuwa Morogoro kuna vyuo vikuu viwili vikubwa, mwanaume anaponijia nisipende kusema nasoma chuo gani, niisikilize yeye kwanza kujua kama ni mwenyeji au la? Kama ni mwenyeji absi nijue anatokea wapi, kama yeye anakaa mjini au anasoma SUA basi nimuambia nasoma Mzumbe, na kama akiniambia yeye ni mwanafunzi wa Mzumbe basi nimuambie mimi nasoma SUA. Aliniambia nisiongee sana, akaniambia na kozi za kutaja lakini nisiingie ndani sana pia aliiniambia kutokana na umbo langu niseme niko mwaka wa kwanza.


Nilikutana na Kaka mmkoja ambaye alijitambulisha kama Samwel (Sio jina lake halisi) na aliniambia anafanya kazi katika Benki moja kubwa maarufu. Alikua mtanashatio na kama nilivyoelekezwa kwakua aliniambia kuwa anaishi mjini nilimuambia nasoma Mzumbe mwaka wa kwanza. Alinisikiliza na hakuuliza maswali, tulikunywa tukaongea na usiku alinipa shilingi laki mbili na kunirudisha nyumbani bila hata kutaka kufanya mapenzi na mimi.


Alichukua namba yangu ya simu na kuondoka, basi baada ya muda nikiwa bado nafikiria kuwa huyu kijana anamini mbona kanipa pesa yote hii na hata hajataka kufanya mapenzi n animi alinipigia simu na kuniambia kashafika kwake na kunitakia usiku mwema. Kwangu ilikua kama maajabu, lakini iliendelea hivyo, kesho yake mchana alitaka tuonane, aliniuliza niko wapi nikamuambia kuwa nipo chuo, akaniomba jioni niende kumuona.


Basi nilikubali, tukapanga kuonana, akanipeleka hoteli moja kubwa tu, tukakaa kisaarabu tukaongea, wakati tunaondoka alinipa laki mbili lakini bado hakuniambia tukalale wote. Hali hiyo iliniumiza sana, nilitamani kumuambia Salma lakini kwa nilivyokua namjua na ninavyojua wanawake wanaojiza nilijua ataninyang’anya mwanaume wangu kwani si mara moja wala mbilia lsiahnizunguka na mimi pia nilishawahi kumzunguka mara nyingi tu.


Hali hiyo iliendelea kama mwezi hivi, Samwel alikua akitaka tuonane tunaongea kila kitu cha mapenzi lakini hanitongozi na nikitoka ananiap pesa tena nyingi, wakati mwingine laki, siku nyingine elfu hamsini na kuna wakati laki mbili. Basi mimi nilizipokea na kwakua alikua hanitafuti kila siku basi siku nyingine niliendelea na wanaume zangu ingawa nilikua makini hasa katika uvaaji ili kama siku nikikutana naye bahati mbaya nisionekane kama malaya.


Siko moja aliniambia nimsindikize Iringa, kwakua sikua na chakufanya na ananipa pesa basi nilikubali nikajiandaa tukaondoka. Tulishukia gest, ila alininunulia nguo nyingi nzuri tu za kuvaa. Kesho yake aliniambia kuwa anataka twende kwao akasalimie, sikua nashida, tulienda lakini nilipofika nilishangaa kuwa ameandaa sherehe kubwa kumbe alienda kunitambulisha mimi kama mchumba wake.


Nilishangaa kwani alikua hata hajawahi kunitongoza, lakini aliniambia kuwa ananipenda na anataka niwe mke wake.


“Sikulazimishi ila nimekuchunguza sana nimegundua wewe ni mwanamke ambaye tunaweza kutengeneza familia.” Kusema kweli nilishtuka lakini kuiona ile nyumba yao na aiana ya maisha yao nilijikuta nakubali anioe. Nikatambulishwa kama mchumba nikapewa zawadi nyingi tu na vitu kibao.


Baada ya hapo tulirudi mjini, lakini bado alikua hataki kunitongoza, aliniambia kuwa hataki kufanya mapenzi na mimi mpaka ndoa. Alinirudisha chuoni nilipomuambia kuwa naishi, kusema kweli mimi mwenyewe hapo chuoni nilikua sipajui, ila alivyonishusha nilijichanganya na wanafunzi mpaka alipoondoka basi nilipanda gari na kurudi mjini.


Nilirudi na kuendelea na mambo yangu, ila jioni Salma aliniambia tutoke kwani kuna mwanaume kampata na anakuja na rafiki yake. Basi mimi nilikubali kutoka naye kwani nilikua sinakitu cha kufanya nilijua kuwa naenda kuonana na mwanaume sehemu ya wazi basi. Lakini tulipofika wkeney hiyo hoteli tulielekezwa vyumbani, tulienda kila mmoja akaingia kwenye chumba chake.


Hapo ndipo nilijua kuwa ilikua sio kuonana bali ni kufanya kazi.


“Akupe hela yako kabla ya kufanya chochote, tumeelewana laki na nusu, laki yako hamsini yangu ya udalali.” Salma aliniambia, niligonga mlango na kuingia, nilikuta Baba mtu mzima, alikua kawasha taa lakini hafifu nilipoingia moja kwa moja nilimuuliza kuhusu hela yangu. alikua ashajiandaa, alionekana mzoefu wa hayo mambo, alienda kuichukua kwenye suruali yake ili kunipa.


Wakati anageuka ananikabidhi ndipo nikamuona vizuri, hakua mwingine bali ni Kaka yake na Samweli ambaye jana yale tu nilienda kutambulishwa. Aliniangalia na kunikumbuka, lakini hakuamini macho yake, aliwasha taa nilijikuta naangalia chini kwa aibu. Kabla hata sijajielezea alichukua simu yake, akapiga namba flani kisha nikasikia anasema.


“Dogo kumbe mjinga sana, unatuita una mchumba kumbe umekuja kubeba malaya kutuletea….”


Ng’ombe wa masikini hazai na akizaa basi anazaa duma! Unafikiri ni nini kitatokea kwa Fatma.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA NANE


Yule Kaka alimtukana mdogo wake na kumuambia kuwa kaleta malaya katika familia yao, mwisho alimuambia anataka ajekatika hiyop hoteli ili kuniona.


“Hakuna kuondoka hapa, nakuahakikishia mpaka mdogo wangu aje umuambie ulikuja kufanya nini hapa?” Aliongea kana kwamba alikua ananizuia. Kusema kweli nilifurahi kutambulishwa, lakini sikua nampenda Samweli, wala sikua nikitaka kuolewa. Ingawa kila siku nilikua nikifanya mapenzi na wanaume lakini hata siku moja nilikua sijawahi kutamani kuwa na mwanaume au kuingia kwenye ndoa.


“Sasa akija na kunikuta katika hali hii nimevaa nguo unafikiri ataamini kuwa ninajiuza, si tufanye kilichonileta hapa ili hata akija akitukuta absia jue mimi ni malaya kweli.” Nilimuambia yule Kaka huku nikivua nguo, aliniangalia kwa mshangao sana, si kitu amabacho alikitegemea kutoka kwangu.


“Unataka kufanya nini? Wewe si ni shemeji yangu?” Aliniuliza huku akijaribu kuziba macho ili asinione.


“Mimi si shemeji yako, sijaolewa na mtu mimi! Unauliza nataka kufanya nini wakati umeniita hapa ili tufanye mapenzo! Kaka nimekuja hapa kufanya kazi na sitaki ujinga katika kazi yangu. kama ni mambo ya mdogo wako mtamalizana wenyewe ila mimi nataka unipe changu kwanza na mapenzi tutafanya!”


Wakati huo nilishavua nguo nakubaki kama nilivyozaliwa, yule Kaka alikua akiniangaia kwa kuibiaibia, nilimsogelea akajifanya hataki, lakini kwa nilivyokua mzuri na uzoefu wangu wa kushawishi nilijua ni lazima ataingia laini. Bila kujijua alijikuta ananikumbatia.


“Hapana Baba! Pesa kwanza, nyie wanaume si watu wa kuaminika, nahitaji unipe pesa kwanza kabla ya kufanya chochote!” Nilimzuia, alikua kazishika zile pesa mkonopni, alinikabidhi, nikahesabu na kukuta ziko sawa, nilizihifadhi kwenye pochi yangu kisha nikarudi nikamkumbatia na kuanza kufanya naye mapenzi.


Tulifanya yetu kama nusu saa hivi simu yake ilianza kuita, alikua ni Samwel aliyekua akimpigia. Aliiangalia bila kuipokea, ilipigwa tena na tena lakini hakupokea. Mwisho alipoona kuwa Kaka yake hapokei simu alinipigia simu, mimi sikusita, niliipokea na kuanza kuongea naye, wakati naongea Kaka yakealikua kifuani kwangu.


“Uko wapi?” Aliniuliza.


“Nipo kazini kwani vipi?” Nilimjibu kwa kisirani, sijui kwanini lakini nilikua na hasira tu, nilihisi kama ananifuatilia maisha yangu hivyo sikujali kitu ambacho kingetokea.


“Unamaanisha nini kazini? Wewe si uliniambia kuwa unasoma Mzumbe?” Aliniuliza.


“Kua na akili na wewe, hivi ukiniangalia mimi ni wa kusoma chuo? Mimi ni Malaya najiuza, sina kazi nyingine, hakuna chaq chuo wala nini? Mtu hata darasa la saba sijamaliza unaongelea habari za chuo?” Nilimjibu kwa ukali, hakuonekana kushtuka ila alitaka kuniona.


“Unajua nakupenda, mimi nimeenda kukutambulisha kwetu, nakupa kila kitu lakini bado umeamua kuendelea kujiuza?” Aliniuliza, kwakweli alikua ananiboa, kwanza niliona kama aniangilia maissha yangu, nimekaa naye muda mrefu anaishia kunipa pesa tu hataki hata kunitongoza.


“Sikiliza Kaka, mimi sikukuomba ukanistambulishe, sikukuomba unipe pesa na kamwe huwezi kuniachisha kazi yangu kwakua tu una pesa. Hii ni kazi yangu, najiuza na sina shida ya pesa, kama unaahitaji huduma njoo chumba namba 22 nipo na Kaka yako….” Niiongea kwa hasira, lakini kabla ya kumaliza Kaka yake alininyanganya simu.


“Wewe una akili kweli unajua yule ni mdogo wangu, akija kutukuta katika hali hii unafikiri atafanya nini?” Aliuliza kwa hasira, nilimshangaa kwani yeye ndiyo alimuita na ndiyo alitaka kuniumbua mimi.


“Wewe si ndiyo umemuita mdogo wako, au unafikiri mimi najali, Kaka, mimi maisha yangu yalishaisha tangu siku Mama yangua liponitelekeza, siku nilipobakwa na bosi wangu ndiyo siku nilianza kuwachukia wanaume, hivyo kama ulidhani labda unanikomoa kwakua nataka ndoa sana basi hapa umechina.


Sina shida ya ndoa na wala sina shida na mdogo wako! kama akiniacha leo kesho nitakua na wanaume wengine kumi wenye pesa zaidi yake!” Yule Kaka alinyanyuka harakaharaka na kuanza kuvaa nguo, mimi nilibakii kitandani namuangalia, alikua akibabaika, anavaa bxer mara kageuza mara kadondoka, yaani ni vituko tu, mimi hata sikujali. Akiwa bado hajamalizia kuvaa nguo Samwel aliingia, tulikua hatujafunga mlango kwani wakati naingia aliponiona ndiyo alianza kupiga simu hata kabla ya kurudishia mlango, wakati tunafanya mapenzi mlango ulikua wazi, si uwazi ulke wa kurudishiwa, hapana uwazi ule wa kufunguka kabisa.


“Unafanya nini hapa na mchumba wangu?”  Samweli aliuliza kwa hasira, mimi bado nilikua kitandani nawaangalia, Kaka yake bado alikua anahangaka na suruali yake.


“Sikiliza mdogo wangu, huyu mwanamke ni Malaya, anajiuza sijui umemtolea wapi lakini huyu si mwanamke wakuoa, nakuambia mimi huyu si mwanamke wakuoa….” Alijiongelesha kana kwamba yeye ni mwema sana.


“Wewe Kaka ni mbwa, shetani mkubwa na huna akili, yaani miaka yote shemeji anahangaikakutafuta pesa wewe ni umalaya tu, kwanini hukomi, unabahati umepata mwanamke mwenye akili mjinga wewe!”


“Yaaani unaniita mimi mjinga kwasababyu ya huyu Malaya, hivi unajua mimi ni Kaka yako na mimi ndiyo nilikusomesha mpaka sasa hivi unakazi nzuri….” 


“Acha kujishaua mwanaume mbwa wewe, ulimsomesha nani? Hivi unadhani kuwa kuna mtu hakujui? Unajiona kama una akili sana lakini kila mtu anajua kuwa mali zote ulizonazo ni za hemeji, wewe huna uwezo wa kununua hata boxer, na ulivyomjinga eti unajifanya kuwa una akili, unasimamia mali kumbe huna kitu, shemeji ni mstaarabu lakini sikua kijua kuwa unafanya ujinga kama huu nina uhakika kuwa hutagusa mali yake hata moja, anakuheshimu lakini namjua, akijua ujinga wako sijui atakufanya nini mbwa kabisa wewe!”


Alimtukana sana Kaka yake ambaye mwanzo hakuonekana kujali.


“Mke wangu hawezi kuniacha, nakuambia ukithubutu kumuambia nakuua, narudia mke wangu hawezi kuniacha, mimi ni mwanaume najielewa, shida kwako wewe ambaye unahangaika na malaya kama hawa! Badala uoe mwanamke anayejielewa unahangaika na malaya, nimetembea na huyu mwanamke ili kukuonyesha kuwa huyu si mwanamke wakuoa, mjinga mkubwa wewe!”


Walianza kushikana na kupigana, mimi niliona kama itakua shida hivyo nilivaa na kuchukua pesa zangu kisha nikaondoka zangu. Wakati wakuondoka Samwel alinifuata na kutaka kuongea na mimi lakini sikutaka kabisa kumsikia, nilijua hakuna jipya ambalo ataniambia, sikutaka kuolewa, nilikua sipendi wanaume wala sikutaka kuwa chini ya mtu. Usiku ulikua bado mchanga kabisa, niliondoka mpaka Kahumba, nikapata kichwa cha elfu thelathini cha kulala nacho mpaka asubuhi.


****


Niliondoka na kuendelea na maisha yangu, nilijua kabisa kuwa nishamalizana na Samwel na hawezi kunitafuta tena. Lakini siku mbili baadaye nilishangaa mtu huyu, anakuja mpaka nilipokua nikiishi. Kumba siki mbili hizo alikua akinifuatilia mpaka kujua nilipokua nikiishi. Nilipomuona tu nilipaniki na kuanza kumtukana nikimuambia kuwa mimi simhitaji na wala sihitaji kuwa nayeye.


“Naomba unisikilize, sikuja kwa ubaya, una maisha yako na mimi sitaki kuyaingilia.” Aliniambia, kwa namna alivuokua anaongea nilijiona mjiga kupaniki, nilimpa nafasi ya kumsikiliza.


“Mimi nakupenda, na ningetamani kuwa na wewe, najua kuwa kuna maisha umepitia na unahitaji kusaidiwa, wewe unaonekana bado mtoto mdogo, sitaki uharibikiwe, naomba unipe nafasi nyingine.” Aliongea kama  vile ananiomba msamaha kitu ambacho kilinikera kwani mimi ndiyo nilimkosea lakini hakuonekana kujali.


“Una matatizo gani, hivi unajua kuwa mimi ni mayala, anjiuza na sisomi chuo?” Nilimuuliza baada ya kuona anatumia muda mwingi sana kujaribu kunishawishi.


“Najua, nilikujua tangu siku ya kwanza uliponiambia unaosoma Mzumbe, namna ulivyokua unaongea ni kama mtu aliyekaririshwa, mimi ni mtoto wa mjini na najua kila mwanamke Moro anasoma chuo.”


Niliona aibu kidogo kuwa tangu mwanzo alikua ananijua na kuamua kukaa kimya.


“Sasa kama ulikua unajua kuwa mimi ni malaya kwanini ulikua unanipa pesa na kwanini ukanipeleka kwenu?”


“Nilifanya hivyo kwakua siku ya kwanza nilipokuona nilikupenda. Sikujali kuhusu kazi yako, najua ndiyo unajiuza lakini huna tofauti na wanawake wengine kibao huko mtaani, kuna wanafunzi wengi wa chuo ambao wanaonekana wastaarabu lakini wanajiuza kwa watu wazima, sijui uliyopitia katika maisha yako mpaka kuamua kujiuza, lakini niamini nikikuambia kuwa nakupenda na nahitaji kukubadilisha, natamani tuanze upya.”


Kusema kweli sikumuelewa, niliona kama ananitania, labda anataka kutembea na mimi ili aniache.


“Kamaunanitaka ni lazima unilipe, siwezi kulala na wewe bila kunilipa vizuri, hapana, kama unanitaka basi pesa mbele.” Nilimuambia, aliniambia kuwa kuhusu pesa yeye hana tatizo lolote, anaweza kunipa kiasi chochote kile ila muhimu nikubali tu kuwa naye.


“Utakua mke wangu hivyo pesa zangu ni zako, sitaki kukuchezea.” Aliniambia, kusema kwelia linichanganya, niliona kama anataka kunifanyia kitu kibyaa, nilimuambia anipe muda wa kufikiria.


“Sasa kuhusu Kaka yako, atakubali kweli unioe?” Nilimuuliza kwa wasiwasi.


“Kaka yangu hahusiki kabisa kwenye maisha yangu, nimeshakupenda na nakuhitaji katika maisha yangu, siwezi kukuacha na yeye hawezi kuingilia maisha yangu kamwe.”


Aliongea sana na mimi nilimsikiliza ili tu amalize, sikua na mpango wa kuolewa na mtu yoyote. Lakini Salma alivyorudi na kumuambia aliniambia kue nikubali kwani nitakua nimeula kimaisha.


“Utajiuza mpaka lini, hata kama humpendi lakini huko mbele utampendi, haya sio maisha kabisa, kama anapesa mkubali. Huko baadaye ukimchoka unamuacha mnagawana mali!” Aliniambia, kusema kwelia linishawishi sana, nilimsikiliza lakini sikutaka, baadaye ndipo aliniambia kuwa kama nikiona naye, hata kama nikikaa kwenye ndoa mwezi mmoja lakini nikitaka kuachana naye basi tutagawana mali.


Baada ya kuniambia hivyo nilikubali kuingia kenye niyo ndoa ingawa ilikua kwa shingo upande. Samwel hakutaka hata nibadilishe dini, aliniambia kuwa ili tufunge ndoa ya haraka basi tufunge ndoa ya Kiserikali akiniahidi kuwa baadaye nikibadilisha dini tutafunga ndoa ya kanisani. Tuliingia kwenye ndoa nikiwa na wasiwasi sana, nilikua bado nachukia wanaume lakini kwake nilihisi labda mambo yaakua tofauti kwakua alikua ni mstaarabu sana.


