Search This Blog

Tuesday, June 21, 2022

NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU!

  

IMEANDIKWA NA IDDI MAKENGO

SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU!


Niliingiwa katika kachumba kadogo, sijui kama kalikua ni kachumba ka nini lakini kalikua kadogo sana na kalikua na giza nene sana. Mume wangu alikua nyuma na tochi akitumulika sisi. Mama yake alikua mbele katangulia huku akiwa kanishika mkono. Kalikua ni kachumba kadogo sana na kalikua na harufu kali sana, hata kupumua ilikua ni shida, nilitamani kutoka na kukimbia lakin niliogopa kwani mume wangu alikua kadhamiria.


JOIN US ON TELEGRAM

“Vua nguo…” Mama yake aliniambia, nilisita kidogo kwani tulikua wa tatu, mimi, Mama mkwe na mume wangu. Niliona aibu kukaa uchi mbale yao wote.


“Hujamsikia Mama, kasema vua nguo.” Mume wangu aliongea huku akinimulika na tochi machoni, nilimkodolea macho kama vile namuambia naona aibu mbele ya Mama yako, naye alinikazia macho kuonyesha msisitizi kuwa alikua hatanii. Nikiwa bado najishauri mama mkwe alinivamia, alishika gauni langu chini na kulivua.


Alifaya harakaharaka, nilibaki na nguo za ndani tu, alinikalisha chini kabisa, akashika Chupi yangu na kuivuta kwa nnje, wakati wote huo mume wangu alikua pembeni akimulila, alikua akinimulika maungo yangu kana kwamba alitaka Mama yake anione vizuri. Nilikua natetemeka kwa hasira, nilificha uso kwa aibu, mume wangu wala hakujali, alikua bize kunimulika hukua kimuangalia Mama yake ambaye naye alikua bize na mwili wangu. nikiwa pale chini Mama mkwe alinipanua miguu na kuziacha sehemu zangu za siri wazi.


“Mulika huku…” Alimuambia mume wangu akimielekeza upande mwingine, mume wangu alimulika. Pembeni kulikua na sahani kubwa kama beseni flani hivi, lilikua limejaa vitu kama nyama zilizobanikwa na kuchemshwa, kulikua na kama mchuzi mweusi uliokua umeunguaa sana. Mama mkwe alichukua mapande ya nyama makubwa makubwa na kuanza kuniingizia sehemu zangu za siri. Wakati huo mume wangu alikua makini zaidi kuangalia, alipiga magoti na kunisoogelea vizuri.


Alimulika vizuri namna Mama yake alivyokua akiyaingiza yale mapande ya nyama, yalikua ni mengi tena makubwa. Lakini chaajabu pamoja na kuona kilichokua kikiendelea sikusikia kitu chochote, niliona kama Mama mkwe ananishikashika tu lakini sikupata hata maumivu kutokana na yake manyama kuingizwa kwenye uke wangu pamoja na kuwa kuna mengine yalikua na mifupa. Aliingiza manyama yote kwa kuanalia ilikua si chini ya kilo tatu, baada ya kumaliza aliniambia nitoke, nilitaka kuchukua gauni langu lakini aliniambia niende hivyo hivyo.


Nilitembea hatakaharaka nikipita sebulani kwa uoga, nilihofia labda wifi na mashemeji zangu watakua bado hawajalala. Lakini nashukuru Mungu kuwa hawakuepo hivyo nilipitiliza mpaka chumbani, nilikaa kitandani na kuanza kulia. Katika maisha yangunyote nilikua sijawahi kufanyiwa vitu kama vile, kwangu ilikua ni mara ya kwanza na niliogopa sana, niliogopa sana, nilikua nalia huku natetemeka nikitamani kukuche niondoke mule ndani, sikua tayari kuvumilia. Mume wangu alikaa kwa muda kidogo kama wa nusu saa ndipo alirudi.


Yeye alikua swa kabisa, aliniongelesha kwa kunichangamkia lakini sikumjibu, kwa kumuangalia alikua ni kama mtu tofauti kabisa kwani alikua yule mwanaume ninayemjua, mchangamfu, mcheshi na mwenye upendo. Si yule ambaye dakika kdahaa zilizopita alikua akinipiga makofi na kunilazimisha kufuata kila kitu ambacho Mama yake alikua anataka nikifanye.


“Mbona umekasirika, inamaana wewe hutaki mtoto?” Mume wangu aliniuliza. Nilinyanyua uso wangu na kumuangalia kwa hasira. “Anaongea kitu gani huyu mpumbavu?” Nilijiuliza kichwani, nilikua nataka mtoto kweli lakini si kwa hali ile.


Kwanza hata haikua na haja kabisa, ndoa yetu ndiyo kwanza ilikua na miezi mitatu, yaani kama ni kufanya mapenzi nikiwa katika siku za hatari tulifanya mara mopja tu, miezi mingine mume wangu alikua kasafiri, sasa ni kwa namna gani kuanza kuwa na wasiwasi ya kupata watoto mpaka kuanza kuhangaika na madawa ya kienyeji. Nilikua naamini kuwa sina tatizo ndiyo maana hata hospitali nilikau sijaenda. Tangu kuona na mume wangu tumekaa mara moja tu kwa mwezi mzima kamili.


Mwezi wa kwanza tu wa ndoa yangu, miezi mingine yote alikua bize na Biashara zake, alikua ni mtu wa kusafiri, sasa ni kwa namna gani kaunza kuhisi kuwa nina tatizo. Kwanza kama shida ni mtoto ningeweza kusema ni yeye kwani katika kipindi hicho alikua anarudi nyumbani kachoka tukifanya dakika kumi tu analala na hataki tena kuguswa. Sasa kwa hali hiyo mtu kweli unaweza kuwaza kuwa una matatizo ya uzazi mpaka kuanza kutumia madawa ya kienyeji? Nilikasirika sana na mume wangu alijua hivyo aliamua kunyamaza kimya, alipanda kitandani na kulala huku akiniacha mimi nikiwa na mawazo yangu.


Sikuwahi kuugua chochote na wala mimi na mume wangu tulikua hatujawahi kuzungumzia suala la mtoto, wala alikua hajaniambia kuwa anahitaji mtoto, kwanz ahata kufanya mapenzi na mimi ilikua shida sembuse kutaka mtoto. Nakumbuka ilikua ni siku ya jumamosi, mume wangu alitoka safari Mbeya, aliporudi alikua na mawazo sana, kulikua kama kuna kitu kinamsumbua kichwa cheka, nilimuuliza na kumdodosa kutaka kujua lakini hakuniambia, alinijibu tu nimuache na niliposisiizia kutaka kujua alikasirika.


Niliamua kunyamaza, nilimuandalia maji kuoga lakini hakuoga, alitoka na kutudi usiku akiwa kalewa. Ingawa alikua anakuywa pombe lakini si kwa kiwango kile, ilikua ni kawaida tu hivyo nilishangaa yeye kunywa mpaka kulewa kiasi kile. Kwakua nilijua kuna kitu kinamsumbua kichwani sikutaka kuwa kisirani, nilinyamaza na kumkaribisha ndani vizuri tu, nilimuandalia chakula lakini alikataa kula na kuingia chumbani kulala, kwakua alikua kalewa nilihisi kashiba amekula huko baa hivyo sikumlazimishia sana.


Niliondoa chakula mezani na kukiweka kwenye friji kisha nikarudi chumbani. Kufika alikua kalala lakini nilipopanda kitandai ili kulala alinyanyuka, alikua analia, nilishangaa na ingawa aliniambia kuwa nisimsumbue sikua na namna nilimuuliza tatizo nini?


“Hivi huoni kama kuna matatizo?” Aliniuliza kwa hasira, kwa namna alivyokua anaongea nilijihisi kama kuna kitu kibaya nimekifanya, niliwaza sana lakini sikukiona.


“Mimi sioni kwani nimekufanyia nini?”


“Ishu sio umenifanyia nini, angalau hata ungeweza kufanya kitu. mwezi wa ngapi sasa tangu tuoane akuna cha mimba wala mtoto?”


Aliniuliza kwa hasira, kusema kweli nilicheka, miezi mitatu ya ndoa mtu anataka mtoto kweli? Nilimuuliza lakinia lihisi kama ninadharau.


“Mshenzi mkubwa wewe, yaani naongea mambo ya maana wewe unajifanya kuleta utani wako wa kinjinga hapa! Mimi nadhareaulika huko nnje na ndugu zangu, marafiki zangu wananicheka wkaajili yako, nakuvumilia muda wote huu huzai lakini wewe unafanya ujinga!” Alifoka hukua kinishika na kunipuiga makofi, tangu kujuana na mume wangu ilikua ni miaka kama minne, kwani tulikutana kipindi niko chuo, katika kipindi chote hicho yeye akiwa anafanya Biashara nilikua sijamuona akiwa vile.


Kwanza alikua hajawahi kunipiga, mara nyingi hata nikimkosea huondoka kwa hasira na akirudi anakua vizuri, tunayaongea na kuyamaliza, nilishangaa sana kumuona akiwa vile. Nililazimika kunyamaza kwani niliogopa sana kupigwa, katika maisha yangu nilishaapa sitakuja kupigwa na mwanaume baada ya X wangu kunipiga na kutaka kunitoboa jicho. Nilikua mpole ili aniache huku nikipanga kuwa subuhi nachukua kila kilicho changu na kurudi kwetu.


Kuona nimenyamaza aliniacha, lakini aliongea mambop mengi, alikua analalamika namna ambavyo Mama yake anampigia simu kila siku akilalamikia kutaka mjukuu, aliniambia namna ambavyo amechoka kuchekwa na wanaume wengine mtaani, namna ambavyo kila mtu anamuona kama si mwanaume kamili. Nilijaribu kumsihi nikimuabia kuwa bado muda ni mchache, nilimuambia kuna watu wanakaa miaka hata kumi bila mtoto na wana amani, nilimbembeleza na kumuambia kuwa aache kuwaza, alinielewa tukalala, aliniomba msamaha kwa kunipiga hivyo hata lile wazo la kuondoka lilifutika lenyewe.


Lakini kumbe mwenzangu hakumaliza,a subuhi alikua ndiyo mtu wa kwanza kuamka kitru ambcho hakikua kawaida yake. Nilimkuat kashaoga na kujiandaa kama anenda sehemu. Nilimuuliza kama ana safri aliniambia ndiyo.


“Jiandae tuondoke!” Aliniambia, nilimuangalia kwa mshangao kwani tulikua hatujapanga safari yoyote ile.


“Wapi?” Nilimuuliza.


“Kwa Mama, jana nilishindwa kabisa kulala, niliongea na Mama anasema kuwa anawez akukusaidia hilo tatizo lako.” Aliongea hukua kinisogelea, mikono yake ilikuja na kushika kiuno changu.


Alinishika kwa nyuma kimahaba hukua kinipumulia sikionio.


“Tatizo gani? Nani kasema nina tatizo?” Niliuliza kwa sauti yataratibu huku nikihisi mapigo yake ya moyo, nilisisimka na nilijikuta namkumbuka X wangu, namna alivyokua akinishika na kunifanyia wakati wa asubuhi, nilikumbuka ile raha ya kufanya mapenzi asubuhi, nilikumbuka vitu vyake vya kitandani, vitu ambavyo mume wangu alikua hana. Nilitamani aendelee kunishika, nilirudisha mikono yangu nyuma na kuushika uume wake kutaka kumhamasisha lakini mwenznagu hakua tayari.


Sekunde tatu nyingi alinisukuma mbele kwa hasira, ni kama tulikua na ugomvi.


“Wewe mjinga nini? Si jana tumeongea kuwa nataka mtoto, sasa ulitaka nipate na nani kama sio wewe? kama hutaki kuzaa na mimi niambie kuna wanwake wengi tu na vizazi vyao wanataka watoto, sema nitafute mwingine.” Aliongea sana kitu ambcho kilinishangaza, alinishika mkopno na kunilazimishia kuingia kwenye gari, hata uso nilikau sijanawa lakini niligundua kuwa alikua kashapanga kila kitu, nguo zangu na kila kitu kilikua kwenye gari.


Alifunga mlango na kuniambia kuwa nitaenda kwa Mama yake na kama sitaki absi anishushe na nijue moja kuwa nikishuka si mume wangu nitafute mwanaume mwingine wa kuishi naye. Kwa namna alivyokua niliogopa kabisa, nililazimika kunyamaza na kufuata kile alichokua akikiongea. Safari ya kwenda Morogoro ilianza, njia nzima alikua akiniambia kuwa nisiwe na wasiwasi kwani kila kitu kitakua sawa, alikua akiniambia kuwa nitakaa kule siku mbili basi, kuna Dawa ambayo Mama yake atanipa na nitapata mimba harakaharaka.


Tulifika nyumbani kwao na kupokewa vizuri, Baba yake alikua hayupo, alirudi baadaye jioni na tukasalimiana vizuri tu. Wadogo zake walinipokea vizuri na hakukua na mazungumzo mengi, ni kama walijua kilichokua kikienda kutokea kwani kwa namna walivyokua wakiniangalia na namna ambavyo walikua wakiongea kwa kificho kificho ni kama walikua wanijadili mimi. Nilinyamaza tu, mume wangu hakuongea na mimi alipofika alinikabidhi kwa Mama yake na kuondoka.


Alirudi usiku kwenye saa nne hivi, tayari tulishakula chakula cha usiku na nilishaingia chumbani kulala.


“Umeongea na Mama?”


“Ndiyo…”


“Amesemaje?” Nilitulia kidogo kwani sikujua anamaanisha nini anaposema kuongea, kitu pekee nilichokua nimekiongea na Mama yeke ilikua ni hali yangu, vipi ndoa na mambo mengine kama hayo, hatukuwahi kuongea mambo ambayo nadhani yeye aliyataka.


“Hajasema kitu, alikua ananiulizia tu hali za nyumbani.” Nilimjibu, alishtuka ni kama kuna kitu ambacho Mama yake alitakiwa kuniambia.


“Hapana, kuhusu matatizo, hili lililotuleta?”


“Hapana, hajagusia. Nilimjibu kwa mkato kwani sikutaka maneno mengi, kusikia vile alinyanyuka na kwenda nnje, baada ya kama dakika tano hivi alirudi akiwa kaongozana na Mama yake.


“Huyo anaondoka hakai sana hivyo mfanyie dawa leo.” Alimuambia Mama yake, nilishangaa kwani sikujua kama Mama yake ndiyo mganga, kwani kwa namna alivyokua kakaa ilionyesha kama ndiyo nimepelekwa kwa mganga.


“Amekubali? Mama alimuuliza, aliniangalia kwa hasira ilinibidi kutingisha kichwa kuoyesha kwamba nilikua nakubaliana na kile aichokua akikiongea Mume wangu.


“Kakubali, hana shida, hata yeye anataka, kachoka maisha haya, mambo hayaendi kabisa na naambiwa tatizo ni yeye, ni lazima wote tuwe kitu kimoja.” Mume wangu aliongea kwa wasiwasia wasiwasi, ni kama kuna kitu alikua anaficha.


“Hakuna kurudi nyuma mwanangu, ukishaingai huku umeingia, mpaka kufanikisha….”


“Mama wewe nawe maneno mengi, mfanyie, huyu ni mke wangu wkanini arudi nyuma, tulishakula kiapo kifo kututenganisha, hakuna kurudi nyuma.”


Mume wangu alimkatisha Mama yake, wote walionekana kuwa na wasiwasi, Mama mkwe alitoa kidawa flani katika matiti yake na kuniambia kuwa nikilambe, nilikilamba, kilikua kichungu sana kiasi cha kutaak kutema. Mume wangu kuona vile alinishikilia na kuwa kama ananikaba kunilazimisha nikakimeza. Nilikimeza, nilikaa kama dakika tatu hivi nikwa kama nimechanganyikiwa flani, nilikua sijisikii vizuri tena, nilikua kama mtu aliyepigwa sindano ya ganzi.


Nikiwa sina hili wala lile nilimuona Mama mkwe wangu akiingiza vidole vyake semu zake za siri, alifanya hivyo Mume wangu akiwa pembeni anamuangalia, alinyanyua gauni lake na kusogeza nguo yake ya ndani na kujiingiza vidole huko. Mume wangu alikua akiaangalia kila kitu, mimi nilikua kama nimeduwaa ni kama nimepoteza fahamu lakini naona kila kitu. alitoa mkono wake na kuniletea mdomoni kwangu akitaka nivilambe vile vidole, nilisita, alipoona nimezubaa alimpa mume wangu ambaye alivilamba.


Kichwani nilikua najihisi kinyaa, nilitamani kutapika lakini Mama mkwe wangu alirudisha tena vidole vyake sehemu za siri na kuvitoa, safari hii alininyooshea mimi na bila kujijua nilijikuta navilamba, vilikua na vitu vya usi nililamba na kumeza. Sijui kwanini nilifanya hivyo lakini baada ya ile dawa ya kwanza nilihisi kama nimepumbazwa hivi, nilikua nikifanya kila kitu walichokitaka, baada ya lile tukio ndipo walinitoa chumbani na kunipeleka katika kale kahumba kadogo na kunifanyia vitu vingine vya ajabu kwa madai kuwa sibebi ujauzito hivyo nina matatizo.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU—-SEHEMU YA PILI


Usiku ule mume wangu hakuendelea kuongea na mimi, alipioga magoti kama anasali kisha akapanda kitandani, alilala huku mimi akiniacha macho. Asubuhi nilichelewa sana kuamka, sijui kwanini lakini nilikua na usingizi mzito sana, niliamka kwenye saa tano za asubuhi tena kwa kuamshwa na Mama mkwe wangu. aliingia chumbani kwetu na kuniamsha, nilishtuka kuona kuwa mume wangu hakua pembeni yangu kwani kwa namna nilivyokua nikijisikia nilihisi kama ni usiku vile. Macho yalikua mazito na kila nilipotaka kufungua niliona giza tu.


“Mbona  sioni vizuri?” Niliuliza, Mama mkwe wangu alinisogelea na kunishika macho, alikua kama anayafungua ndipo nilianza kuona vizuri kama kawaida.


“Utakua ni usingizi, umelala sana, saa tano…” Aliongea huku akinisogezea chai ambayo alikua kaiweka wkenye kistuli pembeni ya kitanda. Huku nikiona aibu niltitaka kunyanyuka kwani nilijisikia vibaya nimeenda ukweni halafu naamka muda ule.


“Hapana, usisimame, wewe bado hali yako mbaya, subiri wewe ni mgonjwa haa hapo nikuhudumie.” Mama mkwe aliniambia, nilishtuka kidogo kwani sikua nikiumwa chochote, wakati naondoka mjini mpaka kwenda kumuona nilikua  mzima kabisa.


Niliulia kidogo nikiiangalia ile chai, abdo nilikua nikikumbuka mambo yaliyonitokea jana yake hivyo nilikua simuamini kabisa Mama mkwe wengu. Nilisi kama kaniwekea kitu, ni kama alikua kwenye akili yangu, aliponiona naiangalia sana ile chai alichukua kikombe akanywa funda moja la chai kisha akaniambia niendelee. Nilitaka kunyanyuka kukaa lakini mwili ulikua mzito, ni kama nilikua nimefungwa mzigo mkubwa kwenye miguu, nilishindwa kuinyanyua.


“Nimefanya nini? Mbona miguu yangu ni mizito namna hii?” Nilimuuliza huku nikizidi kujitahidi kuinyanyua miguu yangu lakini nilishindwa.


“Hakuna chochote, ni dawa ya jana inafanya kazi, utakua vizuri tu karibuni.” Aliniambia, sikutaka kumsikiliza wala kuendelea kunywa chai, nilinyanyua mikono yangu na kuondoa shuka nililokua nimefunikwa.


“Mamaaaa!” nilijikuta napiga kelele, Miguu yangu ilikua imevimba, ilikua kamana manundu manundu ya damu iliyovimbiana, kulikua na manundu meusimeusi kama zile nyama alizokua akiniingizia sehemu za siri jana yake.


“Mmenifanya nini? Mmenifanya nini miguu yangu?” Nilimuuliza Mama mkwe wangu, yeye hakuonekana kupaniki, aliniambia niendeleee kulala mpaka jioni uvimbe wote utakua tayari umeshaondoka. Alinilazimisha kunywa ile chai, aliongea kwa hasira pale nilipokataa na kwa namn aalivyokua akinikodolea macho ni kama nilikua namuogopa flani hivi. Nilikunywa na kulala palepale, mume wangu hakurejea tena mpaka usiku wake. Hapo ndipo waliniamsha,a likuja chumbani yeye na Mama yake na kuniambia kuwa ni wakati wa mimi kuondoka.


Kumbuka nilikua nimelala tangu machana nilipokunywa ile chai ya Mama mkwe mpaka kwenye saa nane usiku ndipo mume wangu alirejea. Walishaniandalia kila kitu, mizigo ilishingizwa kwenye gari na ilikua ni sisi kuondoka. Nilinyanyuka nikiwa najisikia vizuri, miguu ilikua ni kawaida kabisa, sikuona uvimbe wowote na wala hakukua na maumivu ya aina yoyote. Nilimuuliza mume wangu nini kilikua kimetokea, nilimuuliza kama aliiona miguu yangu ilivyokua imevimba lakini hakunijibu, zaidi ya kuniambia kuwa sasa nitapata mtoto mume wangu alikua haongelei chochote kuhusiana na yale mambo yaliyotokea.


Nyumbani mume wangu hakukaa, baada ya siku mbili tu alisafiri kwenda kununua mzigo, alikaa huko kwa siku tatu ila alirudi hakua na kitu, nilipomuuliza nilishangaa ananijibu kwa hasira kuwa nisimfuatilie maisha yake. Nilishangaa na kuamua kunyamaza tu, sikutaka kuongea sana. Alikaa kwa siku tatu nyingine kabla ya kusafiri tena, lakini katika siku zote hizo alikua ni mtu tofauti kabisa, aliakua ni  mtu wa hasira, alikua akijibu majibu ya ajabuajabu na kuongea vitu ambavyo havieleweki. Alikua ni mtu wa kisirani sana mpaka nikawa siwezi hata kuongea naye chochite.


Alisafiri tena lakini aliporudi hakurudi na Gari yake, alikua mwenyewe na nilipomuuliza aliniambia kuwa ameiuza kwani kuna pesa kapeleka sijui wapi na katapeliwa. Wakati huo nilikua katika siku zangu za hatari, nilimuambia nikijua kuwa kwakua alikua na haraka ya kupata mtoto basi niko katika siku zangu za hatari hivyo tufanye mapenzi. Chakushangaza nikuwa hakua tayari kufanya hivyo, kusikia tu hilo alianza kukasirika, alitukana sana, aliniambia mimi ni mjinga, mpumbacvu sina akili kwani wakati yeye anawaza kutafuta pesa mimi nawaza mapenzi tu.


Nilinyamaza kwani sikutaka shari kabisa, aliondoka tena safari hii hata hakuniambia kuwa anaenda wapi. Aliondoka kwa siku tatu bila kuaga na aliporudi alirudi na Mama yake pamoja na mzee mwingine. Sikua nikimfahamu huyo mzee lakini alinitambulisha kama ni Mjomba wake, ndugu yake na  Mama yake, kwakua sikua nikiwajua wote nilikubaliana na kumkaribisha vizuri, Mama mkwe alinichangamkia vizuri na mimi nilimchangamkia ingawa nilihisi kabisa  kuwa kuna kitu.


Mama mkwe na yule Baba walikaa kwa siku moja tu, kesho yake waliondoka, sikujua kuwa walikua wanafanya nini lakini baada ya kuondoka mume wangu alibadilika tena, alirudi katika hali yake ya kawaida, akawa ni mtu wa furaha, alianza kuchangamka na kuanza kuniambia kuhusiana na Biashara zake.


“Kuna fremu nimepata, natraka kukufungulia Biashara kubwa tu, nataka ufranye Biashara, sitaki mambo ya kuajiriwa ajiriwa.” Aliongea, mimi nilimuitikia tu kwani sikutaka kumuudhi, nilitaka kukubaliana na kila kitu anachosema kwani sikutaka abadilike kama awali.


Tuliongozana naye mpaka ilipoile fremu, aliniambia kuwa anataka kufungua duka la vifaa vya ujenzi, nakumbuka ilikua jioni, alifungua ile fremu na tukaingia kuangalia, kila kitu kilishawekwa, alishatengeneza mashelfu, makabati na kila kitu, mzigo tu ndiyo alikua bado hajaweka. Niliiangalia na kumsifia kuwa ni nzuri, sikua nikisifia kinafiki bali ni kweli ilikua ni fremu nzuri na ilikua katika sehemu nzuri ambayo nilijua lazima itakua na Biashara kwani palikua pamechangamka. Nilifurahi kwamba ameanza kunishirikisha katika mambo yake, nilifurahi kuwa alikua amechangamka.


Tukiwa mule ndani wakati tunaangalia fremu alinifuata na kunikumbatia.


“Nimekua bize sana siku hizi, mppaka nashindwa kuwa na wewe, dnoa yetu bado changa lakini hata mapenzi yenyewe hatufanyi.” Aliniambia huku akinishuka kiuno, mwili wake uligusana na mwili wangu, aliiinamia shingo yangu na kuanza kuinyonya, alikua akiinyonya taratibu huku akinitomasatomasa sehemu mbalimbali. Nikweli muda ulikua umepita tangu kufanya mapenzi ya kueleweka, nilisikia raha ya ajabu na nilitaka aendelee, lakini pale kulikua ni dukani na bado geti lilikua wazi.