Ndoa ilifungiwa kwa mkuu wa wilaya lakini baadaye ilifanyika sherehe kubwa sana ambayo alialika kila mtu. Hakukua na kuchangishana wala mimi sikua na ndugu yoyote zaidi ya marafiki zangu, kuhusu wazazi niliongeana Fatma, akanitafutia Mama mmoja na mzee mmoja ambaye alikua ni danga lake wakaja kama wazazi. Sikua na ndugu yoyote na mpaka wakati huo nilikua nikiamini kuwa Mama yangu alishafariki dunia hivyo sikuhangaika hata kumtafuta.


Baada ya ndoa nilihamia kwake, Salma siku zote alinisisitiza kutulia katika ndoa huku akiniambia kuwa ni bahati sana mimi kuolewa. Kutokana na namna mume wangu alivyokua ananionyesha kuwa ananipenmda nilipanga kutulia katika ndoa yangu. nilikua na hamu sana na mume wangu, tangu kujuana naye alikua hajanitaka kimwili, tulikua hatujawahi kufanya tendo la ndoa hivyo siku ya kwana nilijua kuwa itakua shughuli pevu.


Lakini usioku nilipotaka kumgusa aliniambia kuwa amechoka kutokana na mambo ya hausi. Basi nilimkubalia na kwakua sikua na hamu sana nililala mpaka kesho yake ambapo aliamka mapema kwenda kazini. Nilishangaa kwani nilidhani ana ruhusa ila aliniambia hapana, Benki hakuna kupumzika, kwakua nilikua sijui kitu chochote kuhusiana na mambo ya Benki nilikubaliana naye na kumuacha aende kazini.


Usikua lichelewa kurudi, alirudi kwenye saa saba za usiku, kumuuliza aliniambia kuwa alikua bize kazini. Nilishangaa lakini sikutaka kuonekana kama nina mdomo, nilinyamaza na kukubali, nilimtengea cha kula na maji ya kuoga, lakini lilipokuja suala la kitandani aliniambia kuwa kachoka. Hali hiyo iliendelea hivyo hivyo kwa miezi mitatu nya ndoa, alikua hjajanigusa kila nikitaka kufanya naye tendo la ndoa basi ailikua anakasirika na kuniambia kachoka.


Nikimuambia mimi mwili unamahitaji ananiambia kuwa napenda sana ngono. Nilivumilia sana mwisho niakchoka, nilimfuata Salma ambaye alikua ni kama Mama yangu na kumuelezea.


“Labda anakupima, anajua ulikua unajiuza labda anataka kujua kama unaweza kuvumilia bila kufanya mapenzi kwa muda gani hivyo nyamaza, ilimradi anakuhudumia kwa kila kitu absi huna haja ya kulalamika.” Aliniambia, mimi kweli nilinyamaza na sikulalamika tena.


Maisha yaliendelea lakini mwaka uliisha bila mume wangu kunigusa, tulikua vizuri katika kila kitu, alinipa kiasi chochote cha pesa nilichotaka lakini kila lilipokuja suala la tendo la ndoa alikaua ankau mkali. Nilimvumilia nikiamini kuwa ananijaribu kuona uaminifu wake, ingawa nilchoka na nilitamani sana kufanya mapenzi lakini sikuthuburu hata kuchepuka, hakua hata ananifutilia, nilikua na uhuru wangu lakini nilikua namheshimu mume wangu sikutaka kumsaliti.


“Nyumbani kwetu wanataka mtoto! Mimi mwenyewe nataka mtoto!” Siku moja usiku aliniambia, alikua kalewa sana na alirudi nyumbani usiku, nilipomuuliza sababu ndiyo akaanza kuniambia hivyo.


“Sasa mtoto atatoka wapi wakati wewe hutaki hata kunigusa, mimi mwenyewe nataka mtoto lakini nawezaje kumpata mimi peke yangu?” Nilimuambia kwa kulalamimika huku nikijaribu kumgusa kuona kama ataisimkwa labda tufanye mapenzi.


“Hivi huna akili kweli? Kwanini hujiongezi ukaniletea mtoto? Hivi unafikiri kwanini nilioa malaya, umetembea na Kaka yangu kwanini hata usimtafute ukabeba mimba yake? Mimi ninachotaka ni mtoto, nilioa malaya ili ukanitafutie mtoto huko nnje uniletee nilee!” Mume wangua liongea kwa hasira hukua kinisukuma.


NB; INTERVIEW NA AJIRA; Hiki ni Kitabu changu kipya ambacho kinazungumzia mambo ya AJIRA. Kina maelezo kuanzia namna ya kuandika Barua ya kuomba kazi, kuandika CV kujiandaa na usahili. Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kwenye Usahili na namna ya kuyajibu, namna ya kutengeneza Connection za kiajira na namna ya kutumia mitandao kupata ajira.


Kisome kutokana na mahitaji yako ya wakati huo, iwe unajiandaa kwa usahili au ndiyo unaandika Barua au kuandaa Cv. Bei yake ni shilingi elfu kumi. Kupata kitabu unalipia kwa M-pesa No. 0742-381-155 au Tigo Pesa No. 0657-552-222 Jina linakuja Iddi Makengo, sina namba nyingine zaidi ya hizo baada ya hapo kitabu utatumiwa kwa njia ya Whatsapp/Email/Facebook.


ITAENDELEA…


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA  TISA


Nilikua ni malaya kweli, nilikua najua kazi yangu na kamwe sikuwahi kujisikia vibaya kwakuitwa malaya. Lakini siku hiyo nilijihisi hata kufa, kitendo cha Samwel, mume wangu mwanaume ambaye nilidhani kama amenikubali hivyo hivyo na kunipenda kuniita malaya iliniumiza sana. Nilihisi kudhalilika kuona kama alikua anataka nitembee na Kaka yake kwakua tu nilikua ni Malaya ili kumpatia mtoto.


Nilijikuta naanza kulia kama mtoto, nilishindwa hata kumuangaliua usoni.


“Unalia nini sasa? Hivi ulifikiri kweli nilikupenda? Umelala mpaka na Kaka yangu halafu unategemea nikuite mke?”  Aliuliza kwa dharau huku akininyanyu a uso kuhakikisha namuona anavyoongea.


“Mimi sio malaya na kama hunitaki niache….” Nilijaribu kuongea lakini kabla sijamaliza alinitandika kofi la usoni, lilikua ni kofi kali na la kushtukukiza kiasi kwamba nilianza kuhisi kizunguzungu. Kabla sijafanya chochote alinyanyua mguu wake na kunikanyaga tumboni, kilichofuata hapo kilikua ni kipigo kikali, alinipiga sana hukua akinitukana.


“Unanidhalilisha, ndugu zangu wanataka mtoto, rafiki zangu kila siku wanaulizia suala la mtoto lakini wewe umejikalia tu hapa unakula pesa zangu! Nataka mtoto, sijui utabeba mimba ya nani lakini nataka mtoto!” Alinipiga sana kisha akaondoka, hakurudi mpaka asubuihi. Asubuhi aliporudi hakusema chochote, aliingia ndani akabadilisha nguo kisha akaondoka zake na kurudi kazini. Nilikua katika maumivu makali, sikua na mtu wa kuongea naye zaidi ya kumuambia Salma  nilimpigia simu na kumuambia kila kitu kilichotokea.


“Kuazaa sio shida, wewe si una kizai, ila ni lazima ujihakikishie usalama wako, kama anataka umzalie basi muambie akununulia kiwanja na kukujengea, tofauti na hapo muambie kuwa utamuacha.” Aliniambia.


“Kwanini akininunulia kiwanja au akinijengea hawezi kunigeuka, mimi sitaki kulea mtoto peke yangu.”


“Hapana, huyo mwanaume anataka mtoto, anajua hawezi kupata hivyo ukimzalia kama akikusumbua basi unamuachia mtoto, kiwanja kinakua kina jina lako  mambo yanaishia hapo, huna haja ya kuogopa, wewe si kizazi unacho, mimba ngapi ulishawahi kutoa?”


Aliniuliza, kweli niishatoa mimba nyingi hivyo kama ishu ni watoto basi ningekua nao wengi. Niliona hakuna sbaabu ya kumkatalia mume wangu, nilikua tayari kumzalia kwa masharti ya kuninunulia kiwanja na kunijengea. Jioni alirudi akiwa amelewa, alianza kuniongeleshea masuala ya mtoto, alitaka kunipiga lakini nilimuwahi na kumuambia kuwa nipo  tayari kumzalia kama atanijenge nyumba. Nilidhani kama itakua ngumu lakini ni kitu amacho alikiandaa, ingawa aliongea kwa dhrarau lakini alikubali.


“Ndiyo maana napenda malaya, mnawaza pesa tu, nilishajua utataka kitu, basi nilishakununulia kiwanja naanza kukujengea na ukijifungua nakupa gari, ila utamnyonyesha mtoto wangu kwa miaka miwili, baada ya hapo nitakupa nyumba yako na gari yako halafu utaniachia mtoto wangu, sitaki mwanamke na wala sitaki mtoto wangu akujue. Mimi nitamuambia kuwa Mama yake alikufa, sitataka kukuona tena!”


Aliniambia, sikua na shida ya mtoto hivyo nilikubali, nilimuambia anionyeshe nayraka zote ziwe na majina yangu, basi tyulikubaliana nianze mchakato wa kutafuta mtoto.


“Kwahiyo nitafanya nini kuhusu Kaka yako maana anajua umenioa, anaweza kukubali kufanya mapenzi na mimi?” Nilimuuliza.


“Sijui, wewe ni malaya, utajua chakufanya, kaka yangu naye ni malaya kama wewe hivyo mtajuana, ninachotaka ni mtoto, mwezi huu hakikisha unamtafuta na unabeba mimba yake, baada ya hapo sitaki uwasiliane naye tena.” Aliniambia,   ingawa lilikua ni wazo lake lakini alikua anaongea kama vile hataki, alionekana kuwa na hasira na alikua akiniongelesha vibaya kamatakataka hivi.


Nilitamani kumuuliza nifanye nini ili Kaka yake akubali kufanya mapenzi na mimi lakini nilishindwa, niliogopa matusi mengine. Nilibaki kimya lakini yeye alisisiiza kuwa anataka nizae na Kaka yake kwani anataka mtoto awe ni damu yake. Basi nilikubali, kichwani nilikua sijui nitafanya nini kumpata Kaka yake. Siku hiyo ilipita ila kesho yake nilimtafuta Salma, mshauri wangu mkuu na kumuambia amekubali, aliniambia nihakikishe Document na kuhakikisha kabla ya kubeba mimba yake kila kitu tunaandikishana kwa mwanasheria.


Alimtafuta bwana wak emwanasheria na kuniunganisha naye, kwlei mume wangu alikubali kuniandikia kiwanja na kuahidi kuwa nikijifungua ataninunulia gari. Hakuandika kama ni makubaliano ya kumzalia, hapana, hakutaka watu wajue kuwa hana uwezo wa kunipa ujauzito.


“Vipi kuhusu Kaka yake, unafikiri nitampaa vipi?” Nilimuuliza salma ambaye alionekana kuwa na majibu ya karibu kila swali niliokua nalo.


“Kaka yake ni malaya, utampigia simu ukiwa katika siku zako za hatari, omba kuonana naye, muambie una malalamiko kuhusu mdogo wake, kwakua haipendi ndoa yenu basi nina uhakika kuwa atakuja. Baada ya hapo mkiwa ndani lalamika kuwa una mimba ya mdogo wake lakini hajali, hahudumii, mkumbushie jinsi ulivyofurahia siku mlipofanya mapenzi, weka mbwembwe kidogo nina uhakika ataingia laini, fanya naye mapenzi beba mimba yake.


Akitoka hapo hata akija kukuona na mimba atajua ni ya mdogo wake kwani ulienda kumlalamikia kuwa una mimba.” Aliniambia , lilikua ni wazo zuri, nilirudi na kumuambia mume wangu, alilifurahia wazo lakini kama kawaida yake aliishia kunitukana.


“Mbona unanitukana sana kama hutaki nitembee na Kaka yako si uniambie?” Nilimuliza kwani nilishachoka naman alivyokua ananifanyia kana kwamba lilikua ni wazo langu. Lakini ni heri nisingeuliza, tulikua tumelala kitandani nilishtuka mtu kaamka, kanishika na kuanza kunichapa na mikanda, alinipiga sana huku akinituikana.


“Wewe nimekununua? Sio mke wangu hivyo huna haki mya kunihoji kwa chochote kile! Mimi nakutumia tu kama takataka, nimekulipa hivyo nikikasirika au nisipokasirika uamuzi ni wangu!” nilinyamaza kimya na kuapa kuwa sitamuuliza kitu kingine tena kwani sikutaka kuendelea kuumizwa kwasbaabu za kijinga. Maisha yaliendelea, nilipokaribia siku zangu za hatari nilimuambia,  wakati huo Kaka yake alikua Dar , nilimpigia simu na kumuambia kuwa nataka kuongea naye.


Kwanza alishangaa kuona simu yangu lakini kwa namna nilivyokua naongea alihisi kuna tatizo.


“Nilijua tu kuwa hiyo ndoa itakufa, bwana mdogo hawezani na wanawake kama wewe, wewe ni mtu wa starehe, mtoto mzuri anakuweka hapo Morogoro. Kama unataka kuongea na mimi basi tafuta njia njoo huku, mimi huko siji, nimekuja kula maisha huku!” Kaka yake aliniambia, nilimuambia mume wangu akaniambia niondoke nihakikishe tu nikirudi nina mimba na si kitu kingine.


****


Sikua na haja ya kumshawishi kaka yake kufanya mapenzi na mimi,   nilipoanza tu kumlalamikia kuwa nina mimba ya mdogo  wake alianza kumponda na alionekana bado ananitaka. Nilikaa dar kwa wiki nzima, katika kipindi hicho mume wangu hakuwahi kunitafuta au kutaka kujua ninaendeleaje. Ingawa nilikua na mawazi kuhusu kupata mimba lakini nilifurahia sna,a nilifanya mapenzi na kufurahia tendo la ndoa kwa mara ya kwanza, nahisi nikwakua nilikua sijafanya muda mrefu na namna kaka yake alivyokua fundi.


Baada ya kumaliza siku zangu za hatari nilirejea nyumbani, mume wangu alinipokea vizuri akiamini kama nina mimba, hakuniuliza chochote kilichotokea, hakutaka hata kumtaja Kaka yake.  Kwa namna tulivyokua tunafanya mapenzi niliamini kabisa kuwa nimepata ujauzito na niliamini kuwa nitafurahia ndoa  wkani mume wangu angefurahi kuwa nina mimba.


Laskini haikua hivyo, siku zangu za hedhi zilipofika nilijikuta naingia kama kawaida. Nakumbuka ilikua ni usiku, sikunvaa hata Pedi kwani niliamini kabisa kuwa nina mimba. Tukiwa tumelala na mume wangu yeye ndiyo alishtuka na kuniamsha. Damu zilitoka,  tena nyingi kuliko kawaida yangu.


“Niambie umatoa mimba yangu au hukubeba mimba?” Aliniliza huku akiniamsha, niliamka na kukutana ile hali.


“Mimi nilijua kwua nimepata ujauzito, siwezi kutoa….” Nilianaza kujitetea lakini hakunirugusu hata kumalizia kujitetea, nilishangaa ananyanyuuka na kunishika miguu, alinivuta mpaka chini.


“Kwahiyo huna mimba, umeenda kutafuta mtoto lakini  badala ya kufanya kilichokupeleka unaenda kufanya  starehe. Nilijua tu kuwa  sipaswi kukuamini.” Aliongea kwa hasira, wakati huo mimi nilikua chini, alikua anaondoa shuka na sikujua anataka kulifanyia nini.


“Lakini mume wangu mimba haipatiklani siku moja, kuna watu wapo kwenye ndoa wanatafuta mtoto muda mrefu lakini hawapati,  nitajaribu tena nina uhakika safari nyingine nitapata.”


“Hahahaha! Utajaribu tena! Utajaribu tena!” yaani umefanya makusudi usibebe mimba ili ukajaribu tena. Ndivyo ullivyopanga na huyo malaya wako, mimi namjua Kaka yangu, ni malaya sana, ana watoto wengi, hana tatizo lolote, akitaka kumpa mwanamke ujauzito basi atampa, nahisi unanichezea!”


Nilijaribu kujitetea lakini kadri nilivyokua nikiongea ndivyo nilizidi kumpandisha hasira, alichukua lile shuka na kunifuata pale chini, alishika ule upande ambao ulikua na damu za hedhi na kuniambia nipanue mdomo.


“Unataka kufanya nini?” Nilimuuliza huku nikijisogeza pembeni.


“Nataka ujue kuwa sina utani kwenye hili suala la mtoto, nataka mtoto na nitafanya kila kitu nnipate mtotyo, siwezi kuendelea kudhalilika, nina pesa lakini kila mtu ananiona hanithi huko mtaani. Nyumbani kwetu siheshimimi, mimi nahudumia familia, nimewajengea wazazi wangu nyumba kubwa lakini hawaniheshimu kwakua sina mtoto, ninakuipa kazi ukaifanya unaenda kuendekeza umalaya wako, nataka uinyonye hii damu mpaka iishe, shuka langu liwe safi kabisa!”


Aliongea kwa hasira, mwanzo nilihisi utani, lakini baada ya kuniona ninazubaaubaa, alinifuata laelc hini akanipaka shingo, nililazimika kupanua mdomo ili kutafuta hewa, aliingiza ile sehemu yenye damu na kuisokomeza mdomoni, aliniazimisha kuinyonya mpaka damu ziishe. Nilijihisi kinyaa lakini hakujali, aliitoa kiosha akanipa nishike mwenyewe niilambe.


“Kwanini unannifanyia hivi? Mimi si ni mke wako, kama ni mtoto si nimekuambia nitakuzalia, sasa mbona unanifanyia hivi?” Niliongea huku nikilia, lakini yeye hakujali, aliendelea kunisimamia hukua kitaka nilambe shuka mpaka liwe jeupe.


“Nataka ujue kuwa niko siriasi, siku nyingine nikikutuma ujue kuwa unakuja na mimba. Nataka ujue kuwa hii ni akzi, ulikubali nikuoe, ukaniambia nikupe nyumba, basi utafanya ninachitaka na usijejidanganya hata kutaka kutoroka, nitakupata popote kule na nitakuua na mikonoyangu, siwezi kuaibika tena!”


Alipoona silambi alianza kunipiga, alinipiiga sana mpaka nikawa sina namna, nilizilamba damu zote za hedhi mpaka zikaisha, kila nikilamba alikua akiniambia nizimeze, hakuruhusu niteme chini. Kwa uoga nilifanya hivyo, alipoona limekauka aliniambia nirudi kitandani kulala na kuniambia nisimuambie mtu yoyote. Kwa uoga nilirudi kitandani ingawa sikufanikiwa kupata usingizi, nilikua naogopa, nilikua natetemeka nahisi kuchanganyikiwa.