Nilijarubu kujisogeza huku nikimsihi tende nyumbani lakini hakutaka, aliniambia ananihitaji palepale, aliniambia kuwa ana hamu na ile fremu ni ya kwetu hivyo tunaweza kufanya chochote kile mule ndani na hakuna mtu yeyote wa kutuzuia. Nilimuomba basi afunge mlango lakini hakutaka, alijifanya kuwa ana haraka, lakini kwa namna alivyokua akinishika na kuuchezea mwili wangu nilishindwa kujizuia, nilijikuta na kukubali kufanya naye mepenzi palepale kwenye fremu mlango ukiwa wazi.


Tulifanya lakini katikati mambo yakiwa ndiyo yamechanganya ghafla mume wangua lisimama, alitembea mpaka katikati ya duka kisha kurudi tena, ni kama alitaka kuendelea kufanya mapenzi na mimi lakini ghafla nilishangaa kanipiga kofi usoni, lilikua ni kofi zito ambalo lilinifanya kupatwa na kizunguzungu. Hakua akiongea, aliendelea kunipiga huku bado akifanya mapenzi na mimi, alikua akininyanyua ananirusharusha na kurudia kufanya mapenzi na mimi, mwanzo nilivumilia lakini nilipoona kaama anazidi nilianza kupiga kelele.


Hapo ni kama nilikua nimeyaamsha mashetani yake, mume wangu alinyanyuka na kwenda kufunga milango kwa ndani, alienda kwenye shelfu moja akachukua kamba, alinifunga mikono na miguu, akanifunga na kitambaa mdomoni ili nisiweze kupiga kelele. Baada ya kumaliza alianza kufanya mapenzi kama vile alikua ananibaka, alikua na hasira sana na sijui zilitoka wapi. Yute hayo alikua akiyafanya bila kusema chochote, alinipiga na alinifanyia rafu sana mpaka nikawa natokwa na damu sehemu za siri, mume wangu hakujali aliendelea kunifanyia mpaka alivyotosheka.


Alinifungulia kamba na kuondoka zake akinaicha pale chini, hakufunga mlango alinaicha palepale. Nilitamani kuondoka lakini niliishiwa nguvu mpaka asubuhi ndipo nilipozindika, nilivaa nguo zangu na kutoka, kulilikua ndiyo kuna pambazuka hivyo hakukua na watu wengi, nilitembea kwa miguu mpaka nyumbani ambapo hakukua mbali sana. Milango ilikua wazi na nilipofika nilikuta mume wangu kalala sebuleni.


“Mbona umechelewa sana, wewe ndiyo wakunijia asubuhi?” Aliniuliza baada ya kuingia, nilishindwa kumuelewa kwani wakati ule alikua ni mtu mwingine kabisa.


Sikumjibu chochote na yeye hakuendelea kuuliza, niliingia chumbani kuoga na kuangalia majeraha yangu. nilipanda kitandani na kulala nikiwa na hasira zangu, mume wangu hakujali, aliondoka na kukaa kama siku mbili hivi bila kujua kaenda wapi lakini aliporudi alikua mtu mwenye furaha, alinipeleka dukani kwenye duka lilelile ambalo alinifanyia unyama lakini safari hii lilikua limejaa kabisa, alishaleta vitu vingi na kulikua na kijana anauza, aliniambia kuwa nitakua nikikaa pale nikisaidiana na yule kijana mahesabu, nilishaanza kumuogoopa hivyo sikutaka kubishana naye kabisa.


****


Maisha ya dukani yalikua mazuri, dukani tulikua tunauza balaa na kila kitu kilikua kinaenda vizuri, mume wangu alibadilika, ingawa hakuwahi kuzungumzia kwanini alinipiga na kunibaka lakini alibadilika kabisa, alikua ni mtu wa kuwahi kurudi nyumbani, akitaka kusafiri kibiashara hata kama ni nnje ya nchi tuilikua tunaongozana na alikua akinipenda sana. Pamoja na mapungufu na mambo yote aliyokua amenifanyia, pamoja na ukweli kuwa hakuwahi kuniomba msamaha lakini kwa mabadiliko aliyokua nayo nilifurahia na kuamua kumsamehe bila kuombwa msamaha.


Baada ya kama miezi sita hivi tangu mambo yote hayo kutokea nilipata ujauzito, nilimuambia mume wangu ambaye alionyesha kufurahia, alizidisha kunionyesha upendo na kuwa mtu wa kuninunulia zawadi, ili nisiteseke alininunulia Rav 4 mpya kabisa, achana na zile zilizotumiwa na wajapani, hapana yeye alininunulia mpya kabisa. Nilifurahi kwani mbali na kunihudumia mimi lakini pia alikua akihudumia na ndugu zangu, alikua akiwapenda na kusomeshya wadogo zangu, kwakifupi kila kitu kilikua kizuri na ndoa ilikua tamu.


Ujauzito ukiwa na miezi minne nyumbani kwetu kulitokea msiba, kaka yangu mkubwa alifiwa na mtoto wake mchanga wa miezi sita. Nililazimika kwenda, ilikua ndiyo mara yangu ya kwanza kwa mimi kwenda kusalimia nyumbani kwetu tangu kuolewa, mara nyingi nilipokua nikitaka kwenda kilitokea kitu, mara mume wangu kasafiri, mara kuna wageni, mara ananiambia subiri mara hivi mara vile mpaka nashindwa kwenda, mbali na kusalimiana nao kwenye simu nilikua sijawaona wazazi wangu tangu kuolewa, zaidi ya ndugu zangu wachache ambao wanaishi Dar nilikua sijaona mtu mwingine.


Mimi nyumbani kwetu ni Singida, kutokana na hali yangu sikuweza kuendesha mwenyewe Gari hivyo nilimtafuta Dereva amabye alinipeleka mpaka nyumbani, nilifika tukazika. Mwanzo wakati naondoka mume wangu alikua vizuri tu, lakini usiku nimefika alinipigia simu na kuniambia kuwa natakiwa kurudi nyumbani. Nilishangaa kidogo kwani nilimuambia nitakaa wiki moja ili kuweza kusalimia na baadhi ya ndugu ambao bado nilikua sijawaona kwa muda mrefu.


Nilijaribu kumuelewesha mume wangu lakini hakutaka, yeye alikua anasisitiza kuwa natakiwa kurudi nyumbani, tulibishana sana, niliona kabisa hakuna mtu ambaye atanielewa kama nikitaka kuondoka kesho yake, nilimuomba basi nikae hata siku mbili lakini alikataa na cha ajabu zaidi nikuwa alitaka niondoke usiku uleule. Tayari alishampigia dereva na kumuambia niondoke naye usiku huo, aliniambia nitafute sababu ya kuaga hata niseme anaumwa lakini nirudi usiku huohuo. Kwa namna alivyokua akiongea ni kama kulikua na kitu kibaya ambacho kingeweza kunitokea kama ningeendelea kukaa pale.


Kwa namna alivyokua anasisitiza nilimuelewa, nilikua nimetoka nnje kidogo kuongea naye. Nilikata simu na kuanza kurudi ndani ili kuongea na wazazi wangu, bado nilikua nikiwaza ni sababu gani nitawapa mpaka wakubali mimi kurudi usiku ule. Lakini sikufika mbali, ile narudi ndani tu kabla sijaingia nilidondoka chini. Sikupoteza fahamu, nilikua naona na kusikia kila kitu lakini sikuweza kuongea, kunyanyuka wala kupepesa macho, mwili ulikua kama vile umekufa lakini akili na kila kitu kinafanya kazi.


Nilidondoka katikati ya mlango, sikupiga kelele hivyo nilikaa kama dakika moja hivi pale chini mpaka mtu kuja kuniona, wakapiga kelele ndipo nilinyanyuliwa na kulepekwa hospitalini. Walinipima kila kitu lakini nilikua vizuri isipokua nilikua sina ujauzito, nilishangaa kwani mimba ilikua kubwa kabisa na nilishaanza kwenda kiliniki.


“Anahitaji kusafishwa mimba imetoka.” Daktari aliongea akimuambia Mama yangu, kila mtu alishtuka kwani sikua nikiumwa na hata kama ni mimba kutoka sikua na dalili zozote za mimba kutoka zaidi ya kule kudondoka.


Bado nilikua kama mtu aliyepoteza fahamu ingawa niliona na kusikia kila kitu kilichokua kikiendelea pale. Kila mtu alishangazwa sana, kwakua Mama yangu ni mtu wa Dini, Mlokole, alipiga magoti palepale na kuanza kuniombea. Alifanya hivyo kwa kama dakika  moja nilijikuta naanza kutapika, nilikua nikitapika mabonge ya damu makubwa makumwa, yalikua ni mazito lakini yakigusa chini yanachanika kama vipande vipande vya nyama.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU—SEHEMU YA TATU


Jinsi nilivyokua nikitapika ndivyo ambavyo Mama alizidi kuomba, Mama yangu alikua na upako wa ajabu hivyo ni kama alikua anajua kuna kitu kilikua kinatokea, aliendelea kuomba mpaka iakakata kabisa kutapika. Hapo alinyanyuka na kuniangalia.


“Mwanangu umejiingiza kwenye mambo gani?” Mama aliniuliza, ingawa nilihisi kilichokua kikiendelea lakini nilisita kumuambia, sikujua ni kwa namna gani nitamuambia Mama mambo aliyokua akifanya mume wangu, nilinyamaza na kujifanya kama sijamsikia.


Hali yangu bado ilikua mbaya ingawa nilisharudiwa na fahamu, baada tu ya maombi simu yangu iliita. Mama alipokea, hakuongea chochote lakini ilionekana kama mtu aliyekua akiongea naye alimuelekeza kunipa mimi simu, alinisogelea na kunipa simu kisha akakaa pembeni yangu.


Mume wangu hakusubiri hata kusema halooo, hakunisalimia na kuuliza nilikua  naendeleaje, alianza kutukana matusi ya nguoni huku akiniita mchawi, alitukana sana na kuniambia kuwa nifanye nitakachofanya lakini nisikanyage tena nyumbani kwake.


“Umenikosea sana, wewe mshenzi kabisa, sikutaki tena, sitaki kukusikia na sitaki kujua chochote kuhusu wewe! Kwanza huyo mtoto uliyenaye si wakwangu, si mwanangu kabisa, simtaki na tafuta mwanaume mwingine wa kumsingizia mtoto!” Mume wangu alipiga kelele, nilishindwa kuelewa yale yote yalikua yametoka wapi, mimi nilikua hospitalini na kama ni suala la mimi kurudi nyumbani basi nilikua tayari kwa hilo.


Aliongea sana kisha akakata simu bila hata kunisikiliza, bila kujua kuwa nilikua na hali gani? Mama aliniuliza kulikua na matatizo gani katika ndoa yangu, nilimuambia hakuna kitu.


“Mume wangu alikua hataki nisafiri kutokana na hali yangu, mimi nililazimishia hivyo kakasirika.” Nililazimika kudanganya, Mama alijua kabisa kuwa namdanganya lakini hakusema kitu chochote, alibaki kimya kwa muda kisha akaanza kusafisha yale matapishi, wakati huo Daktari aliingia, alishangaa kuona ile hali, aliniuliza nini kilikua kimetokea nikamuambia nimetapika.


Tayari nilishakua na nguvu kama vile hakukua na kitu chochote kilikua kimetokea. Nilinyanyuka na kutaka kuondoka kurudi kwa mume wangu, kila mtu aliniambia kuwa nibaki na kuangalia afya yangu lakini sikua tayari. Daktari aliyaangalia yale matapishi kwa mshangao, yalikua kama manyamamanyama ya viungo vya mwili.


“Ni kama mimba imetokea mdomoni!” Aliniambia.


“Haya ni maajabu sana, katika miaka yangu 20 ya kufanya hii kazi sijawahi kukutana na kitu kama hiki. Alituambia, Mama alipiga tena magoti kutaka kuomba, lakini nilishanyanyuka kuondoka, nilikua siko sawa kabisa na sikutaka Mama kuendelea kuomba.


Walinisihi sana kurudi lakini nilikataa, nilikua kama nimewehuka, nilimuarisha dereva ili tuondoke ile sehemu. Kwakua Dereva alishaambiwa kuniondoa pale alikubali, aliniingiza kwenye gari harakaharaka kama vile ananiiba kishatukaondoka usiku uleule. Kama dakika kumi hivi mume wanu alinipigia simu.


“Umefanya jambo la maana kuondoka, hiyo familia ni wachawi sana, Mama yako atakuua!” Mume wangu aliniambia, mimi nilishtuka na sikumuelewa, aliniambia kuwa nikirudi nyumbani atanionyesha kila kitu ambacho Mama yangu ananifanyia.


Nilishindwa kumuelewa kwani kwa nilivyokua nikimjua Mama yangu suala la uchawi hakua nalo kabisa. Gari iliendeishwa usiku kucha, tulifika Dar saa nne asubuhi. Nilipofika nilishangaa kumuona Mama mkwe wangu kaja nyumbani kwetu.


“Mwanangu wanaume ni wajinga kabisa, hivi kwanini alikurudhusu kuondoka na hali yako hii?” Mama mkwe aliongea hukua kinichangamkia.


“Nimesikia kilichokukuta, watu ni wabaya sana, hawapendi mafanikio ya wengine, mwanangu ukiwa mjamzito huendi msibani, kuna macho mengi na wengi ni watu wabaya kabisa!” Mama mkwe wangu aliendelea kuongea.


Mimi nilinyamaza kimya nikishangaa ni kwa namna gani Mama mkwe alijua yaliyonitokea wakati hata mume wangu nilikua sijamuambia. Nilipotaka kumuambia mume wangu aliishia kunitukana na aliponipigia simu kwa mara ya pili hatukuongea kuhusu afia yangu zaidi ya yeye kumtukana na kumsingizia mambo mengi Mama yangu. Nilijifanya nimechoka na kuingia chumbani kwetu kupumzika, mume wangu alikua chumbani baada ya kuniona hakunisemesha, alijifanya kukasirika akatoka chumbani kwetu na kurudi sebuleni.


Nillijaribu kumsalimia lakini hakujibu, alikua na kisirani flani na kwa namna nilivyokua nimechoka sikujali, niliingia chumbani na kulala. Sikushituka mpaka jioni Mama mkwe alipokuja kuniamsha, aliingia chumbani kwangu akiwa kavaa khanga moja tu. Nilishangaa lakini sikuuliza, kwa niliyokua nimeyaona sikuwa na swali tena.


“Nitakuhudumia mpaka ujifungue….” Aliniambia huku aifunga mapazia.


“Hutakiwi kuyaacha haya wazi.” Aliniambia, nilinyamaza bila kusema chochote, aliniletea chakula na kutaka kunilisha, nilimshukuru na kumuambia kuwa naweza kula mwenyewe lalini alikataa katakata na kuniambia kuwa kaja kunihudumia mimi na si kingine.


Nilikula kwa shingo upande, nilikula harakaharaka ili tu aniondokee mule ndani, baada ya kumaliza kula alichukua vyombo na kuondoka. Lakini sikukaa muda nilianza kutapika, nilitapiika sana vitu vyeusi huku tumbo likikata sana, nilikua nasikia kama kuna  mtu anapita na kisu na kuanza kukata tumboni kwangu. Maumivu niliyokua nikiyapata nilishindwa hata kunyanyuka, nilianza kupiiga kelele kuomba msaada lakini wapi, si Mama mkwe wangu wala mume wangu ambaye alitokezea, nilipata maumivu makali sana mpaka nikapoteza fahamu.


Nilikuja kuzindika usiku wa manane, nilijigeuza kitandani nikipapasa pembeni nikagusa mwili wa mtu, nilidhani ni mume wangu lakini nilijikuta na shika kifua cha mwanamke. Alikua uchi kabisa, niligeuza mikono upande wa pili na kukuta mtu mwingine, huyu alikua ni Mume wangu kwani kwa kumshika tu nilijua ni mwili wake. Nilishtuka nikidhani labda mume wangu alikua kaniletea mwanamke mwingine ndani na kumlaza kitandani kwetu. Nililnyanyuka na kwenda kuwasha taa, alikua ni Mama mkwe wangu.


Alikua kalala kitandani kwetu uchi wa mnyama huku mume wangu akiwa kalala upande wa pili, nilitaka kuzima taa lakini alishtuka na kuamka. Aliokota Khanga yake kisha kujifunika na kwa aibu aliniambia.


“Nilikuja kukuangalia kumbe nimepitiwa na usingizi…” Alitoka na kuniacha na mshangao wangu.  Mume wangu alikua bado kalala hakujua kilichokua kinaendelea. Nilirudi kulala lakini ni kama sikua na usingizi, nilikua nikiwaza ni nini kitatokea kama Mama mkwe wangu akijua kuwa sina mimba, nikikumbuka mambop yaliyotokea mpaka mimi kuipata ile mimba niliamua kukaa kimya, sikutaka kabisa kumuambia mtu yeyote kuwa sina mimba.


****


Mama mkwe wangu hakuondoka, nikiwa naamini kabisa kuwa mimba yangu ilikua imetoka tumbo lilizidi kuwa kubwa, hali hiyo ilinichanganya na kunifanya nirudi kiliniki kwani nilishaacha baada ya kutoka kwetu. Kule nilipimwa na kuambiwa kuwa mimba bado ipo na mtoto anaendelea vizuri, nilimshukuru Mungu ingawa bado nilikua na mwasiwasi kuhusiana na kilichotokea, bado afya yangu ilikua haijatengamaa na Mama mkwe wangu na mume wangu walikua hawaishi vituko.


Nilijifungua salama mtoto wa kike, mume wangu alifurahi sana na mara tu baada ya kujifungua Mama mkwe wangu aliondoka, kwa mtu aliyenihudumia kwa muda mrefu na kunidekeza kipindi nikiwa mjamzito nilitegemea kuwa labda angenihudumia pia baada ya kujifungua. Lakini haikua hivyo, mara tu baada ya kujifungua tena nikiwa hospitalini Mama mkwe wangu alikusanya kila kilicho chake na kuondoka zake. Nilishangaa sana si kitu nilichokitegemea.


Nilitoka hospitalini na kuhudumiwa na Dada wa kazi niliyekua nimetafutiwa na Mama mkwe wangu, Mume wangu hakutaka kabisa mimi kuhudumiwa na mtu mwingine zaidi ya huyo Dada. Ingawa alikua hajaniambia ni kwa namna gani lakini kila siku bado alikua akiniambia kuwa Mama yangu ni mchawi na hawezi kumgusa mtoto wake, alikua akisisitiza hivyo ingawa aliendelea kuwahudumia ndugu zangu kwa kila kitu na kila mara alipokua akiongea na Mama alijifanya mtu mwema.


Kwakua nilikua nikiwapenda ndugu zangu hasa Mama yangu sikuwahi kumuambia maneno ya mume wangu ingawa ilikua ngumu sana kwangu kuelezea ni kwanini sikutaka waje kumsalimia mtoto.  Mwanangu alikua anakua vizuri tu kama watoto wengine, lakini alipofikisha miezi sita nilianza kuona mabadiliko, ingawa mwanzo alikua akiona vizuri lakini aliaacha kuona, macho yalikua hayapepesi na akiangalia kitu anakua kama kakikodolea macho hawezi kugeuza jicho, nilimuambia mume wangu lakini hakujali, aliniambia ni hatua tu za ukuaji.


Nilikaa kimya kwa siku mbili lakini siku moja nilishtuka, alikua kakaa macho yanaangalia chini yanadondosha kama udenda flani. Sijui kama mtakua mnanielewa, achana na machozi ambayo yakitoka hutirririka kwenye ngozi, hapan macho yalikua yanatoa udenda unakua kama vile unaelea mpaka chini. Nilishtuka sana, mume wangu alikua safarini, nilimchukua na kumpeleka hospitalini nikaambiwa kuwa misuli yake ya macho imelegea, lakini nao hawakua na majibu ya uhakika kuelezea udenda wa macho.


Walinipa dawa flani nikarudi nyumbani, hali ile iliendelea, nilimuambia mume wangu kuwa nimeenda hospialini na kupewa dawa lakini ni kama nilimtibua, alikasirika sana, alinitukana mpaka kugikia kunipiga akiniambia ni kwanini nachezea pesa zake wakati mtoto hana tatizo. Nilikaa kimya lakini nikiumia, dawa hazikusiadia, lakini niliogopa kumpeleka hospitalini, nilionga na Daktari mmoja akaniambia nimpeleke hospitali kubwa kwani haikua kitu cha kawaida mtoto kutoa udenda wa kwenye macho.


Mwanzoni mtoto alcihangamka vizuri lakini baadaye alianza kusubaa, alikua anaweza kuka achini mpaka kushikwa shikwa na mainzi lakini wala hashtuki, nilikua naogopa sana lakini sikua na mtu wa kumuambia. Nilivumilia sana mpaka nikashindwa, niliamua kumpigia simu Mama mkwe wangu kumuambia kuhusu mjukuu wake. Alinipa moyo na kuniambia kuwa ndiyo watoto wake wote walivyo, aliniambia kuwa hata mume wangu na wadogo zake nao walikua hivyo hivyo ila walipokua wakubwa walibadilika.


Nilitulia kidogo ingawa sikua na amani kabisa, niliiangalia ile hali mpaka mtoto alipofikisha miezi nane, alianza kusimama na kutembea kabisa, hapo ndipo nilijisikia vizuri kidogo nikiamini kuwa kama kawahi kutembea basi ipo siku hata huko kuzubaa na kutoa udenda wa kwenye macho nako kutaisha. Lakini haikuisha mtoto alipofikisha mwaka mmoja, alirudi tena kwenye kutambaa, miguu yake ilijikunja na kuinyoosha ilikua ni shida sana. Mume wangu alikua anona lakini hakujali, alikua akiniambia kuwa mimi napaniki tu lakini hakuna kitu kibaya.


Mpaka wakati huo bado nilikua nawazungusha ndugu zangu kuja kumuona mtoto, lakini kutokana na hali yake niliamua kumpigia Mama simu na kumuambia kuhusu mwanangu. Mama alipaniki na kuniambia kuwa si kitu cha kawaida. Aliniambia kuwa anataka kuja kumuona lakini nilisita, mume wangu alishaniambia kuwa hamtaki hivyo nilihofia kama akija mume wangu anaweza kumfukuza na mimi kuaibika. Nilimkatalia kwa kumpa sababu sababu nyingi nyingi lakini hakunielewa, nilishampanikisha kwakumuambia hali ya mwanangu.


Mama alikuja kumuona mtoto kinguvu nguvu, mume wangu alikua kasafiri ana sikumuambia ili kukwepesha lawama. Alipokuja na kumuona namna alivyokua alianza kunigombeza ni kwanini muda wote huo mtoto anaumwa na yuko kwenye hali mbaya lakini simpeleki hospitalini. Nilimueleza kuwa mume wangu hataki na Mama mkwe wangu kasema kuwa ni kitu cha kawaida lakini hakujali, aliniambia si kawaida. Kama kawaida yake Mama alipiga magoti na kuanza kuomba, aliomba sana kama vile anakemea, wakati anafanya hivyo hali ya mtoto ilianza kubadilika.


Badala ya hali kuwa mbaya mtoto alianza kuwaka moto, alikua wekundu kama vile anachomwa kwenye taburu, mwili ulikua ukimtoka malengelenge kama vile mtu kaungua. Mama alizidi kuomba na mtoto alianza kulia kwa maumivu, hali ilikua mbaya nikikumbuka na mambo ambayo yalitokea kabla ya kumpata nilihisi kitu kibaya na kumuambia Mama aache kuomba, nilimkatisha Mama maombi, alishangaa na kuniuliza kwanini, nilizuga na kumuambia kuwa mtoto anaungua.


Aligeuka na kumuangalia, kweli alikua na malengelenge kibao katika mwili wake. Ilikua hata shida kumshika, Mama alinigeukia na kuniuliza kama tumemfanya nini mtoto nikamuambia mimi sijamfanya kitu ila sitaki tena aendelee kuomba kwani mtoto anateseka. Alitaka tena kupiga magoti kuomba lakini ghafla yule dada wa kazi aliingia, alimshika Mama na kumsukuma akimfukuza na kumuambia atoke, Mama alishangaa lakini yule binti wa kazi alisema kabisa kuwa hamtaki mule ndani kwani kaja kumla mtoto wangu nyama.


Alikua anaongea maneno ya ajabuajabu na kusema kuwa ni mume wangu kamuambia amfukuze kwani amempigia simu kuwa Mama yuko hapa. Mama hakujali, alipiga magoti tena lakini kabdla ya kuanza kusali yule binti alimuinamia na kumpiga kofi zito usoni. Mama alipepesuka pepesuka na kudondoka chini, alipoteza fahamu, halikua kofi kubwa kiasi hicho, tulimwagia maji akazinduka lakini alikua hawezi kusimama. Nikiwa sijajua nini kimetokea huku mwanangu bado akiwa mwekundu analia Mama aliniambia.


“Mwanangu siwezi kunyanyua mkono wa kulia!” Aliongea kwa shida, kumuangalia upande wake wa kulia ulikua umekauka, umenyauka huku jicho moja limefunga.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU!—SEHEMU YA NNE


Mama hakunyanyuka pale chini, alikua hawezi mpaka nilipomnyanyua, mwili wake ulikua ni mzito sana na alikua kapooza upande mmoja, ilikua shida kwake sana hata kuongea. Nilipata shida sana kumnyanyua kwani yule binti wa kazi hakunisaidia kabisa, nilimnyanyua mpaka kitandani kisha nikaita watu kwenda kumpeleka hospitalini. Waliniuliza maswali mengi kujua kama alikua na presha au alikua na tatizo gani lakini hakua navyo, alikua kawaida tu mpaka pale aliposukumwa na yule biniti.