Asubihi alikua kama kawaida, alinisalimia kama vile  hakuna kitu kilichotokea, ni kama alikua mtu mwingine kabisa. Sikumuongelesha chochote lakini wakati anaondoka kwenda kazini aliniambia kuwa nisijekujaribu kuondoka kwani atanipata. Nilimsikiliza na kumkubalia lakini sikutaka kufia pale, nilipanga kuondoka, baaada tu ya kuondoka kwenda kazini nilikusanya nguo zangu chache na kutoka nnje kuondoka, pale nnje  nilikuta Bodaboda moja, nilimuambia kuwa anataka kwenda mjini.


“Unasafiri Dada?” Aliniuliza.


“Hapana, natoka tu nataka kwenda sehemu.” Nilimuambia, sikua nikimjua hivyo sikutaka ajue mambo yangu, nilimuelekeza nilipokua nikiishi zamani na Salma lakini nilishangaa anaenda sehemu nyingine tofauti.


“Sio huko Kaka?”  Nilimuambia lakini hakusikia, nilitaka kuruka lakini aliongeza speed mpaka nikashindwa kuruka. Alinizungusha sana mpaka akafika kwenye nyumba moja, alisimama lakini hakusimama kawaida,  kabla ya kusimamisha  pikipiki aliruka na kuiachia pikipiki,  ilienda mbele kidogo na kugonga ukuta, ilinidondokea mguu ambapo nilipata maumivu makubwa.


Nikiwa pale chini nimelaliwa na pikipiki yule Kaka alikuja na kuanza kulalamika kuwa nimemsukuma hivyo kuharibu pikipiki yake. Alinitukana sana, watu walijaa na kutaka kunyanyua pikipiki lakini yeye alikomaa akidao mpaka Polisi waje, basi alipiga simu polisi na kama dakika kumi hivi walikuja askari wawili na kunichukua, wakamuambia yule Dereva aende kituoni kuandikisha maelezo mimi nikaondoka nao.


Nilikua nimeumia sana mguu, Begi langu silioni, niliwaomba kunipeleka Hospityalini.


“Wewe ni mhalifu, hatuwezi kukupeleka moja kwa moja hospitalini mpaka ulipe pikipiki ya watu!” waliniambia, walikua kaika gari binafsi, mimi nililazwa siti ya nyuma, wakati nikijua kuwa napelekwa kituoni nilishangaa wananipeleka mpaka kwenye Benki aliyokua anafanya kazi mume wangu. Ni kama walimpigia simu kwani alikua nnje akitusubiri. Gari iliposimama tu alifungua mlango na kuingia siti ya nyuma, akanikalia mguu uleule ambao uliumua.


“Alikua anataka kumuua Dereva Bodaboda kamharibia sana Pikipiki yake.” Askari mmoja alimuambia mume wangu.


“Ulikua unaenda wapi? si nilishakuambia kuwa usijekujaribu kutoroka, nini kilikua hakieleweki?” Aliniambia huku akiushindilia mwili wake juu ya mguu wangu uliokua umeumia.


ITAENDELEA…..


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA   KUMI


Kesi ilihamia kwangu kuwa nataka kumuua Derava bodaboda, aliwaambia wale asikari kuondoka kuashiria kuwa aliwatuma. Niliona anawapa npoti mbili za elfu kumikumi kila mmoja na kisha wakaondoka zao.


“Nilikuambia kuwa huwezi kunitoroka, utabeba mimba na utanizalia, mimi siwezi kuendelea kudharaulika kila siku!” aliniambia, nilipiga magoti kumuomba msamaha lakini hakunisikiliza, aliniambia niingie kenye gari yake, akanipeleka mpaka nyumbani.


Bado nilikua na maumivu makali ya mguu lakini hakunijali, aliniambia hiyo ndiyo itakua adhabu yangu ya kutaka kutoroka kwake.


“Ningekuletea mwanaume kuja kufanya mapenzi na wewe humu ndani, lakini sitaki kwakua utanidhalilisha. Utaondoka ukifikia siku zako, nitakuruhusu lakini hakikisha unarudi. Kama huwezi kubeba mimba ya kaka yangu basi tafuta ya mwanaume mwingine yoyote, nimeshachoka ninachotaka kwasasa ni mtoto tu!” Aliniambia, nilinyamaza na kuitikia kukubaliana naye.


Kusema kweli nilikua naogopa, hakunifungia ndani lakini sikutoka, kwanza mguu ulikua unauma sana lakini nilikua nahisi kila sehemu ana mtu wa kuniangalia kama nitatoroka au la. Nilipofika siku zangu za hatari nilitoka na kukutana na Kaka mmoja ambaye alikua ni mteja wangu mz0efu, nilifanya naye mapenzi bila kinga, nilijifanya nimelewa na  yeye alikua kalewa sana, kweli siku ile nilibeba ujauzito wake, baada ya wioki tatu hivi niliona dalili, nikapima na kukuta ni mjamzito. Mume wangu alifurahi sana, alinifanya kujihisi kama malaika, alibadilika na kuwa nanihudumia kwa kila kitu, hakunitenga wala kuninyanyasa, kila wakati alikua anahakikisha napata kila nilichokua nikikihitaji mpaka nikasahau mambo yote aliyonifanyia.


Katika kujifungua alinipeleka kwa Mama yake, nilijifungua mtoto wakiume mabaye nilifanana naye sana. Hiyo ilimfanya kuzidi kunipenda kwani kila mtu alijua ni mtoto wake lakini kafanana na Mama yake, alimpenda mtoto kuliko maelezo na alikua ananipa kila nilichokua nakitaka. Lakini mtoto alipofikisha miezi sita alianza kulia sana, alikua analia kiasi kwamba kulilkua hakuna kulala, alikua anaamka usiku kama mtu aliyeshtuka kutoka usingizini na kuanza kulia.


Hali hiyo ilitusumbua sana, baadaye alimpigia simu Mama yake na kumuambia hali ya mtoto.


“Tuletee kitovu chake, hiyo ni hali ya kawaida kuna mambo ya kimila ambayo mtto anatakiwa kufanyiwa.” Aliambiwa, kiguu na njia tuliongozana mpaka kwa Mama yake, mimi mambo yavitovu nilikua sijui, hata nilipojifungua Mama yake ndiyo alikichukua na kumpa mume wangu kukihifadhi, sikujua hata kama kina maana yoyote.


“Tulifika kitovu kikatolewa na kupelekwa kwa Bibi yake ambaye ndiyo alikua mkubwa kabisa kwenye ukoo, basi alikichukua akaingia nacho ndani lakini hata nusu saa haikupita alitoka.


“Huyu mtoto si wakwetu, hii si damu yetu ndiyo maana mwenye jina analikataa!” Aliongea kwa sauti, hapo nilikua mimi, mume wangu pamoja an Mama yake mzazi, Mama yake aliniangalia kwa kunikodeolea macho.


“Huyu mtoto ni wakwangu hayo maujinga yenu mengin e siyataki! Kama huwezi kufanya kitu ili mwanangu aache kulia basi kaa kimya lakini si kuanza kuongea ujinga ujinga wako kuwa mtoto si wangu!” Mume wangu alipaniki na kuanza kutukana, aliongea sana kiasi kwamba hata mimi nilishindwa kujitetea, alinichukua ili tuondoke. Mama yake alijaribu kumsihi abaki kusikiliza lakini hakutaka, alimtukana sana yule Bibi na nkumuita mchawi na mnafiki.


Kwa namna alivyopaniki tena ndani ya muda mfupi hakukua na amani tena.


“Kama mnataka mtoto anyamaze basi mrudishe jina la watu, mwenyewe hataki jina lake litumike kwakua si damu yetu!” Yule bibi pamoja na kutukanwa lakini hakujali, aliendelea kushauri huku akitishia kuwa, kama hatutambadilisha moto jina basi kuna mambo mabaya sana yanaweza kutokea. Mume wangu yeye hata hakujali, aliondoka na hakwenda hata kwao, aliniambia kuwa ndugu zake ni wachawi hivyo sitakiwi kurudi.


Njia nzima Mama yake alinipigia simu akitaka niongee na mtoto wake ili arudi nyumbani lakini mume wangu hakutaka, mwisho aliichukau simu na kuitupa nnje ya gari, hakutaka hata kusikia. Tulirudi nyumbani na mume wangu akabaidlisha jina la mtoto, akaniambia kuwa hataki niongee na Mama yake wala mtu mwingine yoyote yule kuhusu kilichotokea.


“Kama ukimuambia mtu ukweli kuwa, Jackson (jina mpya ambalo alimpa mtoto wetu) sio mwanangu basi jua kuwa nitakuua wewe m,toto na mimi nitamalizia kujiua.


Alibadilika na kuwa kam amnyama, niliona hasira zake za zamani zikirudi,  aliongea kwa ukali sana na nilianza kumuogopa tena. Lakini baad aya hapo alikua vizuri sana na alirudi kama kawaida, siku moja usiku tukia kitandani simu yake iliita. Ilikua ni namba mpya, alishafuta namba za ndugu zake na kuwbalock wengine, hakutaka kuongea nao kabisa.


“Nilikuambia kuwa usioe malaya, sasa unaona kilichotokea, hivi unajua kuwa huyo mwanamke wako alinitafuta na kulala na mimi wakati anadai ana mimba yako? Kama ni kweli alikua ana mimba yako kipindi kile inamaana mtoto wako alizaliwa akiwa na miezi 10 au 11 tumboni, nimeongea na Mama ameniambia hutaki kuukubali ukweli ila ndiyo….” Alikua ni Kaka yake, baada tu ya kupoke ahakumsubiri hata mume wangu kusema haloo, alianza kuongea na kwakua simu ya mume wangu ilikua na sauti kubwa nilisiikia kila kitu.


Mume wangu hakumruhusu kumalizia, alikata simu na kuizima kabisa, baadaye alijigeuzia upande mwingine, alionekana kukasirika sana. Katika kumbembeleza nilijaribu kumgusa.


“Mume wangu acha kusikiliza maneno ya watu, huyo mtoto ni wakwako na ataendelea….” Nilijaribu kuongea nikidhani labda namsaidia lakini haikua hivyo, nilizidi kumpandisha hasira. Alinigeukia na kuniwasha kofi huku akinitukana.


“Acha kunipamba mshenzi wewe, huyu mtoto  si damu yangu na kila mtu anajua, umeenda kulala mpaka na Kaka yangu halafu sasa ananitangaza huko kwa ndugu zangu!” Alifoka.


“Lakini wewe ndiyo uliniambia nikalale naye ili hii iwe damu  yenu?” Nilijitetea.


“Hata kama,  lakini ndiyo ukashindwa kupata mimba, hivi unafikiri angekua mtoto wa Kaka yangu jina lingemkataa? Nani angejua? Yaani na umalaya wako wote ukashindwa kubeba mimba yake halafu unakuja kujishaua hapa!’


Ingawa nilikua najua kabisa kuwa si kosa langu lakini nililazimika kukaa kimya, sikutaka kuendelea kumuudhi mume wangu kwani nilikua namjua, anakasirishwa na vitu vidogo na aakikasirika ni mtu wa kunipiga tu. Usiku huo tulilala bila kusemshana, aliamka ausbuhi na kuondoka, aliniachia elfu kumi ya chakula kwakua kila kitu ndani kilikuepo sikuona shida. Basi nilinunua mahitaji ya mtoito lakini usiku alichelewa kurudi. Mpaka inafika saa nane usiku alikua bado hajarudi, nilimpigia simu lakini ilikua inaita tu  bila kupokelewa.


Alirudi kwenye saa tisa hivi na alikua kalewa sana,  alipopanda tu kitandani alizima hoi, nilimvua nguo na kujaribu kumkanda ilia ngalau kupata fahamu lakini hakupata, alikuja kuzinduka ausbuhi kwenye saa nne hivi. Alikua kachelewa kazini, nilimuambia kuhusu kazi lakini aliniambia kuwa haendi na hataki kusikia kelele za mtu. Simku yake ilipigwa sana na watu amabo najua ni rafiki zake kazioni lakini hakupokea. Ilipofika saa nane aliondoka tena, hakuniaga anaenda  wapi na mimi sikuuliza chochote, aliondoka na hakurudi mpaka saa tisa usiku.


Kama kawaida akipanda kitandani anakua yuko hoi sana, mimi niliishia kunyamaza na kumuangalia tu, sikutaka kumuuliza kitu chochote kwani nilihofia kupoteza kazi. Siku hiyoa liwahi kuamka, saa moja alijiandaa na kwenda kazini, hakunaichai hata shilingi kuimi na mimi sikuuliza kitu chochote. Hali hiyo iliendelea, akawa ni mtu  wa mpombe kila siku, ilifikia hatua mpaka wafanyakazi wenzake  walinipigia simu kuniuliza tatizo ni nini lakini sikua na chakumjibu.


Mume wangua liabdilika, akawa ni mlevi wa kupindukia, kuna wakati nilikua napigiwa simu kwenda kumfuata Baa kwakua alikua kaziziwa. Siku moja nakumbuka nilipigiwa simu na kuambiwa niende kumchukua Kahumba, ni sehemu ambayo nilishaizoea na mimi nilikua najiuza pale, nilitamani nisiende lakini niliambiwa kuwa anafanya vitu vya ajabu. Aliyenipigia simu alikua ni rafiki yake askari, walikua kwenye doria akamuona amekaa amelewa.


Nilienda na kumkuta amekaa na wanawake watano, anawanunulia bia huku wakimshikashika na kumchezea.


“Mume wangu twende nyumbani, hii sio sehemu yako.” Nilimaumbia kwa utaratibu huku nikimsika mkono.


“Wewe dada kama ni mume wako ni huko kwako, hapa ni wetu na huyu mwanaume haondoki hapa!” Kibinti kimoja amabcho kilikua kinajiuza pale kiliniambia. Nilikiangalia kwa daharau na kukiambia hiki hakinijui.


“Binti, huyu ni mume wangu wa ndoa,  najua unajiuza unatafuta riziki, lakini huyu kesho anatakiwa kuwahi kazini hivyo nakushauri  achana na mimi, ulichomchuna kinatosha hivyo achana na mimi!” Nilimuambia kwa hasira, nilikua na machungu mengi, nikiangalia nilikua na maisha yangu naweza kujihudumia mwenyewe halafu mwanaume kanichukua kanizalisha halafu anaondoka haachi hata hela ya mboga.


Mume wangu alikua hajali familia kabisa, natimiza majukumu yote ya mke lakini yeye hata hajali, niliona kabisa hii si sawa, nilikua na hasira.


“Nishakuambia mume wako ni huko kwako, hapa ni mume wetu, ataondoka akitaka mwenyewe na sisi tukimaliza kumchuna, eti Baby kwani unataka kuondoka?” Aliongea huku akimshika  mume wangu sehmeu za siri,  mume wangu alinigeukia na kuniangalia kwa dharau.


“Sirudi, huyu si mke wangu ni malaya tu nilichukua kuishi naye, simtaki, ni malaya kama nyie, nimemlipa awe mke wangu hivyo hata msijali  siondoki nyie kuleni maisha, ana litoto laak elitaahira ndiyo anataka nilitunde, mimi silitunzi.


Eti anataka nimpe nyumba hivi ana akili kwei, mimi nimpe nyumba mjiinga kama huyu kisha kazaa, aondoke zake simtaki!” Aliongea kwa dharau sana, niliumia sana hasa alipomuita mtoto wangu taahira, niliumia sana, nilitamani kumrukia na kumtoa hata macho lakini nilijizuia.


Niliona hakuna sababu ya kujidhalilisha nikataka kuondoka, lakini wakati nageuka naondoka yule dada ambaye alikua na kidomo domo alinipiga kofi la makalioni na kuniambia.


“Kumbe na wewe ni malaya kama sisi, nilijua mwanamke wa maana kumbe malaya, ndiyo uondoke bibe mwanaume hakutaki. Kuzaaliswha sio tija haa sisi tuna vizazi nenda kale litaahira lako huko!” nilikua na hasira na nilikua siwezi kumpiga mume wangu, nilijaribu kujizuia lakini yule dada kwa namna alivyonitibua nilishindwa kujizuia.


“Huyu ni wakwangu nitamlamba taratibu na hataamini!” nilijikuta najisemea, nilikua na hasira nyingi katika maisha yangu, kushikwa tako na yule dada hazikua moja wapo ila kumuita mwanangu taahira ilikua ndiyo katibua mizimu yangu yote. Niligeuka na kumshika shingo, sijui nilipata wapi nguvu yakini nilimnyanyua kama katakataka, mikono miwili imemsika shingoni, kabla hajaongea chochote nilim[iga kichwa kikali cha pua, pua ilianza kutoa damu.


“Ongea sasa mbwa wewe! Umemuita nini mwanangu?” Nilimuuliza, bado nilikua nimemkaba, alikua anatapataka. Kabla ya kujibu kuna rafiki yake alinyanyuka na kunishika mikono, alitaka kunipiga kofi lakini nilimuona, nilimuachia yule niliyakua nimemshika kwa kumsukuma, kadondokea kwenye meza ya jirani, wakati watu bado wakizubaazubaa, nilichukua chupa ya bia, nilimtandioka nayo kichwani yule aliyekua anataka kunipiga.


Ilivunjikia kichwani kwake, na kipande kilichokua kimebaki nikawa niko nacho mkononi. Mume wangu alinishika na kutaka kunipiga, hapo nilipata mwanya, nilikua na ghhasira nate, nilichukua kile kipande cha chupa na kumtoboa usoni, kisha nikaanza kukuvuta na kumchana uso mpaka shingoni, hapo ndipo watu walikua washajaa, wakaingilia na kunishika. Nilikua na hasira sana lakini walinizidi nguvu, rafiki yake ambaye ni askari alikua katika doria ambaye ndiyo aliniita alikuja na kuniona katika ile hali.


Walinikamata nikapakizwa kwenye gari ya polisi, mume wangu alipelekwa hospitalini, nilizungukazunguka na Polisi wakiwa kwenye doria yao mpaka inakaribia asubuhi, hawakunipeleka kituoni kama nini. Pale nyuma kwenye gari walikua wakinisema sema tu kuwa nimeoa, nina hasira na mambo kibao. Kulikua na mdada mmoja yeye ndiyo alikua ananitetea kwania likua anamuona mume wangu kila siku na wanawake na vitu alivyokua ananifanyia.


“Hata kama ni mimi ningemtoa ngeu, haiwezekani mwanaume kila siku ni wakufuata Baa!” alilalamika, wenzake walimuambia ni sawa lakini mimi nilibaki kimya tu.