Madaktari waliniambia kuwa kapatwa na Kiharusi “Stroke” na kusema imetokana na matatizo kwenye mishipa ya damu ya ubongo wake. Mama aambaye alikua akiongea kwa shida alikataa na kuniambia kuwa kuna kitu hivyo nimpeleke kwenye maombi. Nilitaka kumtoa hospitalini kwa  nguvu lakini walikataa katakata na kuniambia kuwa nisubiri kuangaliwa hali yake hata kwa siku mbili, niliwaza mambo mengi kuhusiana na Mama na sijui ni kwanini nilijikuta nakubaliana nao.


Siku iliyofuata mume wangu alikuja, nikitegemea kama vile atakasirika kutokana na Mama kuja kumuona mtoto wakati alishakataza alifurahia sana, aliniambia lilikua ni wazo zuri sana Mama kuja, akaniambia kuwa ni Mama yangu na alikua na haki ya kuwaona wajukuu zake, aligharamia matibabu yote na kuniambia kuwa  hata kama ni kupelekwa nnje yam chi basi atampeleka. Alimsalimia Mama kwa uchangamfu na kumpa pole, Mama alikua akimpenda sana mume wangu, pamoja na kuhisi kuwa nyumba yangu haikua sawa lakini hakuwahi kumshuku mume wangu.


Mbele za watu mume wangu alikua ni Malaika na yeye ndiyo alimshawishi Mama mpaka kukubali kupelekwa Nairobi kwa matibabu, ingawa nilifurahi lakini iliniuma kidogo kwani Mume  wangu alikataa katakata kumtibu mtoto wetu lakini alijipendekeza bila hata kuombwa tena kwa gharama kubwa na kwend akumtibia Mama yangu nnje ya nchi. Nilipomuuliza alinigeuzia kibao kuwa simpendi Mama yangu na mimi ndiyo nataka afe, alinikasirikia sana mpaka nikalazimika kuomba msamaha kwani nilijisikia vibaya.


Pamoja na mambo yote hayo lakini bado mume wangu alikua anataka niendelee kukaa dukani, alikua akikasirika sana kama akija na kukuta niko nyumbani. Kutokana na umbeli na kuhitaji matibabu zaidi Mama alilazimika kuja kuishi kwangu, mume wangu alimpokea, hali yake baada ya kutoka Nairobi iliendelea kuwa mbaya, kwasababu hiyo mdogo wangu wakike alilazimika kuja kumhudumia ili mimi niendelee na kazi kwani ilikua ngumu kumuacha na mfanyakazi kwakua nilikua na watu wawili wa kuwhaudumia, Mama na mwanangu.


Mama alishindwa kabisa kuongea, hata ule upande mwingine ambao ulikua haujapooza nao ulianza kupooza, alikua ni mtu wa kufanyiwa kila kitu. kwa upande wamwanangu alikua akikua vizuri tu, hali yake kiafya kwa kumuangalia ilikua ni nzuri, lakini tatizo lilikua ni katika akili yake na ukuaji wa ndani, bado alikua akiendelea kutoa udenda wa macho, alikua haweza kutembea vizuri na kadri umri ulivyokua unaenda ndivyo alivyokua akirudia utoto, mwili unakua lakini anakua hawezi kujifanyia chochote.


Mume wangu alikua ananibana sana, nilikua nikiamka asubuhi saa kumi na mbili ili kufungua duka saa moja kamili na mara nyingi nilikua nikitoka dukani saa nne usiku, karibu kila siku ninaporudi nyumbani nilikuta mwanangu kalala, kutokana na hali yake nilikua sipendi kumuamsha kwani namkuta kashaogeshwa na kulazwa vizuri na kwakua si msumbufu basi mara nyingi asubuhi nikiondoka anakua kalala. Kusema kweli nilikua sipo karibu kabisa na mwanangu na mara nyingi hata kama ikitokea akiamka usiku na kulia kidogo basi mume wangu alitaka dada wa kazi ndiyo ambembeleze.


Hakutaka nimguse kabisa kwakua alidai nimechoka na kazi yangu nikutafuta pesa tu. Siku pekee niliyokua nikiipata na kuwa karibu na mwanangu ilikua ni jumapili tu, hapo ndipo nilikua namuogesha, kumlisha na kumfanyia kila kitu kama Mama. Jumapili moja nikiwa na muandaa  mtoto kwaajili  ya kwenda naye kanisani nilishangaa kuona ukucha wake wa mguu umeoza. Ulikua ni kama mtu aliyekua anatembea na kujikwaa kisha ukucha ukavunjika na kutoka na nyama, kwa kumuangalia alionekana kama vile yuko kwenye maumivu makali ila hata ukiushika alikua hashtuki, alikua kawaida tu.


Nilimuita Dada ambaye ndiyo alikua anamhudumia na kumuuliza nini kimetokea.


“Sijui juzi kilikua ni kipele tu…” Alinijibu kwa mkato huku akitaka kuondoka, nilimuita na kumuuliza hivi ni kwanini hakuniambia na kwanini anataka kuondoka wakati mimi naongea naye.


“Nikuambie wewe kama nani? Kwani wewe ndiyo umejniajiri hapa? Nishamuambia bosi wangu akasema hakuna shida nikuambie ili nini?” Alijibu huku akisimama na kuniangalia kwa dharau, nilimuangalia bila kummaliza, nilikua na hasira na ukiangalia na hali ya mwanangu sikutaka kusumbuana naye, nilinyamaza tu na kuendelea na mwanangu.


“Watu wengine bwana, kisa mtu katangulia kuolewa yeye anakuona kama takataka!” Aliongea kwa hasira, nilimsikia lakini nilinyamaza, akili yangu ilikua kwa mwananangu, nilimchukua badala ya kumpeleka kanisani nilimpeleka Hospitalini,  walishangaa ni kwanini  nilikua sijampeleka tangu mwanzo wakati kidonda ni kikubwa, nililazimika kudanganya kuwa nilisafiri na kukuta dada wa kazi kamuumiza na hakumpeleka hospitalini.


“Ushafukuza huyo binti?” Nesi aliniuliza.


“Ndiyo…” Nililazimika kudanganya, sikutaka anione mzembe na kushindwa kumhudumia mwanangu vizuri.


“Afadhali maana huyu ni mshenzi, huku si kujikwaa inawezekana hata yeye ndiyo kamfanyia hivi!” Nesi aliendelea kuongea.


Sikumjibu kitu nilinyamaza tu, alimaliza kumfunag mguu tukarudi nyumbani, mume wangu alikua safarini, aliporudi nilimuonyesha mguu wa mtoto na kumuuliza ni kwanini hakusema.


“Nawewe unapaniki vitu vidogo, hicho ni kidonda gani cha kuhangaika nacho?” Alinijibu kwa mkato, nilishindwa hata kuendelea kujibishana naye, hasira zilinipanda sana kwnai mume wangu hakujali, nilitaka kumuuliza kuhusu tabia za binti wa kazi lakini niliona kama nitapoteza muda.


“Mama alisema ni kidaonda cha kawaida tu.” Alijiongelesha.


“Inamaana umempigia simu mpaka Mama yako lakini mimi hujataka hata kuniambia, hivi nina umuhimu gani kwako? Huyu ni mwanangu lakini badala ya kuniambia kuwa ana tatizo unampigia simu Mama yako!” Niliuliza kwa hasira, niliumia sana ni kwanini alikua akimshirikisha Mama yake kwa kila kitu lakini mimi ananipuuzia.


“Una akili kweli wewe, hivi mimi kuongea na Mama yangu leo imekua tatizo, wewe Mama yako yuko hapa karibu mwaka sasa, mimi ndiyo namhudumia kwa kila kitu, namtibu, chakula na kila kitu! kuna ndugu yako ashatoa hata senti tano hapa? Lakini ulishawahi kunisikia mimi nikilalamika? Iila mimi kuongea tu na Mama yangu kumuambia kuhusu wajukuu zake imekua nongwa?”


Aliuliza kwa hasira, nililazimika kunyamaza, nilimchukua mwanangu na kuingia naye chumbani. Siku iliyofuata niligoma kabisa kwenda dukani, ingawa mume wangu alikasirika na kutishia hata kuniacha lakini niligoma, nilitaka kukaa nyumbani na mwanangu. Kwenye saa sita mchana Mama mke wangu alinipigia simu.


“Hivi kuna matatizo gani mwanangu?” Mama mkwe aliniuliza baada tu ya kusalimiana.


“Hakuna tatizo Mama…..Mjukuu wako ndiyo anaumwa…” Nilimjibu kwa mkato, lakini yeye hakuonekana kutaka kujua kuhusu mjukuu.


“Mwenzako kanipigia simu analalamika kuwa mmekorofishana kisa kaongea na mimi na hutaki hata kwenda dukani….”


“Hakuna kitu kama hicho Mama, tulipishana tu kauli, ila sijaenda kwakua mtoto anaumwa, kule kuna wafanyakazi watamudu…” Nilimjibu kwa mkato lakini hakutaka kabisa majibu yangu, alianza kunisomea risala kuhusu malezi, akaniambia kuhusu namna ambavyo muem wangu ananipenda na kisha kuan kugusa ugonjwa wa mwanangu na kuniambia kuwa ni kitu cha kawaida. Hapo ndipo alinitibua nilijikuta napandwa na hasira.


“Umemuona huyu mtoto?” Nilimuuliza.


“Hapana….” 


“Sasa kama hujamuona utasemaje kuwa ni kitu cha kawiada, kila kitu kwako ni kawaida, ulianza kuniambia hivyo tangu zamani lakini sasa hivi unaona mtoto kalemaa kabisa unamjaza unjinga tu mume angu hataki hata kumpeleka hopspitalini!”


Niliongea kwa hasira na kumkatia simu, alishanitibua na nilijua kuwa kama nikiendelea kuongea naye basi naweza hata nikamtukana. Alipiga simu nyingi lakini sikupokea, mume wangu alitoka na kurudi baadaye akiniomba msamaha ila sikutaka kumsikiliza nilimuambia kabisa kuwa siwezi kwenda dukani kama mwanangu hajapona.


“Kuna haja gani sasa ya kutafuta pesa kama siwezi hata kumtibia mwanangu pekee!” Nilimuambia na hapo ndipoa liamini kuwa nimeamua siwezi tena kwenda dukani, alikua mpole na kuondoka, akarudi dukani na kwenda kukaa yeye.


Siku tatu zilipita bila mimi kwenda dukani, hali ya mtoto nayo ilidizi kuwa mbaya, alianza kuwa na maumivu makali, akawa halali kila siku usiku ni kuweweseka, kidogda kiliendelea kuwa kikuba, kilsambaa kutoka kwenye kidole kikubwa mpaka kwenye vidole vingine viwili. Nilimrudisha hospitalini, alipimwa kila kitu lakini alionekana hana tatizo lolote ila kidonda kilizidi kuwa kikubwa. Mume wangu hakua akishiriki chochote kuhusiana na hospitalini, kila kitu nilikua nikifanya mimi. Siku moja nikiwa Muhimbili nilikutana na Mama mmoja.


Alikiona kidonda cha mwanangu ambacho wakati huko klilishachukuavidole vyote vya miguu, vilikua vimetoka ngozi na kuwa kama mtua liyeungua, aliniangalia na kuniambia kuwa inawezekana kuwa mwananangu akawa Sukari kwani mume wake alikua na ugonjwa wa sukari na alikua na kidonda kama hicho. Nilishangaa kwania likua ni mdogo sana na alishapimwa tangu mwanzoni na kukutwa hana. Aliniambia kuwa nikapime tena lakini hata baada ya kupima alikua hana.


Alipimwa kama ana Kansa lakini hakua nayo, alipimwa kila kitu na hakua na chochote. Yule Mama ambaye nilichukua mawasiliano yake nilikuja kumtafuta na kumuambia kuwa amepimwa lakini hana tatizo. Aliniomba kukutana naye, aliniambia kuwa hata kama vipimo vinaonyesha kuwa hana sukari lakinia ana kidonda kama cha mume wake, alinipa dawa flani na kuniambia kuwa mume wake aliitumia na kidonda kikakauka. Iliichukua, ilikua ni dawa ya kupaka, nilimpaka kwa wiki moja tu kweli kidonda kilikauka na akawa hana maumivu yoyote.


Wiki hiyo mume wangu alikua kasafiri, alienda China kununuaa vitu kwaajili ya nyumba aliyokua anajenga. Kila kitu alikua ananishirikisha nna tulikua tunajadiliana. Akiwa huko tulipata habari mabya, kuna mzigo mwingine ambao aliununua na kuutuma kabla ulikua umekamatwa Bandarini na ulikua unatakiwa kupigwa mnada kwania likua akidaiwa kodi ya kama milioni mia na ishirini. Mume wangu alipopewa hizo habari ni kama alichanganyikiwa, akiwa kulekule alikua akipiga simu kapaniki akiniuliza kama nimefanya nini huku akinilaumu kuwa mimi ndiyo sababu.


Sikumuelewa kwani hakukua na kitu chochote nilichokua nimekifanya, nilimsihi kurudi ili kufuatilia mambo yake yeye mwenyewe lakini alikataa, cha ajabu alimpigia simu Mama yake ndiyo akaja nyumbani. Alikaa siku mbili tu bila kutoka kwenda popote kushughulikia, aliondoka na siku ya tatu mume wangu alirudi na kila kitu kilikua sawa. Alienda kulipa deni la TRA na bado akapokea na mzigo mwingine. Aliporudi alsihangaa kuona hali ya mtoto imekua nzuri, aliniuliza nini kilikua kimetokea nikamuambia, mwanzo alinyamaza kimya lakini baadaye alibadilika, alianza kudai kuwa mimi simtunzi vizuri mtoto na nibora aende kuishi na Mama yake.


Tuligombana sana kuhusiana na mtoto kwenda kwa Mama yake, nilikataa katakata kwani nilihisi kuna kitu kibaya. Baada ya kuona vile alimfukuza mdogo wangu pale nyumbani ili tu nisipate muda wa kumhudumia mtoto na kumhudumia Mama kwa pamoja. Pamoja na yote hayo lakini sikurudi nyumba, niliendelea kuwahudumia wote huku nikiendelea kubaki nyumbani. Mume wangu alipoona sirudi nyuma aliacha kutoa matumizi. Alimuondoa binti wa kazi pale nyumbani nikawa nimebaki peke yangu.


Nilipomuuliza sababu aliniambia kuwa haoni haja ya kuwa na mfanyakazi wakati mimi nimekataa kufanya kazi.


“Kama wewe unakaa nyumbani huingizi pesa kwanini ni mlipe mtu mwingine kuja kufanya kazi zako?” Aliniambia, hali ilikua ngumu, chakula ilikua shida kwani matumizi alikua anatoa kwa kupenda, kumhudumia Mama nayo ilikua ngumu, kuna wakatio nilitamani hata kumuondoa Mama lakini nilijua kuwa kama akiondoka atakufa kwani nyumbani hakukua mtu wa kumhudumia.


Hali ya mtoto nayo ilizidi kuwa mbaye, Mama liyenipa dawa alikua akihitaji pesa kwani naye alikua ananunua, sikua na pesa hata ya kula, akiba yangu yote niliitumia kwa matibabu ya mtoto kwani mume wangu alikua hatoi chochote na wala alikua hajali. Alimpuuzia mtoto na niliona kabisa kma alikua anamchukia. Hakua akimgusa tena, hata mtoto akilia nayeye yupo alikua anamuangalia tu. Kuna siku nilikua napika jikoni, mtoto alinisaidia nnje alipokua kakaa nikijua kuwa yuko na Baba yake kumbe alimuacha nnje kabisa na kuingia ndani peke yake, mtoto kaaa chini kabisa kwenye mchanga.


Nnje kabisa ya geri la nyumba yetu, kajisaidia na anakula kinyesi chake, Mama mmoja jirani yetu, ndiyo alimuona akamuokota na kuja kuniita.  Kidonda chake kilikua kimejaa mchanga. Tayari kilishaanza kugusa mguu, kilishafika kwenye kifundo cha mguu hivyo ilikua ngumu sana kumfunga. Nilirudi chumbani kumuuliza kwanini alimuacha mtoto sikumuona, nilitoka na kusikia kama mtu anaongea kwenye chumba alichokua Mama yangu mazazazi, nilienda na kufungua mlango, nilimkuta Mume wangu kavua shati, jasho linamtoka na yuko bize kumvua Mama yangu nguo.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU! —SEHEMU YA TANO


Mume wangu alishtuka sana kuniona, kabla hata sijasema chochote alinyanyuka, shati lake kalishikilia mkononi na kunifuata. Alikua kapaniki kama mtu aliyekurubishwa, alionekana kama vile hajitambui flani, alinisogelea na kuanza kukisukuma.


“Unasema mimi na mbaka Mama yako! Hivi una akili kweli, mimi ni wa kubaka maiti!” Alianza kupiga kelele huku akinipiga, kumbuka hapo nilikua sijaongea chochote, niliingia tu na yeye ndiyo alijishuku, alinipiga sana huku akinitukana na kuniambia kuwa hataki kuniona tena mule ndani.


“Uondoke tena na huyu Mama yako, sitaki kuwaona washenzi kabisa nyie!” Aliongea, mume wangu alinipiga sana kiasi cha kushindwa hata kunyanyuka, alinisukumiza kwenye kocho na kutoka huku akiniambia kuwa akirudi hataki kuniona mimi na Mama yangu, aliniambia kuwa nikiondoka nihakikishe kuwa naondoka na mtoto wangu. mama yangu pamoja na kuumwa hawezi kuongea lakini macho yalikua ynafunguka, alikua anaona kila kitu, niliona machozi ya kimtiririka kwa wingi. Kweli nilijisikia vibaya, ili kumuonyesha kuwa sijaumia labda ni kitu cha kawaida nilijitahidi kunyanyuka.


Nilijisogeza mpaka aliapokua kakaa na kumfuta machozi, mwili ulikua katika maumivu makali na kila sehemu ya mwili wangu nilihisi kama vile imevunjwa vunjwa. Mama alikua analia, kila nikimuangalia ni kama alikua anataka kusema kitu flani lakini alishindwa, nilimtuliza huku nikimpa maneno ya uongo uongo ili angalau ajisikia vizuri lakini hakuonekana kujisikia vizuri, niliumia sana kumuona Mama katika hali ile.


Dakika kama kumi hivi mume wangu alirudi, alikua kafura na alikua anatukana ni kwanini mpaka wakati huo mimi na Mama yangu tulikua bado hatujaondoka, nilimuambia tutaenda wapi akasema si kazi yake, hataki kuonona katika nyumba yake na yeye ana mwanamke mwingine. Alichukua simu yake na kuanza kupigai ndugu zangu wengine, aliiongea maneno mengi ya ajabu ajabu akinishutumu mimi kumloga na kumfanyia vitu vya ajabu.


“Njooni mumchukue Mama yenu, nimechoka kuwasiadia, mimi namsaidaia ndugu yenu lakini anakuja kunisingizia mambo ya kijinga, mimi ni wa kumbaka Mama mkwe wangu, kwa uzuri gania alionao? Hivi wkeli mtu kalala kama mzoga mimi nitakua na hisia naye!” Mume wangu alikua kama mtu aliyechanganyikiwa, nilijatibu kumsigi na kumtuliza, dakika mbili alikua sawa na nyingine alitukana. Alitoka tena na kuanza kuongelea sebuleni, alimpigia simu Mama yake kama kumuomba ushauri, mimi nilikua chumbani lakini kwa namna alivyokua anaongea kwa nguvu nilisikia kila kitu.


“Nimeshindwa Mama, nimeshindwa! Masharti magumu na mke wangu kaniona! Sitaki tena Mama, kama unataka njoo ufanye mwenyewe, mimis itaki tena pesa!” Aliongea, ilionekana kama Mama yake anamtuliza lakini yeye hataki kutulia, alikata simu na kurudi chumbani.


“Unasikiliza nini? Ni kitu gani umesikia?” Alipaniki tena na kuanza kunipiga tena, alinipiga kuhu akiniviringisha chini, alinishika miguu akanivuta mpaka nnje, alifungua mlango wa gari yake na kunisukumia ndani, alifunga milango kisha akarudi ndani.


Alimchukua Mama yangu, bila kujali hali yake alimshusha chini, akamshika miguu na kumburuza mpaka nnje, alimuingiza kwenye gari, akarudi na kumchukua mtoto, alikuja naye akamuweka kwenye siti ya mbele ya gari lake, akamfunga mkanda na kuondoa gari, mimi nilikua nikilia nikijaribu kumnyanyua Mama na kumkalisha vizuri kwani alikua kamrushia ndani tu kama Begi. Alendesha gari ka spidi hakujali tulicvyokua tunarushwarushwa.


Alienda mpaka kwa Shangazi yangu mmoja, amabye ndiyo ndugu yangu pekee aliyekua na nyumba yake Dar. Alikua akiishi maeneo ya Pugu, alitushusha na kutuambia kuwa vitu vyetu vitafuata, hakutaka kuslaimia wala kuongea na mtu, alirudi kwenye gari yake na kuondoka. Ilikua ni kama muvi flani hivi, mume wangu kwa muda  alikua kma kichaa. Shangazi zlitupokea, lakini badala ya kuuliza nini kilichokua kimetokea alianza kunishutumi mimi, alinisema sana, kumbe mume wangu alishampigia simu na kumuambia kuwa namtukana kuwa anataka kumbaka Mama.


“Mwanaume wa watu kampeleka Mama yako mpaka Nairobi lakini leo unamfanyia haya? Unataka kumdhalilisha namna hii…” Aliongea maneno mengi sana bila hata kunipa nafasi ya kujitetea, nilijaribu kuongea na kumueleweshja kilichokua kimetokea lakini tayari alsihamuamini mume wangu na hakutaka kunisikiliza. Aliwapigia ndugu zangu simu na kuwaambia kilichokua kimetokea, akasema kuwa hawezi kuishi na sisi hivyo tujipange kuondoka kwani hataki lawama, aliniambia kuwa mimi nina mume na Mama yangu atarudi Singida kwani hawezi kupona kama ni kufa akafie huko.


Maneno yake yaliniumiza sana, sikuamini kuwanyanatoka katika mdomo wake, Shangazi yangu ndugu wa tumbo moja wa Baba yangu.


“Ndoa nikuvumilia, mtu unapata mwanaume mpole kama yule halafu unahangaika kutangatanga, hivi unafikiri kuna mwanaume mwingine atakuja kukupenda? Mtu mwenyewe umezaa kilema, sasa unafikiri nani atataka huo mzigo, kazi huna lakini kumtii mume nako ni shida. Mimi nilishamuambia Baba yako kuwa huyu Mama yenu anawaharibu, mwanamke anajifanya mlokole lakini watoto kashindwa kulea…” Shangazi aliongea maneno mengi sana ya kunisema Mimi na Mama.


Sikujua kama Shangazi yangu alikua na chuko kisai hicho na Mama yangu, aliongea maneno mengi ambayo yalinifanya kuona kama alikua ni mtu mwingine tofauti kabisa, alikumbushia mambo ya nyuma, mambo ya kawaida kabisa akimshutumu Mama yangu.


“Tena asingekua kafa huyo Mama yako ningesema ndiyo alikua anataka kumabaka Kaka wa watu, maana namjua Kaka hapa alioa tatizo!” Aliongea maneno hayo mbele ya Mama yangu, aliongea kana kwamba Mama alikua hasikii, ni mzigo flani au hana akili kabisa yupo yupo tu, Mama alikua anasikia lakini hawezi kufanya chochote zaidi ya kutokwa na machozi tu.


Nilijisikia vibaya kwani alikua hajui hata kitu kilichotokea. Kila mara alikua akikaziania kuwa tunatakiwa kuondoka, hata mimi nilitaka sana kuondoka, ingawa nilikua sijui naenda wapi lakini sikutaka kuendelea kuishi pale. Akilini kuna kitu kilikua kikiniambia kuwa mume angu labda atajirudi na kunisamehe ili tuendelee kuishi, pamoja na yote hayo lakini bado nilikua nampenda na niliamini kuwa labda mimi ndiyo mwenye makosa, sikua na simu, simu nilikua nimeziacha nyumbani kwani nilitolewa kwa kuburuzwa hivyo hata asingeweza kunipigia simu kuniambia nirudi kitu ambacho kiliniumiza kichwa sana.


***


Nilikua nimeshajiandaa kurudi nyumbani, niliwapigia na kuwaambia kuwa tunakuja na Mama, kila mtu alikasirika na mimi ndiyo nilionekana kama mkosaji, lakini kabla ya kufanya hivyo, asubuhi ya siku ambayo tulikua tunaondoka Mama alianza kutetemeka, kuna kitu kilikua kikimshika kama kwikwi na kumtetemsha kama vile ameshikiliwa na mtu. Alikua akipiga kelele sana kuonyesha kuwa yuko katika maumivu makali, hali ilikua mbaya hata Shangazi aliogopa.


Mjomba aliita Bajaji ili kumpeleka hospitalini lakini hatukufika mbali, Mama alifariki dunia wakati tunampeleka hospitalini. Sijui ni kitu gani kilitokea wakati wa msiba wa Mama lakini sikutoa chozi hata moja, nilikua na uichungu mwingi lakini tangu Mama ananifia mikononi mwanu mpaka tunamzika kijijini sikuwahi kutoa chozi. Kila mtu alikua akinilaumu mimi kutokana na kifo cha Mama, ile hali ya mimi kuondoka kwa mume wangu watu waliona kama mimi ndiyo nilisababisha.


Hata mume wangu ambaye alikuja msibani na ndugu zake wakionyesha kuumia sana alikua akinilaumu mimi.


“Umemuua Mama yako lakini nimekusamehe, mimi ni mtu mwema, nakupenda mke wangu, wewe ndiyo unanifanya kuwa na hasira, nilsihasema siwezi kukupiga lakini unaponisingizia mambo ya uongo basi nakasirika. Mama yako hakufa kwa ugonjwa bali kafa kutokana na maneno yako, hunitii mimi mume wako unategemea nini?” aliongea wakati ananibembeleza mimi kurudi kwake. Nilikua sina mpango wa kurudi kwake lakini niliitishwa kikao na kuambiwa kama mume wangu kakubali kunisamehe basi nirudi.


Hakuna mtu aliyekua anajua kilichokua kikiendelea lakini cha ajabu nikuwa wote walikua upande wa mume wangu. waliniona mimi kama mkosaji na kuona kuwa mume wangu kutaka kurudiana naye ilikua ni kama hisani. Sikujua nini kilitokea, lakini baada ya msiba wa Mama mume wangu alibadilika kabisa, alikua mtu tofauti kabisa, hakua na hasira tena kama za zamani, hakua akinitukana alikua akionyesha kunijali. Kutokana na hali ya mwanangu na kutokana na mimi kutokua na sehemu ya kwenda basi niliamua kurudi kwa mume wangu.


Lakini mambo hayakua kama zamani, nilirudi na kukuta Mama mkwe kashahamia nyumbani kwetu, alikuja peke yake,hakuja na Baba mkwe wala ndugu wengine. Aliniambia kabisa kuwa ni wakati sasa wa kutafuta mtoto mwingine kwani anahitaji mjukuu mwenye akili. Nilishangaa maneneo yake kutoka kwa mwanamke ambaye kazaa. Lakini sikua na kauli, Mama mkwe wangu alikua ndiyo kila kitu katika ile nyumba, mume wangu alikua hakohoi, alikua hawezi kuongea kitu mbele ya Mama.


Kila wakati alikua ni “Mama kasema… Muulize Mama… Kwani Mama anasemaje?” Kila kitu ilikua ni Mama! Mama! Mama! Mama mkwe wangu alikua akiamka saa kumi na moja na nusu za asubuhil, alikua ndiyo mtu wa kwanza kuamka, alikua akipika chai na kumuandalia mume wangu maji ya kuoga. Ni kitu ambacho kilinishangaza, mbali na kwamba halikua jukumu lake lakini pia nyumba yetu ilikua na mabafu ya ndani, tena ya maji ya moto na baridi, lakini kwa joto la Da mara nyingi Mume wangu alikua akioga maji ya baridi ila  Mama yake alisisitiza maji ya moto.


Nilimuambia mume wangu kuhusiana na kutokufurahishwa na hiyo tabia, alitoa kisingizia kuwa tangu akiwa mdogo Mama yake ndiyo alikua akimuogesha,a likua akimchemshia maji hivyo nimuache kwania anajisikia vizuri akifanya hivyo.


“Mama mwenyewe kashazeeka, hana kitu cha kufanya hapa, kashazoea kumtengea maji mzee sasa naona anaboreka!” Mume wangu aliniambia, nililazimika kukaa kimya kwani mume wangu alikua akikiasirika kila mara nikimtaja Mama yake, alikua akinishutumu kuwa simpendi na kuongea maneno mengine mengine ya ajabu ambayo sikuyapenda.


Siku moja niliwahi kuamka asubuhi, nilitaka kumsaidia Mama kupika chai, niliamka saa kumi na moja kamili nikiamini kuwa yeye anaamka saa kumi na moja na nusu hivyo kama nikiwahi kuamka basi nitamuwahi hajapika. Nilienda mpaka jikoni, niakwasha taa, lakini niliona kama kuna uchafu juu ya sinki la vyombo, nilishangaa ni nani alikua kachafua wakati mimi ndiyo nilikua  mtu wa mwisho kutoka jikoni na nilifanya usafi. Juu ya sinki kulikua na unga unga, kulikua na sufuria ambayo ilionekana kama imekorogea unga.


Niliwaza labda Mama mkwe wangu aliwahi kuamka na kupika uji wa mtoto, niiliangalia angalia sikuona uji. Lakini kuna kitu kiliniambia ingia chumbani kwa mtoto nenda kamuangalie, niliingia harakaharaka huku mapigo yangu ya moyo yakienda mbio, sijui kwanini nilijihisi hivyo lakini kuna wakati mwili ulikua kama umepigwa ganzi. Nilifika chumbani kwa mtoto na kukuta taa imezimwa, kulikua na giza, niliwasha taa, nilishangaa kumuona Mama mkwe wangu kakaa kitandani, uchi wa mnyama kampakata mtoto wangu.


Alikua akimlisha uji, aliponiona aishtuka na kuniambia nitoke na kufunga mlango, lakini sikutoka, nilisimama palepale, sijui nilipata wapi ujasiri lakini nilimfuata na kumchukua mwanangu, nilimuangalia lakini hakua akimlisha uji wala nini. Ulikua ni unga wa mahindi ambao ulikua umewekwa kwenye maji na kukorogwa, ulikua haujapikwa.


“Kwanini unamlisha mtoto wangu unga?” Nilimuuliza, bado alikua kakaa uchi wa mnyama, nilimsema saana kwa nguvu lakini hakujibu, alinyamaza kimya kapigwa na butwaa. Kelel zangu zilimuamsha mume wangu ambaye alikuja chumbani, aliingia bila kujali kama Mama yake alikua uchi wa mnyama wala Mama yake hakujitahidi kujifunika baada ya kumuona mwanae.


“Nini kinaendelea?” Mume angu aliniuliza, kwa aibu nilimuambie tutoke ili asiendelee kumuona Mama yake katika hali ile, lakini mume wangu hakujali, alimuangalia Mama yake bila kupepesa macho, alimfuata alipokua kakaa na kumuuliza nini kilikua kimekutokea.


“Kakufanya nini tena huyu mwanamke?” Aliuliza, niliona kama kibao kinanigeukia, sikujali kama kuna cha aibu wala nini, nilimuambia mume wangu kuwa nimemuona Mama yake akimisha mtoto wangu unga.


“Nikweli Mama?” Alimuuliza, huku akitingisha kichwa kukataa aliseama.


“Hapana mwanangu, sijui mke wako kapata wapi haya maneno, mimi siwezi kufanya kitu kama hicho.” Aliongea na mume wangu alionekana kumuamini.


“Mpe Mama mtoto aendelee kumlisha, alikua anampa uji si unga.” Mume wangu aliniambia huku akininyang’anya mtoto, alimkabidhi Mama yake aendelee kumlisha, alinishika kwa nguvu na kunitoa nnje, alifunga mlango wa kile chumba cha mtoto, alinichukua mpaka chumbani kwetu na kuanza kunipiga, alinipiga sana akinishutumu kumsingizia Mama yake mambo ya uongo.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU! —SEHEMU YA SITA


Hakuna sehemu ambayo nilikua nimesema kuwa Mama mkwe wangu ni mchawi lakini mume wangu alinipiga, Niliumia sana kwani Mama mkwe wangu alikua akimlisha mtoto wangu unga. Baada ya kunipiga mume wangu aliniambia nijiandae kwenda dukani, nilikua nimeumia sana lakini hakujali, alikua ni kama mtu mpya kabisa, nilijiandaa na maumivu uangu na kwenda dukani. Akili yangu haikua dukani kabisa, kichwa kilikua kikiuma kutokana na maumivu ya kipigo pamoja na kuwaza kuhusiana na mwanangu.


Mume wangu aliondoka na kuniacha pale dukani na wafanyakazi, lakini mchana wake alirudi, aliwaambia wafanyakazi kufunga duka na kuondoka, walimtii, hakutoa sababu, kulikua na wateja wengi lakini aliwafukuza, tulibaki wawili kufunga mahesabu, nilimuuliza kwanini anafanya hivyo ndipo aliniambia kuwa anataka kutengeneza mtoto mwingine. Hela imekua ngumu sana, nataka tufanye tena mapenzi hapa dukani, aliniambia huku akifung mlango kwa ndani  na kuvua nguo.


Watoto ni baraka si unaona biashara ilivyokua baada ya mtoto wa kwanza, unaona maisha yalivyobadilika, tatizo lako wewe ni mjeuri ndiyo maana nakupiga, lakini kama ungekua unaniheshimu na kuacha mdomo mdoo basi ungeishi vizuri. Aliniaambia huku akinivamia na kunishika, nilimuomba turudi angalau nyumbani alikataa.


“Unafikiri wateja watakujakujaje hapa? Hivi wewe mwanamke huna akili, mbona unapenda kuniudhi namna hiyo lakini, kila tukifanya mpenzi hapa Mungu anabariki, una kismat ndiyo maana nimekuoa, wewe ndiyo mwanamke wangu wewe ndiyo unaleta baraha hapa!”


Alionjgea huku akizidisha kufanya mapenzi na mimi, sikusikia chochote, alikua kama vile ananibaka, hakujali kelele zangu, alionekana kufurahia, alifanya mpaka alipomaliza akavaa nguo zake na kuniambia kuwa naweza kufungua duka kuendelea kuhudumia watu wengine. Nilimuomba kufunga duka alikataa.


“Biashara gani inafungwa mchana!” Aliongea kwa kifupi na kuondoka, nilivaa nguo zangu na kujiweka vizuri, nikafungua duka, kweli siku hiyo niliuza balaa, wateja walimiminika kama siafu, hakuna sikua ambayo niliwahi kuuza kama siku ile.


Lakini kitu cha ajabu nikuwa jioni wakati nafunga mahesbau, katika droo sikuona hata Shilingi kumi. Nikisema Shilingi kumi sikuona kabisa, kwa mahesabu ya vitu nilikua nimeuza mzigo wa zaidi ya milioni kumi, lakini sikuona hata Shilingi kumi. Nilipaniki sana nikiwaza ni kitu gani kilikua kimetokea, siku ile nilibaki dukani peke yangu mpaka jioni, hakukua na mtu hata mmoja aliyeingia kaunta na si wateja kwani kila nikiweka pesa huwa nafunga na nakua na funguo, nilirudi nyumbani nikitetemeka kwani zilikua ni pesa nyingi sana.


Pesa ambazo nisingeweza kusema hata nimemrudishia mtu vibaya, nilikua na mawazo mengi, niliogopa hata kumuambia mume wangu. nilipofika Mama mkwe aliniona, aliniuliza nikashindwa kumaumbia, nilimuambia kuwa niko sawa lakini hakukubali, alianza kunidodosa mpaka nikaongea.


“Hayo ni mambo ya kawaida sana kwenye biashara, huna haja ya kukasiriika hizo ni pesa tu…” Aliniambia, hakuonekana kushtuka na aliona kama ni kitu cha kawaida sana.


“Usimuambie mume wako, wanaume wanajua kupaniki, subiri niongee naye mimi nitajua namna ya kumuambia.” Aliongea, kidogo nilipata ahueni kwani nilikua nikiwaza namna ambavyo nitaongea na mume wangu.


Usiku mume wangu aliporudi Mama yake alimuita chumbani, alishiria kuwa anataka kumuambia kuhusu pesa, waliingia chumbani na kufunga mlango, walikaa kwa zaidi ya masaa mawili, mimi nilikua sebuleni nikisubiri kuona namna ambavyo mume wangua tatoka kwa hasira, nilsihajiandaa kwa kipigo.  Lakini haikua hivyo, mume wangu alirudi akiwa kachangamka, kashikilia shati lake mkononi, kifua wazi na alionekana kuwa katoka kuoga kwani mwili bado ulikua na majimaji.


Hakutegemea kuniona pale, alishanaga, alijua kuwa nimeshalala.


“Nimeongea na Mama tumeyamaliza, ila siku nyingine kuwa makini na pesa!” Aliongea hukua kikimbilia chumbani, nilikaa sebuleni kwa muda wa kama nusu saa hivi nikiwaza, nilikua najiuliza alikua anafanya nini chumbani kwa Mama yake muda wote huo. Nilikosa majibu na kuamua kwenda chumbani kulala, lakini nilifika na kumkuta mume wangu kashalala, alikua kavua suruali na kabaki na nguo ya ndani.


Kitu cha ajabu nikuwa haikua nguo yake, ilikua ni nguo ya ndani yakike. Niliiangalia vizuri ili kusema kuwa labda ilikua ya kwangu lakini hapana haikua yangu. Nilijikuta nashikwa na hasira na kumuamsha mume wangu, sikufikiria chochote nilidhani kuwa labda anachepuka au kashakua shoga. Nilimuuliza kuhusu ile nguo ya ndani lakini aliniangalia kwa dharau kisha akasema.


“Yaani unaniharibia usingizi wangu kwa kitu cha kipuuzi namna hiyo? Wewe mshenzi nini?” Alionekana kubadilika, kwa namna alivyokua ameniangalia nilijikuta nanywea na kuacha kuuliza uliza, nilijua tu kuwa nitapigwa na jibu sitapewa.


Nilipanda kitandani na kulala, usingizi haukuja mpaja asubuhi, asubuhi naamka Mama mkwe alikua kashafanya kila kitu, lakini nilipotaka kuondoka aliniambia kuwa nimchukue mwanangu na kwenda naye dukani.


“Kwanini Mama wewe si upo nyumbani?


“Umeshasema nampoga sasa akifa sitaki maneno, mimi nitahudumia mwanangu na wewe hudumia wakwako.” Aliongea kwa mkato, nilishangaa yale mabadiliko kwani pamoja na kugombana jana yake lakini jioni yake alinichangamkia sana, nilimuambia mume wangu na kumuambia kuwa siwezi kwenda na mtoto dukani n bora kubaki lakini alikataa.


“Kweli pale kwako uko bize sana, mimi nitaenda naye…” Aliongea na kumchukua mtoto, nilishangaa sana kwani mume wangu alikua akimchukia sana mtoto wetu, ni nadra sana alikua anambeba na hata akimuona akijisaidia alikua akimuacha.


“Haina shida nitaenda naye tu…” Nilimuambia, nilikua na wasiwasi sana kumuacha mume wangu na mtoto.


“Hapana ile ni Biashara wewe uko bize, mtoto mwenyewe huyu atafukuza wateja tu.” Mume wangu alimchukua kinguivu nakuondoka naye, nilienda dukani lakini sikua na amani, mume wangu alimchukua mtoto tu, hakubeba hata chakula cha mtoto.


Nilikaa kutwa nzima sina amani, nilijaribu kumpigia simu mume wangu mara kwa mara ili kumuuliza kuwa mtoto anaendeleaje lakini hakupokea simu zangu wala kujibu meseji zangu. Nilipaniki na ilipofika saa kumi uvumilivu ulinishinda, niliamua kwenda kumuangalia mwanangu nikijifanya kuwa kuna dawa nimempelekea. Nilifika dukani mume wangu hakuepo, alikua katoka, nilikuta wafanyakazi, nilimuulizia mume wangu wakaniambia kuwa katoka muda mrefu na nilipomuulizia mtoto walinionyesha.


Mtoto alikua amekalishwa kwenye karai la plastiki, hawajamuwekea hata nguo za kukalia, kama unavyojua joto la Dar plastiki ikapata jua, kara lilikua la moto, alikua kaaka kawekwa pembeni kabisa ya duka, kwenye kona, ilikua ngumu kwa mtu kumuona mpaka kuchungulia kwani alikua amezibwa na mifuko ya sementi hivyo vumbi lote kumshukia. Alikua kalala, nilimkimbilia na kumuamsha, nikamtoa kwenye lile karai, wale vijana wafanyakazi waliogopa na kuniambia kuwa wameambiwa kumaucha hapo hata akilia na asimguse mtu, niliwaambia kuwa yule ni mtoto wangu na hakuna mtu wakunizuia.


Nilimchukua na kuondoka naye mpaka nyumbani, huko nilikutana na mume wangu akiwa kakaa sebuleni na Mama yake. Walishangaa kuniona kwani ni kama nilikua nimewafumania, Mama mkwe wangu alikua kajifunga Khanga moja tu, tena imelegealegea hivyo kaucha mapaja yake na sheemu nyingine wazi, hakua hata na nguo ya ndani, mume wangu alikua kavaa Boxer tu, kwakuwaangalia walikua wanatia kichefu chefu, mume wangu alishangaa kuniona  pale, alianza kunifokea kwanini nimemchukua mtoto lakini sikumsikiliza, nilingia zangu chumbani na kumuogesha mtoto, aliku bado kalala nilipomwagia maji ndiyo alizinduka na kuanza kulia.


Mtoto alikua anapumua kwa shida, nilimuomba mume wangu tumpeleke hospitalini lakini alikataa, niliogopa nikajua kuwa atakufa, nilitoka kutaka kwenda hospitalini lakini mume wangu alinikataza, alinishika na kunifungia ndani, kisha yeye na Mama yake walianza kunipiga, walinipiga sana na kunitukana kuwa nataka kuwaharibia familia yao, waliniambia kuwa kama nataka kuondoka niondoke kwani sina maana tena. Mama mkwe amabye siku zote pamoja na vituko alionekana kuwa ananitetea siku hiyo nayo aliniambia kama nataka niondoke.


Nilinyamaza kimya bila kusema chochote, baada ya kumaliza kunipiga waliingia chumbani kwa Mama mkwe wangu na hawakutoka mpaka subuhi. Nilimchukua mwanangu mpaka chumbani, angalau alikua anapumua kidogo ingawa kwa shida, hakua anakula chochote. Usiku wa manane wakati kuna kuchakucha kama kwenye saa kumi kumi hivi Mume wangu alirudi chumbani, alimchukua mtoto na kutoka naye, mimi alinifungia kwa nnjie, alikaa naye mpaka asubuhi ndipo akamleta, mtoto alikua kachangamka kidogo, aliniambia nijiandae kwenda dukani na mtoto ataenda naye na kama nikijaribu kumchukua basi ataniua.


Lakini kabla ya kuondoka mume wangu alipigiwa simu, Baba yake alikua anaumwa sana na wadogo zake walitaka kumleta. Aliongea kwa huzuni kidogo, alinigaukia na kuniambia.


“Baba hali yake mbaya!” Nilijikuta natetemeka tu sijui chakumjibu zaidi ya kumuambia pole, alitoka na kwenda kwa Mama yake.


“Hali imekua mbaya, atakufa….” Nilimsikia akiongea huko ndani.


“Kwahiyo akifa si atazikwa!” Mama mkwe alimjibu.


“Lakini Mama yule ni Baba yangu….”


“Una uhakika gani, anayemjua Baba yako ni mimi Mama yako tu, yule ni mwanaume kama wanaume wengine, nimesema kuwa sitaki kumuona hapa, yule ndiyo atakutia umasikini, ukakumbuka kipindi kile kidogo ufe alikua Baba yako!”


“Lakini Mama…”


“Hakuna cha lakini, nimesema kuwa muache afe, kama ni Baba utapata mwingine, kwanza mimi Mama yako ninatosha, naweza kuwa Baba na kuwa Mama pia. Huwezi kumchukua mtu hata hajielewi elewi na kumleta hapa, hapana, wewe ndiyo unakaribia kufanikiwa, Baba yako akija hapa ataharibu kila kitu. Kama anakufa afe tu mimi simtaki, wewe unanitosha. Unafikiri sadaka zote hizi tunazotoa atakubali kuona tunatoa, mara ngapi amekusingizia mambo ya uongo, mara ngapi ananitukana kuwa mimi natembea na wewe, hajui hata tunayoyafanya lakini yeye anajifanya mwanaume wakati kazi yake ni kutumia tu!”


Mume wangu alionekana kuwa na wasiwasi sana, alitaka kumsaidia Baba yake lakini Mama yake hakutaka, sikujua wamekorofishana nini kwani Baba mkwe wangu ni mtu mpole sana, mtu wa dini na mtu ambaye hana maneno mengi. Haongei na mara zote nilizomjua alikua ni mtu wa salamu, mtu wa kukaa kimya na mtu wa kufuata kila kitua mbacho Mama mkwe wangu atataka. Baada ya kushindwana na Mama yake mume wangu alitoka kwa hasira, alinilazimisha kwenda dukani na kumuacha mtoto.


Nilifika dukani nikiwa na mawazo mengi, kwanza kuhusu mwanangu na pili kuhusu Baba mkwe wangu, nilitamani kumpigia na kujua kilichokua kikiendelea lakini nilijua kuwa mume wangu akijua basi itakua shida. Alishanikataza kuingilia mambo ya familia yake na mara nyingi alikua hapendi kabisa mimi kuongea na Baba yake. Jioni nilirudi nyumbani na kumkuta Baba mkwe wangu nyumbani, alikua kalala sebuleni kachoka, mwili ulikua umekondeana kabaki mifupa, ingawa alijitahidi sana kuchangamka lakini alionekana kuwa katika maumivu mazito.


Mume wangu alikua bado hajarudi, Baba mkwe wangu aliletwa na wifi yangu mmoja, yeye alikua chuo na alienda kujijini kumuona Baba yake, alimleta na ilionekana kuwa hakumuambia mume wangu kwani nayeye alirudi nyumbani alishanga akumuona Baba yake pale. Lakini alimkatibisha vizuri, wifi yangu aliyemleta Baba yake aliondoka siku ileile, alikua hapatani na Mama yake na mara nyingi alikua hataki kuja kwa Kaka yake. Usiku nilimuandalia chakula Baba mkwe wangu kwani Mama mkwe na Mume wangu walikua chumbani muda mwingi wakijifanya kuongea.


Pamoja na hali yake mbaya lakni aliweza kula peke yake, baada ya kumuewekea chakula nilienda kumlaza mtoto niliporudi Baba mkwe wangu aliniita na kuniambia nikae karibu yake. Nilienda na kukaa karibu kwani sauti yake haikua kubwa sana, aliniangalia kwa mshangao kana kwamba ndiyo alikua ananiona kwa mara ya kwanza, aliniangalia kuanzia usoni kushuka chini kisha akanyanyua mkono wake na kunishika usoni huku macho yake yaliyochoka yakiushangaa uso wangu.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU! —SEHEMU YA SABA


“Mwanangu watakuua kama mimi, wewe bado mdogo sana, ondoka katafute maisha yako hutakufa kwakuwa masikini!” Baba mkwe aliongea kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo, alinishika mashavu kama vile mtu mzima anamshioka mtoto kuonyesha msisitizo flani. Alinikodolea macho kwa nguvu mpaka nikaogopa.


“Mimi nilishindwa kuondoka kwa uezembe wangu mpaka najishtukizia tayari nilishakufa, wewe bado una nguvu mwanangu, unajua wanachokifanya huko ndani?” Aliniuliza, nilitingisha kichwa kusema hapana, kabla hajasema chochote Mama mkwe wangu alitokezea.


“Mnafanya nini hapa? Unafanya nini na huyu mwanamke, mwanaume mshenzi kabisa wewe!” Alianza kutukana huku akimfuata Baba mkwe wangu, alimnyanyua na kutaka kumpiga lakini mume wangu alitokea na kuingilia.


“Mama muache Baba, si umuache tu walikua wanaongea hawa…” Mume wangu alimtetea Baba yake. Alimshika Mama yake ili kumuondoa pale kwani alikua kakasirika kafura ana hasira sana, alitukana sana hukua kikumbushia mambo ya zamani, namna alivyomsaidia Baba mkwe, namna alivyomchukua akiwa hana kitu na kumpa mmakazi.


“Unanichafua kwa mwanangu kuwa nafanya ujinga sasa nitakuonyesha, kila siku si unanisingizia kuwa natembea na mwanangu sasa ngoja nikuonyeshe, huyu si mwanaume kama wewe!” Mama mkwe aliongea huklu akimshika mume wangu kiuno, alimuinamisha mume wangu kwa nguvu na kuanza kumla denda, mume wangu alikata ana kumsukuma lakini Mama mkwe hakujali.


“Unaopgopa nini, muonyeshe Baba yako kuwa wewe ni mwanaume, kila siku si anatusingizia tufanye kweli sasa!” Alifoka lakini bado mume wangu alikaataa. Mama mkwe hakumuachia, alimshika suruali, akaingiza mikono yake sehemu ya mbele kisha akaanza kuuchezea uume wa mume wangu.


Alifanya hivyo huku mkono mmoja kamshikilia mume wangu kambana sana, ni kama alikua akijua udhaifu wa mume wangu kwani kwa kawaida ukimshika sehemu hizo alikua akilegea.


“Mama acha! Mama acha Unaniaibisha Mama acha…” Mume wangu alilalamika lakini kwakulegea, alikua akionyesha ushirikiano kwa kumshika Mama yake sehemu mablimbali za mwili wake. Mama hakuacha alizidisha manjonjo na kumvua suruali.  Nilishindwa kuendelea kuangalia nilitoka harakaharaka na kukimbilia nnje.


“Unakimbia nini? Si alikua anakuambia kuwa mimi natembea na mumeo sasa unaogopa nini, nimewaonyesha ili muache kuongea wahsenzi nyie!” Mama mkwe aliongea na kumuachia mume wangu, alirudi chumbani kwake, Mume wangu alibakia pale sebuleni, alishindwa hata kunyanyuka kwa aibu, alikaa kwenye kochi na kuanza kulia kama mtoto. Baba yake alikua akimuangalia muda wote bila kusema chochote, mume wangu alimsogelea Baba yake na kumpigia magoti huku akimuomba msamaha, alikua akilia sana na kwa kumuangalia ni kweli alikua akijtia.


“Nisamehe mimi mwanangu, mimi ndiyo nimeyaruhusu haya, nilimuacha Mama yako kuwa mwanaume ndani ya nyumba na ndiyo maana uko hivi leo…” Baba mkwe naye alianza kulia, ilikua kama sinema, nilishindwa kuvumilia niliingia ndani na kumchukua mwanangu. Sikutaka kuendelea kukaa tena kwenye ile familia, nilitaka kuondoka na mwanangu na kwenda popote lakini si pale. Nilipotoka sebuleni mume wangu aliniona, aliniuliza naenda wapi nikamuambia nimechoka vituko vyao hivyo ni bora kuondoka kama ni kufa nikagie mabali na umasikini wangu.