“Mnajua nimemfungia mtoto wa miezi nane ndani, kama mnanifunga mkanifunge, sitaki mambo ya kuzungushana, nipelekeni nyumbani nikamchukue mwanangu, asije kufia ndani!” niliwaambia wale askari kwa hasira.


“Kumbe una mtoto mdogo, mbona hukusema?” Yule Dada aliyekua ananitete aliniuliza, alionekana kuwa na uchungu snaa na mimi, basi alishauri nirudishwe nyumbani lakini kwani walishapata taarifa kuwa mume wangu   na yule dada niliyekua nimempiga chupa kichwani hawkauumia sana. Basi walinirudisha nyumbani bila kunipeleka kituoni, kw abahati nzuri nilimkuta mwanangu bado kalala.


Nilikaa kama nusu saa hivi mlango uligongwa, nilihisi ni mume wangu, kwa namna nilivyomuumiza nilikua naogopa labda atanifanyia kitu kibaya. Basi nilichofanya ni kuchukua kisu na kukishikilia mkononi. Nilienda mpaka dirishani kusikilizia ni nani.


“Ni  mimi shemeji, nimekuja kukupaq habari mbaya kuhusu mume wako, kuna habari mbaya, napaswa kukusaidia la si vyo kesi imekukalia bibaya.” Aliongea, alikua ni yule askari, nilishusha pumzi kidogo na kwenda kufungua mlango, nilichomeka kisu changu kwenye khanga niliyokua nimejifunga.


“Karibu!” Nilimuambia, aliingia ndani lakini hakusema chochote, alifika mpaka sebuleni na kubaki anashangaa shangaa tu, haongei kitu kabisa.


“Kuna nini shemu? Ni kitu gani kimetokea?” Nilimuulizalakini hakujibu, aliendelea kuangaliaangalia.


“Hakuna habari mbaya zozote ila nimekuja kwakua nakutaka, wewe ni malaya lazima nikupate!” Aliongea huku akinivamia, kilikua ni kitendo cha haraha sana. Alikua anataka kunibaka, kusema kweli sikuona shida kufanya mapenzi na mwanaume yoyote lakini kubakwa niliona kabisa ilikua ni uonevu.


Tulisumbuana sana lakini mwishoa linizidi nguvu, akaanza kuniingilia kinguvu huku ananitukana, nilijisikia vibaya sana,   alikaa kifuani kwangu kama dakika mbili hivi, nilimuacha afanye mambo yake nikiamini kuwa labda atamaliza na kuniacha. Lakini baada ya kuniona nimetulia alibadilika tena.


Naona hata husikii chochote, ushazoea mb** kubwa wewe si Malaya ulikua unajiuza basi ngoja nikuonyesh!” Aliongea huku akitaka kunigeuza kufanya mapenzi na mimi kinyume na maumbile.


Ingawa nilikua Malaya na nilishakutana na wanaume wengi wanataka kufanya mapenzi kinyume na maumbile tena kwa dau kubwa sana lakini sikua tayari kabisa kwa hilo. Nilishaapa kuwa siwezi kufanya kitu kama hicho, nilijifanya kulegea kimwili, nikajigeuza kidogo, lakini wakati nageuka nilikuata na kile kisu amabcho nilikichukua, kilikua kimedondoka chini, bila kufikiria mara mbili nilikiokota, hakaraharaka nilijigeuza na kumchoma na kile kisu mara mbili!


“Mamaaa! Mamaaaaaa!” Alipiga kelele huku akiniachia.


Fatma anazidikupambana, kila siku ni majanga. Kwa wale mnaohitaji vitavu vyangu ni navitabu ya aina nne. Viwili vya mahusiano, kimoja cha ajira na interview na kingine ni cha Biashara. Bei ya Kitabu kimoja ni shilingi elfu kumi. Kupata kitabu unalipia kwa M-pesa No. 0742-381-155 au Tigo Pesa No. 0657-552-222 Jina linakuja Iddi Makengo, sina namba nyingine zaidi ya hizo baada ya hapo kitabu utatumiwa kwa njia ya Whatsapp/Email/Facebook.


ITAENDELEA…


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA KUMI NA MOJA


Kisu kilimpiga mkononi, hakuumia sana, alinyanyuka na kutaka kunivamia lakini bado nilikua nimeshikilia kisu.


“Ondoka nyumbani kwangu la sivyo nakuu! Nakuhakikishia nakuua! Hapo nimekukwaruza tu ila nitakuua!” Nilikua na hasira sana, nilishageuka na kuwa kama mnyama. Nilikua nimemchoma sehemu mbili za mkono, moja hapa karibu na bega na nyingine karibu na kiwiko. Damu zilikua zinamtoka, aliondoka ukua kinitishia.


“Utajua mimi ni nani hapa mjini, ninakuhakikishia kuwa utakuja kufia jela na mume wako hatakutetea kwakua naye ulitaka kumuua!” Aliniambia huku akiondoka, wakati huo mwanangu alikua analia sana.


Nilitupa kile kisu chini, nikaingia ndani na kumchukua mwanangu, nilipanga nguo za mtoto harakaharaka na kuchukua akiba kidogo niliyokua nayo.  Nilikua na elfu hamsini tu lakini niliamini kuwa salama yangu ni kuondoka Morogoro. Nilikua naogopa kuendelea kukaa pale, sikujua niende wapi lakini ilikua ni lazima kuondoka kwani niliamini kama mume wangu akitoka anaweza kumuua mwanangu. Nilitoka usiku huohuo na kuchukua Bodaboda mpaka Stend ya Msamvu, sikua nikijua nalekea wapi?


Kulikua kunakaribia kupambazuka hivyo tayari kulishaanza kuchangamka, magari ya mikoani yalikua yanaingia na nilipofika nilikutana na wapiga Debe. Mpiga Debe wakwanza niliyemsikia alianza kwa kuniuliza.


“Unaenda wapi Moshi au Arusha?” Akili yangu hapo ilifunguka, sijui nini kilitokea lakini nilikumbuka nikiwa mdogo nilishawahi kufika Moshi, sikujua nilifika kufanya nini lakini nilikumbuka nilikua na Mama yangu. Mara nikaanza kumkumbuka Mama, nikaanza kuwaza kuwa nikienda Moshi basi nitaenda kukutana na Mama yangu.


Sikua nikijua chochote kuhusu familia ya Mama labda walikua ni kabila gani au nini lakini nilihisi walishaishi moshi kwani kulikua na kumbukumbu nyingi kichwani kwangu kuhusu moshi. Nilifanya maamuzi kuwa naenda Moshio, sikujua naenda kushukia kwa nani lakini kwakua nilitaka tu kuondoka Moprogoro basi nilikatiketi na kuanza safari ya Moshi, hapo nilikua na amani kidogo, nilijua mume wangu hawezi kunipata wala hatahangika na mimi kwani hata sikubeba damu yake.


Nilifika Moshi jioni, sikua na pesa hivyo hata sikutafuta sehemu ya kulala, nilitafuta tu sehemu ya kula, nikamtafutia na mwanangu maziwa kisha nikaanza kuzunguka kusubiria jua lilzame nilale vibarazani. Usiku huo nililala tu mtaani, bado nilikua sijajua nimeenda Moshi kufanya nini? Nilikua sijajua nini kitaendelea katika maisha yangu ila nilikua na amani kuwa mume wangu hawezi kunipata tena, nilikua na simu lakini nilitoa laini na kuzitupa, sikutaka wanitafute kabisa.


Asubuhi niliamka na kuanza kuzunguka, nilitafuta sehemu ya kula nikala na kumnunulia mwanangu maziwa, nilitafuta choo cha kulipia nikajisaidia kisha kumsafisha mwanangu. Hakukua na joto hivyo niliishia tu kumkausha.  Nilianza kutembea kuzunguka kama chizi tu, napita sehemu za Mama lishe naomba kazi lakini hakuna mtu hata mmoja aliyekua ananipa. Wakati nazunguka nilikutana na ombaomba wengi tu wananiomba pesa lakini sikuwapa kwani na mimi nilikua na matatizo yangu.


“Nisaidie hata hela ya kula mwanangu….” Nilisikia sauti ya Mama mmonja ambaye alikua amekaa karibu kabisa na sehemu ya kupandia Hiace. Nilitaka kumpita kama watu wengine lakini sauti yake ilikua ni ya tofaui kidogo. Kwangu haikusikika kama sauti ya kawaida bali ilisikika kama mziki flani hivi ambao nilishazoea kuusikiliza kwa muda mrefu.


Nilijikuta namsogelea yule Mama kwa karibu, nilishindwa kumtambua kwania likua haoni, macgo yake yalikua yameziba huku uso wake ukiwa na makovu mengi kama ulikua umeungua sana, mdomo umepnda na pua kama imeungana na mdomo hivi. Mtoto wangu akiwa mgongoni nimemfunga na khang, ghafla nilishangaa yule Mama akinishika mkono kwa nguvu.


“Mwanangu, kumbe uko hai! Fatma mwanangu uko hai!” Yule Mama Alinishika mkono kwa nguvu, sijui hata aliuonaje mkono wangu lakini alinibana sana, alisimama harakaharaka na kunivuta upande wake akanikumbatia sana.


Aliponikumbatia sikua na haja ya kuambiwa kuwa huyo alikua ni nani. Ingawa sikumtambua kwa sura lakini shoti niliyoipata kutokana na kumbato lake vilinikumbusha kipindi nikiwa mdogo Mama yangu ananikumbatia.


“Una mtoto? Vipi mwanangu una mjukuu? Umejuaje niko hapa, umekuja kunichukua mwanangu?” aliuliza maswali mengi ambayo sikua na majibu nayo, nilimkumbatia na kumuangalia vizuri, sikua nikikumbuka chochote, Mama niliyekua nikimkumbuka alikua na uso mzuri, kapendeza kama malaika lakini yule alikua kaungua uso mzima yaani sijui nikuambieje.


“Umejuaje kuwa mimi ni Fatma na wewe ni nani?” Nilimuuliza, ingawa akilini kuna kitu kilikua kikiniambia kuwa huyu ni Mama yako lakini kuna kingine kiliniambia hapana, huyu ni tapeli tu!


“Lakini kama ni tapeli anataka kunitapeli nini? Mbona mimi sina pesa, sina kitu chochote, atanitapeli nini mimi? Hata kama ni tapeli, huyu mwanamke haoni sas akajuaje mimi ni mtoto wake?” Nilijiuliza maswali mengi bila majibu, nilikua nahisi niko na Mama yangu, nilikua najua kuwa ni Mama lakini kwa wakati hu nilikuasitaki kuamini.


Wakati Mama yangu anaondoka nyumbani nilikua mdopgo sana, kama miaka saba nane, ila siku hiyo nakutana naye nilikua na miaka 23, miaka zaidi ya 15 halafu nakutana na mtu ananiita jina langu.


“Harufu yako mwanangu, harufu yako, wewe ni mtoto wangu, najua ni wewe, siwezi kukuona lakini harufu yako ni ileile tangu siku ya kwanza unazaliwa. Wamechukua macho yangu lakini hawajachukua uwezo wangu wa kutambua vitu, wewe ni mwanangu na hata siku mojaja hawezai kuchukau hariufu yako kwangu.


Alipohisi simuamini alianza kunielezea mambo mengi kuhusu mimi, alinielezea kuhusu Baba yangu, majina yake, Shangazi yangu ambaye ndiyo alinifukuza. Aliopofika sehemu ya shanghazi nilimuona machozi yanamtoka, alikua analia bila kujijua, sijui alikumbuka nini lakini hata mimi nililia tena kwa hasira, jina la Shangazi lilinikumbusha machungu mengi.


“Kama wewe ni Mama yangu kweli kwanini uliondoka, kwanini uliamua kuniacha peke yangu nateseka?” nilimuuliza, hilo ndiyo swali liliukua linaniumiza kichwa sana, Mama aliyakue ananipenda akaniahidi kuwa kamwe hawezi kuniacha lakini ghafla natoka shule naambiwa ameondoka.


“Shjangazi alinambia umekufa, lakini kumbe uko hai kumbe ulikua unapumua, kwanini uliondoka na kunaicha nikiteseka na Shangazi?” Nilimuuliza huku nikilia, Mama aliniambia tusogee pembeni tukae, ingawa alikua haoni lakini alionekana kuyazoea mazingira ya pale, tulikaa akaniambia nimshushe mtoto na kumpa yeye ili anisaidie kumbemnbeleza kwani alishaanza kulia. Nilimshusha na kumkabidhi mwanangu,a limshiak na kuanza kumbembeleza hukua kiimba nyimbo ambazo nilizikumbuka, ni nyimbo ambazo alikua akiniimbia mimi nikiwa mdogo nanyamaza.


Hata mwanangu aliposika alinyamaza na kutulia kabisa mikononi mwa Mama yangu. Kunamambo mngi nilitaka kusikia kutoka kwa Mama yangu, kwanini aliondoka, mika yote hiyo alikua wapi, je ana maihs amengine? Vipi kwanini yuko katika hali ile, ana0mbaomba mtaani? Ni mambo mengi sana nilitaka kujua. Mama alinituiliza na kuniambia kuwa nitajua kila kitu, pamoja na kutokuona kwake na hali yake ya uso lakini Mama alikua vizuiri katika kuongea.


Alijua kupangilia maneno, alijua kunifariji na kunielezea kwa ufasaha.


“Mimi sikupanga kuondoka mwanangu….” Mama alianza kunielezea kwanini aliniacha kwani ndiyo kitu kilikua kinaniumiza sana, ni swali ambalo nilihitaji majibu ya haraka sana.


“Sikutaka kuondoka, lakini baada ya Baba yako kufariki dunia nilijua kuwa natakiwa kuondoka katika ile nyumba kwani mwanzo nilijua kuwa Baba yako kamuandika kila kitu Dada yake.


Nilitafuta mwanasheria akaniambia kuwa, kisheria kama mali zina majina ya shangazo yako basi ni zake hivyo mimi na wewe hatuna haki yoyote. Kwa maana hiyo ilinibidi ikuwa mole ili kujipanga kwakua nilikua najua ni suala la muda tu Shangazi yako atanifukuza. Kila siku nilikuambia kuwa ni lazima niondoke na wewe kwani wewe ni mwanangu na kama Baba yako aliamua kututelekeza asituachie chochote niliamini hata Dada yake asingekuthamini wewe, hivyo ilikua ni lazima kuondoka na wewe.


Sikua na pesa lakini wakati Baba yako yuko hai nilikua na viakiba vyangu, vipesa nilivyokua nikimuibia, labda wakati mwingine kanipa kahela kadogo basi nabana ili na mimi kuwa na akiba. Kwakua baba yako alikua hataki niwe na pesa, kila dakika alikua akinikagua basi niliamua kucheza mchezo wa kupeana pesa na wamama wenzangu. Kwa mwezi alikua anapokea mtu mmoja, basi kipindi kile nikijiandaa kuwa nikipokea mchezo wangu ndiyo niondoke kuanza maisha na wewe Shangazi yakoa likaua ankazania niondoke.


Sikua nakuonyesha lakini kila sikua likua ananitukana, vitisho vya kutaka kuniua na vitu vingi. Lakini katika yote hayo nilikua nashangaa kitu kimoja, Shangazi yako alikua akisema kuwa nitaondoka lakini ni lazima nikuache wewe, sikujua sababu kwanini akung’anganie wakati anakuchukia na mali zote za Kaka yake kaachiwa yeye. Basi katika chunguza chunguza yangu, kunasiku nikiwa napangua pangua vitu vya Baba yako ndipo nikaona Diary yake, hapo alindika mambo mengi sana kuhusu wewe na namna alivyokua anakupenda.


Kila kitua ichokua anafanya katika maisha yake ilikua ni kwaajili yako mwanangu….” Mama aliongea kwa uchungu, alitulia kidogo na kufuta machozi, sauati yake ilififia ghafla, alikua kama anakumuka kitu. Mimi nilikua nalia lakini kwa hasira, nilishangaa kusikia Baba alikua ananipenda wakati kila kitu alikiacha juu kwa Shangazi nyangu.


“Hakua ananipena Mama, angekua ananipenda asingeniacha na Shangazi,a singakua anakutesa vile, hapana! Baba alikua shetani, siwezi kumsamehe, kaharibu maisha yangu sana!”


Nilimuambia Mama huku nikilia, ilibidi yeye kuacha kulia na kuanza kazi ya kunibembeleza mimi.


“Hapna mwanangu, najua huwezi kuelewa kwakua umeteseka na mimi umeniona nikiteseka lakini ndiyo ukweli. Katika Kitabu cha kumbukumbu cha Bab yako aliandika mambo mengi kuhusu wewe. Nakumuka kuna sehemu aliandika, Leo nimeenda kusaini wosia wangu tena, kila kitu kitabaki kwa mwanangu, ninna viwanja na nyumba kila kitu nimemuandikia mwanangu wapekee Fatma.


Ningemuachia mke wangu kusimamia lakini wanawake si watu wa kuwamaini, najua nikifa hata leo mke wangu ataolewa tena, ataenda kwa mwanaume mwingine, kwa maana hiyo mali zangu zote ataenda nazo, siwaamini wanawake kwani anaweza kumpa mwanaume wake kila kitu na Mwanangu kuteseka. Ingaw animeandika mali zangu zote majina ya wanangu lakini nataka msimamizi awe Dada yangu, yeye ni damu yangu, haa kama akiolewa lakini kwa nilivyokua naye, malezi tuliyopata hawezi kumuumiza mwanangu, dada yangua na akili atanilindia mwanangu…’


Baba yako alioodhesha idadi ya mali na kusema kuwa ni mali zako, kila kitu kina majina yako na kusema kuwa hakuna mtu anaruhusiwa kuuza mali zako mpaka wewe utakapomaliza chuo au ukiwa na miaka 22. Lakini alisema kuwa kama ukifaiki kabla ya wakati huo basi Shangazi yako ndiyo abaki na kila kitu.”


“Inamaana wewe hakukuachia kitu?” Nilimuuliza Mama.


“Hapana, hakuniachia kitu, madai yake nikuwa akiniachia kitu basi nitaolewa, aliandika kuwa kama nataka mali


zake niishi na wewe bila kuolewa mpaka utakapofiksiha miaka 22.”


“Ndiyo maana Mama nakuambia kuwa Baba alikua ni mshenzi,a nastahili adhabu ya moto huko kaburini!”


Mama hakujibu chochote, aliendelea kunielezea.


“Baada ya kuona hivyo nilimtafuta mwanasheria, alisoma na kuelewa kisha kaanza kufuatilia na kugundua kuwa ni kweli Baba yangu aliacha wosina na kweli mali zote zilikua na majina yako. Aliniambia kuwa kutokana na ule wosia basi wifi yangu alikua ni msimamizi ntu, hana uwezo wa kunifukuza na kubwa zaidi hana uwezo wa kuuza kitu chochote kwani mali zote ni mali zako.


Baada ya kujua hivyo nilimuambia Shangazi yako, tulilazimishia na mwanasheria wake ili wosia usomwe na kila kitu kujulikana. Hapo ndipo niliharibu, Shangazi yako alipojua tu kuwa nimejua, nina mwanasheria ananisaidia basi alikasirika, alijua ni lazima kuniondoa pale nyumbani lakinia singeweza kukuondoa wewe kwani ili yeye kupata mali zako ilikua ni lazima wewe ufe na ili kuthibitisha kuwa umekufa kukufukuza isingesaidia, ilikua ni lazima kuwe na cheti cha kifo.


Alianza vitisho na kuniambia niondoke na kukaucha la sivyo atanifanya kitu kibaya. Mimi sikujali, nilimuambia kuwa siwezi kuondoka na kukuacha wewe nyuma. Niliapa kabisa kuwa siwezi kufanya hivyo. Lakini siku ile wakati umeenda shule nilkiwa tu nyumbani walikuja vijana watatu, waligonga mpango nikawafungulia, kabla ya kuongea kitu chochote waliivamia na kuanza kunipiga, walinipiga sana mpaka kupoteza fahamu, baada ya hapo sikujua ni kitu gani kilikua kimeendelea mpaka nilipokuja kushtuka nimefungiwa ndani ya buti ya gari.


Nilikaa kwenye buti ya gari, narushwarushwa mchana kutwa mpaka usiku ndipo walinifikisha hapa Mosi ambapo walijua kuwa ndiyo kwa wazazi wangu. Walinitupa hapa na kuniambia kuwa nisifuatilie tena mambo ya mirathi ya mume wangu, wakanionya kama nikithuburu kukanyaga Dar basi nitakiona cha mtema kuni. Waliniacha usioku uleile na kuondoka, mimi nilikua nimechoka, siwezi hata kunyanyuka mpaka nilipookitwa asubui na wasamaria wema ndiyo nikapelekwa hosipitalini…”


Wakati Mama anaongea mwanangu alikua kimya kabisa, ni kama nayeye alikua anasikiliza, Mama alitulai kidogo, alinyanyua mikono yake na kunishika usoni kisha akamshika na mwanangu.


“Mmefanana sana? Mkwe wangu yuko wapi? Baba wa mtoto yuko wapi? Umeolewa?” aliniuliza maswali ambayo yaliniumiza sana, sikua na majibu yake, nilibaki tu natetemeka kwa hasira, sikutaka kumuelezea Mama stori yangu hivyo nilizuga ili kumuuliza stori yake.


“Vipi Mama kuhusu makovu, nini kilitokea mpaka uso wako ukawa namna hii?”


Kuna MATAPELI wengi ambao wanatumia Jina langu la IDDI MAKENGO, unapomuelekeza mtu instagramu muambie akaunti yangu ni @iddimakengo sina akaunti mbili wala tatu ni moja tu. Unapolipia Kitabu hakikisha jina linakuja IDDI MAKENGO mwingine yoyote ni TAPELI na namba ni mbili tu, narudia mbili tu. M-Pesa No. 0742-381-155 au Tigo Pesa No. 0657-552-222 narudia jian hakikisha linakuja IDDI MAKENGO.


Fatma anakutana na Mama yake, mambo ndiyo kwanza yanaanza, Je, makovu ya Mama yake aliyapata wapi? vipi mpaka sasa hivia anomba, vipi kuhusu maisha yake, je ana familia na watoto wengine? Nisikuchoshe subiri sehemu ya kumi na mbili.


ITAENDELEA…


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA KUMI NA MBILI


Nilimuuliza Mama kuhusu makovu yake lakini hakutaka kunijibu, alikua nna hamu sana  ya kujua kuhusu mimi na kitu kilichotokea katika maisha yangu. Nililazimika kumuelezea kila kitu, mwisho aliishia kulia na kuniomba msamaha kwa kuniacha.


“Mwanangu nisamehe sana, nisamehe wka kukuacha kwa yule shetani….” Aliniambia huku akiaka kupiga magoi.


“Halikua ni kosa lako Mama, ulifukuzwa, usingeweza kurudi.’ Nilimuambia kwa kumpa moyo, ingawa bado nilikua namlaumu kwanini hakurudu tena lakini sikutaka kumuambia.


Kwa aina ya maisha aliyokua akiishi Mama sikutaka kumuongezea tena mzigo wa lawama. Nilitaka sana kujua kuhusu makovu yake, lakini wakati tumekaa tunaongea nilimuona Mama ananza kutetemeka kwa uoga.


“Mwanangu kimbia, ondoka hapa mwanangu, sitaki huyo mtuakuone!” Aliniambia, sikujua kama amejuaje kuna mtu lakini nilipogeuka kulikua na mbaba mmoja mrefu mtu mzima kidogo alikua kasimama pembeni yangu.


“Hivi wewe una akili kweli, badala ya kukaa kuomba unaongea na huyu mbwa mwanzako!” Yule Baba alimuambia, nilijisikia  vibaya kusikia Mama yangu anaitwa mbwa.  Mama ndiyo alikua kambeba mwanangu, nilijikuta nanyanyuka kumuangalia yule mtu. Lakini sijui Mama alijuajenkwani alinishika mkono.


“Mwanangu, acha, mueche huyo mtu, hii vita si ya kwako, muache kabisa, achana naye mimi najua nini chakufanya?” Mama aliniambia.


“Ohhhh mwnao, kumbe huyu ndiyo yule mtoto ambaye kila siku unamlalamikia, kwhiyo nayeye kaja kukusaidia kuomba!” Yule Baba  aliongea kwa sauti yake nzito.  Alikua ni mrefu sana, mimi kusimama nilikua namfika tumboni, hata sikuweza kumuona vizuri, nilimuangalia kwa juu nayeye aliniangalia kwa chini.


“Nawewe unataka kuombaa au utakua kama mke wangu!” Aiongea hukua kishusha mikono yake na kunishika matiti yangu, kulikua na watu na wala hakujali.


“Mama huyu mshenzi ni nani?” Nilimuuliza Mama yangu amabyue naye alishasimama, hakua akiona kitu, mikomno yake ilikua inanipapasa kunishika.


“Acha mwanangu, usimuite hivyo, acha kabisa.” Mama aliniambia,  alionekana kumuogopa sana lakini mimi wala sikumuogopa, niliendelea kumuuliza kutaka kujua yule mtu ni nani lakini Mama hakutaka kuongea.


“Muambie ukweli kuwa mimi  ni Mume wako,  uaniita Baba mdogo binti, mimi ni Baba yako na ndiyo ninamuweka Mama yako mjini!” aliongea hukua kinisukuma pembeni, alimfuata Mama, ni kama alijua sehemu alipokua anaweka pesa zake. Aliingiza mkono kwenye matiti  ya Mama, akatoa kipochi kidogo kisha akatoa  notinoti za pesa na kuzichukua.


“Unaona, badala ya kufanya kazi unakalia kuonea na huyu ngedere wako, nakuambia usipofiklisha hesabu leo nahakikisha kuwa hurudi nyumbani. Halafu huyu ngedere simtaki kwangu labda kama nayeye atakuja kuomba, kama vipi nayeye tumtoboe macho ili awe ombaomba!” Aliongea hukua kicheka, Mama hakumjibu kitu chichote zaidi ya kumuomba msamaha na kumuambia kuw aatajitahidi kufanya kazi ili kufikisha hesabu.  Yule Baba alichukua pesa na kuondoka nazao.


“Huyo ni nani? Mbona unaomab pesa wewe lakini anakuja kuzichukua?” Nilimuuliza.


“Ni stori ndefu mwanangu, ila kwakifupi yeye ndiyo ananisaidia, ni mume wangu hivyuo anachukua pesa kwaajili ya familia, tuna watoto, kuna wadogo zako wanasoma na yeye ndiyo anawahudumia.” Mama aliniambia, nilitaka kudodosa sana lakini Mama hakutaka, alikua anataka sana kurudi kuomba huku akinitaka na mimi niombe na mwanangu ili tufikishe hesabu.


Ingawa sikua na kitu lakini nilikua na kila kitu, nilikua na akili zangu, mikono miwili na miguu miwili, ile kazi ilikua inadhalilisha.  Niliona  aibu kufanya hivyo lakini  kwakua nilihitaji sana kuwa karibu na Mama yangu na kuongea naye kujua kuhusu maswahiba yake nililazimika kuomba kw asiku ile.


“Mama hii kazi hutaifanya tena, yaani leo ndiyo mwisho, nitakulea na kukuhudumia mimi, huwezi kuwa ombaomba wakati mimi mwanao nipo. Hapana mama, utakaa nyumbani na mwanangu mimi nitafanya kazi.”


Nilimuambia Mama tukiwa tumekaa, nilimuonea huruma na niliona kabisa kuwa anadhalilika.


“Kama ni kuhdalilika basi nidhalilike mimi lakini si wewe Mama yanmgu, hapana!” Nilimuambia, Mama hakua anajibu kitu, mjimi nilikasa nanyoosha mikoni nimemshikilia mwanangu, nilishangaa tu watu wananipa pesa, sikua na ulemavu lakini nahisi walimuonea huruma mwananugu. Tulikaa hapo  mpaka usiku ulipoingia.


“Mama tunaenda wapi? Unasema una watoto wengine na una kwako, ni wapi huko?” Nilimuuliza.


“Ni Majengo mwanangu, lakini hatuwezi kwenda mpaska Baba yako aje kunichukua.”


“Inamaana hujui njia, si unapanda tu daladala na kutafuta kituo ch akushukia?” Nilimuuliza, aliniambia kuwa anajua lakini mume wake apendi aondoke mpaka yeye aje.  Tulikaa pale mpaka kwenye saa nn eusiku ndipo yule Baba alikuja, alikuja na gari tena zuri tu. Alituambia tupande wote, mwanzo hakutaka lakini baada ya Mama kumbembeleza san ana kumuonyesha pesa ambao nilikusanya basi alikubali.


Kusema kweli sikuelewa kitu, nilishangaa sana kwamba kama anajiita mume wake na ana maisha mazuri namna ile ni kwanini anamuacha Mama yangu anaomba   barabarani kama  chizi. Tulifika mpaka nyumbani kwake, ilikua ni nyumba nzuri, ina getio zuri na kila kitu kilikua ni kizuri, tulishuka lakini Mama hakuingia katika nyumba kubwa, aliingia katika kashemeukama kakibanda kambwa huko nilikuta kagodoro kametandiokwa chini na  manguo machafumachachafu.


Niliingia na Mama yeye akaenda kuingia katika nyumba kubwa.


“Mama huyu ni mume wako wkeli au ni mtu anakusaidia?” Nilimuuliza.


“Ndiyo ni mume wangu lakini pia ni mtua nanisaidia. Mwanangu ni stori ndefu sana lakini kwasasa sina namna maana yeye ndiyo kashikilia maisha yangu,  siwezi kuondoka na kuwaacha wadogo zako hapa. Nilishafanya kosa la kukuacha wewe mara ya kwanza siwezi kuwaacha na wadogo zako, ni heri kuteseka lakini nikijua kuwa wadogo zako wapo salama.” Aliniambaia, mpaka wakati huo bado nilikua simuelewi Mama, nilikua sijui kama yuko kwenye ndoa au ni kitu ani kimeendelea katika  maisha yake.


“Nenda kamuombe ulale kwenye nyumba kubwa,  mjukuu wangu hapa atateseka, wewe huna tatizo atakuruhusu!”  Mama aliniambia.


“Kwanini uombe Mama, si umsema ni mume wako na mmefunga ndoa?” Nilimuuliza.


“Ndiyo mwanangu, tena ndoa  ya kanisani.” Aliniambia jambo jingine ambalo lilinishangaza tena.


“Inamaana Mama wewe uliabdilisha dini?”


“Nidiyo mwanangu, nilibaidlisha, nililazimika kwakua nilikua nampenda Baba Steven (Sio jina lake halisi) alitaka ufunge ndoa ya kanisani   na wkakua nilikua na hali mbaya sikua na namna.” Mama alielezea.


“Mama, sasa kama ni mume wako tena wa dnoa ana pesa namna hii kwanini anakuacha unaomba omba, mbona sielewi Mama naomba nieleweshe!” Nilimuuliza kwa hsaira, Mama alikua ananizungusha zungsusha kama kuna kitu anaficha ila nililazimsihai mpaka akaamua kuniambia.


“Wakati nakutana na huyu Baba mimi nilikua natafuta kiwanja, huyu Baba alikua ni Dalali, nilipopata haya matatizo ya kutokuona na kuharibikiwa ndugu zangu wlainitenga, sikua na namna zaidi ya kuingia mtaani kuomba.


Hali yangu ilikua mbaya kwani nilikua na vidonda usoni lakini kwakau sikua na chakula basi nililazimika kuomba. Kutokana na hali yangu watuw engi walinionea huruma, walikua wananisaidia, wananipa pesa kuna ambao walikua wananipa hata elfu kumi. Kuna Baba mmoja ambaye sasa hivi Mungu amrehemu alijitolea kunitibu na kunijengea nyumba.


Alinipeleaka hapo KCMC nakweli nilipona kabisa, baada ya hapo alijitolea kunijengea nyumba. Sasa katika kutafuta kiwnaja ndipo nilikutana na Baba Steven, yeye alikua ni Dadali ambaye alinisaidia kutafuta hiki kiwanja, yule Bbaa lihakikisha kiwanja kinakua na jina langu na kunipa Document zote za aridhi. Alianza kunijengea nyumba ya vyumba viwili, na hii ni hiki kipande ambacho naishi hapa, aliniambia nipate sehemu ya kuishi kwanza kabla  wakati yeye anajikusanya kunitafutia wafadhili amabo watanijengea nyumba kubwa.


Alishatengenea na ramani ya nyumba akiniambia iwe kubwa ili niweke na sehemu ya wapangaji kodi inisaidie mbelani. Lakini katika kipindi hicho hata kabla ya kumaliia hiki kibadna ninachoishi Baba wa watu alifariki dunia, hapo ndipo kila kitu kilibadilika, basi nikalazimika kurudi mtaani kuomba, nikaopmba mpaka nikamalizia kachumba haka nikahamia. Wakati huo Baba steven yeye alikua anaendelea na kazi yake ya udalali na alikua ni rafiki yangu sana.


Alikua ananisaidia na mara nyingi ni yeye alikua ananileta nyumbani, basi tukajikuta tunaingia katika mapenzi,  na hapo nikapata ujauzito wa mdogo wako steven. Alichukua vitu vyake na kuhamia kwangu tukawa tunaishi kama mke na mume, nilitaka kuacha kazi ya kuomba na kufungua Biashara lakini alinikaisha tamaa, akaniambia Biashara ni ngumu na kutokana na hali yangu sitaweza kabisa.


Aliniambia kwa hali yangu na kwakua sasa hivi nina mtoto basi nikiendelea kuomba tutafanikiwa. Aliniambia niwe naenda na mtoto na yeye atakua ananisaidia mpaka nimalizie nyumba yangu. sikua na namna. Mtoto wangu akiwa na miezi miwili tu nilikua naye mjini naomba, ukiangalia uso wangu na mwanangu watu walikua wananisaidia sana, kuna hata watu ambao walitaka kuipa mtaji niache kuomba lakini alikataa, hela ya kuomba ilikua kubwa, akanishauri tumalizie ujenzi, ndipo tukajenga hiyo nyumba kubwa mpaka ikaisha kwa ela yangu tu.


Nilipomuambia suala la kuacha kuomba alikataa, mara nilijikuta nina ujauzito mwingine, hapo ndipo alifurahi sana na kuniambia niwe naenda na mtoto na mimba yangu. Wakati huo Steven alikua mkubwa ana miaka mitatu lakini hakutaka nimuache nyumbani pamoja na kuwa na binti wa kazi. Kusema kweli nilikua nahisi kudhalilika hivyo nikamuambia kuwa mimi siwezi kuomba tena, aliponiona kuwa nipo siraisi aliniambia kuwa anataka kufunaga ndoa na mimi kwani ananipenda na hataki kuniacha.


Mimi nilimuambia sawa, kwa hali nyangu nilijua kuwa siwezi kupata mwanaume mwingine wakunipenda kama yeye na hata kutaka kunioa. Nilikubali kufunga naye ndoa ila sikujua sbabau yake ya kutaka kunioa. Kumbe baada ya kuona kuwa nimekasirika sitaki tena kuomba alitaka kubadilisha hati ya nyumba ili iwe na jina lakre na anidhulumu, alishafanya kila kitu lakini ilishindikana kwakua nilikua na hati kabisa ya wizara haikua ni karatasi ya mauziano.


Aliposhindwa ndiyo akataka kunioa, nilikuja klugundua hivyo kwani baada tu ya ndoa alianza kuniambia kuwa anataka tuchukulia nyumba mkopo ili tufungulie Biashara. Mimi nilikubali lakini tulipoenda Benki ili kutaka mkopo ndipo aliumbuka. Kule Benki alikua ahsoangea na mtu ambaye walipanga kuwa, pamoja na kuwa sina Biashara ila nipate mkopo, lakini nikiwa kule tulikutana na Dada mmopja ambaye aliposikia kuwa mimi ni mke wake alishanaa.


Kumbe yule Dada alikua ni mdogo (Mooto wa Baba mdogo) wa na mchumba wake ambaye alikua ashamtolea mahari lakini walikua hawajuani na Baba Steven, basi aliponiona nipo naye alichunguza na kuja kunitafuta. Wakati Baba Steven aanaongea na watu wake alinitafuta na kuniuliza mimi ni nani? Nilijua ni mambo ya Kibenki nikamuambia kuwa yule ni Mume wangu wa ndoa na nyumba amabyo ntunachukulia mkopo ina jina langu, nikamuambia pia kuwa nina mtoto naye mmoja na wakati huo nina ujauzito mwingine, hilo sikua na haja ya kumuambia kwani nilikua na mimba kubwa karibu kujifungua.


Yule Dada aliniuliza mara miamia, ksiahaaknaiambia kuwa nisikubali kusaini chochote kwani naelekea kuibiwa. Nilishangaa lakinia liniambia hivyo kuwa yule Baba Steven ni shemeji yake na kamchumbia Dada yake hivyo kama nikichukua mkopo basi nitatapeliwa.


“Lakini nina ndoa naye ya kanisani?” Nilimuuliza.


“Hata kama lakni jua kuwa ukisaini huo mkopo umetapeliwa!”  Niliona kama ananitania kwani kwa mazingira amabyo nilikua naishi na mume wangu alikua anaonyesha kuwa ananipenda sana, ananijali na kunihudumia vizuri.


Ukiachilia lile suala la kunilazimisha kuomba alikuaananipenda kama malaika, nilijihisi kupendwa na kujiona kama mzima kabisa. Pia nilikua nawaza mpaka mtu ananivumilia mlemavu kamka mimi basia takua na upendo wa ajbu, sikutaka kumsikiliza, lakini wakati huohuo nilishikwa na uchungu, sikua na uwezo tena wa kuweka kidole gumba ili kuchukua mkopo, nilipelekwa hospoitalini nikajifungua mdogo wako wapili.