Aalinigeukia mimi na kuanza kuniomba msamaha, aliniambia kuwa hata yeye alikua hajui kilichokua kimetokea hivyo nimsamehe na hatarudia tena.


“Mama ondoka, muokoe mwanao, huyo mtoto hapa atakufa, ondoka! Ondoka mimi nilishindwa kumlinda wakwangu sasa kawa msukule wa Mama yake ondoka!”  Baba mkwe alinisisitiza kuondoka lakini bado mume wangu aliendelea kubembeleza.


“Mwanangu muache aondoke, Mama yako si mtu atakuua wewe na familia yako, muache aondoke!” Aliongea akimshika mume wangu kumsigi aniache niondoke, mume wangu alinywea kidogo na kuniacha nilitoka mpaka nnje, lakini kabla ya kufika popote Mama mkwe alikuja.


Alinishika na kunizaba vibao viwili.


“Kama unataka kuondoka basi ondoka kivyako, mjukuu wangu niachie mshenzi mkubwa wewe!” Aliongea kwa hasira hukua kininyang’anya mtoto. Alimchukua na kuingia naye ndani, nilimfuata nyumanyuma nikitaka anipe mwanangu, alifika mkapa ndani na kumrusha mtoto chini kwenye sakafu. Mwanangu alipiga kelele za maumivu na kuanza kulia, Mama mkwe alienda na kumvamia mume wangu.


“Hivi wewe una akili kweli, unakalia kumsikiliza Baba yako! Unataka kuwa kama Baba yako maiskini wakutupwa, hivi unafikiri akimchukua mwanao kuna mali tena, nimehangaika sana, nimejitoela sana kwaajili yako, hii familia haina shukurani kabisa!”


Alifoka, mume wangu alimuanmgalia tu, alikua mdogo kama piritoni, kama katoto kadogo kalikokua kakigombezwa na Mama yake kwa kuiba pesa.


“Nimeahangaika sana na hizi mali, siwezi kuruhusu wewe au Baba yako kuzipoteza, kama huyu mbwa wako anaondoka aondoke lakini aniachie mjukuu wangu, hivi wewe mwanamke unafikiri tunakutaka hapa, huna faid ayoyote, ushatuzalia, tulihitaji kizazi chako tu mshenzi wewe ila wewe unaweza kuondoka wakati wowote! Hauna maana kabisa lakini mjukuu wangu hii ni damu yangu, tumeunganishwa na damu wakati wewe hakuna kitu!”


Aliongea kwa ukali, kila mtu alinyamaza hata Baba mkwe naye alinyamaza!


“Unataka kuondoka, ondoka sasa!” Alinigeukia, nilimuambia kuwa mimi siwezi kuondoka bila mwanangu na hata akifanya nini hawezi kunizuia kwani ni mwanangu na mimi ndiyo nina haki naye. Nilimjibu kwa hasira, aliniangalia machoni kisha akaniambia.


“Nimekuamini, nilikua nahitaji hii hasira, nimeona macho yako kuna hasira na ujasiri wa kumlinda mwanao, hivyo ndivyo ambavyo Mama anatakiwa kuwa, kuweza kufanya kitu chochote kile kwaajili ya wanae. Mimi ni Mama nakuelewa hata mimi naweza kufanya chochote kile kuwalinda wanangu!”


Aliongea hukua kiingia chumbani kwake, alikaa kama sekunde kumi akatoka, alinifuata na kunishika mkono, ni kama alikua akiangalia kitu katika mkono wangu. lakini ghafla kitendo kama cha sekunde tano hivi Mama mkwe alichukua mkono wangu wa kulia, akanichana na kitu kama kiwembe kwenye kiganja, damu ilianza kutoka, kabla ssijafanya chochote alijichana nayeye kisha akachukua kiganja chake na kukiunganisha na changu, alinishikilia kwa kunibana mkono kwa muda wa kama sekunde kumi, kuna vitu alikua akiviongea, aliniachia na kuingia chumbani kwake.


“Nimechoka ngoja nikalale, sasa hivi unaweza kuondoka.” Aliongea huku akiingia ndani. Kila kitu kilitokea kwa haraka, hakuna aliyejua kafanya nini, mume wangu alikua akishangaa na lakini Baba mkwe alikua akikohoa kwa nguvu, alipiga kelele na kuwa analalamika kama vile anakabwa,a likohoa kama kuna kitu kimempalia, alipiga kelele mpaka akanyamaza. Mume wangu alienda kumuangalia na tayari alikua kashakauka, Baba mkwe alifariki palepale tukiwa tunamuangalia. Mama mkwe yeye aliendelea kulala hata mume wangu alipomgongea kumuambia kuhusu Baba yake hakuamka.


****


Mama mkwe wangu alihudhuria mazishi ya mume wake kama kawaida, alilia na kuhuzunika kama watu wengine, alionekana kuumizwa kuliko hata watoto wake, kila kitu kilikua kama maigizo. Wakati wote huo mume wangu alikua karibu naye kumfariji na kumpa moyo, watoto wake wengine ni kama walimsusa, kila mmoja alikua na mambo yake. Hata baada ya msiba kila mmoja aliondoka kivyake na hakuna aliyetaka kuwa karibu na Mama yake, walikua wanajua tabia zake na ni kama walikua hawamtaki.


Maneno ya Baba mkwe wangu akiniambia kuondoka bado yalikua kichwani kwangu, yalikua yakizunguka kipindi chote tuko kijijini kwenye mazishi, nilishapanga kuondoka kwani niliamini kuwa Baba mkwe wangu alitoa maisha yake ili kuja tu kuniambia kuwa niondoke. Alikua katika hali mbaya sana lakini kila siku alikua akiwalalamikia na kuwalila wanae ili kuja kwangu kuniona. Sikupanga kumuambia mtu yeyote, nilijua kabisa kuwa mume wangu hawezi kuongea chochote mbele ya Mama yake hivyo kumuambia kuwa naondoka ingekua ni kazi bure.


Baada ya mazishi nilirudi nyumbani, tulirudi na Mama mkwe ambaye sasa ndiyo alikua akisimamia Biashara za mume wangu, inagwa kwa nnje mume wangu alionekana kama mmiliki na kila kitu kilikuua kwa jina lake lakini kiuhalisia yeye alikua ni kama mfanyakazi tu, alikua akifanya kila kitu anachotaka Mama yake na kamwe alikua hawezi hata kusafiri bila kuongea na kukubaliana kwanza na Mama yake. Siku moja mume wangu aliniambia niende dukani, niliondoka na kama kawaida yeye ndiyo alimchukua mtoto kwenda kukaa dukani kwake ambapo alikua akimlaza kama msukule.


Nilishajiandaa kuondoka na nilishakusanya pesa zangu kidogo, ilipofika mchana niliwaaga wafanyakazi, nilishapiga simu kujua kuwa mume wangu yuko wapi na kwakua Mama mkwe alikua nyumbani basi nilipanga kumpitia mwanangu dukani kumchukua kinguvu kisha kuondoka zangu. Nilifanya hivyo na nilifanikiwa kweli kumchukua, nikiwa kwenye Bajaji nilipanga kwenda mwanza, ni kisha Bukoba, ni sehemu ambayo nilishafanya kazi zamani na nilijkua nitaanza maisha huko, lakini kwa siku hiyo ilikua ni lazima kulala nyumba ya wageni.


Niliingia kwenye Bajaji na kumuelekeza sehemu ya kwenda, alienda mpaka kwenye nyumba moja ya kulala wageni karibu kabisa na ubungo kwani nilishakata na tiketi kwaajili ya safari. Alitoka na kufungua bajaji ili nitoke.


“Dada mbona unatoa damu?” Aliniuliza derava Bajaji baada ya kunifungulia, alitaka kushusha mabegi na kunisaidia kubeba mtoto ndipo alipogundua kuwa siti zote za nyuma zilikua zimejaa damu. Sikua nikijua kilichokua kinaendelea mpaka aliponiambia, kweli nghuo na kila kitu kilikua kimejaa damu.


Nilishtuka na pale pale mwanangu naye alianza kulia, wakati huo mwanangu alikua na miaka minne lakini kwa kumuangalia alionekana kama mtoto wa mwaka mmoja, alikua hakui anarudia utoto.


“Mama, una damu…” Mwanangu aliniita. Nilishangaa, nilishikwa na butwaa kwani ilikua ndiyo mara ya kwanza mimi kusikia sauti ya mtoto wangu, alikua kaongea kwa mara ya kwanza.


“Mwanangu umeongea! Mwanangu umeongea!” Nilijikuta napiga kelele sikukumbuka hata kama nilikua na damu zinanitoka. Dereva alinishangaa na mwanangu aliendelea kusema “Mama una damu… Mama una damu…”


Nikiwa sina hili wala lile simu yangu iliita, ilikua ni namba ngeni na nilipopokea nilisikia sauti ya Mama mkwe wangu.


“Unaweza kuondoka sasa, niachie mjukuu wangu wewe ondoka.” Aliongea na simu ilikatwa, baada tu ya kukata simu nilianza kusikia maumivu makali sehemu za siri, nilikua naumia sana huku tumbo likikata, iliishiwa nguvu na kupoteza fahamu. nilikuja kuzinduka kama masaa mawili baadaye, mume wangu alikua pembeni yangu na mwanangu ambaye aliacha kusimama akiwa na miezi nane alikua kasimama pembeni yangu, ilikua ni kama miujiza flani.


“Nilikuambia Mama alisema kuwa hata mimi nilichelewa kutembea na kuongea, unaona mtoto wetu…” Mume wangu aliniambia hukua kitabasamua, kwakumuangalia kwanangu alikua ni kama mtu mpya kabisa, alikua amesimama vizuri anatembea na kuongea kama chiriku.


“Una mimba, Daktari kasema upumzike…” Mume wangu aliongea, lakini kabla ya kumalia Mama yake aliingia.


“Unafanya nini na huyu mchawi, mchukue mtoto wetu tuondoke!” Mama mkwe alifoka, mume wangu alijaribu kumtuliza lakini Mama  mkwe hakujali, aliendelea kufoka na kupiga keleel.


“Mama mimi siwezi kumuacha mke wangu, ana mimba nitamuachaje hapa!” Mume wangu aliongea kwa kujiamini.


Hakuna cha mimba wala nini, hiyo itatoka tu! Nimesema muache tuondoke, mimi ni Mama yako ni lazima unisikilize!” Mama mkwe aliongea lakini bado mume wangu hakumsikiliza, alimchukua mtoto na kumpakata, mume wangu alionekana kufurahia sana namna mtoto alivyokua na afya nzuri na alivyokua akimuita Baba, alionekana kabisa kukereka na amrisha amrisha za Mama yake. Mama mkwe alifokafoka lakini mume wangu hakujali, alikomaa kubaki na mimi mpaka Mama yake akakasirika na kuondoka kwa hasira.


Mume wangu alikaa na mimi mpaka kuruhusiwa, ni kweli nilikua na ujauzito wa mwezi mmoja na niliambiwa kuwa makini kupumzika nisisumbuliwe sumbuliwe kwani naweza kumpoteza. Tulirudi nyumbani na kukuta Mama mkwe katuandalia chakula, alikua kabadilika sanma, hakua yule wa jana yake ambaye alika akitukana kuwa hanitaki. Alionyesha kunijali na kujali mjukuu wake, alinikaribisha vizuri mpaka nikashangaa, alimuomba msamaha mume wangu kwa kumkaripia wakati yuko hospitalini.


“Tangu Baba yako kuondoka nimekua mtu wa mawazo sana, nimekua mpweke sana mwanangu naomba unisamehe.” Alimuambia mume wangu, alinifuata na kunpigia magoti.


“Mwanangu naomba unisamehe, najua siku mbili hizi nimekua mkali lakini nikwakua wote nawapenda, nimeshazeeka na nimekua peke yangu….” Aliopngea kwa huruma, mume wangu alimfuata na kumnyanyua.


“Mama usipige magoti sio vizuri, naelewa unayopitia mke wangu kakusamehe huna haja ya kulia…” Aliongea huku akiniangalia kama vile alikua anataka nitamke kuwa nimemsamehe Mama yake.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU! —SEHEMU YA NANE


Nilishindwa kufanya chochote, nilijua kabisa kuwa Mama mkwe wangu hajabadilika na kuna kitu alikua anakitaka, lakini kwa namna ambavyo mume wangu alikua kaonyesha kunijali nilijikuta namuambia nimemsamehe. Niliongea huku moyo ukivuja damu kwani ndiyo kwanza nilikua nimepata kaamani kidogo baada ya kumuona mwanangu kapona, nilikua nahisia mani kwani karibia miaka mitano ya ndoa nilikua sijawahi kuwa na furaha na yote hayo yalitokana na Mama mkwe.


“Kama hamtakua na amani basi mimi niondoke, najua sina pakwenda mwanangu, Baba yako amekufa kaniacha mpweke na ndugu zako hata hawanitaki, lakini sitaki kuingilia ndoa yenu, nataka muwe na amani nataka kuondoka mwanangu.” Mama mkwe aliongea, alishaandaa chakula lakini kumbe alishaandaa na mabegi akidhamiria kuondoka. Alienda chumbani kwake na kutoa mabegi akitaka kuondoka.


“Unataka kwenda wapi? Huendi popote, wewe ni mama yangu na mke wangu hana shida na wewe, utakaa hapa mpaka utakapochoka kukaa!” Mume wangu alimuambia Mama yake huku akimzuia kutoka.


Lakini Mama mkwe hakujali, alikua ashadhamiria kuondoka, wakiwa bado wanabishana alikuja Kaka mmoja, kijana tu wa makamo na kuchukua mabegi ya Mama yake, mume wangu alimbembeleza sana lakini hakukubali, alimuambia anaondoka ili kumpa amani yeye na mke wake. Moyoni nilikua nashangilia, nilikua nikiamini kuwa kama Mama mkwe wangu akiondoka basi nyumba itakua na amani, Mama mkwe aliondoka na alikataa katakata kusema anapokwenda.


Baada tu ya Mama yake kuondoka mume wangu alibadilika ghafla, alianza kuwa mkimya, alikua kama vile kachanganyikiwa, mtu wa mawazo na mara kadhaa alikua akishinda nyumbani, hakutaka kwenda dukani, nililazimika mimi kuchukua jukumu la kwenda kusimamia maduka yake. Mume wangu alikua na miradi mingi, alikua na duka la vifa nye ujenzi alilokua akiuza juma, mauzo kwa siku yalikua hayapungui milioni kumi. Alikua na duka la spea za magari, alikua na malori ya mizigo na biashara nyingi nyingi. Zote hizo alikua hataki kusimamia, alikua mtu wa mawazo na kila wakati alikua ni mtu wa kuangalia simu yake.


“Mama hajaja dukani?” Aliniuliza, lilikua ni swali lake la kila siku nikitoka dukani na jibu lake lilikua ni hapana. Mama yake alikua kaondoka kimwili lakini alikua kajaa tele mule ndani, usiku mmoja tulikua tunafanya mapenzi na mume wangu, wakati yuko kifuani ghafla alilegea na kuanza kulia, alishuka na kukaa kitandani, alionekana kama kuna kitu kinamsumbua.


“Hivi Mama atakua ananikumbuka kweli? Mbona kaniacha, hapigi hata simu, inamaana hanipendi?” Aliniuliza huku akilia kama mtoto mdogo, nilimuangalia kwa hasira bila kumjibu kwani nilihisi kumtukana.


Nilijifunika na shuka na kulala zangu, yeye alibaki macho akilia kana kwamba alikua kafiwa. Siku nyingine wakati tunafanya mapenzi aliniambia subiri, nilikaa kusubiri akachukua picha moja kubwa ya Mama yake ambayo ilikua katika fremu ya kioo akaiweka kwenye meza ya kitanda kisha akataka tuendelee kufanya mapenzi. Mume wangu alikua kama mtu aliyechanganyikiwa, baada ya kuiweka ile picha alijisikia vizuri, alichangamka na kutaka tuendelee lakini mimi nilishindwa. Nilimuambia siwezi kuendelea kufanya mapenzi, bila aibu alichukua picha ya Mama yake na kwenda nayo bafuni kujichua.


Ile hali ilikua inanitia kinyaa, nilitamani kuondoka lakini nilijua kama nikiondoka basi kila kitu kitavurugika, Biashara ilianza kuwa ngumu, wateja walipungua sana kwa kasi, ghafla nilishangaa yanaibuka madeni ambayo mimi nilikua siyaelewi. Siku moja asubuhi nafika dukani nakuta kuna kufuli kubwa, lilikua ni la TRA na walikua wamefunga duka kwakua tulikua tunadaiwa kodi ziadi ya milioni mia, ilikua ni malimbikizo ya zaidi ya miaka mitano. Nilimuuliza mume wangu akaniambia kuwa hayo mambo Mama ndiyo alikua anamaliza.


Hakujali duka kufungwa na hakujali nyumba yetu moja ilipouzwa na benki. Hali ilikua mbaya, niliamua kuwapigia wadogo zake ili angalau kuja kuongea naye, lakini ni kama kila mmoja alikua hataki kujishughulisha na yeye. Walikua kama wamemtenga, akuna aliyekua akijua alipokua Mama yao na wala hakuna aliyekua akijali.


“Mama kashaondoka kila kitu kitakufa! Wewe ndiyo ulisababisha Mama kuondoka sasa utajua mwenyewe!” Sikumoja mume wangu aliniambia, alianza kunywa pombe na badala ya kulala nyumbani alianza kukesha baa.


Kila siku alikua akija dukani, anachukua kiasi kikubwa cha pesa na kuondoka, anakitumia mpaka kikiishi ndiyo hurudi nyumbani. Wakati mwingine alikua harudi kabisa, nilikua nafanya kazi ya kumtafuta kwenye mabaa na mara nyingi nilikua nikimkuta gest na wanawake. Siku moja nilipigiwa simu na mtu ambaye sikua nikimfahamu, mume wangu alikua kaokotwa kwenye mitaro hajitambui, nilienda hospitalini na kumkuta mume wangu akiwa katika  hali mbaya, alikua kama mtu aliyepigwa kaumizwa mwili mzima.


Alikaa hospitalini kwa wiki mbili ndipo akaruhusiwa, lakinia litoka akiwa na kidonda mguuni, hakikutokana na majeraha hapana, kilianza kama kaupele tu kisha kikaanza kuwa kikubwa taratibu taratibu mpaka kikachukua mguu mzima. Kilikua kikipanuka harakaharaka, alikua katika maumivu makali lakini hospitalini napo walituambia tuondoke atakua akiletwa mara moja moja kusafishwa. Katika zile wiki mbili ambazo nilikua hospitalini kumhudumia mume wangu nilirudi na kukuta Biashara zote zishasimama, yalibaki tu malori lakini maduka yalikua hayana kitu, mume wangu hakua anajali kwania likua katika maumivu makali sana.


Niliendelea kumuuguza mume wangu peke yangu huku ndugu zake wakiwa hawataki kushiriki kabisa, kila nikiwaambia waliniambia kuwa aliyataka mwenyewe na kama ni mali alikula mwenyewe hivyo akahangaike mwenyewe. Walinichia mzigo wote na Mama yake alikua hapatikani kabisa, nilijifungua salama lakini tatizo lilikua ni kwa mwanangu. Nilijifungua mtoto wa kiume ila nilipojifungua tu mtoto alikua na kidonda mguuni. Manesi walinipa moyo na kuniambia kuwa ni kitu cha kawaida ila nilipotoka hospitalini nilishangaa kumuona Mama mkwe wangu yuko nyumbani anatusubiri.


Nilishanga akumuona, mume wangu aliniamia kuwa yeye ndiyo kamtafuta lakni sikuamini, ni kama Mama mkwe alirudi mwenyewe na kwakumuangalia nilijua lazima ana kitu, nilihisi lazima atakua na kitu kaja nacho.


“Mwanangu kaniambia nirudi maisha yamemshinda…” Aliongea huku akicheka, Mume wangu alikua na furaha sana na kila mara wakiongea kidogo walikua wanakumbatiana.


“Kesho kafungue maduka kila kitu kitakua sawa, lakini sasa hivi namtaka huyu mtoto wako.” Aliongea huku akimchukua mwanangu mchanga ambaye ndiyo kwanza alikua na siku moja.


Alimchukua kwa kumnyang’anya, sijui kwanini alifanya hivyo kwani nilikua nampa na ni mjukuu wake, lakini alipomchukua tu alikaa naye chini, aliondoa nguo nilizokua nimemfunika, huku nikiwa nawaza anataka nini, Mama mkwe wangu mbele yangu na mbele ya mume wangu, alishika kitovu cha mtoto ambacho kilikua bado hakijakatika, akakivuta kwa nguvu na kikakatika kwa kunyonfoka.


“Mama aaa! Umemuua mwanangu!” Nilipiga kelele huku nikimvamia, nilimnyag’anya mtoto wangu ambaye alikua akilia sana, alikua akivuja damu nyingi sehemu ya kitovu kwani ilikua kama vile kaking’oa.


Mume wangu alikua akimuangalia tu hakusema chochote, pamoja na kuonekana kuumia lakini alinyamaza kimya.


“Utamuua huyo mtoto mlete!” Aliniambia kuku akininyang’anya mwanangui, nilikataa katakata kumpa mwanangu lakini alimuamrisha mume wangu kunishika. Mume wangu ambaye mwanzo alikua hawezi kusimama kutokana na kidonda cha mguuni alisimama vizuri na kidonda chake, alinishuka na Mama yake akamchukua mtoto kwa nguvu, ailiingia katika mkoba wake, akachukua dawa flani, akampaka mtoto kwenye kitovu.


Alichukua kile kipande kingine cha kitovu akakiweka kwenye chupa ya maji ya Kilimanjaro ambayo alikuja nayo, akakosokomezea huko na kuifunga. Alinirudishia mtoto ambaye alishaacha kulia, baada ya kumpaka ile dawa mtoto damu zilikata kabisa. Mama mkwe alichukua mguu wa mume wangu,a kaupaka dawa ileile aliyokua kampaka mwanangu kwenye kitovu.


“Mimi ndiyo Mama yako, nimekutengeneza jinsi ulivyo, huwezi kuishi bila mimi, nimerudi kwakua nakupenda.” Mama mkwe aliongea hukua kimnyanyua mume wangu na kumkumbatia, mume wangu alibadilika kabsa, akachangamka huku akimshukuru Mama yake kwa kurudi.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU! —SEHEMU YA TISA


Mume wangu alipona na mwanangu kile kidona cha mguuni kilipona kabisa, mambo yalianza kuwa mazuri, Mama mkwe wangu alikua mpole kabisa, alibadilika kwa namna flani mpaka nikaanza kuona tena raha ya ndoa. Kama miezi sita hivi Biashara za mume wangu zilianza kwenda vizuri, niliona kila kitu kinasimama na alikua akinishirikisha kila hatua. Bila hata kumuambia mume wangu alikuja na kuniambia kuwa anataka kujenga kwetu, alikua anataka kutujengea ghorofa, nilifurahia na nilipowaambia ndugu zangu nao walifurahia na kuanza kumuona mume wangu kama Mungu flani hivi.


Nyumba ilijengwa na kuisha jambo ambalo lilizidi kunipa amani na kuanza kumpenda mume wangu. Siku moja mume wangu alierudi nyumbani akiwa amelewa, ni kitu ambacho kilikua kama kimeisha kwa muda baada ya mtoto wetu kupona na Mama yake kurudi alibadilika na kuacha pombe kabisa. Alionekana kuwa na mawazo mengi sana  kwani pamoja na kulewa lakini bado alikua akitokwa na machozi, nilishindwa kukasirika na kutaka kujua kuwa alikua na tatizo gani mpaka kuwa vile.


Bnilitaka kuongea naye lakini alikataa, aliniambia yuko sawa, hata nilipojaribu sana kumuuliza aliishia kulia tu. Mama yake alipokuja alikataa katakata kutoka ndani, alisema ameshiba na hajisikii vizuri hivyo alilala. Nilirudi chumbani na kumkuta mume wangu kalala, sikutaka kumuamsha nilipanda kitandani ili kulala lakini sikupatwa na usingizi, kwa namna nilivyomuona mume wangu alionekana kuwa katika maumivu makali sana na iliniuma sana kushindwa kujua alikua na tatizo gani.


“Mke wangu mimi bora kufa, nimchoka sana….” Ilikua ni sauti ya mume wangu, ulikua ni usiku wa manane nilijua mume wangu alikua jkashalala kumbe bado alikua macho. Nilinyanyuka kitandani na kuwasha taa ili kuongea naye, lakini alikataa, aliniambia nizime taa kwani anaona aibu kuongea na mimi huku ananiangalia usoni.


“Kuna nini mume wangu?” Nilimuuliza huku nikizima taa, nilinyanyuka kitandani na wote tukawa tumakaa, nilimkumbatia mabegani na kuwa kama nambembeleza ilia niambie kilichokua kimetokea.


“Mama mke wangu… Mama….” Aliniambia huku akivuta makamasi na kufuta machozi, alionekana kama alilia muda mrefu wakati mimi nikijua kuwa alikua kalala.


“Mama kafanya nini, mbona kama sasa hivi tuko vizuri?” Nilimuuliza kwa wasiwasi.


“Hapana, Mama hayuko sawa, mamboa nayotaka niyafanye kusema kweli mimi siwezi!” Mume wangu alilalamika, sikumuelewa nilizidi kumuuliza ili kujua ni nini? Hapo ndipo alianza kuniap stori ya maisha yake.