Baada ya kujifungua nilirudi nyumbani, apo ndipo nilishtuka kwani mume wangu alikua ankazania sana mkopo. Nikajiulzia kama Biashara ni ya kwangu kwanini nichukue mkopo sasa hivi wakati bado nimelala ndani, kwanini asisubiri mtoto ahta akue ndiyoa niambie mambo ya mkopo. Nilishtuka kwakweli nikakataa katakata. Katika bishaanabishana hiyo kuna sikua alikuja huyo mchumba wake, mimi niliku nimelala chumbani na mwanangu.


“Nimeshakuambia kuwa huyu ni Mama tu namsaidia lakini si mke wangu, hivi kwa akili zako mimi naweza kuoa mtu mzima kama huyu, huyu si Kama Mama yangu tu, mbona unakua na roho mbaya namna hii, nifunge ndoa mjini hapa usijue?” Alikua anasema, walibishana sana ailionyesha mchumba wake alikua kaambiwa kuhusu mimi na alikua kakasirika. Basi niliposikia hivyo na mimi nilitoka, sikutaka kukaa ndani, nilitoka na kumuambia yule dada kuwa mimi ni mke haslali tena ndoa ya kanisani, nimebadili dini kwajaili yake na kama haamioni nakafuatilie katika kanisa ambalo ulifungia ndoa.


Mume wangu alinifuata na kuanza kunipiga akinikana kuwa nisimharibie maisha yake lakini niliongea kuhakikisha yule Dada anajua nikamuambia mpaka na tarehe ya ndoa.dada aliondoka kwa hasira na sikumsikia tena, mume wangu akabadilika, akawa ni mtu wa hasira, kila siku kunitukana, kunipiga na ammbo mengine mengi. Tulikua tunagombana sana lakini bado alisisiiza kuhusu kuchukua mkopo, mimi nilikataa katakata nikijua kuwa lazima ataniacha.


Basi aliondoka na kuniacha nyumbani peke yangu na watoto, aimchukua mpaka binti wa kazi, sikua na namna zaidi ya kurudi kuomba kwani wakati anaond0ka alichukua kila akiba yangu yote ambayo nilikusanya kwaajili ya Biashara. Nilirudi kuomba na wanangu wawili, kila nikipata pesa najikusanya, lakini nayyeye maisha yalimuwia magumu basi akarudi kwangu akaniomba msamaha lakini akawa kila nikirudi kuomba ananinyang’anya pesa na nikilalamika nikipigo.


Tangu wakati huo ndiyo yamekua maisha yangu. Ananipiga na kunitukaka sana, ananiambia ananisaidia kuishi na mimi, ila pes anachukua kwangu, anakula na wanawake zake, ana watoto kila sehemu ila hataki kuniacha, ananiambia kuwa yeye ni mume wangu hivyo kama nimeichoka ndoa basi nikadai Talaka mimi ili tugawane nyumba.


“Sasa Mama kama ni hivyo kwanini huondoki, kama ni kudai ntalaka dai mgawane hiyo nyumba kwanini uteeke hivi?” Nilimuuliza Mama kwa uchungu.


“Mwanangu, natamani sana lakini siwezi kuacha wanangu, nilifanya kosa kukuacha wewe lakini si hawa wanangu.


Ingawa hawanitambui kama Mama yao alkini angalau nawaona wanakua mbele ya macho yangu.”


“Hawakutambui kama Mama yao, kwanini unasmea hivyo? Si unaishi nao?” Nilimuuliza.


“Ndiyo naishi nao, lakini alininyang’anya tangu wakiwa waodgo akaniambia kuwa hataaka wanangu kujua kuwa wamezaliwa na mwanamke kama mimi kwani itawaathiri kisaikolojia. Alinihamishia mimi huku na huko kwingine wakawa wansihi nawanangu, anawaambia kuwa Mama yao amekufa na mimi ni mtu tu ananisaidia kwakua anaroho nzuri….” Mama alikua anaongea kwa uchungu sana, alikua analia, nilikua nimepitia machungu mengi na kumlaumu Mama yangu kuwa anakula starehe wakati mimi nateseka lakini stori yake iliniumiza sana.


Wakati tukiwa pele Mama ananiambia Yule Baba aliingia, hakugonga hata mlango alikuja moja kwa moja na kuanza kuvua nguo.


“Nataka kufanya mapenzi na Mama yako, vipi unatoka au nawewe unataka kuungana na sisi!” Aliongea huku akicheka, alionekana kwua na dharau sana, hakutaka hata kusubiri jibu langu alimvamia Mama ambaye alikua hata hawezi kujiteteea na kuanza kumvua nguo. Hasira zilinipanda, nilijihisi kutetemeka, alikua anataka kumbaka Maama yangu tena mbele yangu, nilijikuta nanyanyuka na kumuambia.


“Kwanini uhangaike na huyo mlemavu tena mzee wakati mimi mtoto mbichi niko hapa, kama una hamu njoo tumalizane na mimi!” Nilimuambia huku kikimshika kiuona na kumnyanyua.


Kuna MATAPELI wengi ambao wanatumia Jina langu la IDDI MAKENGO, unapomuelekeza mtu Instagram muambie akaunti yangu ni @iddimakengo sina akaunti mbili wala tatu ni moja tu. Unapolipia Kitabu hakikisha jina linakuja IDDI MAKENGO mwingine yoyote ni TAPELI na namba ni mbili tu, narudia mbili tu. M-Pesa No. 0742-381-155 au Tigo Pesa No. 0657-552-222 narudia jian hakikisha linakuja IDDI MAKENGO.


Je, Fatma atafanya kweli mapenzi na huyo Baba mbele ya Mama yake? Vipi kuhusu makovu yalisababishwa na nini? Basi nisikuchoshe, tukutane sehemu ya kumi na tatu.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA KUMI NA TATU


Nilimnyanyua kama moto akanyanyuka, katika kitu nilichojifunza kwenye kazi yangu ya umalaya nikuwa, wanaume wengi wababe ambao wanapenda kuhdalilisha wanawake ni hawana kitu. Yaani wanajiamini tu wanapokua na wanawake wanyonge ambao wamekubali kudhalilika. Lakini ukimkazia na kumuona kuwa naye si chochote kitu basi anajikuta ananywea na kushindwa kufanya chochote.


“Wewe mtoto una akili kweli, unataka kufanya nini? Au unafikiri nitashindwa kufanya mapenzi na wewe mbele ya Mama yako?” Alianza kujichetua, mimi nilimvuta uande wangu, nikashika uume wake na kuuvuta kwangu, Mama alikua anaomba msamaha na kumuomba ku3wa asinifanye kitu chochote.


“Mama huyu hawezi kunifanya kitu kumbe kadude kenyewe kadogo hivi!” Niliongea, si wkamba alikua na maumbile madogo gapana, lakini kw auzoefu wangu nilikua najua kuwa kila mwanaume ukimuambia hivyo basia nachanganyukiwa na kweli alichanganyukiwa.


“Unamaanisha nini?” Aliongea huku akitaka kunikunja kunipiga.


“Baba, kama unataka kunipiga basi ni kitandani sio ngumi, wanaume wenzako wanakomaa kitandani sio kama hivi. Ila kwa hiki kidubwasha chako mimi naona tu utoke kwakua leo ninakikohosi, nikikohoa hiki kinatoka, ondoka humu tutafanya kesho nikiwa sawa!” nilizidi kumuambia, ingawa kulikua na kagizagiza kutokana na mwanga hafifu lakini nilimuona ananyong’onyea, wakati wote naongea hayo yote nilikua nimeshikilia uume wake, yaani ulikua unayeyuka, msisimko unapotea kama kamwagiwa maji ya barafu.


Mama alikua kachanganyikiwa, amesimama haopni kitu lakini anabembeleza kuniombea msamaha, lakini mimi wala nilikua sijali. Kwenye kitu ambacho kilikua hakiniogopeshi katika maisha yangu kwa wakati huo ilikua ni wanaume, nilijua kabisa kuwa hawezi kunibaka, hata kama angekua na nguvu za namna gani lakini alikua ni mwanaume na hana jipya kwangu. Nilishakutana na wanaume ambao wamechanganyikiwa lakini nikiamua haifanyi chochote hanifanyi.


“Acha dharau, huyu mtoto wako simtaki tena hapa! Kesho anaondoka, simyaki tena hapa!” Aliongea hukua kivaa nguo zake, alikua anataka kuondoka.


“Hapana Baba, hii ni nyumba ya Mama yangu, najua kila kitu, huna chochote humu ndani, kesho unaondoka na Mama hii ndiyo mara yako ya mwisho kulala kwenye hiki kibanda cha mbwa, huyu mbwa wako anaondoka kesho na nimuambie tu haondoki na chochote!” Ingawa nilikua sijajua kama nitafanya nini kesho yake lakini nilikua na uhakika kuwa huyo mwanaume anaondoka.


Alianza kufoka nakutukana akijifanya kuwa nyumba ni yake kajenga na jasho lake.


“Baba, hapa kesho unaondoka, ushazoea kumtishia Mam yangu, umemnyang’anya mpaka watoto lakini nakuambia tu kuwa, kesho unaondoka na hawa watoto utawaacha mbwa wewe!” Nilimuambia huku nikimsukuma kutoka nnje, alutoka kama mlevi huku akilalamika kuwa hataondoka na mimi nitaona.


Baada ya kuondoka Mama alipaniki sana.


“Hivu unamjua huyo mtu, kwanini unamuambia hivyo, atatufukuza!” Mama alilalamika, nilijikuta nacheka tu. Alishangaa kwanini nacheka, aliniuliza kama nina plani yoyote ya namna ya kumuondoa huyo Baba lakini nilimuambia sina plan lakini nina uhakika kuwa ataondoka.


“Kama stori uliyonipa ni yakwako basi jua kuwa ataondoka ingawa sijajua ni kwa namna gani? Mama niamini kuwa mimi si yule mtoto ambeya uliniacha kipindi kile. Hatutaonewa tena na nikuambie tu Mama kuwa, nikimalizana na huyu mbwa basi naenda kupambana na Shangazi, mali zote za Baba ni lazima zirudi!”


Nilimuambia Mama lakini hakuonekana kukubaliana na hicho kitu, nilipotaja tu mali za Baba nilimuona kabsailika, uso umejaa uoga ni kama laikua anataka kuniambia kitu lakini alisiota.


“Narudia, Shangazi ni lazima kunirudishia kila kitu, nimteseka sana, mimi si wa kuwa masikini, nitachukua kil akitu na kama kafoji vitu akauza mali zangu basi wataenda jela wote! Mama najua kila kitu sasa hivi, mtaa umenifundisha maisha, ukiwa malaya lazima ujue kila kitu. Ukitembea na Polisi unakua askari, ukitembea na mwanasheria unakua mwanasheria, najua nina haki zangu hivyo lazima kupambana naye!”


Nilimuambia Mama, badoa lisita kuniambia kitu lakini nilizidi kuchombeza kuhusu Shangazi ndipoa lishindwa kuvumilia.


“Mwanangu sitaki yakukute yaliyonikuta mimi, hizi mali tutatafuta nyingine, Shangazi yako si mtu mzuri, ni muuaji anaweza hata kukuua ili tu kubaki na mali!” Aliniambia.


“Mama, namjua Shangazi, najua ni muuaji lakini kumbuka hata hao wauaji nwanakufa. Mama nimeamua, Baba yangu pamoja na ushenzi wake alitafuta mali ili nisife masikini, sitakufa masikini, nitahakikisha kila kitu changu nachukua. Si kwasababu nina shida ya mali hapana bali ni kwakua nataka kumuonesha Shangazi kuwa yeye siop mungu!”


“Mwanangu, nakuomba acha, nimeshakuona sitaki kukupotezas kabisa, kuhusu mali achana nazo, achana na Shangazi yako na achana na huu Baba!” Alizidi kusisitiza na mimi niligoma.


“Uafikiri kwanini mimi ni mlemavu, sikupanga kukuambia lakini naona niokuambie tu ili usijekuwa kama mimi. Nakupenda sana mwanangu, mimi baada ya kuja kutupwa huku moshi nilirudi nyumbani. Ndugu walijua nimefiwa lakini nina msiaha yangu, nilikua najitambua, nikarudi hapa lakini nilikua sina amani kabisa, kila siku nilikua nawaza kuhusu wewe!


Basi nilihangaika kutafuta pesa, nikahangaika kutafuta nauli, lengo langu lilikua ni kuja kukuchukua na nilipanga kuja kukuchukua shuleni. Nilijua kabisa kuwa Shangazi yako hawezi kuniruhusu kukuchukua kwania nakuhitaji ili kuendelea kubaki na mali zako, na kwa waliyokua wamenifanyia nilijua wakiniona wanaweza kuniua.


Kwakua nilijua unasoma wapi na shuleni natambulika kama Mama yako basi nilijipanga kwenda kukcuhukua shule, nilienda kukuomba kukuchukua kwa muda kuwa kuna mataizo nyumbani lakin nikaambiwa kuwa unaumwa hukwenda shule. Basi Mwalimu wako ambaye ndiyo nilikua nawasiliana naye tangu naishi na wewe aliniambia nimpe namba yangu ya simu ili kama kesho yake utakuja shule basia niambie, kweli nilimpa namba yako.


Kesho yake mchana alinipigia simu, aliniambia kuwa upo shuleni hivyo naweza kuja kukuchukua. Kweli nilienda, lakini nilipofika nilikutana na Shangazi yako, alikua ananisubiri getini, akaniambia anataka kuongea na mimi lakini sikutaka. Niligoma kuingia kwenye gari ila alikua na vijana wawilia mbao walinikamata na kuniingiza kwenye gari kwangunvu, Shangazi yako alikua anaendesha gari, alinitukana sana na kunaimbia kwanza mwanzoa linionea huruma lakini sasa hivi atanipa ulemavu wa kudumu au kuniua kabisa.


Huwezi amini aliwaka gari mafuta na kunirudisha mpaka Moshi huku akiniambia kuwa kama nikufa natakiwa kufia kwetu ili asiletewe kesi. Baada ya hapo walinipiga sana na kunimwagia tindikali usoni, walinitupa Barabarani mpaka nilipokuja kuokotwa na watu. Nilipelekwa hospitalini lakini nilikua nishaharibi8ka, macho na kila kitui, nilikaa kwa muda nikaruhusiwa, ndugu zangu walinitenga, wakanikimbia na ndiyo maana nikaanza kuingia mtaani kuomba mpaka sasa haa ndugu zangu sijui wako wapi?”


Mama aliniambia, nilitamani kulia lakini machozi hayakutoka, sikujua kuwa Mama yangu alihangaika sana kunipata, hasira nilizokua nazo juu ya Shangazi nilitamani hata kumuua. Sikuongea chochote, nilibaki kimya mpaka Mama akashtuka.


“Vipi unawaza nini?” Mama liniuliza hukua kinisogelea na kunikumbatia, mwanangua likua kalala pembeni hata hasumbui wka chochote, ni kama alikua ananipa na mimi muda wa kukaa kuongea na Mama yangu.


“Uhuru! Uhuu Mama! Kuanzia kesho hatutateseka tena, wanaume watakaa mabli na sisi, hutanyanyasika tena!” Nilimuambia ingawa hata mimi sikujua nitrafanya nini? Tulilala na Mama tumekumbatiana mpaka mwanangu alipoamka nikaenda kumnyonyesha. Asubuhi yule Baba alikuja na kutaka Mama aende kuomba lakini nilimuambia hapana, Mama haendi popote. Tulibishana sana na kutaka kunipiga ila nilimuambia Mama asiwe na wasiwasi kwani jioni yake huyo Baba atakua mahabusu.


Nilimnyonyesha mwanangu na kumuacha na Mama, niliondoka mpaka mjini, nilikua sijui nitafanya nini ili kumuondoa yule mwanaume. Lakini nikiwa njiani gari niliyokua nimependa ilisimamishwa na Trafiki, hapohapo nilijikuta napata wazo. Nahitaji kwenda Polisi ingawa ikujua kama naenda kufanya nini? Nilishuka stend na kuulizia kituo cha Poisi, kilikua karibu wakanielekeza nikaenda. Kufika hata sikuingia ndani, kulikua na Kaka mmoja tu wa makamo, alikua kasimama anaangalia simu yake, alikua na nyota moja na nilijua kuwa anacheo.


Kwa ujasiri nilimfuata, kwa kumuangalia tu nilijua kuwa ameoa kutokana na pete kidoleni, alionekana mkalimkali.


“Nina shida…” Nilianza kumuambia baada ya kumsalimia.


“Shida gani si uongie kituoni…” Aliniambia huku akiwa bize na simu.


“Hapana, nataka wewe unisaidie, kuna mtu anafanya vitu vya ajabu ila najua kama nikimpeleka kituoni basi hawezi kufungwa kwa chochote. Ila nilikua nahitaji tu uongee naye kwani ninajua anachofanya si sawa.” Aliniangalia kama kwa hasira flani hivi ili niogope, lakini sikuogopa, nina kipaji cha kumsoma mtu, hivyo najua watu wengi ambao wana vyeo, wana madaraka wanapenda kuogpwa, kama usipomuonyesha hofu wala wasiwasi basia nanywea mwenyewe.


“Mimi sifanyi huo ujinga, kama unataka….” Alianza kuongea lakini hata sikumsikiliza namimi nilianza kuongea kumuelezea.


“Mama yangu ni mlemavu, ndiyo kwanza nimemjua jana, anaishi na mwanaume amabye alimdanganya mpaka kuingia kwenye ndoa. Anamlazimisha kuombaomba na kila sikua anamnyang’anya pesa zake hukua kimbaka, nahitaji kumsaidia Mama yangu, kuna nyumba alijengewa na msamaria mwema mwanaume anataka kuichukua…”


Nilimuelezea kila kitu, hata aliipojaribu kunikatisha niliedelelea, nilimuona anakasirika nuisu kunipiga makofi lakini sikunyamaza kwakua nilijua yuko kazini na hawezi kunipiga kofi.


“Mbona king’ang’anizi namna hiyo, hivi unajua naweza kukuweka ndani?” Aliniuliza.


“Uwezo huo unao lakini nina uhakika hutaniweka ndani.”  Nilimuambia kwa kujiamini.


“Kwanini unasema hivyo, kwanini nisikuweke ndani wakati ni king’ang’anizi?” Aliniuliza.