“Mimi nilianza kutembea nikiwa na miaka mitano, Mama yangu ndiyo alikua kila kitu katika maisha yangu, nilizaliwa nikiwa naumwa kama mtoto wetu lakini Mama hakunitupa, aliendelea kunihudumia na katika kipindi chote hicho hakuruhusu mtu yeyeote kuwa karibu na mimi. Hata Baba hakumruhusu, nilikua nikilala naye kitanda kimoja,a kiniogesha na kunifanyia kila kitu, nilipona  kipindi alipozaliwa mdogo wangu, nikawa mtoto mzuri na akili zangu, kila mtu alishangaa kwani yalikua ni mabadiliko ya ghafla.


Kitu amcbho hakikubadilika ni Mama, alikua ananipenda sana na bado alikua akilala na mimi kitanda kimoja hata nilipokua mkubwa. Kuna mambo mengi ambayo Mama alikua akinifanyia nilipokua mtoto, niliyaona yakawaida lakini baadaye nilipokua mkubwa ndiyo nilijua kuwa nimakosa kwani nilijua kuwa si sawa…” Mume angu alitulia, alishindwa kuongea na kuanza kulia.


“Naomba maji mke wangu…” Aliniambia, nililazimika kunyanyuka, nikawasha taa na kwenda kumchukulia maji sebuleni. Niliporudi ndipo nilimuona mume wangu vizuri.


Mwili ulikua mwekundu, kama umevimba, alikua kama ana damu damu usoni ambazo zilikua zimevimbiana.


“Umefanya nini? Vipi umeumia?” Nilimuuliza mume wangu huku nikimpa maji, alionekana kuwa kawaida, aliniambia kuwa hasikii chochote, nilimshika usoni kuona kama vile ana maumivu lakini hapana, alikua sawa kabisa. Alikunywa maji na kuendelea kunisimulia.


“Nilikua nikilala chumba kimoja na Mama, mara nyingi alikua akitoka chumbani kwa Baba na kuja chumbani kwangu, alikua akinilazimisha kusema kuwa naogopa kulala peke yangu. usiku mama yangu alikua akinishikashika na kuniambia kuwa nimchezee sehemu zake za siri…”


Mume wangu alinyamaza tena, aliniomba kuzima taa kwania likua anaona aibu. Kipindi hicho nilikua mdogo tu kama miaka saba, Mama alikua akinilazimisha na kweli nilikau nikisikia raha, lakini nilikua naogopa nikidhani ni kitu kibaya ila aliniambia kuwa yeye ni Mama yangu hawezi kunifundisha mambo mabaya. Niliendelea kufanya hivyo mpaka nilipokua mkubwa, nikiwa sekondari nilikua nishabalehe na nilikua nikifurahia tendo la ndoa, Mama alikua akifanya mapenzi na mimi kila siku ya juma tano na jumapili, hiyo ilikua ni lazima hata kama tulikua na mitihani mama alilazimisha.”


Mume wangu alinyamaza, ni kama alikua anasubiri niseme kitu lakini nilishindwa kuongea. Nilishajua kuwa mume wangu wana uhusiano usioeleweka na Mama yake lakini sikujua kuwa wanafanya mapenzi na tena walianza kipindi wakiwa wadogo.


“Mama hakutana niwe na mwanamke shuleni, lakini nilipofika kidato cha nne alikuja shuleni, kulikua na mwalimu mmoja mke wa mtu Mama akaniambia kuwa nitembee naye na nimpe ujauzito kwani ana nyota nzuri. Sikumuelewa kwania likua ni mwalimu wangu na nilikua hata sijawahi kumtamani achilia mbali kumtyongoza.


Lakini Mama alilazimishia, alimlipa yule mwalimu kunifundisha tution, mwalimu akawa anakuja nyumbani na sijui Mama alimfanya nini lakini mwalimu ndiyo alikuja kunitongoza na tulifanyia mapenzi nyumbani kwetu Mama akiwa sebuleni. Niliona aibu sana na kweli yule mwalimu alipata ujauzito lakini ile mimba ilimsumbua mpaka akaja kufa wakati anajifungua. Mama hakuonekana kujali aliniambia ni mipango ya Mungu lakini mimi nilihisi kuna kitu.baad aya hapo nilianza kufaulu darasani, sikua na uwezo mzuri darasani ila baada ya kifo cha yule mwalimu niligeuka na kuwa nafaulu sana.


Hata mtihani wa mwisho nilipata daraja la kwanza kitu ambcho hata mimi mwenyewe sikukitegemea. Mama aliendelea kuniambia kuwa nina akili, nilienda kidato cha tano na chasita na huko kote alikua akija kunitembelea tunalala gest wote, niliona kawaida kufanya mpaenzi na Mama yangu na kuna kipindi hata nilikua nikimuonea wivu Baba yangu kila mara nilipowaona pamoja.” Hapo mume wangu alinyamaza tena, alichukua maji na kuanza kunywa kisha akafuta  machozi na kuendelea.


“Mama yangu ana control maisha yangu sana, kila kitu ninachofanya ni lazima yeye akubali, Baba alikua hana sauri juu yake ni mara kibao Baba alitaka kumuacha Mama lakini mwisho alirudi na kumuomba msamaha. Ndugu zangu wamenitenga kwakaua wanadhani Mama ananipenda mimi zaidi, wanaona kama kuna mambo mabaya nafanya na Mama. Mimi nilikua naona kama kawaida, nilikua najisikia vizuri kwakua nilishazoea lakini sasa nimechoka, mamboa liyoniambia nifanye mimi mke wangu sitaki, kama ni hizi mali botra kuwa masikini.” Mume wangu aliongea na kunyamaza tena, nilikua na hamu sana ya kujua ni mambo gani ambayo Mama yake alimuambia.


“labda ameambiwa aniue ndiyo maana anaogopa?” Niliwaza, nilitamani kumuuliza lakini niliona nobora kumuacha afunguke.


“Hivi unajua kuwa hata wewe Mama ndiyo aliniambia nikuoe. Nilishakua na wanawake wengi lakini wote aliwakataa ila alipokuona wewe alilazimisha sana nikuoe, aliniambia kuwa wewe una nyota ya mali  na nisije kukuacha.” Aliendelea, aliniambia kuwa kila kitu tulichokua tukikifanya ilikua ni lazima Mama yake kukuabliana nacho kwanza.


“Hata siku za kufanya mapenzi na wewe ilikua ni mama ananipangia, kama ikitokea nina hamu na Mama hataki basi uume wangu unakua hausimami kabisa…”


Aliniambia na kunikumbusha kuwa ni mara nyingi sana nilitaka kufanya naye mapenzi lakini alikua hasisimkwi kabisa.Mume wangua liongea maneno mengi sana namna ambavyo mama yake alikua akimsimamai, namna ambavyo Mama yake alikua akihangaikia ili kulinda mali zake na sbabau za kipindi kile mama yaka kuondoka alitaka kumuonyesha kuwa hawezi kuishi bila yeye.


“Sada Mama kaniambia nitembee na mwanangu kweli mke wangu mimi nitembee na katoto kadogo kama kale….” Mume wangu aliongea huku akilia, kuna kitu kilipita na kunikata kwenye moyo, nilinyanyuka na kutaka kupiga kelele, nilitaka kutoka kumfuata Mama mkwe wangu lakini mume wangu alinizuia.


“Atakuua, Mama namuogopa sana…” Aliniambia huku akinishika na kuniziba mdomo, mume wangu alikua anatetemeka na kwa kumuangalia nilijua kweli kuwa anamuogopa Mama yake.


“Bora mimi kufa nyinyi muishi salama lakini siwezi kumbaka mtoto wangu, hapana nimchoka na haya mambo ya Mama.” Aliongea, nilijikuta natulia, kwa namna ambavyo Mume wangu alikua kapaniki nilijua fika kama na mimi nikipaniki basi hatutafika popote. Nilimtuliza na kumuambia kuwa kama anataka kutoka nilazima kwanza twende kwenye maombi ili wote tuombewe kwani hakuna kitu ambacho kingeweza kushindana na nguvu za giza.


Mume wangua likubali, alinisihi kutulia mpaka siku inayofuata ili kuweza kwenda kwenye maombi, alikua kadhamiria, tulipanda kitandani ili kulala. Nilipitiwa na usingizi lakinia subuhi niliamka mapema ili mimi na mume wangu wote twende kwenye maombi. Lakini nilipoamka mume wangu hakua chumbani, nilidhania liwahi kuamka nikatoka nnje na kumkuta Mama mkwe kakaa sebulani. Nilimuulizia alipokua mume wangu lakini hakutaka kuniambia, alisema tu hata yeye hajui alidhani kuwa labda kalala.


Nilitaka kutoka nnje kumuangalia, lakini kabla ya kufanya hivyo kuna kitu kiliniambia nenda chumbani kwa mtoto, nilitembea harakaharaka kwenda chumbani kwa binti yangu, nilikua na wasiwasi kwani kwa namna ambavyo Mama mkwe wangu alikua kakaa pale na namna alivyokua akiniangalia nilihisi kuwa ladima kuna kitu. Mama mkwe wangu aliniona nilivyokua nikienda, alinyanyuka na kunizuia akiniambia nisiingie huko. Tulishikana na kuanza kuvutana akisema nisiingie lakini mimi nililazimishia huku nikimuita mume wangu kwa nguvu.


“Najua uko huko ndani, toka, sio akili zako mume wangu, toka huko ndani!” Nilipiga kelele, Mama mkwe alinishika kwa nguvu lakini nilifanikiwa kumsukuma na kuuendea mlango. Nilianza kuugonga kwa nguvu na kutaka kuusukuma, lakini kabla ya kufanya hivyo mlango ulifunguliwa na mume wangu alitoka. Alikua uchi wa mnyama suruali yake kashikilia mkononi. Uume wake ulikua umesimaam, alikua kama mtu aliyechanganyikiwa, aliniangalia kwa aibu huku akisema.


“Mama Nimejaribu! Nimejaribu! Mama Nimejaribu! Nimejaribu….” Mume wangu alikua kama kachanganyikiwa, nilimuacha na kukimbilia mpaka ndani, mwanangu alikua kalala kitandani hajitambui, nilimshika kujaribu kumuamsha lakinia likua haamki.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU!—SEHEMU YA KUMI


“Mama nimejaribu imeshindikana, haisimami!” mume wangu alipiga kelele kama chizi huku akimpigia magoti Mama yake, Mama yake alikua akimtukana na kunishutumu mimi kuwa ndiyo namharibia mtoto wake. Mwanangu alikua bado kalala chini, nilijaribu kumuamsha lakini alikua haamki, alikua kama kapoteza gahamu, nilimkagua sehemu zake za siri nakuona kama hajaguswa.


“Sikamgusa mke wangu, nimeshindwa! Haisimami Mama!” Mume wangu alizidi kupiga kelele. Nilinyanyuka na kumfuata Mama mkwe, nilimkunja na kutaka kumpiga.


“Umemuua mwanangu, nitakuonyesha sasa! Kama una ushetani wako basi malizia kwa mwanao lakini si wangu!” Nilitukana huku tukishikana na kuanza kutupiana makonde, tulipigana kweli wkeli huku kila mmoja akimtukana mwenzake. Mume wangu alikua kakaa tu kwenye kochi uchi wa mnyama kama mtu ambaye hajitambui, hakuingilia chochote alikua akituangalia kama vile haoni kilichokua kikiendelea. Aliishia tu kupiga kelele kuwa ameshindwa maejaribu kumuingilia mwenetu lakini haikuwezekana.


“Nanitakufunga mshenzi mkubwa wewe! mauachawi yako malizia huko huko kwa wanao mpumbavu wewe!” Nilimuambia huku nikimsukuma chini, alidondokea kwenye sakafu akiwa hoi, hakuweza hatya kusimama, nikiwa na hasira zangu nilimfuata mume wangu pale alipokua kakaa na kumtandika makofi mawili nikampa suruali yake na kumuambia avae nguo kabla watu hawajamuona. Bado alikua hajilewi elewi hivyo alizivaa kwakua nimemuambia lakini nilimuona kama vile akili zake haziko sawa.


Siku ile ilikua mwisho wangu wa kuishi pale, nilijua kabisa Mama mkwe wangu ana nguvu kubwa sana kwa mume wangu na kama ningebaki pale basi angeniharibia watoto. Niliwapigia ndugu zake na mume wangu lakini hakuna hata mmoja aliyetaka kunisikiliza. Pamoja na kuwaambia kilichokua kimetokea lakini hawakutaka kuingilia.


“Wakati mnakula pesa zenu kwanini hamkutushirikisha, mambo yamekua mabaya ndiyo unajifanya kuona kama una ndugu.” Walinijibu na kunikatia simu, ilikua ni lazima kuondoka na kwakua nilikua bado naweza kwenda dukani na nilishakua na akiba yangu nilipanga kuondoka siku ileile.


Nilirudi kumuangalia mwanangu, alikua bado kalala, nilimuuliza mume wangu kama kamfanya nini akajibu kuwa ni dawa ya usingizi ataamka. Nilimkubalia lakini bado nilikua na wasiwasi, nilimchukua mwanangu mpaka chumbani kwetu, mume wangu alifuata nyuma akiniomba msamaha. Pamoja na kuomba msamaha lakini alionekana kama hayuko sawa, nilihisi lazima kuna kitu Mama yake alimpa kwani jana yake alikua mzima na alikua ni binadamu ila kwa wakati ule nilimuona kama shateni.


“Kwanini umefanya hivyo? Jana si tuliongea kuhusu hichi kitu?” Nilimuuliza lakini hakujibu, alikaa kimya akiniangalia tu, mara kadhaa alileta utani wa kijinga kama kuniambia kuwa nimependeza na mara nyingine kuongea mambo ambayo kiuhalisia yanakua hayahusiani na nilichokua nimemuuliza.


“Hili paa inabidi tubadilishe, tuweke Msouth nyumba itapendeza…” Aliongea mambo ya ajabu ajabu, nilimuambia kuwa mimi naondoka na kumuacha na Mama yake.


“Kweli ukirudi hakikisha unaniletea Icecream, nina njaa sana naziopenda.” Mume wangu aliongea, nilijaribu kumuelewesha kuwa nilikua namuacha na nisingerudi tena lakini hakuonekana kuwa sawa.


“Ukiniacha sasa mimi nitalala na nani? Mimi naogopa kulala peke yangu, Mama kasema kuwa halali tena na mimi eti ni mkorofi…” Aliongea.


“Mume wangu uko sawa kweli….” Nilimuuliza kwa wasiwasi, alianza kuongea mambo ya kitoto.


“NIkuambia kitu, Mama anasema kuwa kadudu kangu kamekua kakubwa, hembu angalia…” Aliongea huku akivua suruali na kunionyesha uume wake.


“Mimi Mama ananichezeaga, akinioogesha ananichezeaaa kanakua kagumuuuu…” Mwanzo nilihisi labda ananichezea akili zangu, nilikusanya nguo zangu pamoja na za watoto na kumuambia kua naondoka.


“Namimi nataka kwenda shule, mimi nataka kusoma, mbona wenzangu wote wanaenda, na mimi naenda…, Mamama! Mamaam! Wananiacha, mimi nataka kwenda shule….” Alipiga kelele huku akitoka kumfuata Mama yake. Nilikua na wasiwasi kidogo kuhusiana na akili yake lakini nilishadhamiria kuondoka. Wakati huo mwananguamlikua kashaamka na alikua vizuri, hakujua kilichokua kinaendelea, alinishangaa nilipokua nakusanya nguo zake nikamuambia kuwa tunaondoka tunasafiri. Nilitka na kumkuta Mama mkwe wangu kakaa sebuleni, nilimuaga kwa dharau na kumuambia kuwa naondoka tena na watoto wangu.


Aliniangalia kwa dharau na kucheka kisha akaniambia.


“Ukiondoka hakikisha kuwa unaondoka na watoto wako wote, kuna mwingine huko nnje anachezea matope ondoka naye. Ungetoka ukamuona kwanza kabla ya kutoka na hao wengine.” Nilimsonya kwa dharau na kutoka nnje ili huku nikiwaacha wanangu wawili ndani, nilichokiona kilinishangaza, mume wangu alikua kavua nguo, kajisaidia kwenye majani na alikua akichezea kinyesi chake. Alijipaka kinyesi mwili mzima. Harakaharaka niliwarudisha watoto ndani na kuwafungia, sikutaka wamuone Baba yao katika hali ile, nilirudi na kumfuata Mama mkwe.


“Umemfanya nini mume wangu? Niambie umemfanya nini mume wangu?” Nilimkunja tena Mama mkwe kutaka kumpiga, alkini yeye hakunigusa, aliishia kucheka kwa dharau huku akiniambia kuwa si nilikua na haraka ya kuondoka basi niondoke.


“Mimi narudi kulala zangu nina usingizi jana sikulala kabisa, ukiondoka funga mlango, hakikisha unamchukua huyo taahira wako hapo nnje, si alijifanya kukuambia kila kitu sasa si umejua, ndiyo mali zilivyopatikana mchukue basi uchukue na mali zake!” Mama mkwe aliongea kwa dharau na kuingia chumbani kwake, alifunga mlango na hata nilipogonga hakutoka tena.


Nilitoka nnje kumuangalia mume wangu, alikua kama mtoto mchanga ambaye hajitambui, nilienda na kuchukua ndoo ya maji. Nilimwagia ndipo alizinduka kidogo, akili zake zilirudi.


“Wewe mshenzi nini, mbona unanimwagia maki?” Aliniuliza hukua kinifuata na kutaka kunipiga.


“Wewe huoni ulichokifanya, hivi huoni kabisa, unaumwa au unanifanyia makusudi?” Nilimuuliza huku nikimuonyesha namna alivyokua kajisaidia na kujipaka kinyesi.


“Nani kajisaidia hapo, nilishakuambia kuwa hawa watoto sitaki kuwaona kwenye majani yangu bila Pampas, unaona sasa!” Alifoka kwa hasira alipoona kinyesi chake kwenye majani.


Nilimuambia ajiangalie kwania likua hajavaa nguo, kujiona vile alinywea taratibu na kukaa chini.


“Nimefanya nini?” Aliniuliza, nilimuangalia bila kuwa na majibu ya kumpa. Alikaa chini na kujikunyata. Aliona mabegi ambayo nilishayatoa nnje wakati najibizana na Mama mkwe kutaka kuondoka.


“Unataka kuondoka, unataka kuniacha peke yangu, mimi naogopa, usiondoke! Usiondoke! Mimi wenzangu kila siku mnasafiri mnaniacha, mimi nabaki peke yangu, usiondoke.” Alianza kulia huku akinifuata na kunikumbatia, niliona kama kaurudia utoto tena, nilimuambia siondoki, nikaingia ndani nikatoa shuka na kumfuta kisha nikamuambia aende bafuni kuoga mimi nikabaki kusafisha pale nnje.


****


Nilitamani sana kuondoka na kumuacha mume wangu lakini sikuweza,  kwa hali aliyokua nayo nisingeweza kuondoka naye pia. Kila siku hali yake ilizidi kuwa mbaya, alikua akirudia utoto na kufanya mambo ya kijinga kijinga. Ilinibidi kumsaidia kusimamia Biashara na ili kumlinda mtoto wangu wakike kwani nilikua sijui ni kitu gani Mama mkwe anaweza kukifanya nilimpeleka bweni hivyo kubaki nyumbani na mtoto wangu mdogo ambaye hata hivyo nilikua nikiongozana naye kila sehemu.


Mume wangu alihitaji uangalizi kama mtoto mdogo, dakika mbili alikua sawa na kuwa mtu mzima lakini dakika mbili nyingine alikua kama mtoto akijisaidia na kujikojolea huku akiongea na kudeka kama mtoto. Mama mkwe wangu aliendelea kubaki pale, hakua akitoka kwenda popote hata kuhusu Biashara hakua akijishughulisha ni kama aliniachia kila kitu mimi mwenyewe. Nilivumilia ile hali nikashindwa, siku moja niliamua kumchukua mume wangu na kumpeleka kwenye maombi, alienda kuombewa na kuombewa lakini sikuona kitu.


Niliendelea na maombi kwa mwezi mmoja hivi, nilikua nikibadilisha wachungaji lakini sikuona hali ya mume wangu kubadilika. Lakini Biashara zilikua zinaenda vizuri, wateja walikua wengi na pesa ilikua ikiingia nyinyi tu. Siku moja nilirudi nyumbani nikiwa nimechelewa, nilikua bize na kufunga mahesabu kwani wateja walikua wengi sana, nilifika na kukuta Mama mkwe wangu ameshalala, niliingia chumbani kumuangalia mume wangu lakini hakuepo, nilizunguka zunguka kumuangalia vyumba vyote sikumuona.


Nilitoka na kwenda kumgongea mlango Mama mkwe wengu, aliniambia nimtafute huko nnje kwani ni muda sana alitoka, hakuonekana kujali kama mtoto wake haonekani. Nilitoka kumuangalia mume wangu na kumkuta kalala kwenye majani. Nilimnyanyua ili twenda ndani lakinia likua hanyanyuki.


“Mke wangu nimeshindwa kusimama….” Aliniambia kwa upole, kwa namna alivyokua akiongea nilijua kabisa kuwa utoto ulishaisha na mtu niliyekua nikiongea naye alikua ni mume wangu ambaye ni mtu mzima.


“Tangu mchana najaribu kusimama lakini miguu mizito.” Aliongea hukua kijitahisi kujiheuza, alikua kalala chali miguu kainyoohsa, alisimika mikono yake chini na kusogeza tena miguu lakini haikusogea.


“Mke wangu kuna nini mbona miguu yangu haisogei?” Aliniuliza, nilikua nimenyamaza kidogo nikisikilizia kitu, nilisikia kitu kama harufu, kwakua nilishamzoea nilihisi labda kama kajisaidia.


“Unasikia harufu?” nilimuuliza, alitingisha kichwa hukua kiniambia hapana, nilimuuliza tena kwa mara ya pili huku nikipepesa macho kuangalia kwani mwanaga wa taa ulikua ukitupiga.


“Utakua umejisaidia wewe!” Niliongea kwa hasira kidogo, pamoja na kufahamu matatizo yake lakini kuna wakati ile hali ilinikera.


“Kujisaidia? Mimi ni mtu mzima mbona unanikosea heshima, nimeshindwa kunyanyuka lakini nina akili kujua kuwa hapa ni nnje siwezi kujisaidia hapa!” Aliongea kwa hasira huku akijaribu tena kujinyanyua lakini alishindwa, sikutaka kubishana naye, nilisikiliza lakini ile haikua harufu ya kitu kinyeshi, ilikua ni harufu kama ya nyama zinaungua.


“Mama atakua aliunguza nyama.” Nilijisemea huku nikimshika kujaribu kumnyanyua, alikua mzito sana sikuweza kumnyanyua nilimuachia.


“Kuna nini, miguu imefanya nini?” Nilimuuliza huku nikimshika miguu yake, nilitegemea atashituka lakini hakukua na kitu.


“Mbona hushtuki nikikugusa, unasikia ninavyokugusa?” Nilimuuliza.


“hapana, hembu gusa tena, sisikii chochote!” Alijibu sasa kwa kupaniki kwani kweli nilikua nikimbonyeza bonyesa miguu yake lakini hakusikia.


“Bonmyeza  kwa nguvu, Mbona sisikii chocchote!” Alipiga kelele, mimi niliendelea kubvonyeza miguu yake huku nikipanda juu mpaka kiunoni kuona kama alikua kapooza mpaka wapi.


Mpaka nafika kiunoni alikua hajihisi chochote, nilishika tena miguu na kuionyeza mara nikasikia “Pofuuuu!” Kidole kilizama kwenye kigimbi cha mguu wakati nambonyeza.


“Mamaaaa!” nilijikuta napiga keleel, nilikua nimeungua, ilikua ni kama nimeingiza kidole changu kwenye chungu cha mafuta.


“Nini? Nini? Mbona unapiga kele, kuna nini?” Mume wangu aliniuliza, nilishindwa kuelewa, nilikipaka kidole mate kwa kukitemea, lakini kilipofika usoni kwangu niliona kama vile kimeshika uchafu, sikujua ni wanini lakini uliganidana.


Nilimvua mume wangu suruali harakaharaka ili kuangalia, kwenye ile sehemu niliyokua nimemshika kulikua na shimo na lilikua linatoa moshi. Kwakuangalia ni kama nyama za ndani zilikua zikiungua. Nilimuuliza kama hasikii maumivu akanijibu hasikii chochote. Nilinyamaza sikutaka kumuonyesha kuwa nimepaniki, bado nilikua sijajua nini kilikua kimetokea. Nilijaribu tena kumnyanyua nikashindwa, nikaingia ndani na kumuambia Mama yake, nilimuomba kuja kunisaidia kumuingiza ndani, sikutarajia kama atakubali lakini alikubali nikamuingiza mpaka chumbani tukamlaza kitandani.


Mama mkwe alitoka na kutuacha pale ndnai, nilichukua simu na kumpigia Kaka mmoja ili kuja kunisaidia kumbeba mume wangu, alikua ni mmoja wawafanyakazi wa duani kwetu ambaye alishayaona baadhi ya mambo na kuamua kuondoka. Sikua nimemuambia kila kitu lakini kidogo alikua akifahamu baadhi ya vitu hivyo nilijua kama nikimuambia anaweza kunisaidia, ni mara kadhaa alishakutana na mume wangu mtaani akiwa kama chizi na kumleta nyumbani bila kumtangaza.


Nilimuambia kuwa nyumbani kuna tatizo mume wangu anahitaji kupelekwa hospitali, lile tundu mguuni bado lilikua linatoa moshi na ukichungulia kulikua kama kuna vitu vinachemka huko.


“Kuna nini mke wangu?” Mume wangu aliniuliza kwani aliona tu moshi na tundu lakini hakuweza kuona kilichokua ndani. Yule Kaka alikuja nilimuambia mume wangu tunatakiwa kumpeleka hospitalini, alikubali lakini huko nako walitumbia hawawezi tumpeleke muhimbili. Wakati tukiwa njiani ndipo yule Kaka aliniambia.


“Shemeji lakini unajua tunapoteza muda, hii si kitu ya hospitalini? Hapa anahitaji maombi!” Aliniambia, wakati huo mume wangu alikua kapitiwa na usingizi, nilikubaliana naye.


Tuligeuza gari mpaka kwa mchungaji mmoja, aliombewa sana lakini haikusaidia, yule Kaka aliniambia kama ni Mama yake anafanya hivyo vitu basi nimpelekee mtoto wake kisha niondoke kama nikumuua amuue yeye. Ilikua ni kama asubuhi, usiku mzima tulikesha na maombi lakini mume wangu hakupata nafuu, zaidi alikua akianza kupata maumivu na kulia. Alilia sana kwenye gari, tulifika nyumbani, nikamuamsha Mama yake na kumtukana huku nikimuambia achukue mtoto wake kwani nimechoka kuhangaika naye.


“Huyu wala bado hajaumwa, si alijifanya mjanja akafikiri natania, nimemuambi akamchukue mtoto wake Boarding hataki! Kama unataka mume wako apone mlete binti yako hapa tukae naye hivi atakuja kukufia na kila kitu kitahamia kwako!….” Mama mkwe aliongea kwa hasira mpaka niliogopa.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU—SEHEMU YA KUMI NA MOJA


Nilijua kabisa kuwa sababu ya Mama mkwe wangu kutaka mwanangu kurudi nyumbani ni kwakua alitaka mume wangu kumuingilia kimwili. Nilijua kuwa kaiteka akili ya mume wangu na kama ningekubaliana na kile kitu basi ningempoteza mwanangu.


“Chagua kati ya mumeo na mwanao, mwanaume anakufa hivyo!” Mama mkwe aliniambia, nilimuangalia Mama mkwe kwa hasira, nilimuona kama mnyama, ni Mama gani ambaye anmgeruhusi mwanae kuteseka namna ile kwasababu tu ya mali.


“Nimewachangua wanangu, huyu ni mtoto wako, ni uamuzi wako kumlinda au kuendelea kumtesa!” Nilimuambia Mama mkwe kwa hasira huku nikiingia ndani, nilikusanya kilichokua changu na kumchukua mwanangu mdogo na kuondoka. Mume wangu alikua katika maumivu makali lakini nilijua fika kamwe Mama yake asingeweza kumuacha akafa, nilijua suluhu pekee kwa mimi kumponya mume wangu ilikua ni kuondoka pale nyumbani mimi na wanangu.


Wakati naondoka mume wangu alikua akilia kama mtoto, alilia kutokana na maumivu na pia kwasababu ya kuondoka kwangu. Alikua akiniomba sana kubaki na kama ni kuondoka basi niondoke naye.


“Nakupenda sana mke wangu, humu nitakufa naomba unichukue….” Mume wangu alipiga kelele, nilimuonea sana huruma kwani baada ya kuniambia kisa chake nilijua kuwa mume wangu hakua mtu katili bali aliharibiwa na Mama yake kipindi akiwa mdogo. Lakini nilijua kuwa ili kumsaidia ilikua ni lazima mimi kumuacha na kuondoka zangu kwani asingeweza niliamini kuwa Mama yake aisingeweza kumfanya kitu chochote.


Nilitoka na kumuacha mume wangu akilia, lakini Mama yake alimtuliza kwa kumuambia.


“Hafiki popote huyo, atarudi mwenyewe kwa kupiga magoti akilia kukuomba msamaha.” Aliongea kwa sauti ya juu akihakikisha kuwa nimesikia, alikua akiniambia mimi kwani alihakikisha kabisa kuwa nasikia. Sikumjali, nilishachoshwa na vitisho vyake hivyo nilitaka kuondoka tu na kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine. Ingawa sikua nimepanga kuondoka siku hiyo lakini tayari nilishajipanga.


Suala la kuondoka nilishaliwaza kabla hivyo nilishaanza machakato wa kutafuta chumba, mwanzo sikutaka kubaki dar ila kutonana na mwanangu kuwa shule niliona kuwa hata kama yuko bweni lakini nahitajika kuwakaribu naye kwani kwa nilivyokua nikimfahamu Mama mkwe basi angeweza kumfanyia chochote. Bila mimi kuwa karibu angeweza kumrubuni mume wangu na kumchukua mtoto, nilitafuta nyumba karibu na shule aliyokua akisoma mtoto wangu ili kuwa karibu naye.


Lakini hata sikufika nilipokua naenda, nilipigiwa simu kuwa mtoto wangu kadondoka shuleni. Nilikimbia harakaharaka, ilikua ni kama masaa mawili tu tangu mimi kuondoka nyumbani kwani kuna sehemu nilipitia kununua baadhi ya vitu kwakua niliondoka ghafla. Nilifika lakini cha ajabu nilimkuta Mama mkwe wangu kashafika.


“Walimpigia simu  Baba yake lakini kashindwa kuja nimekuja mimi….” Mama mkwe alisema, mtoto alidondoka akiwa darasani, alikua kaa kwenye kiti na kudondoka, walipomchukua na kumpeleka kwenye zahanati ya shule alikua sawa.


Lakini alikua akipig akelele kuwa anamtaka Baba yake, anataka kuonana na Baba yake hivyo apelekwe nyumbani. Kuona hivyo ndipo walilazimika kumpigia simu mume wangu, lakini aliyeenda alikua ni Mama mkwe, kutokana na sheria za shule asingeweza kupewa mtoto na kuondoka naye. Mimi na mume wangu ndiyo watu pekee ambao tuliandikishwa hivyo alipoenda na kujitambulisha hawakumtambua, ingawa mtoto alimtambua kama Bibi yake na kutaka kuondoka na yeye walilazimika kunipigia mimi simu ili kufanya maamuzi kwani mume wangu alikua hawezi.


Nilifika na kuwaambia kuwa mimi ndiyo Mama yake na wmanangu hawezi kuondoka na mtu mwingine zaidi yangu, Mama mkwe wangu alitulia tuli.


“Kama kafika Mama yake hakuna shida, muacheni aondoke naye.” Alisema kwa upole, walimu walikubali lakini walitushauri kumpeleka hospitali kubwa kwani kwa namna alivyodondoka ingawa alionekana anaendelea vizuri lakini alihitaji vipimo zaidi, mimi nilikubali lakini Mama mkwe wangu aliniita pembeni na kuniambia.


“Anahiitaji kumuona Baba yake, nimeshasema hawa wanapaswa kuwa pamoja, kama hutaki mmoja ni lazima tuzike na nikuambie tu mimi siwezi kuzika mtoto wangu!”


Nilimpuuza na kumuambia kuwa hata mimi siko tayari kumzika Mwanangu hivyo kama ananitishia basi anapoteza muda, nilimchukua mwanangu na kuondoka naye tukielekea hospitali kwa kupewa gari ya shule. Nilimuacha Mama mkwe pale lakini bado alikua akinisisitiza kuwa yule mtoto hahitaji kulelekwa kokote zaidi ya kumuona Baba yake, mimi nilikataa katakata. Nilikua na hasira sana, namna tulivyokua tunabishana kuila mtu alijua lazima kuna kitu.


“Dada uko sawa na Mama yako?” Nesi aliniuliza, sikumjibu chochote zaidi ya kumuangalia kama vile nakuambia hayakuhusu, nahisi alielewa na hakuuliza tena.


Lakini tukiwa njiani mwanangu alianza kulalamika,.


“Mama nasikia kukojoa…” Mwanzo niliona kama ni kitu cha kawaida, nilikua namuambia vumilia tufike Hospitalini atakojoa lakini aliendelea kupiga kelele hukua kisema kuwa hawezi kuvumilia.


“Mama nimeshindwa naumia Mama, tumbo linauma!” Aliendelea kupiga kelele, nilimuomba dereva kusimamisha gari ili angalau tutafute sehemu ya akakojoe. Lakini kabla ya kusimamisha mwanangu alishajikojolea na haukua mkojo wa kawaida, nguo yote ilikua imeloa damu kama zile za bleed ambazo hutoka mwanamke akiwa katika siku zake lakini hizi zilikua nyingi sana.


“Mama nini? Mbona natoa damu?” Alianza kupige kelel, nilimvua nguo alizokua amevaa na kumuangalia alikua akivuja damu nyingi kutoka sehemu za siri. Pia alikua akilalamika maumivu makali tumboni, alishindwa hata kukaa vizuri, alishindwa kusimama aliishia kupiga kelele. Wote tulibaki tunashangaa kwani alikua  mdogo sana, hata miaka kumi alikua hajafikisha lakini alikua anaonyesha dalili zote za kupata heshi. Ililazimika kutoka kwenda hospitalini, lakini tulipofika tu ile heshi ilikata nha kuwa sawa kabisa.


Walimpima na kusema hakua na chochote ingawa kweli ile damu ilikua ni damu ya hedhi. Alikaa hospitalini usiku mzima kwa uangalizi kisha wakaturuhusu kurudi nyumbani. Nyumbani nilikua na mawazo mengi sana kwani nilijua kuwa yale yalikua ni mapambano ya Mama mkwe wangu na kwa bahati mbaya sana alianza kwa kuwagusa wanangu, ni kitu ambacho nilikitegemea hivyo nilimpeleka mtoto kwenye maombi kama vile kumkinga. Nilikaa kwa siku mbili kumuangalia mwanangu nilipoona kuwa yuko sawa nilitaka kumrudisha shuleni.


Lakini kabla ya kufanya hivyo alianza kulalamika tena tumbo, lilikua likikata sana akawa anapiga kelele na sasa hivi alikua akitokwa na vitu ukeni, hazikua damu tena bali vitu vyyeusi ambavyo vilikua vikitoka kama mabonge mabonge. Nilimuita mchungaji kumuombea, aliomba sana lakini vitu havikutulia, hali ilizidi kuwa mbaya.


“Mama nitakufa nipeleke kumuona Baba yangu…” Mwanangu aliniambia, nilimuangalia kwa huruma nikamuambia hapana, hahitaji kumuona Baba yake bali anahitaji maombi zaidi. Tuliendelea na maombi mpaka usiku lakini haikusaidia, aliendelea kupige kelele kuwa anamhitaji Baba yake.


Maombo ni kama yalitibua kitu katika mwili wake, alianza kuwa kama mtu mwenye mashehtani hivyo kuwa anapiga kelele za kuomba msaada ambao sikuuelewa. Aliishia kumtaja Baba yake,a liweweseka sana, siku nzima hakula chochote na wala hakupumzika, ilifikia hatua mpaka mchungaji akasema kuwa kashindwa na kama inawezekana apelekwe kwa Baba yake. Huku nikiwa najua nini kinaenda kutokea niliamua kumpeleke, nilifanya hivyo kwakua niliona kama mwanangu atakufa.


“Kama anambaka basi ambake ni mtoto wake!” Nilijiongelesha, nilishajua nguvu niliyokua nikipambana nayo ni ya giza hivyo hospitali haziwezi kusaidia.


“Nilikuambia watarudi wenyewe…” Mama mkwe wangu aliongea baada ya sisi kuingia. Mume wangu alikua kalaala chumbani, hali yake ilizidi kuwa mbaya, alikua kapooza mwili mzima kalala, mwili ulikua na matobo matobo na alikua kama anatoa mwoshi.


“Hakuna mtu wa kumdhuru mwanao, kuna maagano  na Baba yake, nyie mlikuja kwangu kutaka mtoto nikawapa, kulikua na maagano na Mungu ambayo bila kutimizwa wote hawawezi kuwa na amani, hakuna kitu kibaya kitakachotokea.” Mama mkwe aliongea huku akilazimisha tabasamu.


Alimuambia mume wangu kunyanyuka kumuona mtoto wake kwani kaja kumuona, lakini kwa hali aliyokua nayo aligeuza tu kichwa kutuangalia. Mume wangu alikua akchoka sana, nuru imepotea na alikua kama mtu aliyekata yamaa.


“Mama naomba kuongea na mke wangu…” Aliamrisha, Mama mkwe mwanzo alikataa na kutaka kunifukuza akiniambia kuwa nishamleta mtoto niondoke lakini mume wangu alisisitiza kuongea na mimi peke yetu. Hakua na namna aliruruhusu, Mama mkwe alitoka nnje. Mume wangfu aliniambia nisogee karibu kwania likua akiamini kuwa Mama mkwe anasikiliza kila kitu na hakutaka Mama yake kusikia chochote.


“Kwanini umerudi, mimi nishakufa ondoka na watoto kimbilia mbali kabisa, msijali kuhusu Mimi, mama nimuuaji atawamaliza….” Alijaribu kunonng’ona lakini kabla hata sijamjibu na kumuambia kilichotokea Mama mkwe aliingia.


“Mnajisumbua bure, mimi si sheteni kama mnavyonifikiria, haya ni maagano yenu na Mungu na si mimi. Ulitaka mtoto ulitaka mali, wote mlishiriki hivyo hamuwezi kukwepa. Kama unataka kuondoka na mwanao basi ondoka lakini jua kuwa mmoja kati yetu ni lazima atamzika mtoto wake na mimi siko tayari kumzika wakwangu.” Mama mkwe aliongea hukua kaifungua mlango kuturuhusu.


Nikikumbuka hali aliyokua nayo mwanangu nilishindwa kuondoka, nilijua fika kuwa siwezi kufika mbali angweza kudondoka na kufia njiani. Akili ilisimama kufanya kazi, nilitamani mtu yeyote kuja na kuniambia kuwa nifanye kitu flani ili kila kitu kiishe. Nilikua naumia kwani nilikua na machaguo mawili, kuondoka na kumuacha mwanangu kuendelea kuteseka na maradhi au kumuacha mwanangu kufanya mapenzi na Baba yake mzazi. Nililia sana, nikapiga magoti kumbembeleza Mama mkwe wangu kunisamehe na kama ni dhabu kunipa mimi lakini hakuonekana kujali, wakati wote alisisitiza kuwa si yeye bali ni maagano yetu na Mungu.


Nilimuambia mume wangu kuwa siwezi kuondoka, ulikua ni uamizi mgumu sana kwangu kwani nilijua sababu ya mume wangu kutaka niondoke kwani alikua hataki kufanya chochote na mtoto wake lakini sikua na namna. Nilimuambia kuwa siondoke, mume wangu alinibembeleza huku akilai, kwa kuaangalia uso wake alikua katika uchungu mkubwa sana, alilia sana lakini sikua na namna, nilimuambia kuwa siwezi kumuacha katika hali ile. Nilitoka nnje huku nikilia, hali ya mwanangu bado ilikua mbaya, alikuakachoka hawezi hata kunyanyua mkono ingawa aliweza kupepesa macho na kuongea kwa shida.


“Mama kwani nimemkosea nini Mungu, mbona mimi nateseka hivi?” Aliniuliza wakati nikijaribu kumlisaha, nilimuangalia na kuona kabisa kama kashakataa tamaa, bila kujijua machozi yalianza kunitoka.


“Usilie Mama, nilikua tu nakutania hata siteseki, usilie Mama…” pamoja na hali yake mbaya lakini aliku akinionea mimi huruma. Kitu amacho nilikigundua baada ya mtoto wangu kupona na kuwa mtoto wa kawaida nikuwa alikua na akili nyingi sana, wakati mwanzo kila mtu alimuona kama hana akili kutokana na ulemavu wake lakini abada ya kupona ndipo niligundua kuwa alikua na akili.


Alikua akijua kila kitu kilichotokea wakati akiwa mdogo, mambo tuliyokua tukiongea na jinsi nilivyokua nikimpigania.


“Najua Baba hanipendi lakini mimi sitakia fe Baba anaumwa sana Bibi anasema kuwa mimi nikikaa na Baba basi hatakufa…” Aliniambia, alikumbuka mambo ambayo Baba yake alikua akimfanyia kipindi anaumwa, namna alivyopkua akimueweka kwenye Box na kumuacha dukania kipigwa na vumbi la simenti, namna alivyokua akimtukana na namna alivyokua akinipiga mara kwa mara hukua kimtukana yeye na kumuona kama mzigo, mambo yote hayo alikua akiyajua na yalikua yakimuumiza.


Nilijaribu kumbembeleza na kumuambia kuwa atapona na atakua sawa, nilijaribu kumuambia namna Baba yake alivyokua anampenda lakini aliniitkia tu ili kujisikia vizuri. Nilijitahidi kumlisha na yeye mwenyewe alijitahidi kula, alikua anajilazimishia kwania litaka kujisikia vizuri kwa ajili yangu. Kila wakati alikua akiniambia kuwa yeye yuko sawa hivyo nisilie. Nilijikaza sana lakini machozi yalikua yanatoka yenyewe na kila wakati mwanangu alinibembeleza akiniambia kuwa yeye yuko sawa na haumwi popote.


Nilimaliza kumlisha na kutoka nnje, niliongea na Mama mkwe nikiwa nimetulia akaniambia kuwa ni maagano, aliniambia hakuna kitu kibaya hvyo nisiogope. Nilirudi chumbani kwetu, mume wangu alikua hajalala, muda wote alikua akilia.


“Usiruhusu hiki kitu kutokea, mimi siwezi kufanya mapenzi na toto wangu!” Aliniambia huku akiniomba sana nimuondoe mtoto. Nilimuelewa lakini nilimuambia hali halisi, nilimuambia kilichoklua kimetokea baada ya kuondoka na mtoto, nilimuambia hali yake na kumuambia maneno ya Mama yake, alinisikiliza lakini hakutaka kuamini, hakua tayari kufanya kile kitu.


“Naamini kuna njia mke wangu, inabidi mimi kujitoa kwaajili ya wanangu, mimi ndiyo tatizo nisipokuepo nina uhakika Mama hatahangaika na nyie….”Alitulia kidogo, aliniomba nimsaidie kitu na kuniambia kabisa niape kuwa nitakifanya.


“Niambie kwanza ni kitu gani?” Nilimuuliza lakini alikataa mpaka nilipoapa kuwa nitamsaidia kukifanya ndipo aliniambia.


“Mimi nikifa hakutakua na mtu wa kufanya mapenzi na mtoto, kwa hali niliyonayo siwezi kupona, nilipo hapa siwezi kunyanyuka, ningeweza ningefanya mwenyewe ila sasa hivi naweza geuza kichwa tu, nataka ukanunue sumu ya panya, niwekee kwenye chakula nataka kufa taratibu, nikifa mwanangu atapona…. Siwezi kufanya mapenzi na mtoto wangu” Mume wangu aliongea huku akinikazia macho kwa msisitizo.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU—SEHEMU YA KUMI NA MBILI


Ilikua siku ngumu sana kwangu, ulikua ni mtihani mkubwa sana kwangu mimi. Mume wangu alikua amanaanisha, alishakata tamaa na aliniambia kabisa kuwa kachoka kuishi.


“Nimeteseka sana mke wangu, nimekua nikifanya mapenzi na Mama yangu mzazi tangu nikiwa mdogo, sijawahi kuwa mtoto, mateso ya kumuingilia mzazi wako ni makubwa sana, sitaki kumuingilia mwanangu lakini nafahamu kama nikiendelea kuwa hai basi Mama ana nguvu kubwa, Baba mpaka anakufa alishindwa kunitetea, alishajaribu sana lakini alishindwa, sidhani kama naweza kupambana na Mama.”


Alitulia kidogo na kuniangalia kwa kunikodolea macho, pamoja na kuchoka sana lakini mume wangu alikua akimaanisha.


“Kuna siku nikiwa mdogo Baba alikuja chumbani, alinikuta nipo kifuani kwa Mama, nilijua Baba ataniua lakini Mama aliniambia kuwa niendelee tu hakuna shida, baba alituangalia tunafanya mapenzi mpaka tunamaliza, hakusema chochote na hakuwahi hata kunigombeza, nilijisikia vibaya sana, kila siku nilikua natamani kumuomba msamaha lakini Mama alinikataza na kuniambia kuwa nilikua sifanyi kitu kibaya, nilikua hivyo nikijichukia na nilijikuta nachukia hata ndugu zangu. Sitaki mwanangu aishi hivyo!”


Mume wangu alikua akiongea kwa huzuni sana. “Siku ile nilitaka kumbaka mtoto wangu, hazikua akili zangu kwani wakati nataka kufanya kile kitendo nilikua nahisi kama kuna mtu ananikaba, nilikua nakosa pumzi na njia pekee ya kupumua ilikua ni kumbaka mwanangu, nilikuja kuzinduka baadaye lakini nilishakosea, hapana, mimi naumwa na najua siku moja nitakufa, sitaki mwanangu kuja kunichukia kama alivyokua akinichukia Baba yangu, au jinsi ninavyomchukia Mama yangu, sitaki kabisakumuachia makovu, mwanangu bado mdogo hakuna kiwango cha mali ambacho kitanipa furaha….”


Lakini kabla ya kumalizia kuongea mlango ulifunguliwa, Mama mkwe aliingia, wote tulinyamaza, alimsogelea mume wangu na kumshika kisogoni kana kwamba alikua akimuangalia kama ana homa au la, aliniangalia kwa dhihaka huku akitabasamu na aliniambia.


“Nilijua tu mwanangu hawezi kunisaliti, nimemlea mwenyewe kwanini anisaliti. Unafikiri yote hayo aliyokua anakuambia alikua amanaanisha, hapana, alikuahamaanishi alikua anakudanganya tu lakini mwanangu hawezi kunisaliti.” Aliongea na kumfunga mume wangu macho kama vile alikua amekufa na alikua anamfunga, mume wangu alifunga macho na kutulia tuli, Mama mkwe alimuacha na kutoka nnje, nilijaribu kumuamsha mume wangu lakini hakuamka.


Kuona vile nilitoka nnje kwa hasira kumuuliza Mama mkwe wangu kama alikua kamfanya nini mume wangu, nilimkuta Mama mkwe kakaa na Binti yangu, mwanangu alikua mzima kabisa anaongea na kucheza na Bibi yake, nilishtuka kidogo.


“Mama njoo tucheze Bibi amenpa uji nimepona.” Mwanangu aliniambia, nilishtuka nikiwaza ni uji gani huo aliopewa, nilikumbuka kipindi alipokua mdogo Mama mkwe wangu alikua akimlisha mwanangu unga kama msukule, niliwaka nakumuuliza kama alimpa nini mwanangu.


“Ingia chumbani kwangu utauona, ni uji mzuri sana…hahahahahah!” Mama mkwe aliongea hukua kicheka kwa dharau. Niliingia harakaharaka ili kuangalia, mlango ulikua wazi, nilifika na kitandani kulikua na vitu vingi tu vibakuli na vimwiko vidogo vidogo, lakini kitu kilichonishtua ilikua ni Condom zilizokua zimetumika, kulikua na condom zaidi ya kumi zilizokua nimetumika. Kuangalia kwenye vile vibakuli niliona kulikua na mbegu za kiume zilikua zimekorogewa pale.


Nilitoka nnje na kumchukua mwanangu, nilimtoa nnje kabisa, nikaleta maji na kuanza kumpa huku nikimuweka vidole mdomoni nikimuambia atapike. Nilijua kabisa kuwa Mama mkwe wangua likua kamlisha mbegu za kiume mwanangu, sikujua ni za nani lakini nilihisi.


“Umekula vitu gani mwanangu?” Niliendelea kujaribu kumtapisha lakini wapi hakutapika.


“Mama mbona unaniwekea  vidole mdomoni?” Mwanangu aliniuliza, nilimuambia kuwa bibi yake kampa sumu hivyo nataka atapike kwani itamdhuru. Nilijitahidi sana, nilikua kama mtu aliyechanganyikiwa, nilijaribu kumtapisha mwanangu lakini hakutapika.


“Mama lakini Bibi hakunipa uji nikala mdomoni, alikua akiniingizia huku…” Aliongea hukua kinionyeshea sehemu za siri. Nilitulia kidogo na kuanza kumuulizia taratibu ndipo aliniambia kuwa Bibi yake aliingia chumbani kwake akiwa kalala hajitambui akamvua nguo na kuanza kumuingizia vitu sehemu za siri ndipo alianza kupata nafuu, alipomuuliza ndipo alimuambia kuwa ni uji, ni dawa ambayo inatakiwa kuingia kwa huko.


Niliacha kumtapisha na kurudi ndani, nilianza kugombana na Mama mkwe wangu.


“Nimekusaidia, mume wangu ni mdhaifu, angemuua mtoto, maaganop yalikua ni yeye kutembea na mtoto wake lakini hakutaka hivyo mimi kama Mama nilikua na wajibu wakumlinda yeye na mjukuu wangu!” Aliongea kwa hasira, nilikasirika na kuanza kumtukana huku nikiamuambia kuwa ni mchawai, nilimuambia amneno mengi na tulishikana kutaka kupigana.


“Nilishakuambia kuwa umuache Mama yangu, kama huwezi kupatana na Mama yangu basi hata mimi hatuwezi kupatana, safari hii unaondoka kwangu!”


Sauti ya Mume wangu ilinishtua, alikua kashapona anatembea kama kawaida, alikuja kutuamua na niliona tayari kashageuka upande wa Mama yake. Nilianza kumuelezea kila kitu kilichotokea lakini hakuniamini, aliniambia kuwa Mama yake hawezi kufanya kitu kama hicho, nimemkosea heshima hivyo ni lazima kuondoka. Nilishangaa kwani baada ya kupona mume wangu alikua amebadilika kabisa, ni kama alikua kasahau kila kitu, alikua upande wa Mama yake na hata nilipomuambia kuhusu mambo aliyokua akiniambia alikana.