“Kwakua unaonekana una akili, na uaonekana una busara. Hivi ngoja nikuulize, kuna askari wangapi humu? Kwanini nimekuja nimekufuata wewe wakati hata sikujui, kwanini nisingemfuata yule wakati hata anacheo kikubwa kuliko wewe?”  Nilimuuliza huku nikimuonyeshea kwakichwa askari mwingine. Alimyuangalia na niliona kama katabasamu kidogl hao ndipo nilijua kabisa nishamteka akili. Binadamu yoyote anapenda kusifiwa na kuonekana ana akili kuliko watu wengine, nilijua hata kama huyo askari nayeye ni mshenzi kama washenzi wangine lakinia ngejisikia raha kuona kuwa kwa kumuangalia mara moja tu nimegundua ana akili na anaweza kunisaidia kuliko wengine.


“Nitajuaje? Kama umetumwa?” Aliniuliza huku akitabasamu.


“Kaka, nimetumwa na nani, ningekua nakuja kukupa pesa hapo sawa labda ungesema nakuchomesha TAKUKURU lakini hapa sina hata shilingiu kumi, yaani hata kama hutaamua kumsaidia Mma yangu ila nikiondioka hapa unatakiw akunipahata elfu tano, nipate nauli na pesa ya kula. labda rushwa ya ngono ndiyo naweza kukupa mila na mimi nilivyohanaika mtaani siwezi kukfanyia hivyo na naweza kukupa na UKIMWI mkakaka mzuri hivi una familia yako nikuue, hapana, wewe nisaidie tu!”


Niliongea kwa kujiamini mpaka yule kaka akawa hana namna, aliniambia niingie ofisini kwake akawa ananielekeza mambo ya kufanya kisheria nikamuambioa hapana.


“Ninachotaka mimi umtie jambajamba ili aondoke pale nyumbani. Hayo mambo ya kisheria yatakuja, nataka yule mwanaume ndiyo adai talaka ili waachane na Mama yangu ilaleo sitaki alale pale.” Nilimuambia, aliniuliza sasa tunafanya nini? Sikua na wazo kwa wakati huo ila nilimuambia atafute gari tukamuone Mama yangu kwanza kabla ya kuongea, nilitaka amsikilize Mama yangu kwanza ili amuonee huruma.


Kwa namna nilivyokua naongea aliniamini, alimchukua askari mwingine na kuchukua gari yake binafsi kisha tukaenda. Alipomuona Mama yangu hata hakushangaa, wote wawili walikua wanamfahamu kwania likua ni ombaomba wa muda mrefu. Waliongea naye kisha akachukua simu yake na kumpigia yule Baba, alimuambia anamhitaji nyumbani. Yule Baba alikuja kwani aliambiwa kuwa ni dili la kutafuta nyumba.


Alipokuja alishangaa kukutana na wale askari. Kwanza alianza kuwaka na kujifanya anawatukana na kuwambia waondoke nyumbani kwake.


“Kwahiyo unasema hii nyumba ni yakwako?” Nilimuuliza yule Baba.


“Ndiyo nimejenhga mwenyewe na nina Document zote.”


“Unaishi humu?”


“Ndiyo!”


“Kila kitu kilichoko humu ni chako?” Nilimuyuliza, wakati huo niliyabeba yale mazungumzo mpaka sakari waliokuja kunisaidia walishangaa.


“Ndiyo kila kitu ni changu na kuanzialeo wewe na Mama yako muondoke humu ndani, nilikua nawasaidia lakini nimeona hamna shukurani hivyo siwataki tena!” Aliongea hukua kinishika kunisukuma.


“Kwahiyo kama unasema kuwa kila kitu ni chako, hata ile kokein chumbani kwako ni yako? Hivyo unataka kusema kuwa unauza dawa za kulevia mbele ya sakari!” Nilimuuliza, alibaki kaduwaa, askari wenyewe walibaki wameduwaa, alibaki anatetemeka hajui hata chakuongea. Yule askari niliyemfuata kituoni alinishika na kunivuta pembeni.


“Hukuongea mambo ya madawa ya kulevia, yametoka wapi hayo umejuaje kuhusu madawa au huu ni mtego?” Aliniuliza kwa ukali kwani alikua hajui kitu chochote kuhusiana na Dawa za kulevia.


Kuna MATAPELI wengi ambao wanatumia Jina langu la IDDI MAKENGO, unapomuelekeza mtu Instagram muambie akaunti yangu ni @iddimakengo sina akaunti mbili wala tatu ni moja tu. Unapolipia Kitabu hakikisha jina linakuja IDDI MAKENGO mwingine yoyote ni TAPELI na namba ni mbili tu, narudia mbili tu. M-Pesa No. 0742-381-155 au Tigo Pesa No. 0657-552-222 narudia jina hakikisha linakuja IDDI MAKENGO.


Unadhani Fatma kafanya nini? Jea ataweza kumuondoa huyo Baba kwake? Je kuna dawa kweli na zimeingajeingaje, nisikuchoshe endelea kufuatilia.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA KUMI NA NNE


“Inamaana ulidhani utakuja kumchukua hivi hivi! Huyu ni mhalifu, lakini hatuna ushaidi wowote, hatuwezi kumukuza, ninachotaka ni nyie kumtia jambajamba hapa mpaka achanganyikiwe!” Nilimuambia yule askari ambaye alikua bado kaduwaa, hakujua mpango wangu wowote. Kusema kweli hata mimi kwa wakati huo sikua na mpango wowopte, nilitaka tu kumtishia ili aondoke.


“Kwahiyo kuna dawa za kulevia huko ndani, halafu unajua hatuna search warrant? Hapa hakuna kesi?” Askari alianza kua muoga.


“Nani kakuambia anataka kesi, mimi nataka jambajamba, tangu lini jambajamba ikahitajio search warrany, wewe nisikilize mimi nifuate mimi!” Nilimuambia huku nikimvuta mpaka alipokua yule Baba, alikua anajitetea kuwa hana kitu chochote na mimi ndiyo nilikua napanga njama ya kumsingizia kesi.


Kwahiyo unataka tyukakague?” Nilimuuliza, mimi ndiyo nilikua naongea sana.


“Twendeni, na kama hakuna kitu mnaondoka humu ndani, nakuambia nakufukuza wewe na Mama yako!”  Aliongea kwa kujiamini na kujifanya anajua sharia.


“Napia hamna RB yangu wala Search warrany, hivyo kama mkikosa kitu jueni nawashitaki wote, hamuwezio kunisingizia mambo ya uongo!” Aliongea, askari walianza kuogopa, hawakuongea lakini niliona kama wanarudi nyima.


“Una uhakika kuna dawa za kulevia humo ndani?” Askari wa cheo cha chini alininong’oneza.


“Kaka, hii nyumba kubwa, nina uhakika wanapika ugali, mnaweza kumkam,ata na unga wa ugali ukifika kwa mkemia mkuu ukageuka ukawa unga mwingine, mbona unaogopa!” Niliongea kiasi kwamba yule askari alianza kuwa na wasiwasi, aliacha kuniona kama binti mdopgo aliyeenda kulalamikia Mama yake kuonewa mpaka kuniona kama askari mwenzake.


“Twende, halafu afande huyu mnamlegezea ndiyo maana anatembea kwa kujiamini, nina uhakika kuna vitu humo ndani!” Nilimuambia, yule Baba alitembea mpaka kuingia ndani, lakini alipofika sebuleni akaambiwa kuhusu kuingia ndani aligoma.


“Mkuu naomba tuongee haya mambo yaishe!” Alianza kuomba msamaha, wale askari walitaka kumsikiliza lakini mimi nilishtuka, nilihisi lazima kuna kitu.


“Mkuu haya mambo si ya kupelekana mbali, mimi huyu Mama nitamuacha na vitu vyake, hii nyumba si yangu kweli mimi ni mgeni naomba nimuache huyu Mama na maisha yake!” Alianza kuongea, hapo ndipo nilijua kabisa kuwa huyu mtu si sawa, lazima kuna kitua naficha huko ndani.


Askari nao walishtuka, niliona kabisa kama wanataka kuongea na kumalizana na yule kaka.


“Dada kweli hakuna haja ya kufika ndani, mnaweza kuyamaliza haya mambo!” yule sakari wa nyota moja aliniambia.


“Unamaanisha nini, maana huyu ni mhalifu, hivi unajua kuwa hii kesi nimeifuatilia kwa muda gani?” Niliuliza, nilihisi kuna kitu yule Baba anaficha, lakini pia nilijua kuwa, kama nikikaa kimya askari wanaweza kunizunguka. Tayari walishahisi mimi ni mtu flani, sikutaka kujitambulisha hivyo lakini niliongea mambo ambayo wangeamini kuwa mimi ni mtu wa usalama.


“Umeifuatilia kivipi mbona sikuelewi Dada?”


“Hamna jity ila ninachosema mnatakiwa kufanya kazi zenu kwa mujibu wa PGO (Huu ni muongozo wa polisi na unajulikana kwa polisi tu).


Niliongea maneno amabyo nilikua nayapata kwa wateja wangu, lengo langu ilikua ni ili waniogope na kudhani kuwa mimi ni mtu flani najua sharia. Kweli ilisaudia kwani walilazimika kukagua, sikujua watakuta nini ila walikuta Nusu gunia la Mirungi. Kumbe yule Baba alikua akiuza mirungi na Mama alikua anajua ila hakuniamba. Walimkamata na kumpeleka kituoni, kule alikaa kama siku tatu hivi akawekewa dahamana na afiki zake, walikua hata bado hawajamfungulia kesi wakijaribu kuongea na mimi ili tuyamalize.


Alihonga polisi lakini ni kama wlaikua wananiogopa mimi kwani hawkautaka kuamini kuwa mimi ni binti tu changudoa. Niliwamabia kama wanataka hiyo ishu iishe basi yeye afungue kesi ya kdai talaka mahakamani na kuandikishana kwa mwanasheria kuwa hahitaji kitu chochote na waoto atamuachia Mama. Basi hakua na namna, alifanya hivyo, akafungua kesi ambayo hata haikuchukua muda, miezi minne tu tulipata talaka na Mama akwa huru.


Maisha yalikua mazuri, niliapa kuwa Mama hataomba tena na mimi sitakua masikini tena. Sikua na akiba yoyote lakini Mama alikua na pesa zake kama milioni moja hivi. Alitaka kurudi kuomba ila niliona ni kama kujidhalilisha. Nilichukua ile pesa na kwenda kutafuta sehemu sokoni, niliamua kuuza nguo za mitumba. Kama baharti tu Biashara ilianza kwenda vizuri lakini kutokana na mahitaji makubwa niliona bado. Nilimshauri Mama kupangisha ile nyumba na sisi kwenda kutafuta nyumba ya kupanga ya hadhi yetu.


Kweli tulipata mpangaji, ilikua ni nyumba kubwa na tulipata kampuni moja ambayo ilikua inatulipa milioni moja na laki mbili kwa mwezi. Hapo ndipo kila kitu kilibadilika, niliacha kuuza mitumba na kufungua duka la vifaa vya simu, lilipanuka taratibu na baada ya mwaka nilikua na duka la simu pale Moshi stend. Maisha yalikua mazuri ila sikua na amani kabisa, ingawa Mama alikua akiniambia kila siku niache kuuatilia mali za Baba yangu kwani sitaniua lakini sikutaka kukubaliana na hiyo hali.


Nilikua naumia sana, sikua na shida na mali ila nilikua na roho ya kisasi sana kwa Shangazi yangu. Kumuacha hivi hivi kwa amani kwangu ilikua ngumu sana. Kila siku nilikua nakumbuka kila kitu alichonifanyia na nilikua naumia sana, kila nikimuangalia Mama na namna alivyokua anateseka kwa ulemavu ambao alisababishiwa na Shangazi nilijiona kama mkosaji kumuacha Shangazi yangu hivi hivi.


Wakati mmoja nikiwa Dar kuchukua mzigo nilishindwa kuvumilia kabisa, niliamua kwenda kumuona na kuangalia anaendeleaje, sikua nawaza kuhusu kuchukua mali zangu ambazo nilikua nimeachiwa na Baba yagu, hapana, kikubwa nilichokua nataka ni yeye kuniona nikiwa nimefanikiwa kwani kila siku alikua ananiambia mimi nitakua ni mu wa kuteseka katika maisha yangu yote.


Nilikua napakumbuka vizuiri nyumbani kwetu amabpo ndipo alikua akiishi Shangazi yangu. nilifika nakumbuka ilikua ni wakati wa jioni, nyumba ilikua ni ileile ingawa kwa wakati huo ilionekana kama ni ya zamani sana imechoka kutokana na nyumba mpya nzuri za mtaani ambazo zilikua zimejengwa hapo jirani. Niligonga mlango na kufunguliwa na Binti mmoja, nilimuulizia Shangazi yangu akaniambia ametoka na mara nyingi narudi usiku hivyo kama kuna maagizo yoyote nimuachie.


Yule binti ambaye alikua ni makamu yangu alikua anaongea kwa nyodo flani, ni kama alikua na haraka zake, yaani alionekana kukerwa na swali langu kuhusu Shangazi. Kutokana an mambo niliyopitia katika maisha yangu nilikua sipendi tena dharau hasa kudharauliwa na mtu ambaye naona kabisa hajanizidi chochote.


“Dada nimekuambia kuwa huyo mtu hayupo, kama una maagizo yake nniachie au mpigie simu uongee naye!” Aliniambia kwa hasira baada ya kuona bado nimesimama na shangaashangaa, sikua hata nikimshangaa yeye, nilikua nikiangalia nyumba ya Baba yangu na kukumbuka maisha yangu ya zamani, kulikua na kumbukumbu nyingi sana katika ile nyumba nzuri chache nyingi mbaya sana.


“Dada husikii, nimekuambia hayupo au nikipe namba yake umpigie?” Aliniuliza kwa hasira tena, nilishtuka ndipo nikamuona kuwa kumbe bado yuko pale, nilimuangalia kwa dharau nikajiuliza hivi huyu mbuzi hanijui?


Wakati kasimama katikati nya mlango kama ananiangalia ili niondoke nilimsukuma kisha nikaingia kwa ndani.


“Niondolee Janaba hapa mbuzi wewe! Ushakua mtu mzima ukitoka kufanya mapenzi unaenda kuoga sio kuja kufungua mlango moja kwa moja, au hujisikii unavyonuka uc***!” nilimuambia kwa hasira, ni kweli alikua katika kufanya mapenzi, kwa uzoefu wangu nilisikia harufu nikajua katoka kufanya mapenzi bila kuoga.


“Unasema nini? Yaani unaingia bila ruhusa nyumbani kwa watu?” Aliniuliza huku akinifuata, akanishika bega kutaka kunivuta kwa nyuma, hapo ndipoa linitibua, niliushika mkono wake na kuuvuta kwa mbele akasogea kisha nikamsukuma akadondoka.


“Nimekuambia usinishike na majanaba yakop mshenzi wewe!” Nilimuambia huku nikiingia ndani, niliongozana mpaka sebuleni, kufika sebuleni nilimkuta Baba mtu mzima kakaa amejifunika taulo tu huku anaangalia TV. Hapo ndipo nilijua kabisa huyo binti alikua anafanya mapenzi na nani tena sebuleni.


“Wewe ni nani? Unafanya nini huku ndani? Nani kakuruhusu kuingia?” Yule Baba alioniuliza, mimi hata sikumjibu, nilijisikia kinyaa nikaenda kukkaa kwenye kiti cha kawaida, sikutaka kukaa kwenye makochi kwani nilijua wahsayatumia sana kwa ujinga wao.


“Baba hembu ongea naye, amekuja hapa anamuulizia Mama mdogo kaingia bila ruhusa!” ule binti aliongea.


“Nyie washenzi yaani mnaitana Baba wakati mmetoka kunyanduana? Makubwa dunia hii!” Niliongea, tulibishanabishana pale wakiniambia niondoke lakini mimi niligoma nakuwaambia kuwa nitamsubiri Shangazi mpaka aondoke.


Yule Baba kuona hivyo alisimama na kwnda ndani kuvaa nguo, alikuja na kunisimamia pembeni yangu huku akinishika na kutaka kunitoa ndani nnje. Kwa kumuangalia alikua na mwili mkubwa, yaani nikisimama namfikia mabegani, mwili ulijaa na kusema kwelia ngetaka kunipiga ni ngumi moja tu mimi hoi au angeweza kuninyanyua mzimamzima na kunitupa nnje. Lakini kutokana na uzoefu wangu kupigana ishu sio nguvu bali timing, kujiamini na kucheza na saikolojia ya mipinzani wake.


“Nyanyuka kabla sijakunyanyua! Ondoka nyumbani kwnagu, kama huyo mbwa mwenzako sijui unamuita Shangazi mnajuana basi msubiri huko nnje lakini si hapa kwangu!” aliniambia hukua kiwa kanisimamia kwa mbele yangu, mimi nilikua bado nimekaa kwenye kiti cha mbao hivi vya kuegemea, nilinanyuka kama nataka kuondoka, lakini akiwa hana hili wala lile nilikinyanyua kile kiti kwa nguvu na kukishushia kwenye vidole vyake vya miguu.


“Mamaaaa!” Nilisikia anapiga kelele, kabla hata hajasikilizia maumivu vizuri nilimpiga teke la kwenye sehemu zake za siri, lilikua teke la nguvu kiasi kwamba alilala na kushindwa kunyanyuka hukua akiugulia maumivu!


“Mshenzi mkubwa wewe na huyu unayemuita mwanao, yaani nyumba wajenge wanaume wenzako wewe uje uiite yako!” sijui kwanini nilifanya vile, wale watu nilikua siwajui wangweza kuwa ni wapangaji, wangeweza kuwa ni watu walionunua ile nyumba ila sikujali, nilihisi tu ni wavamizi na nilijisikia raha kufanya vile.


Yule Baba alikaa chini nusu saa anugulia maumivu, hata aliponyanyuka hakuwa sawa, alikua analia, mtoto wake alitukana sana na kuongea sana lakini mimi hata sikuimjali. Alimpigia simu Shangazi yangu ambaye baada ya kama lisaa limoja hivia likuja pale nyumbani. Wakati huo yule Baba alikua kakaa kwenye kochi, hakuniongelesha, hakuniuliza chochote na wala mimi sikuonekana kujali, yaani kwa jkitu nilichomfanyia nilijua fika kuwa hawezi kunigusa na kama angenigusa tayari nilikua na bisibisi yangu kiunoni ambayo nilikua natembea nayo kila mahali.


“Fatma!” Shangazi aliita baada tu ya kuniona, alibaki kaduwa akama dakika tano, ananiangalia kama haamini, yaani ni kama alikua kaona mzimu, aliniangalia sana kisha akataka kuja kunikumbatia.


“Nimekutafuta sana mwanangu, kumbe bado upo hai…” ASlitaka kuja kunikumbaia lakini nilikua nahasira naye, nilimsukuma kwa nguvu kidogo adondoke.


“Nimekuja kukuona na kuchukua kilichochangu, sikuja kuongea wala kujadiliana chochote, najua uanjua kilichochangu!”


Nilimuambia, alianza kujielezea uongo naman alivyohangaika kunitafuta, alijua nimekufa na mambo kibao lakini mimi nilikua namuagalia tu.