“Wewe ni shetani tu, umekuja hapa umeshajazwa maneno na hao sijui mawifi zako, najua wanawivu kwakua Mama ananipenda, najua wanaona kwakua mimi nafanikiwa ndiyo wanawaza mambo hayo, ujinga mtupu!” Aliongea, nililazimika kunyamaza kwani mume wangu hakutaka kunisikiliza kabisa. Niliingia chumbani nikiwa nalia sijui nini chakufanya, baada ya kama dakika kumi hivi mume wangu aliingia.


“Inabidi uondoke, siwezi kuendelea kushi nawewe, mambo unayomsingizia Mama yangu ni makubwa sana sidhani kama naweza kuendelea kuishi na wewe.” Mume wangu aliniambia.


Nilitamani kumshawishi na kumuambia kuwa sio kweli lakini niliona kama itakua kazi bure, nilimuaba kuwa naondoka lakini nitaondoka na wanangu. Alikataa na kuniambia kuwa watoto wake hawaendi popote nilikuja mwenyewe nitaondoka mwenyewe. Tuligombana sana mpaka kufikia hatua mume wangu kuanza kunipiga, alinipiga sana mpaka Mama mkwe alipokuja na kuingilia kati.


“Usipige mwanamke, huyu ni mke wako, Mama wa watoto wako, hivi utajisikiaje mtu akija hapa na kuanza kunipiga?” Aliuliza, mume wangu alibaki kimya, Mama mkwe aliongea sana kama mtu, akimpa nasaha na kumuambia kuwa hawezi kunipiga namna ile.


“Lakini Mama anakudharau na kukusingizia mambo mabaya…” Mume wangu aliongea kwa kujitetea, Mama yake alimkatisha.


“Hata kama lakini huwezi kumpiga, mke ni mke ni wakulindwa na hayo mambo ya kuondoka hakuna, mtabaki hapa nyie wawili na kama ni kuondoka nitaondoka mimi. Mimi ndiyo nimeingilia nyumba yenu na kama mke wako hanitaki basi ana haki hiyo niache niondoke.” Mama mkwe aliongea na kujifanya kuwa yupo tayari kwa lolote lakini mume wangu alimkatalia na kumuambia kuwa atabaki na kama mimi sitaki ndiyo niondoke. Nilikua na hamu sana ya kuondoka lakini sikua tayari kuwaacha wanangu, nilikua naiogopa sana ile familia kuwaachia wanangu.


“Kwaza mwanamke mwenyewe ana mimba, utamfukuzaje mwanamke ambaye ni mjamzito, utakua ni unyama wa hali ya juu…” Mama mkwe alisema maneno ambayo hata mimi yalinishangaza, sikujua kama nina mimba isitoshe ndiyo nilikua nimetoka kupata siku zangu.


“Sina mimba mimi usinichulie!” Nilimjibu kwa dharau lakini hakujali, aliendelea kusema kuwa mimi ni mjamzito hivyo mume wangu hatakiwi kunifukuza. Mume wangu alionekana kufurahi na kunilaumu ni kwanini sikumuambia, alinikuambatia kwa guraha na kuniomba misamaha mingi, mimi nilimsikiliza tu huku nikimuangalia kwa mshangao kwani nilijua kuwa sina mimba wala nini?


Waliendelea kupongezana kama wajinga, Mama mkwe alionekana kama ana uhakika sana na kuniambia kuwa  niwe makini, alitoa maushauri mengi lakini niliona kama vile ananiboa. Nilitoka sebuleni, nilimkuta mwanangu kakaa anaangalia katuni.


“Bibi  anasema utatuleea mtoto mwingine, mimi nataka awe wakike ili avae nguo zangu…” Aliniambia, nilishindwa chakumjibu, nilitaka kumuambia kuwa sina mimba na hakuna mtoto alitekua anakuja lakini hata mimi kwa wakati huo nilichanganyikiwa, mambo yalitokea kwa harakaharaka sana, niliingia zangu  kwenye chumba cha wageni na kujitupa kitandani kwani nilichoka sana.


****


Mume wangu hakutaka nitoke ndani, alininyang’anya kila ktu ikiwa ni pamoja na simu, alikua hataki niwasiliane na ndugu zangu wala mtu yeyote yule. Nilikaa pale ndani kama mfungwa, alichukua kadi zangu za benki na ahakunia pesa, hata pesa ya matumizi alikua akimkabidhi Mama yake abaye ndiyo alikua akinunua kila kitu. nilibaki pale kwaajili ya wanangu hasa binti yangu lakini alimpeleka bweni na sikuruhusiwa kwenda kumuona. Nilibaki mpweke sana, maisha yalikua magumu sana kwangu nikawa nakaa ndani tu.


Mwanzo sikuamini kama nina mimba lakini nilianza kuona dalili zote za ujauzito, kichechefu chefu na kutapika, miguu kuvimba na presha ilianza kunipanda mara kwa mara. Nilienda hospitalini na kupimwa nilikutwa kweli nina ujauzito wa miezi mitatu, nilishangaa kwani mpaka wakati huo nilikua naona siku zangu, hospitalini nilikua nikienda na mume wangu na alikua akiingia katika kila hatua akiniambia kuwa nimshachanganyikiwa hivyo siruhusiwi kuongea na watu kwani nitawaambia maneno ya uongo.


Mume wangu ni kama alikua kasahau kuwa yeye mwenyewe ndiyo aliniambia kuhusu kufanya mapenzi na Mama yake mzazi, alisahau kabisa kuwa alikua anaumwa na alisahau kuniambia kuwa Mama yake alikua ni mchawi. Niliumia sana kwani nilijua kila kitu na kilichoniumiza zaizi ni mwanangu, nilijua kabisa siwezi kumuona na sikua na uhakika huko shule alikopelekwa Baba yake alikua haendi na kumfanyia vitu vibaya. Manyanayso, mawazo na vipigo vya kila siku vilinifanya kukonda sana, nilibaki tumbo tu.


Siku moja Mume angu alikuja na binti mmoja,a likua ni binti mdogo tu wa kama miaka 16, aliniambia ndiyo atakua akinisaidia kazi za nyumbani kwani kutokana na hali yangu nilitakiwa kupumzika. Kwa namna alivyokua alionekana katoka kijijini kwao kwani walikua wakiongea kilugha na mara kwa mara yule binti alipenda kuja chumbani kwangu kuniongelesha akizungumzia mambo ya huko kwao, mwanzo mimi nilikua simpendi lakini mwisho nilimuona kama rafiki kwani alikua ni mchangamfu sana na kazi alikua akifanya kweli.


Tulizoeana na kwakua muda mwingi nilibaki naye nyumbani kwani Mama mkwe naye alianza kusimamia baadhi ya Biashara za mume wangu hasa akisafiri basi tulikua marafiki na kweli nilimpenda. Siku mona nilikua bafuni, wakati naoga nilidondoka na kupoteza fahamu, nilikuja kuzindika kama baada ya masaa mawili baadaye, yule binti alikua pembeni yangu akiniangalia, nilikua nimelala chini damu zinanitoka sehemu za siri, zilikua damu kama vile mimba imetoka, nilishtuka kidogo kuona zile damu lakini nilishtuka zaidi kumuona tyule binti kazikalia.


Alikua kakaa chini pembeni yangu, ananichungulia sehemu zangu za siri, anaangalia damu zinavyotoka, amezishika kwenye mikono yake na kuwa kama anazisugua sugua,  kama vile umeshikilia kitu unakisugua  na vidole kuangalia utelezi wake. Nilishangaa na kumuuliza kama alikua anafanya nini?


“Dada umeamka?” Aliniuliza kwa mshangao lakini hakuacha kukifanya kile alichokua akikifanya, aliendelea huku akizishangaa.


“Acha ni uchafu huo!” Nilimuambia kwa hasira huku nikinyanyuka kujisitiri, lakini hakuacha, aliendelea huku akiniangalia kwa mshangao.


“Dada unajua kuwa hujabeba mimba?” Aliniuliza, nilimuangalia kwa mshangao lakini yeye alizidi kunikodolea macho kwa mshangao zaidi.


“Unasema nini? Unamaanisha nini?” Nilimuuliza, nikitu ambacho nilikua na wasiwasi nacho muda mrefu lakini nilitaka kujua kuwa kajuaje yale mambo.


“Dada hujabeba mimba, hapa umebeba maiti na ukiendelea hivi hutakuja kujifungua mpaka unakufa, hii mimba lazima itakuua, ndiyo lengo lao, umetolewa sadaka Dada…” Aliniambia maneno ambayo yalinishtua sana, kwanza kwa kumuangalia alikua bado mdogo lakini mamboa liyokua akiyaongea nikiangalia na ile familia niliona kama yana ukweli.


“Kwanini unasema hivyo?” Nilimuuliza.


“Angalia…” Aliongea hukua kinionyesha kipande cha nyama kidogo ambacho kilitoka mwilini mwangu, aliniambia nikishike na  kukisugua kwa viganja vyangu, nilishika na kufanya hivyo lakini bado sikusikia chochote.


“Kina nini mbona sielewi?” Nilimuuliza.


“Huelewi kwakua hujui tofauti, wewe hujabeba mimba bali umebebshwa maiti na lengo ni kukumaliza. Angalia utelezi wake, ungekua una mimmba kungekua na utelezi wa kawaida, lakini haka kuna utelezi wa changachega, hakuna kitu hapa, hii ni mimba ya kutumiwa…”


Likua anaongea kwa kujiamini, ingawa sikua nikimuelewa na sikujua hata aalikua anamaanisha nini wala kujua alijifunzia wapi yale mambo lakini nilijua tu yana ukweli kwani nilibeba mimba katika mazingira ambayo hayaeleweki bila hata mimi mwenyewe kujua. Nilimuuliza alijualia wapi hayo mambo katika umri mdogo namna ile alicheka na kuniambia.


“Mimi nilikua naishi na Bibi yangu amekufa ndiyo nikaletwa huku, kumbe ndiyo maana Baba alikua ananiambia kuwa nikuchunguze kwani una mambo ya kichawi. Kuna mtu kakufanyia haya mambo Dada huwezi kuzaaa.”


Sikumuelewa niliendelea kumdodosa ndipo aliniambia kuwa Bibi yake alikua ni mganga na alishawasaidia watu wengi.


“Nimelelewa na Bibi baada ya Mama yangu kufariki na mimi Baba yangu simjui, Bibi alikua mzee sana hivyo kazi zote nilikua namfanyia mimi, mimi si mganga wala si mchawi lakini najua vitu vya kulogewa, unaweza kulogewa mimba ukabeba mpaka ikakuua. Kama una mkondo wa mali mwanaume hawezi kukuacha wala kukuua kawaida, anakulogea mimba ambayo itakuua wakati unajifungua au katikati ya ujauzito. Mume wako atakua anataka kuoa mwanamke mwingine na hawezi kuoa mpaka wewe ufe kwani wewe ndiyo mwenye mkondo wa mali” Yule binti aliaongea maneno ambayo yalizidi kunitisha.


SITAKI WANIZIKE; NIKIFA NDUGU ZANGU CHUKUENI MAITI YANGU—SEHEMU YA KUMI NA TATU


Nilimuangalia yule binti kwa kuogopa sana, alionekana kama mtoto lakini alikua na mambo makubwa.


“Dada hii nyumba sio ya kukaa, kama wanafanya haya mambo hapana, watakuja kukuua!” Aliniambia huku akinishika mkono, aliniambia kusimama katikati ya zile damu, akaenda kuchukua dekio na kuniambia nisinyanyue miguu, alianza kukausha damu nikiwa nimesimama katikati yake, alikausha mpaka kukakauka kisha akanikausha na miguu.


“Vua hizo nguo…” Aliniambia, nilisitasita kidogo lakini alinikazia macho mpaka nikalazimika kuzivua mbele yake, alizichukua na kuondoka nazo, sikujua kazipeleka wapi lakini alirudi akiwa na nguo nyingine akanipa nikavaa kisha akaniambia kuwa niondoke.


Nilirudi chumbani nikitetemeka kwauoga, maneno aliyokua kaniambia yalinichanganya sana, niliogopa kufa lakini nilimuogopa hata yeye kwa mambo aliyokua akiyafahamu.


“Bibi yangu angekuepo angekusiadia, lakini mimi siwezi, ila kuna kitu nataka nikifanye, mimba yako itatoka, mtu aliyekufanyia hivi vitu ni mtu mkubwa sana kupambana naye ila nikichoma nguo zako moto mimba itato9ka lakini utaumwa sana.” Aliingia chumbani kwangu na kuniambia, nilikua kama nimechanganyikiwa hivyo nilimkubalia kila kitu alichosema.


“Njoo huku…” aliniambia, nilitoka na kumfuata mpaka nnje, alichukua zile nguo zangu, akachukua kiberiti na kuziwasha, alichukua mafuta ya kula na kuyamwagia juu, nilimuuliza ni kwanini akasema hajui yeye alikua anamuona Bibi yake akifanya hayo mambo. Wakati anachoma moto mimi tumbo lilianza kukata, lilikua linauma sana mpaka kushindwa hata kunyanyuka, jinsi moto ulivyokua uankua mkubwa ndivyo ambavyo na mimi maumivu yalizidi, niliumia sana mpaka mopto ulipozimika nilidondoka na kupoteza fahamu kabisa, sikujua kilichoendelea mpaka jioni nilipozinduka nipo hospitalini.


Mume wangu nalikua pembeni yangu, alionekana kuwa na huzuni kubwa, alikua analia kama mtoto huku Mama yake akimfariji. Niliwauliza kilichokua kimetokea wakaniambia kuwa mtoto kafia tumboni hivyo nasubiriwa kujifungua. Sikushtuka sana, nilimuulizia yule binti nikaambiwa yuko nyumbani, nilinyamaza na dakika kadhaa nilianza kujisikia uchungu, nilijifungua tu kawaida lakini tofauti, mtoto wangu alionekana kuwa kawaida, ana viungo karibu vyote lakinia likua ameungua, mweuzsi tii kama mkaa. Mama mkwe kuona alipaniki zaidi, aliniuliza nilikua nimemfanya nini mjukuu wake laikini sikua na jibu.


Ni kama alihisi kuwa kuna kitu nimekifanya, alianza kupiga kelele kuwa mimi ni mchawi na nimeitoa ile mimba makusudi, mume wangu aliwaka na kutaka kunipiga palepale hospitalini lakini kelele za Mama yake zilishtua manesi ambao walikuja na kuwatoa nnje.


“Dada uko vizuri? Kuna tatizo gani?” Nesi mmoja ambaye alionekana binti mdogo  tu aliniuliza. Nilitingisha kichwa kumuambia kuwa niko vizuri lakini hakuniamini, alitaka kunidodosa zaidi nikajifanya kukasirika akaona isiwe shida akatoka zake nnje na kuniacha peke yangu nikiwa sijui nini chakufanya.


Niolikua najisikia vibaya sana kichwa changu kilizungukwa na  mambo mengi, baada kama ya nusu saa hivi yule nesi alikuja tena na kuniuliza kama nilikua nina tatizo. Nilimuangalia kwa hasira nikiona kama anataka kuingilia mambo yangu.


“Dada fanya kazi yako mambo ya familia yangu hayakuhusu!” Nilimuambia kwa hasira akaondoka, nilikaa mpaka siku iliyofuata ndipo niliruhusiwa kuondoka. Nilifika nyumbani sikumkuta yule binti, Mama mkwe aliniangalia kwa hasira na kuniambia.


“Unajifanya mjanjaee, nimemuopndoa mchawi mwenzako tuone kama utafanya nini, na sasa hivi utajuta kuzaliwa mshenzi mkubwa wewe!”


Sikujua kilichotokea kwa yule binti lakini sikuwahi kuwasiliana naye wala kumuona tena, nilisikia tu walimuondoa akaenda kufanya kazi sehemu nyingine. Kwa mambo yaliyotokea Mama mkwe alishtukia kitu. Nilitaka kuondoka lakini Mama mkwe aliniambia kama naondoka basi nimuachie wajukuu wake, mume wangu alikua akimsikiliza Mama yake kwa kila kitu. hapo manyanyaso ndipo yalainza upya, mume wangu alitaka kuniacha lakini mama yake alikataa na kumuambia wazi tena mbele yangu kuwa katika dini yetu hakuna talaka ni mpaka mimi nife ndiyo ataruhusiwa kuoa mwanamke mwingine.


Alianza kuchepuka waziwazi na wakati mwingine akileta wanawake mule ndani bila kujali kama mimi nipo au kujali kuwa Mama yake alikua akiishi pale. Mimi nilishamkatia tamaa na nilikua nikiishi pale kwaajili ya wanangu, lakini mama mkwe aliona wivu na kila siku walikua wakigombana mara kwa mara, mume wangu alikua akimsikiliza katika kila kitu lakini si katika wanawake, alitaka kuniacha na Mama yake hakutaka kabisa aniache. Nilikumbuka maneno ya yule binti ambaye aliniambia kuwa mimi ndiyo niko kwenye mkondo wa mali hivyo mpaka nife ndiyo anaweza kuoa mwanamke mwingine.


Hospitalini niliambiwa kwenda baada ya siku tano kwajili ya kufanyiwa chekup, Mama mkwe alikataa lakini nililazimisha kwani nilijua kuwa ni maisha yangu. Lakini siku moja kabla ya kwenda hospitalini ghafla nilidondoka, mwili uliishiwa nguvu na nikaanza kutapika damu, Mama mkwe alikuepo lakini hakufanya chochote, nilitapika sana mpaka nikawa kama napaliwa na damu. Mama mkwe hakunigusa aliniangalia tu, nilinyanyuka kwa shida na kujikongoja mpaka nnje, majirani waliniona na ndiyo walinisaidia kunipeleka mpaka hospitalini.


Hali yangu ilikua mbaya, walinifanyia uchunguzi lakini hwakaukuta chochote, mimi nilielewa kuwa ni mambo ya kishirikina. Nilikaa hospitalini kwa siku tatu, si mume wangu wala amabye alikuja kuniangalia. Nilikua katika hali mbaya sana na nilihisi kabis anitakufa, nilishakata tamaa ya kuishi na nilijua kuwa njia peke ya mimi kuwa salama ni kwa kufa tu kwani ningeendelea kuteseka. Ndugu walishanitenga na kwakua sikua na pesa tena hata kuwatafuta ilikua shida sana. Nilijua kabisa siwezi kupambana na nguvu za Mama mkwe wangu.


Kila wakati nilikua mtu wa kutapika nyama zilizooza, mpaka madaktari walishangaa. Nikiwa katika hali ile yule nesi ambaye alinidaisi mara ya kwanza alikuja, alianza kuniongelesha mambo mengi mengi na kutaka kuwa rafiki yangu. kwa hali niiyokua nayo nilihitaji mtu kama yule, nilihitaji mtu wa kuongea naye kwani kwa siku tatu mfululizo nilikua sijaongea na mtu yeyote zaidi ya madaktari na menesi, nilihitaji rafiki. Aliniongelesha mambo mengi lakini nilikua nimekata tamaa, nilijua kuwa nitakufa na kuna kitu nilitaka anisaidie.


“Kuna kitu nataka unisaidie…” Nilimuambia, nilikua naongea kwa shida kwani kila nikinyanua mdomo damu zinatoka napaliwa.


“Kitu gani?” Aliniuliza.


“”Najua nitakufa, lakini nikifa sitataka wanizikie, nataka ndugu zangu waj ekuchukua maiti yangu…” Niliongea, alijaribu kunisihi nisiwaze hivyo, alinipa moyo kuwa kila kitu kitakua sawa lakini sikutaka kujidanganya, nilijua kabisa kuwa hakitakua sawa, nilijua kuwa nitakufa.


“Hapana mdogo wangu, huu ndiyo mwisho wangu, nataka uandike namba hii, nikifa wapigie ndugu zangu, waambie nimewasamehe na wachukue maiti yangu, simuamini mume wangu, simuamini Mama mkwe wangu, anaweza kuila nyama maiti yangu…”


Nilizidi kumsihi yule dada, lakini wakati mimi naongea kumuelezea mambo ya kunifaya yeye alipiga magoti. Alifunga macho na kuanza kusali, alikua anasali kimya kimya, aliomba kwa karibu nusu saa kisha akanyanyuka na kuniambia.


“Dada una imani? Unaamini kuwa Mungu yupo?” Aliniuliza, nilimuangalia kwa dharau nikamjibu.


“Siamini, hivi kama kungekua na Mungu angewezaje kuruhusu haya yote….” Niliongea lakini kabla ya kumalizia nilishangaa kwani nilikua naongea vizuri, damu zilikua hazinitoki mdomoni na sauti ilitoka kama kawaida.


Nilijaribu kusimama nikajikuta niko sawa kabisa, mwili ulikua mwepesi niliweza hata kusimama.


“Dada ulikua unasema Mungu…?” Aliniuliza, mdomo ulishindwa kufunguka kuendelea kumkufuru Mungu.


“Nilijua kunha kitu tu siku ya kwanza nilipokuona, Yule Mama kuna mambo alikua anayafanya na nilipoingia alikua anatetemeka nusu kujikojolea nikajua kuna kitu wamekufanyia ndiyo maana nilitaka kuwa rafiki yako.” Yule Nesi amabye alikua binti mdogo tu aliniambia, nilimuuliza kama yeye ni mlokole, mchungaji au anaa nini akaniambia hapana, yeye ni muumini wa kawaida ambaye anaamini kuwa Mungu anaweza kutenda lolote analolitaka liwe.


“Shift yangu imeshaisha muda mrefu na nilikuja hapa kwakua nilijua unahitaji mtu wa kukuongoza, unachohitaji ni imani tu, si kuokoka, si kushinda kanisani na wala si kutangaza kuwa wewe ni wa tofauti, hapana, unachohitaji ni imani tu kuwa Mungu yupo na anaweza kufanya chochote kile.” Aliongea kwa kujiamini, nilimuelezea mambo niliyopitia kwenye ndoa yangu na namna ambavyo nimekua nikiumwa mimi na wanangu.


“Twende nyumbani kwako, nenda kawachukue wanao, hakuna mtu atakufanya chochote, kama ukitembea na Mungu hakuna wakukusumbua.”


Aliniambia lakini bado niliogopa, aliniambia nisiwe na wasiwasi kwani hakuna uchawi nafanya kazi kwa mtu mwenye imani, alifanya mpango nikaruhusiwa kutoka, tulienda kwake, akachukua maji ya Baraka akanipaka kisha akaniambia twende nyumbani kwangu. Nilifika na kuwakuta wote Mama mkwe na mume wangu pamoja na mwanangu mdogo. Walishangaa kuniona, Mama mkwe alipomuona yule Dada alianza kutetemeaka huku akisema kuwa aondoke, akimuita mchawi na mambo mengine. Dada alimuambia kuwa hakuja kugombana bali mimi kumchukua mtoto wetu na kuondoka.


Mume wangu alikataa na kutaka kufanya burugu, yule dada alitoa maji ya Baraka, akayanyunyizia kwenye nyumba kisha akapiga magoti, aliomba kimya kimya, ila kila alipokua anaomba Mama mkwe wangu alikua akipiga kelele. Nesi aliendelea kuomba huku mume wangu akiwa kasimama tu anatuangalia, ni kama alikua kapigwa siindano ya ganzi kaganda kabisa. Nesi aliomba  sana huku Mama mkwe akipiga kelele na mpaka anamaliza mama mkwe alikua kashadondoka chini, amependwa na mashetani anaongea mambo ambayo hayaeleweki.


Aliniambia nimchukue mtoto wangu na baadhi ya vitu kisha tuondoke. Nilimchukua na kuondoka, mume wangu alikua bize kumuangalia Mama yake. Nilienda kukaa kwa yule Nesi, nilikaa kwa wiki mbili, nikaenda kumchukua mwanangu shuleni nikawa nakaa naye, nilitaka kumuondoa shule kwanza kusubiri mambo yapoe.  Mume wangu alikua akinipigia simu kila siku kulalamika kuwa nimemloga Mama yake kwani tangu siku ile Mama yake hakunyanyuka tena, alipata stroke na kupooza upande mmoja.


Hakuna aliyejali kuhusu Mama mkwe wangu, watoto wake wengine hawakuenda hata kumuona. Nilitafuta kazi ya Mama lishe nikawa nafanya, sikutaka kujishughulisha chochote na mali za mume wangu kwani niliona kama ni za kishetani. Ni muda sasa umepita nafuatilia talaka yangu mahakamamani, niliacha kazi ya Mama lishae sasa hivi nimejikusanya nimefungua duka langu baada ya kuuza kiwanja changu amabcho nilikinunua kabla ya kukutana na mume wangu, mali zote, Mama mkwe wangu bado hali ni ileile anaumwa, mume wangu pesa zimemuishia na kauza karibu kila kitu.


Nina maisha yangu sasa hivi na nimeamua kuendelea mbele, ndugu zagu bado sipatani nao vizuri lakini sijali, namshukuru sana Nesi kwani amekua rafiki kwangu na ameokoa maisha yangu. Kupitia maisha yangu nimejifunza kuwa si kila kitu ni chakuvumilia kwani naamini mambo yote yaliyonikuta nikwakua nilivumilia vitu ambavyo sikupaswa kuvivumilia. Si kila mtu atapata bahati ya kukutana na Nesi au Dada wa kazi kama wangu, lakini naamini kupitia kisa changu Kaka iddi kuna watu watajifunza na kuacha kuvumilia mambo ambayo hayavumiliki, nashukuru sana kwa kunipa nafasi katika ukurasa wako.


**MWISHO;

0 comments:

Post a Comment

BLOG