“Ukimaliza kuongea Mama jua kuwa nimekuja kuchukua changu, najua kila kitu, nimeshamuona na Mama yangu na najua ulichomfanyia!” Niimuambia. Alianza kujishtukia na kunniambia kuwa hajui kitu chochote kuhusu Mama yangu lakini nilimuambia kuwa mimi si kwenda pale kuongea bali kuchukua kilicho changu.


“Mali zote hizi ni zangu na kama ulidhani kuwa nimekufa basi umekosea!” Nilimuambia, aliniangalia kwa dharaau hukua kicheka, ingawa cheka yake iliukua ya kupaniki flani, alikua kama ananitisha flani hi hivi.


“Wewe mjinga kweli, huna chako hapa, hizi ni mali  za Kaka yangu na nimeziendeleza, kila kitru ni changu na mume wangu!” aliniambia.


“Mume wako, mume gani, huyu mjinga ambbaye anafanya mapenzi na malaya wake kwenye makochji yetu!” Nilimuambia.


“Kuwa na adabu, huyu ni mume wangu na huyu ni mtoto wetu!”


“Huna mtoto wewe, huwezi kuwa na mtoto mkubwa namna hii na kama ni mwanao basi jua Baba yake anamkula, au unafikiri hizo chupi zinafanya nini hapo kwenye kochi?” Nilimuuliza, wote walishatuka kwani hakuna aliyekua amekumbuka kuondoa nguo zao walizovua wakati wanafanya mapenzi.


Kwenye kochi kulikua na nguo za ndani za kike na kiume zimewekwa pamoja. Shangazai alishikwa na Bumbuwazi, akamgeukia yule mwanaume na kuanza kumshutumu kwua anamsaliti.


Waligombana kwa muda huku mimi nawaangalia. Mwisho niliona yule Baba yalimshinda.


“Utatembeaje na mtoto wako wa kumzaa? Hivi unanisaliti tena ndani ya nyumba yangu!” Shjanazi alimuuliza.


“Nyumba gani yako, hii nyumba ni yangu, si ulibadilisha majina ikawa yangu, sasa ni yangu na wewe acha kuwa mjinga, huyu si binti yangu ni mke wangu, niko hapa kwako kwaajili ya pesa tu ila siwezi kuoa mwanamke kama wewe, mwanamke tumeishi ote mwaka wa nne sasa hivi hata kuzaa huzai nikupeleke wapi?”


Walianza kugombana na kutukanana sana, mimi nilikua nawaangalia tu, Shangazi alionekana kuchanganyikiwa kwani kuna vitu vingi alifanya kwa majina ya huyo Baba. Niliwasikiliza kwa muda ili kupata umbea, jinsi walivyokua wanaongea ndipo niligundua kuwabaada ya mimi kuondoka Shangazi hakubadilisha kitu chochote, lakini alipokutana na huyu mwanaume alimshawishi kutafuta cheti cha kifo changu ili aweze kuwa mrithi wa mali za Baba yangu. huyu mwanaume alimsahwishi kuwa waandike zile mali majina yake ili hata kama ikitokea nikarudi basi isiwe rahisi mimi kuchukua mali za Baba yangu kwani tayari zitakua na majina ya mtu mwngine.


Mwanzo huyu Baba alikua akifanya kazi, ni mwanasheria ambaye hajapata uwaikili abdo, lakini baada ya kukutana na shanazi bai alianza kuishi naye tu na kubadilika kutoka kuwa mfanyakazi na kuwa Baba wa nyumbani. Alimdanganya Shangazi kuw aalikua na mke lakini akafariki hivyo amemuachia mtoto mmoja mkubwa ambaye alikuja naye pale, lakini katika kutukanana niligundua kuwa kumbe yle Baba alikua kaoa, familia yake iko mmkoani ambapo anaenda mara kwa mara na mke wake anajua kuwa mume yuko mjini anafanya kazi.


Wligombana sana mwisho wkaataka kudundana, wakashikana na kuvurugana baadaye wakaacha. Muda wote mimi nilikua nawaangalia, walipomaliza na kutulia nilimgeukia Shangazi yangu na kumuambia.


“Hizi mali ni zangu, ujinga wote mliofanya utawapeleka jela, mimi si yule Fatma wa zamani, huyu Mbuzi wako ni mwanasheria hivyo nadhani anajua kughushi na kuidanganya mahakama, kupata mali kwa udanganyifu ni kosa kisheria na anakaa jela muda gani?” Nilimuambai, walinibishia huku wakinitishia kuwa niende popote lakini mali zile ni zao.


“Tena ondoka hapa, sikutaki ndani kwangu, narudia ondoka hapa!” Shangazi aliniambia huku akinishika na kunisukuma, nilimgeukia na kumuangalia kwa dharau kisha nikemgeukia yule Baba.


“Muambie mwanamke wako aniache, muambie kuwa mimi si kale kabinti ambako alikua anakatesa, muambie kuwa nina hasira naye naweza kummaliza hapa na nikasamehe kila kitu!” nilimuambia yule Baba ambaye alikua ananiangalia kwa u0ga, pamoja na manguvu yake yote lakinia likua anamuogopa.


“Hakuna haja ya kugombana, hembu muache aondoke taratibu!” Yule Baba alimuambia Shangazi hukua kimshika na kumsihi aniache.


“Kuondoka! Hivi nyie mbuzi mna akili kweli, nani kawaambia kuwa mimi nataka kuondoka, niondoke niende wapi, nitabaki humuhumu ndani na hamnifanyi kitu chochote!” Niliongea huku nikimsukuma Shangazi, sikupanga kumfanya kitu chochote lakini alinisukuma kwa hasira,.


“Nani unamuita mbuzi, nimekulea mimi mjinga wewe nakuambia utaondoka la sivyo nitakufanyia kitu kibaya, muulize Mama yako nilichomfanyia!”


Alipomtaja Mama yangu hapo alinitibua, ni kama nilikua nasubiria amtaje, nilihanda kama dakika moja nikimuangalia, matukio yote aliyonifanyia yalinirudia kichwani, nilijikuta napandwa na hasira kisha nikacheka. Niliondoka kama vile natoka, kisha ghafla kabla hajajua nataka kufanya nini nilichomoa ile bisibisi yangu kiunoni, niligeuka hatakaharaka na kuirusha, mimi nilikua nalenga jicho, wakati huo nilikua namuwaza mama yangu hivyo nilitaka kumchoma kwenye jicho,


“Mimi sio yule binti wa zamani na wala siwezi kukuacha unifanyie kama ulichomfanyia Mama yangu!” Niliongea kwa hasira, nikairuisha ile Bisibisi, kwa bahati aliione akatingisha kichwa kidogo kama anageuka, kumbe alinigeuzia sikio, ile bisibisi ilikita katikati ya sikio lake, alipiga kelele za maumivu, mimi sikuiachia, nilimrudia nikamshika nikamkaba kisha nikawa naisindilia sikioni kwake, analpiga kelele, damu zinatoka mimi nashindilia.


Yule Babaa alikuja na kunishika kwa nyuma, nilihisi kama anataka kunibaka, nilikumbuka mara ya kwanza nilipobakwa wakati nafanya kazi za ndani. Sijui nilipata wapi nguvu lakini nilimsukuma, nikaichomoa ile bisibisi nikamvamia tena na kutaka kumchoma nayo, alijitahidi kunyanyuka akanirusha pembeni akatoka nnje, alianza kukimbia  na mimi nilitoka. Alikimbia mbali sikumuona, nilirudi na kumkuta Shangazi yangu kalala pale chini damu zinamtoka yule mwanamke amabye alikua anamuona mtoto alikua anajitahidi kumnyanyua.


“Nimeua!” nilijikuta napiga kelele, sikuatak akuendelea kukaa hapo. Moja kwa moja nilitoka nnje, nikawaza mara mbili kuhusu kutoroka lakini nikasema hapana, kama nikitioeroka ni rahisi kwa polisi kuinikamata, siwezi kumuacha Mama yangu. Bado nilikua nimeshikiliaile bisibisi ina damu nawaza nini cha kufanya.


“Natakiwa niende Polisi, hii ni self difence, hata kama nimeua basi sitafungwa muda mrefu kama nitaonekana kama nilikua najitetea!” niliwaza, haraka haraka nilichukua ile Bisibisi nikajichoma kwenye bega, niliikita kwa nguvu sana mpaka ikagusa mfupa, sikuishia hapo, niliiichomoa na kujichoma kwenye paja, sehemu ya nyama. Baada ya hapo nnilikimbia kutafuta boaboda, wakati natafuta nilikua napiga kelele wanataka kuniua wanataka kuniua.


Damu zilikua zinanitoka, nilipata bodaboda na kuwaambia wanipeleka Polisi.


“Dada unavuja damu sana kwanini nisikupeleke hospitalini!” kaka wa bodaboa aliniuliza.


“Hapana, nataka kuchukua PF3 kwanza.” Damu zilikua zinatoka lakini niliona si damu nyingi sana, bado nilikua nimeshikilia ile Bisibisi, mkononi hivyo nikiwa nyuma ya bodaboda nilijichoma tena shingoni hapo ndipo niliona damu zinachuruzika kwa nguvu kiasi cha kumwagikia na yule Boaboda, alitaka kunipeleka Hospitalini lakini niligoma, niliitupa ile Bisibisi akanipeleka mpaka Polisi.


Alinishusha nikiwa natokwa na damu nyingi, kusema kweli sikua nikisikia maumivu, kwa wakati huo akili yangu ilikua mabli sana, nilikua nahitaji kuonekana kama mimi ndiyo nimeonewa Shangazi yangu ndiyo kanifanyia vile.


“Wanataka kuniua, shangazi yangu anataka kuniua sababu ya mali za Baba yangu, anataka kuniua! Nilikua napiga kelele wakati anshika kwenye bodaboda, hali yangu ilikua mbaya lakini hata nilikua sijali, ni kama niliwehuka flani, askari walinikimbilia na damu zangu.


“Mbona umemleta huku, nini kimeokea?” askari mmoja alimuuliza yule dereba bodaboda.


“Shangazio yangu! Shangazi! Shangazi….” Bodaboda alimuambia kuwa hajui chochote lakini mimi niliendlea kupiga kelele huku nikimtaja Shangazi yangu kuwa anataka kuniua.


Walinichukua mpaka kwenye gari lao, Askari mmmoja aliamrisha iandaliwa PF3 huku wao wakinikimbiza hospitalini kwani nilikua na hali mbaya. Gari ilipoondoka kwenda Hospitalini baada ya kujua kuwa nipo mikononi mwa Askari ndipoa kili lirudi, nikatulia na ghafla ndiyo nilianza kusikia maumivu, nilijikuta napoteza nguvu, mwili uanchoka, natamani kuongea lakini mdomo haunyanyuki, ghafla nilipoteza fahamu sikujua hata nini kimeendelea.


INTERVIEW NA AJIRA; Hiki ni Kitabu changu kipya ambacho kinazungumzia mambo ya AJIRA. Kina maelezo kuanzia namna ya kuandika Barua ya kuomba kazi, kuandika CV kujiandaa na usahili. Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kwenye Usahili na namna ya kuyajibu, namna ya kutengeneza Connection za kiajira na namna ya kutumia mitandao kupata ajira.


Kisome kutokana na mahitaji yako ya wakati huo, iwe unajiandaa kwa usahili au ndiyo unaandika Barua au kuandaa Cv. Bei yake ni shilingi elfu kumi. Kupata kitabu unalipia kwa M-pesa No. 0742-381-155 au Tigo Pesa No. 0657-552-222 Jina linakuja Iddi Makengo, sina namba nyingine zaidi ya hizo baada ya hapo kitabu utatumiwa kwa njia ya Whatsapp/Email/Facebook.


Fatma anamchoma Bisibisi Shangazi yake je ndiyoa memuua au itakuaje, vipi kuhusu yeye hali yake, je hatima yake ni nini? Nisikuchoshe, endelea kufuatilia ukurasa wangu huu ujue nini kitaendelea.


ITAENDELEA….


FATMA; BABA HAKUNA KUPUMZIKA KWA AMANI NATAKA KABURI LAKO LICHEZE!—SEHEMU YA KUMI NA   TANO


Nilizinduka nikiwa hospitalini, nilikua nimeshashonwa na kuwa vizuri, maumivu yaliyokuepo yalikua ni yakawaida. Nilikua nimeumia lakini si sana. Hali yangu ilikua nzuri na nilikua najitambua kabisa, moja kwa moja nilikumkumbuka Shangazi yangu, kwa jinsi nilivyomshindilia ile Bisibisi nilihisi kabisa kuwa alikua amekufa hivyo ilikua ni lazima kufanya kitui ili kuonyesha kuwa mimi ndiyo nilivamiwa na si mimi niliyeanzisha vurugu.


“Nakufaaa! Nakufaaa! Nisaidieni Shangazi anataka kuniua, anataka kuniua!” Nilipiga kelele kwa nguvu, manesi wlaikuja na kunishika lakini sikutulia, nilikua najirusha, naoghopa namtaja Shangazi yangu huku nikiwaomba wanipeleke polisi ili niwe salama kwani Shangazi anaweza kuniua.


“Alitaka kumuua Mama yangu, akammwagia tindikali, sasa hivi nimerudi kudaio mali za Baba yangu anataka kuniua, sitaki, sitaki, siwezi kuka ahapa, atakuja, ana mkono mrefu, nataka niende polisi, nipelekeni hata mahabus, ataniua!”


Nilizidi kupiga kelele, nilipiga kelela mpaka wakalazimika kunichoma sindano ya usingizi. Nilipokuja kuzinduka tena nilitulia, akaja nesi mmoja akaniambia kuwa Shangazi yangu amekamatea na polisi. Nilitaka kumuuliza kama  amepona lakini sikutaka ijulikane kama najua kinachoendelea, nilijifanya kutulia lakini sikua na amanani, nilitaka sana apone kwani sikutaka kuwa muuaji.


“Ameumia sana, hana fahamu lakini Polisi wanamlinda, yuko chini ya ulinzi na akipona anaenda jela moja kwa moja.” Nesi aliniambia.


Nilikaa hospitalini kwa siku tatu nikaruhusiwa kutoka, nilikua vizuri naweza kutembea na kufanya kila kitu. Nilienda polisi kuandika maelezo, niliwaambia kuwa mimi nilikua Dar kibiashara lakini nikaamua kwenda nyumbani kwetu kuongea na Shangazi yangu kuhusiana na Mali za Baba yangu ambazo alikua ameniachia, lakini nilijikuta nipo katikati ya mikono ya Shangazi na mume wake pamoja na binti mwingine ambao walinivamia na kuanza kunipiga.


Shangazi ndiyo alikua na bisibisi, alinichoma sehemu  mbalimbali mwilini mpaka nilipofanikiwa kumnyang’anya ndipo na mimi nikamchoma sikioni kwakujitetea. Nilipopata upenyo nilikiambia na kuondoka kabisa kwa Shangazi na kwenda polisi kushitaki. Niliwaambia kila kitu kuanzia nikiwa mdogo, namna Shangazi alivyokua ananitesa, akaniuza mwanza kwa rafiki yake ambaye alikua ananibaka kila mara mpaka nilipofanikiwakutoroka.


Niliwaambia jinsi nilivyokutana na Mama yangu ambaye alikua amefanywa mlemavu na Shangazi yangu kwakua tu alikua anataka kunichukua. Nikawamabia kuhusu kubadilisha majina ya mali za Baba yangu na kughushi cheti changu cha kifo ili mimi kuonekana nimekufa na yeye kuchukua kila kitu. Yalikua ni malezo marefu, sikuigiza katika kuongea, nilikua nauchungu sana na nilikua naumia sana, kila mtu aliyenisikiliza siku hiyo alitoa machozi na kuniamini.


Baada ya kuandika maelezo nilirudi Gest nilipokua nimeshukia, Baba mmoja ambaye ni Askari alijitolea kunilipia wiki nzima ili kuangalia mwenendo wa kesi yangu. Shangazi alikaa hospitalini wiki mbili, alipozinduka alikamatwa na polisi moja kwa moja alielekea mahabusuingawa hakua amepona vizuri. Sikio lake nililokua nimemchoma lilikua halisikii kabisa, ngoma ya sikio ilikua imetobolewa na kuharibika kabisa hiovyo alikua anasikia upande mmoja.


Yule Baba liyekua akiishi naye alitoroka lakini alifuatiliwa na kukamatwa, walishitakiwa kwa makosa mengi ikiwemo kughushi nyaraka na kupanga njama za mauaji. Baada ya polisi kufuatilia wlaikuta kila kitu ni kweli, kwamba Mama yangu alikua mlemavu na yeye alipohojiwa aliongea kama mimi namna ambavyo Shangazi yangu alimtesa yeye na watu wake wakitaka kumuua.


Wakati wa kesi Shangazi alikubali kurudisha kila kitu, kunirudishia Biashara za Baba yangu na nyumba zake zote huku akiniomba sana nifute ile kesi. Walikuja baadhi ya ambao hata sikuwa nikiwafahamu wakiniambia kuwa sina haja ya kumfunga Shangazi yangu kwakua ni damu yangu. mimi sikua na shida ya mali, sikua nahitaji kitu chochote kutoka kwa Baba, nilichokua nikitaka ni Shangazi yangu kupata mateso kama nilivyopata mimi.


Niligoma kabisa kufanya hivyo lakini walimtafuta Mama na kuongea naye, Mama alinisihi sana kufuta ile kesi, kutokana na Mama nilikubali kufuta kesi. Lakini nilipofika polisi nilikwama, ingaw aniligoma kutoa ushahidi kuhusiana na kesi ya kunishambulia na kutaka kuniua lakini Shangazi na yule Baba walikua na kesi nyingine ya kughushi.


Hapo lilikua ni kosa la jinai ambalo lilikua halihitaji ushahidi wangu, Polisi wlaigoma kabisa kuifuta ile kesi, wakaendelea nayo, Shangazi na mume wake walipatikana na hatia na kufungwa kifungo cha miaka mitatu kila mmoja. Nilirudishiwa vitu vyangu lakini maisha yangu na ya Mama yangu yalikua yameharibika kutokana na tamaa ya mali.


Baba alishindwa kumuamini Mama yangu mzazi na kuamini ndugu yake, Mama yangu leo ni mlemavu hawezi kuona kwkaua tu Baba alikuaa kiishi kwa kuogopa kudhulumiwa na Mama mwisho akampa kila kitu Shangazi ambaye alinidhuluimu. Najua labda alifanya kwa upendo au uopga lakini kila nikiwaza mateso niliyopitia natamani hukoa lipo sipumzike kwa amani kaburi lake licheze tu ili angalau na mimi niwe na amani ila najua haiwezi kutokea hivyo namuombea apumzike kwa amani ili na mimi niwe na amani.


MWISHO! MWAISHO! MWISHO!

0 comments:

Post a Comment

BLOG